Republican, Democrats (USA), Conservative, Liberal na Liberal Democrats (Uingereza) havina ukomo wa uongozi sawa na Chadema

Republican, Democrats (USA), Conservative, Liberal na Liberal Democrats (Uingereza) havina ukomo wa uongozi sawa na Chadema

Pamoja na kwamba nakubaliana na wewe LAKINI ndio kweli tujifunze kwa Rwanda na Uganda? Hao viongozi si ni sisi ndio tumewaweka madarakani? Sema PK hanaga shukurani tu but yule ni kijana wetu kabisa yaani
Ukiwa unataka kufanya kitu cha hovyo huwezi kukosa mtu wa kumtumia kama rejea yako. Tena tutasema na ni wenzetu katika EAC.
 
Na siku CCM kupitia machawa wao wakisema Uganda na Rwanda hawana ukomo wa Rais tuwasikilize na tuwaelewe.

Jinsi watu wa CHADEMA huwa wanapiga kelele juu ya maswala ya hii nchi unaweza kudhani ni watu makini kweli.

Hawa hawa wapambe wa Mbowe siku CHADEMA ikipewa madaraka ya kuongoza nchi, watakuja na mifano ya mbona Uganda na Rwanda hakuna ukomo wa urais.


Mfano wako hauna uhalisia.Usifananishe vyama vya siasa na nchi.kufananisha uongozi wa nchi na vyama vyakisiasa vinaweza ata kufutwa na nchi ikaendelea sio sawa.lakini ukiharibu mambo ya nchi,nchi inaweza kuingia kwenye machafuko na upotevu wa amani tukabaki vilema.Tujifunze kuiheshimu nchi yetu.
 
Wewe ni chama mbadala, unapaswa kuwa mfano kuanzia kwenye taasisi yako.

Kama umegoma kuuachia uongozi wa chama ukidai bado chama kinakuhitaji na hamna wa kutosha kushika nafasi ya mwenyekiti, huoni kama unawaambia watu siku wakikuamini utatumia ujanja huo huo kubadili katiba utawale mpaka ufe?

Chama mbadala kinapaswa kuwa safi na kufanya matendo ya mfano, kama hatutoona tofauti kati ya chama mbadala na chama tawala, hamna sababu ya kuwa kinyume na chama kinachoongoza.
Kwa kweli sijui hata nitakujibu vipi. Na hiyo font yako ndio kabisa.

Amandla...
 
Na siku CCM kupitia machawa wao wakisema Uganda na Rwanda hawana ukomo wa Rais tuwasikilize na tuwaelewe.

Jinsi watu wa CHADEMA huwa wanapiga kelele juu ya maswala ya hii nchi unaweza kudhani ni watu makini kweli.

Hawa hawa wapambe wa Mbowe siku CHADEMA ikipewa madaraka ya kuongoza nchi, watakuja na mifano ya mbona Uganda na Rwanda hakuna ukomo wa urais.



Mkuu tofautisha chadema na chawa wa mwamba kwa upande mwingine.

Hao ni aina za Lucas Mwashambwa na nduguye Tlaatlaah akiwaita jiwe vijana wa hovyo wasiokuwa na mchango wowote kwa taifa hili.
 
Mfano wako hauna uhalisia.Usifananishe vyama vya siasa na nchi.kufananisha uongozi wa nchi na vyama vyakisiasa vinaweza ata kufutwa na nchi ikaendelea sio sawa.lakini ukiharibu mambo ya nchi,nchi inaweza kuingia kwenye machafuko na upotevu wa amani tukabaki vilema.Tujifunze kuiheshimu nchi yetu.
Kwa nchi yetu chama ndio kinatawala, leo hii wanaCCM wakiamua kusiwe na ukomo wa urais WANAWEZA.

Leo CCM ikiamua tuwe na rais wa milele itakuwa hivyo tena kwa utaratibu wa kisheria kabisa.

Sasa kama baadhi ya wana CHADEMA na mwenyekiti wao hawaamini katika ukomo wa uongozi, ni nini kitawashinda wakipewa nchi wasirekebishe sheria na tukawa na rais wa muda wote?

Huwa nawashangaa sana watu wanaosema tutofautishe vyama vya siasa na nchi katika mambo ya uongozi.

Hivi ni wazito kiasi kwamba hamuelewi vyama vya siasa ndio vinaamua nchi iongozwe vipi?
 

Sio kitu kibaya kusema umeishiwa hoja mkuu.
Sio hivyo. Siko humu kubishana bila sababu. Kwa sababu hiyo sitakujibu. Ninachokushukuru ni kuwa haujatumia lugha ya kebehi au matusi katika kunijibu. Natumaini kuna siku tutaweza kubadilishana mawazo katika suala lingine lakini sio hili.

Amandla...
 
Kwa nchi yetu chama ndio kinatawala, leo hii wanaCCM wakiamua kusiwe na ukomo wa urais WANAWEZA.
Hakuna mtu anakataa hilo. Na wanaweza kufanya hivyo kwa sababu ya wingi wao Bungeni na sio kwa sababu Rais ni CCM.

Leo CCM ikiamua tuwe na rais wa milele itakuwa hivyo tena kwa utaratibu wa kisheria kabisa.
Kwamba wafute uchaguzi ili turudi tena kwenye siasa ya chama kimoja? Kinadharia wanaweza lakini in reality hawatathubutu maana itakuwa ni kutangaza wazi kuwa hamna demokrasia nchini. Hata nchi zenye mfumo wa kibabe wana vyama vya upinzani.

Sasa kama baadhi ya wana CHADEMA na mwenyekiti wao hawaamini katika ukomo wa uongozi, ni nini kitawashinda wakipewa nchi wasirekebishe sheria na tukawa na rais wa muda wote?
Hawataweza kwa sababu hamna jinsi wataweza kushinda urais na robo tatu za wabunge. Wakifika hapo tutawapinga kama tunavyo wapinga CCM.

Huwa nawashangaa sana watu wanaosema tutofautishe vyama vya siasa na nchi katika mambo ya uongozi.
Kwa sababu hauwaelewi. Kuongoza nchi kama chama cha siasa ndio kumetufikisha tulipo sasa.

Hivi ni wazito kiasi kwamba hamuelewi vyama vya siasa ndio vinaamua nchi iongozwe vipi?
Vyama vya siasa havina ubavu huo ndio maana kila baada ya muda inabidi vitafute kuhalalishwa na wenye nchi. Ukiona chama cha siasa kina uwezo basi ujue kuna tatizo katika Katiba yao.

Tofauti kubwa ni kuwa uongozi wa chama cha siasa unawajibika kwa wanachama wake tu, sio kwa nchi nzima. Ndio maana upigaji kura unaendana na uanachama sio uraia. Kwa sababu hiyo pool ya uongozi katika chama cha siasa inategemea wangapi wanaunga mkono sera zake. Kama ni chama cha upinzani, lengo lake kubwa ni kuchukua dola. Kwa sababu hiyo watu wanaoweza kukiongoza ni wale ambao wataweza kufanikisha lengo hilo. Na kwa vile hawa sio wengi kujiwekea mipaka kuhusu nani ataweza kuwaongoza ni kujifunga mikono. Ukomo unatakiwa uwekwe na wanachama. Wakiona mgombea hatawafaa wana haki ya kumtoa bila kujali kahudumu kwa miaka mingapi. Vile vile mwanachama yeyote anaejiona ana wito wa kugombea uchaguzi anatakiwa aruhusiwe kufanya hivyo ili mradi maslahi maana yameangaliwa.

Mimi simkubali Lissu lakini naamini kuwa ana haki ( hata wajibu) kufanya hivyo kama anaona chama chake kinaelekea kusiko. Ninachopinga ni kufanya juhudi za wazi za kumnyima Mbowe haki yake ya kugombea. Aidha, kutumia lugha za ulaghai na kebehi ( kwa mafumbo na kujificha) kufanikisha azma yake.

Pamoja na maneno mazuri ya Heche, hawana uwezo wa kutibu majeraha ambayo wamekisababishia chama chao. Kwa mfano lugha ya kusema kuwa watawashughulikia wale wachache ambao kwa mtazamo wao wamekifikisha chama kilipo ni ishara kuwa uongozi wao utakuwa wa visasi. Wakianza kwa kuwashughulikia Wenje, Ntobi na Yericko tutajua ni kwa sababu wamediriki kutofautiana nao. Hiyo haitaziba nyufa bali utaziongeza.

Mimi siishiwi hoja, Mkuu.

Amandla...
 
Singapore ilipata uhuru mwaka 1959. Waziri Mkuu wake wa kwanza alikuwa Lee Kuan Yew ambae alikaa madarakani kwa miaka 31 hadi mwaka 1990. Alikuwa Mkuu wa chama chake cha People's Action Party toka 1954 hadi 1992 hivyo hata alipopatikana Waziri Mkuu mpaya aliendelea na nafasi yake kwa miaka 2. Lee alikuwa mbunge wa jimbo lake toka 1955 hadi umauti ulipomchukua 2015, miaka 60. Faida ya yeye kuongoza kwa muda wote huo ni dhahiri.
Rais Hakainde Hichilema wa Zambia alizaliwa 1962. Amekuwa kiongozi wa chama chake cha UPND kuanzia 2006 mpaka leo. Alikgombea urais mara tano bila mafanikio mpaka aliposhinda 2021. Nae, kama mfanyabiashara mwenzake Mbowe, siasa zimemgharimu sana. Lakini hakukata tamaa na wafuasi wa chama chake hawakukata tamaa.

Amandla...
 
Retited. Tunza hata kidogo heshima uliyobakiwa nayo kwa watu wachache kuna mambo ukiongea watu wanasema hiiiii......
watu darasa la saba hapa JF hawanisumbui! "Naongea" na Ansbert, Kabendera Kabebdera na waandishi engine kama hao.....(and the like!). Kwani JF kuna nini? angalia posts zao utaona kuna tatizo kubwa la intellect ya wachangiaji.......... Walio wengi wenye akili wameachana na JF baada ya kutoka kuwa uwanja/platform ya great thinkers na kuvamia na watu kama wewe!
For your information, I will be abandoning JF soon!
 
Na siku CCM kupitia machawa wao wakisema Uganda na Rwanda hawana ukomo wa Rais tuwasikilize na tuwaelewe.

Jinsi watu wa CHADEMA huwa wanapiga kelele juu ya maswala ya hii nchi unaweza kudhani ni watu makini kweli.

Hawa hawa wapambe wa Mbowe siku CHADEMA ikipewa madaraka ya kuongoza nchi, watakuja na mifano ya mbona Uganda na Rwanda hakuna ukomo wa urais.


Kwani nchi ulizozitaja hazina chaguzi za marais?
 
Ukiwa unataka kufanya kitu cha hovyo huwezi kukosa mtu wa kumtumia kama rejea yako. Tena tutasema na ni wenzetu katika EAC.
Kama ambavyo Juma Mkamia alivopendekeza kwamba tuanze kuchaguana baada ya miaka 7 ili ajipendekeze kwa Magufuli! Nimekuelewa sana kaka
 
watu darasa la saba hapa JF hawanisumbui! "Naongea" na Ansbert, Kabendera Kabebdera na waandishi engine kama hao.....(and the like!). Kwani JF kuna nini? angalia posts zao utaona kuna tatizo kubwa la intellect ya wachangiaji.......... Walio wengi wenye akili wameachana na JF baada ya kutoka kuwa uwanja/platform ya great thinkers na kuvamia na watu kama wewe!
For your information, I will be abandoning JF soon!
Usiondoke. Bado unahitajika.

Amandla...
 
Zama hizi za sasa si za kuwa na chama kimoja kinaongoza peke yake..yaani kuanzia ma-veo, weo, ma-dc, Ma-rc, mawaziri nk siasa za sasa lazima ziwe jumuishi na shirikishi..kila kura iwe na nguvu ya matokeo, vyama vyote vinavyoshiriki uchaguzi na kupata idadi fulani ya kura lazima viwe na nafasi kwenye uongozi..mambo ya the winner takes all hayajatufikisha popote zaidi ya chama kukumbatia wizi, upendeleo, matumizi mabaya ya madaraka, ufisadi na ubaguzi wa kiitikadi..na hivyo si tu chadema, chama chochote kikipata ridhaa ya kuongoza peke yao hawawezi kubadilisha misingi ya uongozi wa nchi km wanavyotaka..ndio maana lazima yawepo mabadiliko ya katiba sasa!
Kibongo bongo winner takes all ndio inafaa, ukishaanza Mkuu wa mkoa chadema, mara Mkuu wa wilaya ACT, bas utaanzisha varangati
 
watu darasa la saba hapa JF hawanisumbui! "Naongea" na Ansbert, Kabendera Kabebdera na waandishi engine kama hao.....(and the like!). Kwani JF kuna nini? angalia posts zao utaona kuna tatizo kubwa la intellect ya wachangiaji.......... Walio wengi wenye akili wameachana na JF baada ya kutoka kuwa uwanja/platform ya great thinkers na kuvamia na watu kama wewe!
For your information, I will be abandoning JF soon!
Ha ha ha.... You are so pathetic. Why havent you abandoned yet? Yaani hao uliowataja ndo watu wakubwa kwako? Wewe utakuwa ndo Ntobi....
 
Huko tulikoiga siasa hizi za vyama vingi huo ndio utaratibu wao. na wana sababu za msingi.

Sababu hizo bado zina mashiko kwa Chadema.

Msikilize Ansbert ngurumo
Habari ya term limit ni uminywaji wa demokrasia. Wananchi wanahitaji kupewa nafasi kumchagua kiongozi wanayemtaka pasipo kuwekewa mipaka.

Tatizo kwa nchi zetu ni baadhi ya viongozi kutumia hila. Mbowe amekuwa tishio kubwa kiusalama kwa kila mtu aliyeonyesha nia ya kumng'oa uenyekiti, ndio mayowe tunayosikia leo toka kwake baada ya kubanwa na Lissu.
 
Back
Top Bottom