Ripoti: Polisi ya Tanzania yashika namba 9 kwa Uweledi Afrika. Kenya haipo popote

Huu ni uchawa...
Mkuu, bora chawa anaweza kuvuka barabara na kuhesabu magari. Lakini huyu mwenzetu ni low zaidi ya chawa. Anajua kujibebisha na kujipendekeza inavyostahiki
 
Ngoja Tusubiri tuone huko mbele ya safari itakuwa hivi hivi au namna gani vipi !!!
🙏🙏💪
 
Uwongo wa mchana kweupe! Huwezi kulinganisha police force na police service! Haya mabumunda hapa yana uweledi gani hata PGO yao ni shida!!
 
Basi Afrika uonevu ni mkubwa sana.
 
Kumbe ni weledi nilidhani ni uweredi. Hapo sawa
 
HONGERA SANA tanpol.
 
Weledi kwa nani?
Labda kwa waliofanya utafiti, chama chetu na viongozi lakini siyo kwa raia
 
Hii ripoti wametumia vigezo gani kupima weledi na ubora wao?

==================================================
Jeshi la Polisi Tanzania linatajwa kuwa moja ya taasisi bora zaidi barani Afrika, utafiti kutoka Shirika la Afrobarometer umeonesha.

Kulingana na ripoti iliyotolewa hivi karibuni na shirika hilo, Jeshi la Polisi la Tanzania ni kati ya taasisi zinazozingatia weledi na taaluma barani Afrika kwa sasa.

Wakati jeshi la Tanzania likiorodheshwa kuwa kati ya taasisi bora zaidi barani Afrika kiweledi, hali ni tofauti kwa majirani zetu Wakenya ambapo jeshi la nchi hiyo limeorodheshwa kati ya taasisi zilizokosa weledi katika utekelezaji wa shughuli zake za kila siku.

Utafiti huo ambao ulifanywa kati ya mwaka 2021 na 2023 katika nchi 39 barani Afrika, linaangazia changamoto wanazokutana nazo raia wakati wa kufanya kazi na majeshi yao ya polisi.

Kulingana na utafiti huo, ni nchi tatu barani Afrika zilizojenga imani na majeshi yao ya polisi, kati ya 39 zilizojumuishwa kwenye matokeo ya utafiti huo.
Nchi zinazoshika nafasi za juu ni pamoja na Burkina Faso, Morocco na Benin, zikiwa na asilimia 68, 64 na 61 mtawalia, wakati Tanzania inashika nafasi ya tisa ikiwa na asilimia 53.

SOURCE: TRT AFRIKA​
 
Ningekua najua kingereza ningewaandikia ile kauli ya Donald Trump kuhus Africa
 
Kama akili za Watanzania ndo hizi ndo maana “Abdul” kawaweka mfukoni
 
Tanzania imetajwa kuwa miongoni mwa nchi 10 bora barani Afrika zenye askari polisi wenye weledi zaidi, kwa mujibu wa ripoti ya hivi karibuni ya Afrobarometer.

Hata hivyo, nchi jirani ya Kenya, imetajwa kuwa miongoni mwa mataifa yenye viwango vya chini vya taaluma ya polisi.

Hayo yamo katika ripoti ya Afrobarometer, iliyofanywa kati ya 2021 na 2023 katika mataifa 39 ya Afrika, ikitoa mwanga juu ya matatizo ambayo wananchi wanakabiliana nayo wanapoingiliana na utekelezaji wa sheria.

Weledi wa vikosi vya polisi kote barani Afrika umekuwa suala la kuchunguzwa kwa muda mrefu, ikizingatiwa jukumu lao muhimu katika kudumisha sheria na utulivu, kutekeleza sheria, na kulinda haki za raia.

Licha ya mafanikio kadhaa, nchi nyingi zinaendelea kukabiliwa na changamoto kama vile rushwa, matumizi ya nguvu kupita kiasi, na ukosefu wa uwajibikaji, jambo ambalo linaondoa imani ya wananchi.
 
Machadema watabisha 🤣🤣👇👇

View: https://www.instagram.com/p/DDuqCSwua3f/?igsh=MXdmN252MXV1amo3cw==
 
Haya ndo ya kuzungumzia kitanda cha jirani na hujawahi kulalia...tunawajua wenyewe hao🤔
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…