Religion and Science hazishindani

Religion and Science hazishindani

Kwanza kabisa nawasalimia.
Leo napenda kuongelea makundi haya mawili duniani. Dini na Sayansi.

Kumekuwa na mjadala mkubwa mno duniani kuhusu haya makundi. Kwanza kabisa kabla ya kuendelea ninapenda kuongelea kitu kinachoitwa faith. Kila mtu dunia yupo na faith kuanzia mototo mpaka Mzee. Unaweza ukawa na faith na daktari, baba, mke wako, elimu, Mungu nk.

Katika suala la faith haijalishi kuwa mwanasayansi au mtu wa dini wote wanakuwa na faith.

Sasa tunakuja kwenye upande wa dini. Dini zimekuwapo miaka na miaka na zinaendelea kuwepo. Msingi mkubwa wa dini ni kwenye swali la WHY!? Kwanini kuna magonjwa, kwanini jua linatoa mwanga nk. Zipo dini za aina tofauti tofauti zingine zipo za zinazoamini Mungu mmoja, zingine Miungu wengi na zingine haziamini uwepo wa Mungu.

Katika kutafuta kujibu swali la why!? Ndipo zinatokea dini na Imani tofauti tofauti kulingana na ujibuji wa swali hilo.

Kwa upande wa sayansi. Kila mtu ni mwanasayansi tangu akiwa mototo. Msingi mkubwa wa sayansi ni kujibu swali la HOW. Mfano ukipewa USB uchomeke kwenye laptop Utakuwa na observation, utatengeneza Hypothesis, Experiment baadae conclusion. Kama conclusion itakuwa poa utatengeneza theory. Kwamba kumbe kuchomeka USB kwenye Laptop alama inayoonesha logo ya USB inatakiwa kuwa juu.

Sasa basi. Kutokana na maelezo haya ni kwamba mwanasayansi na waumini wa dini hawana ugomvi wowote. Bali ugomvi uliopo ni Dini baina ya Dini au Wanasayansi baina ya Wanasayansi.

Ni hayo tu.

Nimevutiwa na mjadala wako na ningependa kuuliza maswali. Samahani yanaweza kuwa nje ya mada.

  1. Umetoa mfano wa kutumia USB na ukajiuliza how it work na mambo mengine. Ningependa nikuulize, je ulipokuwa mtoto au unajifunza dini ulipewa nafasi ya kujiuliza kufanya observation, kujenga hypothesis, kufanya experiment na baadaye kuja na conclusion?
  2. Ukipata nafasi ya kuchunguza maisha ya wanyama, wapo wanaofanya processes zote ulizozitaja kwenye mfano wako wa USB. Kwa mfano nyani wanapotaka kuiba mahindi...wanafanya observations, wanafanya experiment, wanafanya conclusion, na labda wafanya hypothesis zao...je na wao ni wanasayansi...
  3. Je hili wazo liwe la kisayansi ni lazima liwe observation, hypothesis, experiment and conclusion. Je haiwezekani kuwa ni la hypothesis na conclusion....
 
Wewe jifunze hiyo lugha unayoiparamia ya Kiingereza kwanza kabla ya kujishaua.

Complementary ni nini?

Lugha unayotumia tu huijui, sasa mimi nitakuelewaje?
Umerukia kwingine sasa. Lakini umeelewa kuwa sayansi haijibu maswali ya WHY au bado unabisha!?
 
Umetoa mfano wa kutumia USB na ukajiuliza how it work na mambo mengine. Ningependa nikuulize, je ulipokuwa mtoto au unajifunza dini ulipewa nafasi ya kujiuliza kufanya observation, kujenga hypothesis, kufanya experiment na baadaye kuja na conclusion?
Ninauhakika pale ulipoandika neno dini ulikuwa unamaanisha sayansi.
Kama ulikuwa unamaanisha sayansi basi najibu kama ifuatavyo:

Kwanza kabisa tunatakiwa tujue science imetokea wapi. Science imetokana na philosophy of Nature au Natural Philosophy.
Kwa kifupi sayansi yenyewe inajihusisha na namna nature inavyofanya kazi.
Sayansi is the study. Siyo kupewa nafasi nawingine ukiwa mtoto uweze kufanya kitu.

Nilipokuwa ninatoa mfano wa kuchomeka USB kwenye laptop nilikuwa naeleza namna sayansi ilivyo. Kwa kulingana na issue hiyo hiyo ya kusoma nature either huyo mtoto aliona siku moja USB imechomekwa na siku nyingine haijachomekwa.
Kwa lengo la kujifunza neture mtoto mtoto akijiuliza kwanini USB haipo kwenye laptop au kwanini imechomekwa atakuwa na mzigo mkubwa sana wa kujibu swali hilo.
Lakini akijiuliza how USB inakuwa kwenye laptop na inakuwa haipo kwenye laptop itakuwa ni simple kwake kuanza practical na kufikia conclusion.

Kama kuna swali jingine katika hili nitajibu.
 
Ukipata nafasi ya kuchunguza maisha ya wanyama, wapo wanaofanya processes zote ulizozitaja kwenye mfano wako wa USB. Kwa mfano nyani wanapotaka kuiba mahindi...wanafanya observations, wanafanya experiment, wanafanya conclusion, na labda wafanya hypothesis zao...je na wao ni wanasayansi...
Kama ilivyo kwenye comment yangu ya hapo juu.
Sayansi is the study.
Ku process why na how haina shida kwa wanyama hao. Lakini sayansi imeepuka burden ya why.
Why inakutaka ujibu reasons.
How inakutaka kutoa methods
Vilevile unatakiwa kujua How ikishakuwa kwenye conclusion nzuri tunapata theory, law au formula.
Tuje kwa nyani anataka kuiba mahindi.

1. Kama nyani tayari huwa anaiba mahindi na amekuta nyani wenzake wakiwa wanaiba mahindi huyo huyo atatumia formula au law aliyoikuta ikewekwa na nyani wa kwanza ya jinsi ya kuimba mahindi. Sasa hebu jaribu kufikiria huyo nyani sasa anajiuliza kwanini ninaiba mahindi!?

2. Kama nyani ni Mara ya kwanza yupo pekee yake hajawahi kuiba mahindi na anataka kuiba mahindi.
Yupo na njaa ameona mahindi na nyani anajua hayo mahindi ni chakula.
(Naweka kwanza assumptions ili tuweze kutengeneza scenario)
Sasa huyo nyani akianza kujiuliza why ninataka kuiba hayo mahindi!? Sidhani nyani huyo kama ataweza kuiba hayo mahindi.
But akijiuliza how ninaweza kuiba hayo mahindi. Tayari ataanza kutengeneza hypothesis na kuzijaribu.

Mwisho sayansi ni study of nature how works but not why. Nature tayari ipo inafanya processes zake. Hatuwezi tukawa na mzigo wa kujiuliza why. Hilo swali linaachwa kwenye dini.
 
Je hili wazo liwe la kisayansi ni lazima liwe observation, hypothesis, experiment and conclusion. Je haiwezekani kuwa ni la hypothesis na conclusion....
Kama nilivyosema hapo juu kwamba sayansi ni study of nature siyo wazo.

Tunaposoma namna nature inavyo operate siyo wazo. Nature ipo na inaendelea kuwepo. Huwezi ukaleta wazo from no where nje ya nature. Vitu vinavyohusiana na sayansi ni vitu vilivyopo.

Kama nilivyosema Sayansi is the study inakanuni zake. Haiwezekani uruke steps.
Lazima upitie process za kisayansi.
Observation, hypothesis, experiment, conclusion finally (Theory, formula, law or principle)

Haiwezekani ukafanya ukaandika hypotheses kisha ukarukia kwenye conclusion without testing them. Lazima zijaribiwe tuone matokeo ya hizo hypothesis.

Conclusion ipi utaifanya hujafanya testing ya hiyo hypothesis!?
 
Ninauhakika pale ulipoandika neno dini ulikuwa unamaanisha sayansi.
Kama ulikuwa unamaanisha sayansi basi najibu kama ifuatavyo:

Kwanza kabisa tunatakiwa tujue science imetokea wapi. Science imetokana na philosophy of Nature au Natural Philosophy.
Kwa kifupi sayansi yenyewe inajihusisha na namna nature inavyofanya kazi.
Sayansi is the study. Siyo kupewa nafasi nawingine ukiwa mtoto uweze kufanya kitu.

Nilipokuwa ninatoa mfano wa kuchomeka USB kwenye laptop nilikuwa naeleza namna sayansi ilivyo. Kwa kulingana na issue hiyo hiyo ya kusoma nature either huyo mtoto aliona siku moja USB imechomekwa na siku nyingine haijachomekwa.
Kwa lengo la kujifunza neture mtoto mtoto akijiuliza kwanini USB haipo kwenye laptop au kwanini imechomekwa atakuwa na mzigo mkubwa sana wa kujibu swali hilo.
Lakini akijiuliza how USB inakuwa kwenye laptop na inakuwa haipo kwenye laptop itakuwa ni simple kwake kuanza practical na kufikia conclusion.

Kama kuna swali jingine katika hili nitajibu.

Asante kwa jibu lako. Nilikuwa nauliza dini. Je ulipopata mafunzo ya dini ulipewa nafasi za kufanya observations, kujenga hypothesis kufanya experiments, kutoa conclusion? Nimeuliza hivyo kwa sababu umesema sisi wote ni wanasayansi. Au tusime tunakuwa wanasayansi kwenye mambo yanayofanana na USB, na katika mambo kama ya dini tunapuyanga?
 
Kama ilivyo kwenye comment yangu ya hapo juu.
Sayansi is the study.
Ku process why na how haina shida kwa wanyama hao. Lakini sayansi imeepuka burden ya why.
Why inakutaka ujibu reasons.
How inakutaka kutoa methods
Vilevile unatakiwa kujua How ikishakuwa kwenye conclusion nzuri tunapata theory, law au formula.
Tuje kwa nyani anataka kuiba mahindi.

1. Kama nyani tayari huwa anaiba mahindi na amekuta nyani wenzake wakiwa wanaiba mahindi huyo huyo atatumia formula au law aliyoikuta ikewekwa na nyani wa kwanza ya jinsi ya kuimba mahindi. Sasa hebu jaribu kufikiria huyo nyani sasa anajiuliza kwanini ninaiba mahindi!?

2. Kama nyani ni Mara ya kwanza yupo pekee yake hajawahi kuiba mahindi na anataka kuiba mahindi.
Yupo na njaa ameona mahindi na nyani anajua hayo mahindi ni chakula.
(Naweka kwanza assumptions ili tuweze kutengeneza scenario)
Sasa huyo nyani akianza kujiuliza why ninataka kuiba hayo mahindi!? Sidhani nyani huyo kama ataweza kuiba hayo mahindi.
But akijiuliza how ninaweza kuiba hayo mahindi. Tayari ataanza kutengeneza hypothesis na kuzijaribu.

Mwisho sayansi ni study of nature how works but not why. Nature tayari ipo inafanya processes zake. Hatuwezi tukawa na mzigo wa kujiuliza why. Hilo swali linaachwa kwenye dini.

Niliuza kama nyani nao ni wanasayansi kwa sababu naona kama unachanganya curiosity na science. Kila binadamu ana curiosity ya kutaka kujua vitu vinavyomzunguka. Hata baadhi ya wanyama kama nyani nao wana curiosity. Science nayo in curiosity lakini kiwango chake ni cha juu kwa definitions za sasa.

Nadhani unakosea unaposema science is a study of how nature works. Na vilevile unakosea unaposema why tuachie dini.

Kwa mfano wakulima wa mihogo wanaona mihogo yao inakufa kwa ugonjwa usiojulikana. Kupata ufumbuzi wa tatizo hili, serikali inamtuma mwanasayansi aliyesomea elimu ya mimea. Je ni swali gani huyu mwanasayansi anatakiwa kujibu how or why?
 
Kama nilivyosema hapo juu kwamba sayansi ni study of nature siyo wazo.

Tunaposoma namna nature inavyo operate siyo wazo. Nature ipo na inaendelea kuwepo. Huwezi ukaleta wazo from no where nje ya nature. Vitu vinavyohusiana na sayansi ni vitu vilivyopo.

Kama nilivyosema Sayansi is the study inakanuni zake. Haiwezekani uruke steps.
Lazima upitie process za kisayansi.
Observation, hypothesis, experiment, conclusion finally (Theory, formula, law or principle)

Haiwezekani ukafanya ukaandika hypotheses kisha ukarukia kwenye conclusion without testing them. Lazima zijaribiwe tuone matokeo ya hizo hypothesis.

Conclusion ipi utaifanya hujafanya testing ya hiyo hypothesis!?

Kwa hiyo Albert Einstein alifanya experiments gani alipokuja na theory of relativity?
 
Asante kwa jibu lako. Nilikuwa nauliza dini. Je ulipopata mafunzo ya dini ulipewa nafasi za kufanya observations, kujenga hypothesis kufanya experiments, kutoa conclusion? Nimeuliza hivyo kwa sababu umesema sisi wote ni wanasayansi. Au tusime tunakuwa wanasayansi kwenye mambo yanayofanana na USB, na katika mambo kama ya dini tunapuyanga?
Discipline za dini hazihusiani na process hizo ulizozisema. Dini yenyewe inajihusisha sana na kujibu why.
Hebu jaribu kusikiliza hii video kidogo
 
Discipline za dini hazihusiani na process hizo ulizozisema. Dini yenyewe inajihusisha sana na kujibu why.
Hebu jaribu kusikiliza hii video kidogo


Naona haya mawazo unayatoa kwa sababu mtu au kikundi cha watu kimekushawishi kuwa dini inahusika na why na science inahusika na how? Kama unashindwa kujieleza na kutaka mimi ningalie video, basi vitu unavyotaka kuzungumza sio mawazo yako.
 
Umerukia kwingine sasa. Lakini umeelewa kuwa sayansi haijibu maswali ya WHY au bado unabisha!?
Wewe jifunze Kiingereza kwanza kabla ya kuparamia habari za "complementary".

Nimekuwekea list ya maswali muhimu wanayojadikmli wanasayansi.

Kuna swali "Why do we dream".

Kuna swali "Why is there stuff".

Nimekueleza Newton alivyoanza kujiukiza "why do things fall down and not up?".

Haya si maswali ya kisayansi?
 
Wewe jifunze Kiingereza kwanza kabla ya kuparamia habari za "complementary".

Nimekuwekea list ya maswali muhimu wanayojadikmli wanasayansi.

Kuna swali "Why do we dream".

Kuna swali "Why is there stuff".

Nimekueleza Newton alivyoanza kujiukiza "why do things fall down and not up?".

Haya si maswali ya kisayansi?

Kha!! Tunaanza personal attacks sasa hahahaha!!
Usijifanya ujuaji. Kama kitu hukijui tulia ufundishwe.
Kama hujaelewa ninachoongelea ni bora ukatuliza kichwa.
We jamaa unakuwa mgumu sana kuelewa.
Nimejaribu kukuwekea hata references mbalimbali kuhusu sayansi wewe unalazimisha eti Newton alijiuliza why!?

Hebu niambie sasa Alipojiuliza why alifanya nini!?
Unadhani hawakuwepo watu wanajiuliza hivyo!?
Ninakueleza kila wakati halafu una ignore kila ninachokueleza na kufuata simple things kama mjinga.

Nimekueleza maswali yapo mengi tu.
Kuna what, where, which, who etc. Unakimbia kuelewa na kutaka kubishana.
Sayansi ina methods zake (scientific process).

Sayansi haiwezi kamwe kujibu "Why do we dream"
Sayansi haitoi majibu ya reasons hayo ni maswali ya Philosophy siyo ya kisayansi.
Utakaopo elewa how things operates utajibu hayo maswali bila hata kuulizwa.

Nimekueleza sayansi inahusika na Nature ambayo ipo.
Lakini kuuliza why nature is so and so is a philosophical question is not a scientific.

Science inahusika na kutoa majibu how nature operates. Nature ipo lakini tunatafuta kujia how operates. Tukisema why there is something instead of nothing!? Hilo utajibiwa na philosophy au dini.

Nakusihi jifunze kuelewa vitu kwanza.
Hayo maswali yote uliyoyaandika ni maswali ya philosophy yanataka ulete sababu. But science yenyewe inatoa methods.

Mbona vitu simple.
Halafu umeng'ang'ania hilo neno la "complementary" huo ni utoto, unaacha mada. Sitaki tuanze kubishana kuhusu hilo ndiyo maana nimekupuuza katika hilo.
Jikite katika mada. Kama hujaelewa ni uwezo wako wa kufikiri umishia hapo.
 
Naona haya mawazo unayatoa kwa sababu mtu au kikundi cha watu kimekushawishi kuwa dini inahusika na why na science inahusika na how? Kama unashindwa kujieleza na kutaka mimi ningalie video, basi vitu unavyotaka kuzungumza sio mawazo yako.
We jamaa kwani kila kitu unachoandika hapa ni mawazo yako!?
Umeongelea kuhusu relativity hayo ni mawazo yako!?
Hata hii issue ya sayansi hayo ni mawazo yako!?

Ndio maana watu wanaishi kwa kutegemeana. Kuna mkulima, Mwalimu, mfanyabiashara nk.
Sasa tukianza kila mtu atoe only mawazo yake bila references tutakuwa tunarudi kwenye ujima.

Ndio maana kuna vitabu.
Umeuliza maswali nimekupatia ufafanuzi, na kukueleza theory of relativity ilikuwa na experiments zake.

Sasa unaaza kujadili namna ya uwasikishaji wa mada eti mawazo ya watu vikundi nk!!!

Wewe leta maelezo kuhusu how science answer WHY question!?
 
Wewe jifunze Kiingereza kwanza kabla ya kuparamia habari za "complementary".

Nimekuwekea list ya maswali muhimu wanayojadikmli wanasayansi.

Kuna swali "Why do we dream".

Kuna swali "Why is there stuff".

Nimekueleza Newton alivyoanza kujiukiza "why do things fall down and not up?".

Haya si maswali ya kisayansi?

Mimi nilimwekea mfano ambao anaweza ku-relate nao. Wakulima wa mihogo wanaona mazao yao yanakufa kwa sababu zisizojulikana na serikali ikatuma mwanasayansi wa botania, je mwanasayansi huyu anatajibu WHY au HOW? naona karuka swali.
 
We jamaa kwani kila kitu unachoandika hapa ni mawazo yako!?
Uneongea kuhusu relativity hayo ni mawazo yako!?
Hata hii issue ya sayansi hayo ni mawazo yako!?

Ndio maana watu wanaishi kwa kutegemeana. Kuna mkulima, Mwalimu, mfanyabiashara nk.
Sasa tukianza kila mtu atoe only mawazo yake bila references tutakuwa tunarudi kwenye ujima.

Ndio maana kuna vitabu.
Umeuliza maswali nimekupatia ufafanuzi, na kukueleza theory of relativity ilikuwa na experiments zake.

Sasa unaaza kujadili namna ya uwasikishaji wa mada eti mawazo ya watu vikundi nk!!!

Wewe leta maelezo kuhusu who science answer WHY question.

Kama unajaribu kurusha mistari katika mada ambazo unadai una utaalamu nazo ni lazima ujitosheleze angalau katika basics. Inaonyesha umesoma masoma ya sayansi kwa kufundisha na kwa kutumia models ambazo tayari zimeshafanyiwa kazi na kurahisishwa. Hivyo kwa upande wako unaweza kusema science inajihusisha na HOW.

Lakini kwa wale waliofanya groundbreaking discoveries katika science kama Newton, Einstein na wengine WHY was part of their work.
 
Mimi nilimwekea mfano ambao anaweza ku-relate nao. Wakulima wa mihogo wanaona mazao yao yanakufa kwa sababu zisizojulikana na serikali ikatuma mwanasayansi wa botania, je mwanasayansi huyu anatajibu WHY au HOW? naona karuka swali.
Twende taratibu sasa.
Kuna maswali mengi sana mwanasayansi huyo atajiulza.
WHEN, WHICH, WHAT, WHERE nk.
Maswali hayo yanalenga data collection.
Maswali hayo yata formulate maswali mengine.
Mwanasayansi atakachokifanya ni kuchukua sample mbalimbali na kupeleka maabara.
Hawezi akatoa reasons wakati ugonjwa au jambo halijulikani. Ndio maana hawezi akajibu WHY!!? Kama ugonjwa unajulikana utakuwa umefanyiwa experiment itakuwa simple tu Mzee. Atajibu WHY.

Hata hapa bado!?
 
Kama unajaribu kurusha mistari katika mada ambazo unadai una utaalamu nazo ni lazima ujitosheleze angalau katika basics. Inaonyesha umesoma masoma ya sayansi kwa kufundisha na kwa kutumia models ambazo tayari zimeshafanyiwa kazi na kurahisishwa. Hivyo kwa upande wako unaweza kusema science inajihusisha na HOW.

Lakini kwa wale waliofanya groundbreaking discoveries katika science kama Newton, Einstein na wengine WHY was part of their work.
Bro!! Tunabishana vitu simple mno.
Why ni swali pana mno aisee!! Sidhani kama unaelewa upana wake. Ninatamani uelewe!!!
Swali la WHY linataka utoe reasons.
Baada ya kujibu HOW ndio kidogo unaanza kuigusa WHY.

Ngoja nikupatie mifano ya uhakika kutokana na hao uliowataja.

Newton baada ya kufanya findings zake kuhusu kuanguka kwa apple na akaeleza hata mwezi nao unaanguka kutokana na gravitation nk.

But Einstein amekuja akakataa jambo hilo. Yeye kutokana na findings zake akaona sababu ya vitu kuvutwa ni kutokana na SPACETIME ni kama net kubwa imetandikwa kitu kikubwa kikadondoshwq katikati kitu kidogo kikidondoshwa pembeni kitakuwa kinavutwa.

Hapa ninachotaka kukuambia Newton alitupatia experiment za how lakini kujibu why! Bado ilikuwa philosophical vivyo vivyo Einstein katuonesha nature inavyooperate na tukapata formula lakini bado ni ngumu kutuambia WHY!?
 
Back
Top Bottom