Riwaya: I died to save my President

Riwaya: I died to save my President

I DIED TO SAVE PRESIDANT

Sehemu 65

Frank,Obi na vijana
walioongozana nao wakarejea tena
katika makazi ya akina Elvis na kukuta
mlango mdogo wa geti waliouacha
wazi ukiwa umefungwa.
"Mlango huu tuliuacha wazi
lakini umefungwa.Hii inaonyesha
hawa jamaa tayari wamekwisha rejea
na wako ndani" akasema Obi
"Wapange vijana haraka sana
muingie ndani na muwe waangalifu
sana.Jitahidini kuwadhibiti
ninawahitaji wote wakiwa hai"
akasema Frank na Obi akawapa
maelekezo ya kufanya vijana wake
halafu yeye na vijana wanne
wakarukia ndani na baada ya
kuhakikisha kuko shwari wakaelekea
katika mlango wa kuingilia sebuleni wakachungulia ndani hakukuwa na
dalili zozote za mtu licha ya taa
kuwaka.Akajaribu kukinyonga kitasa
mlango ulikuwa umefungwa kwa
funguo.Akawafanyia ishara vijana
wake wakae tayari akatoa funguo
bandia na kuufungua ule mlango na
kisha akaingia sebuleni akifuatiwa na
vijana wawili .Walikagua nyumba yote
lakini hakukuwa na mtu,akampigia
simu Frank
"Mkuu hakuna mtu ila
inaonekana walikuwa hapa muda si
mrefu kwani wamechukua vitu vyao
na kuondoka.Hakuna nguo wala
mabegi tuliyoyakuta wakati ule"
"Damn it !! akasema kwa hasira
Frank huku akiupiga usukani kwa
mikono yake.Akaegemea kiti na
kuzama mawazoni
"Sijawahi endeshwa na mtu
yeyote kama hivi sasa ninavyoendeshwa na hawa
jamaa.Lakini sikati tamaa lazima
watapatikana tu.Mimi huwa sichezewi
kiasi hiki.Watauona moto wangu"
akawaza Frank halafu akamgeukia
Winnie aliyekuwa amefungwa mikono
kiti cha nyuma
"Winnie ninakupa nafasi ya
mwisho ya kunionyesha mahala alipo
dada yako" akasema
"Frank nakuomba mzee uniamini
ninalokwambia.Dada na hao jamaa
niliokueleza wanaishi katika nyumba
hii.Tuendelee kusubiri lazima
watarudi" akasema Winnie.Frank
akatafakari halafu akatoa simu katika
droo ya gari na kumfungua Winnie
mikono akampa ile simu
"Simu yako hii nataka uiwashe na
uwasiliane na dada yako mwambie
kwamba uko hapa na akufuate mara
moja" akaamuru.Winnie akawasha simu ile na kuzitafuta namba za Vicky
akapiga lakini simu ya Vicky haikuwa
ikipatikana.Akapiga tena jibu likawa
lile lile simu ya Vicky haipatikani
"Endelea kujaribu kupiga kila
baada ya dakika kumi.Leo tutaendelea
kukaa hapa hapa hadi asubuhi.Lazima
tuwasubiri" akasema Frank na
kumpigia simu Obi akamtaka atoke
mle ndani na kuwapanga vijana pale
nje wawasubiri akina Elvis
"Uzima wako ni pale dada yako
atakapopatikana lakini kama
ukishindwa kusaidia katika kumpata
basi jihesabu wewe tayari ni mfu"
akasema Frank
"Frank nakuomba tafadhali
usiniue.Kama ningejua mahala
ambako dada anaweza kupatikana
ningewaeleza lakini sijui.Ninafahamu
mahala hapa kwani hata mimi nilikuwa nimefungiwa hapa" akasema
Winnie
" Salama yako ni kama watarejea
hapa lakini kama wasipoonekana
ninasikitika kwamba sintaendelea
kukuacha hai tena" akasema Frank
Masaa yalizidi kusonga bila ya
akina Elvis kuonekana pale
nyumbani.Taratibu kukaanza
kupambazuka na Obi akamfuata Frank
ambaye hakufunga ukope wake
akisubiri akina Elvis warejee
"Mkuu kumeanza kupambazuka
na hawa jamaa hawajareea hadi muda
huu tufanye nini? akauliza Onbi
"Tuondokeni ili watu wasije
wakapatwa na wasi wasi wakitukuta
hapa ila waache vijana wawili
waendelee kuchunguza na pindi
wakiwaona akina Elvis wamerejea
basi watujulishe mara moja.Huyu
msichana mtandoka naye.Hakikisheni mmempa kila aina ya mateso ili aseme
ukweli wake ni nani walimtuma
kwetu?Kama hata baada ya kuteswa
ataendelea kuwa mgumu wa
kusema,kill her"akasema Frank huku
akimtazama Winnie kwa macho
yaliyojaa hasira
"Sawa mkuu" akasema Obi na
kumshusha Winnie kutoka katika gari
la Frank akampakia katika gari lao
wakaondoka zao

*********************

Siku mpya ilianza na habari
kubwa iliyoliamsha taifa asubuhi hii ni
onyo la jeshi la polisi likiwaonya
wafuasi wa vyama vya upinzani
wasithubutu kuhudhuria mkutano
ulioitishwa na viongozi wao kwani
haukuwa na kibali.Hii ni habari kubwa
iliyoandikwa karibu na magazeti yote na kutangazwa na vituo vyote vya
redio na runinga.Wakati habari hii
ikitangazwa Elvis na Steve tayari
walikwisha amka na walikuwa
sebuleni wakitazama taarifa ya habari
kufuatilia kilichokuwa kinaendelea
nchini.
"Hakuna jipya haya yote ni ya
wanasiasa.Tuwaachie mambo yao na
sisi tuendelee na yetu.Nadhani ni
wakati wa kwenda kuanza kumfatilia
Irene Mwabukusi.Nimefikiria na
nimeona itabidi twende wote katika
kazi hii.Irene ana mahusiano na akina
Frank na hatujui yawezekana naye
akawemo katika mtandao wao na
hivyo akawa ni mtu mwenye ulinzi au
yawezekana Frank akatuma watu
kwenda kumuua endapo atagundua
kwamba tumezipata nyaraka zile za
kutolea mzigo bandarini.Watu hawa ni rahisi sana kuua ili mambo yao
yasijulikane" akasema Elvis
"Are you sure?Steven akauliza
"Yes I'm sure.Siwezi kukuacha
ukaenda huko peke yako ni hatari
sana.Wasiliana na Samira kama tayari
amekwisha fika kumchukua Omola
kumpeleka ikulu.Mimi ngoja
nikajiandae kwani siwezi kutoka bila
kubadili mwonekano wangu" akasema
Elvis na kutoka akarejea chumbani
kwake akajiandaa kwa ajili ya kutoka
kwenda kuanza kazi.
"Ouh ! hakika unajua
kujibadilisha mwonekano.Hakuna
yeyote atakayekutambua kwa
mwonekano huo" akasema Steve
aliyeingia chumbani wakati Elvis
akijiandaa.
"Vipi samira umewasiliana naye?
"Ndiyo.Yuko njiani hivi sasa
akielekea hotelini kwa Omola" Good.Inabidi tuzungumze pia na
Omola.Piga simu hotelini
wakuunganishe naye.Halafu itabidi
tutafute simu nyngine tatu kwa ajili ya
Omola,Vicky na Graca ili iwe rahisi
kuwasiliana" akasema Elvis na Steve
akapiga simu hotelini kwa Omola
akaunganishwa naye
"Hallo Steve habari yako?Elvis na
wengine wote hawajambo?
"Wote wazima kabisa.Vipi wewe
hali yako"akauliza Steve na kuiweka
simu katika sauti kubwa ili Elvis naye
aweze kusikia mazungumzo yale
"Hali yangu ni nzuri
kabisa.Imekuwa vizuri umewahi
kunipigia kwani nilikuwa na mpango
wa kuwapigia kuwajulisha kuwa ile
simu ya mdogo wake Vicky
imewashwa lakini inaonekana
amekuwa akizungushwa sehemu mbali mbali .Mpaka sasa bado wako
katika mzunguko." akasema
"Hallow Omola,Elvis hapa
ninaongea" akasema Elvis
"habari yako Elvis."
"Nzuri Omola.Kwa kuwa
unakwenda ikulu asubuhi hii tutahitaji
kuipata hiyo kompyuta yako ili
tuendelee kumfuatilia Winnie na
kufahamu mahala aliko.Jioni ya leo
tutakutana ili utupe mrejesho wa kazi
yako ya leo"
"Sawa Elvis.Mtaipataje?Mnakuja
huku hotelini kuichukua?akauliza
"Ndiyo tunakuja hapo muda si
mrefu.Tusubiri" akasema Elvis na
kukata simu
"Hizi ni habari njema kwa
Vicky.Inabidi afahamishwe ili aweze
kupata moyo kwamba mdogo wake
bado yuko hai" akasema Elvis na
kumalizia kupakia silaha zake katika kibegi kidogo wakatoka na kuelekea
katika chumba walimolala Vicky na
Graca,akagonga mlango na Graca
akaufungua.Macho yake yalionekana
bado amelemewa na usingizi.
"Elvis,karibuni.Habari za
asubhi?akasema Graca huku
akiyafikicha macho yake
"Umeamkaje?Akauliza Elvis
"Nimeamka vizuri."
"Nahitaji kuzungumza na Vicky"
"Vicky?! Graca akashangaa
"Ndiyo"
"Hakuwaaga?Graca akauliza na
akina Elvis wakatazamana
"Hapana.Ameondoka?
"Vicky ameondoka alfajiri
akasema kuna sehemu
anakwenda.Mimi nilikuwa na usingizi
sikumtilia maanani nikajua
atawajulisha." Where is she?akauliza Elvis na
kutoka nje wakalikuta gari lao lipo ila
geti lilikuwa wazi
"Inawezekana labda amekwenda
mahala kutafuta mahitaji ya hapa
nyumbani.Anyway atakaporejea
mwambie sisi tumetoka na asitoke
atusubiri hadi tutakaporejea"akasema
Elvis
"Mnakwenda wapi?
"Tunakwenda kufuatilia taarifa
muhimu kuhusiana na zile nyaraka
tulizozipata jana ofisini kwa
Frank.Usihofu utakuwa
salama.Hakuna anayefahamu mahala
hapa ila uwe makini.Mtu yeyote
akigonga geti usimfungulie kwanza
hakikisha umechungulia na
kumfahamu ni nani.Hatutakawia sana"
akasema Elvis
"Sawa Elvis .Halafu humu ndani
hakuna chochote cha kuandaa"Nadhani Vicky amekwenda
kushughulikia hilo lakini
tutakapokuwa tunarejea tutapita
supermarket na kununua mahitaji
yote yanayohitajika" akasema Elvis
kisha wakaingia garini na kuondoka
"She's very beautifull"akasema
Steve kwa utani
"Steve mambo hayo huu si
wakati wake.Tuna mambo makubwa
ya kujadili .,Kwa sasa tujiulize Vicky
amekwenda wapi?Mbona
hajatujulisha kama anatoka?akauliza
Elvis
"Hata mimi nimeshangaa ila
yawezekana ameona asitusumbue
kutokana na uchovu wa jana"akasema
Steve aliyekuwa katika usukani
"Lakini utaratibu wetu hauko
hivyo.Tuko katika kipindi cha hatari
kubwa na alipaswa atujulishe kuwa
anatoka na anakwenda wapi.Nitamkanya asirudie tena
kitendo hiki cha kuondoka bila kuaga
wenzake" akasema Elvis
"Vicky na mdogo wake
wanafanana tabia.Wote ni wabishi
sana"
"Ubishi wao hauna manufaa
yoyote kwetu zaidi ya kutuweka
katika matatizo.Tazama alichokifanya
Winnie.Ameondoka kwa kiburi lakini
ametua katika mikono ya akina
Frank"akasema Elvis na safari
ikaendelea kuelekea hotelini kwa
Omola.Walisimama katika duka la
kuuza simu Steve akashuka na
kwenda kununua simu tatu pamoja na
laini zake akarejea garini wakaendelea
na safari.
Walifika Maasai Hoteli alikofikia
Omola Steve akashuka na kumfuata
Omola chumbani kwake.Samira tayari alikwisha fika na alikuwa chumbani na
Omola
"Oh Samira kumbe tayari
umefika"akasema Steve
"Nimewahi sana kama
ulivyonielekeza."
"Ahsante sana." akasema Steve
na kumgeukia Omola
"Omola huyu atakayekuwa
dereva wako wa leo na siku zote
anaitwa Samira ni mpenzi wangu
hivyo jisikie amani uko katika mikono
salama"akasema Steve na Omola
akatabasamu
"Nafurahi kukutanana naye
Samira ni mrembo sana.Una bahati
sana kumpata mrembo kama huyu"
akasema Omola halafu akachukua
kompyuta yake na kumkabidhi Steve
na kumuelekeza namna programu ile
inavyofanya kaziHii programu ni mpya kabisa na
CIA ndiyo shirika la kwanza la ujasusi
duniani kuanza kuitumia programu hii
.Japo zipo programu nyingine kama hii
ambazo zinaendelea kutumika lakini
hii ni mwisho wa yote.Ni programu ya
kisasa mno" akasema Omola na
kuendelea kumuelekeza Steve mambo
kadhaa kuhusiana na programu ile
"Ahsante Omola tutaonana
jioni.Tutakuja kukuchukua hapa
hapa.Nadhani kila kitu kuhusiana na
Ikulu Vicky amekwisha
kuelekeza"akasema Steve
"Ndiyo Steve kila kitu nimekwisa
elekezwa na hakuna tatizo
lolote.Mambo yote yatakwenda sawa"
"Nakutakia kila la heri" akasema
Steve na kuanza kupiga hatua
kuondoka halafu akakumbuka kitu
"Nimesahau.Hii hapa ni simu
yako ambayo utakuwa unaitumia ukiwa hapa Tanzania.Ndani ya simu
hii kuna muda wa maongezi wa
kutohja na kuna namba zetu Elvis,ya
kwangu na Vicky.Muda wowote
ukitaka kuwasiliana nasi usisite
kufanya hivyo" akasema Steve na
kumkabidhi Omola simu kisha
akaondoka.Alirejea garini
alikomuacha Elvis
"Sasa mambo yamekaa
vizuri.Kompyuta ya Omola hii hapa"
akasema Steve na kumkabidhi Elvis
kompyuta ile na kumuelekeza
kuhusiana na programu ile
inayotumika kumfuatilia Winnie.
"Kwa mujibu wa programu hii
kwa sasa wako katika mtaa wa
viwandani na anaonekana anaendelea
na safari.Kwa mwendo anaokwenda
nao inaonyesha yuko katika
gari.Anakwenda wapi huku?Anyway
tuendelee kumfuatilia tutajua mwisho wake.Twende tukamtafute kwanza
Irene" akasema Elvis na Steve
akaondoa gari huku Elvis akiendelea
kumfuatilia Winnie
"Wamesimama.Nayafahamu
maeneo haya ni maeneo ya viwanda
na si maeneo ya makazi"akasema Elvis
Steve alifuata maelekezo
yaliyokuwepo katika nyaraka zile za
kutolea mzigo bandarini kuhusu
mahala ilipo kampuni ya Pendeza
Co.Ltd na kufika bila taabu.
"We're here" akasema Steve
akimwambia Elvis ambaye bado
alikuwa ameelekeza akili yake yote
katika kompyuta akimfuatilia Winnie
"Good.Ni duka kubwa na zuri"
akasema Elvis akilikodolea macho
duka lililokuwa mbele yao likiwa na
maandishi makubwa Pendeza Co.Ltd
wakaenda katika maegesho Elvis mimi ninashuka na kuingia
ndani wewe baki hapa hapa ndani ya
gari.Nitamaliza kila kitu
mwenyewe.Kama ukiona hatari
yoyote huku nje nitaarifu haraka sana"
akasema Steve na kushuka akaangaza
angaza kama ilivyo kawaida ya
majasusi kuhakiki usalama halafu
akaanza kupiga hatua kuelekea
ndani.Tayari duka limekwisha
funguliwa na hakukuwa na wateja
wengi asubuhi hii.Mle ndani
akawakuta akina dada watatu
wamesimama wakipeana
michapo,akawasogelea
"Habari zenu akina dada"
akawasalimu kwa uchangamfu
mkubwa
"habari nzuri kaka,habari yako"
"Nzuri kabisa.Nawaona na nyie
mko vizuri.Sura zenu zinanionyesha
hivyo" akasema na wale akina dada wakatabasamu na kufurahia
uchangamfu wake
"Karibu kaka .Tukusaidie
nini?akauliza dada mmoja baada ya
kumuona Steve kama si mnunuzi
"Nina shida na madam Irene.
Nimemkuta au nimewahi
sana?akauliza huku akiwatolea
tabasamu
"Bosi aje saa hizi?Umewahi
sana."
"Saa ngapi anaweza kuja?
"Kuanzia saa nne ndio muda
wake.Ila yupo msaidizi wake unaweza
kumuona huyo naye akakusaidia shida
yako" akasema mmoja wa wale akina
dada
"Hapana nina shida na madam
Irene pekee.Nitakuja tena baadae
kwani maagizo niliyopewa ni kwamba
nionane naye mwenyewe" akasema
Steve na kuwaaga wale akina dada akaanza kupiga hatua
kuondoka.Alipokaribia kufika
mlangoni akageuka na kurudi
"Naombeni mnielekeze kwake ili
nimfuate huko huko" akasema Steve
na kuelekezwa nyumbani kwa
Irene.Akaondoka na kurejea garini
"Irene bado hajafika hapa ila
nimeelekezwa nyumbani
kwake.Twende tumfuate kwani
wanasema huwa anachelewa sana
kufika hapa" akasema Steve huku
akiwasha gari wakaondoka maeneo
yale
"Kuna maendeleo yoyote kwa
Winnie? akauliza
"Inaonekana amesimama.Hili ni
eneo la viwanda na sijui anatafuta nini
huku.Tumalizane kwanza na Irene
halafu tutaenda kumtafuta Winnie"
akasema Elvis Walifika katika nyumba Steve
aliyoelekezwa kuwa ni nyumbani kwa
Irene Mwabukusi.Ilikuwa ni nyumba
kubwa ya ghorofa moja.
"Ni hapa tumefika.Jumba
lenyewe linaonyesha ni mtu
anayejiweza sana" akasema Steve na
kuendesha gari taratibu hadi karibu
na geti akashuka na kwenda
kubonyeza kengele ya geti.Baada ya
dakika moja dirisha dogo lililokuwa
pembeni ya geti likafunguliwa na
msichana mmoja akajitokeza.
"Karibu.Nikusaidie nini?
"ahsante sana.Nahitaji kuonana
na madam Irene"
"Una miadi naye?
"Hapana sina miadi naye ila nina
shida naye ya dharura nimemfuata
ofisini kwake nikaelekezwa kumfuata
hapa nyumbani"
"Nimwambie unaitwa nani? Walifika katika nyumba Steve
aliyoelekezwa kuwa ni nyumbani kwa
Irene Mwabukusi.Ilikuwa ni nyumba
kubwa ya ghorofa moja.
"Ni hapa tumefika.Jumba
lenyewe linaonyesha ni mtu
anayejiweza sana" akasema Steve na
kuendesha gari taratibu hadi karibu
na geti akashuka na kwenda
kubonyeza kengele ya geti.Baada ya
dakika moja dirisha dogo lililokuwa
pembeni ya geti likafunguliwa na
msichana mmoja akajitokeza.
"Karibu.Nikusaidie nini?
"ahsante sana.Nahitaji kuonana
na madam Irene"
"Una miadi naye?
"Hapana sina miadi naye ila nina
shida naye ya dharura nimemfuata
ofisini kwake nikaelekezwa kumfuata
hapa nyumbani"
"Nimwambie unaitwa nani? Mwambie Lukas ninatoka
kampuni ya kusafirisha mizigo ya
Shamsi " akasema Steve na yule
msichana akaondoka na baada ya
dakika tatu akarejea na kufungua geti
na akawakaribisha ndani akina
Steve.Walikaribishwa katika sebule
nzuri sana yenye samani za
kupendeza.
"Karibuni .Mama amesema
mumsubiri hapa atakuja muda si
mrefu" akasema yule msichana na
kuondoka akawaacha akina Elvis peke
yao
"Kuna watu hapa duniani
hawafahamu nini maana ya shida
wanaishi kama vile wako katika sayari
nyingine" akasema Steve kwa sauti
ndogo wakiwa pale sebuleni
wakimsubiri Irene lakini Elvis
hakumjibu kitu macho yake yalikuwa
katika kompyuta akiendelea kumfuatilia Winnie.Baada ya dakika
tano mama mmoja mnene mwenye
umri wa kati ya miaka arobaini hadi
arobaini na tano akatokea.Kwa mavazi
aliyokuwa amevaa ilionyesha wazi
kuwa alikuwa amekwisha jiandaa
tayari kwa kutoka kwenda katika
shughuli zake.
"Karibuni" akasema yule mama
.Steve na Elvis wakasimama
kumsalimu
"Madam Irene
shikamoo."akasema Steve huku
akimfuata na kumpa mkono kana
kwamba wanafahamiana hali
iliyomfanya Irene naye atabasamu na
kufurahia uchangamfu ule wa Steve
"Habari nzuri sana .Karibuni"
akasema huku akipeana mkono pia na
Elvis halafu wote wakaketi
"Samahani kwa kukusumbua
madam Irene tumefika dukani wakatuambia kwamba utachelewa
kufika ikabidi tukufuate hapa
nyumbani" akasema Steve
"Karibuni sana ila sina hakika
kama tunafahamiana.Mmeseam
mnatokea kampuni gani?akauliza
Irene
"Hapana hatufahamiani ila
tumekutafuta kwa ajili ya
mazungumzo ya kibiashara.Sisi tuna
kampuni yetu ya usafirishaji ....."
akasema Elvis na kuinuka akachomoa
makaratasi kutoka katika mfuko wa
koti na kumfuata Irene pale alipokuwa
amekaa kwa dhumuni la
kumuonyesha zile karatasi.Mara tu
alipoketi kitini akainua koti lake na
bastora ikaonekana.Irene akastuka
sana na kugeuka haraka na Steve naye
akainua koti lake ikaonekana bastora
na akamfanyia ishara ya kukaa kimya.Macho yakamtoka pima.Kwa
sauti ndogo Elvis akamwambia
"Usipige kelele wala
kutaharuki,inuka na tuongozane hadi
katika gari.Ukithubutu kupiga kelele
au kufanya chochote tunakufumua
kichwa chako.Now let's go!! akaamuru
Elvis huku akisimama na Irene naye
akasimama,Steve akaichukua
kompyuta yao wakaanza kuondoka
mle ndani.Walitembea kana kwamba
hakuna tatizo lolote.Sura ya Steve
ilionyesha tabasamu muda wote na
hakuna yeyote ambaye angehisi kuwa
Irene alikuwa ametekwa.Walifika
katika gari la akina Elvis Steve
akamfungulia mlango wa nyuma
akaingia kisha nao wakaingia garini na
kuondoka.


********************** I have to do anythng I can to get
Winnie back.Hawa jamaa akina Elvis
hawana uchungu kama nilio nao mimi
na ndiyo maana hawaonyeshi juhudi
zozote za kutaka kumtafuta
Winnie.Siwezi kumuacha ndugu yangu
wa damu akiendelea kuteswa bila
kufanya jitihada zozote za kumuokoa.I
must do something" akawaza Vicky
baada ya kuondoka katika nyumba
walikohamia.Alikuwa anatembea kwa
miguu na kwa mbali akaiona piki piki
inakuja,akapunga mkono na piki piki
ile ikasimama akamuelekeza dereva
ampeleke katika kituo cha
taksi.Dereva akaendesha kwa
mwendo wa kasi na kwa muda wa
dakika nane wakafika katika kituo cha
taksi akashuka na kuchukua taksi
iliyompeleka moja kwa moja
nyumbani kwake.Kitu cha kwanza alipofika nyumbani ni kuuliza walinzi
kama Winnie amefika pale akaelezwa
kwamba hajafika akaingia ndani
haraka haraka na kuwasha simu yake
akazitafuta namba za Frank na
kumpigia.
"Vicky!! ikasema sauti ya Frank
kwa mshangao
"Frank where are you?akauliza
Vicky
"Where are you? Frank naye
akauliza
"Niko hapa nyumbani
kwangu.Frank we need to talk"
"We need to talk?Frank akauliza
"Yes we need to talk"akasema
Vicky na Frank akavuta pumzi ndefu
akauliza
"What do you want?
"I want Winnie back!!
Badala ya kujibu Frank akaangua
kicheko kisha akasema You want me to free
Winnie,surrender yourself to me and
I'll let her go" akasema Frank
"Where are you now?
"You want to kill me too?akauliza
Frank
"Frank I only want Winnie,
nothing else"
"If you want Winnie back stay
where you are" akasema Frank na
kukata simu
Vicky alihisi kutetemeka kwa
ndani,alikuwa anaogopa
"Mwili unanitetemeka kwa woga
lakini sina namna nyingine lazima
nifanye hivi ili Winnie awe huru.Ni
bora kama nikiteswa mimi kuliko
Winnie hana kosa lolote.Sijui nini
kitatokea akina Elvis wakigundua
kwamba nimefanya hivi,lakini wao
ndio chanzo cha haya yote.Kama
wasingeniingiza katika mpango wao wa kumuua Pascal haya yote
yasingenikuta.Nadhani ni wakati
muafaka wa kuachana na hizi kazi na
kuendelea na shughuli zangu
nyingine.Kuendelea kuzifanya ni
kuendelea kumuweka hatarini ndugu
yangu Winnie" akawaza Vicky.
Mara tu alipomaliza kuzungumza
na Vicky simuni,Frank akampigia Obi
"Obi nimepigiwa simu muda si
mrefu na Vicky anataka kujisalimisha
ili kumuokoa mdogo wake"
"Unamuamini?akauliza Obi
"Bado sijamuamini yawezekana
huu ukawa ni mtego wanataka
kuutumia hivyo waache vijana wawili
hapo mlipo waendele kumchunga
Winnie halafu wewe na wengine wote
mjipange kwenda kumchukua Vicky
nyumbani kwake.Nataka apotezwe
fahamu ili asifahamu mahala
anakopelekwa.Chukueni kila aina ya tahadhari ili kuhakikisha kwamba
hakuna mtu yeyote anayewafuatilia
kwani kuna uwezekano mkubwa watu
hawa wanaomtumia wakamtanguliza
kama chambo ili waweze kunipata
kirahisi kama walivyofanya kwa
Pascal.Umenielewa Obi?
"Nimekuelewa mzee"
"Vipi kuhusu wale vijana
tuliowaacha katika ile nymba kuna
ripoti yoyote wametuma?
"Nimezungumza nao muda si
mrefu na mpaka sasa hakuna mtu
yeyote aliyefika pale nyumbani"
"Ok sawa wasiondoke waendelee
kubaki hapo hapo ili tujue ni nani
anaishi hapo" akasema Frank na
kukata simu akainuka na kwenda
kuchukua chupa ya mvinyo
akaimimina katika glasi na kuanza
kunywa huku uso ake ukiwa umejaa
hasira Hatimaye umekuja
mwenyewe.Wewe ndiye mwenye
majibu ya maswali yangu yote.Sipati
picha mateso nitakayokupa Vicky"
akawaza huku akiendelea kugugumia
mvinyo kwa fujo


***********************


Imekuwa ni kawaida ya Patricia
kutokupata usingizi usiku na badala
yake huanza kupata usingizi mida ya
alfajiri.Akiwa katika usingizi mzito
asubuhu akasikia simu yake
ikiita,akajiinua kivivu na kuichukua
akatazama mpigaji alikuwa ni
Meshack Jumbo.Haraka haraka
akaipokea
"Shikamoo mzee Jumbo" Marahaba Patricia,habari za
asubuhi?
"Nzuri kabisa mzee wangu"
"Patricia nimekupigia
kukujulisha kuwa leo hii utahama
hapo kwa akina Juliana.Kuna nyumba
nimekutafutia maeneo ya Peninsula ni
nzuri ambayo utaishi hapo kwa muda
wakati tunakutafutia makazi ya
kudumu.Tumeona tukuondoe hapo
kwani panaonekana si mahala salama
kwa wewe kuendelea kuishi hasa kwa
wakati huu ambao tunafanya
uchunguzi wa lile suala la
Juliana.Ninakwenda kukamilisha
taratibu za malipo asubuhi hiyo na
jioni ya leo kila kitu kitakuwa tayari
kwa wewe kuhamia hapo"akasema
Meshack
"Mzee Jumbo nakushukuru sana
kwa kunijali.Hata hivyo nakuomba
usisumbuke mzee wangu kutafuta nyumba kwani kuna sehemu
nitakwenda kuishi yenye usalama
zaidi.Rais na mke wake wameniomba
nikaishi nao ikulu hadi hapo
nitakapokuwa nimeweza kujitegemea
tena.Wale wazee wananipenda sana
na wananichukulia kama sehemu ya
familia yao hivyo usihofu kuhusu mimi
mzee Jumbo nitakuwa salama"
"Hilo ni jambo zuri sana
wamelifanya kwani pale ikulu kuna
ulinzi na usalama wa kutosha
sana.Hata hivyo bado nitaendelea
kufuatilia nyumba hii ili pale
utakapoondoka ikulu uweze kuwa na
sehemu ya kuanzia.Patricia najua
wewe ni mgumu sana kukubali vitu
hasa kutoka kwa watu wenye
mahusiano na Elvis lakini nakuomba
usikatae hili ninalotaka kulifanya kwa
ajili yako.Elvis nilimpenda kama
mwanangu na kwa sasa hayupo tena na jukumu la kukulea ninalibeba
mimi hivyo ninaanza kwa kukutafutia
makazi.Muda wowote ukichoka kuishi
ikulu utakwenda kuishi katika hiyo
nyumba niliyokutafutia"
"Ahsante sana mzee
Jumbo.Ninashukuru kwa hilo" akajibu
Patricia huku akitabasamu
"Ni lini unahamia Ikulu?
"Nimepanga kwenda ikulu baada
ya msiba wa hapa kumalizika.Nataka
nishiriki nao katika mazishi ya baba
yao ndipo niondoke.Ni watu wema
sana kwangu hivyo siwezi kuondoka
kabla msiba haujamalizika"
"Patricia ninakushauri ufanye
haraka sana kwenda ikulu kwani kuna
viashiria vinatuonyesha mahala hapo
si salama kwa wewe kuendelea
kuwepo hivyo itakuwa vyema kama
utahamia ikulu leo hii hii.Hata ukiwa
kule utaendelea kuwatembelea na kuungana nao katika msiba lakini
kitendo cha kuendelea kuishi hapo si
salama"
"Mzee Jumbo ahsante sana kwa
ushauri wako nitaufanyia kazi japo
Juliana atasikitika sana kama
nikiondoka na kumuacha peke yake"
"Hautamuacha peke yake Patricia
bado utakuwa na muda wa kwenda
kuungana nao katika msiba
tunachohitaji sisi ni kukuondoa tu
hapo"
"Nimekuelewa mzee
wangu.Nitafanya kama ulivyoelekeza
nitawasiliana na mama mke wa rais
nitamjulisha kuwa nitahamia kwao
leo"
"Good.Thank you very
much.Usimweleze mtu yeyote hata
Juliana kuwa unaondoka kwao kwa
sababu za kiusalama.Waeleze kwamba
rais amesisistiza uende ukaishi nao na wewe huwezi kumkatalia" akasema
Meshack Jumbo akaagana na Patricia
"Analolisema Meshack ni jambo
la kweli.Familia hii ya akina Juliana
inaonekana inawindwa sana na mimi
kuendelea kuishi hapa kunaweza
kuniweka matatani.Ngoja niondoke
zangu nikaishi ikulu sitaki tena
matatizo zai......."Patricia akatolewa
mawazoni na simu ya Dr Washington
"Habari za asubuhi Dr
Washington"
"Habari yangu nzuri,hofu yangu
kwako.Umeamka salama?
"Nimeamka salama kabisa."
"Ni hicho pekee ninachohitaji
kukisikia kutoka katika mdomo wako
kwamba unaendelea vyema" akasema
Dr Washington na halafu ukimya
ukapita
"Patricia utanisamehe kwa hili
lakini nina hamu sana ya kukuona.Nafahamu bado una
machungu mazito ya kifo cha mumeo
lakini naomba kama utaniruhusu
nikutembelee nije nikujulie
hali.Nataka nikufariji ana kwa
ana.Toka yalipotokea matatizo haya
hatujaonana na hii inanipa wakati
mgumu sana hata katika kutenda kazi
zangu.Kila wakati picha yako inakuja
kichwani kwangu.Nahitaji nikuone
Patricia,tafadhali nielekeze mahala
ulipo ili nikutembelee" akasema Dr
Washington.Patricia akavuta pumzi
ndefu na kusema
"Dr Washington hata mimi
nimekukumbuka sana na ningependa
kuonana nawe ila mazingira niliyomo
kwa sasa hayaruhusu mimi na wewe
kuonana.Tuendelee kuwasiliana
simuni na siku moja tutaonana tena"
akasema Patricia Nimekuelewa Patricia ila bado
nina swali moja.Utarudi tena
kazini?akauliza Dr Washington na
Patricia akachukua muda kidogo
kujibu
"Bado sijajua nini nitakifanya
kama nitarejea tena kazini au
vipi.Nitakujulisha maamuzi
nitakayochukukua kwani maisha
yangu tayari yamebadilika sana na
hayatakuwa kama yale niliyoishi
wakati niko na mume wangu.Dr
Washington ahsante kwa kunijulia
hali tutawasiliana siku nyingine"
akasema Patricia na kukata simu
tayari machozi yalikuwa yanamtoka
"Machozi haya ya kumlilia Elvis
hayatakauka kamwe.Elvis alikuwa ni
sehemu kubwa ya maisha yangu.Kuna
nyakati ninaomba utokee muujiza na
nimuone tena mume wangu mbele
yangu lakini haiwezekani.Elvis is gone.Kuna nyakati hata mimi
ninatamani kama ningekufa ili
nikaungane na mume wangu huko
aliko kwani naamini maisha yangu
yatakuwa magumu sana bila yeye"
akawaza Patricia na kujilaza tena
kitandani


*********************


Dr Makwa Tusangira na waziri
mkuu mstaafu David walikuwa mezani
wakipata kifungua kinywa kwani Dr
Makwa alilala hapa nyumbani kwa
David kwa hofu ya kukamatwa na
polisi baada ya kutangaza kufanyika
kwa mkutano wa hadhara uliopigwa
marufuku na jeshi la polisi.Wakiwa
mezani wakiendelea kupata kifungua
kinywa pamoja na maongezi mbalimbali simu ya Dr Makwa ikaita
akaipokea haraka
haraka.Akazungumza kwa dakika
zaidi ya kumi na mtu aliyempigia
halafu wakaagana huku uso wake
ukiwa na tabasamu kubwa
" Nilikuwa nazungmuza na
familia yangu tayari wamevuka mpaka
wa Namanga na wameingia Kenya.Ni
hao tu waliokuwa wananipa wasi
wasi.Ahsante sana David kwa msaada
wako mkubwa wa kuiondoa familia
yangu.Sitaki ipate misuko suko ya aina
yoyote" akasema Dr Makwa
"Dr Makwa siku zote familia
huwekwa mbele.Ningekushangaa sana
kama ungeacha familia yako hapa
Tanzania wakati unafahamu fika kuwa
machafuko makubwa yanakwenda
kutokea.Leo inazinduliwa rasmi safari
ya kuelekea ikulu.Hakikisha tafadhali kila kitu kinakwenda vizuri hatuhitaji
uzembe wa aina yoyote ile"
"Usihofu David kila kitu
kinakwenda vyema na hakuna uzembe
wowote utakaotokea.Tumejipanga
vizuri.Frank alifanya vyema sana
kuhakikisha tunapokea pesa jana na
zimetusaidia mno katika maandalizi
na matunda yake utayaona" akasema
Dr Makwa kisha wakaendelea na
mikakati mingine huku simu ya Dr
Makwa ikiita kila wakati akiwasiliana
na watu mbalimbali kuhusiana na
maendeleo ya mipango yao


****************

Steve aliendesha gari hadi karibu
na daraja ambalo ujenzi wake ulikuwa
umesimama akaegesha pembeni. "I'm going out.Endelea naye"
akasema Steve na kushuka akafungua
mfuniko wa injini na kujifanya
anatengeneza
"Irene naomba nisikilize kwa
makini sana.Hatuna tatizo nawe ila
kuna mambo tunataka kuyafahamu
kutoka kwako hivyo nakuomba uwe
mkweli kwa kila nitakachokuuliza."
akasema Elvis
"Ninyi ni akina nani?Mnataka
nini?Niambieni ni kiasi gani cha pesa
mnahitaji niwalipe but please don't
hurt me" akasema Irene huku macho
yake yakilengwa na machozi
"Hatuhitaji pesa Irene ila
tunachohitaji ni taarifa.Wewe ndiye
mmiliki wa kampuni ya Pendeza
Co.Ltd?
"Ndiyo.Hiyo ni kampuni yangu"
akajibu Irene Unaimiliki wewe mwenyewe
kwa asilimia mia moja au kuna mtu
mwingine unashirikiana naye?
"Hii ni kampuni yangu kwa
asilimia mia moja.Hakuna mtu
mwingine ninayeshirikiana naye"
"Are you sure?
"Yes I'm sure"
"Irene ninarudia tena kuuliza
kwamba kuna mtu yeyote
unayeshirikiana naye katika kumiliki
kampuni hii?
"Hakuna mtu mwingine,mmiliki
ni mimi peke yangu"
"Unaifahamu kampuni inaitwa
McLorien?
"Ndiyo ninaifahamu.Hao ni
washirika wangu wa biashara
.Wanatuuzia mzigo wa nguo na vatu
kutoka Marekani na Ulaya"
"Mara ya mwisho ilikuwa lini
kupokea mzigo kutoka kwao? Ni miezi kadhaa imepita"
"Mingapi?
"Miezi kama mitano au sita hivi"
"Hakuna mzigo wowote
umepokea kutoka katika kampuni hii
wiki tatu zilizopita?
"Hapana hakuna mzigo wowote
tumepokea"
"Are you sure?
"Yes I'm sure" akajibu Irene kwa
kujiamini
"Good.Unamfahamu
Frank?akauliza Elvis na swali lile
likamstua Irene akababaika
"Frank?..akauliza
"Frank yupi?akauliza tena
"Brigedia Frank"
Irene akawaza halafu akasema
"Hapana simfahamu mtu huyo"
"Are you sure?Elvis akauliza Yes I'm sure"akajibu Irene.Elvis
akamtazama kwa sekunde kadhaa na
kusema
"Irene wewe ni dada yangu na
nilikuonya toka awali kwamba
unieleze ukweli mtupu kwa yale
nitakayokuuliza lakini wewe
unanidanganya.Umeniudhi kwa
kuniambia uongo na mimi huchuia
sana mtu anaponieleza uongo"
"Sijakudanganya kaka yangu
simfahamu mtu huyo anaitwa brigedia
Frank"akasema Irene.Elvis akashusha
kioo cha gari na kumuita Steve
akamtaka aingie garini waondoke
"Mnanipeleka wapi?
"Nilikupa nafasi ukaichezea sasa
ni wakati wetu wa kuutafuta ukweli
kwa kutumia nguvu.Hatukutaka
kutumia njia hii lakini
umetulazimisha" Mtaniumiza bure kaka zangu
mimi simfahamu huyo Frank
nawaomba mniamini
tafadhali"akasema Irene.Steve
akawasha gari wakaondoka.Mara tu
walipoingia barabarani Elvis akatoa
karatasi mfukoni akazikunjua na
kumuonyesha Irene
"Hizi ni nyaraka za kutolea mzigo
bandarini ambazo zinaonyesha kuwa
wiki tatu zilizopita umepokea mzigo
wa viatu kutoka kwa kampuni ya
McLorien"
Irene macho yakamtoka mdomo
ikamtetemeka hakujua aseme
nini.Nyaraka zile zilieleza kila kitu
"Umekataa kwamba hujapokea
mzigo wowote kutoka kwa kampuni
ya Mclorien kwa miezi mitano au sita
lakini nyaraka zinaonyesha umepokea
mzigo wiki tatu zilizopita.kwa nini umetudanganya? akauliza Elvis na
Irene akamtazama kwa woga akasema
"Samahani kaka..Samahani
sana.Naombeni tuzungumze"
"Mazungumzo ni kutueleza
ukweli tu.Unamfahamu Frank?
"Hapana simjui Fr....."kabla
hajamalizia sentensi yake Steve
aliyekuwa katika usukani akageuka
kwa kasi ya ajabu na kumnasa kibao
kikali usoni
"Don't lie to us !! akasema na
kuendelea kuendesha
"Jamani naombeni msiniumize
simfahamu Frank"akasema Irene
"Nyaraka hizi tumezitoa katika
ofisi yake.Kwa nini
usimfahamu?Tueleze haraka
mahusiano ya Frank na kampuni
yako"akasema Elvis Nimekwisha waeleza kaka
zangu kwamba simfahamu kabisa
huyo Frank!! akasema Irene
"Unazidi kunipa hasira
Irene.Ninakupa nafasi ya mwisho
utueleze unamfahamu Frank? akauliza
Elvis
"Jamani naombeni mniamini
kwamba simfahamu Frank" akasema
Irene.
"Steve naomba vifaa vyangu"
akasema Elvis na Steve akafungua
droo ya gari na kumrushia kiboksi
kidogo akakifungua akatoa koleo
ndogo na kuukamata kwa nguvu
mkono wa Irena akakibana kidole kwa
koleo na Irene akapiga kelele kwa
maumivu makali aliyoyapata
"Tell me the truth! akasema Elvis
lakini Irene aliendelea kulia.Elvis
akamnasa kibao kikali halafu
akaukamata tena mkono wake na kukibana kidole kingine kwa koleo
lakini bado Irene aliendelea kushikilia
msimamo wake wa kutokumfahamu
Frank.Elvis akazidi kukasirika
akamshika kwa nguvu na kumlaza
katika kiti halafu akachukua kisu
kidogo
"Ninakwenda kuliondoa jicho la
kwanza na kama utaendelea kuwa
mbishi nitaliondoa jicho la
pili.Akasema na kumkandamiza Irene
kichwa na kukipeleka kisu sehemu ya
chini ya jicho na Irene akaanza kuhisi
kitu chenye nya kali kikiichana ngozi
yake
"Basi !! basi !! nitawaeleza
ukweli!! Usinimize tafadhali
nitakueleza kila kitu!! akasema Irene
na Elvis akamuachia.Tayari damu
ilikwisha anza kutoka sehemu ya
chini ya jicho la kulia.Irene akavuta pumzi haraka haraka hakuamini
kilichotaka kumtokea.
"Nataka majibu haraka sana"
akasema Elvis.Wakati haya yakitokea
gari lilikuwa katika mwendo mkali na
hakuna yeyote aliyeweza kuona
kilichokuwa kinaendelea ndani kwani
vioo vyote vilikuwa na rangi nyeusi
halafu Steve alifungua mziki kwa sauti
kubwa.
"Irene naomba usinipotezee
muda wangu.Nipe majibu haraka
sana"akasema Elvis
"Nitakueleza kaka angu ila
naomba msiniumize.Nitawaeleza kila
kitu"akasema Irene na kumtazama
Elvis kwa woga halafu akaendelea
"Frank ndiye mmiliki wa
kampuni hii ya Pendeza Co.Ltd"
akasema na kunyamaza kidogo
akafuta damu na kuendelea Hakutaka kujulikana kama
anamiliki hii kampuni hivyo
akanitumia mimi ili niwe kama
mmiliki wake lakini ukweli yeye ndiye
mwenye kampuni.Frank hajihusishi
na lolote katika kampuni hii zaidi ya
kuagiza mzigo na kutukabidhi."
"Frank ndiye huagiza mzigo?
"Ndiyo.Mimi humpelekea orodha
ya bidhaa tunazozihitaji na yeye
huagiza kutoka nje na baadae huja
kutukabidhi kwa ajili ya kuuza"
"Wiki tatu zilizopita kontena
zaidi ya kumi za viatu zimetolewa
bandarini.Mmeupokea mzigo
huo?akauliza Elvis na Irene
akababaika
"Irene answer me!! akafoka Elvis
"Tulipokea jozi chache za viatu
kwani bado havijapakuliwa katika
makontena.Upakuzi utakapokamilika basi tutaupata mzigo wote" akasema
Irene
"Mnasubiri upakuzi?Mnapakulia
wapi mzigo wenu mkiutoa bandarini?
"Mzigo unapokuja ni Frank
ambaye hushughulikia kila kitu na
kisha huenda kuupakua na ndipo
hutuletea kwa ajili ya kuuza.Mahala
anapopakulia hata mimi sipafahamu
na sijawahi kumuuliza kwani shida
yangu mimi ni kupata mzigo
pekee.Wakati mwingine mzigo huwa
unakuja kwa ajili ya maduka yetu
yaliyoko nchini jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo na Burundi."
"Mna maduka mengine Congo na
Burundi?
"Ndiyo tuna maduka mengine
mawili makubwa nchini Congo na
Burundi" akasema Irene. Namna gani huwa mnayatoa
makontena yenu bandarini? akauliza
Elvis na Irene akabaki kimya
"Irene usitake kuniudhi
tena.Nitakuondoa jicho lako sasa
hivi"akasema Elvis kwa ukali na Irene
huku akionyesha woga mkubwa
akasema
"Frank ndiye anayesimamia
utoaji wa makontena bandarini lakini
ninavyofahamu kuna watu huwa
wanatusaidia katika utoajia
makontena hayo"
"Mnapotoa makontena hayo
hupita katika mtambo maalum wa
kuchunguza na kuoa kilichomo ndani?
akauliza Steve
"Hapana hayapiti huko"
"Kwa nini?akauliza Elvis na Irene
akabaki kimya
"Kwa nini?akauliza tena lakini
Irene akabaki kimya Irene nataka majibu.Kwa nini
makontena yenu hayapiti katika
ukaguzi?akauliza Elvis lakini Irene
hakufumbua mdomo wake.Kufumba
na kufumbua akajikuta amenaswa kofi
kali sana lililomuangusha kitini na
damu ikaanza kutoka mdomoni.Elvis
akamkandamiza tena kichwa na
kukipeleka kisu jichoni
"Wait !!! wait !!.akasema Irene
"Irene tafadhali naomba usicheze
nami kabisa.!! Answer my questions !!
akasema Elvis
"Mizigo yetu haipiti katika
ukaguzi kwa sababu Frank hudai kuna
mizigo yake huwa anaipakia ndani ya
mzigo huo wa nguo au viatu ambayo
hataki ijulikane na ndiyo maana
mizigo haipiti katika ukaguzi"
"Ni mzigo gani huwa anaupakia
ndani ya makontena hayo ya viatu? Hajawahi kunieleza.Hiyo ni siri
yake mwenyewe na ndiyo maana
hushughulikia mizigo yote yeye
mwenyewe"
"Nani mshirika wake mkubwa
katika biashara zake ukiacha wewe?
"Frank ana marafiki wengi
wakubwa anaoshirikiana nao katika
mambo mbali mbali lakini katika
biashara hii ni mimi pekee
ninayeshirikiana naye"
"Nani unayemfahamu ambaye
anashirikiana naye kwa karibu zaidi?
"Ni Pascal ambaye ameuawa juzi"
"hakuna mwingine?
"Frank anafahamiana na watu
wengi hivyo sijui yupi anashirikiana
naye katika jambo gani ila huyo Pascal
ndiye muda mwingi walikuwa
wote.Huyo ndiye rafiki yake kubwa
ninayemfahamu"akasema Irene.Elvis akamtazama kwa muda halafu
akasema
"Tutakuacha uende zako ila
usimweleze Frank chochote juu yetu
sisi.Ukifanya hivyo you'll
die.Umenielewa Irene? akauliza Elvis
"Nimewaelewa na nitafanya
kama mlivyonielekeza,sintamwambia
Frank" akasema Irene na Elvis
akamuelekeza Steve aegeshe gari
karibu na hoteli 66.Palikuwa na taksi
nyingi pale Steve akashuka
"Get out of the car.Chukua taksi
na uende nyumbani!! akasema
Elvis.Irene akashuka kwa woga Steve
tayari alikwisha mtafutia gari
akamfungulia mlango na kumtaka
dereva ampeleke Irene mahala
atakapomuelekeza na dereva wa taksi
akamuuliza Irene mahala anakotaka
apelekwe akamuelekeza
wakaondoka.Steve alipohakikisha taksi ile imepotea kabisa akaingia
garini kisha nao wakaondoka
"Kwa nini umemuacha
aende?Steve akauliza
"Hana msaada tena kwetu.Tayari
amekwisha tueleza kile
tunachokitafuta hivyo hakuna haja ya
kuendelea kumshikilia.Kwa maelezo
yake ni wazi ndani ya makontena hayo
ndimo hupakiwa silaha ndiyo maana
hayapiti katika ukaguzi.Hapa
inaonyesha kuna mtandao uko
bandarini na ndiyo maana imekuwa
rahisi kwao kutoa mizigo yao bila
wasiwasi wala kukaguliwa.Hizi ni
taarifa nzuri sana
tumezipata.Makontena hayo huja
kama mzigo wa nguo na viatu kisha
hutolewa bandarini na halafu
husafirishwa kwenda Congo na
Burundi kama viatu na huko ndiko
huuziwa waasi.Haya ni mafanikio makubwa sana tumeyapata lakini
bado tunahitaji kuchimba zaidi na
kufahamu Frank anashirikiana na
akina nani katika biashara hii?Lengo
ni kuhakikisha mtandao wote
tunaung'oa.Hakuna
atakayesalia"akasema Elvis
"Nakubaliana nawe Elvis
kwamba sasa tumepata picha ya
kueleweka kuhusiana na biashara ya
silaha anayoifanya Frank.Nguvu
kubwa sasa tuielekeze katika
kumchunguza Frank ili tuufahamu
watu anaoshirikiana nao"
"Tunapaswa kufanya uchunguzi
pia bandarini kujiridhisha namna
makontena hayo yanavyotolewa na
tufahamu ni akina nani wanahusika
katika jambo hilo.Vile vile tusubiri
taarifa kutoka kwa Omola ili tufahamu
kuhusiana na kampuni ya
McLorien.Irene nimemuachia huru makusudi kabisa kwani naamini
atamueleza Frank na akipata taarifa
hizi atastuka sana na ataanza kutafuta
namna ya kujihami na sisi tutampata
kirahisi.Kwa sasa tuendelee
kukusanya vielelezo kuhusiana na hii
biashara.Bado hatuna ushahidi wa
kutosha kwamba ndani ya makontena
hayo kuna silaha" akasema Elvis
"Nimekupata vyema Elvis.Vipi
kuhusu Winnie?akauliza Steve
"Oh tumemsahau kabisa Winnie"
akasema Elvis na kuichukua kompyuta
"Bado inaonyesha yuko pale
pale.Tuelekee eneo la mtaa wa
viwanda.Huko ndiko aliko"
"Anafanya nini huko? akauliza
Steve
"Yawezekana amefichwa huko
kwani wale jamaa hawataweza
kumuachia hadi wahakikishe
wamempata dada yake"akasema Elvis na gari likasimama katika taa kabla ya
kuingia katika barabara ya Chaguso.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
I DIED TO SAVE PRESIDANT

Sehemu 66

Vicky alitoka chumbani kwake
baada mlango wa sebuleni kugongwa
akaenda kuufungua akakutana na
mlinzi
"Kuna watu wanakuuliza
mama"akasema yule mlinzi
"Waruhusu waingie
ndani"akasema Vicky na mlinzi yule
akaenda kuwafungulia geti wakaingia
ndani.Kutoka ndani ya gari wakashuka
watu wanne wakiongozwa na
Obi.Vicky akahisi woga
"Hallo Vicky.Tumekutana
tena.Uko tayari?akauliza Obi
"Mnanipeleka wapi?
"Unakotakiwa kwenda.Kama uko
tayari ingia garini tuondoke" akasema Obi na Vicky akaongozana nao hadi
katika gari lao akaingia na
kuondoka.Mara tu walipovuka geti Obi
ambaye alikuwa amekaa kiti cha
nyuma pamoja na Vicky akamuomba
kijana aliyekuwa amekaa mbele
ampatie vifaa vyake
"Mnataka kunifanya nini?
akauliza Vicky kwa wasi wasi
"Relax Vicky.This is just a
procedure.Hutakiwi kufahamu mahala
unakoelekea hivyo naomba usiwe
mbishi" akasema Obi na kutoa sindano
katika mkoba ule akavuta dawa fulani
katika kichupa na kumchoma Vicky
katika .Hazikuisha sekunde thelathini
Vicky akalala usingizi mzit😵bi
akatoa simu na kumpigia Frank
"Mkuu tayari tunaye Vicky"
"Good.Fanyeni kama
nilivyowaelekeza hakikisheni
mnachukua kila aina ya tahadhari kwani watu wanaomtumia wana
mbinu nyingi"akasema Frank
"Tuko makini sana.Tutakujulisha
tukifika" akasema Obi na kukata
simu.Walikuwa makini sana katika
kuangalia kama kuna mtu yeyote
aliyekuwa anawafuata
nyuma.Walikwenda hadi katika
nyumba moja maeneo ya Mijiwe na
kuingia ndani.Haraka haraka Vicky
akashushwa na kupakiwa katika gari
lingine ambalo lilipita katika geti la
nyuma na kupita katika njia
iliyokuwemo shambani halafu
wakatokea katika barabara kubwa
wakaendelea na safari
"Kama walikuwa wanatufuatilia
kwa namna yoyote ile hapa
tumewalamba chenga ya mwili"
akasema Obi huku akicheka.
Waliendelea na safari hadi katika
nyumba ambayo Winnie aliletwa usiku wa jana wakaingia na Vicky
akapelekwa katika chumba akafungwa
pingu miguu na mikono kisha
akamchoma sindano nyingine na
wakaamuacha azinduke.Obi
akamjulisha Frank kuwa tayari
wamekwishamfikisha Vicky sehemu
husika
"Good Job Obi.Sasa jipeni muda
wa kuchunguza kama hakuna yeyote
anayemfuatilia mimi niko njiani
ninakuja hapo"akasema Frank


******************


Jina mtaa wa viwanda lilitokana
na eneo hilo kutengwa maalum kwa
ajili ya viwanda.Kulikuwa na viwanda
vikubwa zaidi ya kumi vinavyofanya
kazi na vingine vikiwa katika hatua mbali mbali za ujenzi.Kulikuwa na
majengo makubwa makubwa na
mengine yalizungushiwa ukuta
mkubwa.Steve aliendesha gari
taratibu huku Elvis akitumia
programu ile katika kompyuta
kutafuta mahala alipo Winnie.
"Ni maeneo haya hapa" akasema
Elvis baada ya kufika katika eneo la
kilichokuwa kiwanda cha saruji
ambacho kwa sasa hakifanyi
kazi.Mwekezaji wa kiwanda hiki
alishindwa kukiendeleza
akakitelekeza na kung'oa mashine
zote muhimu na kubaki magofu.Elvis
na Steve wakashuka garini na
kuangaza angaza.Watu waliokuwa
njiani hawakuwa wengi kutokana na
muda huo wengi kuwa makazini.
"Programu inatuonyesha ni eneo
hili la kushoto ambako kuna hiki
kiwanda cha saruji" akasema Elvis Ukuta uliozunguka kiwanda hiki
ulibomoka bomoka na hivyo
kupafanya kuwa ni sehemu ambayo
vijana hupenda kujificha na kuvuta
bangi.Doria za mara kwa mara za
polisi ndizo ziliowakimbiza vijana hao
eneo hili na kuondoa kitisho
kilichokabili raia hasa wafanyakazi
waliokuwa wanafanya kazi katika
viwanda vilivyoko eneo hili
waliokuwa wakiporwa fedha na mali
zao kila uchao.
Steve na Elvis wakaambaa na
ukuta wakakuta sehemu iliyoanguka
wakaingia ndani.Walitembea kwa
tahadari kubwa wakipita majengo
kadhaa yaliyotelekezwa bila kukutana
na mtu yeyote na mara wakatokea
katika jengo kubwa la ghorofa moja
ambalo lilionekana kama awali
lilitumika kama ofisi ingawa kwa sasa
hakukuwa na madirisha wala milango.Lilibaki gofu.Steve aliyekuwa
ametangulia mbele akasimama na
kumsukuma Elvis arejee nyuma
"Kuna nini? akauliza Elvis
"Kuna mtu amejificha pembeni
ya lile jengo anavuta sigara" akasema
Steve
"Good.Zunguka kwa nyuma mimi
nitamuwahi kwa mbele" akasema
Elvis na Steve akanyata akapita
pembeni ya mtambo mmoja mkubwa
uliotelekezwa pembeni ya jengo lile
bila kuonekana akazunguka nyuma ya
lile jengo akaruka dirisha na kuingia
ndani akaanza kupanda ngazi
kuelekea juu alikokuwa yule jamaa
akivuta sigara.Elvis akamuona Steve
akipanda ngazi taratbu naye akaiweka
sawa bastora yake iliyofungwa
kiwambo cha kuzuia sauti.Yule jamaa
alikuwa ameegemea ukuta akivuta
sigara akionekana kujisahau kabisa.Mara akastuliwa na sauti ya
kitu kama jiwe lililoanguka nyuma
yake.Akaitupa sigara na haraka
akageuka nyuma kutazama kuna nini
lakini hakuona chochote
"Peter ! akaita lakini
hakujibiwa.Haraka haraka akatumia
ngazi zilizokuwa nje akaanza kushuka
haraka haraka lakini kabla hajafika
cini akatokea Elvis na kumtaka
asimame alipo.Yule jamaa kwa woga
akageuka na kutaka kurudi juu lakini
akakutana na Steve akiwa na
bastora.Kwa ujasiri na wepesi wa aina
yake akaitoa bastora kwa lengo la
kupambana na akina Steve lakini Elvis
tayari alikwisha kiona kitendo kile na
hakumpa nafasi kwani kwa shabaha
ya aina yake akaupiga risasi mbili
mkono ule uliokuwa umeshika
bastora akaanguka chini.Steve
akamuwahi na kumvuta juu akamuingiza ndani.Elvis akaangaza
kila upande na hakuona mtu
yeyote.Akapanda ngazi haraka haraka
akamfuata Steve kule juu
"Tuambie wewe ni nani na
unafanya nini hapa? akauliza Steve
"Jamani naombeni msiniue.."
"Hatutakuua kama utatueleza
wewe ni nani na unafanya nini hapa?
akauliza Elvis lakini yule jamaa
hakujibu kitu alikuwa anagugumia
kwa maumivu huku damu nyingi
ikiendelea kutoka katika jeraha.
Elvis akamkanyaga katika jeraha
la yule jamaa ambaye alipiga ukelele
mkubwa wa maumivu.
"Beka !! ikasikika sauti ikiita.Elvis
akamuinamia yule jamaa
"Huyo ni nani anakuita?akauliza
kwa sauti ndogo
"Ni mwenzangu tuko naye hapa"
akajibu yule jamaa Muite aje hapa haraka sana
lakini usimueleze kama tuko hapa"
akasema Elvis na kumnyooshea
bastora.
"Peter njoo huku! akasema yule
jamaa kwa sauti iliyojaa
maumivu.Steve na Elvis wakajificha na
mara Peter akaingia mle ndani
"Peter kimbiaaaaa!!! akasema
Beka na Peter akataka kugeuka
akimbie lakini Steve akacheza vizuri
na bastora yake na kumpiga risasi
mbili za mgongo akaanguka
chini,akamuwahi na kuichukua
bastora yake.Akamgeuza akamtazama
lakini alikuwa katika dakika zake za
mwisho.
"Can he make it? Elvis akauliza
"No he won't" akasema Steve
"Mwenzako roho yake
inachukuliwa na ziraili muda huu
nawe utamfuata muda si mrefu endapo hautatueleza ninyi ni akina
nani na mnafanya nini hapa?Kwa nini
mna silaha?
"Msiniue jamani.Sisi tuko hapa
tumepewa kazi ya kufanya"
"Kazi gani na nani kawapa kazi
hiyo?
"Kuna mtu tunamlinda
hapa.Tumepewa kazi na Obi"
"Yuko wapi huyo mtu
mnayemlinda?Kafanya nini?akauliza
Steve
"Ni msichana na hatujui kafanya
nini.Sisi tumepewa kazi ya
kumlinda.Obi ndiye anayefahamu
kafanya nini"
"Inuka haraka tupeleke mahala
alipo huyo msichana" akasema Elvis
na Steve akamshika mkono
akamuinua yule jamaa ambaye
akawapeleka katika chumba
walimomfungia mtu ambaye walikuwa wanamlinda.Msichana
mmoja aliyechafuka damu akiwa
ameinamisha kichwa alikuwa
amefungwa kamba katika
kiti.Haikuhitaji nguvu kubwa
kugundua kwamba yule msichana
alikuwa ameteswa sana
"Winnie !! akaita Elvis na kwa
taabu Winnie akainua kichwa.Hakuwa
na nguvu kabisa.Elvis akamgeukia
yule jamaa na kumtandika ngumi
iliyompeleka hadi chini.
"Mnawezaje kufanya ukatili huu
kwa msichana huyu asiye na kosa
lolote? akasema kwa ukali Elvis na
Steve akaanza kumfungua Winnie
kamba alizofungwa
"Nisaidieni jamani mnipeleke
hospitali."akalia yule jamaa ambaye
jeraha lake liliendelea kutoa damu.
"Elvis !! akasema Winnie kwa
sauti dhaifu baada ya kufunguliwa Winnie you'll be fine" akasema
Elvis na kumuinua Winnie akaanza
kushuka naye chini.
"Jamani nitakufa nipelekeni
hospitali" akalia yule jamaa.Steve
akamtazama kwa hasira na kuchomoa
bastora yake
"You'll go to hospital in hell!!
akasema na kuachia risasi nne na
kuuondoa uhai wa yule jamaa
"Hizi ni salamu kwa hao
wanaowatuma mpambane na watu
msiowafahamu" akasema na kushuka
ngazi haraka haraka kumfuata Elvis
"Umemuacha yule jamaa?
"I killed him"
"Good" akasema Elvis
wakitembea haraka haraka hadi
walipofika katika gari lao .Kulikuwa
na watu wachache wakipita
barabarani lakini hawakuwajali wakampakia Winnie na kuondoka
eneo lile
"Wamemtesa sana"akasema
Steve
"Winnie hakupaswa kupitia haya
yote aliyoyapitia.Mateso haya ni
makubwa sana kwake.Hakustahili"
akasema Elvis
"Naamini kwa haya yaliyomkuta
atakuwa amejifunza akiambiwa
asifanye kitu fulani basi atii.Kama
angesikia tuliyomweleza
yasingemkuta haya yaliyomkuta.Nini
kinafuata baada ya hapa? akauliza
Steve
"Kwa sasa tumshughulikie
Winnie hali yake iboreke halafu
tusubiri taarifa kutoka kwa
Omola"akasema Elvis na kumpigia
simu Dr Philip akamuelekeza mahala
walikohamia na kumtaka afike haraka
sana *****************

Samira na Omola waliwasili
ikulu na hawakupata taabu katika
kuingia kwani taarifa za kuwasili kwa
Omola tayari zilikuwepo.Wasaidizi wa
rais wakamjulisha Omola kwamba rais
hataweza kuonana naye kwa muda ule
kwani alikuwa katika kikao muhimu
hivyo alitoa maelekezo kwamba
atakapofika apelekwe moja kwa moja
kwa makamu wa rais ambaye tayari
amekwisha zungumza naye.Omola na
wasaidizi wale wa rais wakaelekea
moja kwa moja hadi katika ofisi ya
makamu wa rais ambako ilimlazimu
Omola kusubiri kwani tayari makamu
wa rais alikuwa na mazungumzo na
watendaji kadhaa wa ofisi yake.Saa
nne na nusu ndipo makamu wa rais
alipomaliza mazungumzo na watendaji wake na akataarifiwa
kwamba Omola tayari amekwisha
wasili akaelekeza aingie ofisini kwake.
"Karibu sana" akasema makamu
wa rais akimkaribisha Omola.Uso wa
Dr Shafi ulionyesha tabasamu baada
ya kumuona mrembo yule ambaye
kwa wajihi alioutengeneza alionekana
kweli mwandishi wa habari
"Nashukuru sana mheshimiwa
makamu wa rais"akajibu Omola
"Naitwa Omola Otola ni
mwandishi wa habari za
mazingira.Ninafanya kazi na shirika
lisilo la kiserikali ambalo kazi yake ni
kutunza na kuhifadhi mazingira.Katika
shirika letu kuna kitengo cha habari za
mazingira na tuna jarida la mazingira
litokalo kila mwezi hivyo tunazunguka
sehemu mbalimbali duniani kutafuta
habari za mazingira na kuziandika
katika jarida letu.Kikubwa tunachoangalia katika nchi
tunazozitembelea ni namna
wanavyotunza na kuhifadhi
mazingira.Ni mara ya kwanza tunafika
Tanzania kuandika habari za
mazingira.Katika Afrika ni nchi ya
kwanza kuitembelea na tumeamua
kuandika habari za Tanzania katika
jarida letu kwa sababu ni nchi
inayokua kwa kasi kiuchumi.Takwimu
zinaonyesha kuwa kumekuwa na
ongezeko kubwa la shughuli mbali
mbali za kiuchumi hususan viwanda
na katika shughuli hizi za kiuchumi
uchafuzi wa mazingira hauwezi
kukosekana hivyo ni muhimu kujua
namna serikali ya Tanzania
inavyokabiliana na suala la uchafuzi
wa mazingira,namna inavyotunza
mazingira ya fukwe,namna
inavyotunza na kuhifadhi misitu na
vyanzo vya maji.Kwa ujumla tunataka
kufahamuu mazingira kwa upana
wake hapa Tanzania" akasema Omola
"Omola ninashukuru sana
kukufahamu.Mheshimiwa rais
amenipigia simu na kuniueleza
kwamba utakuja kuonana nami hivyo
nikupe ushirikiano.Ni kweli ofisi
yangu ndiyo inayoshughulika na
masuala yote ya mazingira na
nitakueleza kwa upana wake
kuhusiana na mazingira kwa
ujumla.Utaniwia radhi kwani kwa sasa
ninahitaji kupata mapumziko kidogo
halafu tutapata wasaa wa
kuzungumza utaniuliza maswali na
mimi nitakujibu na nitakuelekeza pia
kwa watu wangu wanaohusika na
mazingira na utapata mambo mengi
kupitia kwao.Kama hutojali naomba
tuongozane kupata chai" akasema
makamu wa rais na Omola hakujivunga akakubali wakaongozana
na Dr Shafi kupata chai.
"Karibu sana Tanzania Omola.Ni
mara yako ya kwanza kufika
Tanzania?akauliza Dr Shafi
"Ndiyo mheshimiwa makamu wa
rais.Ni mara yangu ya kwanza kufika
Tanzania.Ni nchi nzuri
nimeipenda.Nimekuwa nikizisikia sifa
zake kwa muda mrefu na leo
nimefurahi kuwa hapa.Nimekutana na
watu wakarimu sana kama vile
nilivyokuwa nikisikia kwamba
waTanzania ni watu wakarimu
mno.Kikubwa kilichonifurahisha ni
namna serikali ya Tanzania
inavyojitahidi kuupaisha uchumi
wake.Hatua zinazochukuliwa na
serikali ya Tanzania katika kuinua
uchumi zinazaa matunda na sasa
uchumi wa Tanzania ni moja ya chumi
za mfano barani Afrika na duniani kwa ukuaji wake wa kasi"akasema Omola
na Dr Shafi akatabasamu
"Ni kweli Omola,uchumi wa
Tanzania unakua kwa kasi kubwa
sana kwani hii ni mipango ya serikai
kwamba kabla ya kufika 2025
Tanzania iwe imeingia katika uchumi
wa kati na kwa namna uchumi
unavyoendelea tunaamini tutafika
lengo hilo" akasema Dr Shafi
wakaendelea na mazungumzo
mengine na wakati wakiendelea
kupata chai makamu wa rais
akafuatwa na kujulishwa kwamba
kuna waziri amekuja anahitaji
kuzungumza naye.Dr Shafi akamtaka
radhi Omola kwamba amepatwa na
dharura na akamuomba aendelee
kumsubiri amalize mazunumzo yake
na waziri aliyemtembelea.Baada ya Dr
Shafi kuondoka Omola akapata nafasi
na kumpigia simu Elvis Omola mambo yanakwendaje
huko? akauliza Elvis baada ya kupokea
simu
"Tayari nimeonana na makamu
wa rais na muda mfupi uliopita
nimekuwa naye ila hatujafanya
mazungumzo yoyote amepata dharura
kuna waziri amekuja ana
mazungumzo naye ila akimaliza
tutazungumza"
"Vipi kuhusiana na ile taarifa ile
kuhusiana na kampuni ya McLorien
ambayo uliahidiwa kuipata leo?
akauliza Elvis
"Oh! Ahsante kwa
kunikumbusha.Nipe muda kidogo
niwasiliane na mtu wangu kama ana
taarifa zozote amezipata kuhusu hiyo
kampuni"akasema Omola na kukata
simu akachukua kijitabu kidogo
kutoka katika mkoba wake akazitafuta
namna fulani nakupiga akazungumza kwa dakika moja na kukata simu
halafu akampigia Elvis
"Elvis mtu wangu amenijulisha
kwamba tayari amekwisha nitumia
taarifa katika barua pepe
yangu.Nitakapokuja jioni tutaifungua
tujue nini amekipata kuhusiana na
kampuni hiyo ya McLorien"
"Sawa Omola.kazi njema.Kama
kuna msaada wowote unauhiaji
nijulishe tafadhali" akasema Elvis
akaagana na Omola na kukata simu na
Omola akaendelea kumsubiri makamu
wa rais hadi alipomaliza kikao na
waziri kisha akamuita Omola ofisini
kwake wakaanza
mazungumzo.Makamu wa raia
akampa Omola muhtasari wa hali ya
mazingira ulivyo hapa nchini na
akamueleza namna
wanavyoshughulikia suala la uharibifu
wa mazingira.Ulikuwa ni muhtsari mrefu na wakati akiendelea Omola
akaomba samahani kwani kifaa kile
kidogo alichokuwa anakitumia
kurekodia kilionyesha
kujaa.Akafungua mkoba wake na
kukiminya kichupa kidogo mithili ya
kichupa cha uturi halafu akachukua
kifaa kingine cha kurekodia
akakiweka mezani akaendelea
kumrekodi makamu wa rais.Sekunde
chache makamu wa rais akaanza
kupiga chafya.
"Oh sorry" akasema Dr Shafi na
kutoa kitambaa mfukoni
"Tunaweza kuendelea" akasema
lakini ghafla akaanza tena kupiga
chafya mfululizo
"Excuse me" akasema na kuinuka
akaelekea katika mlango mdogo
ulioonekana kama maliwato.Kwa
muda wote ambao alikuwa amekaa na
makamu wa rais aliweza kumsoma vizuri na kugundua kwamba alikuwa
anatumia kalamu nyekundu ambayo
aliitoa katika mfuko wake wa koti.Kwa
kasi ya ajabu akafungua mkoba wake
na kutoa kitu fulani kidogo na
kukiweka ndani ya kalamu ile
aliyokuwa anaitumia makamu wa rais
halafu akatoa kitu fulani kama kichupa
cha dawa akakiweka puani kama vile
anavuta hewa ya kile kilichokuwamo
ndani ya ile chupa kisha akatoa tena
kichupa kile mithili ya kichupa cha
uturi na kukipuliza karibu na meza ya
makamu wa rais.Baada ya muda
kidogo makamu wa rais akarejea
"Samahani sana
Omola.Nimepatwa na hii chafya ya
ghafla" akasema makamu wa rais na
,mara tu alipoketi akaanza tena kupiga
chafya mfululizo.
"Pole sana mheshimiwa makamu
wa rais"akasema Omola Usijali Omola.Naomba samahani
sana kwa hali hii iliyonitokea"
akasema makamu wa rais na kuinuka
akaingia tena maliwat😵mola akaiona
mezani simu ya mkononi akaichukua
na kuifungua akatoa kadi ndogo ya
kuhifadhia kumbu kumbu
iliyokuwamo na kuingiza kadi yake
halafu akabonyeza namba kadhaa na
programu fulani ikaingia katika ile
simu ya makamu wa rais.Haraka
haraka akaitoa ile kadi yake na
kuirejesha ile ya makamu wa rais na
kuiweka simu mahala
ilipokuwa.Kitendo kile kilichukua
muda mfupi sana.Sekunde chache tu
baada ya kuirejesha simu,mlango
ukafunguliwa na makamu wa rais
akarejea.
"Omola utanisamehe sana
ninaona hali yangu imebadilika ghafla
hivyo ninahitaji kuonana na daktari wangu mapema.Nadhani itakuwa
vyema kama tukiendelea na
mazungumzo zaidi kesho"
"Sawa mhesimiwa,nitakuja tena
kesho.Pole sana" akasema Omola na
kutoka.Bado Samira alikuwa garini
akimsubiri wakaondoka


*******************

Frank aliwasili katika nyumba
alikopelekwa Vicky,akawakuta vijana
wa Obi wakiwa wameimarisha ulinzi
"Kazi nzuri Obi.Mna hakika
hakuna yeyote aliyekuwa
anawafuatilia?akauliza Frank
"Hapana mkuu hakuna yeyote
aliyetufuatilia"
"Are you sure Obi? akauliza
Frank Ndiyo mkuu.Tumechukua kila
aina ya tahadhari hadi kufika
hapa.Nimewatuma vijana wamefanya
uchunguzi wa eneo lote kuzunguka
hapa hakuna hatari yoyote"
"Vipi kuhusu Vicky,
mmemchunguza hajafungwa kifaa
chochote cha kurekodi mazungumzo?
akauliza Frank
"Hana kifaa chochote
tumemfanyia uchunguzi wa kutosha"
"Good.Where is she?akauliza
Frank na Obi akampeleka katika
chumba alimokuwamo Vicky.Mlango
ukafunguliwa na taa ikawashwa Vicky
tayari alikwisha zinduka.
"Hallow Vicky.Dunia imekuwa
ndogo sana hatimaye tumeonana
tena" akasema Frank huku
akitabasamu
"Winnie yuko wapi? Not so fast pretty
lady.Tunakwenda taratibu hatua kwa
hatua.Mimi nawe tuna mazungumzo
marefu sana siku ya leo" akasema
Frank na kumuita Obi akamtaka
amfungue Vicky pingu alizokuwa
amefungwa.
"Samahani sana Vcky kwa
kukuleta hapa kwa staili hii lakini
imenibid kufanya hivi kwa ajili ya
tahadhari"
"I'm so dissapointed with you
Frank.Kwa nini umenifanyia hivi?Kwa
nini ukamtuma huyu mtu wako kuja
kututeka?Kwa nini umemteka mdogo
wangu na kumpa mateso? Nijibu
Frank kwa nini umenifanyia
haya?Dont you trust me
anymore?akasema Vicky huku
akilengwa na machozi
"Ninakuamini Vicky lakini kwa
mambo yaliyotokea ndani ya siku mbili hizi nimepata mkanganyiko na
sina hakika kama nitakuamini tena"
akasema Frank
"Kitu gani kinakufanya
usiniamini?
"Ninataka unishawishi nikuamini
tena.Nataka unieleze kwa nini
ulimuua Pascal?Nimeumia sana kujua
kamba umeshiriki katika kifo
chake.Tuanzie hapo nieleze kitu gani
kimekufanya umuue Pascal? akauliza
Frank na macho yake yakaanza
kubadilika na kujaa ukatili
"Una hakika ni mimi ndiye
niliyemuua Pascal?Kwa nini
unanihusisha na jambo kama
hili?Mimi ninawezaje kumuua mtu
wangu wa karibu?Wewe na Pascal ni
watu wangu wa karibu na hata mimi
nimeumizwa vile vile na kifo
chake.Tafadhali nakuomba
usinihusishe na jambo kama hilo.Mimi si muuaji.Nilikubali kumuua kanali
Norman kutokana na fedha nzuri
aliiniahidi Deus lakini mimi si
muuaji.I'm not a kiler" akasema
Vicky.Frank akainuka na kumsogelea
"Vicky tell me the trust.Kwa nini
ulimuua Pascal?
"Frank please I'm not a killer"
akasema Vicky
"C'mon Vicky tell me the truth
why you killed him? Who sent you to
kill him?akauliza Frank huku akipiga
kitanda kwa mikono,tayari hasira
zilianza kumpanda
"Frank mambo haya yote
umeyatoa wapi?Aliyekwambia
kwamba mimi nimemuua Pascal
amekudananya.Siwezi kufanya jambo
kama hilo.I'm not a killer like you"
akasema Vicky.Frank akamtazama
kwa hasira Vicky naomba unisikilize
vyema.Frank huyu unayezungumza
naye hapa si Frank yule ambaye
umemzoea.I'm real Frank the killer!
Hivyo nakupa angalizo kuwa makini
sana unapozungumza nami.Nipe
majibu ya maswali yangu
ninayokuuliza or else I'll destroy
you.Dont force me to do that. I'm
asking again why you killed Pascal and
who sent you?
"Frank nimekwisha kueleza
kwamba sihusiki na jambo
hilo.Naomba unieleze kwa nini
unamshikilia mdogo wangu?Where is
she?
"Vicky please I dont want to
destroy you my dear.Tell me the trut.I
swear I'll understand and let you
go.Ninaamini huwezi kufanya jambo
kama hili wewe mwenyewe lazima
kuna mtu amekutuma na huyo ndiye ninayetaka kumjua.Huyo ndiye
ninayemuhitaji" akasema Frank
"Frank nakuomba tusiendelee
kupoteza muda wakati unafahamu
fika kwamba sijahusika na siwezi
kujihusisha na jambo kama
hilo.Naomba usiyachoshe masikio
yangu kwa jambo hilo.Nataka nimone
Winnie" akasema Vicky
"C'mon Vicky.Usitake kulifanya
suala hili likawa gumu zaidi .Tell me
the truth!! akafoka Frank
"There is no truth!! Vicky naye
akafoka.Frank akamtazama kwa
hasira halafu akasema
"Nisikilize vyema.Usijidanganye
kwamba sifahamu
ulichokianya.Ninajua kila kitu.Tayari
nimefuatilia na nimegundua wewe
ndiye uliyempigia simu Pascal
ukamuita aje kule hotelini na huko
ukamuua.Nani alikutuma ufanye hivyo? akauliza Frank.Maneno yale ya
Frank yakamstua Vicky lakini
akajikaza ili Frank asigundue.
"Thats not true.Sijawasiliana na
Pascal kabla ya kifo chake" akasema
Vicky na kuzidi kumpamdisha hasira
Frank akamnasa kofi kali
"Yes you called him !!!akafoka
Frank
"If you don't tell me the trruth I
swear I'm going to destroy you and
Winnie!!
Vicky aliyekuwa ameanguka
kitandani kufuatia kofi kali la Frank
akainuka aliposikia jina Winnie
likitajwa
"Dont dare touch her!!! akasema
Vicky
"Kama hutanieleza ukweli nani
alikutuma umuue pascal nitamuua
Winnie tena mbele ya macho yako.Ninakupa nafasi ya mwisho
.Niambie ukweli !!
"Frank tafadhali nakuonya
usimguse mdogo wangu.Cheza na
mimi utakavyo lakini si
Winnie.Uliyekuwa unanitafuta ni mimi
na si Winnie.Yeye hahusiani kwa
lolote na wewe ndiyo maana
nimejileta kwako ili umuachie
Winnie.Please let her go!! akasema
Vicky
"Uhai wa Winnie uko mikononi
mwako.Wewe ndiye utakayeamua
kumuua au kumuacha hai.Kama
utanieleza ukweli Winnie ataendelea
kuwa hai lakini kama utanificha
nitaanza kwanza kumtoa uhai Winnie
na wewe utafuata tena kwa mateso
makali mno"
"Ni ukweli upi unautaka Frank? Tell me everything.Niambie nani
kakutuma umuue Pascal?Nani
unashirikiana nao?
"Nimekwisha kwambia hakuna
mtu yeyote aliyenituma na wala
ninayeshirikiana naye"
"Where is Elvis?!!! akauliza Frank
kwa ukali
"Elvis?!! Vicky akashangaa
"Ni nani huyo Elvis?akauliza
"Usijifanye humjui Elvis.Yule
jamaa aliyekufuata akaanza
kukuchunguza kuhusiana na kifo cha
kanali Norman"
"That man is dead!.Isn't he? Tena
wewe mwenyewe ndiye uliyeniambia
kwamba mmemuua sasa iweje
uniulize yuko wapi wakati unafahamu
mahala alipo?akauliza Vicky
"Vicky unajifanya mjanja sana
siyo?Kwa taarifa yako tayari Winnie
ametueleza kila kitu.Ametuelezakuhusu Elvis na mwenzake Steve
ambao waliwateka na kukulazimisha
uwaonyeshe mahala nilipo.Kwa nini
hutaki kunieleza ukweli kuwa ni wao
ndio waliokutumia ili kumpata
Pascal?Kwa nini unanificha jambo hilo
wakati tayari ninalifahamu?akauliza
Frank na Vicky akatoa kicheko
"Do you believe her?akauliza
"Winnie amekudanganya"
"Hapana
hajanidanganya.Alifahamu kwamba
ninakutafuta kwa ajili ya kufahamu
kwa nini ulishiriki katika mauaji ya
Pascal na akanieleza kwamba wewe
huhusiki bali ulilazimishwa kumuita
Pascal hotelini.Alinieleza kila kitu ili
niweze kukuacha huru kwani ana
wasiwasi wale jamaa wanaokushikilia
wanaweza wakakuua. Alinitaka
nikuokoe kutoka katika mikono ya hao
jamaa aliowataja kwa majina ya Elvis na Steve.Kama haitoshi alinieleza pia
kwamba katika nyumba hiyo
mliyokuwa mnashikiliwa yupo pia
mwanangu Graca ambaye alitoroshwa
na Elvis kutoka afrika ya
kusini.Nilimtaka akanionyeshe mahala
hapo mnaposhikiliwa tukaenda na
hatukukuta mtu yeyote.Ninataka
kuwafahamu hao jamaa ni akina
nani?Kwa nini
wananitafuta?Ninavyofahamu ni
kwamba Elvis aliyemtorosha Graca
kutoka Afrika kusini tayari amefariki
dunia nataka kujua ni Elvis yupi huyo
aliyekuwa anakushikilia?Ninahitaji
sana kuwafahamu hawa jamaa ni
akina nani na wako wapi.Sina shida
yoyote na wewe Vicky.Ninakuomba
tafadhali nieleze ukweli kuhusu hawa
jamaa ninawahitaji sana" akasema
Frank Frank narudia tena kukueleza
kwamba Winnie
amekudanganya.Nashangaa mambo
haya yote aliyokueleza ameyatoa
wapi.Hakuna mtu yeyote aliyetuteka
zaidi ya yule aliyekuja kutaka
kututeka nyumbani ambaye ninaamini
wewe ulimtuma ukiamini kwamba
nimehusika katika kumuua
Pascal.This is a big lie.Hakuna Elvis
wala Steve ninaowafahamu.It's a lie"
akasema Vicky
"Vicky tafadhali huu si wakati wa
utani.Nieleze ukweli tafadhali."
akasema Frank
"Ukweli upi unaouhitaji
Frank?Nimekueleza kila kitu kwamba
Winnie alikudanganya"
"Hapana.Hakunidanganya.Sina
mahusiano yoyote na Winnie na sina
hakika kama ananifahamu lakini
alinipigia simu akahitaji kuonana nami na tulipoonana akanieleza haya yote
akiomba nikusaidie kwani uko katika
matatizo" akasema Frank na
kumtazama Vicky kwa hasira halafu
akauliza
"Where were you last night?
"Last night? akauliza Vicky
"Ndiyo ulikuwa wapi?
"Hayo ni masuala yangu binafsi
ambayo hutakiwi
kuyafahamu"akasema Vicky
"I need to know Vicky.Kwa
mujibu wa Winnie uliwaahidi hao
jamaa kwamba utawapeleka mahala
ambako unaamini wanaweza kunipata
na jana usiku nikiwa katika nyumba
ambayo Winnie alinipeleka akidai
ndiko mlikokuwa mnashikiliwa
nikataarifiwa kwamba kuna watu
wamevamia katika nyumba yangu ya
shambani na wakaingia katika ofisi
yangu ninamohifadhi mambo yangu ya siri wakachukua kila walichoona
kina wafaa.Ninaamini waliofanya
hivyo ni hao jamaa waliokuwa
wanakushikilia na ninaamini wewe
ndiye uliyewapeleka huko kwani
uliwaahidi kufanya hivyo.Vicky
ninarudia tena kukuomba kwa mara
ya mwisho hawa watu ni akina nani na
wanataka nini kwangu?Ninataka
kujua huyo mtu anayeitwa Elvis ni
yupi?
"Frank sitaki kuendelea
kuzungumza tena masuala hayo
ambayo nimekwisha kueleza kwamba
si ya kweli.Tafadhali nionyeshe alipo
Winnie!!Let her go!! akasema Vicky
huku akihisi mwili unamtetemeka
kwa ndani.Frank akazidi kumtazama
kwa hasira
"Vicky sikutaka kukufanyia hivi
lakini umenilazimisha wewe
mwenyewe nikuharibu and I'll destroy you!! akasema na kutoka akamkuta
Obi amesimama nje ya mlango
"Obi huyu mwanamke bado
mgumu kusema chochote.Sikutaka
kumtesa lakini amenilazmisha
kufanya hivyo.Ninataka umfunge na
twende naye kule aliko mdogo
wake.Nitamtesa na atasema kila kitu
na hata ikibidi kumuua mdogo wake
nitafanya hivyo.Leo lazima niupate
ukweli!! akasema Frank na Obi
akaingia ndani ya kile chumba
akamfunga Vicky kitambaa
usoni,akamfunga pingu za mikono
akamtoa mle ndani na kumfungia
katika buti ya gari wakaondoka
kuelekea mahala walikomuacha
Winnie

****************Elvis na Steve walimpitia Dr
Philip mahala walikopanga wakutane
wakaelekea moja kwa moja katika
makazi yao mapya.Elvis akamueleza
kila kitu kilichotokea na mahala
walipofikia katika uchunguzi wao
"Poor girl.Ameingia katika
matatizo ambayo
hakuyategemea.Hakupaswa
kufanyiwa ukatili wa namna hii.Watu
hawa wana roho za kinyama
sana"akasema Dr Philip huku
akimuangalia Winnie namna
alivyochafuka kwa damu
"Ni watu makatili sana lakini siku
zao zinahesabika.Tayari tumepata
mwangaza mkubwa kuhusiana nao na
nina uhakika muda si mrefu sana
tutakuwa tumepata taarifa kamili za
kuhusiana na mtandao wao" akasema
Elvis na safari ikaendelea hadi
walipofika katika makazi yao.Haraka Winnie akashushwa na kuingizwa
ndani Dr Philip akaanza
kumuhudumia.Wakati Winnie
akiendelea kuhudumiwa Elvis
akamuita pembeni Graca
"Vicky hajarejea?akamuuliza
"Hapana hajarejea"akajibu Graca
na taarifa ile ikamshangaza sana
Elvis.Steve akatoka haraka kwenda
kununua mahitaji kwani hawakuwa
wamepitia sehemu yoyote wakiwahi
kumpatia huduma Winnie
"Vicky amekwenda wapi?Kwa
nini hakuaga tujue anakwenda wapi?
akajiuliza Elvis na kutolewa mawazoni
baada ya simu yake kuita.Mpigaji
alikuwa Omola
"Omola mambo
yanakwendaje?akauliza Elvis
"Mambo yanakwenda
vizuri.Tayari nimeondoka kwa
makamu wa rais na ninaelekea hotelini.Naomba aje mtu kunichukua"
akasema Omola na muda huo huo
Elvis akampigia simu Steve akamtaka
akamchukue Omola hotelini kwake.
"Anaendeleaje?Elvis akauliza
baada ya kuingia katika chumba alimo
Winnie
"Anaendelea vyema.Tumuache
apumzike na akiamka ataendelea
kutumia dawa za kumsaidia kutuliza
maumivu.Amepata michubuko kwa
nje lakini haionyeshi kama
ameumizwa kwa ndani hivyo dawa
hizi zitamsaidia" akasema Dr Philip na
kwa kuwa alimaliza kazi yake
aliyoitiwa akaagana na akina Elvis
akaondoka.Hakuwa amekuja na gari
hivyo ikamlazimu kutembea kwa
miguu kutafuta taksi.Wakati
akiwasubiri akina Omola,Elvis
akaenda kujipumzisha chumbani
kwake Vicky amekwenda wapi?Kwa
nini akaondoka kimya kimya bila
kuaga?Staili yake ya kuondoka inanipa
mashaka sana hata hivyo ngoja
tuendelee kumsubiri.Kingine
kinachoniumiza kichwa ni namna gani
akina Frank walivyoweza kumpata
Winnie?Amewaeleza mambo
gani?Atatueleza kila kitu
atakapoamka.Imekuwa ni jambo zuri
kumshirikisha Omola katika
operesheni hii kwani bila yeye
tusingeweza kumpata Winnie kwa
haraka namna hii..." Elvis akatolewa
mawazoni baada ya mlango wake
kufunguliwa akaingia Graca
"Elvis poleni sana na hongereni
kwa kufanikiwa kumpata Winnie"
akasema Graca na kukaa karibu na
Elvis
"Tumewahi kumpata kabla ya
wale jamaa hawajamuumiza sana" Vipi kuhusu zile nyaraka
tulizozipata jana ofisini kwa
baba,kuna maendeleo yoyote
yamepatikana?
"Nyaraka zile ni muhimu sana na
uchunguzi wake
unaendelea.Zimetusaidia tumepiga
hatua kubwa na tumepata mwangaza
kuhusiana na biashara hii ya
silaha.Tumefanikiwa kumpata Irene
mwabukusi ambaye nyaraka
zinaonyesha ndiye mmiliki wa
kampuni ya Pendeza Co.Ltd .Irene
amekiri kwamba kampuni ya Pendeza
ni kampuni ya Frank lakini yeye ndiye
msimamizi mkuu.Mizigo imekuwa
inatumwa kutoka kampuni ya
McLorien kuja katika kampuni ya
Pendeza na muagizaji mkuu wa mizigo
hiyo ni David.Ikifika Tanzania mizigo
hiyo hutolea bila kufanyiwa ukaguzi
na kisha David huipeleka mahala ambako hutoa silaha na kisha
hupeleka mali katika maduka
yake.Irene anadai kwamba Pendeza
Co.Ltd iko pia katika nchi za Congo na
Burundi.Tunahisi kuwa David
anatumia kampuni hii ya Pendeza
kupitishia mizigo ya silaha.Tunataka
tuichunguze pia kampuni ya McLorien
ambayo inaonekana ndiyo inayotuma
mizigo kwa kampuni ya
Pendeza.Tunamsubiri Omola ambaye
aliomba msaada kwa wenzake
wamsaidie kuichunguza kampuni hii
ya McLorien na tayari amekwisha
tumiwa majibu katika barua pepe
akifika ataifungua na tutajua nini
wamekipata kuhusiana na kampuni
hii.Graca mambo yanakwenda vizuri
usiwe na hofu tutahakikisha yeyote
anayejihusisha na mtandao huu
anafikishwa mbele ya sheria" Sina cha kusema
Elvis,ninawaombea wewe na wenzako
mfanikiwe katika suala hili ili na mimi
niweze kuwa huru kwani bila baba na
mtandao wake kumalizwa nitaendelea
kuishi maisha kama ya ndege ya
kujificha ficha.Lakini kwa kuwa niko
nawe karibu siogopi tena.Elvis
nakuomba usiivunje ahadi uliyonipa
kwani ukifanya hivyo utauvunja moyo
wangu vipande.Nimepitia mengi
magumu,nimepita katika giza nene na
sasa nimeanza kuona mwangaza
katika maisha yangu hivyo sihitaji
kuumizwa tena.Lizingatie hilo"
akasema Graca na kumbusu Elvis
akaelekea chumbani kwake
"Graca anasema kweli,amepitia
mengi magumu na hapaswi kuumizwa
tena na mimi nimekwisha muahidi
kwamba nitakuwa naye kimapenzi na
tayari amechanganyikiwa juu yangu.Nitafanya nini wakati bado
ninampenda Patricia?Ngoja niyaweke
pembeni masuala haya ya wanawake
nimalize kwanza masuala muhimu
kisha nitajua nini cha kufanya."
akawaza Elvis
"Nina uhakika mkubwa kwamba
Frank anaitumia kampuni hii ya
Pendeza kupitishia silaha.Ndani ya
makontena hayo yanayotumwa
ninaamini ndimo silaha hupakiwa na
ndiyo maana makontena hayo
hutolewa bila kufanyiwa ukaguzi
wowote ili kuficha kile kilichomo
ndani yake.Frank huyapeleka katika
shamba lake na kule hupakua silaha
na kisha huzisafirisha kwenda nchini
Congo.Tayari mwanga huo nimeupata
lakini bado nahitaji ushahidi
zaidi.Nahitaji kuwafahamu wote
waliomo katika mtandao huu"
akaendelea kuwaza Elvis ****************

Frank na Obi wakiwa na vijana
wao wakawasili eneo la viwanda
ambako Winnie alikua
amepelekwa.Baada ya kufika katika
jengo alimokuwamo Winnie,Vicky
akashushwa toka katika buti ya gari
na kufunguliwa kitambaa.
"Hapa ni wapi? akauliza huku
akitetemeka
"Quiety!! akasema Frank na
kumtaka Vicky apandishwe
ghorofani.Vijana wawii wakamshika
Vicky na kuanza kumpandisha juu
Frank na Obi wakiwa wametangulia
mbele.Obi akamuongoza Frank katika
chumba alimokuwa amefungiwa
Winnie lakini wote wakapatwa na
mshangao mkubwa sana baada ya kukuta chumba kitupu na kamba
alizofungiwa zilikuwa zimekatwa na
kutupwa
"beka!!!! akaita Obi lakini
hakujibiwa
"Peter !!! akaita tena lakini
akajibiwa na ukimya mkubwa
"Somehing is wrong ! akasema
Obi kwa sauto ndogo na kutoka
haraka mle chumbani
"Obi nini kimetokea?Wako wapi
vijana?Winnie yuko wapi? akauliza
Frank akimfuata Obi nyuma.Ghafla Obi
akasimama kama mtu aliyekutana na
kitu cha kutisha akahisi miguu
inamuisha nguvu akapiga magoti na
kushika kichwa
"Oh my God!! akasema Obi na
mara Frank naye akaingia mle ndani
ya kile chumba na kuwakuta vijana
wawili wakiwa wamekufa kwa
kupigwa risasi Who did this !!! akasema Frank
kwa mshangao na kwa hasira
akamfata Vicky akamuwekea bastora
kichwani
"Utanieleza wapi walipo watu
uliowasaidia kumuua Pascal? akasema
na kumshika Vicky nywele
akampeleka katika chumba kile
walichouawa wale vijana wawili
"You see this?!akauliza
"Waliofanya hivi ni hao wenzako
unaoshirikiana nao.Ukitaka nikuache
hai nieleze wako wapi?
"Winnie yuko wapi? Siwezi
kusema chochote bila kumuona
Winnie.Show me Winnie and I'll tell
you everything" akasema Vicky Frank
akapandwa na hasira akamrushia
ngumi nzito iliyompeleka chini
akamkalia juu na kuanza
kumporomoshea makonde Mkuu imetosha.Utamuumiza
huyu na tutakosa kila kitu" akasema
Obi na kumvuta Frank ambaye
alikuwa amepandwa na hasira isiyo
kifani.Uso wa Vicky uliloa damu na
mara simu ya Frank ikaita.Akaitoa
mfukoni na kutazama mpigaji alikuwa
ni Irene akasogea pembeni
"Irene" akasema baada ya
kuipokea
"Frank where are you? I need to
see you !! akasema Irene
"Kuna tatizo Irene? akauliza
Frank
"Chochote unachokifanya achana
nacho nakuhitaji hapa nyumbani sasa
hivi.Kuna jambo la msingi sana"
"Irene ni jambo gani hilo?Huwezi
kunieleza simuni?
"Frank believe me acha kila
unachokifanya na uje hapa nyumabani
ninakusubiri.Usipuuze tafadhali"akasisitiza Irene.Frank
akazama katika tafakari
"Frank !! akaita Irene
"I'm coming there" akasema
Frank na kumtaka Obi wazungumze
"Obi kuna dharura imejitokea
ninahitajika sehemu fulani.Take care
of everything here.Mrudisheni Vicky
na hakikisha anaongea.Do everything
you can to make her tell us
everything!! akasema Frank na
kuondoka haraka haraka akionekana
kuchanganyikiwa
"Bastard !! akapiga usukani wa
gari baada ya kukumbuka miili ya
wale vijana wawili waliouawa na
Winnie kutoweka
"Nani huyu aliyefanya
haya?Amefahamuje kama Winnie
yuko pale? Winnie alikuwa ni muhimu
sana kwetu kwani bila yeye Vicky
hawezi kutueleza jambo lolote.I'm back to square one.Watu hawa tayari
wanaonekana kunifuatilia kila
mahala,na wanafahamu kila
ninachokifanya.I must find them
immediately!! akawaza akiendesha
gari kuelekea nyumbani kwa Irene
"I think Winnie and Vicky are
playing a game with me.Kauli zao
zinakinzana.Winnie anadai kwamba
walikuwa wametekwa na watu ambao
amewataja kwa majina na mmoja wa
watu waliotajwa ni Elvis lakini Vicky
amekana kutekwa na watu hao.Winnie
ametupeleka hadi mahala walikokuwa
wanashikiliwa lakini hatukukuta mtu
yeyote mahala hapo na tukiwa hapo
ofisi yangu shambani ikavamiwa na
mpaka sasa hakuna mtu yeyote
aliyeonekana akiingia ndani ya
nyumba hiyo.Leo tena Vicky
amejitokeza na kukana kila kile
alichokisema Winnie na kama haitoshi Winnie akatoroka.What kind of game
are they playing?How could I be such
a fool?!! How could I let them fool me
like this?! akawaza na kuupiga
usukani kwa hasira
"Vicky atanieleza kila kitu
leo.Nitampa kila aina ya mateso hadi
atakaponieleza ukwe.." Frank
akatolewa mawazoni baada ya simu
yake kuita.Alikuwa ni David
"Hallow David" akasema Frank
" Hallo Frank.Habari za leo?Vipi
maendeleo yako ?
"Ninaendelea vyema.Vipi wewe?
"Hata mimi ninaendelea
vyema.Nimekupigia kukujulia hali
kwani toka asubuhi sijaipata simu
yako.Tuko katika hatua kubwa sana
hivi sasa tunapaswa kuwa na
mawasiliano ya karibu na kupeana
taarifa za mara kwa mara juu ya kile
kinachoendelea kujiri.Dr Makwa amelala nyumbani kwangu kwa
kuhofia kukamatwa na amekuwa
akiwasiliana na wenzake kuhusiana
na kinachoendelea na taarifa
anazoendelea kupokea ni kwamba kila
kitu kinakwenda vyema na maandalizi
yanaendelea ya mkutano wa leo.Jioni
ya leo lazima tuwe na kikao tujadili
kuhusu mambo yalivyokwenda na
kinachoendelea.Baada ya mkutano wa
leo tutapata picha kamili ya namna
operesheni yetu inavyokwenda"
akasema David
"Sawa David.Tutakutana jioni ili
tupeane taarifa zaidi kuhusu
operesheni hii" akasema Frank
"Frank are you ok today?akauliza
David
"Why?Frank naye akauliza
"Unaonekana hauko sawa.Vipi
kuhusu mazishi ya pascal? Ni kweli siko sawa David kuna
jambo fulani linaniumiza kichwa
sana.Kuhusu Pascal bado sijapata
taarifa kamili ni lini anazikwa.Nitapita
msibani baadae kupata taarifa kisha
nitakujulisha"
"Frank umesema kwamba kuna
jambo linakuumiza kichwa.Ni jambo
lipi?Linahusiana na hili suala
letu?Kama linahusiana na sisi liweke
wazi tulifanyie kazi haraka.Hatutaki
kikwazo chochote kwa sasa"
"Ni suala binafsi ninaweza
kulishughulikia"
"Sawa Frank tutawasiliana
baadae"akasema David na kukata
simu
"Sijui kwa nini nimeanza
kumchukia David.Huyu jamaa ninahisi
anaweza akahusika pia katika kifo cha
Pascal.Lakini suala ili la kifo cha Pascal
bado lina ukakasi.Winnie aliwataja Elvis na Steve kwamba walimteka
Vicky na kumlazimisha kumuita Pascal
pale hotelini kisha wakamuua.Madam
Elizabeh naye akadai kwamba yeye
ndiye aliyemuua
Pascal.Ninaposhindwa kupata jibu ni
je madam Elizabeth ameshirikiana na
hao akina Steve?Nilimuuliza kuhusu
kushirikiana na Vicky na akadai
kwamba ndiyo alishirikiana na Vicky
..oh gosh I'm confused.Ngoja niliendee
taratibu hili suala nikiliendea kwa
pupa litanichanganya.Mwenye majibu
yote juu ya suala hili ni Vicky.Nina
uhakika nikimtesa atanieleza ukweli
wote kama kweli alitumwa na madam
Elizabeth au vipi.Kama kweli
alimtuma nitachunguza nijue Pascal
alifanya jambo gani hadi
akauawa?akaendelea kuwaza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom