Riwaya: Machinga mimi Masikini

Riwaya: Machinga mimi Masikini

popote pale changamoto hazikosekani, mji huu unakumbwa na changamoto zipi?
Kuna kitu kinaitwa Continuous Improvement.... Niki-refer maneno aliyosema Rais wa Kampuni ya Toyota - Eiji Toyoda...;

If you put your mind to it, water can be wrung even from a dry towel. - Eiji Toyoda, Toyota Motor Corporation President 1967-1982

Kwahio kwenye continous improvement haisubiri changamoto bali kila wakati mnafikiria jinsi ya kuboresha na kupunguza gharama - kwenye huu mji ni jinsi ya kuboresha, kuokoa mazingira na kupunguza muda wa kufanya kazi kwa kutumia automation; na kwa kumpa fursa kila mtu kutoa changamoto zao na kuwapa watu fursa ya kutatua changamoto hizo na vyuo vilivyopo kutatua hizo changamoto mji huu unakuwa pro-active badala ya reactive; kila siku kila mtu anawaza ni vipi ataboresha na kama akipata suluhisho analiweka mezani linafanyiwa kazi na kupewa kipaumbele cha kuwa a reality.....

Utaona zaidi kwenye hatua ya Tisa: Continuous Automation and Innovation from All.
 
Bila shaka hapo ina maana siasa hazipewi kipaumbele??
Siasa ni majadiliano jinsi ya kugawana scarce resources sasa kama badala ya kutumia muda kugawana kilichopo tunatumia muda mwingi kuzalisha kinachotakiwa hata siasa itakuwa ni part time...

Kwenye hili hebu pitia hapa ingawa sijamalizia hili andiko

 
HATUA YA TISA: Utumiaji Mashine kila Inapowezekana na Ubunifu toka kwa Wote (Continuous Automation and Innovation from All)

Kama kuna jambo au changamoto ambayo huwa inafikiriwa kila siku na kila wakati katika mji wetu ni jinsi gani ya kupunguza kazi za kufanya ili kuongeza muda wa starehe na kufanya mambo mengine kama vile ubunifu na kutatua / kuboresha maisha yetu.

Kuna msemo mwingine ambao Busara alikuwa anatukumbusha kila siku..., Tunafanya kazi ili kutimiza mahitaji na sio kufanya kazi ili mradi tu umefanya kazi au kupata cha kufanya.., Kama jambo linaweza kufanywa na mashine kwanini ulifanye wewe; kuna mambo ambayo ni ya muhimu zaidi kuwekeza muda wako, kama vile kufikiri, ubunifu, starehe na kufurahia maisha, sio kuangaika kutafuta kila dakika na kusahau kufurahia hicho unachotafuta.... au kutumia muda mwingi kufanya kilekile badala ya kufikiri jinsi ya kuboresha unachofanya ili ukifanye kwa ufanisi....

Na hilo ndio tulilofanya, kila wakati tunawaza jinsi ya kufanya kazi kwa ufanisi na kupunguza kazi za kufanywa na watu ili kila mtu aweze kufanya kazi kwa masaa machache iwezekanavyo, Nakumbuka kuna siku Busara aliniambia kuhusu Japan; Kwamba mfumo wa Cradle to the Grave walikuwa wanautumia sana Japan, yaani mtu alikuwa anaangaliwa na kuhudumiwa tangia anavyozaliwa mpaka anapokufa, na pesa hizo za huduma zilikuwa zinatoka kwenye pesa inayokusanywa na serikali, mifuko ya pensheni kwa kuwahudumia wazee n.k...., sasa ukizingatia duniani hakuna cha bure lazima pesa hii itoke mahali fulani, na kwa Japan wale waliokuwa wanafanya kazi (vijana) waliweza kuwasupport wazee, sasa tatizo likaja pale ambapo wazee wanapokuwa wengi kuliko vijana wanaofanya kazi utaona kwamba mfumo kama huu sio endelevu sababu itafika wakati wanaohitaji huduma ni wengi kuliko wawezeshaji wa hio huduma, na mfumo huu uliigharimu sana Japan na hakuna sehemu ambayo inaweza ikafanikiwa kwa mfumo huu kwa muda mrefu. Lakini laiti kama wawezeshaji / uwezeshaji huu usingetemea nguvu kazi ya watu wachache bali mashine na automation basi mfumo huu ungekuwa endelevu.

Hata enzi za utumwa na ukabaila ni kwamba watu wengi walikuwa wanafanya kazi ili kuwanufaisha wachache ambao walikuwa wananyonya jasho la wengi (wachache waliishi kama wafalme wakati wengi wakiwezesha maisha ya hao wachache) na mfumo huu ungeendelea kustahimili iwapo hao wengi wangeridhika na kuona kwamba ni haki ya hao wachache kunufaika kwa jasho lao; (wafalme wamechaguliwa kuwaongoza wao na ni jambo la kujivunia kuwatumikia). Katika mji wetu tumefanikisha hayo kwa kupata watumwa ambao hawalalamiki wala hawachoki wala hawana hisia (Mashine na Automation)

Kila kazi inayoweza kufanya na mashine kwa sasa inafanywa na mashine na zile ambazo bado zinahitaji watu vyuo vyetu na watu wanafikiria kila wakati ni jinsi gani kuviwezesha vifanywe na mashine

Jambo hili limesababisha masaa ya kufanya kazi yapungue maradufu.

Nakumbuka mwanzo wakati Busara anafafanua faida ya automation ulitokea ubishi baina yake na rafiki yangu ambaye kwa bahati mbaya baada ya Benki kuanza mfumo wa mawakala na kuongeza matumizi ya computer alijikuta amepunguzwa kazi....., Alimwambia busara hizi robot kuna siku zitachukua kazi zetu zote!!! Hawa wanasayansi wanaharibu kabisa mfumo wa kidunia, mimi ni mfano halisi.., nakumbuka zamani tulikuwa tunahitaji watu lukuki kuhesabu pesa..., sasa hivi sio tu kwamba kuna money counter yaani hata pesa zenyewe hazipo ni mwendo wa kubonyeza namba na pesa imetoka point A kwenda B.

Busara alimuelewesha kama mfumo mzima utakuwa unategemeana wala hilo lisingetokea..., Mfano kama watu elfu moja walikuwa wanatakiwa kufanya kazi masaa nane kwa siku kabla ya automation na watu mia tano baada ya automation badala ya kuwapunguza kazi hao watu mia tano watu wote 1000 watabaki ila badala ya kufanya kazi masaa nane watafanya masaa manne au kwa kubadilishana shift kwa kila mia tano kufanya kazi kwa wiki....

Kwa mji wetu hayo yamewezekana sababu kwanza kabisa watu ndio kipaumbele na tumehakikisha watu hawa wanaweza kufanya kazi karibia zote katika mji na kazi zenyewe zimerahisishwa na kuwa rahisi ili wengi waweze kuzifanya kwa wepesi ili wapate muda wa kufanya mengine yenye faida zaidi kama vile kufikiria jinsi ya kuboresha... kama kazi kwenye sekta moja zikipungua zinawapa muda watu kufanya kazi kwenye sekta nyingine zinazohitaji nguvu kazi.

Mji pia unatoa motisha kwa watu kuwa wabunifu; yaani ubunifu kwa wote. Kwa kutumia teknolojia mtu yoyote ana fursa ya kuchangia mawazo ya kuboresha mji wetu. Na hili limewezekana kwa kutumia njia zifuatazo:-

A) Kama vile Amazon wanavyotumia mfumo wao wa Virtual Box, mji wetu una portal kwenye mtandao ya (Mawazo na Ushauri) ambapo kila mtu anaweza kutoa ushauri, dukuduku au mawazo ya jinsi ya kuboresha.

B) Ili kuendelea kupata mchango wa wazee na watu waliostaafu na kuwajumuisha katika utendaji wa mji wazee wanatumika kama washauri kwenye mambo tofauti na wao pia wanafursa ya kutoa mawazo yao kama wanajamii wengine.

C) Kila mwaka kuna mashindano ya Mawazo / Ideas ambapo washindi / timu iliyoshinda huwa wanazawadiwa holidays / trips za kwenda kuvinjari sehemu tofauti za dunia.

D) Kila changamoto inapotokea huwa changamoto hizo wanapewa mashule / vyou na taasisi za uchunguzi na uboreshaji na mji kuwekeza kwenye utafiti huo ili kuupatia ufumbuzi

E) Tunajua fika kwamba kuthamini na kutambuliwa ni bora zaidi hata kushinda zawadi za malipo / mali; ndio maana vitu kama Nobel Prize thamani yake ni zaidi ya pesa; Ndio maana mji wetu una kitabu cha Mawazo Bora (Ideas Book) ambacho mawazo yote bora ambayo yamefanyiwa kazi yamewekwa katika kitabu hicho yakionyesha mchakato mzima tangia wazo linazaliwa mpaka kufanyiwa kazi na wote waliohusika wameorodheshwa kama asante kwa mchango wao.
 
HATUA YA KUMI: Kuhakikisha Hakuna anayebaki Nyuma (Ensure No One is Left Behind)

Kwenye maisha kuna wale ambao kwa sababu moja ama nyingine hujikuta mambo yamewaendea kombo na maisha yamewatupa mkono; hawa ni kina sisi wazamani, mafukara, wasiojiweza na ombamba. Lengo la hatua hizi kumi lilikuwa ni kuwawezesha hawa ili waweze kurudi au kuingia ulingoni na kuwa wazalishaji.

Wengi wetu tulikuwa hatuna makazi, ombaomba, mayatima na tulionekana kama mzigo kwa taifa, lakini kwa kuhakikishiwa kwamba kuna kazi zenye ujira hata kwa wale walemavu na wasiojiweza kwa kuwapa kazi kulingana na uwezo wao; hata wasio na nguvu kuna kazi za kutumia akili zao na wale wenye maguvu, nguvu zao zinatumika kwa maslahi ya kila mmoja wetu. Na kwa kufanya hivyo ndio ilikuwa tiba ya kuodoa umasikini na unyonge wetu. Na shida ilikuwa mwanzo kwa sasa uwepo wa mashine za kutosha kazi za kufanya nazo ni chache na nyepesi.

Tuliondoa matabaka na kuhakikisha kuna usawa kwa kuwekeza kwa watu na kuhakikisha kila mtu ana fursa ya kuchangia na kupata ujira wa kuwezesha maisha yake katika mji. Hili lilisaidia sana kuondoa uhitaji wa misaada au watu kuwa ombaomba na kuhitaji hisani ya fulani ili kuweza kuishi. Tangia mwanzo tulikuwa hatupendi kuomba omba tukijua fika duniani hakuna cha bure na tukicheza tunaweza kuuza utu wetu au kuwa vibaraka (kama unavyojua huwezi kumbishia mfadhili wako); kwa kuweza kujitegemea tumeweza kutatua matatizo yetu kwa uendelevu.

Katika mji wetu Hatima ya kila mtu ipo mikononi mwake mwenyewe na hata kwa bahati mbaya ukipotea njia au kuteleza ni rahisi kurudi kwenye njia na kuendelea; kila mtoto anayezaliwa ana fursa sawa na mwingine haijalishi kama ni yatima au mzazi wake hakutimiza majukumu, ana fursa za kutengeneza kesho yake mwenyewe.

Tulijua kabisa kwamba watu ni malighafi muhimu sana na kutokuwatumia watu kwa manufaa ya jamii, kwa kutokuwawezesha baadhi au kuwapa ujuzi wachache ni kupoteza nguvu kazi kubwa ambayo ingeweza kutumika.

Ingawa tupo sehemu nzuri na tunapanga kuendelea ila ndoto yetu kubwa ni kuwa na miji kama hii yetu inayotuzunguka ili miji hii iweze kusaidiana na kufaidika wote kwa usawa bila kunyonyana au kushindana na kwa kufanya hivyo tutahakikisha yafuatayo:-
  1. Umasikini, Njaa, Ukosefu wa makazi, unyonyaji wa baadhi ya watu au sehemu unatoweka
  2. Uhakika wa Elimu na Ujuzi ili kuhakikisha watu wanapata ujira utakaohakikisha wanamudu gharama za Afya na Matumizi mengine yote bila kusahau starehe na uhakika wa mafao pindi wanapozeeka
  3. Kila mtu ni mwanajamii hakuna anayebakizwa nyuma, hii itaondoa matabaka (wao na sisi) hivyo kuondoa hatari ya watu kurubuniwa na kuzaa chuki na hasira jambo ambalo ni mazalia ya ughaidi.
  4. Kila mtu ana makazi na anuani za kudumu jambo ambalo linaleta usalama na ujirani kwa kila mwanajamii kuhakikisha wale ambao ni dhaifu mfano watoto hawanyanyaswi
  5. Mji ambao ni endelevu na unajitegemea kila nyumba ni kiwanda kidogo na kinazalisha nishati (solar panels zinavuna umeme na uchafu unatumika kama mbolea)
  6. Jamii ambayo watu wanafanya kazi kwa muda mchache iwezekanavyo kukibakiwa na kazi za kufanya ambazo hata wanafunzi au wale wanaotaka pocket money wanaweza kufanya kuongeza kipato
  7. Mabadiliko ya fikra ambapo watu hawaheshimiki sababu ya kujilimbikizia mali, bali wanaheshimiwa sababu ni nguvu kazi ya mji na wanachofanya ndio kinaboresha mji, ukizingatia kwamba hata matumizi na kukusanya / kutoa uchafu ni faida kwa jamii.
  8. Fikra ambapo kazi zote zinaonekana zina manufaa sawa, sababu kila kazi ina umuhimu katika jamii na sio kuangalia baadhi ya kazi kama jambo la mwisho mtu kulifanya iwapo hakuna kingine cha kufanya.
  9. Jamii ambayo ni salama na kuna usalama, ndani ya mji kuna uhakika wa usalama; na kuna CCTVs Kamera ambazo zinahakikisha watu dhaifu hawanyanyaswi na wazazi kutokuwa na uoga kwamba watoto wao wanaweza kupata shida yoyote.
  10. Mji ambao wakazi wanaweza kuacha milango yao wazi au kuacha mifuko, mabegi yao kwenye sehemu za wazi bila woga wa kwamba zitachukuliwa sababu ya uwepo wa CCTV
  11. Jamii ambayo kila mtu ana fursa ya kushiriki, na changamoto zinatatuliwa kwa uwazi na kwa kushauriana na yoyote yule anaweza kutuma mchango wake wakati wowote (virtual idea box)
  12. Jamii ambayo mawazo yanafanyiwa kazi kama ni mazuri na kuyafanya yawe halisi na kwa manufaa ya wote na sio kuyapatia hati miliki ili wachache ndio wanufaike nayo.
  13. Jamii kama inavyopaswa iwe, muingiliano kati ya watu na mazingira yao ambayo yana manufaa kwa watu na mazingira, kila uchafu mabaki ya kitu kimoja ni malighafi ya kitu kingine

Na haya yote ni endelevu na yanajitememea bila kuhitaji hisani wala misaada ya watu wengine, kama tutakavyoona kwenye Mahesabu (Financials)
 
"kila mtoto anayezaliwa ana fursa sawa na mwingine haijalishi kama ni yatima au mzazi wake hakutimiza majukumu, ana fursa za kutengeneza kesho yake mwenyewe".
hapa naomba ufafanuzi zaidi
 
kuwezekana kwa mambo hayo, kunatokana na uwepo mdogo wa watu ndo maana maendeleo yamepatikana si ndio!
 
"kila mtoto anayezaliwa ana fursa sawa na mwingine haijalishi kama ni yatima au mzazi wake hakutimiza majukumu, ana fursa za kutengeneza kesho yake mwenyewe".
hapa naomba ufafanuzi zaidi
Kila mtoto anayezaliwa ana fursa ya kupata elimu kulingana na uwezo wake hata kama ni kipofu mwisho wa siku atakuwa trained kuweza kufanya vitu ambavyo hata kipofu anaweza kufanya; Kama ni Mbunifu kuna fursa za kubuni, kama ana nguvu sawa na wengine atapewa fursa ya kupata ujuzi wa kazi zote zilizopo kwenye mji, hivyo mtoto katika mji anaangaliwa kama mbegu ambayo inapandwa ili istawi......, Ustawi wa mtoto utausaidia mji sababu bila kupanda hio mbegu ni hasara kwa mji...

Ingawa kila mzazi anakatwa kwenye mshahara wake wa mwezi pesa ya ada kwa watoto kama mzazi hayupo basi sio kosa la mtoto wala haitakuwa faida kwa mji kutokumsomesha huyo mtoto hivyo atasomeshwa...

Kama mzazi ni mpuuzi yaani hata hayo masaa machache hataki kufanya kazi kwahio watoto kushindwa kupata ada ya kusomeshwa huyo atakuwa muhalifu kama wahalifu wengine yaani huyo ni kama mchawi na mara nyingi unashauriwa kama huwezi / hutaki majukumu basi usipate familia / majukumu ila mtu wa hivi sababu atakuwa hawezi kumudu maisha ndani ya mji wala hawezi kuwa ombaomba sababu utamaduni wa huu mji hatutaki ombaomba kwahio utamaduni wa mji umehakikisha hakuna watu wa namna hii (wakimbia majukumu yao)
 
kuwezekana kwa mambo hayo, kunatokana na uwepo mdogo wa watu ndo maana maendeleo yamepatikana si ndio!
Kuwezekana kunatokana na hatua ya kwanza na ya Pili; The Right Infrastructure na An Optimum Transparent Community - Yaani 1) Miundombinu Sahihi 2) Idadi Sahihi ya Wakazi Wazalishaji....
Kwahio katika mji kuna idadi sahihi ya watu kulingana na kazi zilizopo; kuna kazi za kutosha kuhakikisha mahitaji yote yanapatikana; kuna watu wa kutosha kuhakikisha uchafu unaozalishwa unaweza ukatumiwa kama bidhaa / nishati ya jambo lingine.... Kuna nyumba za kutosha kutokana na wingi wa watu; kama mji ukijaa yaani watu wengi kuliko uwezo wa mji ni bora kutengeneza mji mwingine ambao utakuwa optimum;....... Nikinukuu maneno ya busara....

Nakumbuka maneno ya Busara, aliwahi kuniambia kuwa na makazi ya watu bila watu hao kuwa na kipato ni kutengeneza jamii ya waharifu (ghettos), na kuwa na kazi bila makazi ni kutengeneza makazi duni (slums)

Niliwahi kumuuliza…, hivi kweli tunaweza kuwakatalia watu kuhamia kwenye mji wetu, si tutakuwa hatuwetendei haki? Busara aliniambia kama mji mmoja ukijaa unaweza kutengeneza mji mwingine sehemu nyingine…, hakuna maana kuwa na watu ambao hawana uhakika wa kipato cha kuwawezesha kuishi katika sehemu husika, kufanya hivyo ni mwanzo wa kupoteza ufanisi, muda si muda utashangaa jamii nzima inakuwa ya wabangaizaji kwa kugombania kidogo kilichopo badala ya kupeana fursa ya kutengeneza zaidi ili kila mtu anufaike. Kama unakumbuka kitu muhimu kuliko vyote katika jamii ni watu, na kuwarundika watu sehemu moja badala ya kuwapa fursa ya kuzalisha ni kupoteza nguvu kazi. Hakuna sababu ya kuwa na wakazi ambao hawana kipato au watu wenye kipato ambao hawana makazi.

Kumbuka kijana ili huu mji ufanikiwe ufanisi ni wa muhimu sana na jamii yenye idadi sahihi ni kiungo muhimu sana katika ufanisi…, aliendelea Busara, ili kufanikiwa kunahitajika kuwe na mabaki / uchafu wa kutosha ili kutengeneza gesi asilia, lazima kuwe na watu wa kutosha kuzalisha na kufanikisha mahitaji ya watumiaji na pia ufanikishaji huo uhakikishe unatoa kipato kwa wazalishaji ambao ni wakazi.
 
The Financials ; Mahesabu:
Baada ya mji wetu kujenga miundombinu ambayo mpaka sasa mikopo mingi tumeshalipa mji wetu ni endelevu na unajiendisha ingawa mji wetu una wakazi elfu Hamsini mji ungeweza kuwa na watu hata laki 5 ni kwamba miundombinu ingejengwa kulingana na wakazi husika.

Katika watu elfu 50, mji wetu una wazazi kama elfu 20 ambao wanafanya kazi na kulipwa pesa 500USD, (tunaweza kuziita units lakini kwa kufanya andiko hili lieleweke vizuri tutaziita Dollars) ; Hii inagharimu mji 10M USD kama malipo ya wakazi, tukichukulia familia nyingi zina wastani wa watu wanne Mama; baba na Watoto wawili pato la familia ni kama 1000USD kwa mwezi.

Elimu: Kila Mzazi analipia watoto wake elimu 100USD kwa mwezi (Yatima wanasomeshwa bure) kwahio (watoto 20,000 x 100USD) inamaanisha 2M USD zinakwenda kwenye Elimu kila Mwezi.

Chakula; Kila mtu ana uhakika wa kupata chakula bora (milo mitatu kwa siku) kutoka kwenye migahawa minigi iliyopo katika mji, ambapo wazee wanapata chakula bure, kila mtu analipa 80USD kwa ajili ya Chakula Bora (Milo Mitatu kwa Siku); kwahio mji wa watu elfu Hamsini ukiondoa wazee elfu 10 unakusanya (40,000 x 80USD) 3.2M USD kwa ajili ya kuhakikisha kila mtu anatapa variety ya chakula bora.

Afya: Huduma za afya zinapatikana kwa kila raia na mji wetu unajikita zaidi kwenye kinga kuliko kuponya; kwahio tumejikita zaidi kwenye uchunguzi wa Tiba asilia na elimu ya afya kwa watu wote; na sababu tunajua wazee ni sehemu ya jamii yetu na ni hatima ya kila mmoja wetu watu wa uangalizi (social care) ni muhimu sana na hii ni moja ya ajira za kudumu ambazo tunajua hata tukifanya automation kiasi gani bado itahitajika. Ili kugharamia afya ukiondoa wazee kila mtu anatoa 20USD kwa mwezi kwahio (watu 40,000 x 20USD) mji unakusanya 800,000USD kwa ajili ya Afya kwa wote kila mwezi.

Marekebisho / Ukarabati; ili kufanya watu waweze kuishi vizuri ndani ya mji na katika mji safi na unaopendeza kuna kazi katika kapu la kazi za ukarabati, usafi na recycling; kwa kufanikisha hili kila nyumba inatoa 10USD kwa mwezi (nyumba 10,000 x 10USD) jumla ya 100,000USD zinakusanywa kila mwezi kwa ajili ya Usafi.

Usafiri: Kuna usafiri wenye ufanisi ndani ya mji na wa kwenda kwenye sehemu za kazi (eco - industrial parks) usafiri huu mbali na kuwa fanisi ni rafiki kwa mazingira. Na kutokana kwamba usafiri huu ni wa kutumia nishati ya umeme na sio mafuta kwahio uendeshaji wake ni wa gharama nafuu ukizingatia gari la mafuta lina sehemu nyingi za injini tofauti na umeme kwahio service yake ni gharama nafuu. Kwa wale wanaotaka kwenda nje ya mji wanaweza wakakodisha magari kutoka mradi wa kukodisha wa mji. Ili kufanikisha usafiri na usafirishaji kila mtu ukiondoa wazee anapewa ticket ya kusafiri bila kikomo ndani ya mji na kwenda kwenye sehemu za kazi, ticket hiyo itamgharimu kila mkazi ukiondoa wazee 10USD (kwahio mji utakusanya watu 40,000 x 10USD jumla ya 400,000 USD kwa mwezi kuhudumia usafiri (kumbuka hapo nishati inakusanywa bure kwahio gharama ya uendeshaji ni ndogo sana)

Makazi; Pamoja na uhakika wa ujira kila mkazi kila mtu ana uhakika wa Makazi; Makazi bora ya gharama rafiki ambayo mkazi analipia kwa muda mrefu bila riba. Wamiliki hawa wa nyumba wanalipa 100USD kila mwezi ili kutunisha mfuko wa nyumba. Pia nyumba hizi zinaweza kutumiwa kama mafao ya uzeeni mara nyingi wazazi hawa wakizeeka wanauza nyumba kwa Jiji na kuhamia kwenye nyumba za wazee ambapo kuna msaada na uangalizi mzuri zaidi. Kwahio ada ya Makazi kutoka kwenye nyumba elfu 10 Mji unakusanya (nyumba 10,000 x 100USD) jumla 1M USD kila mwezi.

Mafao ya Uzeeni; Kwa kusaidia watu wakistaafu wapate mafao ya uzeeni ingawa huduma nyingi ni bure kwa wazee kila mtu katika maisha yake ya ufanyaji kazi anachangia 20USD kwa mwezi kwa ajili ya mfuko wa Mafao; Hivyo mji unakusanya kutoka kwa wazazi 20,000 x 20USD jumla ya 400,000USD kwa ajili ya mfuko wa mafao ya uzeeni.

Kwahio kwa ufupi; Mji utatumia 10M USD kwa ajili ya mishahara kila mwezi; na ukiondoa pesa ambazo mji utazipata katika mauzo ya starehe, na bidhaa nyinginezo ambazo watu watanunua kutoka kwenye pesa yao inayobaki baada ya matumizi mji utakusanya 2M kutoka kwenye Elimu; 3.2M kutoka kwenye Chakula kwa wote; 800,000 USD kwa ajili ya Afya; 100,000 USD kwa ukarabati wa mji. 400,000 USD kwa usafiri na usafirishaji; 1,000,000USD kwa ajili ya Makazi na 400,000 USD kwa ajili ya mafao ya Uzeeni; kwahio mji utakusanya 7.9M moja kwa moja na pesa nyinginezo kutoka kwenye Starehe na manunuzi mengine.

Tukiangalia kwa upande wa mtumiaji yaani Kaya; familia ya watu wanne yenye mama na baba ambao wanafanya kazi kwenye mshahara wao wa 1000USD kwa mwezi baada ya kila mmoja wao kufanya kazi kwa muda mchache iwezekanavyo; matumizi yatakuwa kama yafuatavyo:-
  • 200 USD kwa elimu ya watoto wao wawili (Baki 800USD)
  • 320 USD kwa chakula bora kwa mwezi mzima - watu wanne (Baki 480USD)
  • 80 USD kwa ajili ya Afya (20USD x watu wanne) (Baki 400USD)
  • 40 USD kwa ajili ya Usafiri (watu wanne) (Baki 360)
  • 20 USD mafao ya Uzeeni (watu wawili) (Baki 320)
  • 10 USD kwa ajili ya Usafi (Baki 310)
  • 100 USD kwa ajili ya Makazi (Baki 210)
Kwahio hawa wazazi wawili watakuwa na angalau 105 USD kila mwezi kwa kila mmoja kuweza kutumia anavyotaka kwa matumizi mengine ukizingatia matumizi muhimu mengine yote yametekelezwa.

Nakumbuka wakati tunapiga mahesabu haya wakati bado tunaishi kwenye mabanda yetu katika kijiji kabla hakijawa mji; Nilimuuliza Busara..., Vipi kuhusu watu ambao hawapo kwenye Mpango wa Mji na wanataka kutembelea huu mji, ni nini kitakachowazuia kufisadi bei nafuu za vitu vinavyouzwa ndani ya mji au kununua vitu ndani ya mji kwa bei nafuu na kuviuza pengine ? Najua kwenye nyumba tuna sheria ya kulinda kwamba mmiliki anaweza kuuza wakati wowote ila kuuza kwake atauzia mji kwa bei ya gharama za wakati huo hii itazuia watu kununua nyumba nyingi ili kupangisha wengine..., lakini ni kipi cha kuzuia watu kununua bidhaa nyingine na kuzifanyia magendo ?

Rafiki yangu akadakia huenda Busara anataka kuanzisha pesa yake mwenyewe yaani pesa ya mji tofauti na pesa nyingine......

Busara alijibu haraka hapana kutengeneza pesa yenu wenyewe ni kinyume cha sheria na kwa kufanya hivyo tunaweza kujikuta mikononi mwa sheria..., Kumbuka hizi Pesa nimesema tu pesa ili kuweza kueleweka zaidi tunaweza kuziita units / tokens au hata credits... kumbuka mji utakuwa cashless na bidhaa, manunuzi mshahara na kila kitu kitakuwa kinafanyika electronically kwa kutumia mfumo wa Block Chain..., Fulani akilipwa mshahara na akinunua kitu inaonekana kabisa kwamba unit hii imetoka hapa imekwenda pale na ikirudi tena kwenye mji hapo tutakuwa tumetengeneza utajiri (creating wealthy from productivity) tofauti na mifumo ya sasa ambapo pesa / wealthy inatengenezwa kutoka hewani na mabenki yanavyotoa mikopo....

Na kwa kujibu swali la rafiki yangu kuhusu watu wa nje ambao watataka kununua bidhaa au kufurahia maisha tutawapokea kwa mikono miwili na kwa ukarimu na kuwahudumia....

Eeehh ?!!! Nilijikuta nauliza kwa mshangao, kivipi ?

Busara aliendelea kama nilivyoshaelezea miamala yote ndani ya mji itakuwa ni ya ki-elektroniki kwa kutumia mfumo wa block chain; na kama nilivyosema kuwa na mfumo wa cashless utafanya miamala kuwa rahisi. Kwahio kila mgeni anayeingia kwenye mji atabadilisha pesa zake kwa kununua tokens / credits za kwenye mji ili aweze kufanya manunuzi ndani ya mji.

Anabadilisha kwa Exchange Rate...., Kiwango gani cha pesa ? niliendelea kudadisi....

Swali zuri sana...., kama ulivyoshagundua bidhaa ndani ya mji zitakuwa na gharama nafuu sana zenye faida ndogo sana na bidhaa ambazo hazitengenezwi ndani ya mji zitanunuliwa kwa wingi na kwa bei za jumla kwa ajili ya matumizi ya mji...., hivyo basi kwa mji kuhakikisha inapata fedha ya kuweza kununua bidhaa ambazo haitengenezi ndani ya mji na pia kuzuia watu kutumia mianya ya bei nafuu kujinufaisha..., mambo mawili makuu yatafanyika;

Moja:
Kubadilisha pesa kutoka currency / pesa moja kwenda kwenye tokens / credits za mji itazingatia bidhaa ambazo mji unatakiwa kununua kwa wakati huo kutokana na mahitaji yake na ni kiasi gani pesa hio inaweza kununua bidhaa hio...., mfano kama tuna uhaba wa mchele na kubadilisha pesa kukazingatia kilo moja ya mchele, na tuseme kwa wakati huo kilo moja ya mchele ni 1USD; mji unaweza kuamua kilo kumi za mchele ni sawa na Credit/Token Moja ya Mji yaani sawa na 10USD. Kwahio kwa kipindi hiki mtu mwenye US Dollars atapewa City Credit 1 akitoa 10USD. Na hii inatafanyika kwa watu ambao hawapo kwenye program ila kwenye miji ambayo inashirikiana na ipo kwenye mpango huu wataweza kutumia credit za miji yao bila haja ya kubadilisha.

Nilijikuta nasema..., kinadharia inapendeza lakini utendaji wake na mafanikio yake bado yananitia shaka..., enhee nini jambo la pili;

Mbili:
Utakuwa umeshagundua kwamba kwa watu waliopo kwenye huu mfumo bei ya bidhaa ni nafuu sana na mfumo huu umehakikisha unapata faida finyu sana ili kuhakikisha watu wake wanabudu bei na kubakiwa na pesa ya kufanya mambo mengine...., Hivyo basi vitu kama Afya, vyakula vya ziada, vinywaji na vilevi n.k. vitakuwa na bei ya juu kidogo kwa watu ambao hawapo kwenye mfumo na wamepata credit zao kutokana na kubadilisha pesa zao..

Nakumbuka yule jamaa mtata aliyekuwa amechoshwa na maisha yetu ya kijijini kipindi kile aliuliza kwa dhiaka..., Ngoja kidogo Mzee...., tuseme kwamba mimi ni kinyozi....

Kwa usahihi zaidi tuseme wewe ni mkazi wa mji mwenye ujuzi wa kunyoa....

Sawa..., tuseme ujuzi wangu ni wa kiwango cha juu duniani hakuna mwingine na naweza kwa kichwa kimoja kulipwa dollar 10..., hii inamaanisha nikiwahudumia watu 10 kwa siku naweza kupata 1500USD ambayo ni mara tatu ambacho takipata kwenye mji wenu...., kwanini nibakie kwenye mji wenu badala ya kujiajiri kwa kuwa na banda langu la kunyoa.

Busara alimuangalia kwa muda wa kama dakika tano...., nikaanza kuwaza huenda leo Busara ameshikika, Naam kwanini usiwe na duka lako mwenyewe..., Ni kweli ni bora na faida zaidi ufanye hivyo, na sisi kama mji kama tunaweza kuiga ujuzi wako tutafanya hivyo na kufundisha wengine ili waendelee kufanya ulichokuwa unafanya wewe...

Jamaa alitoa kicheko na kutoa tabasamu la kejeli...., kwahio pamoja na kufanya yoote uliyofanya mwisho wa siku mnaweza mkajikuta wajuzi, wabunifu na watu wenye vipaji wanaondoka kwenye mji wenu...

Polepole kijana, aliendelea Busara...., nimekubaliana na wewe kwamba unaweza ukatengeneza banda lako mwenyewe lakini nina uhakika hauwezi kupata manufaa sawa na manufaa ambayo ungeyapata kama ungebakia kwenye mji, kwa pesa ya ziada ambayo utaipata.

Kwanini ?!! jamaa aliuliza....

Kwanza kabisa kuwa na miundombinu ya kisasa kwenye jengo la kisasa na la kifahari na wahudumu wanaojali na kupenda kazi yao utahitaji uwekezaji mkubwa sana jambo ambalo litapunguza faida yako.., bila kusahau gharama ya pango.... Pia kumbuka hii ni package (kifurushi) ambacho pesa ni sehemu ndogo sana ya mpango mzima; Kwahio unaweza ukawa na dollar zako 1500 bila nyumba, mafao ya uzeeni, mpango wa afya, elimu kwa watoto wako, uhakika wa chakula bora, uhakika wa usafiri n.k.

Jamaa alicheka kwa kebehi..., kwani siwezi kuvipata hivyo sehemu nyingine ?

Busara aliendelea kwa upole..., ni kweli unaweza, lakini nina uhakika huwezi kupata ubora unaopatikana kwenye mfumo na kwa gharama sawa ya mfumo..., bila kusahau kutokuwa na msongo wa mawazo kwa kufahamu fika kwamba maisha yako yote yana uhakika tangia siku unazaliwa mpaka siku unapoaga dunia, na wapendwa wako wote utakaowaacha watakuwa kwenye mikono salama. Vilevile utakuwa umeondokana na sintofahamu ya kutokujua lini wateja watakuja au utaendelea kuwa kinyozi bora mpaka lini au ushindani utakuondoa pindi akija mtu bora kuliko wewe....

Nina uhakika atakuwa hana anasa ya kufanya kazi kwa masaa machache iwezekanavyo...., niliongezea...

Kweli kabisa, alisema Busara mwisho wa siku anaweza kujikuta anafanyia kazi pesa badala ya pesa kufanya kazi kwa ajili yake... (anakuwa mtumwa wa pesa)

Nakumbuka tulipotoka..., nikiona tulipofika kweli ni makubwa yamefanyika, na haya yaliweza kufanikiwa kwa kutumia nguvu na kuwa na Dira, yaliweza kufanikiwa sababu wote waliofanikisha mafanikio hayo walikuwa na kiu, walikuwa na uduni waliotaka kuondokana nao na mafanikio hayo yalifanyika kwa juhudi zao wenyewe...

Kwa mfano mimi nisingekuwa mbangaizaji na nina shughuli zangu za kufanya mtu angekuja na kuniambia niachane na kidogo nilichonacho ili niende kutafuta kingi ambacho hakina uhakika...., kwa hakika nisingemsikiliza na ningempuuza, lakini sababu maisha yangu na waliotuzunguka yalikuwa duni na tulikuwa hatuna pa kukimbilia pindi tukatapo tamaa tulihakikisha tunafuata hatua kwa hatua kuelekea kwenye kesho yetu tuliyoitamani.

Kweli Maisha Matamu Sana Haya.....
MWISHO
 
wazo zuri kabisa!
japo nina swali vp kuhusu serikali husika mfano kodi au kuzuia dola husika kuingilia mamlaka hii(jumuiya hii BORA) ?
 
wazo zuri kabisa!
japo nina swali vp kuhusu serikali husika mfano kodi au kuzuia dola husika kuingilia mamlaka hii(jumuiya hii BORA) ?
Watu ndio wana nguvu watu ndio wanaiweka serikali madarakani; Kodi ni mkataba baina ya watu na serikali yao ili waweze kuletewa huduma... Kwenye hili andiko imetumika bottom up approach; badala ya kusubiri serikali iwafanyie kazi hawa watu wameamua kujifanyia wenyewe (yaani masikini wenyewe wameamua kujikomboa) Kuhusu kodi labda kwamba serikali inawalinda n.k. wanaweza wakaendelea kutoa; ila sababu ni wao ndio wanawachagua hao wanaodai kodi itabidi waeleze hio Kodi wanayowapa inawafanyia nini iwapo Chakula, Malazi, Mavazi na Huduma karibia zote wanajifanyie wenyewe...

Kodi ndio watachukua ila itabidi waeleze hio kodi wanachukua ili waifanyie nini na ni kiasi gani wanachukua na kama ni value for money..., Ingawa kwa macho yangu inabidi wafurahi kazi yao kuwa rahisi zaidi sababu wale ambao kwa sasa wanaonekana kama mzigo wa taifa (omba omba na wachafuzi wasiolipa kodi) wamegeuka kuwa Nguvu Kazi yenye kujihudumia na kuzalishia taifa pamoja na kuwa watumiaji....

Ndio maana hapo mwisho nimeweka angalizo badala ya kuwa na fedha yao wenyewe wanaweza wakawa na voucher / token ambayo mtu yoyote anaweza akanunua bidhaa za ndani ya mji lakini inabidi abadilishe pesa zake za madafu apewe token
 
...
MWISHO
Ebhana nzuri, shukrani sana kumbe huku ndipo kuna the greatest story of change written in JF.

Zaidi nimependa ulivyoitafsiri pesa na jinsi inavyotengenezwa kweli. Pesa ni kama cheti kinachosema nimechangia jamii thamani x (credit) hivyo nastahili wanajamii kunitendea thamani x. Asante.

Na kikubwa umeitatua kanuni (code) ya msingi kwamba tunachohitaji wote ni kuwa sehemu ya thamani ya jamii. We are social animals after all.

Hii ingepewa tuzo kama story of change hall of fame....... au zaidi watu wa dira ya taifa, sijui tume za uchumi wakukodi wakulipe na wakupe ulinzi. Kazi ya jamii hii inastahili kulipwa na jamii ambayo ni serikali. Na serikali ndo sisi. Kazi nzuri.

👊👏👏👏👏👏👏👏👊
 
Ebhana nzuri, shukrani sana kumbe huku ndipo kuna the greatest story of change written in JF.

Zaidi nimependa ulivyoitafsiri pesa na jinsi inavyotengenezwa kweli. Pesa ni kama cheti kinachosema nimechangia jamii thamani x (credit) hivyo nastahili wanajamii kunitendea thamani x. Asante.

Na kikubwa umeitatua kanuni (code) ya msingi kwamba tunachohitaji wote ni kuwa sehemu ya thamani ya jamii. We are social animals after all.

Hii ingepewa tuzo kama story of change hall of fame....... au zaidi watu wa dira ya taifa, sijui tume za uchumi wakukodi wakulipe na wakupe ulinzi. Kazi ya jamii hii inastahili kulipwa na jamii ambayo ni serikali. Na serikali ndo sisi. Kazi nzuri.

👊👏👏👏👏👏👏👏👊
......na haya yaliweza kufanikiwa kwa kutumia nguvu na kuwa na Dira, yaliweza kufanikiwa sababu wote waliofanikisha mafanikio hayo walikuwa na kiu, walikuwa na uduni waliotaka kuondokana nao na mafanikio hayo yalifanyika kwa juhudi zao wenyewe...

Kwa mfano mimi nisingekuwa mbangaizaji na nina shughuli zangu za kufanya mtu angekuja na kuniambia niachane na kidogo nilichonacho ili niende kutafuta kingi ambacho hakina uhakika...., kwa hakika nisingemsikiliza na ningempuuza, lakini sababu maisha yangu na waliotuzunguka yalikuwa duni na tulikuwa hatuna pa kukimbilia pindi tukatapo tamaa tulihakikisha tunafuata hatua kwa hatua kuelekea kwenye kesho yetu tuliyoitamani.

Conclusively utaona kwamba watunga sera wengi au watu wengi wanaonufaika na status quo ni vigumu kuwa initiators wa kitu tofauti..., kwa macho yao everything is okay or what we have is the best that can be...
 
Back
Top Bottom