Ripoti za CAG na Ufisadi: Ni kipindi cha TAKUKURU kutajirika

Ripoti za CAG na Ufisadi: Ni kipindi cha TAKUKURU kutajirika

Stuxnet

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2011
Posts
13,417
Reaction score
23,310
Majuma 2 yaliyopita yalitawaliwa na mijadala ya ufisadi kutoka kwenye ripoti ya CAG kwa mwaka 2021/22. Sina haja ya kuingia ndani kuhusu ni nani wanahusika na ni fedha kiasi gani wamepiga.

Kwanza nawapongeza CAG na timu yake kwa kufanya kazi ILIYOTUKUKA. Inawezekana katika Taasisi za kujivunia nchini kwa sasa National Audit Office iliyo chini ya CAG ikawa ni ya pili kwa umahiri baada ya TPDF.

Ninachotaka kuwatahadharisha Watanzania wenzangu ni kwamba MSITEGEMEE makubwa yeyote kutoka hii TAASISI ya TAKUKURU kwa hao wanaotuhumiwa na CAG. Kwa kiasi kikubwa watuhumiwa wa ufisadi kwenye ropoti ya CAG ya 2021/22 watakwenda kugawana UFISADI na Maafisa wa TAKUKURU.

Wanaofikishwa Mahakamani na TAKUKURU ni wale wenye kesi za rushwa ndogo kama Mapolisi, Mahakimu, Manesi au Waalimu. Na hawa wanapokea kati Tsh 50,000 hadi Tsh 1,000,000.

Hawa wenye mabilioni wanagawana na maofisa TAKUKURU halafu ushahidi unavurugwa kwa kunyofoa nyaraka muhimu kwenye majalada au kupoteza jalada zima.

Kuna principle ya 'Quis custodiet ipsos custodes?' kwa Kiingereza who watches the watcher. Ni nani anayemchunguza TAKUKURU kwa Tanzania?

Ni wakati sasa Serikali kupitia Bunge likaweka chombo cha kuikagua TAKUKURU, kinyume cha hapo ni kutoitendea haki CAG na timu yake.

Au Serikali kupitia Bunge ibadili sheria ili CAG mwenyewe awafikishe Mahakamani watuhumiwa wake. Assuming kuwa anajengewa uwezo wa ku prosecute.

Tusijeshangaa hapo baadaye naye CAG akaacha kuripoti hizi kashafa kwa KUMALIZANA na watendaji huko huko, kwa kuwa kazi yake inaishia kuwatajirisha maafisa TAKUKURU.
 
Kuimba kupokezana boss

Kikishaundwa chombo cha kuchumchunguza takukuru tusisahau kuunda pia chombo kitakachochunguza chombo kinachomnguza takukuru

Sasa hii kitaalamu inaitwa suistanability
Je hicho chombo cha kuchunguza TAKUKURU kinaitwaje?
 
Namkubali JPM, ilikuwa akipata info za kuthibitika umeiba pesa za Umma,

Unaletewa siafu, utang'atwa Hadi useme pesa zilipo,

Mali zilishikiliwa Hadi irudishe pesa za Umma.

Demon CRASIE Kwa wasioelimika, wasio na Uzalendo ni KAZI Bure.
 
Tanzania, na Afrika, ili ziendelee vikobo, tumbua tumbua, sweka ndani, timua timua, ni vitu vya lazima kuwepo.
 
Namkubali JPM, ilikuwa akipata info za kuthibitika umeiba pesa za Umma,

Unaletewa siafu, utang'atwa Hadi useme pesa zilipo,

Mali zilishikiliwa Hadi irudishe pesa za Umma.

Demon CRASIE Kwa wasioelimika, wasio na Uzalendo ni KAZI Bure.
JPM alileta siafu kwa ajili ya fedha za umma zikizoibwa, hatimaye fedha alizichukua yeye na kuzificha China. Usitukumbushe maisha ya huyo DIKTETA
 
Petty corruption inafanyika daily kwa kila mara na ndo maana sect 15(1) (a) na (b) zinawatia sana ndani watumishi mbalimbali wa Umma na sekta binafsi na huishia kwa NPS tu Mikoani siyo kwa DPP. PCCB wapige kazi kumsaidia mama na hili jambo.
 
Namkubali JPM, ilikuwa akipata info za kuthibitika umeiba pesa za Umma,

Unaletewa siafu, utang'atwa Hadi useme pesa zilipo,

Mali zilishikiliwa Hadi irudishe pesa za Umma.

Demon CRASIE Kwa wasioelimika, wasio na Uzalendo ni KAZI Bure.
Mbona zile 1.5 trillion mpaka leo hatujui zilipo? Au hizo siafu zinachagua watu wa kuwauma?
 
Ila asiwe mwizi kama aliyepita.
Nimecheka Sana watu bhana mmevurugwa yaan hamumuogopi Rais, miaka ile watu walikuwa wanazikimbia ID zao wasiojulikana walikuwa tishio.

Unaweza kulala usiku ukaota mtu asiyejulikana yupo mgongoni lazma uamke kwenda kukojoa tu
 
Petty corruption inafanyika daily kwa kila mara na ndo maana sect 15(1) (a) na (b) zinawatia sana ndani watumishi mbalimbali wa Umma na sekta binafsi na huishia kwa NPS tu Mikoani siyo kwa DPP. PCCB wapige kazi kumsaidia mama na hili jambo
Wanachoweza PCCB ni hizo tu petty corruption kwa kuwa hakuna fedha ya kugawiwa. Lakini grand corruption ni fedha ndiyo inaongea
 
Back
Top Bottom