Reli ya Usambara na vita ya Tanga

Reli ya Usambara na vita ya Tanga

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Reli ya Usambara, Moshi-Tanga ndiyo reli ya kwanza kujengwa ndani ya Tanganyika. Ilijengwa miaka ya 1890's. Reli hiyo ilianza kujengwa na kampuni binafsi na baadaye ikachukuliwa na serikali ambayo iliimalizia hadi Arusha. Lengo kuu lilikuwa kuunganisha bandari ya Tanga na eneo la kaskazini ambako kulikuwa na mashamba makubwa ya wakulima wa Kijerumani. Lakini kwenye plan ilikuwa reli hiyo ifike hadi Mwanza.

Wakati wa vita ya kwanza ya dunia reli hiyo ilifanya kazi nzuri sana ya kusafirisha wanajeshi kwenda Tanga. Kwenye WWI, vita ya kwanza kabisa kupiganwa ndani ya Tanganyika ilipiganwa Tanga. Inaitwa vita ya Tanga au vita ya nyuki. Kwenye hiyo vita kamanda wa Ujerumani von Lettow-Vorebeck alikuwa amepanga kuwa ili kudeal basi atashambulia sehemu yake nyeti, reli ya Mombasa-Uganda. Hivyo wanajeshi wengi walikuwa wamekusanyika huko Moshi.

Baada ya kusikia kuwa manowari za Uingereza zilikuwepo huko Tanga, akaanzisha oparesheni ya haraka haraka kusafirisha vikosi kuelekea Tanga kwa treni. Kwenye vita hiyo jeshi la Wajerumani na Waafrika 1,000 lilipambana na Waingereza na Wahindi 8,000. Jeshi la Uingereza lilipigwa vibaya sana. Huyu jamaa Vorbeck alikuwa kamanda hasa. Wahindi waliounda sehemu kubwa ya jeshi la Uingereza walichinjwa sana. Inasemwa watu 1,500 walifariki huku wajerumani wakipoteza kama watu 80 hivi. Baadaye jeshi lao likakimbilia Zanzibar kwa aibu kubwa.

Kwenye hiyo vita kulizuka nyuki waliowashambulia askari, hasa wa jeshi la Uingereza. Ndiyo maana inaitwa pia vita ya nyuki.

Tulipopata uhuru serikali ikajenga Coastal Railway ili kuunganisha reli ya Usambara na reli ya kati. Wazo hilo la kuunganisha reli ya Usambara na ya kati alikuwa nalo Lettow Vorbeck. Aliona jinsi ilivyokuwa vigumu kusafirisha wanajeshi kutoka reli ya kati kuelekea maeneo ya kaskazini.

Wajerumani walikuwa watu wa kazi hasa.

1698776358796.png
 
Najiulizaga, tungeendelea kutawaliwa na Mjeruman, je, tungekuwa kama tulivyo leo hii au tungekuwa fasta katika kufikiri, kupanga na kutekeleza?
Tungekuwa kazi kazi
Mangilimaa

Ova
 
Reli ya Usambara, Moshi-Tanga ndiyo reli ya kwanza kujengwa ndani ya Tanganyika. Ilijengwa miaka ya 1890's. Reli hiyo ilianza kujengwa na kampuni binafsi na baadaye ikachukuliwa na serikali ambayo iliimalizia hadi Arusha. Lengo kuu lilikuwa kuunganisha bandari ya Tanga na eneo la kaskazini ambako kulikuwa na mashamba makubwa ya wakulima wa Kijerumani. Lakini kwenye plan ilikuwa reli hiyo ifike hadi Mwanza.

Wakati wa vita ya kwanza ya dunia reli hiyo ilifanya kazi nzuri sana ya kusafirisha wanajeshi kwenda Tanga. Kwenye WWI, vita ya kwanza kabisa kupiganwa ndani ya Tanganyika ilipiganwa Tanga. Inaitwa vita ya Tanga au vita ya nyuki. Kwenye hiyo vita kamanda wa Ujerumani von Lettow-Vorebeck alikuwa amepanga kuwa ili kudeal basi atashambulia sehemu yake nyeti, reli ya Mombasa-Uganda. Hivyo wanajeshi wengi walikuwa wamekusanyika huko Moshi.

Baada ya kusikia kuwa manowari za Uingereza zilikuwepo huko Tanga, akaanzisha oparesheni ya haraka haraka kusafirisha vikosi kuelekea Tanga kwa treni. Kwenye vita hiyo jeshi la Wajerumani na Waafrika 1,000 lilipambana na Waingereza na Wahindi 8,000. Jeshi la Uingereza lilipigwa vibaya sana. Huyu jamaa Vorbeck alikuwa kamanda hasa. Wahindi waliounda sehemu kubwa ya jeshi la Uingereza walichinjwa sana. Inasemwa watu 1,500 walifariki huku wajerumani wakipoteza kama watu 80 hivi. Baadaye jeshi lao likakimbilia Zanzibar kwa aibu kubwa.

Kwenye hiyo vita kulizuka nyuki waliowashambulia askari, hasa wa jeshi la Uingereza. Ndiyo maana inaitwa pia vita ya nyuki.

Tulipopata uhuru serikali ikajenga Coastal Railway ili kuunganisha reli ya Usambara na reli ya kati. Wazo hilo la kuunganisha reli ya Usambara na ya kati alikuwa nalo Lettow Vorbeck. Aliona jinsi ilivyokuwa vigumu kusafirisha wanajeshi kutoka reli ya kati kuelekea maeneo ya kaskazini.

Wajerumani walikuwa watu wa kazi hasa.

View attachment 2799430
Siku hizi tueshindwa kuitegemeza reli ya Kaskazini hata baada ya miaka 60+ ya uhuru na hata licha ya kuwa na watu zaidi ya 60 million!
 
Wajerumani wameahidi kurejesha mafuvu yetu kutoka Ujerumani. Labda yakirudi hali itabadilika
 
Najiulizaga, tungeendelea kutawaliwa na Mjeruman, je, tungekuwa kama tulivyo leo hii au tungekuwa fasta katika kufikiri, kupanga na kutekeleza?
Nchi ingekuwa kama South mzee. Ingawa bado ingeishia kwa wala rushwa hawahawa
 
Najiulizaga, tungeendelea kutawaliwa na Mjeruman, je, tungekuwa kama tulivyo leo hii au tungekuwa fasta katika kufikiri, kupanga na kutekeleza?
Tungekuwa MBALI Sana hata hawa wajinga wanajiita chawa usingewasikia
Nb ila tungekoma !! Mjerumani alikuwa mjeuri sana
 
Reli ya Usambara, Moshi-Tanga ndiyo reli ya kwanza kujengwa ndani ya Tanganyika. Ilijengwa miaka ya 1890's. Reli hiyo ilianza kujengwa na kampuni binafsi na baadaye ikachukuliwa na serikali ambayo iliimalizia hadi Arusha. Lengo kuu lilikuwa kuunganisha bandari ya Tanga na eneo la kaskazini ambako kulikuwa na mashamba makubwa ya wakulima wa Kijerumani. Lakini kwenye plan ilikuwa reli hiyo ifike hadi Mwanza.

Wakati wa vita ya kwanza ya dunia reli hiyo ilifanya kazi nzuri sana ya kusafirisha wanajeshi kwenda Tanga. Kwenye WWI, vita ya kwanza kabisa kupiganwa ndani ya Tanganyika ilipiganwa Tanga. Inaitwa vita ya Tanga au vita ya nyuki. Kwenye hiyo vita kamanda wa Ujerumani von Lettow-Vorebeck alikuwa amepanga kuwa ili kudeal basi atashambulia sehemu yake nyeti, reli ya Mombasa-Uganda. Hivyo wanajeshi wengi walikuwa wamekusanyika huko Moshi.

Baada ya kusikia kuwa manowari za Uingereza zilikuwepo huko Tanga, akaanzisha oparesheni ya haraka haraka kusafirisha vikosi kuelekea Tanga kwa treni. Kwenye vita hiyo jeshi la Wajerumani na Waafrika 1,000 lilipambana na Waingereza na Wahindi 8,000. Jeshi la Uingereza lilipigwa vibaya sana. Huyu jamaa Vorbeck alikuwa kamanda hasa. Wahindi waliounda sehemu kubwa ya jeshi la Uingereza walichinjwa sana. Inasemwa watu 1,500 walifariki huku wajerumani wakipoteza kama watu 80 hivi. Baadaye jeshi lao likakimbilia Zanzibar kwa aibu kubwa.

Kwenye hiyo vita kulizuka nyuki waliowashambulia askari, hasa wa jeshi la Uingereza. Ndiyo maana inaitwa pia vita ya nyuki.

Tulipopata uhuru serikali ikajenga Coastal Railway ili kuunganisha reli ya Usambara na reli ya kati. Wazo hilo la kuunganisha reli ya Usambara na ya kati alikuwa nalo Lettow Vorbeck. Aliona jinsi ilivyokuwa vigumu kusafirisha wanajeshi kutoka reli ya kati kuelekea maeneo ya kaskazini.

Wajerumani walikuwa watu wa kazi hasa.

View attachment 2799430
tunahitaji kufufua reli hizi zote.
 
Sio kwa serikali hii ya CCM. Hawana mpango huo. Sababu kubwa ni kwamba wamiliki wa mabasi na malori ndio watunga sera na wapitisha sheria kule bungeni
just imagine, tungefufua reli ya Tanga hadi Moshi, tukafufua reli ya kati, na TAZARA zote zikawa SGR na zinatumia umeme, watu wakasafiri kwa train za haraka na mizigo ikasafirishwa kwa train za haraka. maisha mbona yatakuwa mazuri sana. nchi zote zilizoendelea zimeweka mfumo huo. hiyo reli ya kati SGR inaendelea kutengenezwa, ila reli ya tazara na ile ya Tanga hakuna hata fununu. tupate wapi kiongozi mwenye maono?
 
Back
Top Bottom