Riwaya: Hekaheka za Komando Zedi Wimba na Jasusi Honda huko Somalia

Riwaya: Hekaheka za Komando Zedi Wimba na Jasusi Honda huko Somalia

RIWAYA; URITHI WA GAIDI

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA KUMI NA TISA


***

Inspekta Kenge alikuwa katikati ya barabara huku akipiga mluzi usioeleweka masikioni mwake..

Mara akapigiwa honi na gari lililokuwa nyuma yake.

"unaendesha kama unaingia kwako bwana!!" Alilalama konda wa gari lililopiga honi na kumpita Inspekta.

Inspekta Kenge akajinunisha ndani ya gari, kisha akaongeza mwendo na kuanza kulifuata gari lile lililokuwa linapiga ruti za Mbagala hadi kawe.

Mbele kulikuwa kuna foleni!

Gari lilisimama na Kenge nae akasimamisha gari lake kisha akashuka kwa gadhabu na kumfuata dereva,akamshusha na kuanza kumsomea lisala.

"Hivi hujui kuona magari mengine ni ya serikali na waliomo ndio serikali yenyewe,au hujui sheria zinatukataza kukimbiza magari kwenye misongamano ya watu vyombo vingine vya usafiri"

Dereva akataka kujitetea; Kenge akamzuia.

"yani serikali inaongea na wewe unaongea, bado konda wako amenitukana, inamaana hukuona kuwa alieko kwenye gari ni Inspekta?"

Ebanaee!.

Dereva akagwaya!

Mara gari zikaruhusiwa kusogea na zilizposogea gari la Inspekta na lile la abiria havikusogea!

Bado waliendelea kulumbana,honi zilipigwa kwa fujo na magari yaliokuwa nyuma yao.

Inspekta mtata alirudi ndani ya gari lake baada ya kutupiwa chini kiasi cha pesa ya kununulia dawa ya kusafishia viatu vyake.

Inspekta Kenge alikuwa amevurugwa na mambo mengi siku hiyo ikiwemo suala la Remi kuhusika katika mauaji ya ofisa wa jeshi la polisi.

Kilichomchanganya zaidi ni kuona tangu aanze kazi yake amekuwa akipigiwa simu na kupewa maelekezo namna ya kufanya kazi yake.

Tangu lini nikaelekezwa mimi.

Kenge alipiga ngumi kwenye usukani na kusababisha mlio mkali wa honi huku yeye mwenyewe akiruka kwa msituko.

Alikumbuka namna alivyopokea simu na kupewa maelekezo ya kuandika kuhusu mkasa ule na aliahidiwa pesa ya kutakata endapo Remi angekubali kusaini maelezo yale.

Alijikuta anakunja sura kama kaonja kamasi za mtoto.

Alijikuta anamchukia Remi.

Kwa nini!

Kwa sababu Remi alikataa kusaini karatasi zile.

"Siwezi kusaini karatasi ulizoandika wewe na kamwe sitakaa nifanye hivyo, kama mtaniacha nifie humu sawa" Alikumbuka maneno ya Remi.

Remi kutokusaini inamaanisha yeye hatopata mpunga aliohadiwa na mtu anaempigiaga simu.

Alifyonza!

"Kile kipigo nilichompa nikirudi atatia adabu na kusaini mwenyewe" Alijisemea tena.

Kenge alihitaji kufanya jambo moja ili kujiweka katika mazingira mazuri ya kuendelea kuaminika kwa wakubwa wake.

Alihitaji kuwa karibu na ukweli zaidi kuliko uongo anaopangiwa kuufanya.

Mawazo yake yalimwambia anahitaji kukutana na mhariri wa gazeti la Chaupeku; gazeti la udaku ambalo kwa ufukunyuku wake alifanikiwa kujua ndilo lililosambaza picha na taarifa kwenye magazeti mengine.

Alihitaji kukutana na mhariri ili ajue yeye alizipataje hizo picha na ni nani alimtumia.

Kwake aliona ni silaha kubwa kujua pande mbili za mchezo ule.

Hatimae alifika kwenye ofisi zile na kushuka kwa madaha huku akirekebisha miwani yake usoni.

Wakati Kenge anafika ni wakati ambao mhariri alikuwa kwenye mazungumzo na Sajenti Kobelo na bado walikuwa katika ubishani.

Kenge aliingia.

Akamkuta Sajenti ambae hakuonekana kujali uwepo wake pale.

"Sajenti nashindwa kuelewa kwa nini hunipigii saluti" Alihoji Inspekta huku akivuta kiti na kukaa.

"Sijavaa military fatigue" Sajenti alijibu kwa mkato.

Kenge akatabasamu kimajivuno.

"Nadhani unapaswa kunipisha, ni wakati wangu bwana mdogo" Alisema Kenge.

Sajenti akasimama na kuanza kuelekea mlangoni.

"Afu hii haipo mikononi mwako na ni kosa kisheria" Alisema Kenge huku akikaa..


Sajenti hakujibu akatoka.

Ndani ya ofisi walibaki mhariri mkuu na Inspekta Kenge.

Kenge alijawa na wivu baada ya kumkuta Sajenti akiwa ndani ya ofisi zile na ile aliitafsiri kama dharau na pia inaweza kumuondolea sifa kwa wakubwa wake endapo Sajenti atafanikiwa kujua ukweli kabla yake.

Akajikuta anataka kuhakikisha kama kweli Sajenti alikuwa pale ni kuhusu sakata lile.

Akauliza swali la kijinga tu.

"Huyu bwana mdogo alikuwa hapa kwa sababu gani eti"

"kazi yangu hainiruhusu kusema shida za wageni wetu kwa watu wengine" Alijibu mhariri ambae alikuwa ni kijana wa makamo tu na haiba ya upole.


Kenge alitabasamu!

"Naitwa Inspekta Kibe Kengeleo au wengi huniita Kenge nina maswali machache ndugu mhariri" Alijitambulisha Kenge..

Mhariri ambae kibao juu ya meza kilimtambulisha kama J Malao alitabasamu bila kutanabaisha dhamira yake ya kutabasamu.

"Jana habari kubwa ilikuwa ni mauaji, na gazeti lako lilikuwa la kwanza kupata picha na habari,naomba kufahamu ilitoka wapi habari ile ama mwandishi gani alieipata na wapi alikoitoa"

J Malao aligabasamu tena.

"Ni kinyume kabisa na maadili ya kazi yangu, na ndio mana unaona habari imeandikwa na mwandishi wetu" Alijibu J Malao.

Kenge aligafirika!

Mara simu ya J ikaita,akaipokea na kisha akasikiliza kidogo na kukata.

"Bwana afande, nadhani tunahitaji kutoka kidogo hadi nyumbani kwangu" Alisema J Malao huku akiinuka kwenye kiti.

Kenge bila kufikiri akasimama na kichwani akihisi huko waendako kuna taarifa anazozihitaji.

Kama alidhani kuna taarifa zinapatikana bure alikosea sana.

Kwa kuwa J Malao hakuwa na usafiri, basi iliwalazimu watumie gari la Inspekta Kenge.


Kenge hakutaka kujishugulisha na kujua alipoelekea Sajenti Kobelo baada ya kumkuta ofisini kwa mhariri.

Makazi ya J Malao yalikuwa ni mbezi mwisho.

Baada ya foleni ya hapa na pale hatimae gari la Kenge liliingia kwenye makazi ya J Malao na kwenda kupaki pembeni kidogo ya mlango wa kuingilia ndani kwa J.

Walishuka huku wakisema mawili matatu bila kugusia lililowapeleka pale.

Waliingia ndani na J alimkaribisha Kenge.

Nyumba haikuwa na samani za bei kubwa wala haikuonekana kuwa na hadhi kubwa licha ya kupangiliwa vyema muoenekano wake wa ndani.

"Chochote ambacho ungependa kutumia tafadhali" Alisema J.

Kenge alitikisa kichwa kukataa kisha akasema.

" Nadhani ni wakati sasa wa kupeana habari kuhusu swali langu"

J alitabasamu, na hilo lilimfanya Kenge ajue ni moja ya tabia za J Malao mhariri yule wa gazeti la Chaupeku.

"Sina hakika kama maelezo yangu yanaweza kukutosheleza afande" Alisema J

Kenge alikunja sura na kufanya azidi kuonekana kituko kwa sura yake isiokuwa na mpangilio maalumu wa muonekano.

J alielewa!

"Namaanisha maelezo sina bali nina kitu ambacho nahisi kinaweza kukusaidia kufika unakokutaka" Alisema J.

"Ok unaweza kunionesha tafadhali, nipo nyuma ya muda" Alisema Kenge.

"Nisubiri kwa dakika mbili tafadhali" Alisema J huku akinyanyuka na kuelekea chumbani kwake.

Kenge alingojea sebuleni.

Ilikuwa ni dakika mbili; zikaongezeka na kuwa dakika kumi na hatime nusu saa; J hakutokea.

Kenge aliona kama ni dharau anafanyiwa.

Akaanza kuita!

Aliita midomo mitatu bila kupokea majibu na kwa kuwa alikuwa na asili ya kuwehuka kwa muda, basi hakutaka kudadisi, akanyanyuka na kumfuata huko huko chumbani.

Akasukuma mlango.

Dimbwi la damu!!

Kenge akaruka juu kwa woga na badala ya kuruka kurudi alikotoka; yeye aliruka kuvuka mwili wa J Malao na kusogea kitandani.

Eeh!!

Alibwata kwa mshangao!

Mlango ulifungwa na alipotupia macho alikutana na pande la mtu likiwa na bastola mkononi yenye kiwambo cha kuzuia sauti.

E bwana eeh!

Kenge alidata; chini kunamaiti na mlangoni kasimama mtu mwenye bastola na sio mtu tu bali ni jitu lenye sura isio na masihara hata chembe.
 
Tuko pamoja mzazi na kazi imekaa kizazi sana unanirudisha kuleeee kwa tiga mumba mkimbizi

*real is not real fake is not fake*
 
Daaah.!! Unanifanya hadi mapigo ya moyo yaende mbio broo mwendo wa mabasi ya mwendo kasi kila nisomapo mstari kwa msitari, hongera sana, kweli Kenge kakutana na likengee lenzieee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
safi sana riwaya nzuri lakini jifunze kutumia kiswahili fasaha, usitumie sana lugha za mtaani za kihuni, hakika utakuwa mwandishi nguli, tamathali za semi, methali, zinaongeza ladha
 
Nahitaji sana ushauri kama huu
Ahsante sana komredi
na kuongezea mkuu jina la riwaya limekuwa refu mno mpaka linaboa ungetafuta jina fupi linalobeba ujumbe wa riwaya kwa mfano ingekuwa mimi kutokana na mahangaiko anayopitia remi ningeita hii riwaya "REMI" ingependeza zaidi au "OPERATION SOMALIA"
 
na kuongezea mkuu jina la riwaya limekuwa refu mno mpaka linaboa ungetafuta jina fupi linalobeba ujumbe wa riwaya kwa mfano ingekuwa mimi kutokana na mahangaiko anayopitia remi ningeita hii riwaya "REMI" ingependeza zaidi au "OPERATION SOMALIA"
Jina ni fupi mbona!! Inaitwa URITHI WA GAIDI. title ya uzi ni kuvutia wasomaji tu ila sio jina la riwaya
 
Ďrdďdđfďėďďrfd
RIWAYA; URITHI WA GAIDI

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA KUMI NA SABA

****

Remi alikuja kuzinduka akiwa amelala sakafuni na alikuwa na maumivu nyuma ya kisogo chake, maumivu ambayo hakujua yalisababishwa na nini.

Alitulia na kurejesha kumbukumbu zake na ndipo alipokumbuka vizuri kitu cha mwisho kumkumba ilikuwa ni maumivu kama ya kuchomwa sindano nyuma kidogo ya kisogo chake na pia alihisi anadondokea mikononi mwa mtu.

Alinyanyuka chini alipokuwa amelala na kujaribu kuangaza ila hakuona mwanga zaidi ya kidirisha kidogo kilichokuwa juu kabisa ukutani.

Pua zake zilinusa harufu nzito iliokuwa mle chumbani.

Akajaribu kupapasa ukutani labda ataona sehemu ya kuwashia taa, ila hakuona.

Hakujua alipoteza fahamu kwa muda gani hadi wakati huo alipojikuta akiwa amelala sehemu ngeni kabisa.

Akakaa chini na kuegemea ukuta, kisha akatulia na kuacha kichwa kiwaze yanayomsibu.

Wala hakufikiria sana, mlango ukafunguliwa na wakaingia wanaume wawili waliokuwa na kamba mikononi mwao na walipomfikia bila kumuuliza wakamfunga mikono na miguu kisha wakambeba mzegamzega na kwenda nae sehemu nyingine bila kusema kitu.

Kwa makadirio walikuwa wamekata kona za korido kama nne hivi na kwa kudhania alihisi yupo kwenye nyumba ya horofa.

Wakaingia kwenye chumba kilichokuwa na taa kali na wakambwaga chini bila huruma kisha wakatoka na kumwacha akijizoazoa kunyanyuka.

Akanyanyuka!!

Hakuwa peke yake mule ndani.

Kulikuwa kuna mtu amekaa kwenye kiti huku akiwa ameshika kisu kikali akikichezea kwenye vidole vyake.

Mtu yule alikuwa na asili ya watu wa India.

Alikuwa anatabasamu kana kwamba alifurahia uwepo wa Remi pale ndani.

"Kaa kwenye kiti tafadhali" yule mtu alisema.

"Naitwa Sultani" Akijitambulisha bila kusuburi Remi akae kwenye kiti.

Remi alikaa!

"Nambie wataka nini kwangu" Alihoji Remi.

"kwani unajua u wapi hapa?" Alisema Sultani.

"Ni mtoto tu ndo anaweza asijue alipo ila sio mimi. Kwanini mmeniteka?" Alihoji Remi.

Sultani alicheka.


"Ni kweli umetekwa, ila unaweza kuwa huru ukionesha ushirikiano" Alisema Sultani.

"wewe usivyojua alipo hata mimi sijui" Alijibu Remi.

"Remi;tatizo huwa unajiona shujaa sana wewe ila ushujaa ukizidi hugeuka kuwa upumbavu" Alisema Sultani huku akipitisha kisu kwenye mdomo wake.

Remi hakujibu!!

"Sikia,kutwambia alipo mumeo ni safi sana mana si wewe ama mumeo watakaoendelea kuteseka na haya masahibu" Alisema Sultani huku akiwa analamba kisu kwa ulimi wake.

"Nimekwabia vile usivyojua alipo, hata mimi sijui alipo aisee" Remi alizidi kushikilia msimamo wake.
.
Sultani alicheka kinafiki.

"Ok tuachane na mumeo, vipi kuhusu ukurasa wa Bombay?" Alisema Sultani.

Remi alitumbua macho, lilikuwa jambo geni kwake kulisikia.

"Ndo nini hicho?" aliuliza Remi.

"Hizi ni karatasi nne zenye maneno ya kiarabu, na zilipotea miaka kadhaa nyuma na inasadakika zipo hapa nchini" Alisema Sultani.

"Hebu usinichanganye tafadhali, mara mume wangu mara karatasi, sasa mimi nahusika na lipi hapo eti" Alisema Remi huku akionekana dhahiri akiwa amepagawa kwa maneno hayo.

"Yote unahusika nayo, kwa sababu mumeo alionana na Ahmed; Gaidi ambae ndie aliepotea na vitu hivyo" Sultani alisema huku sasa macho yake yakiwa yameanza kubadilika kama mtu aliekula pilipili.

Remi aligwaya!

"Ninyi watu mwanifurahisha sana aisee, yani kila siku maigizo na sijui kabisa uhusika wangu katika hizi show" Alisema Remi.

"Sio tena muda wa showtime bali ni muda wa event kabisa na bado uhusika wako upo" Alisema Sultani na hapo Remi akabutwaika baada ya kusikia showtime.

Hapo alijua kabisa bado yuko mikononi mwa watu wale wale wanaompa tabu kila siku.

"Kwa sasa hatutakuumiza, ila wakati mwingine hatutakuwa na swalia mtume juu ya jambo hili, lakini pia kwa usalama wako, endapo ukiona karatasi yoyote usioielewa basi toa taarifa" Alisema Sultani


"Nitoe taarifa kwa nani" Alihoji Remi.

"Mwanamke mjanja kama wewe nani akwambie pa kutoa taarifa? Ukiziona sisi tutajua umeziona na tutazifuata" Alisema Sultani huku akinyanyuka.

Aya!!

Yakoje mambo haya, mara nitoe taarifa mara watajua, duh! Sasa kwa nini hawakuniacha hadi wajue nimeziona ndo watokee? Alijihoji Remi na alipokuja kutazama alipokuwa sultani hakumuona tena.

"Kapita wapi bwege huyu?" Alijihoji Remi huku akigeuka huku na huko pasi kumuona Sultani.

Akiwa bado na taharuki, mara akaanza kuhisi baridi sana ndani ya chumba kile huku kila dakika ikiongezeka.

Mara ukaanza kutoka na mvuke wenye harufu nzuri sana na Remi alipovuta akaanza kupoteza fahamu taratibu.

**

Saa sita baadae Remi alizinduka kutoka kwenye koma ya kifo na usingizi
.

Akashangaa kuona akiwa amelala kwenye sofa, akaamka haraka na kutulia.
Dakika moja mbele akarudiwa na ufahamu wake na ndipo alipotupia macho kwenye ukuta.

Lahaula!!

Alikuwa yupo ndani kwake na alikuwa akimtizama mumewe kwenye picha.

Alipagawa!!

Alijua kabisa pale sio sehemu sahihi kwake na alihitaji kuondoka pale haraka iwezekanavyo.

Kitu ambacho hakujua ni kuwa ile ilikuwa imepangwa iwe vile.

Alipotaka kufungua mlango ili atoke, alikutana na domo la bastola huku polisi kama sita wakifungua mlango na kuingia ndani harakaharaka na yeye kubaki akiwa kama kapigwa sindano ya ganzi.

Mbele yake alikuwa amesimama ofisa mwenye cheo cha Inspekta na alikuwa na tabasamu lisiloeleweka kama ni chafya alitaka kupiga ama alikuwa anataka kucheka ama kulia.

Usoni alipachika miwani ya macho na kufanya aonekane kama Mr Bean.

"Niite Inspekta Kibe Kengeleo; au wengi hupenda kuniita Kenge na upo chini ya ulinzi kwa tuhuma za mauaji na kuwakimbia polisi, lakini pia unatuhumiwa kutaka kuhujumu uchumi wa nchi na pia kuishi nchini kinyume cha sheria" Kenge alimsomea makosa yake mtuhumiwa wake ambae alikuwa ameganda kama sanamu la posta akiwa hajui ni vipi yametokea hayo yanayomtokea.

Kilichofuata ni kupigwa pingu kisha wakatoka nae na kumpandisha kwenye karandinga na kutimua nae kuelekea kituo cha polisi kwa taratibu zaidi.

Remi alikuwa mikononi mwa polisi.

***

Habiba alimtumia ujumbe mfupi Kobelo akiwa ameambatanisha na namba mbili za simu ambazo pia kila namba aliweka jina la mmiliki wake.

Namba ya kwanza ilioonekana kuwa eneo hilo, mmiliki wake alikuwa ni Davis Minja. Huyu alimtambua kama mwandishi alietekwa.

Na namba ya pili ilikuwa na jina la mmiliki ambae ni Seki Zayd.

Kobelo akatuma tena ujumbe kwa Habiba ya kuwa alihitaji kujua ilipo namba hiyo wakati huo.

Habiba alijibu ujumbe ule kwa kusema namba ile inaonekana ipo posta kwenye jengo la mamlaka ya mapato.

Sajenti Kobelo aliharakisha kutoka na kuelekea nje kulikokuwa na gari lake kisha akaingia na kutia moto kuelekea posta huko.

Kwa kutumia uzoefu wake wa kuishi ndani ya jiji la Dar; alikatisha njia zisizo rasimi na hatimae aliingia posta akiwa ametumia saa moja na nusu tu.

Aliegesha kwenye maegesho ya wafanyakazi wa ofisi zile na kumtumia ujumbe Habiba ambae nae alijibu kwa kumwelekeza kuwa mtu yule bado alikuwa maeneo yale.

Kobelo aliendelea kungojea hadi nyakati za jioni ambapo ofisi zilikuwa zinafungwa.


Akapokea ujumbe wa Habiba ya kuwa mtu yule alikuwa anatoka na amekaribia alipo.

Kweli Kobelo aliona bwana mmoja mrefu wastani akiwa ameshika vitabu akifungua mlango wa gari jeupe.

Kobelo alijaribu kumpigia.

Bwana yule alipokea na Kobelo akakata.

Alipata hakika ya mtu wake anaemfuatilia.

Akaunga msafara kumfuata bwana yule ambae alikuwa na kitambi cha kuzugia umasikini.


Safari yao ilikuwa ni ya mdogomdogo kwa sababu ya foleni, lakini hatimae walifika walikokuwa wanaenda.

Mtu yule aliegesha gari kando ya barabara na kushuka kuelekea kilipo chuo huria Kinondoni.

Kobelo nae alishuka na kuelekea huko.

Bwana yule hakuingia chuoni ila alizunguka na kuwa kama anafuata ofisi za kuchapa na kurudufu karatasi zilizokuwa kule na hatimae safari yake iliishia kwenye gari moja la kifahari.

Bwana yule hakuingia, bali kioo kilishushwa na bwana yule akapokea bahasha fulani na kuanza kurejea kwenye gari lake.

Kobelo nae alifuata.

Alipanda kwenye gari na kutokomea kuelekea njia ya kawe.

Kobelo nae alikuwa nyuma.

Bwana yule aliingia kwenye nyumba moja nzuri iliokuwa na geti zuri la kisasa.

Kobelo hakuwa na namna, alipaki mbele kidogo kisha akangojea giza liingie ili akwee ukuta.


**

Giza lilitamalaki na ni wakati huo ambao Kobelo nae alikuwa amevaa kofia yake pana na kuvaa gloves mikononi huku akiwa ameshika kisu kidogo mkononi mwake.


Akatumia ukuta wa nyumba ya pili kupata msaada wa kuingia ndani ya nyumba ile.

Na hatimae alidondoka kistadi pembeni kidogo ya kichaka cha maua.

Na alipotaka kusimama, alisikia silaha kubwa ikikokiwa nyuma yake.

"Tulia Kanga wewe"

Sauti ya jitu ilikoroma.
Ffffr

Sent using Jamii Forums mobile app
 
RIWAYA; URITHI WA GAIDI

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA ISHIRINI


Kenge alibaki akimtizama yule bwana ambae alikuwa anachezesha shingo yake ambayo ilikuwa inatoa mlio kama mvunjiko wa kijiti kikavu.

Kenge alitazama vyema bastola ya jitu lile ikiwa imeenea vyema kwenye mikono yake. Kenge akapiga hesabu ni jinsi gani ataweza kuvuka maiti iliomiguuni mwake na kumfanyia shambulizi bwana yule ambae hakujua wepesi wake.

Kenge akajionya!

Akatabasamu kinyonge, hakuwa na namna.
Alitegemea jitu lile lipokee tabasamu lake kirafiki ila ndio kwanza alikutana na macho makali yaliokuwa mbali na mzaha.

"Fanya kile unachoelekezwa, tofauti na hapo unajitakia matatizo tu" Lilionya jitu lile.

Kenge akatikisa kichwa kukubaliana nae na hapo hakutaka kukaa mule, akavuka maiti ya J na kutaka kulipita jitu lile.

Kosa!

Kenge alijikuta akirudishwa nyuma kwa nguvu baada ya kupigwa kofi usoni lililoubganisha midomo na uso kiujumla.

Kenge alitoa mguno kama mbwa koko.

Kenge akagadhibika!

Kenge hajawahi kupenda dharau na akichukia huwa haoni ukubwa wa mtu ama uwezo wa mtu; Kenge aliona Katdharauliwa na jitu lile.

Akaachia ngumi nzito alioamini inaujazo wa kulitetemesha jitu lile lililokuwa limejaa kimazoezi.

Ngumi yake iliishia shingoni mwake na tofauti na matarajio yake, aliona jitu lile likichezesha tu shingo yake na kuweka bastola pembeni.

Ebanaee!!

Kenge alinywea gafla huku akijitahidi kujichekesha ili kutengeneza urafiki bandia.

Cheko lake halikusaidia!

Kenge alishikwa ukosi wa shati yake kisha akabebwa na kunyanyuliw juu kama karatasi na kutupwa kitandani ambapo alidunda mara moja na kuangukia chini.

Kenge alilia kama mbweha!

Kenge akataka kujizoa chini, ila hakufanikiwa alishikwa shati lake usawa wa mgongo kisha akanyanyuliwa tena na kutupwa kwenye kabati la nguo na kwenda nalo chini huku akisikia mvunjiko wa vioo vya kabati lile nae akitoa mguno kama mtoto anaeugulia maumivu ya bakora.

Jitu liliunguruma kwa gadhabu huku likimtizama anavyojinyanyua chini bila mafanikio.

Kenge alijitahidi kunyayuka na hatimae alifanikiwa na kukaa kitako.

Alilishuhudia jitu lile likienda kuokota bastola yake chini na kisha likamnyooshea huku uso ukiwa mbali na masihara.

Kenge aligwaya!

Jitu lile likaondoa kitunza usalama huku likianza kukenua meno kifurahia kifuatacho. Kenge hakuwa na namna zaidi ya kungojea hukumu, nguvu zake hazikuwa kitu mbele ya baunsa yule.

Mara likatokea tukio ambalo Kenge haelewi hadi leo hii lilitokeaje ila alikuja kushangaa jitu lile likijibwaga chini na kuacha bastola yake ikisambaratika chini huku ikitoa milio ya risasi bila mpangilio.
Na ndani hawakuwa wawili tena bali walikuwa ni watatu na watatu alivyoingia ndio ilimshangaza Kenge.

Alikuwa ni Sajenti Kobelo ambae alikuwa nje ya chumba kile akifuatilia kwa makini sauti za humo ndani.
Sajenti alikuwa nyuma ya msafara wa J Malao na Inspekta Kenge; na pia alifanikiwa kusogea hadi karibu na mlango na yote yaliotokea mle ndani aliyanasa vyema kabisa na sasa alikuwa ameingilia mpango wa jitu ambalo lilitaka kutoa uhai wa Inspekta kama lilivyotoa uhai wa mhariri J Malao.

Jitu lilishangaa kikumbo lilichopigwa na mtu mwenye mwili mdogo kuliko wake.

Hata!

Halijawahi kuangushwa na mwili mdogo, likajinyayua na kusimama kisha likaunguruma kwa gadhabu na kwenda kumvaa Kobelo.

Likaambulia patupu! Kobelo alikuwa mwepesi kubaini hila zake, akaepa na kusimama pembeni kisha akaruka mtindo safi wa kuambatanisha miguu yake na kulisukumia dhoruba ile lile baunsa ambapo alilipiga mbavuni.

Baunsa likaenda chini tena ila safari hii lilimwangukia Kenge na kuwa juu yake.
Kenge akaguna kwa maumivu na uzito wa baunsa lile ambalo wakati huo lilikuwa linajitikisa ili kujiinua.

Kenge akaona linamwelemea, akatumia mbinu ya kitoto kabisa, akalitekenya.
Baunsa likasimama kwa gadhabu ya kutekenywa likaachia kwenzi mujarabu ilioenda kutua utosini mwa Kenge na kumzubaisha kwa sekunde kadhaa.

Baunsa halikuwa na shida na Kenge; likajiinua tena kwa jaziba na kumwendea kwa pupa Kobelo.

Kobelo alielewa anapambana na jitu lenye nguvu, yeye alitumia akili tu ili awe bingwa wa pambano lile.

Akaruka hadi juu ya kitanda kisha akafanya kunesa kidogo na kwenda juu kisha akakunja goti na kushuka kulikabili baunsa lile.

Mbinu ilitiki.

Goti likatua kichwani mwa baunsa na kumsambaratisha chini kama kiroba cha mavi ya kuku, likabweka kama taahira.

Bahati mbaya bado ilikuwa kwa Kenge.

Baunsa alidondoka karibu na alipokuwa Kenge ambae alikuwa bado amezubaa na kwenzi ya baunsa.

Baunsa hakutaka kupigwa peke yake nae akamchapa kibao Kenge wote wakiwa chini; Kenge akarejewa na fahamu ila akakabiliana na maumivu ya shavu lake, akaachama ili upepo umwingie kinywani kumpunguzia maumivu.

Baunsa akaachana na Kenge akamvaa tena Kobelo; safari hii Kobelo hakupiga hesabu zake vyema akajikuta akijaa mikononi mwa baunsa kisha akapigwa kichwa matata pajini mwa uso wake na kuona nyota za rangi ya nyeusi.
Baunsa halikumwachia, likamnyanyua na kumtupia ukutani na kumwacha Kobelo akigugumia kwa maumivu ya dhoruba ile.

Baunsa akamfuata pale chini.

Kosa!

Kobelo kwa utalamu wa hali ya juu akaserereka kutoka alipo na kumvaa baunsa miguu mwake kisha akajiweka pembeni na kumwacha baunsa akienda chini kwa kupiga magoti na Kobelo akawa kama anainuka chini na kuacha mkono mmoja chini kisha akaachia mateke mawili kwa mpigo wa tofauti ya sekunde moja kila teke moja lilipotua shingoni mwa baunsa. Baunsa hakuwa na namna alienda tena chini kama zigo la karanga mbichi.

Bahati mbaya kwa Kenge; Baunsa akamwangukia kwenye mguu uliokuwa umejeruhiwa na vioo vya kabati..

Kenge akapiga ukunga kama bikira.

Hakuna aliemjali na Baunsa akataka kuinuka ila alichelewa alijikuta akijaa kwenye kabali ya miguu ya Kobelo ambae alimpiga kabali ya kumrukia huku amekunja miguu na alipotua alitua na shingo ya Baunsa na akapiga soti ya kubinuka, miguu ilibinuka na shingo la ulisikika mlio mmoja tu wa kuvunjika kwa kitu kikavu.

Baunsa alitikisika mara moja na kutulia.

Habari yake iliisha.

Kobelo akamfuata Kenge ambae alikuwa bado ameshika mguu kwa maumivu.

"Pole afande!!" Alisema Kobelo.

"Lakini sikukuita uje kunisaidia ujue" Alijitutumua Kenge kwa maumivu.

"Hata mimi najua, vipi umeumia" Aliuliza Kobelo.

"aah! Afande haumiagi ujue, afu ungechelewa kidogo ningemtoa nyongo huyu baunsa uchwara" Kenge alijitapa.

Kobelo alitabasamu tu na kutazama pembeni ambapo aliona mwili wa J ukiwa umelelala katikati ya dimbwi la damu.

Akaachana na Kenge ambae alikuwa anajitutumua kibwege.
Akaugeuza na kufanya kitendo cha haraka sana ambacho Kenge hakuona.

Alikwapua simu janja mfukoni mwa J na kuifutika mfukoni mwake na kuendelea kuipekuwa maiti taratibu.

"Wewe bwana mdogo acha kazi isiokuhusu, niache nimpekue mwenyewe, kesi hii ipo kwangu na sijui unaingilia kwa masilahi ya nani" Kenge alifoka.

Kobelo alijiinua taratibu bila kusema neno na kuanza kuondoka mle ndani.

"wee! tulia hapo hapo unamwachaje mkubwa wako akiwa kama hivi, ndivyo ulivyofunzwa chuoni?" Alifoka Kenge.

Kobelo alicheka tena na kumgeukia Kenge.

"Afande si useme unaogopa hilo jabali lililolala hapo? Usijali halitaamka fanya taritibu askari wengine waje hapa afande" Alisema Kobelo huku akilinyooshea kidole baunsa liliokuwa limelala bila uhai.

"Mh nani aogope, mimi au" Kenge Aliuliza kibwege tu.

Kobelo alitabasamu na kufungua mlango wa chumba na kutoka huku akiamini kabisa Kenge atadanganya watu ya kuwa yeye ndie alieliuwa lile baunsa.

Akapepea kuendelea na hamsini zake na huku nyuma Kenge akapiga simu kituoni kuomba msaada wa maaskari zaidi katika eneo lile.
 
Back
Top Bottom