Riwaya: Hekaheka za Komando Zedi Wimba na Jasusi Honda huko Somalia

Riwaya: Hekaheka za Komando Zedi Wimba na Jasusi Honda huko Somalia

RIWAYA; URITHI WA GAIDI

NA; BAHATI MWAMBA

SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU



***

Haji Makame aliona akizubaa umauti utamkuta, hivyo kwa kujitoa aliamua kuendesha gari katikati ya umati wa watu wale ambao walikuwa tayari kuiwinda roho yake kwa udi na uvumba.

Risasi zilidi kurindima kwa fujo.

Hakujali!

Aliongeza kasi ya gari lake ambalo bado lilikuwa linapatwa na risasi huku akikoswa na mabomu ya hapa na pale.

Hakuna anaependa kifo jama!!

Baada ya wale watu kuwa wameziba njia, walishangaa ujasiri wa mtu wao kuendelea kuendesha bila kuogopa milio ya risasi.

Ilikuwa ni patashika kwenye mitaa ile.

Watu wale waliona wakiendelea kukaa barabarani si ajabu watagongwa na lile gari ambalo licha ya kudhurika pakubwa bado liliweza kuendelea na Safari na sasa ilikuwa inawalenga wao.

Walijikuta wanahama barabara bila kupenda.

Na Haji alipita kwa kasi ya kimbunga huku bado mawe na risasi vikizidi kumuandama.

Bahati ilikuwa kwa Haji na hatimae alifanikiwa kutoka kwenye mitaa ile, ila nyuma alisikia magari yakija kwa kasi.

Hakutaka wajue anakoelekea.
Haraka alishuka ndani ya gari na kutoa bastola yake kisha akalenga upande wa hifadhi ya mafuta na kuachia risasi kisha hakasubiri,akatimua mbio na kuacha gari lake likiteketea kwa moto.

Alitokomea vichochoroni na kurejea kwenye makazi yao.

**

"Pole sana kamanda" Alisema Zedi huku akijitahidi kumsafisha majeraha alioyapata.


"Dah! yule mwanamke ni hatari sana aisee,yani mitaa yote ile wamejaa vibaraka wake" Alisema Haji.

"Na hapo ndipo inabidi tupitie kuufikia ukweli" Alisema zedi huku akiinuka na kuelekea kwenye droo kutoa dawa zaidi.

"Ok tumeshajua tatizo yule mtoto na Imamu wanaishia nyumba moja kifuatacho sasa!" Alisema Haji.

"Nadhani kuna haja ya kuingia ndani ya nyumba ile" Alisema Zedi.

"Inawezekana vipi kuingia wakati inaonekana inalindwa sana" Haji alionesha mashaka yake.

"Itabidi tumpe ugonjwa yule binti" Alisema Zedi kifupi huku akifungua kibegi chake na kutoka na kichupa kidogo na kukitikisa.


"Hiyo nini Komredi," Aliuliza Haji.


"Hiki ni kirusi Maria na tulikitengeneza Pakistani kwa kazi kama hii" Alisema Zedi huku akitoa huyu kichupa kingine chenye ukubwa kama ule ule wa kichupa cha kwanza.


"Hii ni tiba yake" Alisema Zedi.

"kinafanyaje kazi sasa" Aliuliza Haji.

"Hii kitu akiambukizwa, anakuwa na tatizo la kustukastuka kila mara na mwilini hukosa nguvu" Alisema Zedi.

Haji aliguna.

"Usiwe na shaka, hakuna daktari atakaeweza kuponyesha hii kitu zaidi ya hii dawa" Alisema Zedi.


"Ok!! Mpango ukoje sasa" Aliuliza Haji.

"Inabidi tutege barabarani na kisha, tutengeneze ajali bandia ili kuwavuta wale walinzi na baada ya hapo tutajua cha kufanya mana inatakiwa ivutwe hewa yake ili iweze kufanya kazi" Alisema Zedi.

Haji alitikisa kichwa kwa kukubaliana na mpango huo.

Mara ujumbe wa kengele ya tahadhari ulilia kutokea kwenye kompyuta iliounganishwa na Honda kwa mawasiliano ya dharura.

Haji aliruka kwa kasi na kuifikia huku akimsikia Zedi akiguna kwa fadhaa.


"He's in trouble" Alisema Haji huku akiwa ameshindwa kuelewa afanye nini ili kuondoa hali iliomkumba gafla.

Zedi alibaki akizunguka asijue la kufanya.

"Imekuwa haraka sana aisee" Alilalama Zedi.

Haji aliishia kushusha pumzi tu.

****

Honda alikuwa amebebwa kwenye gari akiwa chini ya ulinzi mkali wa wapiganaji wa AIAI.

Kwa mtazamo tu alijua kutakuwa kuna tatizo limejitokeza.

Akaamua kuwa na subira huku mawazo lukuki yakipita kichwani mwake.

Woga nao haukuwa mbali.

Safari yao ilikuwa ni ya kimya kimya hadi waliporejea tena kwenye lile jumba kubwa lililokuwa Sadan.

Aliamriwa kushushwa na kuingizwa ndani ya nyumba ile kisha wakamfungia kwenye chumba chenye giza.

Honda alishindwa kuelewa ni kitu gani kilikuwa kinaendelea.

Akiwa bado anawaza hili na lile mara mlango ulifunguliwa na alirejeshwa tena sebuleni na mara hii alikutana na wapiganaji wengine tofauti na waliokuwa wamemleta pale.

Hawa walikuwa ni wapiganaji ambao kwa mtazamo tu alijua inaweza kuwa ni makomando waliofuzu hatua zote kwa jinsi walivyokuwa wanaonekana.

Walikuwa sita jumla yao.

Bila maelezo walimuomba aongozane nao kuelekea nje ambako walipanda gari lingine na kuelekea katikati ya mji.
.

Walipofika Old Mogadishu walisimamisha gari na kumfunga kitambaa usoni na kisha safari ikaendelea hadi walipoingia ndani ya geti la nyumba ambayo hakufahamu ukubwa wake.


Mawazoni mwake alijua labda walistukia nyendo zake wakati anaenda kutoa taarifa ya kuhusu njama za mauaji ya Rais wa Kenya ambayo yalivurugwa dakika za mwisho.

Alijua hawezi kupona kwa kuwa msaliti huwa haponi Zaidi ya kuchinjwa.

Mwili ulimzizima.

Alihofia kwa kuwa suala lile tayari ilikuwa limeshaleta mzozo baina yao, na tayari kikosi chao cha upepelezi kilikuwa kimeshaingia mjini kujua kilitokea nini hadi jaribio lao lilishindwa dakika za mwishoni.

Honda aligwaya ila alijipa ujasiri bandia.

Aliketishwa kwenye kiti kisha akavuliwa kitambaa usoni na hakuwa peke yake pale alipokalishwa.

Mbele yake kulikuwa kuna kijana mmoja mwenye asili ya watu wa Saudia na mzee ambae alikuwa na asili ya kisomali.


Mzee yule alimtambua.

Na ndie alikuwa lengo la operesheni yao.

Huyu ndie alikuwa FLAMINGO kwa lugha yao ya kazi ile.

Alikuwa ni Mohamed Farrah Aidid kiongozi wa kikundi cha Al-Islamiya.

Alitetemeka ndani ya mwili wake bila kuonekana nje.

Wapiganaji waliomleta waliopewa ishara fulani na ndani ya dakika moja alishangaa akiwa amepigwa pingu mikononi na miguuni kwa kasi ya ajabu.

Wapiganaji wale walikuwa si mchezo.


Kijana yule wa kisaudia alitoa picha mbili.

Moja akamuonesha Honda.


Honda alitamani kuona akiota na akiamka aambiwe ni masihara tu yale.

Ila haikuwezekana.

Alikuwa amepewa picha ya Haji Makame.

Picha ile iliambatanishwa na kipande cha gazeti, kilichokuwa na picha tatu, picha yake akitambuliwa kama Ahmed Twalib na picha nyingine ikiwa ni ya Zedi akitambulishwa kama ni Aahmed Boka Ghailan na nyingine ikiwa ni ya Haji ambae haikuwa na maelezo mengi zaidi ya kumhusisha na kutoroka kwa Ahmed gerezani.


"Ahmed; mtu huyu yupo hapa Mogadishu na kama walivyondika wamarekani ndivyo yupo hapa kukutafuta" Alisema Mohamed Farrah.

Honda alitikisa kichwa kukataa.

"Huyu jamaa simfahamu kabisa" Alijitetea Honda.

Mohamed alicheka kisha akampa ishara tena yule kijana wa kisaudia na kijana yule akatoa picha nyingine mbili na kumpa Honda.

Honda alizidi kuchanganyikiwa zaidi.

Picha moja ilikuwa ni ya kwake akiwa na mavazi ya kijeshi na picha nyingine ilikuwa ni ya Haji akiwa na mavazi ya kipolisi huku cheo chake kikijionesha mabegani.


"Hizi ni taarifa kutoka kwenu Tanzania; na mara ya mwisho ulikuwa kazini mwaka juzi ila sisi Ahmed tunaemtafuta alitoweka tangu mwaka 1998 baada ya shambulio la ubalozi wa marekani jijini Nairobi." Alisema tena Mohamed Farrah.

Ebana ee!

Kitumbua kimeingia mchanga mapema.


"Ila umekuwa ukitumika kutuhujumu, na hata mauaji ya Osama inasadikika ulitengenezwa tena na ulifanikiwa kumhujumu Osama hadi mauti yake" Aliendelea Kuongea Mohamed Farrah Aidid.


Kitu kimoja alichogundua Honda ni kuwa watu wale licha ya kuzipata taarifa zake ila hawakuwa wakimjua Ahmed halisi na hilo likampa afueni kidogo japo hakujua hatima yake.
.

Honda alikana kuzijua picha zile na akasingizia ya kuwa labda zimechongeshwa tu ila si yeye.

Watu wote waliangua kicheko cha dhihaka mule ndani.

"Ok! Mengine tutaongea badae, ila kwa sasa tunahitaji jambo moja tu" Mohamed Farrah alisema na kuweka kituo na kumtazama Honda.


Mlinzi mmoja akaweka kitabu kikubwa chenye ukubwa kama msahafu kwenye meza karibu na Honda.

Honda akaoneshwa ishara ya kukifunua, nae akafunua.

Alikutana na maandishi ya kiarabu.

Lugha ile aliilewa!..

Kwa haraka alijua kile ni kitabu cha wosia kilichokuwa na mambo mengi ikiwemo Fatwa'a nyingi kuhusu maonyo Osama kwa wamarekani na namna ya kupambana na wabaguzi wa nchi za kiarabu.

Kifunikwa kitabu na kuondolewa.

"Kitabu hiki kimeondolewa kurasa sita za katikati na ndizo kurasa muhimu katika kitabu hiki, na inasemekana ulihusika katika kuzinyofoa kurasa zile" Alisema Mohamed Farrah.

Ebana eeh lilikuwa ni jambo jipya kwa Honda.

Hakujua kabisa kitabu kile na kurasa hizo zinazoongelewa.

Akabaki njia panda na mateso yalinukia.
Kazi nzuri bwana Kudo. Hongera...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
***

Haji na Zedi hawakulala, mana hawakujua ni kitu gani kitamkuta mwenzao huko aliko.

Wakati wao wakimuwazia vile, tayari Honda alikuwa ameiingizwa kwenye chumba cha mateso huku akiwa amevuliwa nguo zote.

Yule kijana wa Kisaudia aliona ile pete ikiwa kwenye uume wa Honda na alipoishika akashindwa kuelewa ni kitu gani kile.

Pete ile ilikuwa imetengenezwa maalumu kwa ajili ya kushikwa na Honda peke yake na kama ikishikwa na mtu tofauti basi sehemu ilipounganishwa hutoa taarifa ya hatari.

Kijana yule akaitazama kwa makini ila akaona ni pete za kawaida tu ambazo huvaliwa na watu wenye mikuyenge mikubwa mikubwa.

Hakuitilia shaka zaidi na akaitupa chini.

Likaletwa dumu la mafuta ya taa na kumwagwa mwilini mwa Honda kisha wakamuuliza zilipo zile karatasi za kile kitabu.

Akashindwa kusema.

Na kitu alichogundua ni kuwa zile karatasi zilikuwa na umuhimu mkubwa sana kwa wale watu kuliko hata uhusika wake katika kuwapepeleza.


Alikaa kimya.

Mafuta yalipomwagwa mwilini yakasalia kidogo kwenye dumu na yakamiminwa chini na kusambaa kisha jamaa mmoja alikaa pembeni na kiberiti.

Leo tutakuchoma moto Ahmed." Alisema yule kijana.


***

Mapambazuko yaliwakuta Haji na Zedi wakiwa wameshajadiliana vya kutosha kuhusu namna ya kufanya ili waweze kusambaza kirusi Maria.

Walijiandaa na kutoka nje ya makazi yao na kuelekea kutega njia ambayo waliamini gari lililombeba binti yule litakuwa linapita.

Kabla ya saa mbili kamili, gari moja la bei mbaya liliwapita njiani, na wao walilifuata kwa nyuma na walipofika makutano ya mnara wa kijeshi, wakafanya hila za kutaka kulipita gari lile likiwa katika mzunguko wa mwanajeshi asiefahamika.

Wakaparazana na kukosa mwelekeo na kwenda kuingia kwenye bustani ya mnara ule.

Walinzi wawili walishuka kwa gadhabu na kuliendea gari la Zed huku wakitukana.

Zedi alishuka!

Kwa makusudi aliongea lugha tofauti na kiingereza huku wale jamaa nao wakiongea lugha tofautitofauti, mara kingereza,mara kisomali ili mradi wapunguze jaziba zao.

Lengo la kuongea Kiswahili ni kutaka mlinzi wa tatu nae ashuke.

Na kweli alishuka, na Haji nae akashuka.

Haji alikifungua kichupa kile na kukiziba mdomo kwa kidole chake kisha akakifumbata mkononi.

Ajabu ni kuwa mlinzi wa tatu alieshuka alikuwa anaongea kiswahili safi kabisa.

Jamaa yule anaezungumza kiswahili aliwatuliza wenzie kisha akaanza kuongea na Zedi na hata Haji alipofika waliendelea kuongea kiswahili.

Walinzi wale ilitakiwa wawahi kutoka pale ili mwanafunzi awahi shule.

Hivyo ilikuwa ni kujitahidi kusawazisha suala lile.

Zedi aligundua wanataka kuondoka, hivyo akaanzishaa tena mgogoro kwa kuonesha yeye ndie amekosewa na wale jamaa.

Zogo likazuka upya!

Haji alikaa makini kwa ule upande ambao aliamini yupo mwanafunzi.

Mwanafuzi nae aliona anacheleweshwa, akashusha vioo vya upande wake.

Kosa!.

Macho makali ya Haji yalikuwa sambamba na na kwa wepesi wa hali ya juu akajifanya nae amaeingiwa na jaziba kwa kurusha mikono hovyo na pale ndipo alipokirusha kichupa kile chenye kirusi Maria.

Mtoto yule alikiona kichupa kile na bila kujua akakichukua na kukinusa kisha akakitupa nje na kuwaita walinzi wake.

Walifanikiwa!


Baada ya kufanikiwa walituliza mashetani yao nao walipanda gari na kuondoka huku wakiwa wametumia dakika saba tu na walijua ndani ya dakika kumi askari wa Mogadishu wangeliwakuta pale.


Waliondoka wakijipongeza huku Haji akitema kidonge alichokuwa amebugia ili kuzuia a athari za kirusi kile wakati alipokuwa amekifungua.


Walirejea kwenye makazi yao na kuanza kupanga mikakati ya namna watakavyoweza kuingilia tiba ya binti yule.

Haji alikaa kwenye kompyuta na kuanza kupika taarifa na wasifu wa mganga bingwa wa magonjwa ya kuambukiza ambae alikuwa anafanya kazi kwenye hospital kubwa pale Mogadishu kama mganga mkuu.

Na hapo walipata mtu mwenye sifa sawa na zile walizozihitaji.

Na waliangukia kwa Dr Azam.

Zedi alichukua vifaa vyake na kukaa kwenye kioo huku Haji akiwa anaendelea kupika taarifa za Dr Azam.

Alibadili maeneo muhimu na hasa mawasiliano,aliweka anuani ya barua pepe na namba za simu za kwao,kisha akaifunga kompyuta na kumgeukia Zedi.


"Aisee! wewe mtu ni hatari yani hutofautiani na sura ya huyu jamaa kabisa."Alisema Haji huku akichukua kamera yake kumpiga picha Zedi ambae alikuwa amefanikiwa kujichongea sura sawa na ya Dr Azam.

"Hii ni raha ya ukomando,kila kitu MI see rahisi kukifanya" Alijigamba Zedi.

"Ila hatuwezi kufanya hii kazi vizuri bila Azam mwenyewe kutoweka mjini" Alisema Haji.


"Upo sahihi, hebu tumtafute mjini na tutoweke nae" Zedi aliafiki.

***

Jioni ya siku ile Zedi na Haji walikuwa na kazi moja tu, nayo ni kuhakikisha wanajua alipo Dr Azam.

Walifanikiwa kujua anapoishi na kwa uzoefu wao wa kuteka watu ambao hawana madhara, walifanikiwa kumchukua na kuondoka nae hadi kwenye makazi yao.


Wakati wao wakimteka Azam; Imamu Shafi'I alikuwa anapokea taarifa kutoka kwa tabibu wake ya kuwa mwanae amepata maambukizi ya ugonjwa wa ajabu hajapata kuona na hajui kama aliwahi kusoma popote kuhusu ugonjwa ule.

Ugonjwa ule ulisababishwa na kirusi ambacho kina shambulia seli nyeupe kwa kasi kubwa sana na kupelekea mwili kukosa nguvu na mgonjwa kuwa anastukastuka kila mara.

Imamu alipagawa!

Kwa haraka alituma sampo ya damu ya binti yake kila kulipokuwa na tabibu wanaefahamiana.

Na hadi giza linaingia alikuwa amepata majibu yenye kufanana na kila tabibu alishindwa kujua ni wapi atapa dawa za kuzuia kirusi kile kisifanye kazi.

Na pia wapo waliomtahadharisha ya kuwa siku chache zijazo binti yule anaweza kukosa uhai.

Hali ilizidi kuwa mbaya kupindukia.

Imamu Shafi'I aliita watu wake wa karibu usiku ule na kuwataka ushauri.

Wengi walishauri walivyoweza ila mmoja alishauri aitwe Dr Azam; mganga mkuu wa hospital ya old Mogadishu.

Haraka haraka haraka wasaidizi wake waliingia mtandaoni kutafuta sifa za Dr yule.

Walijiridhisha na taarifa zake,kisha wakampigia simu.

Walikubaliana kuonana ahsubuhi katika mnara wa kanisa katoliki.

***

Zedi na Haji walipongezana baada ya kuona ujumbe wa barua pepe kisha ukafuata ujumbe wa simu.

Makubaliano yalifanyika na wakajipanga kufanya walichokubaliana.


**

Ahsubuhi kama kawaida Dr Azam wa bandia alitumia gari la Dr Azam wa kweli na kuelekea nalo kule kwenye mnara wa kanisa katoliki kama walivyokubaliana.

Ungelimtazama Zedi; basi ungeamini ndie Dr Azam halisi.

Alipofika pale, alipigiwa honi na gari moja lililokuwa limepaki pembeni ya duka moja la vifaa vya baiskeli.

Akaenda na gari lake ila alishuka kijana mmoja na kumwomba ashuke aache pale gari lake na apande kwenye gari lao.

Dr Azam wa bandia alitii.

Alichukua kibegi chake chenye vifaa tiba na kupanda ile gari.

Safari ilianza.
 
*** Haji na Zedi hawakulala, mana hawakujua ni kitu gani kitamkuta mwenzao huko aliko.
Wakati wao wakimuwazia vile, tayari Honda alikuwa ameiingizwa kwenye chumba cha mateso huku akiwa amevuliwa nguo zote.
Yule kijana wa Kisaudia aliona ile pete ikiwa kwenye uume wa Honda na alipoishika akashindwa kuelewa ni kitu gani kile.
Pete ile ilikuwa imetengenezwa maalumu kwa ajili ya kushikwa na Honda peke yake na kama ikishikwa na mtu tofauti basi sehemu ilipounganishwa hutoa taarifa ya hatari.
Kijana yule akaitazama kwa makini ila akaona ni pete za kawaida tu ambazo huvaliwa na watu wenye mikuyenge mikubwa mikubwa.
Hakuitilia shaka zaidi na akaitupa chini.
Likaletwa dumu la mafuta ya taa na kumwagwa mwilini mwa Honda kisha wakamuuliza zilipo zile karatasi za kile kitabu.
Akashindwa kusema.
Na kitu alichogundua ni kuwa zile karatasi zilikuwa na umuhimu mkubwa sana kwa wale watu kuliko hata uhusika wake katika kuwapepeleza.
Alikaa kimya.
Mafuta yalipomwagwa mwilini yakasalia kidogo kwenye dumu na yakamiminwa chini na kusambaa kisha jamaa mmoja alikaa pembeni na kiberiti.
Leo tutakuchoma moto Ahmed." Alisema yule kijana. ***
Mapambazuko yaliwakuta Haji na Zedi wakiwa wameshajadiliana vya kutosha kuhusu namna ya kufanya ili waweze kusambaza kirusi Maria.
Walijiandaa na kutoka nje ya makazi yao na kuelekea kutega njia ambayo waliamini gari lililombeba binti yule litakuwa linapita.
Kabla ya saa mbili kamili, gari moja la bei mbaya liliwapita njiani, na wao walilifuata kwa nyuma na walipofika makutano ya mnara wa kijeshi, wakafanya hila za kutaka kulipita gari lile likiwa katika mzunguko wa mwanajeshi asiefahamika.
Wakaparazana na kukosa mwelekeo na kwenda kuingia kwenye bustani ya mnara ule.
Walinzi wawili walishuka kwa gadhabu na kuliendea gari la Zed huku wakitukana.
Zedi alishuka!
Kwa makusudi aliongea lugha tofauti na kiingereza huku wale jamaa nao wakiongea lugha tofautitofauti, mara kingereza,mara kisomali ili mradi wapunguze jaziba zao.
Lengo la kuongea Kiswahili ni kutaka mlinzi wa tatu nae ashuke.
Na kweli alishuka, na Haji nae akashuka.
Haji alikifungua kichupa kile na kukiziba mdomo kwa kidole chake kisha akakifumbata mkononi.
Ajabu ni kuwa mlinzi wa tatu alieshuka alikuwa anaongea kiswahili safi kabisa.
Jamaa yule anaezungumza kiswahili aliwatuliza wenzie kisha akaanza kuongea na Zedi na hata Haji alipofika waliendelea kuongea kiswahili.
Walinzi wale ilitakiwa wawahi kutoka pale ili mwanafunzi awahi shule.
Hivyo ilikuwa ni kujitahidi kusawazisha suala lile.
Zedi aligundua wanataka kuondoka, hivyo akaanzishaa tena mgogoro kwa kuonesha yeye ndie amekosewa na wale jamaa.
Zogo likazuka upya!
Haji alikaa makini kwa ule upande ambao aliamini yupo mwanafunzi.
Mwanafuzi nae aliona anacheleweshwa, akashusha vioo vya upande wake.
Kosa!.
Macho makali ya Haji yalikuwa sambamba na na kwa wepesi wa hali ya juu akajifanya nae amaeingiwa na jaziba kwa kurusha mikono hovyo na pale ndipo alipokirusha kichupa kile chenye kirusi Maria.
Mtoto yule alikiona kichupa kile na bila kujua akakichukua na kukinusa kisha akakitupa nje na kuwaita walinzi wake.
Walifanikiwa!
Baada ya kufanikiwa walituliza mashetani yao nao walipanda gari na kuondoka huku wakiwa wametumia dakika saba tu na walijua ndani ya dakika kumi askari wa Mogadishu wangeliwakuta pale.
Waliondoka wakijipongeza huku Haji akitema kidonge alichokuwa amebugia ili kuzuia a athari za kirusi kile wakati alipokuwa amekifungua.
Walirejea kwenye makazi yao na kuanza kupanga mikakati ya namna watakavyoweza kuingilia tiba ya binti yule.
Haji alikaa kwenye kompyuta na kuanza kupika taarifa na wasifu wa mganga bingwa wa magonjwa ya kuambukiza ambae alikuwa anafanya kazi kwenye hospital kubwa pale Mogadishu kama mganga mkuu.
Na hapo walipata mtu mwenye sifa sawa na zile walizozihitaji.
Na waliangukia kwa Dr Azam.
Zedi alichukua vifaa vyake na kukaa kwenye kioo huku Haji akiwa anaendelea kupika taarifa za Dr Azam.
Alibadili maeneo muhimu na hasa mawasiliano,aliweka anuani ya barua pepe na namba za simu za kwao,kisha akaifunga kompyuta na kumgeukia Zedi.
"Aisee! wewe mtu ni hatari yani hutofautiani na sura ya huyu jamaa kabisa."Alisema Haji huku akichukua kamera yake kumpiga picha Zedi ambae alikuwa amefanikiwa kujichongea sura sawa na ya Dr Azam.
"Hii ni raha ya ukomando,kila kitu MI see rahisi kukifanya" Alijigamba Zedi.
"Ila hatuwezi kufanya hii kazi vizuri bila Azam mwenyewe kutoweka mjini" Alisema Haji.
"Upo sahihi, hebu tumtafute mjini na tutoweke nae" Zedi aliafiki. ***
Jioni ya siku ile Zedi na Haji walikuwa na kazi moja tu, nayo ni kuhakikisha wanajua alipo Dr Azam.
Walifanikiwa kujua anapoishi na kwa uzoefu wao wa kuteka watu ambao hawana madhara, walifanikiwa kumchukua na kuondoka nae hadi kwenye makazi yao. Wakati wao wakimteka Azam; Imamu Shafi'I alikuwa anapokea taarifa kutoka kwa tabibu wake ya kuwa mwanae amepata maambukizi ya ugonjwa wa ajabu hajapata kuona na hajui kama aliwahi kusoma popote kuhusu ugonjwa ule.
Ugonjwa ule ulisababishwa na kirusi ambacho kina shambulia seli nyeupe kwa kasi kubwa sana na kupelekea mwili kukosa nguvu na mgonjwa kuwa anastukastuka kila mara.
Imamu alipagawa!
Kwa haraka alituma sampo ya damu ya binti yake kila kulipokuwa na tabibu wanaefahamiana.
Na hadi giza linaingia alikuwa amepata majibu yenye kufanana na kila tabibu alishindwa kujua ni wapi atapa dawa za kuzuia kirusi kile kisifanye kazi.
Na pia wapo waliomtahadharisha ya kuwa siku chache zijazo binti yule anaweza kukosa uhai.
Hali ilizidi kuwa mbaya kupindukia.
Imamu Shafi'I aliita watu wake wa karibu usiku ule na kuwataka ushauri.
Wengi walishauri walivyoweza ila mmoja alishauri aitwe Dr Azam; mganga mkuu wa hospital ya old Mogadishu.
Haraka haraka haraka wasaidizi wake waliingia mtandaoni kutafuta sifa za Dr yule.
Walijiridhisha na taarifa zake,kisha wakampigia simu.
Walikubaliana kuonana ahsubuhi katika mnara wa kanisa katoliki. ***
Zedi na Haji walipongezana baada ya kuona ujumbe wa barua pepe kisha ukafuata ujumbe wa simu.
Makubaliano yalifanyika na wakajipanga kufanya walichokubaliana.
**
Ahsubuhi kama kawaida Dr Azam wa bandia alitumia gari la Dr Azam wa kweli na kuelekea nalo kule kwenye mnara wa kanisa katoliki kama walivyokubaliana.
Ungelimtazama Zedi; basi ungeamini ndie Dr Azam halisi.
Alipofika pale, alipigiwa honi na gari moja lililokuwa limepaki pembeni ya duka moja la vifaa vya baiskeli.
Akaenda na gari lake ila alishuka kijana mmoja na kumwomba ashuke aache pale gari lake na apande kwenye gari lao.
Dr Azam wa bandia alitii.
Alichukua kibegi chake chenye vifaa tiba na kupanda ile gari.
Safari ilianza.
tupia kipande kingine
 
***

Dr Azam wa bandia alipofika ndani ya gari na gari likaondolewa na kisha ikaanza safari ya kumzungusha Dr yule.

Dr Azam wa bandia aliwaza ya kuwa zile ni mbinu tu zinazotumika ili asijue wanakoelekea.

Dereva alizungusha gari zaidi ya dakika arobaini na tano na hakuonesha dalili ya kusimamisha gari.

Dr Azam aliamua kuwapunguzia safari,akajilaza na kukoroma.

Dereva na wasaidizi wake bila kujua hila ya Dr; wao walijua kweli Dr kalala hivyo walizunguka kidogo na hatimae waliingia nyumbani kwa Imamu Shafi'I.

Dr aliamshwa na vijana waliompokea.

Akapiga miayo ya uchovu kisha akajivuta na kurekebisha miwani yake na kushuka.

Kama mwewe angani, akazungusha macho yake kwa haraka sana na kufanikiwa kuona walinzi sita wenye bunduki wakiranda huku na huko.

Dr Azam wa bandia aliona mmoja wa walinzi akiwa na mbwa.

Akashanga!

Muislam safi kamwe huwezi ona mbwa akiranda nyumbani kwake hata kwa bahati mbaya hasa nyumba yenye uzio kama ile.

Hapo Dr Azam wa bandia alikubaliana na mawazo ya Haji kuwa Imamu na watu wake walikuwa wanatumia uislamu kama mwamvuli wa kufanya mabaya yao.

Dr alitukana kimoyomoyo.

Alikaribishwa ndani na Imamu Shafi'I na baada ya utambulisho alipelekwa kwenye chumba maalumu alichokuwa amelazwa binti yake.

Dr alijitia kusikitika kwa hali aliomkuta nayo binti yule.

Kila nusu dakika binti alikuwa anastukastuka na mwili ulianza kumpauka huku midomo ikiwa imekauka.


"Naombeni mlete maji ya kunywa" Aliagiza Dr Azam.

Walinzi wakaangaliana kisha Imamu akasema "Tulizuiwa kumpa maji jana Dr"

Dr Azam akamgeukia na kumkata jicho kali.

"Mimi ndie Dr na naomba mlete maji, mnazidi kumdhoofisha kwa kutokumpa maji,msiogope tafadhali" Alisema Dr Azam huku akiwa bize kuweka sawa vifaa tiba vyake.

Maji yaliletwa na Dr akamywesha yule binti.

Binti akapata kauli kwa mara ya kwanza tangu usiku uliopita.

Imamu alitabasamu kwa kitendo kile.

"Mgemuua huyu mtoto aisee" Alilalama Dr Azam.

Dr Azam alichukua damu kidogo na kuihifadhi kwenye kifaa maalumu kisha akaweka kwenye mkoba wake na kisha akaendelea kumkagua hapa na pale binti yule.


"Naiomba hewa tafadhali" Dr alisema huku akiinuka kuwatazama walinzi waliokuwa mle ndani.

Imamu aliwapa ishara nao wakatoka.

Alibaki Imamu Shafi'I ndani ya chumba kile.

Dr Azam alikuwa na sababu za kumbakiza Imamu mule ndani.

"Hii inaweza kuwa imesababishwa na nini Dr" Alihoji Imamu huku akikaa kwenye kiti kilichokuwa pembeni ya kitanda.

"Kwa haraka naona ni ugonjwa wa mlipuko kutoka kwa wanyama au basi alikula chakula chenye kuukataa mwili wake" Alijibu Dr.

"Chakula kinapimwa kabla ya kuliwa Dr; labda mnyama na sijui ni mnyama gani" Alisema Imamu Shafi'I.


"Huwezi jua katika mazingira yake ya kujidai" Alijibu Dr Azam.

Imamu alikunja uso kisha akasema
"Inabidi nimbadilishie walinzi, wamekuwa wazembe sana siku hizi".

Dr hakujibu.

Mara simu iliita na Imamu akampiga jicho Dr kwa wizi na kuipokea.

Kama imamu alidhani Dr hajamuona alikosea sana.

Macho ya Zedi Wimba p.a.k Dr Azam yalimnasa vyema kabisa na hilo ndilo lililomfanya awatoe walinzi mle ndani na kumbakiza Imamu peke yake.


Kabla ya kuongea Imamu alimuuliza Dr Azam

"Hivi kwenu ni wapi, waonekana si msomali eti"

"Kwetu ni South Africa" Alijibu Dr

Imamu aliongea kwa kipakistani(punjaban).

Kama alijua komando aliepembeni yake ni zwazwa basi alikosea sana.

Pakistani walikaa zaidi ya mwaka mmoja kabla ya kuanza kazi ile, hivyo moja ya lugha waliofundishwa ni hiyo Punja inayozungumzwa sana na watu wa mashariki mwa Pakistani.

Dr alielewa kilichozungumzwa, ila akaendelea na huduma yake ya msingi kwa yule mtoto wa kike.

Imamu alimaliza kuongea na simu kisha akaendelea kumtazama Dr Azam.

Dr Azam nae hakutaka kuendelea kuweka muda mrefu pale ndani hivyo,akachukua vidonge viwili na kumpa yule mtoto.

"Inabidi nikafanyie utafiti hii damu kisha nitakuja na majibu kuhusu aina ya dawa inayoweza kutumika kumtibu ila hizo dawa nilizompa zitamsaidia hadi keshokutwa nitakaporejea" Alisema Dr Azam.

Imamu alionekana kuwa na shaka.

Kwa nini?

Kwa sababu alihitaji mwanae apone haraka na pia alikuwa na sababu yake kubwa zaidi ambayo hakutaka kabisa Dr Azam afike pale siku hiyo.

Siku hiyo ambayo Dr aliahidi kurejea na majibu ni siku ambayo alitarajia kupokea ugeni nyeti sana na kwa kawaida akipokea wageni wa aina hiyo kamwe mgeni mwingine huwa had huruhusiwi kuingia ndani ya jumba lile.


Jitahidi iwe hata kesho Dr" Alisihi Imamu Shafi'i.

Dr alizidi kusisitiza huku akiweka sababu zake zenye mashiko kabisa.

Mwisho Imamu kwa kujali afya ya mwanae aliamua kukubali ombi la Dr.

Dr Azam alitolewa nje na kusindikizwa hadi ndani ya gari lililomleta kisha wakaanza tena kumzungusha kwenye vichochoro vya Mogadishu.

Saa moja badae walimfikisha kwenye lile duka la vifaa vya baiskeli na kumwacha apande kwenye gari lake.

Dr alielekea kwenye kituo chake cha kazi huku akiamini kabisa kuna watu maalumu waliwekwa kumfuatilia.
.
Dr alitabasamu baada ya kuwa amemtega Imamu kuhusu kwenda kwake siku ya tatu yake na alifanya vile baada ya kumsikia akiongea kuhusu kupokea wageni muhimu.

Dr Azam wa bandia alitaka kuwaona wageni wale.

Hakika hesabu zao zilikuwa sahihi kwa wakati huo.


***

Honda alikuwa hatamanila kwa kipigo alichopata na mwili wake ulikuwa umebabuka baada ya kuwashwa na moto.

Bahati nzuri ni kuwa moto hakumfikia kichwani na pia hakumpa madhara makubwa kwenye ngozi yake.

Ila vidonda vilipatikana.
Alikuwa amelipuliwa kwa dakika moja tu.

Alikuwa amefungwa na kuachwa aning'nie kwenye kamba huku chini kukiwa kumewekwa chupa zilizopondwa pondwa na hivyo kumfanya muda mwingi akunje miguu na kila alipoishusha aliishia kuchomwa na chupa.


Mwili vidonda na miguu ni vidonda vya kukatwa na chupa huku damu ikiwa inamwagika.


Pembeni yake alisimama jamaa ambae alikuwa ameshika bakora ya mpira.

Hakika alipitia mateso.

Yule kijana wa kisaudia alikuwa amesimama huku akingoja apewe majibu ya zilipo hizo karatasi ambazo zilikuwa zimepewa jina la Ukurasa wa Bombay.

Honda hakuwa na jibu la kuwapa.

****

Siku ya tatu iliwadia na Dr Azam alienda pale pale alipoambiwa angojee.

Alifika na kulikuta gari lile lile lililokuwa limemfuata siku iliopita.

Utaratibu ukawa ule ule na akapandishwa kwenye gari na kuzungushwa.

Nae hakubadilika alilala baada ya dakika thelathini kisha aliamshwa walipowasili kwenye jumba la Imamu.

Kama kawaida, macho yake makali yakanasa sura za walinzi sita aliowakuta siku ile pamoja na mbwa na pia aligundua kuna walinzi wengine zaidi waliokuwa wapo pale ndani.

Siku hii Dr Azam alikaguliwa na vifaa vya kisasa ili kama anasilaha aweze kuisalimisha.

"Dr; samahani kwa kinachotokea ila lazima usalama uzingatiwe" Imamu alimuomba radhi Dr Azam kisha akamwongoza wakaelekea kwenye chumba cha tiba.


"Dawa zako zimemsaidia sana mwanangu, anacheza hivi sasa na ameanza kurejewa na nguvu zake" Alisema Imamu Shafi'I.

Dr alitabasamu tu.

Kitu kingine alichogundua Dr Azam; ni kuwa nyumba ile hakukuwa na mwanamke hata mmoja tofauti na yule mtoto wa kike wa Imamu Shafi'I.

Dr Azam alitoa kichupa chenye tiba na kumchoma mtoto kisha akachukua dawa nyingine tena na kumchoma mtoto na hazikupita dakika sita mtoto alipitiwa na usingizi.


"Itabidi nisubiri hadi azinduke ndipo niondoke, hii ni kwa usalama wa afya yake" Alisema Dr Azam.

Imamu akang'aka!

Hakutaka Dr aendelee kupoteza muda pale.

****

Nb;bado hujachelewa ofa! Riwaya hii itakufanya usome nyingine zaidi kwa kuilipia Tsh 1000/= yani elfu moja utapata riwaya mbili, zile ambazo hujawahi kusoma kutoka kwangu.

Malipo fanya hapa 0758573660.
Whatsapp 0658564341.

Hakikisha jina limesoma Bahati Mwamba
 
***

Dr Azam wa bandia alipofika ndani ya gari na gari likaondolewa na kisha ikaanza safari ya kumzungusha Dr yule.

Dr Azam wa bandia aliwaza ya kuwa zile ni mbinu tu zinazotumika ili asijue wanakoelekea.

Dereva alizungusha gari zaidi ya dakika arobaini na tano na hakuonesha dalili ya kusimamisha gari.

Dr Azam aliamua kuwapunguzia safari,akajilaza na kukoroma.

Dereva na wasaidizi wake bila kujua hila ya Dr; wao walijua kweli Dr kalala hivyo walizunguka kidogo na hatimae waliingia nyumbani kwa Imamu Shafi'I.

Dr aliamshwa na vijana waliompokea.

Akapiga miayo ya uchovu kisha akajivuta na kurekebisha miwani yake na kushuka.

Kama mwewe angani, akazungusha macho yake kwa haraka sana na kufanikiwa kuona walinzi sita wenye bunduki wakiranda huku na huko.

Dr Azam wa bandia aliona mmoja wa walinzi akiwa na mbwa.

Akashanga!

Muislam safi kamwe huwezi ona mbwa akiranda nyumbani kwake hata kwa bahati mbaya hasa nyumba yenye uzio kama ile.

Hapo Dr Azam wa bandia alikubaliana na mawazo ya Haji kuwa Imamu na watu wake walikuwa wanatumia uislamu kama mwamvuli wa kufanya mabaya yao.

Dr alitukana kimoyomoyo.

Alikaribishwa ndani na Imamu Shafi'I na baada ya utambulisho alipelekwa kwenye chumba maalumu alichokuwa amelazwa binti yake.

Dr alijitia kusikitika kwa hali aliomkuta nayo binti yule.

Kila nusu dakika binti alikuwa anastukastuka na mwili ulianza kumpauka huku midomo ikiwa imekauka.


"Naombeni mlete maji ya kunywa" Aliagiza Dr Azam.

Walinzi wakaangaliana kisha Imamu akasema "Tulizuiwa kumpa maji jana Dr"

Dr Azam akamgeukia na kumkata jicho kali.

"Mimi ndie Dr na naomba mlete maji, mnazidi kumdhoofisha kwa kutokumpa maji,msiogope tafadhali" Alisema Dr Azam huku akiwa bize kuweka sawa vifaa tiba vyake.

Maji yaliletwa na Dr akamywesha yule binti.

Binti akapata kauli kwa mara ya kwanza tangu usiku uliopita.

Imamu alitabasamu kwa kitendo kile.

"Mgemuua huyu mtoto aisee" Alilalama Dr Azam.

Dr Azam alichukua damu kidogo na kuihifadhi kwenye kifaa maalumu kisha akaweka kwenye mkoba wake na kisha akaendelea kumkagua hapa na pale binti yule.


"Naiomba hewa tafadhali" Dr alisema huku akiinuka kuwatazama walinzi waliokuwa mle ndani.

Imamu aliwapa ishara nao wakatoka.

Alibaki Imamu Shafi'I ndani ya chumba kile.

Dr Azam alikuwa na sababu za kumbakiza Imamu mule ndani.

"Hii inaweza kuwa imesababishwa na nini Dr" Alihoji Imamu huku akikaa kwenye kiti kilichokuwa pembeni ya kitanda.

"Kwa haraka naona ni ugonjwa wa mlipuko kutoka kwa wanyama au basi alikula chakula chenye kuukataa mwili wake" Alijibu Dr.

"Chakula kinapimwa kabla ya kuliwa Dr; labda mnyama na sijui ni mnyama gani" Alisema Imamu Shafi'I.


"Huwezi jua katika mazingira yake ya kujidai" Alijibu Dr Azam.

Imamu alikunja uso kisha akasema
"Inabidi nimbadilishie walinzi, wamekuwa wazembe sana siku hizi".

Dr hakujibu.

Mara simu iliita na Imamu akampiga jicho Dr kwa wizi na kuipokea.

Kama imamu alidhani Dr hajamuona alikosea sana.

Macho ya Zedi Wimba p.a.k Dr Azam yalimnasa vyema kabisa na hilo ndilo lililomfanya awatoe walinzi mle ndani na kumbakiza Imamu peke yake.


Kabla ya kuongea Imamu alimuuliza Dr Azam

"Hivi kwenu ni wapi, waonekana si msomali eti"

"Kwetu ni South Africa" Alijibu Dr

Imamu aliongea kwa kipakistani(punjaban).

Kama alijua komando aliepembeni yake ni zwazwa basi alikosea sana.

Pakistani walikaa zaidi ya mwaka mmoja kabla ya kuanza kazi ile, hivyo moja ya lugha waliofundishwa ni hiyo Punja inayozungumzwa sana na watu wa mashariki mwa Pakistani.

Dr alielewa kilichozungumzwa, ila akaendelea na huduma yake ya msingi kwa yule mtoto wa kike.

Imamu alimaliza kuongea na simu kisha akaendelea kumtazama Dr Azam.

Dr Azam nae hakutaka kuendelea kuweka muda mrefu pale ndani hivyo,akachukua vidonge viwili na kumpa yule mtoto.

"Inabidi nikafanyie utafiti hii damu kisha nitakuja na majibu kuhusu aina ya dawa inayoweza kutumika kumtibu ila hizo dawa nilizompa zitamsaidia hadi keshokutwa nitakaporejea" Alisema Dr Azam.

Imamu alionekana kuwa na shaka.

Kwa nini?

Kwa sababu alihitaji mwanae apone haraka na pia alikuwa na sababu yake kubwa zaidi ambayo hakutaka kabisa Dr Azam afike pale siku hiyo.

Siku hiyo ambayo Dr aliahidi kurejea na majibu ni siku ambayo alitarajia kupokea ugeni nyeti sana na kwa kawaida akipokea wageni wa aina hiyo kamwe mgeni mwingine huwa had huruhusiwi kuingia ndani ya jumba lile.


Jitahidi iwe hata kesho Dr" Alisihi Imamu Shafi'i.

Dr alizidi kusisitiza huku akiweka sababu zake zenye mashiko kabisa.

Mwisho Imamu kwa kujali afya ya mwanae aliamua kukubali ombi la Dr.

Dr Azam alitolewa nje na kusindikizwa hadi ndani ya gari lililomleta kisha wakaanza tena kumzungusha kwenye vichochoro vya Mogadishu.

Saa moja badae walimfikisha kwenye lile duka la vifaa vya baiskeli na kumwacha apande kwenye gari lake.

Dr alielekea kwenye kituo chake cha kazi huku akiamini kabisa kuna watu maalumu waliwekwa kumfuatilia.
.
Dr alitabasamu baada ya kuwa amemtega Imamu kuhusu kwenda kwake siku ya tatu yake na alifanya vile baada ya kumsikia akiongea kuhusu kupokea wageni muhimu.

Dr Azam wa bandia alitaka kuwaona wageni wale.

Hakika hesabu zao zilikuwa sahihi kwa wakati huo.


***

Honda alikuwa hatamanila kwa kipigo alichopata na mwili wake ulikuwa umebabuka baada ya kuwashwa na moto.

Bahati nzuri ni kuwa moto hakumfikia kichwani na pia hakumpa madhara makubwa kwenye ngozi yake.

Ila vidonda vilipatikana.
Alikuwa amelipuliwa kwa dakika moja tu.

Alikuwa amefungwa na kuachwa aning'nie kwenye kamba huku chini kukiwa kumewekwa chupa zilizopondwa pondwa na hivyo kumfanya muda mwingi akunje miguu na kila alipoishusha aliishia kuchomwa na chupa.


Mwili vidonda na miguu ni vidonda vya kukatwa na chupa huku damu ikiwa inamwagika.


Pembeni yake alisimama jamaa ambae alikuwa ameshika bakora ya mpira.

Hakika alipitia mateso.

Yule kijana wa kisaudia alikuwa amesimama huku akingoja apewe majibu ya zilipo hizo karatasi ambazo zilikuwa zimepewa jina la Ukurasa wa Bombay.

Honda hakuwa na jibu la kuwapa.

****

Siku ya tatu iliwadia na Dr Azam alienda pale pale alipoambiwa angojee.

Alifika na kulikuta gari lile lile lililokuwa limemfuata siku iliopita.

Utaratibu ukawa ule ule na akapandishwa kwenye gari na kuzungushwa.

Nae hakubadilika alilala baada ya dakika thelathini kisha aliamshwa walipowasili kwenye jumba la Imamu.

Kama kawaida, macho yake makali yakanasa sura za walinzi sita aliowakuta siku ile pamoja na mbwa na pia aligundua kuna walinzi wengine zaidi waliokuwa wapo pale ndani.

Siku hii Dr Azam alikaguliwa na vifaa vya kisasa ili kama anasilaha aweze kuisalimisha.

"Dr; samahani kwa kinachotokea ila lazima usalama uzingatiwe" Imamu alimuomba radhi Dr Azam kisha akamwongoza wakaelekea kwenye chumba cha tiba.


"Dawa zako zimemsaidia sana mwanangu, anacheza hivi sasa na ameanza kurejewa na nguvu zake" Alisema Imamu Shafi'I.

Dr alitabasamu tu.

Kitu kingine alichogundua Dr Azam; ni kuwa nyumba ile hakukuwa na mwanamke hata mmoja tofauti na yule mtoto wa kike wa Imamu Shafi'I.

Dr Azam alitoa kichupa chenye tiba na kumchoma mtoto kisha akachukua dawa nyingine tena na kumchoma mtoto na hazikupita dakika sita mtoto alipitiwa na usingizi.


"Itabidi nisubiri hadi azinduke ndipo niondoke, hii ni kwa usalama wa afya yake" Alisema Dr Azam.

Imamu akang'aka!

Hakutaka Dr aendelee kupoteza muda pale.

****

Nb;bado hujachelewa ofa! Riwaya hii itakufanya usome nyingine zaidi kwa kuilipia Tsh 1000/= yani elfu moja utapata riwaya mbili, zile ambazo hujawahi kusoma kutoka kwangu.

Malipo fanya hapa 0758573660.
Whatsapp 0658564341.

Hakikisha jina limesoma Bahati Mwamba
Malipo yangu yamefika?
 
Back
Top Bottom