Ripoti ya CAG 2021-2022: TRC ilimkataa mzabuni wa Tsh bilion 616.4 na kumpa mzabuni wa tsh trilion 1.119 bila sababu za msingi

Ripoti ya CAG 2021-2022: TRC ilimkataa mzabuni wa Tsh bilion 616.4 na kumpa mzabuni wa tsh trilion 1.119 bila sababu za msingi

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Mzabuni wa bei nafuu alitenda Dola 263 Wakamchukua wa Dola 478.



Kwa Hali hii Masanja anapendwa kuwa Ofisini Kwa Ajili ya nini?

Hawa wezi wasiishie kufutwa kazi tuu Bali wafikishwe Mahakama, TAKUKURU mnafanya nini?

---
SHIRIKA la Reli Tanzania (TRC) linakabiliwa na changamoto katika utekelezaji wa ujenzi wa reli ya kisasa - SGR ambazo zinajumuisha gharama kubwa, upotevu wa fedha na majadiliano ya mikataba yasiyolinda maslahi ya taifa na hivyo kuathiri ufanisi na utelekezaji wa mradi huo.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere amesema TRC ilikataa zabuni mara mbili kwa ajili ya manunuzi ya vichwa vya treni na umeme, makochi ya abiria ambapo mzabuni aliyekuwa na bei ya chini alikuwa na dola za marekani milioni 263.4 na kufanya manunuzi yasiyo na ushindani kwa dola za marekani milioni 478.5.

Maamuzi haya yalisababisha ongezeko la dola za marekani milioni 215.4 sawa na ongezeko la asilimia 82. Hili ongezeko halikuwa la lazima.
 
Wizi kama huu sio wa kuchekea,TRC ya kadogosa mara kadhaa imekuwa ikilazimisha single source Kwa bei kubwa sana lakini wanawakalia kimya..

Nahisi.ccm Huwa inanifaika na wizi wa Mali za umma.
 
Mzabuni wa bei nafuu alitenda Dola 263 Wakamchukua wa Dola 478.



Kwa Hali hii Masanja anapendwa kuwa Ofisini Kwa Ajili ya nini?

Hawa wezi wasiishie kufutwa kazi tuu Bali wafikishwe Mahakama, TAKUKURU mnafanya nini?

---
SHIRIKA la Reli Tanzania (TRC) linakabiliwa na changamoto katika utekelezaji wa ujenzi wa reli ya kisasa - SGR ambazo zinajumuisha gharama kubwa, upotevu wa fedha na majadiliano ya mikataba yasiyolinda maslahi ya taifa na hivyo kuathiri ufanisi na utelekezaji wa mradi huo.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere amesema TRC ilikataa zabuni mara mbili kwa ajili ya manunuzi ya vichwa vya treni na umeme, makochi ya abiria ambapo mzabuni aliyekuwa na bei ya chini alikuwa na dola za marekani milioni 263.4 na kufanya manunuzi yasiyo na ushindani kwa dola za marekani milioni 478.5.

Maamuzi haya yalisababisha ongezeko la dola za marekani milioni 215.4 sawa na ongezeko la asilimia 82. Hili ongezeko halikuwa la lazima.
Ubora ulikuwa sawa, na je warranty ya matengenezo ilisema vipi? Pengine tuwekewe kila kitu wazi ili hata ikitokea lawama, iwe yenye kustahili.
 
Ubora ulikuwa sawa, na je warranty ya matengenezo ilisema vipi? Pengine tuwekewe kila kitu wazi ili hata ikitokea lawama, iwe yenye kustahili.
Ndio maana watajibu hizi hoja
 
Hii taarifa kubwa kabisa na ya kusikitisha iliyotolewa na CAG leo tarehe 29.03.2023 mbele ya Raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassani kwamba ununuzi wa mabehewa kuna ubadhilifu mkubwa ulifanyika ambapo zaidi ya mabilion ya fedha yamekwapuliwa.

Mimi kwa maoni yangu ni vizuri raisi pamoja kwamba amesema wampishe basi watu hao kunakila sababu ya kukamatwa na kuhojiwa kuhusiana na ubadhilifu huo, pesa zaumma haziwezi kuwa zinakwapuliwa halafu watu wapo na wanaona sawa kwa waliyoyafanya. hii haikubaliki hata kidogo.

FB_IMG_1680108134268.jpg
 
Back
Top Bottom