Ripoti madai ya sumu Mto Mara zina utata, zimetofautiana, wataalam wamezichambua

Ripoti madai ya sumu Mto Mara zina utata, zimetofautiana, wataalam wamezichambua

Tukiachana na hayo uliyo mention je kwanini ripoti zitofautiane?

Kuna mmoja katiyao ametudanganya? Kwanini atudanganye? Nani yuko nyuma ya huo uongo?
Umesomea nini ndugu yangu? Kama umesomea arts, siyo kosa lako.

Ile taarifa ya kwanza ilikuwa ni observation. Hii ya pili ni taarifa inayotokana na uchunguzi.

Na unapoanza uchunguzi, ni lazima uwe na hypothesis. Yawezekana kabisa hypothesis ilikuwa ni kuwa utando wa mafuta uliokuwa ukionekana juu, ukasema ni kemikali. Lakini baadaye uchunguzi ukaikataa hypothesis yako.

Jibu la uchunguzi ni uchunguzi wenyewe, siyo hypothesis au observation.
 
Ukweli ni kwamba hizo sumu zinatiririshwa kutoka mgodini, kwa maana nyingine hatua za kisheria zinapaswa kuchukuliwa...

NEMC wanatuabisha sana...
Wewe unajua mto uliko na mgodi uliko? Kuna siku ng'ombe watakufa Dodoma, watu watasema ni kwa sababu ya sumu za mgodi wa Barrick Buzwagi!!

Ujinga ni mzigo mzito kuliko mizigo yote, japo ujinga hauvunji mgongo.

Wanaotaka uchunguzi ufanyike tena wajiorodheshe, ikionekana ni wengi, iletwe timu ya wataalam hata kutoka nje, ufanye uchunguzi, lakini najua wanaotaka isemwe kuwa ni sumu za mgodini, jibu lisipokuwa hivyo, watasema Barrick wamehonga.

Tunaofanya na multinational companies, tunajua jinsi ilivyo ngumu kwa makampuni hayo kukupa hela ya hongo.

Ni rahisi sana kampuni inayomilikiwa na mtu mmoja au watu wachache kuliko hizo public companies.
 
Wewe unajua mto uliko na mgodi uliko? Kuna siku ng'ombe watakufa Dodoma, watu watasema ni kwa sababu ya sumu za mgodi wa Barrick Buzwagi!!

Ujinga ni mzigo mzito kuliko mizigo yote, japo ujinga hauvunji mgongo.

Wanaotaka uchunguzi ufanyike tena wajiorodheshe, ikionekana ni wengi, iletwe timu ya wataalam hata kutoka nje, ufanye uchunguzi, lakini najua wanaotaka isemwe kuwa ni sumu za mgodini, jibu lisipokuwa hivyo, watasema Barrick wamehonga.

Tunaofanya na multinational companies, tunajua jinsi ilivyo ngumu kwa makampuni hayo kukupa hela ya hongo.

Ni rahisi sana kampuni inayomilikiwa na mtu mmoja au watu wachache kuliko hizo public companies.
Mkuu samahani, naomba nikuulize kidogo, vipi unafahamu zaidi kuhusu "Chemical speciation"
 
Kiukweli Prof. huyu achunguzwe kwa possibility ya kuwa compromised!.
Kinyesi cha ngombe ni chakula cha samaki na ni soluble in water, hakuna kinyesi chochote cha ngombe kuua Samaki!.

Sii wengi wanafahamu jinsi makampuni makubwa ya madini yalivyo tayari to spend billions kujisafisha kuliko kushitakiwa kwa kumwaga sumu ardhini.

hawakuanza Leo, kwa wanaokikumbuka kisa cha mto Tigiti.

This is not the first time wataalamu wetu kuwa compromised. Ngoja na mimi nijipange kuandika bonge la IJ.
huko nyuma niliwahi kuuliza


Hivyo nashauri wataalamu wetu hawa wachunguzwe!.
P
Aisee....hii ripoti ya huu utafiti imezua maswali mengi zaidi, wakati ilitakiwa itoe majibu.

Inabidii hii ripoti ipingwe kwa utafiti sio maneno tu.
 
Umesomea nini ndugu yangu? Kama umesomea arts, siyo kosa lako.

Ile taarifa ya kwanza ilikuwa ni observation. Hii ya pili ni taarifa inayotokana na uchunguzi.

Na unapoanza uchunguzi, ni lazima uwe na hypothesis. Yawezekana kabisa hypothesis ilikuwa ni kuwa utando wa mafuta uliokuwa ukionekana juu, ukasema ni kemikali. Lakini baadaye uchunguzi ukaikataa hypothesis yako.

Jibu la uchunguzi ni uchunguzi wenyewe, siyo hypothesis au observation.
Kama kawaida yenu kukimbilia elimu ambayo haikidhi hata mahitaji.

Taarifa ya mwanzo ilisema matokeo ya kimaabara yamebaini kuna kiwango kikubwa cha mafuta. ( we uliyesoma sayansi mtu akisema matokeo ya kimaabara nadhani unamuelewa vizuri)

Taarifa ya pili haijazungumzia hata kidogo uwepo wa mafuta kwenye maji.

"Chanzo cha samaki kufa mto Mara chatajwa | Mwananchi" Chanzo cha samaki kufa mto Mara chatajwa | Mwananchi
 
Kwa maoni ya wengi yalivyo na angepatikana kiongozi wa kupenda kukurupuka, sijui saa hii tungekuwa tunazungumza lugha moja?
 
Juzi kati niliona memba humu JF akiandika juu ya taarifa za kemikali zenye sumu kutoka mgodini zilivyoharibu mazingira kwenye Mto Mara na kusababisha vifo vya samaki na pamoja maji kuwa meusi.

Baadaye habari hiyo ikasambaa na kuwa kubwa mwisho Serikali ikiingilia kati na kufanya uchunguzi kuhusu taarifa hizo.

Ripoti ya awali ikatolewa, wakagusia kuwa hakuna sumu bali ni mafuta ndiyo maana Oksijeni ikawa ndogo kwenye maji, wakasema wanaendelea kuchunguza kwa nini maji yamekuwa meusi.

……………………

NANUKUU KILICHOSEMWA SIKU HIYO…
“Akizungumza na waandishi wa habari Machi 12, 2022 jijini Mwanza, Mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria (LVBWB), Renatus Shinhu ametaja vijiji vilivyoathirika kutokana na uchafuzi huo kuwa ni Kirumi, Kwibuse, Marasibora, Ketasakwa na Ryamisanga.

“Uchunguzi wa kimaabara umeonesha mambo mawili ikiwemo kuwepo kwa kiwango kikubwa cha mafuta kuliko kiwango kinachokubalika kwa mujibu wa viwango vya ubora wa maji Tanzania (TZs 2068:2017),” amesema Shinhu.

MWISHO WA KUNUKUU


…………………….

Sasa baada ya ripoti hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Selemani Jaffo akaunda kamati maalum ya kitaifa kuchunguza chanzo cha mabadiliko katika Mto Mara yaliyosababisha maji ya mto huo kubadilika rangi na kuwa nyeusi.

Ndipo ripoti hiyo ya leo Jumamosi Machi 19, 2022 ikatolewa ikiwa na sababu nyingine tofauti, yenyewe ikisema kuwa eti wingi wa kinyesi cha ng’ombe na mkojo ndiyo sababu ya maji kuwa meusi na hatimaye kusababisha vifo vya Samaki wengi.

Inafikirisha kidogo, sasa kufikia hapo tumuamini nani, wale waliosema Samaki wanakufa kwa sababu ya mafuta kuwa mengi tena wakataja kabisa kuwa ni Dizel na Petrol, hawa wengine wanatuaminia kinyesi…

…………………….

NANUKUU RIPOTI YA KAMATI MAALUM YA KITAIFA ILIYOUNDWA NA SERIKALI
Akitoa matokeo ya uchunguzi Jumamosi Machi 19, 2022 mjini Musoma, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Samuel Manyele amesema kuwa hali hiyo imetokana na kuwepo kwa kiwango kikubwa cha kinyesi cha mifugo mtoni pamoja na uozo wa mimea ndani ya mto hasa mimea vamizi kama vile magugu maji na matete.

Amesema kuwa hali hiyo ilisababisha kupungua kwa kiasi kikubwa kiwango cha oksijeni ndani ya mto na hivyo maji kubadilika rangi na kuwa na harufu mbaya huku samaki wakikosa chakula na hivyo kusababisha vifo vyao.

MWISHO WA KUNUKUU


…………………………………..

Baada ya hapo nimewatafuta wataalamu wawili wa masuala ya ufugaji, mmoja ni kutoka Serikalini na mwingine ni sekta binafsi na kuwauliza kuhusu uwezekano wa samaki kufa wengi kutokana na kinyesi na mkono wa ng’ombe, hawa hapa wanafafanua…


Mtaalam wa kwanza
“Kwa kawaida kinyesi cha ng’ombe huwa ni sehemu ya chakula kwa Samaki na viumbe wengine kwenye maji, ndiyo maana kwenye mabwawa yanayofuga Samaki huwa ni kawaida kuona wafugaji wakitumia kinyesi hicho kwa ajli ya chakula cha Samaki.

“Ikitokea kwenye bwawa unalofugia kinyesi kikawa kingi kupitiliza kinaweza kusababisha kukosekana kwa oksijeni kutokana na kuziba njia kwa juu, hali hiyo ikiendelea kwa muda inaweza kusababisha samaki wakafa kweli.

“Lakini kwa sehemu kama mto au ziwa au bwawa kubwa mara nyingi kinyesi kikiwa kingi kinasambaa hivyo kinayeyushwa, tena kwenye mto au ziwa ni ngumu zaidi kusema kinyesi kimeziba na kukosekana kwa oksijeni.

“Ni ngumu kuona kinyesi kimeziba oksijeni kwenye mto wakati unajua maji ni mengi na kadiri kinyesi kinavyoingia kwenye maji ndivyo kinavyosambaa.

“Kingine ni kuwa kama kweli hali hiyo imetokea unatakiwa kujiuliza imetokea kwa muda gani, yaani imechukua muda mrefu kiasi gani hadi hali hiyo ikatokea, kama ni ndani ya muda mfupi basi hilo ni tatizo lingine, kama ni muda mrefu inamaanisha mlundikano huo ulitakiwa kuonekana mapema na siyo ghafla.

“Kitaalam ikitokea samaki wengi wamekufa kwenye mto au ziwa au bahari ndani ya muda mfupi basi hapo kuna tatizo, ama kuna sumu au kuna kemikali ambao haziendani na samaki.”


Mtaalam wa pili
“Inapotokea kuna magugu au majani mengi kwenye maji kisha kukawa na kinyesi kingi kinajaa kwenye maji, oksijeni itakosekana na itahatarisha maisha ya samaki.

“Hilo linaweza kutokea lakini iwe ni katika sehemu ndogo ya maji ambayo inakuwa na mrundikano wa vitu nilivyoeleza hapo juu, lakini kusema tu ni kinyesi na mkono, swali ni kuwa hali hiyo imetokea kwa muda gani yaani namaanisha mrundikano umechukua miezi mingapi?

“Kingine kinachonipa wasiwasi kuhusu hiyo ripoti ni kuwa maji yamekuwa meusi, hilo kitaalamu sina hakika nalo, ingekuwa imetokea kwenye kibwawa kidogo nisingekuwa na wasiwasi, lakini maji kuwa meusi kwenye mto kisa mikojo na kinyesi nafikiri nahitaji kujifunza zaidi kutoka kwa hao wataalam.”

Pia soma...
Madai ya sumu Mto Mara kutoka migodini, wananchi wazuiwa kutumia maji, kula samaki, uvuvi, Serikali yatoa tamko
Vifo vya Samaki Mto Mara: Kamati ya Dharura yaundwa kuchunguza Samaki wanaodaiwa kufa kwa Sumu
Mungu njoo itawale Africa
 
Juzi kati niliona memba humu JF akiandika juu ya taarifa za kemikali zenye sumu kutoka mgodini zilivyoharibu mazingira kwenye Mto Mara na kusababisha vifo vya samaki na pamoja maji kuwa meusi.

Baadaye habari hiyo ikasambaa na kuwa kubwa mwisho Serikali ikiingilia kati na kufanya uchunguzi kuhusu taarifa hizo.

Ripoti ya awali ikatolewa, wakagusia kuwa hakuna sumu bali ni mafuta ndiyo maana Oksijeni ikawa ndogo kwenye maji, wakasema wanaendelea kuchunguza kwa nini maji yamekuwa meusi.

……………………

NANUKUU KILICHOSEMWA SIKU HIYO…
“Akizungumza na waandishi wa habari Machi 12, 2022 jijini Mwanza, Mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria (LVBWB), Renatus Shinhu ametaja vijiji vilivyoathirika kutokana na uchafuzi huo kuwa ni Kirumi, Kwibuse, Marasibora, Ketasakwa na Ryamisanga.

“Uchunguzi wa kimaabara umeonesha mambo mawili ikiwemo kuwepo kwa kiwango kikubwa cha mafuta kuliko kiwango kinachokubalika kwa mujibu wa viwango vya ubora wa maji Tanzania (TZs 2068:2017),” amesema Shinhu.

MWISHO WA KUNUKUU


…………………….

Sasa baada ya ripoti hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Selemani Jaffo akaunda kamati maalum ya kitaifa kuchunguza chanzo cha mabadiliko katika Mto Mara yaliyosababisha maji ya mto huo kubadilika rangi na kuwa nyeusi.

Ndipo ripoti hiyo ya leo Jumamosi Machi 19, 2022 ikatolewa ikiwa na sababu nyingine tofauti, yenyewe ikisema kuwa eti wingi wa kinyesi cha ng’ombe na mkojo ndiyo sababu ya maji kuwa meusi na hatimaye kusababisha vifo vya Samaki wengi.

Inafikirisha kidogo, sasa kufikia hapo tumuamini nani, wale waliosema Samaki wanakufa kwa sababu ya mafuta kuwa mengi tena wakataja kabisa kuwa ni Dizel na Petrol, hawa wengine wanatuaminia kinyesi…

…………………….

NANUKUU RIPOTI YA KAMATI MAALUM YA KITAIFA ILIYOUNDWA NA SERIKALI
Akitoa matokeo ya uchunguzi Jumamosi Machi 19, 2022 mjini Musoma, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Samuel Manyele amesema kuwa hali hiyo imetokana na kuwepo kwa kiwango kikubwa cha kinyesi cha mifugo mtoni pamoja na uozo wa mimea ndani ya mto hasa mimea vamizi kama vile magugu maji na matete.

Amesema kuwa hali hiyo ilisababisha kupungua kwa kiasi kikubwa kiwango cha oksijeni ndani ya mto na hivyo maji kubadilika rangi na kuwa na harufu mbaya huku samaki wakikosa chakula na hivyo kusababisha vifo vyao.

MWISHO WA KUNUKUU


…………………………………..

Baada ya hapo nimewatafuta wataalamu wawili wa masuala ya ufugaji, mmoja ni kutoka Serikalini na mwingine ni sekta binafsi na kuwauliza kuhusu uwezekano wa samaki kufa wengi kutokana na kinyesi na mkono wa ng’ombe, hawa hapa wanafafanua…


Mtaalam wa kwanza
“Kwa kawaida kinyesi cha ng’ombe huwa ni sehemu ya chakula kwa Samaki na viumbe wengine kwenye maji, ndiyo maana kwenye mabwawa yanayofuga Samaki huwa ni kawaida kuona wafugaji wakitumia kinyesi hicho kwa ajli ya chakula cha Samaki.

“Ikitokea kwenye bwawa unalofugia kinyesi kikawa kingi kupitiliza kinaweza kusababisha kukosekana kwa oksijeni kutokana na kuziba njia kwa juu, hali hiyo ikiendelea kwa muda inaweza kusababisha samaki wakafa kweli.

“Lakini kwa sehemu kama mto au ziwa au bwawa kubwa mara nyingi kinyesi kikiwa kingi kinasambaa hivyo kinayeyushwa, tena kwenye mto au ziwa ni ngumu zaidi kusema kinyesi kimeziba na kukosekana kwa oksijeni.

“Ni ngumu kuona kinyesi kimeziba oksijeni kwenye mto wakati unajua maji ni mengi na kadiri kinyesi kinavyoingia kwenye maji ndivyo kinavyosambaa.

“Kingine ni kuwa kama kweli hali hiyo imetokea unatakiwa kujiuliza imetokea kwa muda gani, yaani imechukua muda mrefu kiasi gani hadi hali hiyo ikatokea, kama ni ndani ya muda mfupi basi hilo ni tatizo lingine, kama ni muda mrefu inamaanisha mlundikano huo ulitakiwa kuonekana mapema na siyo ghafla.

“Kitaalam ikitokea samaki wengi wamekufa kwenye mto au ziwa au bahari ndani ya muda mfupi basi hapo kuna tatizo, ama kuna sumu au kuna kemikali ambao haziendani na samaki.”


Mtaalam wa pili
“Inapotokea kuna magugu au majani mengi kwenye maji kisha kukawa na kinyesi kingi kinajaa kwenye maji, oksijeni itakosekana na itahatarisha maisha ya samaki.

“Hilo linaweza kutokea lakini iwe ni katika sehemu ndogo ya maji ambayo inakuwa na mrundikano wa vitu nilivyoeleza hapo juu, lakini kusema tu ni kinyesi na mkono, swali ni kuwa hali hiyo imetokea kwa muda gani yaani namaanisha mrundikano umechukua miezi mingapi?

“Kingine kinachonipa wasiwasi kuhusu hiyo ripoti ni kuwa maji yamekuwa meusi, hilo kitaalamu sina hakika nalo, ingekuwa imetokea kwenye kibwawa kidogo nisingekuwa na wasiwasi, lakini maji kuwa meusi kwenye mto kisa mikojo na kinyesi nafikiri nahitaji kujifunza zaidi kutoka kwa hao wataalam.”

Pia soma...
Madai ya sumu Mto Mara kutoka migodini, wananchi wazuiwa kutumia maji, kula samaki, uvuvi, Serikali yatoa tamko
Vifo vya Samaki Mto Mara: Kamati ya Dharura yaundwa kuchunguza Samaki wanaodaiwa kufa kwa Sumu
Maprofessor tunazidi kukosa heshima mbele ya jamii sababu ya michongo.
 
Professor wa mchongo
Sisi seer au mystic huwez kutundaanya hata kama hatuna taaluma hiyo. Kwa hisia za ndani huyo prof.. niliona uwongo hasa kwa namna alivyokuwa anaeleza .
 
Mto Mara ni mto mkubwa kuliko mingi iliyopo hapa nchini.

Mara River - Wikipedia

Mto upi hapa nchini wasiokunywa na kujisaidia humo mifugo?

Kwamba yaliyotokea mto Mara madhara ya mifugo kujisaidia mle?

Inatupa taabu sisi kama wananchi kulielewa hili na hasa kumbukumbu zikituelekeza kuliko na kadhia tata kama hizi huko siku za nyuma:



Ni vyema serikali ikatoa ufafanuzi wa kina kuhusiana na ripoti hii ikiwamo kufanyika kwa uchunguzi huru.
 
Ikumbukwe,
Ni professor uyu uyu akiwa mkemia mkuu wa serikali aliempima LISSU mkojo kwenye ile kesi yake ya uchochezi.[emoji4]
 
Kiujumla ametumia formula zilezile zilizeta matokeo ya papai kuwa na COVID. Waambie wavivu waandike ripoti utaonyeshwa Hadi chanzo Cha sumu.
 
Kwani Profesa Msukuma anasemaje? Mtazamo wake kwenye hili kwenye enzi hizi za utandawazi, utaalamu na teknologia ni upi?😳😲
 
Kiujumla ametumia formula zilezile zilizeta matokeo ya papai kuwa na COVID. Waambie wavivu waandike ripoti utaonyeshwa Hadi chanzo Cha sumu.

Hii nchi ngumu sana. Wenyewe wakijivunia - the end to justify the means.
 
Back
Top Bottom