SEHEMU YA 23
Patrick akaamua kupambana kwaajili ya kumtetea Tusa.
Wakati Patrick anajipanga kupambana huku Mashaka na Maiko nao wanapanga namna ya kuondoka na Tusa.
Patrick akamfata tena Maiko.
PATRICK: Kwahiyo umedhamiria kabisa Tusa aende na Mashaka?
MAIKO: Tatizo liko wapi Patrick? Fikiria mambo ya pesa kwanza.
PATRICK: Hapana, nampenda sana Tusa siko tayari kumpoteza kizembe hivyo.
MAIKO: Sasa unataka kufanyaje Patrick? Unataka kupambana? Unajua wazi huna la kufanya sababu unataka ataenda hutaki ataenda tu.
PATRICK: Lakini huo ni uonevu Maiko, Tusa ndiye binti pekee nimpendaye.
MAIKO: Duniani kuna wasichana warembo maelfu kwa maelfu, na ukiwa na pesa unampata yeyote umtakaye, sasa wewe kinakushinda nini kumtoa Tusa mmoja na kuingiza pesa nyingi zitakazofanya uwapate kama hao zaidi ya kumi! Fikiria mara mbili Patrick, mwanamke si ndugu yako ikitokea tenda uza mmoja uwapate wengi zaidi bila ya shida.
PATRICK: Mmh! Na mama yangu ulitaka kumuuza nini?
MAIKO: Deborah nilimpenda ila alitiwa uwaruwaru na wewe, alikuthamini wewe tu hadi kuniibia na kutoroka nawe.
PATRICK: Ila ingetokea kama hivi ungemuuza?
MAIKO: Patrick, weka hili kwenye akili yako, pesa kwanza mapenzi baadae. Mwanamke si chochote kwenye pesa, hawa ni viumbe dhaifu huwa tunawatoa sadaka tu kwanza wapo wengi sana humu duniani.
PATRICK: Kwahiyo nisimtetee Tusa?
MAIKO: Wazo lako la kumtetea Tusa lifute kabisa kwenye kichwa chako, Mashaka ni mtu hatari sana anaweza kukumaliza ingawa bado mimi nakuhitaji. Cha msingi fikiria pesa tu Patrick.
Patrick akawaza sana, akaona akitumia nguvu atashindwa kumtetea Tusa kwamaana Maiko ana kundi kubwa sana, akaamua kutafuta njia nyingine ya kumuokoa nayo ni kuwa karibu na Maiko.
Pamela alikaa na kufikiria sana kuhusu mtoto wake, alikosa raha kabisa, muda wote aliona sura ya Tusa ikimjia kwa huzuni.
PAMELA: Mama, lazima nifanye kitu kuhusu mwanangu.
REHEMA: Utafanyaje sasa?
PAMELA: Naenda Arusha kumtafuta mama.
REHEMA: Mmh utaanzia wapi sasa?
PAMELA: Popote pale lakini lazima nikamtafute kwakweli.
REHEMA: Nakuhurumia mwanangu mmh! Ni kweli roho inauma kuhusu huyo mtoto, lakini wewe kwenda Arusha naona kama utahatarisha maisha yako vile.
PAMELA: vyovyote itakavyokuwa mama lakini lazima nikamtafute mwanangu, nimepanga kati ya siku mbili tatu niondoke, nitaongea na Tina atakuja kukaa na wewe hapa mama.
REHEMA: Lakini mwanangu....
PAMELA: Usinizuie mama, nimeshaamua.
Pamela hakutaka ushauri zaidi, alishaamua kwenda kumtafuta mwanae, akawa anapanga safari ya kwenda sasa.
Patrick akiwa amewaza sana, akaenda tena kwa Maiko huku akionekana kufurahia kile kitendo cha Tusa kuchukuliwa na mashaka.
PATRICK: Hivi safari yenyewe lini?
MAIKO: Ni kesho kutwa bhana.
PATRICK: Natamani hata iwe kesho.
MAIKO: Kwanini?
PATRICK: Aaah mi nawaza mkwanja bhana, nataka niongeze magari mengine.
MAIKO: Umekuwa mjanja sasa Patrick, huo ndo uanaume. Sio kufikiria hawa wanawake wasio na faida.
PATRICK: Hivi ataenda nae wapi?
MAIKO: Dubai bhana ila analalamika kuwa mwanamke mwenyewe anatapika tapika damu kila mara.
PATRICK: Kama anataka kufa si afe tu.
MAIKO: Akifa kabla ya kazi ataharibu bhana, huyu atamalizwa kazi ikiisha halafu atakuwa bonge la dili.
Patrick akaanza kutambua tambua nia ya Maiko kuwa ni kummaliza Tusa kabisa ili asiwepo tena katika uso wa dunia.
Patrick akaenda kumuona Tusa ambaye alikuwa anatia huruma sana, ingawa Patrick alikuwa na roho mbaya kipindi hicho ila alimuhurumia sana Tusa na hakuweza kumuangalia kwa muda mrefu.
Patrick akaenda kuzungumza na Mashaka kwa mara ya kwanza.
PATRICK: Umemuonaje yule binti? Anafaa sana eeh!!
MASHAKA: Tena sana, yani yule binti ana vivutio vingi sana kwenye mwili wake.
PATRICK: Kumbe umejaribu kumchunguza kidogo?
MASHAKA: Nimemchunguza ndio, kwanza ile michirizi yake ile saivi ndio dili, nimefurahi sana kumkuta nayo, halafu ule mwanya pia ni dili na ile shingo yake ya kujikata mmh! Alikuwa demu bomba sana, isingekuwa biashara hata na mimi ningemchumbia.
PATRICK: Michirizi ndio nini kwani?
MASHAKA: Mistari flani hivi kwenye mwili, wengine huwa wanasema ni mistari ya unene sijui ingawa si kila mwenye nayo ni mnene. Basi ile nayo wameagiza sasa.
PATRICK: Hii biashara ni nzuri sana, halafu mimi nawajua wengi tu wenye hiyo mistari.
MASHAKA: Tatizo ile imejificha, vipi unaweza kunilengeshea mmoja ili niondoke na viungo vyake wakati naondoka na Tusa?
PATRICK: Hakuna tatizo, kesho nitawapatia mmoja mkashughulike naye.
Patrick alitafuta njia ya kuweza kushughulikia kile anachokiwaza kwenye akili yake.
Akamfata na Maiko,
PATRICK: Nimeongea na Mashaka kasema kuwa mwanya nao ni dili saivi.
MAIKO: Sasa utasaidiaje kwa hili?
PATRICK: Kuna mdada nimemzoea huyo, nae pia ana mwanya. Unaonaje nikuunganishe naye ili tummalize na tujitengenezee pesa zaidi?
MAIKO: Wazo zuri sana, sasa itakuwaje?
PATRICK: Kesho kama vipi nitakuunganisha nae.
MAIKO: Hayo ndio mambo ya kufikiria, kitu pesa tu.
PATRICK: Ila wapo wengi tu.
MAIKO: Ni kweli, ila huwa poa kama mtu akiwaunganishia. Unafanya kazi haraka hapo.
Patrick akaonao ngoja ajaribu bahati yake.
Pamela akajiandaa kwaajili ya safari ya kwenda Arusha.
PAMELA: Mama, kesho asubuhi na mapema naondoka na Mtei kwenda Arusha, na tiketi nimeshakata.
REHEMA: Yani umedhamiria kabisa Pamela?
PAMELA: Yani hii ndio sirudi nyuma, najua Adamu atashangaa akirudi toka huko Bagamoyo ila ndio hivyo akija mwambie tu.
REHEMA: Kwanini usingemngoja mshauriane?
PAMELA: Mama, naona anakawia tu, ngoja niende itajulikana hukohuko Arusha.
Kesho yake asubuhi na mapema, Pamela akasafiri na kuelekea Arusha.
Patrick akaenda kuzungumza na machangudoa wawili na kuwanunua.
Akaenda kuwaweka hotel tofauti na kuwaahidi pesa nyingi baada ya huduma, walichotakiwa kufanya ni kumsubiri tu, aliwakabidhi pesa kidogo kama kianzio ili wasiondoke, kila changudoa mmoja aliamini kuwa Patrick yuko kwa mwenzake kwahiyo akawa anangoja amalize kule ili nae aje kufanya kazi yake.
Patrick alipofika karibia na nyumba ya Maiko, akampigia simu Mashaka kwanza na kumuelekeza alipoacha funguo, kitendo hicho kilimfanya Mashaka ajiandae na kuchukua baadhi ya vijana na kuondoka nao, halafu akampigia simu Maiko, nae ikawa hivyo hivyo kwa mawazo yao watamkuta Patrick eneo la tukio.
Patrick akaingia getini kwa Maiko na gari yake, chumba alichowekwa Tusa alibaki mlinzi mmoja tu, ikabi Patrick amlaghai mlinzi huo na kumtuma huku akidai kuwa atabaki yeye, yule mlinzi akaenda alipotumwa.
Patrick akaingia ndani na kumbeba Tusa begani akampakia nyuma ya gari na kuondoka, mlinzi wa getini hakujua lolote, kwahiyo alimfungulia geti na kutoka.
Patrick hakutaka kupoteza muda sehemu yoyote, akaendesha lile gari kwa mwendo wa ajabu ili mradi afike mahali ambapo ataweza kujificha na Tusa kwanza huku akitafuta usafiri wa haraka wa kuwaondoa kabisa eneo hilo.
Pamela akiwa ndani ya Arusha, hatambui hili wala lile.
Alipofika alilala nyumba za kulala wageni na kesho yake akaanza kumsaka Tusa, katika pitapita zake akakutana na mwanaume wa makamo ambapo Pamela alimuona ni mwanaume mwenye heshima zake kumbe alikuwa ni Maiko ambaye yupo katika harakati za kuwatafuta Patrick na Tusa.
Pamela akaamua kumuuliza kuhusu Tusa.