Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #81
SEHEMU YA 65
“Haya, po pote pale ni sawa.”
Waliingia ukumbini na kukaa juu ya makochi. Wote walikuwa wamechoka lakini Fuad alikuwa amechoka zaidi.
Mara Fuad alipiga makelele na kumwita Kijakazi, “Kijakazi!”
“Bee!” Kijakazi aliitika mbio mbio.
“Hebu tuletee maji ya kunywa.”
Haikuchukua muda mara Kijakazi aliingia ndani na jagi la maji pamoja na gilasi. Aliviweka vitu hivyo juu ya meza iliyokuwapo katikati ya ukumbi buo na bapo hapo alitoka nje.
“Yule ni nani?” aliuliza mmoja wa wale watu.
“Yule ni mzee wangu. Yupo hapa siku nyingi tokea uhai wa marehemu baba yangu,” Fuad alijibu.
“Alaa!” alisema yule mtu.
Kila aliyetaka kunywa maji alijitilia mwenyewe ndani ya gilasi na kunywa. Fuad alikaa juu ya kiti akiwa amechoka sana hata hakuweza kujiinua.
“Naam, sasa mnasemaje?” Fuad aliuliza.
“Sisi hatuna maneno mengi. Jambo tunalotaka kukwambia ni kwamba hili shamba tumekwisha lipima na sasa litakuwa ni mali ya serikali na tutawagawia wale wakulima wasiokuwa na ardhi, lakini ilivyokuwa na wewe ni mtu vile vile na unahitaji kuendesha maisha yako basi tutakukatia eka tatu katika sehemu yo yote ile unayotaka mwenyewe na sehemu hiyo itakuwa yako wewe.
Fuad alishtuka, roho ilimruka na alikaribia kuzimia. Hakuwa na la kusema, kabaki kushangaa, kinywa wazi. Machozi yalianza kumlengalenga lakini ilimbidi ajizuie kulia Mara alianza kusema kwa unyonge. “Hivyo nd’o mnaninyang’anya shamba langu?”
“Ala! Kwani hawakuja watu kukwambia habari ya sheria ya ardhi iliyopasishwa na serikali ya kimapinduzi?” aliuliza mmoja katika wale watu.
“Ah Walikuja, lakini...”
Fuad hakuwa na la kusema. Alikuwa hata hajui analolisema wala analolifanya.
“Lakini nini?” aliuliza yule mtu.
“Lakini hili ni shamba langu, haki yangu mwenyewe nimerithi kwa marehemu baba yangu!”
“Kama tulivyokwambia, sisi ni wajumbe tu na mjumbe hauawi. Maneno yotu nd’o kama tulivyokwisha kukwambia. Kama una malalamiko yo yote unaweza kufika makao makuu ya onsi yetu huko mjini.”
“Ah haya bwana, mimi sina la kusema. Fanyeni mna. vyotaka,” Fuad alisema shingo upande na mnyonge kabisa.
Pale pale wale watu walitoka na kumwacha Puad amekaa pale ukumbini. Alibakia pale pale juu ya kiti amepigwa na bumbuazi hajui la kulifanya. Hamaki zilikuwa zimemjaa lakini alizidiwa nguvu. Usiku ulikuwa umekwisha ingia na Fuad aliwasha karabai na baadaye akarejea pale pale alipokuwa amekaa juu ya kiti.
Kijakazi ambaye alikuwa amekaa pale palenjeya nyumba aliingia ndani kwenda kumwangalia Fuad baada ya kumwona kimya kwa muda mrefu. Alinyatia kidogo pale ukumbini, na alipochungulia ndani humo alimwona Fuad amelala usingizi juu ya kiti. Huruma za moyo zilimjaa na aliweza kubaini mara moja kwamba watu wale walikuja kumkera Bwana wake. Alikwenda mpaka karibu yake akapiga magoti chini na kuanza kumvua viatu vilivyokuwa vimechafuka kwa dongo jekundu.
Mara Fuad alizindukana na kumsukumia teke Kijakazi.
“Unafanya nini hapa? Nani kakwita? Tokea lini ukathubutu kuingia ndani humu bila ya kuitwa. nyama mkubwa wel” Fuad alipiga makelele.
Kijakazi alianguka chini vibaya kidogo kichwa chake akipige sakafuni. Alijiburura nyuma na kuegemea ukuta huku amejikunyata kama mtu aliyeshikwa na baridi kali.
“Haya, po pote pale ni sawa.”
Waliingia ukumbini na kukaa juu ya makochi. Wote walikuwa wamechoka lakini Fuad alikuwa amechoka zaidi.
Mara Fuad alipiga makelele na kumwita Kijakazi, “Kijakazi!”
“Bee!” Kijakazi aliitika mbio mbio.
“Hebu tuletee maji ya kunywa.”
Haikuchukua muda mara Kijakazi aliingia ndani na jagi la maji pamoja na gilasi. Aliviweka vitu hivyo juu ya meza iliyokuwapo katikati ya ukumbi buo na bapo hapo alitoka nje.
“Yule ni nani?” aliuliza mmoja wa wale watu.
“Yule ni mzee wangu. Yupo hapa siku nyingi tokea uhai wa marehemu baba yangu,” Fuad alijibu.
“Alaa!” alisema yule mtu.
Kila aliyetaka kunywa maji alijitilia mwenyewe ndani ya gilasi na kunywa. Fuad alikaa juu ya kiti akiwa amechoka sana hata hakuweza kujiinua.
“Naam, sasa mnasemaje?” Fuad aliuliza.
“Sisi hatuna maneno mengi. Jambo tunalotaka kukwambia ni kwamba hili shamba tumekwisha lipima na sasa litakuwa ni mali ya serikali na tutawagawia wale wakulima wasiokuwa na ardhi, lakini ilivyokuwa na wewe ni mtu vile vile na unahitaji kuendesha maisha yako basi tutakukatia eka tatu katika sehemu yo yote ile unayotaka mwenyewe na sehemu hiyo itakuwa yako wewe.
Fuad alishtuka, roho ilimruka na alikaribia kuzimia. Hakuwa na la kusema, kabaki kushangaa, kinywa wazi. Machozi yalianza kumlengalenga lakini ilimbidi ajizuie kulia Mara alianza kusema kwa unyonge. “Hivyo nd’o mnaninyang’anya shamba langu?”
“Ala! Kwani hawakuja watu kukwambia habari ya sheria ya ardhi iliyopasishwa na serikali ya kimapinduzi?” aliuliza mmoja katika wale watu.
“Ah Walikuja, lakini...”
Fuad hakuwa na la kusema. Alikuwa hata hajui analolisema wala analolifanya.
“Lakini nini?” aliuliza yule mtu.
“Lakini hili ni shamba langu, haki yangu mwenyewe nimerithi kwa marehemu baba yangu!”
“Kama tulivyokwambia, sisi ni wajumbe tu na mjumbe hauawi. Maneno yotu nd’o kama tulivyokwisha kukwambia. Kama una malalamiko yo yote unaweza kufika makao makuu ya onsi yetu huko mjini.”
“Ah haya bwana, mimi sina la kusema. Fanyeni mna. vyotaka,” Fuad alisema shingo upande na mnyonge kabisa.
Pale pale wale watu walitoka na kumwacha Puad amekaa pale ukumbini. Alibakia pale pale juu ya kiti amepigwa na bumbuazi hajui la kulifanya. Hamaki zilikuwa zimemjaa lakini alizidiwa nguvu. Usiku ulikuwa umekwisha ingia na Fuad aliwasha karabai na baadaye akarejea pale pale alipokuwa amekaa juu ya kiti.
Kijakazi ambaye alikuwa amekaa pale palenjeya nyumba aliingia ndani kwenda kumwangalia Fuad baada ya kumwona kimya kwa muda mrefu. Alinyatia kidogo pale ukumbini, na alipochungulia ndani humo alimwona Fuad amelala usingizi juu ya kiti. Huruma za moyo zilimjaa na aliweza kubaini mara moja kwamba watu wale walikuja kumkera Bwana wake. Alikwenda mpaka karibu yake akapiga magoti chini na kuanza kumvua viatu vilivyokuwa vimechafuka kwa dongo jekundu.
Mara Fuad alizindukana na kumsukumia teke Kijakazi.
“Unafanya nini hapa? Nani kakwita? Tokea lini ukathubutu kuingia ndani humu bila ya kuitwa. nyama mkubwa wel” Fuad alipiga makelele.
Kijakazi alianguka chini vibaya kidogo kichwa chake akipige sakafuni. Alijiburura nyuma na kuegemea ukuta huku amejikunyata kama mtu aliyeshikwa na baridi kali.