Riwaya: SIN

Riwaya: SIN

SIN 49

Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)

Age ……………………………………………………18+

Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188

ILIPOISHIA

“Ingekuwa ina pendeza zaidi kama ungeendelea kukaa na mke wako wa ndoa. Kuliko kupambana na vijana kwa ajili ya kugombania mabinti wadogo.”
Kauli hiyo ya RPC Karata ikaustua sana moyo wa nabii Sanga, akasimama na kumgeukia RPC Karata aliye achia tabasamu pana sana usoni mwake.

“Unasemaje wewe?”
Nabii Sanga aliuliza kwa dharua kubwa sana.

“Ni hivi. Acha kumdanganya mke wako kwa kutembea na binti mdogo kama Magreth. Tambua kwamba Magreth ana mchumba wake anaitwa Evans na ana mpenda sana na wewe unachunwa mjini hapa mzeee hahahaaaahahaaaa……..”
Nabii Sanga akaanza kuvimaba kwa hasira. Mrs Sanga machozi yakaanza kumwagika usoni mwake kwani jambo alilo kuwa ana lihisi kumbe hata RPC ana lifahamu tena kwa mapana.

ENDELEA

“Kijana una vuka mipaka, nitakupoteza”
Nabii Sanga alizungumza kwa hasira sana huku akimkazia macho RPC Karata.

“Hee!! Unanitisha ndani ya ofisini yangu na umesahau kwamba hapa ni wapi wewe? Upo kituo cha polisi na unaye zungumza naye hapa sio ispekta ni RPC wa mkoa mzima. Toka ofisini kwangu kabla majini yangu hayajabadilika na nikakusweka ndani. Sasa wewe nenda kajichanganye kama alivyo fanya mke wako katika kukuteka na majambazi wake mchwara. Alafu utajua kwamba hichi kiti sijakikalia bahati mbaya. Utafia jela na nikuambie jambo moja macho yangu yote yana waangalia nyinyi. Jichanganyeni”
RPC Katara alizunhgumza kwa kujiamini huku akimtazama nabii Sanga. Mrs Sanga akamshika mkono mume wake na taratibu wakaanza kuondoka eneo hilo.

“Huyu kijana amekuwa jeuri sana. Nitamuonyesha mimi ni nani?”

Nabii Sanga alizidi kuzungumza kwa hasira. RPC Karata mara baada ya kushuhudia gari la nabii Sanga likiondoka eneo hilo la polisi. Akatoa simu yake ya mkononi na kumpigia kijana wake anaye husika katika maswala ya upelelezi.
“Njoo ofisini kwangu”
“Sawa mkuu”
RPC Karata akarudi kwenye kiti chake na kukaa, huku akitafakari ni jinsi gani anavyo weza kumfwatilia nabii Sanga katika kila hatua atakayo piga. Kijana huyo mrefu na aliye valia nguo za kiraia, akaingia ofisini humo, akampigia saluti mkuu wake wa kazi, kisha akakaa kwenye kiti kilichopo mbele ya meza ya mkuu wake.

“Milinga kuna kazi hatari sana nina hitaji kukupatia kuanzia hivi sasa”
“Sawa mkuu. Ni kazi gani?”
RPC Karata akamgeuzia Milinga laptop yake na kumuonyesha video iliyo rekodiwa na kamera za barabarani katika eneo la Mwenge, zikionyesha jinsi gari ya mrs Sanga ikimgonga dereva bodaboda pamoja na abiria wake.

“Hiyo ni ajali ambayo ilisababishwa na mrs Sanga. Hawa watu wamekuwa wakitumia muamvuli wa dini katika kufanikisha mambo yao. Kama hapa unaweza kuona kwamba ana makosa makubwa sana, ila nimepewa oda kutoka ikulu ya kumuachia, ikiwa raia wa kawaida huwa ni lazima wakumbane na adhabu kali sana”

“Nahitaji kuanzia hivi sasa uwe karibu sana na hii familia. Ikiwezekana hata uokoke na utafute nafasi katika kanisa hilo. Hakikisha kwamba una fwatilia nyendo za nabii Sanga hatua by hatua”
“Sawa muheshimiwa. Ila nina weza kukuuliza swali?”
“Uliza tu”
“Hii kesi ina husiana sana na askari wa usalama wa barabarani. Je kuna jambo jengine tofuati na hili ambalo una hitaji nilifwatilie as person matter au ni kutokana na ajali na kupewa oda kutoka ikulu kumuachia huru?”
Nabii Sanga akashusha pumzi taratibu, kutokana ana muamini sana kijana huyu Milinga.

“Una kumbuka kuna siku nilitolewa hapa na walinzi wa Ikulu na nikapelekwa Ikulu?”
“Ndio nina kumbuka?”
“Unakumbuka juu ya swala la yule kijana Tomas ambaye tulikuwa tuna mtafuta?”
“Ndio nina mkumbuka na hadi sasa hivi hatujamtia nguvuni.”
“Basi ishu ilikuwa hivi. Yule kijana alikuwa ana mahusiano ya kimapenzi na mke wa nabii Sanga. Kutokana na utamu kolea wa mapenzi yao, walipanga njama za kumteka nabii Sanga na wakawatumia wale majambazi tulio waua”
“Nabii Sanga aliweza kulifahamu jambo hilo. Hivyo alinipa kazi ya kumuua Tomas na mimi ndio niliye mtorosha Tomas ndani ya kituo hichi pasipo hata askari yoyote kuweza kugundua. Nikiwa katika harakati ya kumuua, nabii Sanga alinipigia simu na nikiomba nimuachie huru.Ila kutokana na askari kugundua kwamba Tomas hayupo basi ilitubidi kuingia katika ule msako. Raisi Mtenzi unaifahamu historia yake vizuri, hivyo aliweza kujua fika mtu wa pekee aliye mtorosha muhalifu ni mimi. Raisi alinipa masaa ishirini na nne niwe nima mpata la sivyo nina stakiwa kijeshi”
“Ilibibidi kuwa muwazi kwa muheshimiwa raisi hivyo alinisamehe. Ila jambo baya sana alilo lifanya huyu mzee hakudhubutu hata kuniomba msamaha kwa kile kilicho tokea. Leo hii mara baada ya mke wake kuachiwa huru, ana nitisha na kuniambia kwamba ana nionyesha na ata hakikisha nina ondoka hapa Dar na kuepelekwa Kagera. Siwezi kuwa mwema zaidi ya hapo. Tafadhali hakikisha una nipatia siri zao nyeti kuhakikisha kwamba tuna muangusha”
“Sawa mkuu nime kuelewa. Nitaifanya kazi yako kwa asilimia mia moja”
“Nita shukuru, nina imani una fahamu ni wapi kwa kuanzia?”
“Ndio muheshimiwa hakuna tatizo”
Afande Milinga akaagana na RPC Karata na kutoka ofisini hapo, huku kichwani mwake akianza kupangilia mfumo mzima wa kazi yake jinsi utakavyo kwenda.
***

Julieth na Evans wakafika Mlimani City. Wakaingia katika duka la wauazaji wa bidhaa za apple. Dada aliye zungumza na Evans masaa mawili yaliyo pita akabaki akimshanga kwa jinsi alivyo fungwa bandeji hiyo mikoni mwake.

“Si ume toka hapa ukiwa mzima?”
“Wee acha tu dada yangu. Nimepata ajali hapo Mwenge”
“Jamani pole sana”
“Asante”
“Ni ajali ya nini?”
“Pikipiki”
“Umegongwa au?”
“Hapana nilikuwa kwenye pikipiki, tugagongwa na gari bwana”
“Pole sana kaka, yaani kweli binadamu tuna tembea na vifo mkonini”
“Wee acha tu”
“Simu yako si kama ile pale”
“Ndio”
Julieth akamnunulia Evans simu hiyo na Evans. Julieth akampigia simu baba yake ili kufahamu ni jambo gani linalo endelea.

“Tupo njiani tuna elekea nyumbani na mama yako”
“Sawa je gari langu vipi lime achiwa?”
“Sijafwatilia bwana mambo ya magari. Huyo mgonjwa wako ana endeleaje?”
“Amesha ruhusiwa hospitalini”
“Fidia ana taka nini?”
“Aha…sija zungumza naye kuhusiana na swala la fidia”
“Zungumza naye kisha urudi nyumbani sasa hivi”
“Sawa baba”
Julieth akakata simu, akamuomba Evans wakae kwenye mgahawa wa Samaki Samaki ili waweze kuzungumza mambo mawili matatu. Evans hakuwa na kipingamizi cha aina yoyote. Wakaagiza chakula na taratibu wakaanza kula.
“Ahaa baba ameniuliza kama kuna fidia ya aina yoyoye ambayo una weza kudai ili tukupatie”
“Hapana usijali. Kutokana simu yangu ime rudi hakuna tatizo”
“Kweli”
“Ndio Julieth”
Evans alizungumza huku akiendelea kuudadisi uzuri wa Magreth.

“Aha samahani Evans hapa mjini una jishuhulisha na shuhuli gani?”
“Nimemaliza chuo, nilipata matatizo ya kuvamiwa na vibaka na wakaniibia vyeti vyangu vyote”
“Aisee pole sana”
“Nashukuru”
“Sasa una ishije hapa mjini kama huna kazi?”
“Nimejishikiza kwa msichana mmoja ambaye ni mpenzi wangu. Japo ame nieleza kwamba ana mpenzi wake. Ila bado nina endelea kutafuta tafuta maisha si unajua wana wake muda wowote wana badilika”
“Ni kweli, sasa ina huyo mwanamke mpenzi wake yupo wapi?”
“Hajanieleza, japo ana kiri kwamba ana nipenda. Ila ndio hivyo maisha yake hayo ame tengenezewa na mwanaume wake”
“Pole sana Evans na ume somea maswala gani?”
“Nimesomea mambo ya biashara”
“Ahaa ngoja kuna kampuni ya usafirishaji nina hitaji kuifungua mwezi huu. Basi nita kupa nafasi ya umeneja”
“Kweli?”
“Haki ya Mungu. Nimeagizia roli ina ya Benz zipatazo hamsini. Zitakuwa zina chukua mizigo bandarini, kupelekea nje ya nchi”
“Aissee hongera sana. Je nina weza kukuuliza swali?”
“Uliza tu”
“Pesa zote hizo umezitoa wapi ikiwa una onekana ni binti mdogo”
“Wazazi wangu ni mabilionea. Wana pesa nyingi sana, hivyo waliniuliza ni mradi gani ambao ningependa kufanya. Nikaona ni heri nifungue biashara hiyo. Gari hizo zipo baharani na zina tokea nchini Ujerumani”
“Nashukuru kukutana na wewe na nina kuahidi kwamba nita simamia kampuni yako na itwa kwenda vizuri sana”
“Sawa kikubwa ni kujituma. Japo mmi ni mwanafunzi ila ni mfwatiliaji mzuri sana katika maswala ya pesa”
“Sinto kuangusha.”
“Kesho kama uta pata muda. Tukutane ili niweze kukupatia pesa ambayo una weza kupangisha nyumba ya kwako mwenyewe. Hapa nina fikiria endapo mwanaume huyo ata kuja kukukuta ndani ya nyumba ya demu wake ita kuwaje? Au hilo hujawahi kulifikiria?”
“Nimelifikiria ila mwanamke huyo ameniambia kwamba yupo tayari kupoteza kila kitu ili mradi awe na mimi?”
“Si kwa dunia ya sasa hivi. Ana kudanganya sana huyo mwamke, hakuna mtu ambaye ata kubali kuishi katika maisha ya umasikini kisa mwaume. Hapana amekuingiza cha kike na tena na kutafutia matatizo makubwa sana”
Maneno ya Julieth kidogo yakaanza kumpa wasiwasi Evans.
“Ila sijui lakini, ila kwa asilimia kubwa ya wanawake wa hapa mjini, hususani wale ambao wana wana pata wanaume wa kuwawezesha, wana mambo mawili. Yupo tayari kukufanya wewe kuwa kaka yake pale atakapo kuwa na mwanaume huyo au kukuacha kabisa. Kuwa makini sana Evans”
“Nimekuelewa dada yangu”
“Sawa muda wangu ni mdogo, acha niondoke hapa, niwahi nyumbani na pia nifanye taratibu za kulitoa gari langu polisi”
“Sawa nina shukuru kwa muda wako”
Julieth akafungua pochi yake na kutoa laki moja na kumkabidhi Evans.

“Kodisha taksi ikufikshe nyumbani. Angalia usije ukapanda pikipiki ukapata tena matatizo”
“Nina shukuru sana”
Wakaagana na Evans akaanza safari ya kurudi kigamboni, huku Julieth akirudi nyumbani kwa baba yake. Evans akajifikria kwa muda na kuona hakuna haja ya kurudi nyumbani muda hao. Moja kwa moja akaelekea kwenye mgahawa wa Magreth. Kwa bahati nzuri akamkuta Magreth aliye jawa na mshangao mara baada ya kumuona mume wake akiwa katika hali hiyo.

“Kuna nini kimekupata mume wangu”
Evans akamuelezea Magreth hali halisi ya tukio lilivyo tokea. Hakumuelezea kukutana na Julieth kwani ana imani kwamba kupitia msichana huyo basi ana weza kupata msaada mkubwa sana utakao mtoa kimaisha.

“Basi twende nyumbani uka pumzike”
“Wewe si upo kazini mpenzi wangu?”
“No ila hali yako sio nzuri, twende nyumbani sasa hivi uka pumzike”
Magreth alizungumza kwa msisitizo. Evans hakuwa na pingamizi lolote zaiid ya kukubaliana na mke wake huyo. Magreth akaacha majukumu yote ya kuendesha mgahawa huo kwa Juma, kisha yeye na Evans wakaondoka na kuianza safari ya kuelekea nyumbani kwao Kigamboni.
***

Nabii Sanga akafika nyumbani kwake huku akiwa amejawana hasira kali sana. Akapitiliza hadi chumbani kwake, akafungua shelf ya kuhifadhia nyaraka zake muhimu pamoja na bastola yake. Akachukua bastola yake na kuichomeka kiunoni kwa nyuma.

“Una kwenda wapi mume wangu?”
Mrs Sanga alizungumza huku akimtazama mume wake aliye fura kwa hasira.
“Sitaki maswali ya kipumbavu. Wewe hujaona udhalilishanji nilio pewa na yule kijana”
“Mume wangu, nakuomba uzuie hasira yako. Kumbuka kwamba wewe ni mtumishi wa Mungu mbele ya macho ya watu. Itakuwaje pale watu wakisikia kwamba ume fanya mauaji?”
“Sijali mimi, nita hakikisha kwamba nina mfundisha adabu. Ninakwenda na nikirudi hapa ninataka unipe majibu ya wapi ulikuwa unakwenda hadi uka gonga mtu. Umenielewa wewe mwanamke”
Nabii Sanga alizungumza kwa msisitozo huku akimtazama mke wake. Mrs Sanga hakuwa na uwezo wa kumzuia mume wake. Nabii Sanga, akafungua kabati linalo hifadhia kofia zake, akachukua moja ya kofia na kutoka ndani humo. Akabadilisha gari na kutumia gari aina ya BMW X6 ambayo ni mara chache sana amekuwa akiitumia. Kilicho mkasirisha nabii Sanga si dharau za RPC Karata, ila kitu kinacho muumiza moyoni mwake ni kuhusiana na mahusiano ya Magreth na Evans kijana ambaye alimsaidia hospitalini kwa kumlipia matibabu mara baada ya kuchomwa kisu na wahuni wa mtaani.

‘Lazima nimuue huyu ngedere. Hawezi kunichukulia mwanamke wangu ninaye mpenda’

Nabii Sanga alizungumza huku akizidi kuongeza mwendo wa gari lake.Akafika nyumbani kwa Magreth, akalisimamisha gari lake katika moja ya dula la karibu na nyumba hiyo. Akashuka na kuanza kutembea hadi getini kwa nyumba ya Magreth. Akatoa funguo za geti hilo na kufungua, akaingia ndani. Ukimya wa nyumba hiyo haukumuogopesha nabii Sanga. Akafungua mlango wa mbele wa nyumba, akaingia na kuufunga kwa ndani.
Nabii Sanga moja kwa moja akaeleka chumbani kwa Magreth na kuingia ndani,kitu kilicho mshangaza na kumuumiza roho yake ni kukuta nguo za mwanaume.

“Huyu malaya ana ujasiri gani wa kuishi na mwanaume ikiwa kila kitu hapa ni mali yangu?”
Nabii Sanga alizidi kuzungumza kwa hasira kali sana. Akaichomoa bastola yake na kukaa kitandani hapo huku akimsubiria Magreth na Evans kwa hamu sana.
ITAENDELEA

Haya sasa nabii Sanga anawasubiria Magreth na Evans wafike nyumbani hapo, je itakuwaje wakirudi ikiwa hawatambua uwepo wowote wa nabii Sanga? Endelea kufwatilia kisa hichi cha kusisimua, usikose sehemu ya 50.

Tuonane kesho
 
Nabii sanga atakuja kudundwa na kijana wa Rpc Karata wakati anataka kumfyatulia risasi Evance.

Evance atamtombeanao Jurieth halafu amalizie kwa mke wa nabii Sanga
 
SIN 50

Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)

Age ……………………………………………………18+

Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188

ILIPOISHIA

Ukimya wa nyumba hiyo haukumuogopesha nabii Sanga. Akafungua mlango wa mbele wa nyumba, akaingia na kuufunga kwa ndani.
Nabii Sanga moja kwa moja akaeleka chumbani kwa Magreth na kuingia ndani,kitu kilicho mshangaza na kumuumiza roho yake ni kukuta nguo za mwanaume.

“Huyu malaya ana ujasiri gani wa kuishi na mwanaume ikiwa kila kitu hapa ni mali yangu?”
Nabii Sanga alizidi kuzungumza kwa hasira kali sana. Akaichomoa bastola yake na kukaa kitandani hapo huku akimsubiria Magreth na Evans kwa hamu sana.

ENDELEA
Nabii Sanga akatazama kitanda hicho alicho kalia huku machozi yakimlenga lenga kwa uchungu sana. Kitanda ambacho alikuwa ana lalia na mwanamke anaye mpenda leo hii yupo mwanaume mwengine anaye lalia. Nabii Sanga akatazama jinziza kiume jinsi zilivyo jaa katika kabati la nguo la Magret huku zikichanganyikana na nguo za Magreth. Kelele za geti kufunguliwa, zikamfanya nabii Sanga kunyanyuka kwa haraka na kufungua la chumba hicho na kufungulia dirishani. Akawaona Magreth na Evans wakishuka kwenye gari hilo alilo wanunulia. Magreth akafunga geti hilo, ila kilicho mshangaza nabii Sanga ni bandeji aliyo fungwa Evans mkononi mwake.

Baada ya Magreth kufunga geti hilo, akamshika Evans kiuno na kuanza kuingia naye ndani. Nabii Sanga akatazama ni sehemu gani ambayo ana weza kujificha, kwa haraka akakimbilia bafuni huku bastola yake ikiwa mkononi.

‘Lazima nimwage mtu ubongo wake’

Nabii Sanga aliwaza huku bastola yake akiwa ameishika vizuri sana. Evans akaka kwenye moja ya sofa la sebleni hapo huku akijihisi mwili mzima kuchoka.

“Sijui yule dereva wa watu kama atakuwa hai”
Evans alizungumza huku akimtazama Magreth alieye fungua friji kubwa lililopp sebleni hapo.

“Tuta fwatilia taarifa zake. Mume wangu una uhakika kwamba dokta ame kueleza huja pata tatizo lolote kwa ndani?”
“Ndio, ni michubuko midogo midogo kwa maana ile ajali ilipo tokea. Nilirushwa mbele hivi, hivyo sikukubali kutua kama mzigo, ilinibidi kubingirika kitandani ili kuendena na ule msukuko nilio upata.”
“Mmmmm ila Mungu ame husika katika hilo kwa maana sasa hivi ungekuwa na majanga”
“Ni kweli, njoo hapa”
Evans alizungumza na Magreth akamfwata sehemu hiyo. Magreth akamkalia Evans mapajani mwake. Evans akamtazama Magreth kwa muda usoni mwake, kisha akampokonya glasi ya maji aliyo ishika na kuiweka mezani.
“Nini tena baby”
“Nina hamu na wewe”
Evans alizungumza huku akimgeuza Magreth na kumkalisha mkao ulio wafanya watazamane huku Magreth akiwa ameyakalia mapaja ya Evans. Kutokana Magreth leo alijiandaa kwa ajili ya kumburudisha nabii Sanga na akakosa huduma yake, hakuona haja ya kumnyima penzi Evans. Taratibu wakaanza kunyonyana lipsi zao huku kila mmoja akiwa amejawa na furaha kubwa sana. Magreth akamvua Evans tisheti aliyo ivaa na taratibu akaanza kupitisha viganja vyake kwenye kifua hicho.

‘Twende ndani baby”

Magreth alizungumza huku akihofia kamera zilizo fungwa sebleni hapo kwa pendekezo la nabii Sanga. Evans akambeba Magreth.
“Baby utaumia mkono”
“Hakuna cha kuumia mpenzi wangu”
Evans alizungumza huku akipiga hatua za kuelekea ndani ya chumba hicho. Wakaingia ndani na taratibu akamlaza Magreth kitandani huku akimnyonya shingo yake. Miguno ya kimahaba ya Magreth ikazidi kumchanganya nabii Sanga. Hakuamini maishani mwake kama ipo siku Magreth atakuja kumsaliti. Nabii Sanga akafungua mlango wa bafuni humo taratibu na kuchungulia kitandani. Akamuona jinsi Magreth anavyo nyonywa maziwa yake kwa fujo Evans.

Nabii Sanga akafungua kwa nguvu mlango huo na kutoka chumbani hapo na kuwafanya Evans na Magreth kukurupuka na kuacha hicho wanacho kifanya. Macho yakamtoka Magreth huku mapigo yake ya moyo yakimdunda kwa kasi sana. Nabii Sanga akavua kofia hiyo na kumfanya Evans aweze kumfahamu mzee huyo, ukiachilia umaarufu wake wa kuwaponya watu, ila ni mzee ambaye alimsaidia katika matibabu yake.

“Mage Mage Mage. Huyu ndio panya anaye kufanya una nisaliti mimi?”
NabiiS anga alizungumza kwa hasira sana huku akimtazama Magreth aliye chukua mto na kujiziba maziwa yake huku mwili mzima ukimtetemeka kwa woga.

“Kijana huyu hakukuambia kwamba mimi ni mume wake?”
Evans akamtazama Magreth aliye anza kumwagikwa na machozi yatokanayo na woga. Nabii Sanga akaunyanyua mkono wake ulio shika bastola na kumuelekezea Evans usoni mwake.

“Ninakuua humu humu ndani alafu hakuna mjinga yoyote ambaye ata jua juu ya uwepo wako. Fala wewe”
Nabii Sanga alizungumza huku bastola hiyo ikiwa ime lenga kichwa cha Evans amabye naye yupo kwenye wakati mgumu. Woga ume mtawala mwili mzima, leo ana amini ndio mwisho wa maisha yake, kwani kama aliponyoka ponyoka kufa kwa kugongwa na gari basi haamini kama ana weza kutoka mikononi mwa nabii Sanga.

“Mu..me wa…ngu nakuomba u…u…msamehe Evans”
“Funga bakuli lako malaya wewe. Nikupe nini eheee, nimefanya kila liwezekanalo kwa ajili yako, ila haya ndio matusi ya maliyo yako eheee?”
Nabii Sanga alizidi kufoka kwa hasira sana.

“Shuka kitandani kenge wewe”

Taratibu Evans akatii amri hiyo na kushuka kitandani huku miguu yake ikiendelea kumtetemeka.
“Huwa sinaga huruma na watu wanao jaribu kuchovya vidole katika mzinga wangu wangu wa asali”
Nabii Sanga alizungumza huku akimuelekezea Evans bastola ya kichwa tayari kwa kumfumua ubongo wake.

***

“Tomas mume wangu, hivi kuna haja yoyote ya sisi kuondoka hapa Afrika kusini kuelekea Nigeria?”
Mke wa Tomas alizungumza huku akwia amekilaza kichwa chake kifuani mwa mume wake.
“Itabidi kwa maana kuna endapo askari wakafanya upelelezi na kufahamu kwamba tume muua yule jamaa ita kuwaje?”
“Ni watu wangapi huwa wana uwawa hapa Afrika kusini na hakuna sheria zinazo chukuliwa dhidi yao. Kwenye hii nyumba mimi nina jiona tupo salama”
“Sawa nita jaribu kumshawishi ndugu yangu. Akiona ina faa basi tuta endelea na maisha yetu hapa. Ila ni lazima tuangalie ni nii cha kufanya na tusiwe tuna ishi na kuwa tegemezi kwa mtu”
“Sawa mume wangu. Nipo tayari kukuunga mkono katuka jambo lolote ambalo una lifanya mume wangu”
“Kweli?”
“Ndio”
Taratibu Tomas akaanza kunyanyana ndimi na mke wake. Kutokana wote wapo kama walivyo zaliwa, ikawa ni rahisi sana kwa kuanza mtanange huo wa kukata na shoka. Ndani ya dakika hamsini, kila mtu akwa amesha ridhishwa na mwezake. Tomas akashuka kitandani mara baada ya mke wake kupitiwa na usingizi, akavaa nguo za kulalia ambazo walizinunua madukani. Akatoka chumbani humo na kuingia katika chumba walicho mlaza mtoto wao na kumkuta akiwa amelala. Akaelekea selbeni na kumkuta Ngosha akitazama filamu.

“Vipi huja lala kaka?”
“Yaa usingizi haupandi kabisa.”
“Kwa nini?”
“Mmmm nawaza mambo mengi sana. Unajua hili genge ninalo limiliki nina ona nilisambaratishe.”
Ngosha alizungumza kwa upole huku akimtazama Tomas usoni mwake.
“Kwa nini kaka, ikiwa wana kuletea faida kubwa?”
“Ni kweli, ila wao pia wana maisha. Wana taka kutengeneza familia kama wewe, unajua uwepo wa mke wako na mtoto wako humu ndani. Nimeona mabadiliko makubwa sana kwenye moyo wangu na mimi pia nina bidi niwe na familia. Umri una kwenda kaka na hizi mali zote endapo ikitokea nikafariki nani ata kuwa ni mridhi?”
Ngosha alizungumza kwa msisitizo huku akimtazama Tomas usoni mwake.
“Unahisi vijana wako wata hitaji kutawanyika?”
“Ndio jambo ambalo nina liwazia.”
“Ila ngoja nikushauri kitu”
“Nishauri ndugu yangu”
“Hii nchi sio chimbuko letu. Una pesa nyingi sana kwa nini usiende kuwekeza Tanzania. Kuna kesho na kesho kutwa, itatulazimu kuondoka katika hii nchi hii. Pesa tunaweza kubeba je majumba”
“Ni kweli ndugu yangu. Unajua toka bi mkubwa afariki nchini Tanzania, nimekuwa ni mtu wa kuitenga sana ile nchi. Ndugu wote walio baki, waling’ang’ania mali na mimi niliamua kujitafutia za kwangu na mwishowe nasikia wame kula mali zote na wame fulia”
“Sawa ndugu ila huwekezi kwa ajili yao. Ila una wekeza kwa ajili ya kizazi chako.”
“Niushauri mzuri sana ndugu yangu. Nitaufanyia kazi”
“Nashukuru kwa hilo. Eheheee!! Shemeji yako amenishauri kwamba ikiwezekana tuendelee kuishi tu hapa nchini Afrika kusini. Hakuna haja ya kuelekea nchini Nigeria”
“Kwa nini ameshauri hivyo ikiwa kuna mauaji yalitokea pale ndani?”
“Ni kweli, ila kwa jinsi vijana wako walivyo fanya usafi na kusafisha eneo lile sidhani kama kuna polisi ana weza kugundua kama ndani ya nyumba ile kume tokea mauaji”
“Sawa kama ndio anavyo hitaji. Je upo tayari kuifanya ile biashara ya kuchukua wanawake nchini Tanzania na kuwaleta huku kwa ajili ya bishara?”
“Nitalifikiria hilo”
“Sawa je biashara ya unga au nimueleze Adela kwamba una hitaji muda zaidi?”
“Nipe wiki moja kaka nita kupatia jibu”
“Sawa ndugu yangu. Hivi Tanzania ni biashara gani ina lipa zaidi kwa maana wewe kule ulikuwa dalali na una fahamu watu wengi”
“Ukifungua kumbi za Starehe na kumbi za maharusi. Uatapata pesa nzuri sana”
“Basi katikati ya wiki hii nitakwenda nchini Tanzania kuhakikisha kwamba nina fanya upelelezi wangu wa kutosha na kuhakikisha kwamba nina fungua biashara nzuri sana ambayo ita lipa”
“Sawa kaka, nami nina tamani sana kurudi nchini humo ila yale majanga yana weza kuni kumba tena”
“Usijali, nitafanya upelelezi wa jambo lako nan ita kuambia ni ninikinacho endelea”
“Poa kaka, ila yule mjinga nabii Sanga hakikisha una nijia na full data zake. Yaani nitahitaji kumuua kwa mikono yangu mimi mwenyewe”
Ngosha akamtazama Tomas kwa umakini sana kisha akamnyooshea dole gumba akimaanisha kwamba ata lifanyia kazi jambo hilo.
***

“Mama yupo wapi?”
Julieth alimuuliza dada wa kazi.
“Yupo chumbani”
Julieth akapandisha gorofani, akasimama mlangoni mwa chumba hicho cha wazazi wake. Akaanza kugonga tartaibu.

“Nani?”
“Mimi mama”
“Ingia”
Julieth akaingia na kumkuta mama yake akiwa amelala kitandani. Taratibu Julieth akaka pembeni yake huku akimtazama usoni mwake.

“Mama una jisikiaje?”
“Vizuri”
“Kesi ime kwisha?”
“Hapana wameniachia kwa dhamana ila itanibidi kuripoti polisi kesho”
“Ila una jisikiaje?”
“Nina mawazo mengi sana na nikweli baba yako ana mahusiano na Magreth”
“Umejuaje mama?”
“RPC alizungumza mbele yetu kwa maana kulitokea kuto kuelewana kati ya baba yako na RPC”
“Sasa mama uta mfanya nini Magreth”
“Kosa sio la kwake. Kosa ni la baba yako.”
Mrs Sanga alizungumza kwa sauti iliyo jaa masikitiko makubwa sana.
“Ila sinto muacha salama huyu binti ni lazima nidili naye. Nita hakikisha nina muua kwa mikono yangu mimi mwenyewe.”
“Mama!”
“Ndio lazima nifanye hivyo na wewe nina kufundisha kwenye maisha yako. Usiruhusu mwanamke mwengine akakchukulia mwanaume wa maisha yako. Hususani mume uliye funga naye ndoa. Hakikisha kwamba una pigania ndoa yao hadi dakika ya mwisho. Una nielewa?”
“Ndio mama”
“Kwanza una mchumba?”
“Sina”
“Ulisha wahi kupenda?”
“Hapana mama, kama ninge penda. Ningekueleza wewe ndio msiri wangu”
“Sawa. Baba yako alihidi akirudi ata hitaji kufahamu ni wapi tulikuwa tuna elekea. Hakikisha hufungui kinywa chako kumueleza tuliyo yafanya leo ume nielewa?”
“Usijali mama katika hilo. Nahitaji kulitoa gari langu je nifwate hatua gani?”
“Mmmm wasilana na mwanasheria wa familia. Ana weza kukusaidia katika hilo”
“Sawa mama cha nifanye hivyo”
Julieth alizungumza huku akitoka ndani humo kwa mama yake. Akawasiliana na mwanasheria wa familia na kumuomba aweze kufika nyumbani hapo.
***

Magreth akajikaza na kushuka kitandani hapo huku akiendelea kulia kwa uchungu. Taratibu akapiga magoti pembeni ya nabii Sanga na kuishika miguu yake yote miwili.
“Sanga mume wangu nina kuomba nisamehe. Sinto rudia kufanya kosa hili tena”
Magreth alizungumza kwa uchungu sana. Maneno ya Magreth yakamuumiza sana Evans moyo wake, akayakumbuka maneno ya Julieth kwamba hakuna mwanamke hapa mjini ambaye ana weza kusaliti mali kwa ajili ya mapenzi.
“Mimi na huyu panya hapa una mpenda nani?”
Magreth taratibu akamtazama Evans kisha akamtazama nabii Sanga aliye ishika bastola yake aliyo muelekezea Evans bastola hiyo.

“Nakupenda wewe tu Sanga. Kumbuka kwamba wewe ndio mwanaume wangu wa kwanza kunitoa usichana wangu. Kumbuka hata leo nimeshinda kukupa penzi kule hotelini hii yote ni kutokana na tatizo lililo jitokeza. Nisamehe mume wangu nakupenda sana”
Maneno ya Magreth yaka mnyong’onyeza sana Evans, akajikuta akijuta ni kwa nini amemfahamu Magreth na kufanya mambo yote ikiwemo la kumsaidia kumuokoa kutoka mikononi mwa vibaka ambao mwishowe aliambulia kuchomwa kisu na chupuchupu afariki dunia.
ITAENDELEA

Haya sasa Evans leo ame fahamu ukweli wote kuhusiana na penzi laMagreth na nabii Sanga. Je Evans ata fanikiwa kutoka mikononi mwa nabii Sanga? Endelea kufwatilia kisa hichi cha kusisimua, usikose sehemu ya 51.
 
SIN 51

Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)

Age ……………………………………………………18+

Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188

ILIPOISHIA

“Mimi na huyu panya hapa una mpenda nani?”
Magreth taratibu akamtazama Evans kisha akamtazama nabii Sanga aliye ishika bastola yake aliyo muelekezea Evans bastola hiyo.

“Nakupenda wewe tu Sanga. Kumbuka kwamba wewe ndio mwanaume wangu wa kwanza kunitoa usichana wangu. Kumbuka hata leo nimeshinda kukupa penzi kule hotelini hii yote ni kutokana na tatizo lililo jitokeza. Nisamehe mume wangu nakupenda sana”
Maneno ya Magreth yaka mnyong’onyeza sana Evans, akajikuta akijuta ni kwa nini amemfahamu Magreth na kufanya mambo yote ikiwemo la kumsaidia kumuokoa kutoka mikononi mwa vibaka ambao mwishowe aliambulia kuchomwa kisu na chupuchupu afariki dunia.

ENDELEA

Maneno ya magreth kidogo yakamfariji nabii Sanga na kuiyayusha hasira yake ambayo imevuka kiwango chake cha kwaida.

“Wewe mbwa, nikifumba macho na kufumbua nina kuhitaji uwe ume potea ndani humu”
Evans hakutarajia kupata nafasi kama hiyo. Kwaharaka akatoka chumbani hapo, alicho kikumbuka kukichukua sebleni ni boksi lenye simu yake pamoja na tisheti aliyo kuwa ameivaa. Akatoka kwa kasi katika nyumba hiyo ya Magreth na kutoweka kabisa katika mtaa huo kwani akionekana basi ana weza kuuwawa na nabii Sanga. Nabii Sanga taratibu akachuchumaa huku akimtazama Magreth usoni mwake, akamkumbatia huku akimpiga mabusu mfululizo.
“Yaani ingekuwa sio wewe. Ningemuua yule mshenzi, hawezi kukuchukua kirahisi rahisi”
Nabii Sanga alizungumza kwa majigambo. Akamnyanyua Magreth na kumlaza kitandani, haraka haraka akavua nguo zake, akaitanua miguu ya Magreth ambaye bado ana endelea kulia na kujutia kuzungumza maneno ambayo ana amini kwa namna moja ama nyingine yame muumiza sana Evans. Ila kwa upende mmoja amefanya hivyo ili mradi kuyaokoa maisha ya Evans ambayo yalikuwa yapo hatarini sana kupote. Nabii Sanga hakujali Magreth yupo kwenye hali gani ila alicho kifanya ni kuhakikisha kwamba ana kata kiu yake ambayo ni kwa muda mrefu sana ilikuwa ina mkabili.
***

Evans akafika katika kituo cha daladala huku akiwa haamini kama yupo hai. Katika maisha yake hii ndio mara yake ya kwanza kunyooshewa bunduki tena kwa lengo la kuuwawa.

‘Niende wapi mimi?’

Evans alijiuliza huku akiendelea kushangaa dalala zinazo simama na kuondoka katika kituo hicho. Kutokana kwenye wallet yake kuna pesa ya kutosha, akakodisha bajaji ikampeleka hadi maeneo ya Kinondoni, akapangisha chumba katika hoteli ya Nemax. Akatoa simu hiyo iliyopo kwenye boksi, akaiweka chaji. Akajizala kitandani huku akeindelea kuyafikiria maneno ya Magreth.

“Ina bidi ni move on”
Evans alizungumza huku akijizungusha zungusha kitandani.

‘Daa simu line yangu nime iacha kwa huyu mshenzi. Ila hakijaharibika kitu nita tafuta line nyingine na sinto hitaji niwe na mawasiliano naye kabisa’

Evans aliendelea kupanga mikakati yake. Siku nzima hakutoka nje ya chumba hicho na aliagiza chakula ndani humo humo. Asubuhi na mapema, akamuazima mmoja wa wahudumu simu yake kwa ajili ya kuwasiliana na Julieth. Akaiingiza namba ya Julieth katika simu ya mhudumu huyo na kuiweka sikioni mwake. Simu ikaita na baada ya muda ikapokelewa.

“Habari za asubuhi”
“Salama nani mwezangu”
“Evans”
“Ohhoo Evans mbona ume tumia namba mpya?”
“Yaa kuna matatizo kidogo niliyapata. Imenilazimu kuazima simu ya mtu hapa nilipo”
“Matatizo gani na upo wapi?”
“Nipo Nemax Hotel”
“Hapo Kinondoni?”
“Ndio”
“Basi nina kuja sasa hivi”
“Sawa nipo chumba namba mia na kumi na tano”
“Sawa nina kuja”
“Hii ni namba ya muhudumu wa hapa hotelini”
“Sawa usijali”
Evans akakata simu na kumrudishia muhudumu huyo wa kike. Akampatia noti ya shilingi elfu kumi kama asante yake na kurudi chumbani kwake. Halikuisha hata lisaa moja Julieth akafika hotelini hapo huku akiwa amevalia kofia ambayo ime uficha uso wake kwa asilimia kubwa sana. Akafika katika chumba cha Evans akagonga na kufunguliwa mlango. Evans akamkatibisha, wakasalimiana kwa kumbatiana kisha Julieth akaka kwenye moja ya sofa.

“Samahani sana kwa kukusumbua asubuhi asubuhi hii”
“Usijali ni mambo ya kawaida. Ehee niambie ni nini kimetokea?”
“Mume wa yule demu alifika jana nyumbani. Yaani nimeponea chupuchupu bado nusu tu aniue kwa kunipiga risasi”
“Jamani”
“Ndio hivyo dada yangu”
“Pole sana Evans. Ila jana nilikuambia, umeona sasa. Hayajapita hata masaa ishirini na nne, kile nilicho kisema kimekuwa”
“Ndio hivyo”
“Pole hapa ume chukua chumba kwa muda gani?”
“Siku na saa nne ina nibidi kuondoka”
Julieth akafungua pochi yake na kutoa kiasi cha laki tatu na kumkabidhi Evans.
“Ongeza muda wa kukaa hapa hotelini. Nina kwenda polisi asubuhi hii na mwana sheria wangu kwenda kuitoa gari yangu. Baada ya hapo tuta wasiliana tujue ni wapi tuna anzia katika kutafuta nyumba ya kuishi”
“Nashukuru sana Julieth”
“Usinishukuru. Hivi ni vitu vya kawaida tu”
Julieth alizungumza hukua kiachia tabasamu pana usoni mwake. Ukweli ni kwamba jana usiku Julieth hakuweza kupata hata lepe usingizi kwa kumuwaza Evan. Kwenye maisha yake ametongozwa na wanaume wengi sana ambao wengi wao wana mfwata kwa ajili ya uzuri na utajiri wake. Ila kati ya wanaume hao wote hakuwahi kumpenda wala kumjibu hata mmoja wao. Ila kwa Evans amejikuta moyo wake ukiachanua kwa hisia kali za kimapenzi kwa kijana huyo ambaye ame kutana naye kwenye ajali tu.
“Nimefunzwa kushukuru kwa kila jambo hivyo usishangae kwa mimi kushukuru kwangu”
“Sawa Evans, acha mimi niwahi polisi centra. Ila nakuomba ufanye jitihada za kusajili laine yako”
“Nimepoteza vitambulisho vyangu, yaani hapa nilipo nipo mimi kama mimi”
“Oohoo basi nita kusajilia. Una penda kutumia voda au tigo?”
“Tigo”
“Basi nitakuletea. Hakikisha huondoki hapa hotelii hadi nitakapo rudi”
“Usijali”
Julieth akamtazama Evans kwa muda. Akatamani kumuambia jambo ila akashindwa kabisa na kujikuta akiondoka pasipo kuzungumza ukweli wa hisia zake.
***

Hadi ina timu saa moja asubuhi Magreth hakuweza kupata hata lepe la usingizi. Mizunguko yote minne aliyo ienda nabii Sanga, hapakuwa na mzuko hata mmoja ambao uliweza kumridhisha kimapenzi. Hisia na akili zake wala hazipo kwa mzee huyo anaye koroma pembeni yake. Magreth akashuka kitanda, akachukua simu yake na kutoka ndani humo. Akanza kuitafuta namba ya Evans na kumpigia, ila kila alipo jaribu kufanya hivyo hakuweza kumpata hewani. Furaha ikazidi kupotea Magreth kwani mwanaume anaye mpenda ndio hivyo amesha utibua moyo wake.
‘Ehee Mungu nita fanya nini mimi?’

Magreth alilalama huku machozi yakimwagika usoni mwake. Akarudi chumbani na kumkuta nabii Sanga akijigeuza geuza.
“Baby”
Magreth alimuita nabii Sanga haku akimtingisha tingisha.

“Mmmm”
“Kume pambazuka. Amka”
“Saa ngapi hivi sasa?”
“Mbili kasoro asubuhi”
Nabii Sanga akajinyoosha viongo vyake huku akipiga miyayo mfululizo.
“Huja kwenda kwako, ita kuwaje kw make wako”
“Achana naye hana jambo la kunieleza”
Nabii Sanga alizungumza huku akishuka kitandani hapo. AKajisaidia khaja ndogo na kurudi chumbani.
“Leo nahitaji unipikie chakula kizuri sana na nita lala hapa hapa hadi kesho”
“Kesho?”
“Ndio una shangaa nini? Au una hitaji yule mjinga wako aweze kurudi hapa?”
“Hapana”
“Ila?”
“Nisamehe mumewangu. Kumbuka nina mgahawa wa kusimamia”
“Wewe kaa nyumbani hapa kwa maana kama ni huo mgahawa si nime ume ufungua kwa pesa yangu?”
“Ndio”
“Basi hata wateja wasipo kuja nita kulipa hicho kiasi unacho ingiza kwa siku”
Nabii Sanga alizdi kujiamini kwani ana nguvu kubwa sana ya pesa ambayo ina muwezesha kumshawishi mtu yoyote kwa kila jambo analo lihitaji.
***

Mrs Sanga hakuweza kumuona mume wake hadi kuna pambazuka. Wasiwasi ukaanza kumjaa kwa maana kila anapo jaribu kumpigia simu, hampati hewani. Mrs Sanga akafikiria ni eneo gani ambalo mke wake ana weza kuwepo, kwani kuondoka na bastola yake jana mchana sio jambo la kawaida.

‘Au atakuwa amekwenda kwa yule malaya wake?’

Mrs Sanga aliwaza huku akijaribu kuunganisha matukio ya siku iliyo pita. Akaikumbuka kauli ya RPC Karata, aliye mshutumu kwa kutembea na msichana mdogo amabye ana mpenda mpenzi wake ambaye ana itwa Evans.

“Pumbavu sana huyu mwanaume”
Mrs Sanga alizungumza huku akikurupuka kitandani hapo. Akaingia bafuni na kuoga haraha haraka, akajiandaa na kuondoka nyumbani hapo kwa kutumia gari lake. Breki yake ya kwanza akafika katika Mgahawa wa Magreth. Akasimisha gari lake kwenye maegesho, aikaitazama saa yake ya mkononi na ina muonyesha ni saa mbili asubuhi.

Akashuka kwenye gari lake hili, huku akiiweka vizuri miwani yake. Akaangaza pande zote za mgahawa huo na kutafuta kiti ambacho hakina mtu na akaketi.

“Karibu sana mama”
“Nashukuru nina weza kupata kifungua kinywa”
“Ndio mama. Vyakula vyetu ni kama hivyo vilivyo andikwa kwenye hiyo menu”
Mrs Sanga akachukua kitabu hicho kilicho andikwa aina ya vyakula. Akachagua chai ya maziwa na yai moja pamoja na chapatti moja. Muhudumu huyo akaondoka na mrs Sanga akaendelea kuchunguza kila mtu anaye ingia na kutoka katika mgahawa huo. Muhudumu huyo akalete akaleta chakula hicho kabla ya kuondoka mrs Sanga akamzuia.

“Samhani, bosi wenu yupo wapi?”
“Aha…hajafika bado”
“Huwa ana fika kazini saa ngapi?”
“Mmmm huwa ni saa kumi na mbili. Ila toka alivyo ondoka jana mchana hakuweza kurudi labda nimuite meneja msaidizi aweze kukupa maelezo zaidi”
“Nitashukuru mwanangu”
Dada huyo akaondoka na baada ya muda akarudi akiwa ameongozana na Juma.

“Mama meneja msaidizi ndio huyu hapa”
“Sawa asante. Samahani kijana”
“Bila samahani mama yangu”
“Bosi wenu Magreth nina weza kumpataje kwa maana hadi sasa hivi nime ambiwa hajafika kazini”
“Ni kweli bosi jana aliondoka na mume wake mida ya mchana na mume wake alikuwa ana umwa”
“Ohoo kwa hiyo leo kuna uwezekano mkubwa wa yeye kuto kufika ofisini?”
“Sijajua kwa maana bado sija wasiliana naye”
“Hambu jaribu kuwasiliana naye ili ikiwezekana niweze kuonana naye kwani nina shida naye muhimu sana”
“Ni shida binafsi au shida ya kiofisi?”
“Ya kiofisi sana.Ila itakuwa ni vizuri sana kama nita zungumza naye mimi mwenyewe”
“Sawa, je nina weza kufahamu shida hiyo katika ofisi ina husian ana nini?”
Mrs Sanga akaka kimya kwa sekunde kadhaa huku akitafakarini ni jambo gani ambalo ana weza kumdanganya kijana huyo.

“Nahitaji kumpa tenda ya kutuletea chakula cha mchana ofisini kwangu. Nina wafanyakazi mia tatu hivyo una weza kuona kwamba ni oda kubwa sana hiyo. Nivyema nika zungumza naye uso kwa uso”
Juma kusikia ofa hiyo akajikuta akipagawa kwa furaha. Akampigia simu Magreth na baada ya sekunde kadhaa simu hiyo ikapokelewa.
“Bosi habari yako”
“Salama Juma vipi hapo kazini”
“Mambo yanakwenda safi sana bosi. Kuna mama mmoja hapa ana hitaji kuonana na wewe, ana hitaji kutupatia tenda ya kuwahudumia wafanyakaiz wake wa kampuni zaidi ya mia tatu”
“Mia tatu kwa kila siku au?”
“Eti mama ni wafanyakazi mia tatu kwa kila sikua au?”
“Ndio kuanzia juma tatu hadi juma mosi”
“Amesema kuanzia juma tatu hadi juma mosi. Hivyo ana hitaji kukutana na wewe ili muweze kuzungumza uso kwa uso ni jinsi gani muna weza kukubaliana juu ya oda hii”
Magrerth akakaa kimya huku akitafakari nini la kumjibu Juma.

“Kutokana leo siwezi kutoka nyumbani. Basi nina kuomba uweze kumleta nyumbani kwangu. Sawa”
“Sawa boss”
Juma akakata simu na kumtazama Mrs Sanga kwa tabasamu pana sana.

“Amesema twende nyumbani kwake. Je una weza kukubaliana na hilo”
“Hakuna tatizo, nina usafiri wangu na tuna weza kwenda.”
Mrs Sanga alizungumza kwa furaha kwani lengo la kwenda kwa Magreth sio hizo oda za chakula kwa wafanyakazi wake. Lengo la kwanza ni kupafahamu kwa adui yake huku akiamini kwa asilimia kubwa sana mume wake ata kuwepo nyumbani kwa Magreth.
ITAENDELEA

Haya sasa Mrs Sanga leo ana kwenda nyumbani kwa Magreth kuonana anaye uso kwa uso, je akimkuta mke wake ni kitu gani ambacho ata kifanya? Endelea kufwatilia kisa hichi cha kusisimua, usikose sehemu ya 52.
 
Mama mchungaji ni mjinga sana,kwa madhambi yake yote bado anapata wivu??
 
SIN 52

Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)

Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188

ILIPOISHIA

“Kutokana leo siwezi kutoka nyumbani. Basi nina kuomba uweze kumleta nyumbani kwangu. Sawa”
“Sawa boss”
Juma akakata simu na kumtazama Mrs Sanga kwa tabasamu pana sana.

“Amesema twende nyumbani kwake. Je una weza kukubaliana na hilo”
“Hakuna tatizo, nina usafiri wangu na tuna weza kwenda.”
Mrs Sanga alizungumza kwa furaha kwani lengo la kwenda kwa Magreth sio hizo oda za chakula kwa wafanyakazi wake. Lengo la kwanza ni kupafahamu kwa adui yake huku akiamini kwa asilimia kubwa sana mume wake ata kuwepo nyumbani kwa Magreth.

ENDELEA

Mrs Sanga wakaingia ndani ya gari hilo na wakaanza kuelekea nyumbani kwa Magreth.
***

“Ni nani umemuambia aje nyumani kwako?”
Nabii Sanga alimuuliza Magreth mara baada ya kutoka sebleni.

“Ni mfanyakazi wangu wa mgahawani alinipigia na kunieleza kuna mteja ana hitaji oda ya chakula katika kampuni yake na ana wafanyakazi mia tatu”
“Waoo ni good deal”
“Yaa ndio maana nime waeleza waweze kufika hapa kwa maana muhusika ana hitaji nizungumze naye uso kwa uso”
“Ni jambo zuri ila sio jambo zuri kumkaribisha mtu usinye mfahamu nyumbani kwako. Chakufanya waambie mukutane kwenye hoteli yoyote hapa Kigamboni, nina imani itakuwa ni jambo zuri na rahisi. Isitoshe mimi pia nipo hapa nyumbani, sinto penda watu waje kunikuta hapa au kukuta gari langu hapa. Umenielewa”
“Nimekuelewa mpenzi”
Magreth akampigia Juma simu na kmuomba waelekee kwenye hoteli ya Double Z na watakutania hapo.

“Sawa bosi”
Juma alijibu na simu ikakatwa. Magreth akaelekea bafuni, akaoga huku kichwa chake kikiwa na mawazo mengi sana juu ya Evans. Anatamani sana kuendelea na mahusiano na Evans, ila kila akikumbuka alipo toka kwenye ufukara wa kutembeza maandazi mtaani, ana jikuta akikata tamaa kabisa ya kuweza kukubaliana na swala la kuwa na Evans kwa mana hatamani kabisa kurudi chini. Magreth akajiandaa vizuri na kutocha chumbani humu. Akamkuta nabii Sanga akitazama kipindi chake kinacho rushwa kwenye televishion.

“Mage hivi kwa nini uliacha kuimba kwaya ya kanisani kwangu?”
“Mmmm kipindi kile majukumu yalikuwa ni mengi. Biashara ilikuwa ngumu sana, hivyo utakuta nikitoka kutembeza maandazi huwa nina choka sana na mwishowe nikaona hakuna jinsi zaidi ya kuachana na kazi hiyo”
“Basi wewe nenda huko alafu ukirudi tuzungumze juu ya swala la kuimba kwako. Natamani kukuona ukiimba wewe kama wewe, ukatoa albamu zako na kuuza, hiyo itakuwa ni njia moja yawapo nzuri ya kukuza kipawa chako, jina lako na ukazidi kutanuka kiuchumi”
Maneno ya nabii Sanga yakaanza kumfurahisha Magreth ambaye kwa sasa tamaa ya umaarufu na pesa ndio vimemkaa moyoni kuliko hata upendo wa dhati kati ya nabii Sanga na Evans.

“Sawa mume wangu”
Magreth akambusu nabii Sanga mdomoni mwake kisha akatoka ndani humu. Akingia ndani ya gari lake na kuianza safari ya kuelekea katika hoteli hiyo.

Mrs Sanga akambidi kukubaliana na ombi la Juma, wakafika katika hoteli hiyo, wakakaa sehemu nzuri na kuagizia vinjwaji.
“Pale kwenye mgahawa wenu kwa siku muna weza kupata wateja wangapi?”
“Mmmm….wengi sana”
“Kwa kukadiria wana weza kufika wangapi?”
“Elfu moja na miatano hadi elfu mbili.”
“Aisee kumbe muna watu wengi hivyo?”
“Yaa kuna kipindi wana kuwa hawatoshi pale. Hivyo nina mpango wa kumshauri boss kununya sehemu ya juu katika lile gorofa, ili kama ni watejawengine basi waweze kukaa juu”
“Ni kweli, kwa idadi hiyo ya wateja ina bidi kuongeza eneo”
“Yaa”
“Je mume wa bossi wako una mfahamu?”
“Ndio nina mfahamu ni kijana mmoja hivi. Jamaa yupo very smart na endapo boss ata endelea kuwa na yule jamaa basi nina asilimia mia moja wata fika mbali sana”
Simu ya Juma ika ita, akaitazama na kukuta ni Magreth, akaipokea na kumuelekeza sehemu walipo kaa. Magreth akaingia ndani ya hotele hiyo, akaanza kuelekea sehemu alipo kaa Juma na mwana mama huyo aliye mpa mgogo na kushindwa kuiona sura yake. Magreth akafika sehemu hiyo, akamsalimia Juma kwa furaha, kitendo cha kukutanisha macho yake na mrs Sanga, akastuka kidogo hadi Juma akahisi kuna jambo.

“Habari yako binti?”
Mrs Sanga alianza kusalimia huku akitengeneza sura iliyo jaa tabasamu pana usoni mwake. Magreth akabaki akiwa amesimama huku akiwa amejaa na mshangao, kwani ana mfahamu mrs Sanga vizuri sana.

“Bosi una salimiwa au kuna tatizo”
“Aha…ha…hapana. Salama”
Magreth alishikwa na kigugumizi.

“Karibu ukae”
Mrs Sanga alizungumza na taratibu Magreth akakaa hukua kimtazama mrs Sanga usoni mwake.

“Kijana una weza kutupisha nika zungumza na bossi wako?”
“Ndio hakuna shaka”
Simu ya Magreth ikaanza kuita, akaitoa kwenye pochi yake. Akaona jina la dada Vivian, akaitazama kwa sekunde simu hiyo kisha akaipokea.
“Mage habari yako”
“Salama dada”
“Mbona upo kimya toka juzi huja tujibu, kuna tatizo?”
“Nisamehe sana dada yangu, mume wangu alipata ajali. Ila nitakupigia nina kikao kidogo hapa”
“Ohoo pole sana ana endeleaje?”
“Ana endelea vizuri. Mungu ana saidia”
“Sawa hakikisha leo una wasiliana na mimi kwa maana baba ana ulizia ume fikia wapi, hivyo nina shindwa kumpatia jibu”
“Usijali dada yangu”

Magreth akakata simu na kutazamana na mrs Sanga ambaye sura yake iliyo kuwa na tabasamu ime potea. Magreth akashusha pumzi kidogo na kujiamini kwa kujibu chochote ambacho ata ulizwa na mwana mama huyo.

“Nimekuja kwa jambo moja tu na nina hitaji uni sikilize vizuri wewe mwanamke. Achana na mume wangu na endapo uta endelea naye nita kuua kwa mkono wangu mimi mwenyewe ume nilewa?”
Mrs Sanga alizungumza kwa sauti ya chini iliyo jaa msisitizo na wao wawili tu ndio wana weza kuisikia.

“Hahaaaa….samahani. Umechanganyikiwa mama?”
“Sijachanganyikiwa, nina ushidi wa wewe kutembea na mume wangu. Sasa achana naye na kama una hisi kwamba uta endelea kuvuna pesa za familia yangu. Haki ya Mungu tambua kwamba ume kosea kuingia kwa mwanaume wa mtu. Leo nina zungumza ila siku nyingine nita ongea kwa vitendo”
Magreth akatabasamu huku akimtazama Juma aliye kaa meza ya pili kutoka hapo walipo keti.
“Hivi unajua kwamba sikuogopi. Pili hivi una tambua kwmaba mimi ndio niliye warekodi mukifanya uchafu ofisini kwa mume wako tena kanisani. Unajua ile video bado ninayo kwenye simu yangu ya zamani. Hivi una tambua nikihitaju kuisambaza mitandaoni jinsi ulivyo kuwa ukifir** na Tomas dunia nzima ita jua uozo wa maisha yako. So usinitishe kama ni kisu mimi nimeshika mpini na wewe na mumeo mume shika makali, nikihitaji kuvuta basi muta poromoka kama embe linavyo toka juu na kuanguka chini. Sawa mrs Sanga”
Magreth alizungumza kwa kujiamini huku akimkazia macho mrs Sanga aliye anza kumwagikwa na jasho huku wasiwasi mwingi ukiwa ume mjaa. Hakuwahi kuwazia kama binti huyo ambaye kipindi cha nyuma amekuwa ni muumini wa hali ya chini, leo hii ana mtisha kiasi hicho.

“Kutokana ulimteka mume wako wewe mwenyewe. Basi nina kueleza ukweli, nita mchuna hadi pale nitakapo ridhika na pesa atakazo kuwa amenipatia kisha nitakurudishia makapi. Siku nyingine usije kijinga jinga nita kufundisha adabu na ole wako ujidanganye kutuma watu kama ulivyo mtumia mume wako. Yaani kabla hawajaniteka na kuniua basi video yenu itakuwa hewani”

“U…u…n….a…j…ia…mini nini wewe”
Mrs Sanga alizungumza huku akiwa amejawa na kigugumizi kikali sana. Magreth akaingia kwenye akaunti yake ya google drive alipo hifadhia video hiyo, akaipakua na kumuonyesha mrs Sanga aliye jikuta akizidi kutetemeka kwa woga.

“Hichi ndicho ninacho jiaminia. Sasa wewe nikanyage bahati mbaya mimi nikulipue makusudi. Sitishiki kijinga na wala usipate shida ya kuhangaika kuhisi kwamba nina tembea na mume wako. Ninakudhibitishia kwamba nina tembea na mumeo tena na nina muamrisha vile nipendavyo sasa ngoja nikapandikize sumu ya kukuacha alafu uone kama utaendelea kubaki nyumbani kwake. Mjinga wewe”
Magreth mara baada ya kuzungumza hivyo akaiingiza simu yake ndani ya pochi. Akanyanyuka na kumtazama mrs Sanga anaye kabiribia kupandwa na presha.
“Kamalizane kwanza na kesi yako polisi, au unataka nimuonge RPC akupeleke ndani ukapotelee huko. Eheeee? Nikutakie siku njema”
Magreth mara baada ya kuzungumza maneno hayo, akampa ishara Juma na wakatoka hotelini hapo na kumuacha mrs Sanga akihisi moyo wake ukipasuka kwa presha.

“Vipi bosi mume kubaliana?”
“Mpumbavu yule mama”
Magreth alijibu kwa hasira hukua kifungua mlango wa gari lake na kuingia ndani. Juma akazuguka upande wa pili na kupanda.

“Mpumbavu kivipi?”
“Ananiambia ohoo achana na mume wangu, sijui vimepanda na kushuka. Sasa mimi pale kwenye mgahawa ni wanaume wangapi nina zungumza nao kwa urafiki. Sasa sijui ana nichukuliaje na siku nyingine akija pale kwenye mhahawa. Hakuna kumuhudumia”
“Sawa bosi nime kuelewa”
“Jana mume ingiza kiasi gani?”
“Mulio kumi na moja”
“Moja iache ofisini, hizo kumi chukua gari ukaniletee.”
“Sawa mkuu”
Magreth akafika nyumbani kwake. Akamkabidhi Juma gari lake kisha kish yeye akaingia ndani, Juma akaondoka na kuelekea mgahawani.

“Mbona ume kasirika?”
“Si limke lako lina kuja kunitisha oohoo achana na mume wangu. Nilijua ni mtu wa maana kumbe ananiletea mambo yake ya kifala hapa”
Magreth alifoka hadi nabii Sanga akajawa na mshangao.
“Mke wangu?”
“Ndio kwani na wewe una wake wangapi bwana. Nisikilize kitu kimoja Sanga, japo nina kipenda sana ila maisha ya kuishi kwa vitisho na kutishiwa tishiwa siyataki. Kama una shindwa kumuhimili huyo mke wako niambie kabisa nitafute ustarabu wangu. Umasikini wangu na kupokea hizi mali zako isiwe chanzo cha mimi kuingia kaburini ikiwa hata miaka thelathini sijafikisha. Umenielewa?”
Magreth alizidi kufoka huku machozi yakianza kumwagika usoni mwake. Nabii Sanga akahisi kama kichwa kinalipuka kwa hasira ya gafla aliyo ipata. Hakutarajia kama ipo siku mke wake ana weza kukutana na Magreth.
“Ume muacha wapi?”
“Mpigie bwana mke wako ata kuambia yupo wapi? Alafu unisikilize jambo moja na wewe. Nipo tayari kurudi kwenye kachumba kamoja na kuuza maandazi kwani huo ndio urithi alio niachia mama yangu. Musininyanyase kwa pesa zenu umenielewa”
Nabii Sanga katika kipindi chote hakuwahi kumuona Magreth akiwa katika hali ya hasira kama hiyo. Nabii Sanga akaingia chumbani, akavaa nguo zake haraka haraka, akaichukua bastola yake na kutoka chumbani hapo.
“Kama utashindwa kuachana na mke wako. Tafadhali nina kuomba usirudi hapa nyumbani kwangu tena”
Maneno ya Magreth yakamfanya nabii Sanga kumtazama kwa sekunde kadhaa kisha akatoka nje. Akaelekea kwenye duka la jirani alipo liacha gari lake. Akaitafuta namba ya mke wake na kumpigia, simu ya mrs Sanga ikaita kwa muda na kukatika. Akapiga tena na simu ikakatwa jambo lililozidi kumfanya nabii Sanga kujawa na hasira kali sana.

‘Huyu malaya hanitambui mimi leo ni lazima nimuue kwa maana ana niiingilia sana kwenye raha zangu’

Nabii Sanga alizungumza hukua akiondoka kwa kasi eneo hilo hadi muuza duka akamabaki na mshangao mkubwa.
***

Julieth akafanikiwa kulitoa gari lake polisi, kutokana eneo la mbele limepata itilafu, akamkabidhi mwanasheria wa familia yao kulipitisha gereji huku naye akilitumia gari la mwanasheria huyo kuelekea hotelini alipo Evans. Simu yake ikaanza kuita, akaitoa kwenye mfuko wa suruali yake na kukuta ni mama yake ndio anaye mpigia. Akaipokea na kuweka loud speaker. Julieth akastuka mara baada ya kusikia sauti ya mama yake akilia.

“Mama”

Julieth aliita huku akipunguza mwendo wa gari hilo na kulisimamisha pembeni ya barabara.

“Mama una nini?”
Sauti ya Mrs Sanga ikaka jambo lililo zidi kumfanya Magreth kuchanyikiwa sana kwani hakuwahi kumsikia mama yake akilia kwa uchungu kiasi hicho.

Julieth akakata simu huku machozi yakimlenga lenga, akampigia tena mama yake, simu yake ikaanza kuita na ikakata. Akapiga tena huku jasho likianza kumwagika usoni mwake, simu ikapokelewa na suati ya mwanaume.
“Wewe ni nani uliye pokea simu ya mama yangu?”

Julietha liuliza kwa msisitizo huku akiwa amejawa na wasiwasi mwingi sana.
“Mimii ni msamaria mwema, mama yako amepata ajali hapa Kigamboni na gari lake limedumbukia kwenye mtaro na hapa wasamaria wema tuna jitahidi kumukoa”
“A…a….h…me….pata aj…ali?”
“Ndio na hali yake sio nzuri kabisa”
Julieth akajikuta akiponyokwa na simu yake mkononi. Machozi yakaanza kumbubujika mashavuni mwake na kujikuta akishindwa hata kuendesha gari hilo kwani nguvu zote za mwili zimemuishia.
ITAENDELEA

Haya sasa Julieth amapeta taarifa ya mama yake kupata ajali, nini chanzo cha ajali ya mrs Sanga na je nabii Sanga ata mfundisha mke wake adabu ? Endelea kufwatilia kisa hichi cha kusisimua, usikose sehemu ya 53.
 
SIN 53


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188

ILIPOISHIA

Julieth akakata simu huku machozi yakimlenga lenga, akampigia tena mama yake, simu yake ikaanza kuita na ikakata. Akapiga tena huku jasho likianza kumwagika usoni mwake, simu ikapokelewa na suati ya mwanaume.
“Wewe ni nani uliye pokea simu ya mama yangu?”

Julietha liuliza kwa msisitizo huku akiwa amejawa na wasiwasi mwingi sana.
“Mimii ni msamaria mwema, mama yako amepata ajali hapa Kigamboni na gari lake limedumbukia kwenye mtaro na hapa wasamaria wema tuna jitahidi kumukoa”
“A…a….h…me….pata aj…ali?”
“Ndio na hali yake sio nzuri kabisa”
Julieth akajikuta akiponyokwa na simu yake mkononi. Machozi yakaanza kumbubujika mashavuni mwake na kujikuta akishindwa hata kuendesha gari hilo kwani nguvu zote za mwili zimemuishia.

ENDELEA

Julieth taratibu akajipangusa machozi yake. Akaitazama simu yake iliyo aguka pembeni yake. Akaiokota, akaitafuta namba ya mama yake na kumpigia. Majibu ya kuto kupatikana kwa simu ya mama yake yakazidi kumchanganya sana Julieth kwani hatambu ni wapi atakuwepo mamayake.
***

Mrs Sanga akakaa kwa sekunde kadhaa hotelini hapo huku akitafakari aliyo ambiwa na Magreth. Woga ulio changanyika na mawazo mengi sana ukamfanya kichwa chake kuanza kuuma. Taratibu akanyanyuka huku akibebe pochi yake, akaanza kutembea kwa mwendo wa taratibu huku akilini mwake akiwazia video inayo milikiwa na Magreth, endapo ita samba ulimwenguni, basi hato jua ni wapi aiweke sura yake.

“Samahani mama, umesahau kunipatia pesa ya vinywaji”
Muhudumu aliye wahudumia vinywaji alimsimamisha mrs Sanga. Taratibu akafungua pochi yake na kutoa noti ya shilingi elfu kumi na kumpatia muhudumu huyo. Hakujali kuhusiana na chenchi iliyo salia katika kiwango hicho cha pesa. Akatoka nje na kuingia kweye gari lake. Mrs Sanga akaanza kuondoka eneo hilo huku akiliendesha gari lake kwa mwendo wa taratibu sana. Mawazo ya ajali aliyo ipata siku iliyo pita, bado ana yakumbuka vizuri sana. Simu yake ikaanza kuita, akaitazama na kukuta ni simu ya mume wake, mapigo ya moyo yakazidi kumuenda kasi kwa maana ana amini kwa asilimi kubwa, mazungumzo yote aliyo zungumza na Magreth ameweza kuelezwa. Mrs Sanga hakuona haja ya kuweza kuipokea simu hiyo, akakata, ikapigwa kwa mara nyingine, akakata. Hazikupita hata dakika mbili ukaingia ujumbe wa meseji, akaufungua na kuusoma.

‘NIMEKUVUMILIA VYA KUTOSHA SASA LEO NITAKUONYESHA MALAYA WEWE’

Ujumbe huo kutoka kwa nabii Sanga ukamfanya Mrs Sanga kuzidi kuchanganyikiwa, maumivu ya kichwa yakazidi kuongezeka huku yakiambatana na kizunguzungu kikali sana. Mrs Sanga akajikuta akiachia mskani wa gari hilo huku akiishika kichwa chake. Gafla akastukikia gari lake likitoka barabarani na kuingia kwenye mtaro mkubwa ulipo pembezoni mwa barabara hiyo. Gari hilo likaserereka huku mrs Sanga akipiga kelele za kumuta Mungu wake. Gari likagonga kwenye karabati na kusimama. Mrs Sanga akazidi kupandwa na presha, akaichukua simu yake na kumpigia Julieth huku akilia kwa woga mwingi sana. Simu yake ikapokelewa, mrs Sanga akatamani kuzungumza jambo ila kashindwa na kujikuta akilia huku damu zikimwagika usoni mwake, kioo cha mbele kime pasuka. Wasamaria wema wakiwemo waendesha pipikipin a bajaji walio kuwa katika eneo la barabara hiyo wakawahi eneo la tukio. Wakaanza kusaidiana kumtoa mrs Sanga katika gari hilo.
“Huu mama nina mfahamu, ni mke wa nabii Sanga”
Mwenyekiti wa waendesha pikipiki hao alizungumza huku akimtazama mrs Sanga aliye poteza fahamu.
“Tumuwahisheni hospitalini”
Muendesha bajaji mwengine alizungumza.
“Oya hakuna kibaka yoyoye kusogelea gari. Yaani hapa kikiondoka hata kioo cha pembeni ya hili gari tuna dili na vibaka woten na muna tujua kwa maana tuta wasaka”
Mwenyekiti huyo aliuzungumza huku akiwatazama vijana wawili ambao ni wavuta bangi. Mwenyekiti hiyo akainga ndani ya gari hilo, akatoa simu pamoja na pochi ua mrs Sanga. Simu ya mrs Sanga ikaanza kuita, namba hiyo inayo ita ime andikwa my dauther, ikimaanisha ni mtoto wa kike wa mrs Sanga. Akaipokea na kuzungumza na binti huyo. Muendesha taksi mmoja akaileta taksi yake eneo la tukio, wakamuingiza mrs Sanga katika siti ya nyuma, mwenyekiti huyo akaingia hukua kiwaagiza vijana wake kuhakikisha wana imarisha ulinzi katika eneo hilo hadi pale polisi watakapo fika.

“Ila gari ya huyu mama haikuwa kwenye mwendo wa kasi, yaani sijui imekuwaje ame pata ajali?”
Dereva taksi huyo alizungumza huku akiongeza mwendo kasi wa gari lake.

“Ladba kuta kuwa na hali fulani ime mkumba ndani ya gari kwa maana hata mimi nime shuhudia jinsi akidumbukia kwenye mtarao ule”
“Au emelewa?”
“Hapana huyu ni mwana mama nina mfahamu ni mwema sana mume wake ni yule nabii Sanga.”
“Ahaa yule nabii anaye fanya fanya miujiziza ya kuponya watu?”
“Yaa huyo huyo”
“Aisee sasa sijio ame kubwa na nini mama wa watu?”
“Duu simu yake ime zima chaji sasa sijui familia yake tuta wasiliana nayo vipi”

Mwenyekiti huyo anaye julikana kwa jina la Ngoko alizungumza huku akiitazama simu hiyo ya mrs Sanga ambayo alikuwa ana wasiliana na mtoto wa mrs Sanga.

“Duu sasa una uta wasiliana naye vipi?”
“Ninayo namba ya mume wake acha ni mpigie”
“Sawa”
Ngoko akaitafuta namba ya nabii Sanga na kumpigia, simu ikaanza kuita na kumfanya ageuke nyuma na kumtazama mrs Sanga aliyepoteza fahamu.
***

Nabii Sanga mara baada ya kumtumia mke wake meseji ya vitisho, akazidi kuongeza mwendo wa gari lake kuelekea nyumbani kwake. Akiamini kwa asilimia mia moja ata mkuta nyumbani mke wake. Simu yake ikaanza kuita, akaitazama kwa sekunde kadhaa na kukuta ni namba ngeni. Akataka kuikata ila aka ipokea.

“Ndio”
“Habari yako nabii Sanga”
“Salam nani?”
“Nina itwa Ngoko ni miongoni mwa waaumini wa kanisa kalo”
“Una hitaji nini/’

‘Nabi Sanga hapa ninavyo zungumza nina muwahisha mke wako hospitalini. Amepata ajali ya gari na hali yake sio nzuri kabisa.”
Nabii Sanga akafunga breki za gafla za gafla na kuzifanya tairi za nyuma kuserereka barabarani hadi baadhi ya watu walipo eneo hili wakajawa na mshangao mkubwa.
“Amepata ajali wapi huku Kigamboni?”
“Sasa mpelekeni Agakhan niwakut hapo”
“Sawa mchunguji?”
“Nashukuru”
Nabii Sanga akakata simu, kwa haraka akageuza gari lake na kunza kuelekea eneo la hopistali ya Agakhan. Kutokaa na foleni za hapa na pale, ikamchukua nusu saa kufika hospitalini hapo. Ngosha mara abada ya kumuona
nabii Sanga akamfwata na kusalimiana naye.

“Mimi ndio nilite kupigia Nabii”

Ngosha alizungumza kwa unyenyekevu huku akimtazama nabii Sanga.
“Ahaa..shukrani sana ndugu Mungu azidi kukubariki”
“Hii ni simu ya mama pamoja na pochi yake, ni vitu mihimu ambavyo niliona nivitoe kwenye gari”
“Ohoo Mungu akubariki, je hali ya mgonjwa ina endeleaje?”
“Tumewakabidhi madaktari na hadi sasa hivi bado hatujapata jibu. Ila wata kueleza”
Nabii Sanga akaongozana na Ngosha pamoja na muendesha taksi huyo hadi kwenye eneo la chumba anacho fanyiwa matubabu mrs Sanga.
“Nabii nilikuwa nina zungumza na mwanao. Simu ya maam ilikata chaji, hivyo sikumpatia taarifa kamili kwamba ni wapi mama alipo, ila nilifanikiwa kumueleza kwamba mama amaepata ajali”
“Asante sana”
Nabii Sanga akampigia simu Julieth na kumueleza wapo hospitali ya Agakhan na kama ni kufika basi afike haraka sana. Baada ya dakika kumi mlango wa chumba hicho ukafunguliwa na akatoka nesi wa kihindi aliye valia sketi fupi.

“Nesi hali ya mke wangu ina endeleaje?”
“Bado tupo kwenye matibabu, kwa sasa sina la kuzungumza. Samahani”
Nesi huyo baada ya kuzungumza maneno hayo, akaanza kutembea kwa kasi kwenye kordo hiyo na kumuacha nabii Sanga na wezake wakimsindikiza kwa macho tu. Julieth mara baada ya kufika eneo hilo, akaelekezwa na baba yake ni wapi alipo. Julieth akafika eneo hilo na kuwasalimia Ngosha na dereva taksi huyo.

“Mama amepatwa na nini?”
“Kwamaelezo ya hawa vijana walio msaidia ni kwamba amepata ajali. Gari liliingia kwenye mtaro”
“Kwani alikuwa kasi kaka?”
“Hapana alikuwa kwenye mendo wa kawaida sana ambao hatujui ni kitu gani ambacho kilitokea hadi akazama ndani ya mtaro”
“Katika kama hichi hakikisha mama yako huwa aendeshi gari. Ile ajali ya jana nina imani kwmaba bado ina mtafuna akilini mwake.”
“Sawa baba”
“Vijana muna jishuhulisha na nini?”
“Mimi ni dereva pikipiki na huyu mwenzangu ni dereva taksi”
“Kwa kweli nina washukuru sana kwa kila jambo ambalo mume lifanya kwaa mke wangu. Kesho asubuhi nina omba muweze kufika pale kanisani kwangu, kidogo niwapatie kazawadi”
“Tunashukuru sana nabii”

Nabii Sanga akatoa laki mbli na kuwakabidhi.

“Hiyo ni pesa ya mafuta. Ila kesho musikose mida ya saa nne nne kufika ofisini kwangu”
“Tuna shukuru sana nabii”
Ngosha na rafiki yake wakaondoka na kurudi maskani kwao.
“Umefanikiwa kutoa gari lako?”
“Ndio”
“Lipo wapi?”
“Nime mkabidhi mwana sheria alipeleke gereji. Hapa nimekuja na gari lake”
Nabii Sanga na mke wake wakaka eneo hilo kwa zaidi ya lisaa moja na mrs Sanga akatolewa na kupelekwa chumba cha wagonjwa mahututi.


“Dokta ni kitu gani kinacho msumbua mke wangu?”
“Ni mstuko wa moyo ambao tume jitahidi kwa kadri ya uwezo wetu tume hakikisha kwamba hali yake tuna iweka sawa. Je kuna jambo ambalo ni baya lilimpata na kumpelekea kuwa katika wasiwasi?”
“Ndio jana aligonga muendesha pikipiki”
“Basi hakikisheni kwamba muna muweka mbali sana na maswala ya magari na jambo jengine hakikiesheni kwamba hapewi habari za kustukiza, lazima kabla ya kuwepa habari apatiwe muda kidogo ili asipate hilo tatizo la mstuko wa moyo. Mambo mengine tuta endelea kuwaeleza taratibu taratibu”
Daktari huyo wa mwenye asili ya Kihindi aliwaeleza nabii Sanga na Julireth ambao wote wapo kwenye chumba hicho, wakishuhudia jinsi mrs Sanga anavyo hema kwa kutumia mashine maalumu za oksijeni.
“Sawa dokta je kuna tatizo jengine lililo sababishwa na ajali hiyo?”
“Madhara ya ajali ni huko kukatwa na kioo kidogo hapo usoni. Ila hakuna madhara mengine zaidi ya hayo”
“Sawa sawa dokta tuna shukuru”
“Muna dakika tano za kumtazama kisha mutoke”
“Tuna shukuru”
Baada ya daktari huyo kutoka, nabii Sanga akaanza kumuombea mke wake huku wakishirikiana na Julieth. Walipo maliza kusali wakatoka nje ya chumba hicho.

“Kwa nini una msaliti mama yangu?”
Swali la Julieth likamstua sana nabii Sanga kwa maana hakutarajia kulisikia swali kama hilo tena kuto kwa mwanaye wa mwisho ambaye ana mpenda kuliko hata watoto wake wa kwanza wa kiume.

“Nani ame kuambia nina msaliti mama yako?”
Julieth akamtazama baba yake kwa macho ya hasira sana. Machozi yakaanza kumwagika pasipo kulia, ikionyesha ni ishara ya maumivu makali sana ambayo yana toka moyoni mwake.
“Ulishindwa kumuajiri hadi ukaamua kumfungulia Mgahawa tena kwa pesa za familia eheeee?”
Nabii Sanga akazidi kujawa na maswali mfululizo na mshangao, kwani habari hizo anazo zisikia mtoto wake hakupaswa kabisa kuweza kuzifahamu.
“Na…nani nime mfungulia mgahawa?”
“Baba wewe ni mtumishi wa Mungu. Kama una ficha hilo jambo kwa waumini wako, ila tambua Mungu humfichi chochote. Mungu ana ona hadi ndani yako. Angalia baba yangu usije ukamuua mama yangu kwa maradhi. Nina jua kila jambo unalo lifanya na Magreth na hadi jana mama kumgonga yule muendesha pikipiki chanzo ni sisi kufahamu kwamba mupo Bagamoyo hotelini na pale tulikuwa kwenye gari tuna kuja kuwafumania huko. Baba nina mambo yako mengi sana. Tafadhali usi mtese mama yangu”
Nabii akahisi nguvu zikimuishia, taratibu akaka kwenye benchi lililopp nje ya chumba hicho. Julieth akaka huku akijifuta machozi usoni mwake.
“Mama yangu ana pitia kipindi kigumu sana. Anapitia mateso makali sana ambayo hastahili kupitia. Nina imani kwamba hata kuendesha kwake gari taratibu na kulizamisha kwenye mtaro chanzo ni uchafu wako baba kwa nini una kuwa hivyo?”
“Juliy mwanangu”
“Beee?”
“Mama yako yeye ndio ame ifikisha hii familia hapa”
Nabii Sanga alizungumza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake.
“Kivipi ikiwa wewe kiongozi una fanya mambo kama haya. Baba wewe ndio umefikisha hii familia hapa na wala sio mama. Mama alikuwa amesimama asilimia mia moja kwenye dini, ila wewe baba ndio ulimtoa kwenye uwepo huo. Ngoja nikuambie siri ambayo wewe hujui kama mimi nina ijua”
Nabii Sanga akamtazama Julieth kwa mshangao huku akisubiri kuifahamu siri hiyo. Julieth akajipangusa machozi kwa kutumia leso kisha akamtazama baba yake huku macho yakiwa yamejawa na uwekundu utokanao na kulia.
“Mule ndani mimi ndio mtu wa kwanza kugundua kwamba wewe ulifanya mapenzi na yule kijana wa kiume kutoka nchini Nigeria. Baba niliumia sana kwa maana nilisha anza kumpenda yule kijana bila ya wewe kukueleza ukweli. Ila nipo kuona una muingilia kinyume na maumbile, niliumia na kukiri kwamba sinto kuja kukaa na kupenda tena maishani mwangu. Mama alipo shuhudia lile jambo alipoteza hadi fahamu kwa maumivu. Kuanzia pale baba mama hakuwa tayari kukusujudia kwa uchafu ulio ufanya na ndio maana alifanya kile alicho kifanya.”
Maneno ya Julieth yakamfanya nabii Sanga kuanza kutetemeka mwili mzima huku woga ukiwa umemtawala. Siku zote alihisi kwamba siri hiyo ana ifahamu mke wake pekee.

“Hii siri sikuwahi kumueleza mtu yoyote zaidi yako wewe. Sijawaambia kaka zangu kwa sababu sikuhitaji kuisambaratisha familia yangu.Baba”
“Na…anammm”
“Sinto kuja kukaa na kuona familia yangu ina sambaratika kwa ajili ya malaya mmoja ambaye ki umri amenipita sijui ni miaka miwili tu. Yule Magreth unaye tembea naye ni sawa na mwanao baba, hamfikii hata kaka yanu wapili.”
Julieth alizungumza kwa msisitizo huku akilia kwa uchungu mwingi sana.

“Sasa baba ni hivi. Chukua simu yako sasa hivi na umpigie yule malaya Magreth na umueleza kwamba wewe na yeye basii. Usipo fanya hivyo ninaapa kwa Mungu, haki ya Mungu baba nitakwenda kuzitoa siri zako zote kwa kaka zangu na ukiwa mbishi wakuelewa. Nitawaambia waumini wako mauvu yako moja baada ya jengine ambayo umeyafanya ikiwemo kutumia nguvu za giza katika utumishi wako”
Julieth alizungumza huku macho yakiwa yamemtoka kwa hasira, nabii Sanga akahisi moyo wake una pasuka kwa sharti hilo alilo pewa na Julieth, mtoto anaye mpenda kuliko kitu chochote kwenye maisha yake.
ITAENDELEA

Haya sasa nabii Sanga amepewa sharti ambalo limemuacha njia panda, je achague familia na siri zake zibaki ndnai ya familia au amchague Magreth? Endelea kufwatilia kisa hichi cha kusisimua, usikose sehemu ya 54.
 
Daah kumekucha.

Sio mchezo.

Nilichojifunza ni kwamba matatizo hayalundikwi yanatatuliwa, unalundika lundika siku moja likitoka nje yanatoka yote hapo ndo utaiona kumbe hii dunia ni ndogo sana huna pa kujificha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Story Kali sana sema inaanza kuboa uwasilishwaji wake viepisode vifup alaf moja to siop poa
 
Story Kali sana sema inaanza kuboa uwasilishwaji wake viepisode vifup alaf moja to siop poa
Mkuu hii ni ya kujitolea kama una haraka wasiliana na mtunzi umlipe atakupa yote. Niliahid ntatuma kila siku na natuma kila siku siku nikimis nafidia siku inayofata
 
Back
Top Bottom