Riwaya: Msako wa Hayawani

Riwaya: Msako wa Hayawani

Duh!mleta uzi kafariki?kifupi hadithi imefika mwisho baada ya kufika kembo alimwambia kassim wageni wako hawa na kassim akawauliza shida yao ndipo denny akamuuliza kama anamjua asha rajabu?kassim akasema hamkumbuki ndipo denny akamkumbusha kisa cha miaka 25 ilopita akamwambia ulimpa mimba.Kassim akajibu lakini nilimsaidia denny akajibu kwa kumchoma visu na kimoja kilinipata hapa akararua shati lake kufumba na kufumbua yule bepari akachomoa bastola na kurusha risasi denny akafanya kembo kama kinga na risasi zikampata kembo na kumrusha.
Dakika hiyo hiyo kassim akaruka kimanga na kukimbilia nje denny akamfuata na kukuta kaliwasha benz denny nae akawasha Bentley na kuanza kufukuzana betty akalia ili asubiriwe haikuwepo nafasi hiyo,watu wakaweka pembeni magari yao ilikuwa kama mashindano kwani madereva wote wawili walikuwa hodari yaani ikawa kama mashindano ya mjerumani na mmarekani mpaka wakafika katika mlima hatari wa kata hewa uliosifika kwa kona nyingi na madaraja membamba.

Kwa hiyo?
 
Kirchhoff unavyo comment kwa hiyo nimeshindwa kukuelewa hebu weka wazi kwa hiyo ina maana gani?
 
Hapana ndugu yangu kinachonisikitisha ni kuwa hadithi imefikia mwisho hata kurasa moja haiishi na watu wanataka kujua khatma yake na mleta uzi haonekani,na kwa kuwa kitabu nilikisoma nikajaribu kukumbuka ilivyoisha so unaposema kimajungu sidhani kama upo sahihi.
 
Ok lengo langu ni hili baada ya kufukuzana wakafika katika daraja jembamba benz likiwa mbele na daraja haliruhusu magari mwili kupita denny akakanyaga mafuta mpaka mwisho na pua ya Bentley ikaanza kuingia darajani na kulisukuma benz likaporomoka kwenye korongo na kuwaka moto kassim akatoka akipiga yowe akiwa ameungua na ndio kilikuwa kifo chake.Ndio mwisho wa hadithi huo sina mbwembwe za kueleza sababu sina kitabu hapa na hayawani akawa amekufa kwelikweli.So kama nitakuwa nimefanya kosa kiungwana mnisamehe ila hadithi iliishia hapooo.
 
Umefanya vema umekata kiu ya wengi. Sasa tunadhani hata yule wa tutarudi na roho zetu anaweza awe kavuta ka vipi tutafutie
 
Pamoja wadau kitabu hicho ninacho but kipo mbali na sehemu nilipo so nilikuwa naumia kuona jinsi watu walivyo na hamu kisha mleta uzi haonekani.Wacha tuendelee na mchakato kama kuna mtu ataenda kwangu nitamuagiza poleni ndugu zangu.
 
na vip kuhusu kule hosptal kwa yule mzee baba ake denis maana iliishia pale anapotakwa kuchomwa sindano ya sumu
 
Duh!mleta uzi kafariki?kifupi hadithi imefika mwisho baada ya kufika kembo alimwambia kassim wageni wako hawa na kassim akawauliza shida yao ndipo denny akamuuliza kama anamjua asha rajabu?kassim akasema hamkumbuki ndipo denny akamkumbusha kisa cha miaka 25 ilopita akamwambia ulimpa mimba.Kassim akajibu lakini nilimsaidia denny akajibu kwa kumchoma visu na kimoja kilinipata hapa akararua shati lake kufumba na kufumbua yule bepari akachomoa bastola na kurusha risasi denny akafanya kembo kama kinga na risasi zikampata kembo na kumrusha.
Dakika hiyo hiyo kassim akaruka kimanga na kukimbilia nje denny akamfuata na kukuta kaliwasha benz denny nae akawasha Bentley na kuanza kufukuzana betty akalia ili asubiriwe haikuwepo nafasi hiyo,watu wakaweka pembeni magari yao ilikuwa kama mashindano kwani madereva wote wawili walikuwa hodari yaani ikawa kama mashindano ya mjerumani na mmarekani mpaka wakafika katika mlima hatari wa kata hewa uliosifika kwa kona nyingi na madaraja membamba.

Walivyofika darajani magari yote yakapinduka wakafa wote.

............THE END......
 
Hapana ndugu yangu kinachonisikitisha ni kuwa hadithi imefikia mwisho hata kurasa moja haiishi na watu wanataka kujua khatma yake na mleta uzi haonekani,na kwa kuwa kitabu nilikisoma nikajaribu kukumbuka ilivyoisha so unaposema kimajungu sidhani kama upo sahihi.

Mkuu achana nae,ila kiukweli hivyo ndivyo hadithi ilivoishia. Kassim Hashir alipata ajali akafa
 
Big black nigga hawakueleza kuhusu mzee makete na mambo ya hospital mchezo iliishia darajani betty alipokuja anakuta kassim hashir anaungua akasema safari hii atazikwa yeye kiukweli kisha denny akamwambia alivyo muuliza fensi kuhusu kassim hashir akamjibu go to hell hapo ndo mwisho.
 
nawashukuru wote kwa kuimaliza simulizi hii japo kiubishi ubishi tumemaliza hatuhitaji tena kuamshiwa hamu.
 
Niliwahi siti ya daladala na kujitenga dirishani, nikawa natazama mlangoni jinsi abiria wenzangu wanavyobanana mlangoni, kila mmoja akitaka aingie ndani ya gari kabla ya mwingine. Hii shida ya usafiri tabu sana, Rais ajaye na Serikali yake lazima wafanye kitu.

Mara katika purukushani za mlangoni, nilimuona Yahaya wa Lady Jaydee anapenya na kufanikiwa kuingia ndani. Nikiwa namtazama Yahaya na ‘usmati’ wake alivyoingia kwenye daladala, akanipa bonge la mshangao baada ya kuja kukaa kwenye siti pembeni yangu.

Nikajua Yahaya lazima atanikomalia nimlipie nauli, ikabidi nijifanye sijamuona, nikawa siangalii tena ndani ya gari, macho yote niliyaelekeza nje.

Kwani nilifanikiwa basi? Nilishtushwa na kelele za Yahaya: “Ooh Maloto!” Tayari amenishtukia, nilipogeuka kumtazama, akaniambia, “Good to see you.”

Ni kawaida ya Yahaya kuongea Kiingereza kama silaha yake ya kujionesha ni mtu fulani hivi! Baada ya salamu tu akaniambia: “Leo nimeamua kupanda daladala kwa sababu nataka kujifunza hali ya maisha ya Mtanzania wa kawaida. Kosa kubwa ambalo sisi wenye pesa huwa tunalifanya ni kuacha kuishi maisha ya watu wa kawaida.”

Akaendelea: “Halafu leo nimetoa ofa ya magari kwa kila mtu nyumbani kwangu. Magari yangu yote 21 yamechukuliwa, mimi nimekosa. Kila memba wa familia yangu nimempa gari na milioni 10 za kutumia. Hiyo ni ofa ya siku nzima leo.

“Huwezi kuamini, houseboy wangu leo anaendesha lile Hammer langu, housegirl anajiachia na Range Rover Sports . Lile Bugatti kama la Mayweather analo mkata majani ya ng’ombe. Lazima kuwajali watu unaoishi nao. Nimegawa magari mpaka mimi mwenyewe nimekosa. Ndiyo maana nimepanda daladala. Ila nimewaambia wasiniharibie magari yangu, usiku nikirudi nyumbani niyakute salama.”

Yahya kwa ‘fiksi’ hawezekaniki, mimi nimeshamzoea na hanisumbui kichwa, tatizo kwenye daladala alikuwa anazungumza kwa sauti, watu wanatutazama.

Nilikuwa najishtukia watu watahisi mimi na Yahaya letu moja. Si wanamuona ni rafiki yangu? Wanasema nitajie rafiki yako nikwambia wewe ni nani!

Akaanzisha mada nyingine. “Unajua leo nilirejea nyumbani alfajiri. Usiku mzima nilikuwa kwenye kikao cha usuluhishi. Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe alinibembeleza sana nikamsuluhishe na Katibu Mkuu wake Dk. Willibroad Slaa.”

Hapo nikashindwa kuvumilia, nilimjia juu: “Wewe Yahaya ni muongo sana, ndiyo maana Lady Jaydee alikuimba. Mbowe aache watu wenye heshima zao akufuate wewe ndiye umsuluhishe na Slaa. Usiniletee hizo zako za kuleta.”

Akatoa kicheko cha dharau na kusema: “Wewe unanichukulia poa kwa sababu nimekupa nafasi ya kunisogelea, na labda ni kwa vile tumepanda wote daladala. Ndiyo maana matajiri wenzangu huwa hawapendi kushirikiana na watu wa chini kwa kukwepa dharau kama hizi."

Yahaya akaendelea kunidanganya: “Kikao kilifanyika nyumbani kwa Dk. Slaa. Ila Slaa mkoloni sana, aliponiona nimepaki gari langu Aston Martin db9 nyumbani kwake, wakati anatupokea aliniuliza napata wapi pesa kwa sababu magari yangu yote ni ya kifahari sana. Huko nyuma iliwahi kunigombeza sana aliponiona naendesha Lamborghini.

“Mke wa Dk. Slaa, mama yetu Josephine Mushumbusi alipotuona mimi na Mbowe, bila hata kutusalimia, aliingia ndani mbio, akaweka muziki wa Ali Kiba, Mapenzi Yanarun Dunia, kikasikika kipande… unatema bigijii kwa karanga za kuonjeshwa.

“Hicho kipande kikawa kinajirudiarudia… unatema bigijii kwa karanga za kuonjeshwa.”

Yahaya sasa kwenye daladala alikuwa anasikika peke yake, akaendelea: “Sauti ya muziki ilikuwa kubwa. Mimi nikawa sijashtukia, kumbe Mbowe ameona hilo ni dongo lake, akamwambia Slaa amweleze mkewe aache mipasho, nani katema bigijii kwa karanga za kuonjeshwa?”

Yahaya akazidi kutawala mazungumzo kwenye daladala: “Tulikwenda mpaka sebuleni. Muda huo muziki ulikuwa umezimwa, nafikiri Dk. Slaa aliagiza uzimwe. Tukiwa tumekaa, Josephine alisogea na kukaa jirani. Mara akaimba… unatema bigijii kwa karanga za kuonjeshwa! Mbowe akajibu, sijaja hapa kupigwa vijembe. Nimekuja kukushawishi urejee kwenye Chama, tumempokea Edward Lowassa ili iwe rahisi kuiangusha CCM.

“Josephine akaingilia kati, akamuuliza Mbowe, kwa hiyo ukisikia baridi kali ndiyo unachoma moto nyumba yako ili upate joto? Mbowe akajibu, mama unapaswa kuelewa ujio wa Lowassa CHADEMA na UKAWA ni mpango wa Mungu. Dk. Slaa akaja juu, unasema nini wewe Freeman? Huo hauwezi kuwa mpango wa Mungu, labda mpango wa Ibilisi.”

Hapo ikabidi niwe mkali, nikamsemea mbovu Yahaya: “Unajua humu kwenye gari wapo watu wenye heshima zao, na wanaweza kuamini uongo wako. Jamani huyu mtu ni muongo, haya anayoyasema yote ni uongo. Hana ujanja wa kuwa karibu na Mbowe wala Slaa. Huyu ndiye Yahaya aliyeimbwa na Lady Jaydee.”

Nilizungumza vile kwa msisitizo ili watu wapuuze maneno yake, vilevile waone sifungamani naye. Pamoja na ‘kumchana’ mbele za watu, wala Yahaya hakubabaika, akasema kwa mapozi: “Mimi ni mtu mkubwa, najulikana na ndiyo maana Mbowe aliona mimi ndiye nafaa kumsuluhisha na Slaa.”

Yahaya akaniuliza: “Hivi wewe mbishi unajua maana ya Coup d'etat?” Nikamjibu: “Ni kundi dogo la watu kupindua Serikali au Utawala, mara nyingi kikundi hicho husingizia kuungwa mkono na wengi.”

Nilipojibu hivyo, Yahaya akasema, “Umejibu vizuri kuliko nilivyotaka, wewe una akili. Kwa taarifa yako Dk. Slaa amepigwa Coup d'etat ndani ya CHADEMA.”

Unajua sipendi kudanganywa na pale nilikuwa naumia sana. Haraka haraka nilimwambia Yahaya, “Dk. Slaa hajapinduliwa CHADEMA na Mbowe amesema nafasi yake ya Ukatibu Mkuu bado ipo, akitoka mapumziko atarejea kukalia kiti chake.”

Yahaya akacheka: “Teh teh teh! Halafu na wewe Maloto unajiita Mwandishi wa Habari, hata kuchanganua mambo huwezi. Slaa amepinduliwa nafasi ya kugombea Urais CHADEMA na UKAWA. Akina Lowassa walimteka Mbowe kisha wakajitwalia nafasi ya kugombea Urais."

Nilimtazama Yahaya kwa jicho la kutaka afafanue. Abiria wote ndani ya daladala walikuwa kimya, Yahaya alitawala Baraza: “Tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu 2010, Slaa alihakikishiwa atagombea Urais 2015 ndani ya CHADEMA. Na baada ya UKAWA kukubaliana, jina la Dk. Slaa ndilo lilikuwa kipaumbele. Yaani alikuwa anasubiri kutangazwa tu na alishahakikishiwa kila kitu, ghafla akashtukia Lowassa ndiye mgombea.

“Wewe si unakumbuka CHADEMA walikataa matokeo mwaka 2010? Wakamtangaza Dk. Slaa kuwa ndiye Rais wa mioyo ya Watanzania, kwamba Rais Jakaya Kikwete alishinda kwa bao la mkono. Dk. Slaa alivimba kichwa na kuamini kuwa 2015 ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania labda Mungu amchukue au kumpa maradhi yenye kumuondolea sifa za kugombea. Hata mama yetu Josephine alikuwa anatembea ki-festiledi-festiledi.”

“Hebu maliza uongo wako, hicho kikao chenu kiliishaje?”, nlimuuliza Yahaya. Maana namjua kwa maneno mengi, huwa hamalizi.

Akasema: “Kikao hakikuisha vizuri, wakati Mbowe anajenga hoja za kumshawishi Slaa amkubali Lowassa, Josephine alitoka, kumbe alikwenda kuwasha muziki.

“Aliweka wimbo wa Jaguar, Kigeugeu. Nimtazame nani, nimwamini nani (nani) … wananigeukia. vigeugeu... vigeugeu... vigeugeu wananigeukia. Mbowe alimsihi tena sana Dk. Slaa amshawishi kuzima muziki, maana vijembe havitasaidia kupatikana kwa suluhu.

“Bila hata kuambiwa, Josephine alipunguza sauti ikawa chini. Kisha yeye mwenyewe akawa ndiye anaimba kwa sauti ya juu. Dunia nizamishe ama uniweke niishi pekee yangu, kwani ninapomwamini kila binadamu, mwishowe ananigeukia. Nimtazame nani, nimwamini nani (nani) wananigeukia. Vigeugeu… vigeugeu… vigeugeu wananigeukia.”

Kuna dada alikuwa anasikiliza kwa makini ripoti ya kikao cha suluhu ya Mbowe na Slaa kutoka kwa Yahaya, ikabidi naye atie neno, “Hapo inavyoonekana Josephine alivuruga mazungumzo ya suluhu au siyo!”

Yahaya akajibu: “Subiri kwanza, Josephine akiwa anaimba, alikuja mpaka pale sebuleni na kumtazama Mbowe, akamuuliza angekuwa yeye ndiye kafanyiwa kama Slaa angekubali?

Mbowe alijitetea kwamba hiki ni kipindi cha kupokea upepo mkubwa na kusafiri nao ili kwenda kukiangusha Chama Cha Mapinduzi. Tungemsimamisha Slaa tusingeishinda CCM.

“Josephine akamhoji Mbowe, hawezi kuishinda CCM kivipi wakati mwaka 2010 alishinda? Mbowe akashtuka, akasema Slaa hakushinda mwaka 2010. Josephine akawa mbogo, hakushinda wapi, siyo wewe uliyetangaza nchi nzima kuwa Dk. Slaa kaibiwa kura na Rais Kikwete?

“Josephine akaendelea kumbana Mbowe, mwaka 2010 mlitoka Bungeni Rais alipoingia kwa sababu ya kupinga matokeo. Sasa kama mwaka 2010 alishinda, inashindikana vipi kushinda tena 2015? Vinginevyo utangaze kuwa mlisema uongo kuwa Slaa alishinda na aliibiwa kura.”

Ukimya ukitawala sehemu tunaita Shetani kapita, na ndivyo ilivyokuwa ndani ya daladala. Kisha Yahaya aliendelea, “Kwa kifupi hata mimi niliona Josephine ana hoja nzuri. Hivi kama kweli CHADEMA walituaminisha Slaa anakubalika na anapendwa, kwa nini wamempokea Lowassa na kumtupa Slaa?

“Tunaweza kukubaliana kuwa CHADEMA walikuwa wanawadanganya Watanzania kuwa Slaa ni Rais wa mioyo ya Watanzania. Tunaweza kukubaliana kuwa stori ya Slaa kutoswa CHADEMA ni ukumbusho wa msemo wa kuacha mbachao kwa msala upitao.”

Nilimkatisha Yahaya: “Acha kukoleza maneno yako, kikao kiliishaje?”

Yahaya akasema: “Mwafaka haukupatikana, baada ya kuona Josephine anaimba sana, Mbowe kwa hasira alimgeukia Dk. Slaa akamwambia, usiyempenda kaja, utaamua mwenyewe kusuka au kunyoa, sisi tunaenda zetu Ikulu kwa safari ya uhakika na matumaini.”

“Chee chee chee,” kondakta alitutikisia sarafu kuomba nauli yake. Yahaya akamwelekeza kondakta nalipa mimi. Nikacheka kisha nikamwambia, “Fiksi zako zote, eti ulikuwa unawasuluhisha Mbowe na Slaa, kumbe hata nauli ya daladala unagongea.”
 
Huo 👆 ndo Mwisho wa Hadithi yetu Msako wa Hayawani Na Hayawani kesha patikana na ndo Kapewa Mamlaka ya Kutuvusha ktk Gurudumu hili Myaka mitano Ijayo
Masikitiko ni Kwa wale waloongoza Msako pasina kujua nani Akusudiwae Kusakwa wakizani ni Wao kumbe Ndivyo sivyo

Hii ndo TanZania Yetu zaidi ya Uijuavyo
 
Si haki kabisa mnavyotutendea
Mkijua huu msako ni Uzi pendwa na kutuekea porojo ilhali mkiamini tutapita na tutasoma.
Baraza hii kwetu wengine ni mahala pa kuturejeshea utulivu wa mioyo baada ya kumtumikia mkoloni siku nzima jumlisha kuganda kwenye foleni SAA kadhaa tukirejea kwenye pagala zetu.
Alieanzisha huu Uzi kwa lengo la kutudorishia na alaaniwe ikibidi dole gumba lake lioze.
 
Back
Top Bottom