Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #81
SEHEMU YA 54
Mara akashikwa bega, kugeuka nyuma ni Mwita akiwa na wanajeshi wengine watatu.
Patrick akashtuka hadi wale wakamshangaa kwani hakutarajia kuonana na Mwita kwa wakati huo ukizingatia ameshafanya mambo mabaya,
MWITA: Vipi Patrick mbona umeshtuka? Inamaana hukutarajia kukutana na mimi huku Mwanza?
PATRICK: Aah! Kumbe ulishakuja Mwanza!
MWITA: Patrick, umesahau jamani!! Si uliniambia mwenyewe kuwa nitangulie Mwanza? Na siku niliyoondoka nikakwambia, tangia hapo sijakupata tena hewani hadi nakuona leo.
PATRICK: Dah! Nilisahau bhana, kule nilipoenda hakuna umeme kabisa ndomana sikuwa hewani, nimechajia hapahapa Mwanza leo.
MWITA: Basi hawa ni wanajeshi wenzangu, wenyewe kikosi chao kipo huku Mwanza.
PATRICK: Basi vizuri kuwafahamu.
Patrick sasa akajisikia amani kidogo maana mwanzoni alidhania ameshtukiwa alichofanya.
MWITA: Sasa vipi kuhusu ile ahadi Patrick?
PATRICK: Ile ya kuhusu baba yako?
MWITA: Ndio.
Patrick akaamua kumuelekeza Mwita mahali alipoambiwa na Yuda ili yeye aendelee na mishe zake zingine kwanza, kwavile Mwita hakuwa mwenyeji mzuri wa Mwanza ikabidi aende na wale wenzie kule alipoelekezwa na Patrick.
Deborah na Pamela waliamua kuingia ndani ili kuongelea mambo mengine.
DEBORAH: Jamani hapa tumelia sana tena tumelia vya kutosha, hebu tuwashe na radio kwanza tujiliwaze na kupata habari tofauti tofauti.
PAMELA: Kweli kabisa Deborah ili tupunguze machungu yetu.
Deborah akainuka na kuwasha radio na muda huo huo wakasikia tukio la mauaji ya wanajeshi mkoani Singida.
PAMELA: Jamani majanga gani hayo?
DEBORAH: Zaidi ya majanga, ni binadamu gani mwenye roho mbaya kiasi hicho? Yani anachinja kama kuku!!
MARIUM: Ingekuwa Maiko yupo huko Singida ningesema ni yeye tu,
PAMELA: Kwanini Maiko na si mtu mwingine?
MARIUM: Kwasababu yeye ndio mwenye roho ya kinyama namna hiyo.
DEBORAH: Kwanza mimi ndio sielewi mwenzenu, kwanini Maiko kawa ndugu wa Adamu? Dah!
FAUSTA: Wote nadhani hilo swala haliwachanganyi, mimi mwenzenu ndio sielewi hata itakuwaje yani sielewi kabisa.
Maiko aliweka msiba mkubwa sana moyoni mwa wanawake hawa na hawataweza kumpokea kama mwanafamilia kwa aliyowatendea.
Tusa na Sele wakiwa Mwanza wanamuona Mwita na wenzie wakipita, Tusa anajibanza huku akimkumbatia Sele kwa nguvu kabisa.
Tusa hakutaka kumuachia Sele, alijikuta akiwaogopa wanaume wote kasoro Sele ambaye aliishi nae kwa kubembelezwa.
TUSA: Sele, nakuomba unirudishe kwa mama. Nataka nirudi nyumbani na mama yangu ili nikaishi tena na familia yangu.
SELE: Tulia Tusa, yote yana mwisho haya.
TUSA: Kwakweli Sele unanipenda na unateseka kwaajili yangu, tamaa imeniponza Sele. Nilidhani wanaume wote duniani ni Sele, kumbe kuna wakina Patrick, John, Maiko na Mwita. Sikulijua hilo, Sele una moyo wa kipekee, moyo wa tofauti. Nimeoza mimi Sele ila bado hutaki kuniacha, nanuka mimi ila bado upo karibu yangu.
Tusa alizidi kumkumbatia Sele huku machozi yakimbubujika.
Muda ambao Mwita na wenzie walipita mahali hapo ni muda huo pia Patrick nae alikatisha mahali hapo, wakina Mwita hawakuwaona Tusa na Sele ila Patrick aliwaona na kuwashangaa kilichowafanya wakumbatiane pale njiani, akaanza kuwafata pale walipo.
Mashaka aliumia sana moyo na kuendelea kumfatilia Maiko.
Akafika hadi mahali ambako Maiko alikuwa akifanya maongezi na mama yake na pacha wake pia.
Mashaka alifika na kuingia huku akiwa na hasira sana.
MASHAKA: Maiko, kitu ulichonifanyia nakwambia ipo siku utalipia.
Kuangalia pembeni akamuona dada yake bi.Rehema.
REHEMA: Hivi wewe Mashaka, mambo yako mangapi umeyalipia? Maovu uliyoyatenda unadhani yamesahaulika?
Mashaka akamuangalia sana dada yake hakutaka kuongea kitu cha zaidi ila akaondoka na kwenda kutafakari.
"Yani mimi ndio nikose kila kitu? Ila Maiko kwa maovu yake yote bado apate furaha ya maisha? Labda kama Mashaka nitakufa lazima nifanye kitu"
Mashaka alikuwa na hasira sana juu ya Maiko ukizingatia alikuwa anajua ndiye mwanae wa pekee.
Mwita alipelekwa na wanajeshi wenzie hadi mahali walipohisi ndio penyewe walipoelekezwa.
Mwita akagonga mlango, Maiko akajua Mashaka amerudi ikabidi ajiandae kwaajili ya kupambana.
Ila alipofungua mlango akamuona Mwita, naye Mwita akaingia ndani na kumwambia.
MWITA: Nimekutafuta sana baba, kwanini unanifanyia hivi?
MAIKO: Mmh!! Unanijua mimi vizuri?
MWITA: Nakujua ndio na picha zako ninazo baba.
MAIKO: Picha zangu? Alikupa nani?
MWITA: Alinipa mama, ngoja nikuonyeshe picha yake.
Mwita akatoa picha ya mama yake na kumkabidhi Maiko, akaitazama ile picha na kumkumbuka vizuri huyo mwanamke.
MAIKO: Kweli wewe ni mwanangu.
Maiko akamkumbatia Mwita, bi.Rehema na Adamu wakabaki wanashangaa tu. Ikabidi Maiko awatambulishe kwa ufupi.
Akawapatia na picha ya mwanamke aliyezaa nae.
MAIKO: Huyu ndiye mwanamke niliyezaa nae ila sikuwa naishi nae ilitokea tu tukampata huyo mtoto.
Maiko alificha ukweli wa mambo juu ya huyo mwanamke.
Bi.Rehema alipoangalia picha ya mwanamke huyo sura yake ilimjia vilivyo.
REHEMA: Mbona kama....., hebu ona na wewe.
Akamkabidhi na Adamu aitazame vizuri.
ADAMU: Mmh!! Ni huyu huyu mama.
Adamu na bi.Rehema wakajikuta wakitazamana kwa mshangao.
Tusa na Sele wala hawakumuona Patrick anavyowafata, Sele akasimamisha gari ya kukodi halafu wakapanda na kuondoka, Patrick nae akawafata kwa nyuma, yeye alikodi bodaboda.
Walienda moja kwa moja hadi karibia na nyumbani kwa Deborah wakashuka, wakawa wamesimama huku wakiongea, Patrick nae akashuka na kuwafata kwani wivu ulishamshika kwa jinsi alivyowaona.
Nia yake ni kujua kuwa kwanini walikuwa wamekumbatiana pale njiani.
Mara akashikwa bega, kugeuka nyuma ni Mwita akiwa na wanajeshi wengine watatu.
Patrick akashtuka hadi wale wakamshangaa kwani hakutarajia kuonana na Mwita kwa wakati huo ukizingatia ameshafanya mambo mabaya,
MWITA: Vipi Patrick mbona umeshtuka? Inamaana hukutarajia kukutana na mimi huku Mwanza?
PATRICK: Aah! Kumbe ulishakuja Mwanza!
MWITA: Patrick, umesahau jamani!! Si uliniambia mwenyewe kuwa nitangulie Mwanza? Na siku niliyoondoka nikakwambia, tangia hapo sijakupata tena hewani hadi nakuona leo.
PATRICK: Dah! Nilisahau bhana, kule nilipoenda hakuna umeme kabisa ndomana sikuwa hewani, nimechajia hapahapa Mwanza leo.
MWITA: Basi hawa ni wanajeshi wenzangu, wenyewe kikosi chao kipo huku Mwanza.
PATRICK: Basi vizuri kuwafahamu.
Patrick sasa akajisikia amani kidogo maana mwanzoni alidhania ameshtukiwa alichofanya.
MWITA: Sasa vipi kuhusu ile ahadi Patrick?
PATRICK: Ile ya kuhusu baba yako?
MWITA: Ndio.
Patrick akaamua kumuelekeza Mwita mahali alipoambiwa na Yuda ili yeye aendelee na mishe zake zingine kwanza, kwavile Mwita hakuwa mwenyeji mzuri wa Mwanza ikabidi aende na wale wenzie kule alipoelekezwa na Patrick.
Deborah na Pamela waliamua kuingia ndani ili kuongelea mambo mengine.
DEBORAH: Jamani hapa tumelia sana tena tumelia vya kutosha, hebu tuwashe na radio kwanza tujiliwaze na kupata habari tofauti tofauti.
PAMELA: Kweli kabisa Deborah ili tupunguze machungu yetu.
Deborah akainuka na kuwasha radio na muda huo huo wakasikia tukio la mauaji ya wanajeshi mkoani Singida.
PAMELA: Jamani majanga gani hayo?
DEBORAH: Zaidi ya majanga, ni binadamu gani mwenye roho mbaya kiasi hicho? Yani anachinja kama kuku!!
MARIUM: Ingekuwa Maiko yupo huko Singida ningesema ni yeye tu,
PAMELA: Kwanini Maiko na si mtu mwingine?
MARIUM: Kwasababu yeye ndio mwenye roho ya kinyama namna hiyo.
DEBORAH: Kwanza mimi ndio sielewi mwenzenu, kwanini Maiko kawa ndugu wa Adamu? Dah!
FAUSTA: Wote nadhani hilo swala haliwachanganyi, mimi mwenzenu ndio sielewi hata itakuwaje yani sielewi kabisa.
Maiko aliweka msiba mkubwa sana moyoni mwa wanawake hawa na hawataweza kumpokea kama mwanafamilia kwa aliyowatendea.
Tusa na Sele wakiwa Mwanza wanamuona Mwita na wenzie wakipita, Tusa anajibanza huku akimkumbatia Sele kwa nguvu kabisa.
Tusa hakutaka kumuachia Sele, alijikuta akiwaogopa wanaume wote kasoro Sele ambaye aliishi nae kwa kubembelezwa.
TUSA: Sele, nakuomba unirudishe kwa mama. Nataka nirudi nyumbani na mama yangu ili nikaishi tena na familia yangu.
SELE: Tulia Tusa, yote yana mwisho haya.
TUSA: Kwakweli Sele unanipenda na unateseka kwaajili yangu, tamaa imeniponza Sele. Nilidhani wanaume wote duniani ni Sele, kumbe kuna wakina Patrick, John, Maiko na Mwita. Sikulijua hilo, Sele una moyo wa kipekee, moyo wa tofauti. Nimeoza mimi Sele ila bado hutaki kuniacha, nanuka mimi ila bado upo karibu yangu.
Tusa alizidi kumkumbatia Sele huku machozi yakimbubujika.
Muda ambao Mwita na wenzie walipita mahali hapo ni muda huo pia Patrick nae alikatisha mahali hapo, wakina Mwita hawakuwaona Tusa na Sele ila Patrick aliwaona na kuwashangaa kilichowafanya wakumbatiane pale njiani, akaanza kuwafata pale walipo.
Mashaka aliumia sana moyo na kuendelea kumfatilia Maiko.
Akafika hadi mahali ambako Maiko alikuwa akifanya maongezi na mama yake na pacha wake pia.
Mashaka alifika na kuingia huku akiwa na hasira sana.
MASHAKA: Maiko, kitu ulichonifanyia nakwambia ipo siku utalipia.
Kuangalia pembeni akamuona dada yake bi.Rehema.
REHEMA: Hivi wewe Mashaka, mambo yako mangapi umeyalipia? Maovu uliyoyatenda unadhani yamesahaulika?
Mashaka akamuangalia sana dada yake hakutaka kuongea kitu cha zaidi ila akaondoka na kwenda kutafakari.
"Yani mimi ndio nikose kila kitu? Ila Maiko kwa maovu yake yote bado apate furaha ya maisha? Labda kama Mashaka nitakufa lazima nifanye kitu"
Mashaka alikuwa na hasira sana juu ya Maiko ukizingatia alikuwa anajua ndiye mwanae wa pekee.
Mwita alipelekwa na wanajeshi wenzie hadi mahali walipohisi ndio penyewe walipoelekezwa.
Mwita akagonga mlango, Maiko akajua Mashaka amerudi ikabidi ajiandae kwaajili ya kupambana.
Ila alipofungua mlango akamuona Mwita, naye Mwita akaingia ndani na kumwambia.
MWITA: Nimekutafuta sana baba, kwanini unanifanyia hivi?
MAIKO: Mmh!! Unanijua mimi vizuri?
MWITA: Nakujua ndio na picha zako ninazo baba.
MAIKO: Picha zangu? Alikupa nani?
MWITA: Alinipa mama, ngoja nikuonyeshe picha yake.
Mwita akatoa picha ya mama yake na kumkabidhi Maiko, akaitazama ile picha na kumkumbuka vizuri huyo mwanamke.
MAIKO: Kweli wewe ni mwanangu.
Maiko akamkumbatia Mwita, bi.Rehema na Adamu wakabaki wanashangaa tu. Ikabidi Maiko awatambulishe kwa ufupi.
Akawapatia na picha ya mwanamke aliyezaa nae.
MAIKO: Huyu ndiye mwanamke niliyezaa nae ila sikuwa naishi nae ilitokea tu tukampata huyo mtoto.
Maiko alificha ukweli wa mambo juu ya huyo mwanamke.
Bi.Rehema alipoangalia picha ya mwanamke huyo sura yake ilimjia vilivyo.
REHEMA: Mbona kama....., hebu ona na wewe.
Akamkabidhi na Adamu aitazame vizuri.
ADAMU: Mmh!! Ni huyu huyu mama.
Adamu na bi.Rehema wakajikuta wakitazamana kwa mshangao.
Tusa na Sele wala hawakumuona Patrick anavyowafata, Sele akasimamisha gari ya kukodi halafu wakapanda na kuondoka, Patrick nae akawafata kwa nyuma, yeye alikodi bodaboda.
Walienda moja kwa moja hadi karibia na nyumbani kwa Deborah wakashuka, wakawa wamesimama huku wakiongea, Patrick nae akashuka na kuwafata kwani wivu ulishamshika kwa jinsi alivyowaona.
Nia yake ni kujua kuwa kwanini walikuwa wamekumbatiana pale njiani.