Mara baada ya kuahirishwa kikao cha Bunge jana jioni, Waziri Mkuu aliitisha kikao cha Mawaziri na Manaibu wao akidai ni kikao cha KIKAZI.
Katika kikao hicho aliwaambia kwamba serikali ilikua na nia njema katika suala zima la Richmond na kwamba mawaziri wanaothubutu kushabikia ripoti ya Richmond watajuta na itawagharimu. Akawaambia watumie nafasi zao "Kuwaelimisha" wabunge wote kuhusu nia njema ya serikali katika Richmond ili wasiishambulie. Wanasema aliingia akiwa hana raha na alipotoka wenzake walibaki wameduwaa na wakitafakari kwamba wanaambiwa watetee ripoti ambayo hawajui inasema nini!
Wakasema wanasubiri waione ili wajue ni wapi imekosewa ndipo wajue nini cha kusema, lakini hawawezi kujadili ama kutetea HEWA kwani na wao ni Wabunge ambao wametumwa na wapiga kura wao na hawana UHAKIKA na nafasi za UWAZIRI bali UBUNGE ndio walikotumwa. HATA HIVYO wakaambiwa kwamba SERIKALI HAITAWASILISHA TENA LEO ripoti ya Richmond katika kikao cha wabunge wa CCM bali itawasilishwa kwa wabunge wote na kujadiliwa. LOLOTE linaweza kutokea kati ya LEO (Jumanne) NA KESHO (Jumatano) siku ambayo JK alitoa nafasi ya mwisho kwa wabunge wa CCM KUWATOSA Mawaziri wanaoona kuwa ni MZIGO kwao.
Hapa Dodoma kuna TENSION ya hali ya juu
Na ifuatayo ndiyo ripoti ya kamati ya kina Mwakyembe: