SIN 219
Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)
Age ……………………………………………………18+
Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188
Website………………………………………………
www.storyzaeddytz.com
ILIPOISHIA
“We…e.ww…eee ni nani hadi una nivua madaraka?”
“Mkuu sio mimi ila katiba ina nielekeza kama raisi ata shindwa kutoa amri katika kipindi ambacho jeshi lina hitaji kuingia vitani basi huna sifa ya kuongoza kwa kipindi hicho. Tafadhali kuna watu na wageni wengi waliopo hapa ikulu hivyo nina kuomba ujiheshimu katika hilo la sivyo vijana wangu wata tumia nguvu.”
Raisi Mtenzi akamtazama jenerali wa jeshi kwa macho makali na yaliyo jaa hasira. Akanyanyuka taratibu na akatoa simu yake mfukoni na kumkabidhi jenerali wa jeshi na taratibu akatoka ofisini hapo huku wanajeshi hao wawili wakihakikisha hazungumzi na mtu yoyote wala kuingia sehemu yoyote hadi katika chumba maalumu ambacho ata kaa humo hadi pale oparesheni ya kuwaondoa wanajeshi wasio julikana itakapo kishwa ndani ya nchi.
ENDELEA
Jenerali wa jeshi akamtazama mr the Brain kwa sekunde kadhaa kisha akatoka ofisini hapo na kurudi katika ukumbi huo.
“Tusikilizane”
Jenerali wa jeshi alizungumza na watu wote wakaa kimya kumsikiliza. Kijana wake mmoja akachukua bibilia pamoja na bibilia kwa ajili ya kumuapisha kuchukua nafasi ya muda kuongoza nchi. Watu wote waka simama huku wafanyakazi wengine wakiwa wana jiuliza kimoyo moyo ni wapi alipo raisi Mtenzi. Jenerali wa jeshi akala kiapo hicho na akawa raisi wa muda. Baada ya zoezi hili kuisha jenerali akakakwenye kiti ambacho ana kaa raisi peke yake wakiwa ndani ya chumba hicho.
“Nchi kwa sasa ime weza kuvamiwa na maadui. Hatuwezi kufumbia macho hawa maadui wanao endelea kuivamia hii nchi na jeshi likiwepo. Niwahakikishie jambo moja tu. Tuta wapiga tena tuna wapiga kipigo cha mbwa Koko.”
Jenerali alizungumza huku wakuu wa majeshi wa kambi zote nchini Tanzania wakiwa wana fwalilia kikao hicho kwa kupitia mfumo wa video call.
“Muna jua ni nini cha kufanya. Wanajeshi wote ambao wame ingia nchini Tanzania waanze ushambuliwa sasa hivi”
“Sawa mkuu”
Wakuu wa kambi zote za jeshi wakajibu kwa pamoja na shuhuli ya kuwasaka wanajeshi ambao hadi sasa hawajajuliakana kama ni wa nabii Sanga ikaanza.
***
“Raisi Mtenzi amepigwa chini”
Samson alizungumza huku uso wake ukiwa ume tawaliwa na tabasamu pana sana.
“Una maanisha nini?”
Josephine aliuliza huku macho yame mtoka.
“Niliweza kumtumia rafiki yangu ninaye fanya naye kazi pale ikulu video zile za wale wanajeshi wa nabii Sanga na aliweza kuziweka hadharani na ameniambia kwamba jenerali wa jeshi alihitaji kuanza kufanya mashabulizi kwa wanajeshi hao ila raisi Mtenzi akwa hatoa amri. Hivyo jenerali wa jensi ame weza kuongoza nchi kwa muda hadi pale watakapp waua wanajeshi wote walio vamia nchi”
“Ime wezekana vipi kwa raisi kutolewa madarakani?”
Magreth alihoji.
“Ina wezekana na katiba ina mruhusu jenerali wa jeshi kuchukua madaraka kwa muda pale tu raisi anapo onyesha ana lege lega kutoa maamuzi hususani pale nchi inapo kuwa katika wakati wa kuvamiwa. Hivyo adui yetu sasa tuna weza kumpiga mbele na nyuma”
Samson alizungumza kwa kujiamini.
“Aisee Mungu ni mwema. Ata sikiliakilio chetu”
“Ndio hivyo sister Josephine”
“Jenerali wa jeshi ni rafiki wa baba mzuri tu. Je nina weza kuonana naye?”
Cleopatra alizungumza huku akiwatazama wezake.
“Una taka kuonana naye umuambie nini?”
“Nimpe picha halisi kwamba wanajeshi hao ni wa nabii Sanga na pia nina hitaji kuwafutia nyinyi makosa na muweze kutoka nje tena na kufanya kazi kama kawaida”
“Hilo ni wazo zuri. Cleopatra ana weza kusafisha majina yetu na adui yetu akakamatwa na kusekwa ndani”
Evans naye alishauri.
Josephine akatafakari kwa muda kisha akamtazama Cleopatra usoni mwake.
“Una weza kwenda ila ina bidi kuzungumza na RPC Karata kwanza. Mage mpigie RPC”
“Sawa”
Magreth akampigia RPC Karata na kumueleza mpango wake na RPC Karata akamtuma mlinzi wake kwa ajili ya kumchukua Cleopatra.
“Cleopatra nina kuomba ukawe very smart utakapo kutana na jenerali wa jeshi. Tuna hitaji kuwa hurukwa maana hatuna makosa ambayo yana weza kutufanya kuwa katika hali kama hii”
“Musijali nina elewa kila kitu”
“Jamani nime weza kupata location ya meli ya nabii Sanga ilipo”
Samson alizungumza huku akiendelea kuminya minya laptop yake na watu waote wakatazama laptop hiyo.
“Vizuri niingizie hiyo location kwenye simu yangu na nikifika ikulu nita muonyesha jenerali.”
Samson akafanya hivyo na kumuingizia Cleopatra ramani inayo onyesha ni wapi ilipo location ya meli ya nabii Sanga. Hazikupita dakika tano dereva wa RPC Karata akafika nyumbani hapo na wakaondoka na Cleopatra.
“Ina bidi twende kuvamia meli hiyo”
Evans alizungumza wa kujiamini na kuwafanya watu wote kumtazama.
“Shemeji hatuwezi kupambana na watu wengi kama hao tuta kufa. Tumuombee Cleopatra aweze kuaminika huko anapo kwenda”
Josephine alizungumza kwa upole huku kila mmoja akiwa ameyaweka matumaini yake kwa Cleopatra
***
Wanajeshi wa nchi ya Tanzania wakasambaa katika jiji la Dar es Salaama huku shuhuli za usafiri na shuhuli nyingine zikisimama kwa muda. Hapakuwa na mwananchi aliye ruhusikwa kutembea wala magari yanayo toka mkoani kuingia katika jiji la Dar es Salaam. Kwa ufupi jiji zima lime zibitiwa na wanajeshi. Wanajeshi wa nabii Sanga ambao wameingia jiji Dar es Salaama kwa lengo la kumsaka mrs Sanga wakaanza kupatwa na machale ya kuona hali ya utulivu inayo endelea ndani ya jiji hilo.
“Mkuu tuna ona jiji limetulia hakuna raisi wana otembea wala magari?”
Kiongozi wa kikosi hicho alizungumza na nabii Sanga kwa kutumia simu.
“Una maanisha nini?”
“Yaani jiji lipo kimya hatuoni magari wala watu. Au ndio hiyo shuhuli ya kumtafuta mke wako?”
“Ndio si muna jua kwamba amesha kuwa makamu wa raisi hivyo musiogopo. Hakikisheni na nyinyi muna ifanya kazi niliyo waagiza”
“Sawa mkuu”
Nabii Sanga akakata simu na mkuu huyo wa jeshi la nabii Sanga akaamrisha vijana wake kuingiza magari yao yapatayo thelathini huku yakiwa yamejaa wanejeshi katika jiji la Dar es Saalam.
“Wame ingia kwenye mtego wetu”
Mwanajeshi mmoja wa Tanzania aliye kaa gorofa ya tano alizungumza kwa kutumia simu ya upepo huku akitazama gari hizo kwa kutumia darubini. Wanajeshi wa Tanzania walio samba maeneo mbalimbali katika jiji la Dar es Salaam waliweza kusikia sauti hiyo ya mwenzao.
“T Zero wapo wangapi?”
“Zipo gari thelathini na tano mkuu na tume ziweka katikati”
“T Tena una nisikia?”
Jenerali alizungumza na vijana wake wote wakamsikia.
“Ndio mkuu nina kusikia”
“Troops yako ina watu wangapi?”
“Watu ishini mkuu”
“Hakikisheni kwamba hatoki mtu”
“Sawa jenerali”
Wanajeshi wa Tanzania walio jificha katika magorofa eneo la Morroco. Wakaziweka silaga zao tayari kw amashambulizi. Mkuu wa kikosi cha wanajeshi wa nabii Sanga akatoa ishara ya gari hizo zikasimama.
“Moyo wangu una poteza amani kabisa?”
“Kwa nini mkuu”
Kijana wake alimuuliza.
“Huu ukimya sio wa kawaida katika jiji la Dar es Salaam. Yaani hadi sasa hivi hatuoni hata daladala moja?”
“Hata mimi nina shangaa mkuu”
“Na kama mrs Sanga angekuwa ana tafutwa, basi tungeona polisi wakiwa wame zagaa kila mahala. Ila ni kimya na sio kawaida”
“So mkuu turudi au?”
“Ngoja kwanza”
Mkuu huyo akafungua mlango wa gari lake aina ya JEEP, akachukua darubini yake na kuanza kutazama kwenye magorofa yaliyopo eneo hilo la Morocco mataa.
“Fuckk ambushhhhhh!!”
Alizungumza mara baada ya kumuona mwanajeshi mmoja akiwa amemuelekezea bundiki. Kitendo cha kujaribu kuingia ndani ya gari, akatandikwa risasi ya bega na akaanguka chini. Mvua ya risasi ikaanza kuwanyeshea. Hakika hapakuwa na aliye tarajia kukutana na kipigo kama hicho. Wanajeshi wa Tanzania wakazidi kuwashambulia wanajeshi wa nabii Sanga ambao walijikuta wakitawanyika kwa kukimbia huku kila mmoja akijitahidi kuhakiki ana okoa maisha yake kwani ambushi hiyo hawakuitegemea.
***
“Mbona mitaa ipo kimya sana?”
Cleopatra alimuuliza mlinzi wa RPC Karata huku wakiwa katika gari hilo la RPC.
“Kun oparesheni inayo endelea ya wanajeshi hivyo hakuna gari wala mtu anaye ruhusia kukota nje kwa msaa zaidi ya sita.”
“Duuu”
“Ndio”
“Mbona wewe una endesha?”
“Hii gairi ni ya RPC hivyo ina julika”
“RPC mwenyewe yupo wapi?”
“Ikulu”
“Sawa sawa”
Wakafika ikulu na kijana huyo akaeleza kwamba Cleopatra ni mgeni wa RPC hivyo akaruhusiwa kuingia.
“Uta pumzika hapo hadi RPC atakapo toa commanding room”
“Sawa je jenerali yupo?”
“Ndio naye yupo kwenye chumba hicho. Wakitoka ndio uta kutana nao”
“Sawa”
Cleopatra akaa kwenye chumba maalumu cha wageni kupumzika. Mlinzi wa raisi Mtenzi akaingia sebleni na kumuita Jery pembeni ili wazungumze. Wakatoka nje ya seble hiyo kwa ajili ya mazungumzo.
“Vipi?”
“Sio shwari”
“Una maanisha nini?”
“Mzee kwa sasa yupo kizuizini na nchi ina ongozwa na jeshi na jenerali sasa hivi ndio raisi wa muda”
Jery akastuka sana huku akimtazama mlinzi huyo.
“Acha kunitania?”
“Huo ndio ukweli. Raisi kwa sasa yupo kizuizini na haruhusiwi kuonana na mtu yoyote na hadi hapa ninavyo zungumza ni kwamba wana jeshhi wame funga mitaa yote na watu wote wapo ndani, huko barabarani hakuna gari linalo ruhusiwa kutembea”
“Hembu hayo melezo njoo uyazungumzie huku ndani kwa maana nina hisi una nichanganya”
Wakarudi sebleni na kuka kwenye sofa zilizop hapo sebleni.
“Baba kuna tatizo lime tokea”
Jery alianza kuzungumza na kumfanya nabii Sanga kukaa vizuri.
“Kuna nini mwanangu”
“Ahaa baba ame wekwa kizuizini na sasa hivi jeshi ndio lina ongoza nchi”
“NINI?”
Nabii Sanga alihamaki huku akihisi kama tumbo likimkata kwa maumivu makali.
“Ndio mzee. Sasa hivi jenerali wa jeshi ndio raisi wamuda. Amemtoa madarakani raisi Mtenzi na kumuweka kizuizini mara baada ya kugundua kwamba kuna wanajeshi ambao wame vamia jiji hili na hawajulikani ni wapi walipo tokea. Raisi alipaswa kutoa amri kwa jeshi ila akashindwa. Hivyo ilimlazimu jenerali kuchukua mamlaka na inavyo sadikika kwamba wanajeshi hao ndio walio mteka makamu wa raisi’
Nabii Sanga akahisi kama nguvu za mwili zikimuishia. Taratibu akakaa chini huku mapigo yake ya moyo yakimuenda kasi sana.
“Baba upo salama?”
Jery aliuliza huku akimsogelea baba yake mkwe.
“Yaa nipo salama. Vipi ime kuwaje?”
“Hapa ninavyo zungumza wanajeshi hao wame pewa ambushi ya maana na sidhani kama wata weza kutika ndani ya hili jiji wakiwa hai”
Maneno ya mlinzi huyo yakazidi kumfanya nabii Sanga kuhisi mapigo yake ya moyo yanayo kwenda kwa kasi kubwa yata toboa kifua chake.
“Baba hii presha”
Jery alizungumza huku akikimbilia chumbani kwake. Akamkuta Julieth akiwa ame lala fofofo kitandani.Jery kwa haraka akachukua kisanduku chake cha kuhifadhia vifaa vya huduma ya kwanza. Akatoka chumbani hapo na kurudi sebleni na kumkuta nabii Sanga akiwa ameiweka simu yake sikioni mwake. Simu ya kijana wake aliye toka kuongea naye muda mchache ulii pita, ina endelea kuita pasipo kupokelewa. Jasho jingi lina mwagika nabii Sanga usoni mwake, hakika katika siku aliyo pata mapigo ya kutisha ni leo.
“Baba kaa vizuri nikupime presha?”
“Hapana Jery. Nina hitaji kuondoka hapa ikulu, muamshe Julieth tuna ondoka sasa hivi”
“Samahani mze hilo halito wezekana kwa maana sisi walinzi wote wa raisi tume pokonywa silaha zetu. Ime tolewa hakuna mtu hata mmoja kutoka nje ya ikulu hii.”
“Nahiaji kuonana na huyo jenerali wa jeshi?”
“Haiwezekani mzee wangu. Yaani hapa ninavyo kuambia ni kwamba kuanzia getini hadi ndani ya ikulu, wanao linda ni wanajeshi na sio sisi walinzi wa raisi”
“Sawa ila nina hitaji kuondoka now. Jery muamshe Julieth tuna ondoka sasa hivi nina kwenda kuonana na huyo jenerali wa Jeshi”
Nabii Sanga alizungumza na kutoka sebleni hapo na kuwaacha Jery na mlinzi huyo kushangaa. Nabii Sanga akamuomba mwanajeshi mmoja kuitiwa jenerali wa jeshi.
“Mkuu kwa sasa yupo bize”
“Muambie ni dharura nina hitaji kuondoka”
Nabii Sanga alisisitizia, kutokana nabii Sanga ana sifa nzuri na watu wengi wana mfahamu kwamba ni mtu wa Mungu basi mwanajeshi huyo akamuelewa na akalekea katika commanding room na akamnong’oneza jenerali wa jeshi.
“Ana taka nini?”
“Sijajua mkuu ila na sehema ni muhimu sana”
Jenerali wa jeshi akatazama jinsi wanajeshi wake wanavyo endelea kupambana na wanajeshi wa nabii Sanga. Akanyanyuka na kutoka nje kwa maana hata yeye ana muheshimu sana nabii Sanga na isitoshe ni mara kadhaa ame kuwa akihudhuria katika kanisa la nabii Sanga kwa ajili ya kusali.
“Habari yako Jenerali”
“Salama heshimiwa yako mtumishi”
“Nashukuru ndugu yangu. Nina omba nafasi ya kuweza kuondoka hapa ikulu na kuelekea nyumbani kusali”
“Ahaa samahani mtumishi wa Mungu hivi sasa nchi ipo katika hali ya hatari hususani hapa Dar es Salaama hivyo huto weza kutembea kwa gari huko barabarani ni hatari sana”
“Nime kuja na helicopter yangu na nina imani nita ondoka nayo. Nina kuomba niondoke na mkwe wangu pamoja na binti yangu. Kukaa hapa ikulu na mke wangu alitekwa mbele ya macho ya watu wengi hivyo nina kosa amani sana ndugu yangu nina kuomba sana uweze kuniruhusu’”
Jenerali wa jeshi akamtazama nabii Sanga anaye omba kwa unyenyekevu. Kutokana ni mtu anaye muamini na kumuheshimimu sana, akamruhusu aweze kuondoka na helicopter yake.
“Mungu akubariki katika kila ulifanyalo”
“Nina shukuru sana mtumishi”
Nabii Sanga akarudi sebleni na kumkuta Jery na Julieth wakiwa salama. Wakaondoka na kuelekea kiwanja cha helicopter. Wakaingia kwenye helicopter hio na taratibu ikaanza kupaa kuelekea hewani.
“Tuelekee nchini Kenya”
Nabii Sanga alimueleza rubani wake na akatii.
“Baba vipi mama?”
“Ata patikana na kila jambo lita kwenda vizuri. Jery nina kuamini na nina imani kwamba uta mlinda mwanangu”
“Ndio baba nipo tayari kufa kwa ajili ya mke wangu”
Jery alizungumza kwa msisitizo huku akimshika mkono wa kulia Julieth ambaye naye amejawa na wasiwasi kwa maana Jery alimueleza kinacho endelea huko mtaani na Jery pekee ndio hajui baba yake mkwe na mke wake ni watu wa aina gani.
***
“Jenerali pia kuna binti ana hitaji kukuona”
Mlinzi wa jenerali wa jeshi alizungumza kabla ya jenerali hajarudi kwenye chumba cha kuongozea oparesheni hizo.
“Ni nani?”
“Mtoto wa mzee Mbogo”
“Yupo hapa nchini?”
“Ndio na yupo hapa ikulu. Yupo katika chumba cha mapumziko”
“Twende nikamuone”
Jenerali akaanza kuongoza kwa mwendo wa haraka hadi katika chumba hicho. Alipo ingia tu, Cleopatra akanyanyuka kwa haraka na kamkimbilia na kumkumbatia kwa nguvu huku akiangua kilio cha uchungu sana. Jenerali akamkumbatia kwa dakika kadhaa Cleopatra kisha akamuachia.
“Cleopatra mbona una lia mwaangu?”
“Ba mdogo, baba ame uwawa?”
Jenerali akastuka sana huku akimtazama Cleopatra usoni mwake kwa maana anacho jua yeye ni kutekwa kwa mzee Mbogo ila swala la kuuwawa kwake halitambui kabisa.
“Na nani aliye muua?”
“NABII SANGA NA WANAJESHI WAKE”
Jenerali macho ya mshangao yakamtoka kiasi cha kuhisi kupagawa. Akamtazama Cleopatra machoni mwake na kugundua kwamba anacho kizungumza ni kitu cha ukweli kwani ana mfahamu Cleopatra toka utotoni mwake na ana muelewa vizuri sana.
****************************************************************************************************************
****
ITAENDELEA
Haya sasa. Cleopatra ame mueleza jenerali ukweli na ameaminika. Nabii Sanga, mkwe wake pamoja na mwanaye wana kimbilia nchini Kenya wakia katika helicopter je nabii Sanga ta kamatwa ikiwa jenerali kwa sasa ndio ana ongoza nchi? Usikose sehemu ya 220.