Ripoti ya Richmond Bungeni (FULL TEXT) na yatokanayo

Ripoti ya Richmond Bungeni (FULL TEXT) na yatokanayo

Hivi mheshimwa kabisa mkubwa wa mhimili mmoja wa dola, hivi kila kitu lazima wewe ujibu au useme?

Mkuu ameulizwa yeye, sasa wewe unategemea ajibu nani? Au unataka alete ujinga wa kusema mimi sio msemaji wa bunge.
 
Roma locuta causa finita. Maanake Roma (kwa wakatoliki) ikishatamka ndio mwisho wa mjadala. Sita (speaker) kisha nena Rostam alie na kusaga meno! File closed
 
WAPENDE WASIPENDE SITTA MWANAUME WA KUJIAMINI - SALAMU KWA SOPHIA KONDO a.k.a. SOPHIA SIMBA
 
Kwa mujibu wa sheria. hakuna taasisi yoyote yenye mamlaka ya kuhoji maamuzi ya Bunge. Bunge ni chombo cha uwakilishi wa wananchi. Na bunge lina kanuni zake na taratibu zake.

Kama Rostam amekuwa hakubaliani na maazimio ya Bunge, basi ana haki kabisa kimsingi kutumia taratibu za Bunge kulirudisha suala lake tena Bungeni lijadiliwe.

Vile vile taarifa au ripoti ya Bunge haiwezi hata kidogo kutumika mahakamani kama ushahidi . Ni lazima either PCCB au Polisi wafanye uchunguzi wao ndio upatikane uthibitisho wa kusimamisha kesi.

Nilikuwa najiuliza. hao majaji watasimama katika sakata hili kama nani?
 
Tena apewe Fast track process, moja kwa moja ndani...hakuna purpose ya kuhangaika na process...ni gaidi, should be arrested for treason kwa kuiba mali za wananchi

Mwenye nafasi ya kumwambia JK atusaidie, kwani RA anamfuko mkubwa kiasi gani kuiweka Serikali na watanzania mfukoni mwake?
 
Rostam anapasww kuwa yuko jela muda huu na hata nafasi ya kutaka ahopjiwe na majaji asingeweza kuitoa hapa ,
 
Nimechoka kumsikia... Igunga bila RA inawezekanaaaaa!
waamke, ila kwa wapiga kura hawa, mmh safari bao ndefu, mimi huwa nawaangaliaga Watanzania wenzangu, wasomi na wasio wasomi, waelewa na wasio waelewa, wajinga na waelevu, sijui kitu gani kilituroga, mimi naumia sana, wengi wanaogopa kuwaangusha hawa mapapa wa ufujaji, wanawapigia kura katika lindi kama hili la umasikini, Tanzania ,ni nani aliekuroga ?
 
RA, the king maker of Tanzania politics since 1990s....

Kwa kuwa CCM ni chama kilichochokaa baada ya kuachana na asili yake (jembe na nyundo), na kukumbatia matajiri aina ya RA kubakia madarakani (kuanzia serikali ya mtaa hadi uraisi) ni wakati sasa kuanguaka kwa njia ile ile waliyoacha asili yao...

If we can frustrate RA and go away then CCM should fall the same time to give as NEW HOPE with better nation for ALL.

Utawala uliopo ni zao la RA!!!Alituhadaa wotee kupitia mgombea wake..
Yupi muhimu kuondoa kwa ajili ya MABADILIKO YA KWELI????????
 
Rostam anapasww kuwa yuko jela muda huu na hata nafasi ya kutaka ahopjiwe na majaji asingeweza kuitoa hapa ,


Sitta amenipa raha sana. Hawa mafisadi wanataka kutuvuruga. Huyu RA kama anataka kuchunguzwa au anadhani alionewa aende mahakamani. Vinginevyo akae kimya kwa sababu nafasi ya kujitetea alikuwa nayo wakati kamati inafanya kazi zake au mbele ya bunge zima. Naona anataka kutumia pesa labda kuhonga majaji ili kudhalilisha bunge. Ni upuuzi mtupu kuongelea uchunguzi tena badala ya utekelezaji. Kama siyo upuuzi wake na EL kung'ang'ania walionewa na kumchanganya JK, hili suala lingeshakuwa historia. I am sick and tired with RA na his entire criminal and corrupt syndicate!!
 
People you must be joking. Jamaa amekamata bunge, mahakama na executive. Hata leo hii akisema aachie nyadhifa zote, yaani asiwe mjumbe wa CC, NEC na mbunge, still anaweza kuendelea na influence yake. Kama mnakumbuka Pablo Escobar aliwekwa gerezani lakini aliweza ku-operate effectively kutoka gerezani. Am sure for a person of RA calibre unaweza kushangaa anatengenezewa cell nuzri kuliko chumba cha Movenpick, akawa na simu yenye connection nzuri kuliko hata mimi wa oysterbay na akala chakula kizuri kuliko hata jamaa wa masaki, na biashara zake zikawa zinaendelea vizuri kuliko hata Mengi.

The guy needs to be eliminated from political sphere (not killing him), afanywe kama alivyofanywa Mrema. The question is who will start this, wakati wote wenye madaraka hayo wako mfukoni mwake?
 
Rostam anatafuta majaji ambao anahakika hatakosa mtu wake. Kila kona ya serikali ya JK kunamabawa ya Rostam, hata TAKUKURU. Nyuma ya ombi la Rostam anataka kuaminisha watu kuwa Bunge la Tanzania halina mamlaka juu yake. Na kwa hiyo yeye yupo juu ya watanzania wote kwa sababu Bunge ni mwakilishi wa Watanzania. Huyu mtu hafai na anadhalilisha nchi, mamlaka yote ya Tanzania na watanzania wote. Huyu ni mhaini, ni wa kukamata na kuweka kizuizini haraka kama alivyofanya Nyerere pale mfanyabiashara mmoja aliposema ameiweka serikali mfukoni. Watanzania tuamke ni mtu gani huyu wa kudharau mamlaka iliyowekwa na watanzania? Kwake yeye Bunge litakuwa na mamlaka pale atakapoweka Spika wake. Ndio maana walitaka kumfuta uanachama Spika wetu, mtetezi wa Watanzania. Pamoja na ubovu wako wa uongozi, JK huyu Rostam nawe mtu wa kwanza kwa wewe kuweka kizuizini kwa sababu anadharau mamlaka halali ya nchi pomoja na watanzania wote.

Mods naomba thread hii muiache kwa muda kwa sababu ya unyeti wa kichwa chake cha habari, halafu utaipeleka mahali pake.

Hicho unachosema ni sawa na kumwambia JK ajiweke kizuizini. Hata hivyo ni kitu ni rahisi sana kwa JK kujisweka ndani au hata kujinyonga kuliko kumgusa RA. Ulishawahi kuota umekamatwa na baunsa la miraba minne ya ukweli (a kind of gradiator)?? Hayo ndiyo yaliyomkuta ndugu yetu JK. Inabidi tumuonee huruma na kumuombea. He is restrained from every angle. I wish we could get someone to help and rescue him. May be the USA can ofer a helping hand by applying the Noriega strategy!
 
well.. anatakiwa afunguliwe mashtaka huyu Rostam sijui kwanini wanamremburia macho
Ramadhan Semtawa na Exuper Kachenje

SIKU moja baada ya mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, kutaka Tume huru ya majaji kuchunguza upya kashfa ya Richmond; Spika wa Bunge, Samuel Sitta amesema maamuzi ya Bunge yaliyofikiwa juu sakata la kampuni hiyo, hayawezi kuchunguzwa na mhimili mwingine wa dola.

Juzi Rostam alijitokeza kuzungumzia msimamo wake huo na gazeti hili, baada ya taarifa zisizo rasmi kumnukuu kwamba, alitoa hoja hiyo mbele ya Kamati ya Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi, ilipokutana na wabunge wa CCM mjini Dodoma.

Akizungumzia msimamo huo wa Rostam ambaye Kampuni yake ya Caspian inatajwa kufanya mawasiliano na Richmond, Spika Sitta alisema mwa mshangao: "Aaa...hakuna kitu kama hicho kinachoweza kufanyika!"

Ripoti ya Kamati Teule ya Bunge chini ya Dk Harrison Mwakyembe, haikuwataja Rostam na Edward Lowassa kuwa wamiliki wa Richmond, isipokuwa Caspian ya Mbunge wa Igunga, anuani yake ilitumiwa katika mawasiliano wakati wa mchakato huo.

Baada ya taarifa hiyo bunge lilipitisha maamuzi kufuatia ushauri wa kamati hiyo teule na kumpa Lowassa kujipima mwenyewe kuhusiana na madai yanayomhusisha na mchakato wa zabuni ya Richmnond.

Lowassa alijipima na kuangalia nafasi yake ya Uwaziri Mkuu; kisha akatangaza kujiuzulu huku Rostam akiwa kimya. Lakini siku za hivi karibuni aliibuka na kuishutumu ripoti ya Dk Mwakyembe kwamba ilipotosha ukweli.

Spika Sitta alisisitiza kuwa haingii akilini, kwa Rostam kutaka uchunguzi wa suala hilo ufanywe na majaji.

"Kwanza, labda nikwambie tu, maamuzi yaliyofikiwa na Bunge katika Richmond hayawezi kuchunguzwa upya na mhimili mwingine wowote wa Dola," alisisitiza na kuongeza:

"Tunazungumzia kumaliza suala la Richmond si kuanza upya, kama ana pesa zake (Rostam) za kulipa majaji, ni huko huko, lakini hilo haliwezekani".

Spika alisema ushahidi mbalimbali ulionyesha uhusiano wa mawasiliano ya mbunge huyo na Richmond kisha Dowans.

"Hivi mnataka ushahidi upi zaidi, ushahidi wa mawasiliano ulionyesha jinsi mtu huyu alivyokuwa akiratibu Richmond kisha Dowans," aliongeza Spika.

Mbunge huyo wa Urambo Mashariki ambaye aliingia katika kiti cha uspika na kauli mbiu ya Kasi na Viwango, alisema: “Kwanza serikali pia haina pesa za mchezo. Yaani sasa hivi zitoke pesa nyingine kuchunguza Richmond wakati wananchi wana matatizo makubwa kiuchumi na kijamii".

Alihoji kwamba; Richmond ilichunguzwa na watu wakapewa nafasi kujitetea, lakini hawakufanya hivyo sasa wanataka nini?


Kuhusu tuhuma za kuileta Richmond, alisema ni upuuzi kwani zipo barua hata 20,000 ambazo aliziandika akiwa Mkurugenzi Mtendaji (TIC), kuhusu wawekezaji mbalimbali.

"Haingii akilini hata kidogo, hivi wewe (alimtaja mwandishi) kama tulikutana mwaka 2000, halafu tukaachana, ukija kufanya ujambazi leo na mimi nitakuwemo?" alihoji. (somo katika mantiki-MM)


Alikiri ni kweli aliwahi kuandikia barua Richmond kwa ajili ya kufunga bomba la mafuta la Mwanza, kwa ushirikiano na akina Elisante Muro, lakini kampuni hiyo ilibainika kuwa haiwezi kazi.

Richmond iliwahi kukataliwa na Wizara ya Nishati na Madini kufunga bomba hilo mwaka 2004, msimamo ambao ulitolewa na Kamishna wa Nishati, Bashir Mrindoko.

Spika alifafanua zaidi akisema: "Ningeweza kuhusika au kuwajibika kama kashfa hiyo ingetokea katika mradi wa bomba la mafuta," alisema na kuongeza:

"Kampuni ilikwishabainika kuwa haina uwezo, wakaileta tena, wakaipokea na kuipigia debe ipate tenda wakati ilishakataliwa katika mradi wa bomba la mafuta. Eboo..!"

Alipoulizwa kuhusina na hoja ya Rostam ya kutaja achanguzwe na majaji watatu, Wakili wa Mahakama Kuu, Bob Makani, alisema anashangazwa na kauli yake (Rostam) kutaka kuundwa tume ya majaji kuchunguza upya kashfa hiyo.

"Namshangaa Rostam, yeye ni nani mpaka anataka achunguzwe na majaji? Jamani tuheshimu Bunge, tuheshimu kamati za Bunge na maamuzi yake," alisema Makani.

Makani ambaye pia ni Mwenyekiti mstaafu wa Chadema alisisitiza jana akisema: "Yeye (Rostamu) ajitetee tu, hawezi kusema iundwe kamati ya majaji. Majaji ni watu wazito, hawawezi kumchunguza yeye."

Alisisitiza kuwa, mbunge huyo anapaswa kuheshimu maamuzi ya Bunge.

"Lazima kamati za Bunge ziheshimiwe, ninachosema yeye ajitetee tu kwa tuhuma zake na si kutaka iundwe kamati ya majaji," alisema Makani alisisitiza.

Juzi Rostam, akijibu maswali ya gazeti hili kuhusu taarifa hizo alizozitoa mbele ya kamati ya mzee Mwinyi, alithibitisha na kusema mbali na kuchukuliwa hatua za kisheria, endapo tume hiyo huru ya majaji itabaini kuwa anahusika na ufisadi wowote wa Richmond; afukuzwe katika nafasi zote anazoshikilia katika chama (CCM) na Bunge.

Rostam ni mjumbe wa Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM; lakini amekuwa akitajwa kama mmoja wa vigogo walioleta kampuni ya Richmond yenye taarifa tata za kutoka Costa Rica na Marekani na kuwezesha kusainiwa kwa mkataba kati yake (Richmond) na Tanesco Juni 23, 2006.

Lakini baada ya kusakamwa kwa muda mrefu, alipopata nafasi katika kikao cha kamati ya Mzee Mwinyi na wabunge wa CCM, ilidaiwa kuwa Rostam alizungumzia kuundwa kwa tume huru kuchunguza kashafa nzima ya Richmond kwa madai kumba, Kamati teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk Mwakyembe ilipotosha.

Hata hivyo, katika majibu yake kwa gazeti la Mwananchi, baada ya kuwasiliana naye kwa kumtangulizia maswali kuhusu ukweli na mantiki ya kauli hiyo, alisema hawezi kuzungumzia ya kikao cha CCM, lakini ana maoni ya kuhusu sakata la Richmond.

"Msimamo wangu tangu Tume Teule ya Bunge itoe taarifa yake bungeni uko pale pale. Ripoti ilijaa upotoshaji na uongo. Nilitaka kuzungumza bungeni nikazuiwa," alisema.

Tangu sakata hilo litokee bungeni Februari 2008, kumekuwa na mvutano kati ya Bunge na Serikali katika utekelezaji wa maazimio yaliyofikiwa, ikiwa ni pamoja na kuwachungulia hatua maafisa wote wa serikali walioshiriki kwenye uzembe wa kupisha zabuni ya Richmond.

Source: Mwananchi
 
SIx anamjua fika RA na mafisadi wengine na ninadhani anajua mipango yote inayofanyika kuwasafisha mafisadi, na anajua RA aliposema ahojiwe na majaji ni nini kingelifuata baadaya hapo, ndo maana amepuuza hoja za RA. Yawezekana majaji walishapangwa.
 
Back
Top Bottom