Riwaya: "Hujuma Nzito"

Riwaya: "Hujuma Nzito"

Hiyo inaitwa mbuzi kafia kwa muuza supu! Nathaniel kazi anayo, Kama kawa naweka alama. Tupo pamoja kamanda mpasta!!!
 
RIWAYA- HUJUMA NZITO-PART 32

[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
"Nisemehe dada yangu nisamehe sirudii tenaa...Nakufaa jamani!" alikuwa analalamika yule majeruhi kwa maumivu ya ajali na mateso anayopewa na Yasmine. Aliamua kuja nae viwanja vya Tanganyika Packers vilivyopo maeneo ya Kawe ili amfundishe adabu.

"Nani kakutumeni mnifuatilie nyenzo zangu nitajie haraka sana sasa kabla sijakubadilikia tena!!" akiongea Yasmine huku amechomoa bisu lake kubwa lenye ncha kali anachofanya ni kuchomachoma kwenye yale majeraha yake ya ajali kikatili sana. Hali ambayo ilikuwa inazalisha maumivu makali sana kwenye mwili wake.

"Mie simfahamu vizuri, ila Cobra yule mwenzangu aliyevaa fulana nyeupe ndio anamjua vyema nilisikia akimtaja kwa jina Nath-Masterminder ndio mwenye kazi hii" alijibu kwa haraka haraka huku anahema kwa nguvu ya kupata afueni kidogo. "Mlitaka kuniua kwa dau la shilingi ngapi? kenge nyie..!" aliuliza Yasmine huku akimtishia kutaka kumtoboa jicho kwa kisu.

"Wooooooooh....tobaaa, hapana dada sisi tulikuwa tunakufuatilia tu, afu tumpe ripoti yeye mwenyewe ndio alitaka akuue kwa mikono yake ya sisi ni visarata tu...!" alijibu kwa uoga yule mjuba mpaka Kachero Yasmine akajikuta ameshindwa kujizuia na kicheko. Alipozidi kumbinya na kuona hana lolote alijualo akamtelekeza pale pale kiwanjani anaagaragara na maumivu na kutimka zake anaelekea nyumbani kwa Nathanieli.

Barabara ilikuwa ipo safi muda huo haina msongamano kiasi ya kwamba ndani ya nusu saa tu alikuwa ameshafika karibia na anapoishi Nathanieli. Kwanza alipitiliza njia ya kuingilia nyumbani kwa Nathanieli akiwa anatokea Mwenge. Gari yake alienda kuiacha Hongera Bar, kisha akaanza kurudi mashimashi akitembea pembezoni mwa barabara upande wa kulia. Mgongoni alibeba begi lenye dhana za kazi anazohitaji usiku ule. Barabara hiyo aliyokuwa anatembea daima huwa ni yenye giza kuja uelekeo wa Chuo cha Ustawi wa Jamii.

Kabla hajaifikia fensi ya Chuo hicho akapenya kwenye ushoroba mwembamba. Akaanza kukiacha Chuo Cha Ustawi wa Jamii upande wa kushotoni kwake, akazidi kwenda uelekeo wa mkono wake wa kulia. Akatembea kama umbali wa makadirio ya dakika 5 akizipita nyumba kadhaa, mpaka akafika kwenye transfoma ya umeme iliyokuwa imejitenga kando. Alipofika hapo akasimama kwenye nguzo zile mbili za umeme zilizoshikiza transfoma hiyo.

Akaangalia kushoto na kulia kama mkwapuzi anavyofanya, hakuona mtu yoyote. Akaanza kutoa vifaa vyake vya kazi alivyobeba toka garini. Akaisogelea transfoma hiyo na kuanza kuikorokochoa kwa msaada wa kurunzi yake. Haikichukua hata dakika 3, transfoma ile ikabutuka kwa sauti ya kishindo kizito kilichosikika eneo lote lile la Bamaga linalohudumiwa na trasfoma hiyo.

Giza totoro likatawala eneo lote, hima hima akafyatuka nduki mpaka nyumba ya 3 mbele yake yenye roshani mbili. Nyumba ambayo nayo ilikuwa imetawaliwa na giza. Alipofika hapo kwa mbinu zake za kimedani za vita akafanikiwa kuruka ukuta wa nyumba hiyo na kutua salama bila kishindo chochote. Akaganda kwa dakika kama 2 hivi akashangaa hamna hata mbwa. Muda huo huo akasikia jenereta linaunguruma na umeme ukawaka.

Akashukuru Mungu kwa kufanya haraka kuingia kabla ya kuwashwa kwa umeme. Kwa sababu ni mara yake ya pili kuingia ndani ya nyumba ile hakupata tabu njia za kupita kuingia ndani huku akijikinga na kamera za ulinzi. Taa za ndani ya nyumba zilikuwa zimezimwa kuashiria hamna mtu. Ni taa za nje pekee ndio zilikuwa zinawaka kipindi hiko kwa ajili ya kiusalama na kung'arisha mazingira ya nje.

Akafanikiwa kukwea mpaka ghorofani kupitia bomba la Kupitisha maji taka toka juu ya roshani kushusha chini. Kwa zana zake makini za kazi akafanikiwa kuingia ndani ya nyumba kupitia dirisha la jikoni. Moja kwa moja bila kuwasha taa akaenda mpaka mlango wa chumba kulala cha Nathanieli. Kwa kutumia mkungu wa funguo malaya bandia alizonazo akafanikiwa kufungua chumba hicho na kuingia.

Alipoangaza chumbani mule kwa kurunzi akakuta hakuna dalili za uwepo wa mtu yoyote. Kwa kutumia kurunzi yake hiyo akaangaza kwenye meza ndogo ya kujisomea iliyopo pale chumbani akakuta kuna daftari yenye ganda gumu jeusi kwa nje likiwa limefunguliwa.

Akavutika kwenda kuangalia nini kilichokuwa kinasomwa muda mfupi uliopita na Nathanieli. Akakutana na dondoo za kikao cha Nyasa Empire Supporters (NES) kilichofanyika asubuhi yake. Tabasamu lenye bashasha mpwitompwito likajengeka usoni mwake. Akazisoma dondoo hizo kwa umakini zikielezea mpaka safari ya marehemu Dr.Pius Chilembwa ya kuelekea nchini Afrika ya Kusini nyumbani kwa Profesa. Alipomaliza kusoma dondoo hizo kwa umakini mkubwa ndipo akatanabahi kumbe walimgusia yeye kwenye kikao chao hicho lakini bila kumtaja jina lake.

Aahaaaaah...Kumbe ndio maana Nathanieli kawatuma wahuni wake wanifatilie nyendo zangu..!" alinong'ona peke yake, huku akijiapiza lazima amtangulize akhera Nathanieli kabla hajamharibia kazi yake iliyomleta Benki Kuu. Kazi ambayo ilikuwa inakaribia ukingoni kumalizika. Siku za washirika wa Nyasa Empire Supporters (NES) kuishi raha mustarehe wakivuta hewa safi ya uraiani zilikuwa zinahesabika kwa vidole.

Haraka haraka kwa kutumia mtandao wa simu yake akampasha taarifa hizo mpya Bosi wake, Kachero Manu ikiwemo ya ujio wa Dr Pius Chilembwa nchini Afrika ya Kusini. Akamtumia pia picha za Dr. Pius Chilembwa alizoziskani kazini kwake kule Benki Kuu.

Alipomalizana na Kachero Manu akaanza kujisikia kichwa kinagonga kwa mbali. Akakumbuka kuwa amesahau kunywa dawa zake alizoshauriwa na Daktari wake. Ikabidi hapo hapo achomoe tembe zake kwenye mfuko wa suruali yake ili afanye maarifa ya kuzimeza.

Akaelekea mpaka ilipo friji ndogo iliyomo ndani ya chumba kile na kuifungua kisha akaichomoa chupa ya maji ambayo ilikuwa bado haina ubaridi wa kutosha. Akameza tembe zake huku akisukumizia na maji.
Baada ya hapo akaelekea moja kwa moja ukutani na kuwasha kiyoyozi ili kuleta ubaridi wa kutosha ndani ya chumba kile. Akaelekea kwenye kitanda na kukalia huku amening'iniza miguu yake chini ya sakafu. Akavua koti lake lililokuwa linampa joto na kuliweka pembeni.

Akabakia na fulana nyepesi iliyomkaba vyema na kukichora vyema ramani ya maeneo ya kifua chake. Akaichomoa bastola yake na kuikamata vyema mkononi akimsubiria mbaya wake afike. Alitaka ampe mshtuko wa ghafla Nathanieli, mshtuko ambao utamfanya asiyaamini macho yake. Ataona kama mzuka wa Yasmine umeshuka ghafla jumla jamala mpaka chumbani kwake bila kutoboa popote.

Kachero Yasmine akatupia jicho simu yake ya mkononi akakuta ni saa 5:00 za usiku. Akaamua kuulaza mgongo wake kwenye mto pembeni ya kitanda huku anachezea simu yake ya mkononi bastola kaegesha kwenye mapaja yake.
Kile kiyoyozi alichowasha kilikuwa ni kosa kubwa la mwaka kwake. Kiliupoza vyema mwili wake na joto la nje, na kuupa starehe muruwa isiyomithilika. Akajikuta anaanza kusinzia bila kupenda, ghafla akaanza kukoroma usingizi mzito ulimvaa bila kupenda akiwa juu ya kitanda cha Nathanieli.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
"Yasmiii...Yasmii.... njoo giza linaingia let's go...baby time is over...!" Kachero Manu alikuwa anamuita pacha wake kwa sauti ya kudekeza akimchombeza kwa lugha ya kimombo, wakiwa wapo kwenye kisiwa cha Bongoyo, kilichopo kaskazini mwa Jijini la Dar es Salaam. Kisiwa hicho kilikuwa kipo karibu na Msasani Peninsula.
Walikuja hapo Kisiwani kwa kutumia boti ya kukodi toka “Slipway Hotel” wakiwa wanaendesha wenyewe boti hiyo. Walikuwa wamefika tokea saa 5 asubuhi na sasa ilikuwa ni saa 12:37 jioni.

Waliogelea, walikula maakuli anuwai mbalimbali na mashrabu tofauti tofauti kuanzia Soda, juisi mpaka mvinyo. Walicheza kila aina ya michezo kuanzia riadha, mpira wa mikono mpaka mieleka.
Ili mradi mtoko wao siku hiyo ulikuwa na madhumuni ya kusahau shida zao chini. Walitaka kubanjuka kwa furaha zote kama vile dunia ni pepo ndogo, hamna kifo, hamna kuugua wala umaskini wala tabu na mateso yoyote.

Kachero Manu alishachoka vibaya sasa alikuwa anahitaji kurudi nyumbani tu magharibi hiyo akaupumzishe mwili. Wakati huo Kachero Yasmine kwa jinsi alivyokuwa anayakata maji bila kuchoka utasema ndio amekuja pale Kisiwani muda mfupi tu uliopita. Kuogelea Kachero Yasmine kwake ilikuwa ni zoezi analolipenda sana na kajifunza kuogelea kwao Zenji tokea ana umri wa miaka 4.

Kachero Yasmine aliposikia wito ule wa Bosi wake Kachero Manu akatii bila shuruti na kuanza kurudi nchi kavu. Kachero Manu alikuwa amevaa bukta yake nyepesi ya kijani huku juu amevalia singlendi nyeupe. Chini alikuwa amevaa sendo nyeusi zenye ufito wa chata ya 'Adidas'. Aliposimama Kachero Manu uelekeo wake wa macho ulikuwa kule anakotokea Yasmine.

Kwa uchokozi tu na kwa jinsi alivyozoea kumtia shemere Bosi wake, Yasmine alipotoka tu nje ya bahari akawa anatembea kwa mikogo mithili ya mlimbwende wa Miss Tanzania juu ya jukwaa anategemea kupata maksi za majaji. Juu Yasmine alikuwa amevalia kitopu maalumu cha kuogelea kilichoshindwa kabisa kusitiri tumbo lake dogo na kukiacha wazi kitundu cha kitovu chake.

Pedo yake ya rangi ya pinki ilimchora vyema umbo lake namba 8 la mahaba. Pedo hiyo kamwe haikuzuia makalio yake laini yaliyokuwa yakitikisika kimahesabu yasionekane. Miguuni alikuwa yupo peku peku na kuviacha wazi vidole vyake virefu vilivyobanana vizuri.
Kachero Manu kila siku yupo na pacha wake wa kazi Yasmine miaka nenda rudi lakini kila uchao alikuwa anamuona ni mpya machoni mwake. Sasa hii leo ilikuwa sifa bin makusudi kwa jinsi macho yake yalivyokuwa yanamthaminisha pacha wake akiwa amelowana maji tepetepe mwilini.

Nywele zake za singa, Kachero Yasmine ambazo kila siku anazifungaga mchicha, leo zilikuwa zimemwagika mwa mwa mwa mpaka mgongoni zikiwa zimetota maji. Kadri alivyokuwa anasogea karibu ndipo Kachero Manu mapigo yake ya moyo yalipokuwa yanazidi kumdunda kwa hawaa ya kufanya mapenzi.
Moja ya miiko yao Makachero ilikuwa mkiwa kazini, kazi na dawa ni marufuku kabisa. Lakini leo uzalendo ulikuwa unataka kumshinda Mzee mzima.

Ibilisi wa ngono alikuwa anampa tashwishi za kupupia maovu, amempanda kichwani anamwambia "hamna Bosi Mtanika hapa, mpo wawili tu, mkomalie kweli huenda akakutunuku penzi".
Alipofika karibu tu katika umbali sifuri, Kachero Manu akajikuta anaropoka bila kuangalia, maneno yanabubujika tu kinywani huku tayari ameshakibambia kiuno cha Yasmine anakitomasatomasa.


"Hakika mtoto umeumbika mithili ya malaika,
Japo mbinguni sijafika lakini na uhakika kwa kila mwanaume rijali akikuona lazima udenda churu churu churu utamchuruzika.
Naomba japo yako dakika nipate kukueleza moyoni yaliyonifika!
Kwani siwezi tena kuficha jinsi navyokuhusudu mtoto Yasmine".

Kachero Manu alijua kuilenga hiyo siku ya kujinadi kwa kumwaga sera zake. Kwani Yasmine alikuwa nae amezidiwa haswa na ashki, ndio maana muda mrefu alikuwa yupo majini kujiliwaza, huku akimkumbukia mpenzi wake Dr.Rishedy Shareefy anayefanya maisha yake huko Arabuni nchini Qatar.

Kwa mwaka mpenzi wake huyo huwa anakuja nchini Tanzania si chini ya mara 4 lakini safari hii alikuwa amekaa muda mrefu sana hajaja kwa muhibu wake Kachero Yasmine kutokana na janga la ugonjwa hatari wa "Covid-19" lililoitikisa dunia.

Hali hiyo ilikuwa inamuweka kwenye mazingira magumu sana, kujizuia na mihemko ya mwili wake. Yasmine alipotupa macho kwenye kifua cha Bosi wake kilichoumbika kutokana na mazoezi na lishe bora anayekula, akazidi kulainika kama mlenda.

Akajikuta anakubali kila anachofanyiwa na Kachero Manu. Kachero Manu akaona fursa ndio hiyo, asije akachekwa akaambiwa shamba la mahindi limepandwa karibu na jirani Kibogoyo anashindwa hata kuiba hindi la kuchoma. Akawa sasa anamkunja na kumuangusha chini ya mchanga pacha wake Yasmine. Kulikuwa hamna maneno tena, bali vitendo ndio vinaongea zaidi.

Kachero Yasmine alikuwa yupo ndotoni pale kitandani kwa Nathanieli alipojilaza na kupitiwa usingizi wa ghafla usio hata na adabu. Akawa anaota yupo kwenye mahaba mazito na Bosi wake Kachero Manu katika kisiwa cha Bongoyo kumbe hakujua yupo chumbani kwa adui yake na yupo kwenye hatari.

Ilipofika saa 5:30 za usiku Nathanieli alikuwa ndio anawasili pale nyumbani kwake. Akapiga honi na kufunguliwa geti akaingia na kuegesha gari lake. Baada ya kuongea mambo mawili matatu kuhusu matukio ya pale nyumbani na Shamba-Boi wake akapandisha juu ya nyumba yake. Akiwa hana wasiwasi wowote akafika na kufungua mlango wa chumba chake.

Alipowasha taa tu ya chumbani mwake alipigwa na mshtuko wa ghafla nusra aanguke chini kwa presha. Alichokiona kitandani pake kilimstaajabisha sana. Mwanamke mrembo akiwa amejifunga kilemba kichwani mwake, juu kavalia fulana iliyochongoa chuchu chake ndogo alikuwa amejilaza kitandani mwake.
Mwanzoni aliogopa kumsogelea akijua huenda ni Jini mahaba amejigeuza mwanamke kuja kumtega.

Lakini alipomuangalia vizuri akaona ana bastola mapajani mwake. Akapata nguvu kujua huyu ni adui yake. Akachomoa bastola yake kiunoni, akavaa ujasiri na kuanza kumsogelea kwa tahadhari kubwa akiogopea isije ukawa ni mtego kwake.
Alipomkaribia kabisa na kumgeuza sura yake, ndipo akamgundua kuwa ni Yasmine. Alipomuona ni yeye tena akiwa amebeba silaha akajua asilimia 100% kabisa kuwa ni adui yake. Alikuwa anataka kumuamsha usingizini ili apambane ana kwa ana, lakini akili na mwili vilikuwa vinakosa ushirikiano
ITAENDELEA
MAMBO YANANOGA SANA
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji123][emoji1732][emoji1732].

Sent from my TECNO CC6 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom