RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.
MTUNZI : ALEX KILEO..
SEHEMU YA KUMI NA SITA NA KUMI NA SABA.
______________
ILIPOISHIA
_______________
Baada ya kula na kuoga, wote walikaa
sebuleni
wakawa wanaangalia filamu za
Tanzania, kayoza akavunja ukimya,
"mama, baadae yenyewe si ndio sasa
hivi?, tuadithie basi" Kayoza
alimkumbusha mama yake,
"khaa!, nawe
nae usahau?" Mama kayoza
akamwambia mwanae kwa utani
huku anacheka.
"matatizo
yanasahaulika nini?", kayoza
akamjibu mama yake.
"haya basi,
nianzie wapi?" Mama kayoza akauliza
huku akimuangalia mwanae.
"anzia mwanzo" kayoza
akajibu huku akitega masikio ili
kusikiliza kisa kilichopelekea yeye
kuwa mtu wa kubadilika na kuwa
kama mnyama.
Mama kayoza akaanza
kuwaelezea...
____________
ENDELEA...
_____________
Alianza namna hii, "mimi
nilipoolewa na baba yako, nilimkuta
ana fedha zake za kutosha, alikuwa
ana magari makubwa ya kubebea
mizigo, alikuwa na daladala pale
Bukoba mjini, alikuwa na gari ndogo
tatu za kutembelea, na nyumba tatu
pia.
Kwa hiyo yeye alitoka Bukoba
mpaka Kilimanjaro kuja kunioa mimi,
kwa madai ya kuwa alinipenda toka
zamani na alikuwa ananifuatilia chini
chini.
Baada ya ndoa nilitoka nyumbani na kuhamia kwenye nyumba ya baba yako ambayo aliijengea Bukoba.
Ila baada ya kuhamia Bukoba,
nilikaa pale nyumbani kwangu wiki
mbili ndani, hakuna hata jirani
mmoja aliyekuja kuniona, mule
ndani nilikaa na wafanyakazi tu, na
baadhi ya ndugu wa baba yako
ambao walikuwa ndio
wananichangamsha changasha, ila
kingine kilichokuwa kinanishangaza ni
kwamba kila ilipofika mwisho wa
mwezi, baba yako alinunua, mbuzi
wawili weusi na kondoo mmoja, alafu
wanaukoo wote walikuja pale
nyumbani, walikuwa wanaingia katika
chumba kimoja kilichopo uwani na kujifungia uko, mimi sikuruhusiwa kuingia.
Na nilipomuuliza, yeye
aliniambia kile chumba ni kitakatifu,
mimi sikuwa mtu wa kuhoji hoji sana,
kwa hiyo sikutaka kudadisi zaidi kwa maana nilipojaribu kufanya hivyo uso wake ulionesha kutofurahishwa na maswali yangu.
Ila niliendelea kujiuliza mwenyewe ni nini utakatifu
wa hicho chumba?.
Wanandugu wa baba yako na baba yako mwenyewe waliendelea kuingiaingia katika
chumba iko ambacho ni kikubwa,
kilikuwa na uwezo wa kubeba watu
mia na zaidi.
Kingine cha kushangaza ni kwamba, wote walikuwa wanavaa
mavazi meusi, iwe shuka au nguo ya
kawaida, ili mradi mwanamke avae
nguo ndefu hadi katika vidole vya
miguu yake.
Na kila siku wanayoingia katika hicho chumba ikifika usiku mkubwa,
walichukua magari makubwa ya
mizigo na kuenda wanapopajua
wenyewe, pamoja na wale mbuzi na
kondoo.
Ila baadae baba yako alikuja
kuniambia kuwa uwa wanaenda
kutoa sadaka katika mzimu wa mababu
zao walikufa miaka iliyopita, na kwa sasa yeye ndio
kaachiwa mamlaka ili autunze mzimu mmoja ambao ni mkuu kuliko mizimu yote wanayoiabudu.
Sikufurahishwa
na hali hiyo, ila sikutaka kumuudhi
mume wangu, baada ya miaka miwili
ya ndoa, nikajifungua mtoto wangu
wa kwanza ambae ni kaka yako", Mama Kayoza aliongea kisha akamimina maji katika kikombe na kunywa,
"mama mbona
huyo kaka yangu simfahamu, au yupo mbali na nchi hii?" kayoza
akahoji.
"Subiri sasa mbona una
haraka hivyo?" mama Kayoza
akauliza huku akimshangaa mwanae,
"Maswali ni lazima, sasa nisipouliza utajuaje kama nimekuelewa?" Kayoza alihoji
"Sikiliza kwanza, maswali utauliza nikimaliza kusimulia" Mama kayoza alijibu kisha akaendelea,
"baada ya kumzaa
kaka yako wa kwanza, furaha
iliongezeka katika familia yetu, ila kitu ambacho
kilikuwa kinanitatiza ni kuwa,
majirani hawakutaka kabisa
kunizoea na wala hawakutaka hata kuja kutujulia hali kipindi nimejifungua, sikujua sababu, ila siku
moja kuna jirani mmoja ndio
akanipasulia sababu, eti kuwa mume
wangu na ukoo wake ni wachawi wa
kutupwa, na kila mke aliyemuoa
hakukaa hata mwaka, alikufa,
wananishangaa mimi nimemaliza
miaka mitatu, na ninae mtoto
mkubwa tu wa mwaka mmoja.
Kiukweli ile habari ya wanawake kufa
iliniogopesha, ikabidi jioni ilipofika
nimuulize mume wangu, kwa kuwa
alinipenda alinieleza ukweli...
_____________________________
SEHEMU YA KUMI NA SABA.
_____________________________
Aliniambia kuwa, kila mwanamke
ambaye alimuoa, alimshauri aachane
na mambo ya mizimu, ilo suala
lilimuudhi na kuwaua kwa njia ya
kuwadhoofisha kiafya, ila mwisho wa
siku, mzimu wenyewe ukamshauri
asioe mwanamke ambae anatokea
Bukoba, ndo akaja kunioa mimi.
Akaendelea kuniambia
"tangu nimekuoa, sijaona hata siku
moja ukifatilia mambo yangu, na leo
ndio umeniuliza kwa mara ya kwanza
kuhusu mambo yangu yaliyopita
kipindi cha nyuma".
Baada ya baba
yenu kuniambia maneno haya,
niliridhika nayo kabisa na wala sikutaka kuuliza tena ingawa nilianza kuishi kwa hofu.
Baada ya miaka miwili nilifanikiwa
kuzaa mtoto wa pili, na hapo tukapanga
tusizae tena, na baba yako kwa mara
ya kwanza akaniambia kuwa
anaachana na mambo ya mizimu, mimi
nilipingana nae, ila hakunielewa.
Mimi niliendelea kupingana nae kwa sababu
nilihisi kuwa ndugu zake wanaweza
kuona mimi nilimshawishi baba yenu kuachana na mambo ya mizimu.
Baada ya
miezi sita tangu aitoe kauli ya
kuachana na mizimu, ni kweli aliacha kununua kondoo wa kuchinjwa kila mwisho wa mwezi, na pia aliwaambia ndugu zake warafute sehemu ya kufanyia ibada zao kwa kuwa yeye hakuwa tayari kuendelea na hizo ibada.
Mwanzo walikuwa wagumu kumuelewa, ila baadae walikubaliana nae ila kwa shingo upande.
Baada ya mwaka mmoja, tulianza kufilisika, gari zilipata ajali
kiutatanishi zikafa, nyingine
alidhulumiwa na ndugu zake ambao
walikuwa wanazisimamia, na hatua
ya mwisho kabisa na ambayo sikuwa
naifikiria kabisa, ni kwamba baba
yako aliamua kuuza nyumba zake
zote, hadi ile tuliyokuwa tunakaa,
kisha akatuchukua mimi na kaka
zako akatupeleka kijijini kwa mama
yake, ambaye ni bibi yako.
Huko sasa ndipo mauza uza yakaanza, Siku moja
wakati natoka kisimani kuchota maji,
nikamkuta kaka yako mkubwa,
amekufa kifo cha ajabu sana,
shingoni alikuwa na alama za meno,
kile kifo hata baba yako
kilimshangaza, tuliomboleza tukalia tukazika, mwishowe tukasahau.
Siku ya harobaini baada ya kile kifo, usiku wakati tumelala
na baba yako, tulishtushwa na
upepo mkali ulioezua paa la nyumba
tuliyokuwa tunakaa, wote tukakurupuka kitandani na kuanza kushangaa hiyo hali, wakati
tunautafakari ule upepo, kilitokea
kiumbe cha ajabu sana, wote tukabaki na mshangao ulioambatana na uoga.
Kile kiumbe hakikuonekana kujali hali tuliyonayo, kilimwambia
baba yako kuwa kinaitwa
NDIFU, ni mzimu wa ukoo, na kimekuja kutaka hifadhi, baba yako
akapata ujasiri na kumuuliza alikuwa
anataka hifadhi ya nini?, kile kiumbe
kikasema kinataka kuishi ndani ya mwili
wa mtu alie hai, baba yako
akamwambia sawa aende tu
akaishi, kile kiumbe kikakataa na
kusema anataka kuishi kwenye mwili
wa baba yako au kaka yako ambae
ndio huyo tu, tuliebaki nae, baba
yako akakataa.
Kile kiumbe kikasema,
kitu kitakachotokea asubuhi
tutakapoamka tusishangae, Kisha
upepo mkali ukakibeba na paa la
nyumba yetu likarudi kama
mwanzo, tukabaki tunashangaa huku kila mmoja akiwaza lake, ila mwisho tukajadiliana na kukubaliana tusubiri mpaka kesho ili tuone hicho kitakachotokea, tukalala.
Kesho tulipoamka ndipo
tukapata kitu kilichotupa mshtuko,
kiasi kwamba nikapoteza fahamu...
******ITAENDELEA******
the Legend☆