Ripoti ya ACT-Wazalendo juu ya ukiukwaji wa kutisha haki za binadamu katika uchaguzi wa Zanzibar

Ripoti ya ACT-Wazalendo juu ya ukiukwaji wa kutisha haki za binadamu katika uchaguzi wa Zanzibar

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Jana kiongozi mkuu wa chama cha ACT-Wazalenda ndugu Zitto Zubeir Kabwe ameitisha mkutano wa waandishi wa habari na kuelezea mambo mazito ya ukiukwaji wa haki za binadamu wa kutisha uliofanywa na vyombo vya usalama huko Zanzibar.

Akieleza waandishi wa habari yaliyojiri, Ndugu Zitto alitoa takwimu za watu waliouawa kwa kupigwa risasi, kubakwa, kuteswa, na kufanyiwa kila aina ya ukatili.

Wakati huohuo, Ndugu Zitto ameeleza kuwa ameandika barua kwa jumuia za Kimataifa ikiwemo jumuia ya Madola, EAC, AU na ICC na kuambatanisha ushahidi juu ya matukio ya kinyama kanbisa yaiyojiri katika uchaguzi huo

Pia ndugu Zitto amesema Katibu wao mkuu wa Zanzibar ndugu Mazrui hajulikani alipowekwa na vyombo vya usalama, hajulikani kama yuko hai au la, akasema kuwa ndugu Mazrui kabla hata ya kukamatwa na polisi alikuwa anatumia dawa kutokana na kuwa aifanyiwa operesheni siku chache nyuma na kwa hiyo tangu akamatwe zaidi ya wiki sasa hana hizo dawa

Wakati huo, Chama cha ACT-Wazalendo kimetoa ripoti ya awali ya taarifa ya ukandamizaji wa kutisha, utesaji na ukatili waliofanyiwa watu wa Zanzibar

Ripoti hiyo imesambazwa mitandaoni na iko wazi kwa kila mtu kujionea.

MY TAKE
Vitendo hivi vya kutesa na kuumiza watu bila hatia havitapita hivihivi, wote waliohusika watakuja kulipia ushenzi na ukatili waioufanya kwa wananchi.

Ni aibu kubwa sana kwa vyombo vya usalama kutesa na kuumiza wananchi wanaotumia haki yao ya msingi ya kikatiba kufanya siasa au kutaka kumchagua wanayemtaka.

Vyombo vya usalama viwaambie wananchi wa Tanzania, hawa wananchi waliouawa kwa risasi huko Zanzibar wana kosa gani waliloifanya la kustahiki kupigwa risasi na kupotezewa maisha yao?

Tunaunga mkono jumuia ya Kimataifa kuchunguza mauaji haya ya Watanzania wasio na hatia ili sheria ichukue mkondo wake kwa waliohusika!
 
Wahenga walisema"akili za kuambiwa changanya na zako"

Yaani viongozi wakuu wa vyama vya upinzani hawana hata makovu ya kipigo kutoka vyombo vya dola lakini ambao hawakuchangana na zao "wanavuna walichokipanda".

Hii ni bongo!
 
Zitto ni mnafiki, mchonganishi, asiye na msimamo, na mbaya ziadi ni mtu mwenye uchu wa madaraka
√ Mnafiki - alimsaliti mgombea Urais ambaye yeye mwenyewe alimwomba;
√ Mchonganishi - badala ya kutetea zao la mchikichi jimboni kwake amekuwa akitetea zao la korosho, mikoa ya kusini;
√ Kutokuwa na msimamo - badala ya kujenga chama chake, kwenye kampeni akadiriki kumuunga mkono mgombea Urais wa CHADEMA, chama kilichomfukuza uanachama; na
√ Alijiunga na ACT-Wazalendo na kujipachika cheo cha kiongozi Mkuu nje ya Katiba ya Chama wakati alipojiunga.
 
Zitto ni mnafiki, mchonganishi, asiye na msimamo, na mbaya ziadi ni mtu mwenye uchu wa madaraka
√ Mnafiki - alimsaliti mgombea Urais ambaye yeye mwenyewe alimwomba;
√ Mchonganishi - badala ya kutetea zao la mchikichi jimboni kwake amekuwa akitetea zao la korosho, mikoa ya kusini;
√ Kutokuwa na msimamo - badala ya kujenga chama chake, kwenye kampeni akadiriki kumuunga mkono mgombea Urais wa CHADEMA, chama kilichomfukuza uanachama; na
√ Alijiunga na ACT-Wazalendo na kujipachika cheo cha kiongozi Mkuu nje ya Katiba ya Chama wakati alipojiunga.
Bora mtu mchonganishi kuliko liuwaji
 
Wahenga walisema"akili za kuambiwa changanya na zako"

Yaani viongozi wakuu wa vyama vya upinzani hawana hata makovu ya kipigo kutoka vyombo vya dola lakini ambao hawakuchangana na zao "wanavuna walichokipanda"

Hii ni bongo!
1.Lissu ana makovu ya risasi 16.

2. Mbowe ana kovu la kuvunjwa mguu.

3. Rehema James Mkoha ana kovu la kupigwa na kuumizwa vibaya miguuni.

3. Salome Makamba ana kovu la kupigwa na vijana wa Katambi.

4. Ezekiel Wenje ana kovu la kuondokewa na ndugu yake kwa kuuwawa akiwa nyumbani kwake na green guard.

5. Ismail Jussa yuko Nairobi akiuuguza majeraha kwa kupigwa na kuvunjwa mguu.

6. Catherine Ruge ana kovu la kupigwa na polisi kwenye ofisi ya mkurugenzi wa halmashauri.

7.Dr Mahadhi Mmoto ana kovu la kupigwa na wahuni wa ccm huko Nachingwea.

8. Mazrui hajulikani alipo mpaka sasa alitekwa wakati wa uchaguzi.

Wenye makovu ni hao je niorodheshe na marehemu ?
 
Wahenga walisema"akili za kuambiwa changanya na zako"

Yaani viongozi wakuu wa vyama vya upinzani hawana hata makovu ya kipigo kutoka vyombo vya dola lakini ambao hawakuchangana na zao "wanavuna walichokipanda"

Hii ni bongo!
Mazurui ,Jussa hawana makovu?
Haupo seriaz kabisa wewe
 
1.Lissu ana makovu ya risasi 16.

2. Mbowe ana kovu la kuvunjwa mguu....
Tena mtu kama Rehema James wamemuonea sana aisee
Wamempiga dada wa watu asiyejua hata kutokana na bado wakapora ushindi wa kishindo
 
Back
Top Bottom