Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
...................mwakyembe Is Always Good..na Kabla Ya Mawaziri Kutajwa Wakati Ule Alikuwa Akijua Angekuwamo....jk Alimvuta Mtandao Kuogopa Asijiunge Kwa Mwandosya...ila Nasgangaa Kwa Nini Akawa Mtandao Matumaini..kati Ya Wana Mtandao Original Kuna Ambaye Haziivi.....
Katika Historia Ya Bunge Sijawahi Kuona Ripoti Iliyokuwa Nzito Namna Hii Kwa Uwazi Wa Kila Kitu...nina Imani Hata Spika Na Waziri Mkuu Hawakujua Ingesomwa Kavu Kavu Namna Hii..
Sasa Ndio Mtaona Kwa Nini Spika Alikuwa Akijaribu Kuikwepa Isisomwe ..alikuwa Ame Pre View Akaona Ni Motoo..
Kwa Analysis Ya Haraka Ujasiri Alioonesha Mwakyembe Inaonekana Una Baraka Za Mkuu....kaamua Kujisafisha ...mnajua Jk Is Always A Good Politician...nitoke Vipiii????...sasa Kwa Muda Tutasahau Za Bot..alafu Baada Ya Hili ...akiwaletea Na Single Iliyopo Jikoni Ya Tume Ya Jaji Bomani Aka Zitto Commetee..itakuwa Funika Bovu ..na Itazima Yote Haya...mtakuwa Na Mengi Ya Kumshabikia Sterling Jk Mwaka Huu...hadi Mwisho Wa Mchezo....
Kwa mara ya kwanza kuanzia kuanzishwa kwa bunge la vyama vingi Tanzania. Nimeshuhudia mbunge shujaa kutoka chama tawala akielezea, kinaga ubaga, mapungufu ya serikali ya chama tawala, katika bunge bila ya kujali maslahi ya chama tawala.
Dr. Mwakyembe anstahili kila sifa iwe kutoka kwa wapinzani, chama tawala, au wasio na chama chochote cha kisiasa. Kwani amejitowa muhanga kwa ajili ya wananchi wote wa Tanzania.
Leo, Dr. Mwakyembe amefunguwa ukurasa mpya wa siasa Tanzania, kwa mara ya kwanza serikali inaanikwa madhambi yake hadharani na mbunge wa chama tawala.
Heko Dr. Mwakyembe, nakuombea Mwenyeezi Mungu akulinde na maadui na wote uliowa-wafichuwa wana kila sababu ya kukufanyia uadui.
Mimi naona kwa sasa hongeza ziende kwa Mwakyembe na kamati yake, they have done their job without fear or favour. JK nitampongeza kama recommendations zilizotelewa atazifanyia kazi bila kumuangalia mtu usoni. Nitaboreka sana kama huu mpira nao ataamua kuwatupia PCCB, Polisi na Mwanasheria Mkuu, he needs to make a decision now.
Kwa upande mwingine, nadhani sasa wabunge wetu wameamka na hawataki tena kutumika kama rubber stamp which is a good thing kwetu walalahoi.
Tusimlaumu Hosea wala msabaha.hawa wote walipata Maelezo kutoka kwa Bwana Mkubwa<ndanda Lowassa E.N Al fasadi>
Huyu Dr Mwakyembe ninamjua vyema na ninaweza kutoa opinion yangu kuwa ni mbovu tu amekuwa akisapoti ufisadi na wizi wa ccm kinafiki underground.
Alikuwa wapi wakati kina Shivji na wasomi wengine wakichambua mikataba ya madini na suala la kufukuzwa zitto bungeni. This guy amekuwa ndio source ya magazeti ya mwizi na mkoloni Rostam Aziz kwa kutoa vigezo vya kisheria ambavyo vinapindishwa ili kutetea serikali.
Mwakyembe hafai kabisa na kuwamo kwake kwenye hii kamati ni ushahidi tosha kuwa huu ni usanii Kikwete anacheza hapa
Wanasheria wasomi wengi Tanzania walipondea hadharani issue ya bunge kufukuzwa bungeni na uhalali wa Buzwagi, huyu the so called rebel Mwakyembe alikuwa wapi?
Uko Kyela Mwakyembe wanamwona kama msanii tu,jimbo limemshinda na naona mwaka 2010 kazi ipo na ndo maana ameanza kujipendekeza kwa mwungwana....Mwakyembe sio yule wa zamani naona siasa zimemshinda na ameshindwa kujifunza toka kwa Mwandosya pamoja na kukaa naye kwa karibu sana,hana msimamo na ameanza kuunga mkono mwungwana.
na hawa kina Mwakyembe, is all that we have, Mzindakaya the former real leader wa kutotishika na serikali, sasa amekuwa a compromise, kaput finish wamepa hela kidogo that was it,
Mtanzania, bwana usianze kunitega ndugu yangu. Majina yao hayakutajwa hadharani na vyombo vingine vya habari kwa sababu ya nafasi zao na mimi niliombwa kuheshimu hilo na ninaheshimu. Ila nakuahidi endapo yatatokea mabadiliko ya Baraza hilo na wakawekwa nje kama wao wenyewe wanavyotarajia basi I'll be at liberty kuwataja
Hizo ni comments ya watu then ukisoma comment zao za leo kuhusu Dr. HM unamsifia sana.Mwakyembe anabadilika sana siku hizi, ila inaonekana anaenda zaidi kwenye usanii kuliko kwenye usmart wake uliomjenga all these years