Ripoti ya Richmond Bungeni (FULL TEXT) na yatokanayo

Ripoti ya Richmond Bungeni (FULL TEXT) na yatokanayo

What makes "usalama wa Taifa" any better than "heshima ya serikali"?

Si tumeona jinsi wizi wa BOT/ Meremeta ulivyotaka kuhalalishwa kwa sababu za "usalama wa taifa", kwa nini tuamini any blank statement kuhusu withholding information based on "usalama wa taifa"?
 
hahaha umeconcrude then unataka jibu dah!mkuu hii kali.
Lakini kwa kifupi kazi aliyo fanya Mwakyembe ni kubwa sana na ni nzuri kwani ukumbuke kuwa TAKUKURU waliisafisha RICHMOND na wakazima kabisa uvumi.
LAkini huyu jamaa akafumua tena lakini amebakiza mkia ambao nao utamaliziwa hivi karibuni ni kipolo tu usiwe na hofu yatafumuka sana na zaidi ya hayo hivi punde.
 
Nimesoma makala ya mwandishi mmoja nikakutana na hili kwa kweli Mwakyembe kama ni kukosea hapa ulikosea sana.Inakuwaje anasema kuwa 'walificha baadhi ya mambo kulinda 'heshima' ya serikali?'.Naomba nieleweshwe kidogo hapa.Ni heshima gani hii serikali inayo kama siyo ujinga.Angesema wanaficha baadhi ya mambo 'kulinda usalama wa taifa'hapo angeeleweka japo kidogo.
Ni bora mheshimiwa huyu ambaye siku za karibuni amejizolea sifa kemkem kama shujaa wetu yeye na kamati yake kufafanua hii kauli tete.
Hivyo basi hatutashangaa hata pale mmoja wa 'majeruhi' mmoja wa kisiasa kudai kulikuwa na uwezo wa 'kuchomekea' baadhi ya mambo ili kuhalalisha makosa ya baadhi ya waheshimiwa waliotuhumiwa na kamati hiyo?
Mheshimiwa kwa niaba ya wakereketwa wengi tunakuomba utoe ufafanuzi wa ziada kuhusu kauli yako.

Unaposema kwa niaba ya wakereketwa wengi unamu-inlude na nani?! Nani unataka apoteze muda wake kumwelewesha mtu mwenye akili yenye uzembe wa kufikiri mpaka atafuniwe kila kitu?!

Kwa taarifa yako, hakuna aliyetayari kuingizwa kwenye kundi lako la wenye mtindio wa ubongo. Waachie wenye akili inayojishughulisha wasonge mbele na Mwakyembe wao, kwani wao walishamwelewa kamanda wao.
 
hahaha umeconcrude then unataka jibu dah!mkuu hii kali.
Lakini kwa kifupi kazi aliyo fanya Mwakyembe ni kubwa sana na ni nzuri kwani ukumbuke kuwa TAKUKURU waliisafisha RICHMOND na wakazima kabisa uvumi.
LAkini huyu jamaa akafumua tena lakini amebakiza mkia ambao nao utamaliziwa hivi karibuni ni kipolo tu usiwe na hofu yatafumuka sana na zaidi ya hayo hivi punde.

Hivi siku hizi humu JF si ruhusa ku air out your opinions,kuhabarisha ama kuuliza?Please give me a break.
 
I was just airing out my opinion on what I thought he was very much mistaken.

Kama ulikuwa unatoa maoni yako mbona uliwahusisha na watanzania wengine kwamba wanahitaji kueleweshwa kama wewe??!!!!! Kwani tulikwambia hatujamwelewa kamanda wetu Mwakyembwe?!!
 
Mwakyembe anapoficha mambo kulinda ‘heshima ya serikali'

Chesi Mpilipili Julai 2, 2008
Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo


KUNA mambo kadhaa yanayofanywa na viongozi wa nchi hii ambayo ni kielelezo tosha cha jinsi kulivyo na ombwe la watu wanaostahili kweli kuwa na kuitwa viongozi wa wananchi.

Ni mambo ambayo ni kielelezo halisi cha jinsi viongozi wetu walivyo tayari kuweka kando maslahi ya waliowachagua kushika nyadhifa walizo nazo iwapo kwa kufanya hivyo watakuwa wanapalilia maslahi yao kwa kwa mamlaka za juu zenye nguvu zaidi kuliko wapiga kura wao.

Naomba nizungumzie matukio mawili tu ya hivi karibuni kama mifano hai. Matukio haya yametokea kwenye nyanja mbili tofauti; lakini zinazohusiana na maisha ya kila siku ya Watanzania. Siasa na michezo.

Tuanze na lile la michezo. Siku chache zilizopita kulikuwa na taarifa za mgogoro mdogo wa viongozi kwenye moja ya timu mbili kubwa za soka, ukubwa ambao sio lazima uwe ni kutokana na usakataji wa kabumbu mahiri wa timu hizo.

Mgogoro huu ulianza pale uongozi wa klabu hiyo ulipofanya kilichoelezwa kuwa ni kumsimamisha mweka hazina wa klabu hiyo kutokana na makosa ambayo hayakuwekwa wazi zaidi ya kusemwa kuwa ni 'kuvunja kanuni za uongozi.'

Taarifa hii ya uongozi wa klabu ikafuatwa siku chache baadaye na taarifa kutoka kwa mweka hazina wa klabu ambaye pamoja na mambo mengi alisema kuwa anasubiri barua rasmi kutoka kwa viongozi ili na yeye 'alipue mabomu'!

Kiongozi yule wa karne ya ishirini na moja wa klabu yenye mamilioni ya wanachama, wapenzi na mashabiki akasisitiza kwamba alikuwa na mengi tu ya kuyasema kuhusiana na viongozi wenzake na angeyasema mara tu baada ya kupata barua rasmi ya kusimamishwa!

Kama vile haitoshi, siku chache baadaye katika kile wengi walichoona kuwa ni kutafuta huruma ya wapenzi wa klabu hiyo, kiongozi huyo aliibuka tena na kudai kuwa alikuwa ameandika barua ya kuomba aruhusiwe kukarabati uwanja wa klabu hiyo ambao ulikuwa mahututi lakini alikuwa hajapata jibu kutoka kwa viongozi waliomsimamisha!

Kwangu mimi, na bila shaka kwa wapenzi wengi wa michezo nchini, hiki kilikuwa ni kilele cha unafiki. Huyu alikuwa ni kiongozi wa muda mrefu tu kwenye safu za uongozi za klabu hiyo ya soka na kama angekuwa na nia ya kweli ya kuukarabati uwanja wa klabu yao angeweza kufanya hivyo pengine bila hata kuhitaji kuomba ruhusa kwa mtu zaidi ya kutoa taarifa tu!

Lakini alikuwa amesubiri hadi wenzake walipomsimamisha uongozi ndipo akaona ule ndio ulikuwa muda muafaka si tu wa yeye kukarabati uwanja wa timu yake bali zaidi mno kuwatangazia wanachama jinsi alivyoandika barua kwa viongozi wenzake ili kupewa amana hiyo lakini alikuwa hajajibiwa!

Hilo ni moja. Kubwa zaidi lilikuwa lile la kuwaambia wanachama kuwa alikuwa na mambo mengi ya kusema kuhusiana na uozo uliomo kwenye uongozi uliomsimamisha lakini alikuwa anasubiri kwa hamu uongozi huo umpe rasmi barua ya kumsimamisha ili na yeye alipue mabomu!

Tatizo la viongozi wengi wa nchi hii ni kuwachukulia Watanzania kuwa ni maamuma wasiojua kuchanganua mambo. Haikuhitaji akili za ziada hapa kung'amua kuwa alichokuwa anafanya kiongozi huyu ni kutetea unga wake tu kwa kuwatingishia kibiriti viongozi wenzake na haikuwa kwa ajili ya manufaa ya klabu na wanachama wake.

Kwa maana nyingine, kiongozi huyu aliyechaguliwa na wanachama wa klabu alikuwa anamfahamu uozo uliokuwa ndani ya safu ya uongozi wa klabu yao lakini alikuwa anasubiri atofautiane na viongozi wenzake kwanza ndipo aone umuhimu wa kuwaambia wanachama juu ya uozo uliopo kwenye uongozi wa klabu yao!

Na hii pia iwe mpaka apewe barua ya kusimamishwa kazi kwanza ndio aumwage uozo huo hadharani. Bila barua, uozo huo ungeendelea kuwa siri yake! Hawa ndio viongozi wetu wa michezo.

Tuhamie kwenye siasa. Wakati kashfa ya EPA ilipoanza kushika kasi, taarifa za baadhi ya magazeti zilituambia kuwa kuna kiongozi ambaye alikuwa anasema kuwa iwapo angetajwa tu kuhusika na kashfa hiyo basi asingekubali kwenda na maji peke yake. Angekufa na mtu.

Kwa maana nyingine ni kwamba kiongozi huyu angetaja majina ya wahusika wa kashfa hiyo iwapo tu yeye angetajwa kuhusika. Kama wasingemtaja, basi, naye asingewataja na kwa maana hiyo Watanzania wanaosubiri kwa hamu kubwa majina ya wahusika hao, watasubiri mpaka wachoke.

Kwa vile hizi zilikuwa ni taarifa za magazeti ambazo hakuna jina lililotajwa, naomba tuziache kama zilivyo na badala yake tuhamie kwenye yale yaliyotokea majuzi pale mjini Dodoma kwenye kikao cha Bunge kinachoendelea huko sasa.

Wakati anachangia hotuba ya bajeti ya ofisi ya waziri mkuu, mwenyekiti wa kamati ya Bunge iliyoundwa kuchunguza utaratibu uliotumika hadi kampuni ya Richmond kupewa tenda ya kufua umeme, Mh. Dk. Harrison Mwakyembe ametoa kauli tete ambayo kwa hakika imewachanganya watu si haba.

Kwanza, Mh. Mwakyembe alieleza kushangazwa kwake na wabunge waliokuwa wanatoa hoja za kuwasafisha watuhumiwa wa kashfa ya Richmond na kuwataka kama hawakubaliani na uchunguzi wa kamati yake, basi, wavunje kanuni husika za Bunge ili mjadala wa Richmond urudishwe tena Bungeni kujadiliwa upya.

Akaenda mbali zaidi kwa kusema kuwa iwapo mjadala huo utafunguliwa tena, basi, kamati yake ingeyasema hata yale ambayo kamati yake ilikuwa imeficha kuyasema ili kulinda heshima ya Serikali iliyo madarakani!

Hii kwa hakika ilikuwa ni kauli nzito na ya kushitua kutoka kwa mtu ambaye Watanzania walio wengi wanamuona ni shujaa kutokana na kuongoza kamati iliyotoa taarifa iliyosababisha waziri mkuu na mawaziri watatu kujiuzulu kwa mpigo, 'tetemeko' ambalo halijawahi kutokea nchini.

Binafsi, nimejikuta nikiifananisha kauli hii na ile ya yule kiongozi wa timu kubwa nchini aliyesema kuwa anangoja apewe kwanza rasmi barua ya kusimamishwa uongozi na viongozi wenzake ndipo na yeye ataje uozo ulio kwenye uongozi huo!

Tungeelewa iwapo Mh. Mwakyembe angesema kuna mambo waliamua kuyaficha kwa vile kama wangeyasema yangeweza 'kuhatarisha usalama wa taifa letu'. Hili tungekubaliana nalo. Lakini 'ili kulinda heshima ya serikali'?

Ni kauli ya utata ambayo bado najitahidi kujipa matumaini kwamba pengine ilimtoka tu kwa bahati mbaya Mh. Mwakyembe kutokana na jazba aliyoonyesha kuwa nayo kama hotuba yake ilivyoonyesha na hakufikiria madhara yake pale wananchi watakapoanza kuichambua.

kwa hakika, kauli ya Mheshimiwa Mwakyembe imezua maswali mengi zaidi kuliko majibu miongoni mwa Watanzania wanaomchukulia kama shujaa wao. Ni mambo gani hayo makubwa zaidi ambayo kamati ya Mh. Mwakyembe iliyaacha kuyasema au kuyaweka katika ripoti yao ili ‘kulinda heshima ya serikali'?

Iweje wabunge wetu hawa waone kuifichia serikali yale ambayo yangeweza kusababisha heshima yake ipungue ni muhimu zaidi kuliko kutuwekea wazi kila kitu sisi waajiri wao na kutuacha tuamue wenyewe ni lipi ambalo litaitia aibu serikali na lipi halitaitia aibu?

Je, kwenye hadidu za rejea za kamati yao teule kulikuwa na kanuni inayowataka kuficha mambo ambayo wangeona ni mazito mno kiasi cha kuhatarisha heshima ya serikali? Ni kigezo gani walichotumia katika kuamua kuwa haya ni mambo mazito na yangeweza kuiaibisha serikali na haya sio mazito tuyaweke wazi?

Na baada ya kauli hii ya utata ni kipi sasa kitatufanya tusiamini maneno ya 'majeruhi' mmoja wa kisiasa aliyesema kuwa kama kamati hiyo ilikuwa na uwezo wa kuamua kutosema baadhi ya mambo, basi, pia ilikuwa na uwezo wa 'kuchomekea' baadhi ya mambo ili kuhalalisha makosa ya baadhi ya waheshimiwa waliotuhumiwa na kamati hiyo?

Tunadhani ni vizuri Mheshimiwa Mwakyembe na kamati yake akaharakisha kufafanua kauli tete yake hii. Yeye bado ni shujaa kwa Watanzania walio wengi.

Tusingependa Watanzania wafike mahali pa si tu kumfananisha na yule kiongozi wa klabu anayengoja apewe barua ya kusimamishwa uongozi na wenzake ndipo atuambie uozo wa uongozi wao; bali pia tusingependa tuanze kujiuliza ni upande gani wa kipande chake cha mkate Mheshimiwa Mwakyembe anachoona kimepakwa siagi. Upande wetu wapiga kura au upande wa serikali?
 
..ina maana kuna mambo Dr.Mwakyembe ameyaficha.

..kama kuna aliyoyaficha je kuna aliyotunga na kutumbukiza kwenye ripoti?

..Tanzania tuna watu wa ajabu-ajabu kweli.

..nakala imetoka kwenye gazeti la raia mwema. nawaamini hawa.
 
Let not our adulation for Dr. Mwakyembe's good work blind our sense of judgement and commitment to impartiality, for those of us who claim any at all.
 
Kumbuka kuwa Mwakyembe ni mbunge tena wa CCM, kwa maneno ya Kitila hapa ni kuwa alipaswa kuhifadhi heshima ya serikali yake na chama chake katika kuanguka. Hivi angemtaja mkuu wa kaya ingekuwaje? naye angengatuka? tujiulize maswali magumu zaidi.
 
Na baada ya kauli hii ya utata ni kipi sasa kitatufanya tusiamini maneno ya 'majeruhi' mmoja wa kisiasa aliyesema kuwa kama kamati hiyo ilikuwa na uwezo wa kuamua kutosema baadhi ya mambo, basi, pia ilikuwa na uwezo wa 'kuchomekea' baadhi ya mambo ili kuhalalisha makosa ya baadhi ya waheshimiwa waliotuhumiwa na kamati hiyo?

Mhhhhh!

Nani anatakiwa kuaminishwa hayo?

Finaly fisadi ni fisadi tu...playing with words and time....doesnt lead us anywhere!!

Extinction of all those with wrong motive with our nation is a MUST,... just a matter of time.
 
..ina maana kuna mambo Dr.Mwakyembe ameyaficha.

..kama kuna aliyoyaficha je kuna aliyotunga na kutumbukiza kwenye ripoti?

..Tanzania tuna watu wa ajabu-ajabu kweli.

Perspicacious....
 
Kumbuka kuwa Mwakyembe ni mbunge tena wa CCM, kwa maneno ya Kitila hapa ni kuwa alipaswa kuhifadhi heshima ya serikali yake na chama chake katika kuanguka. Hivi angemtaja mkuu wa kaya ingekuwaje? naye angengatuka? tujiulize maswali magumu zaidi.

Kwa kazi kubwa aliyoifanya Dr. Mwakyembe sidhani kama ni busara kuja na conclusion bila kujua details za maelezo ya "kuilinda serikali" Ni vizuri kama tungepata maelezo hayo kwa undani then tuje na conclusion
 
Hivi siku hizi humu JF si ruhusa ku air out your opinions,kuhabarisha ama kuuliza?Please give me a break.

Kevo,
Mie nakupa BREAK maana huo MDODMO wako Mhhh??
Nafikiri Mwakyembe akiuona basi ATAROPOKA yote ya moyoni. Sasa wee mbona wawa Mkali? Wee watoa maoni yako kwa kumshambulia MWakyembe, POA KABISA. Sasa wengine wakitoa yao kwa kukushambulia wewe, Ehhh unafunua mdomo na kufoka "FAAAAHH". Koboko wee, mkuki kwa nguruwe ehh?
Kevo, Siasa ni kama mcheza kamali. Ukisikiliza wimbo wa Kenny Rogers The Gambler anakuambia wazi kabisa. Lazima ujue karata inaendaje na ile karata ya kumaliza mchezo lazima ujue UNAIWEKA MWISHONI maana itaja kukuokoa. Na la muhimu zaidi lazima ujue ni lini UISHIE MITINI. Nyerere alijua, Kaunda hapana. Mugabe yeye ndiyo kabisa, wala hajui kuna kamali, kamali yake yeye lazima ashinde yeye tu kama Afande Idd Amin.
 
Bubu ataka kusema,
Mkuu habari yako nzuri sana lakini binafsi naona umechaganya mambo kidogo na sheria... Huyo Mhasibu wa timu ambaye alisema anasubiri barua ya kuachishwa kazi ili ayaseme mengi ya Viongozi wengine...
Binafsi, nimeelewa tofauti..Yawezekana kutokana na sheria za timu hiyo kuna habri ambazo hazitakiwi kutolewa nje kulingana na kanuni za chama hicho cha mpira kalipopewa ajira...Akisema leo wakati bado ni mwajiriwa timu inaweza kumshitaki kwa hasara zote atakazo sababisha ikiwa aliweka mkataba na timu hiyo. Ndio dunia ya leo mkuu ndio dunia hiyo hatuna tena mitume...
Mathlan, Ushindi wa timu hiyo dhidi ya timu nyingine ya nje kulitumika fedha kupata ushindi (kununua ushindi)... Hili ni kosa kubwa sana kimichezo lakini linafanyika na huwezi kuitoa siri hiyo nje kama mwajiriwa. Pia Spy hao kina james Bond 007 wanavyokubali kuingia nchi za watu na kuchukua habari za kijeshi kuhusiana na nchi hiyo.. Ni kosa kubwa sana hili lakini linakubalika within nchi inayomtumia. Na ni kosa kubwa kusema ukweli ama kutoa siri ya nchi yako kwa kile wanachokifanya dshidi ya nchi uliyotumwa ati kwa sababu unaona sii haki ama huwatendei haki wananchi wa nchi unayoishi kama spy.
Hivyo kuomba kwake kazi ya kuutengeneza uwanja haiwezi kuwa ni kosa ikiwa bado yupo kazini kama mwajiriwa na huwei kusema kwa nini leo ndio kaomba kuufanyia ukarabati uwanja huo hali wewe hapo ulipo hufahamu chanzo cha mgogoro kati ya kiongozi huyo na viongozi wengine. yawezekana kabisa kuwa uwanja huo ndio sababu kubwa ya mgogoro wote miaka hadi miaka kutokana na matumizi ya fedha katika nyanja zisizokuwa kianzio cha kukuza mtaji wa timu...
Ni maoni yangu kuhusiana na huyo mhasibu.. Sasa tukirudi kwa Mwakyembe, nadhani hukusoma kipengele kinachosema. Nitanukuu maelezo yake kama ulivyoandika:-

Mh. Mwakyembe alieleza kushangazwa kwake na wabunge waliokuwa wanatoa hoja za kuwasafisha watuhumiwa wa kashfa ya Richmond na kuwataka kama hawakubaliani na uchunguzi wa kamati yake, basi, wavunje kanuni husika za Bunge ili mjadala wa Richmond urudishwe tena Bungeni kujadiliwa upya.
Hapa mkuu unaweza kuona kwamba report ya Mwakyembe ilkuwa inabanwa na baadhi vipengele vya kanuni ambavyo vimezuia mjadala huo kuwa wazi bungeni. Bunge letu ni sawa na kuwepo mahakamani..
Mkuu hata katika sheria za wazi kwetu wananchi Mwizi au Muuaji hubanwa na mahojiano kwa kiasi fulani na anaweza kutosema baadhi ya mambo hadharani kwa sababu ni ushahidi unaotakiwa kortini.. Ndio maana hata unapowekwa kibano polisi ama kuhiojiwa na wanahabari kama unaye Lawyer kuna mambo fulani muhimu anaweza kukukataza kuyasema..Hii haina maana unaficha ukweli isipokuwa ni tahadhali ya kutovunja sheria ama kufungua mlango kwa maswali mengi nje ya korti ambayo yanaweza kabisa kuharibu kesi yako..

Kwa hiyo mkuu Mwakyembe kasema wazi tuvunje kanuni husika za Bunge ili mjadala huo ufikishwe bungeni...hapo ndipo penye haki ya mwananchi, ile report kama ulivyoiona imezikwa kifo cha mbwa lakini kamaingefika Bungeni basi habari hii isingekuwa na msalie.. pale ndipo wananchi wanapoweza kupata ukweli wote kisha hatufahamu hao Mafisadi watajiandaa vipi kama watagundua kile Mwakyembe alichokuwa nacho mkobani!..
 
Kwa kifupi ni kwamba kuna watu wetu wa uwt waliohusika na hii ishu kwa nia njema na mbaya, lakini bado huwezi kuziweka habari hizo zote hadharani kwa sababu wengine wahusika bado ni active wa uwt, sasa hizi ndio tunaita siasa za kiutu-uzima,

Mbunge na Shujaaa Mwakyembe, amefanya the best he could kulingana na mazingara ya kiserikali na kisiasa tuliyonayo Tanzania, kumbukeni wakuu kuwa siasa za bongo sio za huko majuu, naona mara nyingi tunachanganya sana hili,

Mwakyembe bado ni shujaa wangu na wa taifa langu, asiyekubali uwanja uko wazi na wewe ni kuingia tuone vitu vyako, nafikri Mwakyembe anayo haki ya kuwauliza wabongo kama muanzisha topic kuwa je toka atoe hii ripoti iliyowapeleeka mwaziri wawili na waziri mkuu kujiuzulu, wewe kama mwananchi umefanya nini hasa kama nyongeza ya pale alipoishia?

Mkuu ni haki yako kuuliza, kama ilivyo haki yetu not only kukuuliza ila ni pamoja kukuelimisha zaidi, kwani sio siri kuwa uwezo wako wa kufikiri na kuelewa unapoishia ni level ndogo sana kwa hii JF.

Ahsante Mkuu!
 
Kuhani,
Inaonyesha hana imani na Mwakyembe (Richmond) pamoja na yule mhasibu wa timu gani sijui kutokana na wao kutosema ukweli wote kuhusiana na maswala.....
Nina hakika Mwakyembe anawamjua nani mmiliki wa Richmond isipokuwa kisheria hatakiwi kuwasema wazi (Acuse fellow members) wahusika ktk report yake kwani haikuwa kazi yake na alitegemea Bunge lingechukua hatua ya Mapendekezo yake.. Na ndio maana anasema kama kweli wanataka kupata ukweli basi kanuni husika ya bunge inayozuia kurudishwa kwa swala hili bungeni..
Kwa hiyo kashindwa kuona kwamba hao wabunge wetu wanawasafisha viongozi kina Lowassa bila kuwa na Biblia mkononi... hawana ukweli mzima wa hoja na imezuia kunukuu ama kusoma biblia kisheria sasa hapa mkuu kweli makosa ni ya Mwakyembe!..
 
Inaonyesha hana imani na Mwakyembe (Richmond) pamoja na yule mhasibu wa timu gani sijui kutokana na wao kutosema ukweli wote kuhusiana na maswala.....

Mkandara,

Bubu amebandika hiyo habari kama ilivyo. Sidhani kwamba ina maanisha anaamini ya humo au hayaamini. In a way jamaa ni kama journalist fulani hivi wa JF, anaweka kitu kama kilivyo. Kuna wakati ana append mawazo yake kwenye posti ya chini lakini sio safari hii.

Au?
 
Well, kama nilivyokwisha sema unapoandika kitu ni muhimu sana useme wewe unafikiria vipi laa sivyo itachukuliwa kuwa wewe pia unaafiki..!..
Lao hii mimi siwezi kuandika kitu fulani humu bila mimi mwenyewe kuwa na mtazamo tofauti ama kukubaliana na mawazo ya mwandishi laa sivyo habario hiyo haina maana kuiweka humu..
 
Back
Top Bottom