Riwaya: "Hujuma Nzito"

Riwaya: "Hujuma Nzito"

Mkuu acha kuharibu.

Hao unaowatumia kwenye emails unawauzia au???

Kama unawapa bure tambua unatuonea sisi ambao hatuhitaji kutumiwa.

We bana Kisha ishushe hapa hapa mpaka mwisho kama ulivyosema kuwa itafika mwisho ili wote tuimalize kwa pamoja.

By.
mjumbe wa kamati ya roho mbaya.
 
nasubiri riwaya iwekwe hapa mpaka mwisho ndo nije kusoma mwanzo mwisho.
NOTE: silipii riwaya, nasoma bwerere
 
Mkuu acha kuharibu.

Hao unaowatumia kwenye emails unawauzia au???

Kama unawapa bure tambua unatuonea sisi ambao hatuhitaji kutumiwa.

We bana Kisha ishushe hapa hapa mpaka mwisho kama ulivyosema kuwa itafika mwisho ili wote tuimalize kwa pamoja.

By.
mjumbe wa kamati ya roho mbaya.
Sio.riwaya Hii wanayoiomba ni nyingine kabisa

Sent from my TECNO CC6 using JamiiForums mobile app
 
RIWAYA-HUJUMA NZITO-PART 39


️[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Kachero Manu alishawasili eneo la tukio tayari kwa kuhudhuria mkutanoni. Siku hiyo ya mkutano Hoteli hiyo ya "The Pride of Indian Ocean" ilikuwa inalindwa na askari wa kike warembo waliokodishwa toka nchini Ethiopia wakiitwa kwa lakabu ya "Black-Guard". Askari ambao kama watavua gwanda zao na kuvikwa libasi za ulimbwende basi mmoja wao anaweza kushinda taji la "Miss World"'. Walikuwa ni visura haswa ambao nmoja wao akikubali uwe nae unaweza kuuza hata nyumba yako ya urithi ili mradi tu upate pesa za kumhudumia yeye asije kukuacha kwenye mataa.

Walinzi hao zaidi ya 20 walijigawa kivitengo kwa ajili ya kulinda Hotelini pale. Walinzi wa kila siku walipewa mapumziko maalumu siku hiyo wasitie mguu eneo hilo. Ni wafanyakazi wa usafi na wapishi tu wa Hotelini hapo ndio walikuja kazini kama kawaida yao. Yasmine taarifa zote za mkutano kufanyikia hapo alikuwa anazipata kupitia vifaa vya siri alivyovifunga nyumbani kwa Flora kupitia mazungumzo ya Dr Pius Chilembwa na washirika wake. Kizuri zaidi hata Professor Potchefstroom nae alifikia nyumbani kwa Dr Pius Chilembwa.

Yasmine kupata kibali cha kuingilia hapo Hotelini, alimsaka dada mmoja muajiriwa wa kitengo cha usafi hapo Hotelini na kumtongoza ampe kitambulisho chake cha kazini. Pia alimtaka siku hiyo asikanyage kabisa ofisini. Alielekezwa nia na madhumuni ya Kachero Yasmine Hotelini hapo, akafanikiwa kukipata kitambulisho chake cha kazi. Yasmine akapewa Alifu Bee Tee za mazingira na utamaduni ya usafi Hotelini hapo ili asije kuyaboronga mambo.


Yasmine habari yake ikawa imeshawezekana ya yeye kutinga pale Hotelini "The Pride of Indian Ocean".
Pia Yasmine kupitia idara iliyopo chini ya Wizara ya Ardhi inayohusika na upitishaji wa ramani za majengo, akapata mchoro mzima wa jengo hilo la Hoteli ya kisasa lililojengwa na kampuni ya kigeni na mkandarasi tokea Uisraeli. Kufanikiwa kufika Hotelini hapo ni mwendo wa nusu saa kwa boti yenye kasi kutoka Ufukwe wa Kunduchi.


Kachero Manu yeye kufika Hotelini nae haikuwa tatizo, ila tatizo kubwa ni kwake ni namna ya kuingia katika ukumbi wa mkutano. Katika kuimarisha usalama wao zaidi kwa ajili ya kuhofia mamluki kupandikizwa kutokana na kupotea kwa 'Man-Temba', kifo cha kutatanisha cha Nathanieli, kupotea kwa nyaraka za siri za Dr Pius Chilembwa na mengineyo yaliyowafanya vigogo wa juu watumie mtindo wa kuingia kwa kutumia nywira ya siri. Nywira ambayo kila mwanachama wa 'Nyasa Empire Supporters' (NES) aliitumia pindi aliposajiliwa kwa mara ya kwanza kundini.


Tangazo la ghafla lilitoka hapo hapo kabla ya kuingia ukumbini wakiwa katika foleni za kuingia ukumbini. Kifaa maalumu kiliwekwa kinachokutaka uingize nywira ya siri ndio mlango ufunguke uingie ndani. Mwanachama ulikuwa unapewa nafasi ya kujaribu namba yako ya siri mara tatu tu ukikosa, unakamatwa na kwenda kuhojiwa.


Kachero Manu jasho jekejeke lilikuwa linamtiririka akiwa katikati ya foleni hawezi tena kuchomoka huku walinzi wakiwa makini kutaka kuwatia mbaroni washukiwa wowote wale. Ikafika zamu yake Kachero Manu ya kubonyeza namba za kitufe kile ili mlango umruhusu kuingia ukumbini. Alishajua habari yake imekwisha atageuzwa kuwa asusa ya mkutano huo wa 'Nyasa Empire Supporters' (NES).


Akawa anawaza hasira atakazokuwa nazo Dr. Pius Chilembwa na Professor Potchefstroom jinsi watakavyomshukia kama kipanga anavyokishukia kifaranga cha kuku. Hasa kwa kutambua kumbe alikuwa ni kirusi kilichopandikizwa kwao na Usalama wa Taifa. Akajipa moyo, chambilecho 'tumbo la shari huzaa heri'.


Akaanza kubofya mara ya kwanza, mashine ikapiga kelele ya kukataa kuwa namba ya siri iliyoingizwa sio yenyewe. Akajitutumua kubahatisha tu kwa kubonyesha namba yoyote ile huenda fali njema ikamuangukia mlango ukafunguka. Mashine ikagoma kwa mara ya pili huku ikimpa nafasi ya mwisho ya kujaribu. Walinzi wale sasa wakamsogelea kwa ukaribu zaidi kumbana ili asije akawatoroka tayari walishamtilia mashaka.


Kachero Manu uso wake ulishapigwa na fedheha na soni huku akijua tayari kashakamatika kirahisi bila hata kunusa ukumbini. Akajitutumua tena kwa mara ya mwisho kujaribu kuingiza namba, huku akiomba kila aina ya dua. Kilichotokea alishtukia tu kashapigwa mtama wa nguvu na wale walinzi wa kike. Tayari akabebwa mzobemzobe kama mpira wa kona anagombaniwa anapelekwa sehemu kusikojulikana.


Tenge tehanani ikaibuka zogo mtindo mmoja wakifurahia mfumo huo utakaosaidia kukamatwa kwa mamluki wote waliopandikizwa.
Washirika wote wakafanikiwa kuingia kwenye mkutano huo kasoro Kachero Manu pekee. Mkutano huku ukiwa unaendelea baadhi ya vigogo wa NES wakawa wapo na Kachero Manu wanamdodosa kwa undani.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]

"Hongera sana Kachero Manuel Yosephu kwa kazi nzuri uliyoifanya mpaka sasa" alifungua maongezi yake Chew-Master kwa sauti nzito, akiwa ameficha uso wake kwa kitambaa maalumu. Hakutaka Kachero Manu atambue anaongea na mtu gani. Walikuwa ni watu wanaotambuana kiundani kabisa kutokana na kukutana katika vikao mbalimbali vya ulinzi na usalama wa nchi.

"Lazima nikubali uwezo wako hasa kutokana na kwamba hamna mtu aliyejaribu kuitikisa ngome yetu akabakia salama. Nadhani ulisikia kilichompata Inspekta Mengi Matunda kashabakia mifupa mitupu huko kaburini pindi alipochaguliwa kufanya taftishi ya kundi letu la Nyasa Empire Supporters (NES)" akaweka kituo cha maongezi yake akawasha sigara yake kisha akasimama na kuelekea mpaka kwenye kiti alichofungwa Kachero Manu. Akapiga pafu ndefu kisha akamuinamia Kachero Manu kisha akampumulia moshi wa sigara usoni mwake.

"Koh..koh..koh...stupid, stop this you coward...!" aliongea kwa shida Kachero Manu huku akiwa anakohoa kutokana na kupaliwa na moshi wa sigara. "Ha..Ha... Ha ..Ha....Kachero namba wani wa nchi ya Tanzania, tulitamani uwe Kachero namba wani kwenye utawala wa Dola ya Nyasa kama ungetulia tuli na kuacha kiherehere chako. Hivyo kimbelembele chako cha kujifanya mtu wa kazi kimekuponza, umetukwepa sana kuanzia kule Arusha kwenye ajali ya bomu kwenye gari ulivyookolewa kimiujiza na mizimu ya babu zako wa Kimwera" aliendelea kumsomea risala yake ya kifo yenye kebehi ndani yake.
"Stop talking non-sense....kama kidume cha mbegu vua hiyo maski usoni, vinginevyo mie naona unaniimbia taarabu tu, kwa sauti yako nyororo" aliongea Kachero Manu kwa kumkatisha maongezi huku akiombea itokee fursa ya wafanye makosa aweze kuwageuzia kibao.

Askari wale wa kike ambao hawajui lugha ya kiswahili hata ya kupapasia waliweka silaha zao za kivita, mkao wa kushughulika. Wao wakati wote walikuwa wanawasiliana kwa lugha ya Kiingereza tu. Maneno yale ya dharau yaliyotamkwa na Kachero Manu dhidi yake yalimchoma vilivyo Chew Master. Uso wake ulibadilika na paji lake kutengeneza matuta. Akapiga mluzi uliosababisha ajitokeze kipande cha mtu mwenye miraba minne mweusi tii.
Mtu huyo alikuwa amebeba pasi ya umeme mkononi mwake.

Haraka haraka bila kuambiwa chochote akaenda kuichomeka ukutani kwenye soketi ya umeme, kisha akamvamia Kachero Manu na kuanza kuirarua singlendi yake, akimuacha kidari wazi. Pasi ikawa imeshashika moto kisawasawa. Akaikamata pasi na kumuwekea kifuani Kachero Manu.

"Aaaaaaaaah....Aaaaaaah....Aaaaah..". Kachero Manu alikuwa analalamika kwa maumivu makali. Chew-Master alikuwa anacheka mbavu hana jinsi Kachero Manu anavyoteseka kwenye moto wa pasi.
"Yule nyau mwenzako wa kike anayejifanya muajiriwa wa Benki Kuu, nae muda sio mrefu atakamatwa, amechoropoa nyaraka muhimu nyumbani kwa rafiki yake Flora, hivyo huna msaada leo, tutaondosha roho zenu na kukutupa baharini miili yenu iwe chakula cha samaki" aliendelea kubwabwaja Chew-Master maneno ya kumtia hasira.

Baada ya mateso ya moto wa pasi, ikaanza adhabu ya mijeledi ya mgongoni toka kwa wale walinzi wa kike toka Ethiopia. Kipindi chote wakati atateswa alikuwa anarekodiwa video kwa kutumia simu ya mkononi. Huku 'Chew Master' akimchagiza kuwa atakapokufa video yake itakuwa inaonyeshwa kwenye vipindi vya televisheni kila siku kabla ya kusomwa taarifa ya habari kama mmoja wapo wa maadui wa Dola ya Nyasa.

Baada ya muda fulani, likaja agizo la Kachero Manu kupelekwa kwenye ukumbi wa mkutano ili ashuhudiwe na watu wote, wafuasi wote wa 'NES'. Akafunguliwa kamba kutoka kwenye kiti na kukokotwa akiwa sasa amefungwa pingu za mikononi. Mwili wote ulikuwa unavuja damu, huku akitembea kwa kuchechemea kutokana na maumivu ya vipigo. Kachero Manu kifo alikiona kabisa kipo mbele ya uso wake kinakaribia kumvaa kimuondoshe duniani.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
ITAENDELEA

Sent from my TECNO CC6 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom