Narudia tena kusema kitu kile kile acha ulomolomo ,uliandika ujinga bila kufikiri ila hutaki kuona huu ukweli.
Pengine unaishi Dodoma na hukuwahi kujua au kuona gharama za kusafiri kwenda Dodoma zilivyo kubwa na zaidi ni risk sana Kwa sababu gani? Ili kupunguza gharama kidogo za kukaa Dodoma ,wengi walikuwa wanasafiri siku moja kabla ya usaili kwenda Dodoma Kwa wanaotokea Dar es salaam au mikoa iliyo karibu na Dodoma ,hapo risk inakuja pale gari limeharibika njia na uwezekano wa kufika Dodoma siku hiyo ili awahi usaili siku inayofata ni mdogo sana na huyu mtu Kuna uwezekano akakosa usaili. Au umepata kazi tayari hivyo hujui madhila yanatowakumbuka na gharama wanazokutana nazo wasailiwa.
Ukiona Kila mtu anapongeza huo mfumo jua kapitia gharama zisizoelezeka ,wewe unapokuja na gharama za bando wenye akili wanaona unaleta vioja kwenye mambo ya msingi. Hata utumie bando la 20000 ni nafuu kuliko kwenda Dodoma.
Mimi nimejibu kulingana na ulichoandika na nimegundua jambo Moja kubwa uliandika uroporopo ambao huwezi kutetea Kwa hoja