THE SPIRIT THINKER
JF-Expert Member
- Sep 9, 2019
- 419
- 652
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA KUMI: SPECTRE
To the end (mpaka mwisho) 11
Tariq Haji
0624065911
Baada ya roboti hilo kushushwa uwanjani, milango ikafungwa pamoja na ngao maalum zilizotengenezwa kwa nguvu ya sumaku (electromagnetic force field "EMFF"). Lengo la EMFF kuzuia mawimbi makali yenye madhara yatakayosababishwa na shughuli za mashine hiyo.
Mzee Rozalive na wengine wakapanda sehemu iliyokuwa juu na kukaa eneo ambalo lilitumika kuangalia majaribio hayo. Siyo wao tu, hata baadhi ya wafanyakazi wengine nao walikaa maeneo kama hayo wakitaka kushuhudia labda miujiza ingetokea. Maana wao walijaribu mbinu zote lakini Spectre hakuinua hata kidole.
"Kuna mtu anataka kujiaibisha leo"
"Hahaha, halafu nimesikia ni bwana mdogo hata bado unyevunyevu nyuma ya masikio yake haujakauka" "Fufu watu wengine hawajui kipi bora kwao"
Baadhi ya waangaliaji walikuwa wakinong'ona, hakuna alietaka kuamini kama roboti lililolala katika eneo hilo kwa miaka karibia mia na hamsini bila kuinua hata kidole kama lingetikisika.
Dakika tano, kumi, kumi na tano, bado kimya.
"Ah, hili pande la chuma labda lishakufa" aliongea profesa Bagani. Watu wote walikuwa kimya wakiliangalia roboti lililosimama uwanja bila hata kutikisika. Na kuna baadhi wakawa tayari wameanza kuonesha dharau.
Fwoooosh!!
Vitu kama maji vikatoka kwenye maungio ya Spectre, ukafuata mvuke mwingi mweupe. Watu wote wakatoa macho, hata wale ambao tayari walishaanza kuondoka wakasimama na kugeuka.
Vruuum!!!
Mashine ikanguruma na kusababisha mtetemeko ulisikika mpaka kwa waangaliaji, taratibu vyuma vya nje vya Spectre vikaanza kutikisika na kujipanga sehemu zake. Watu wakazidi kushangaa, roboti iliyolala miaka mia na hamsini imeamka mbele yao.
"Karibu, tafadhali ingiza jina lako" sautu ikasikika masikioni mwa Baston.
"Baston" alijibu.
"Karibu Baston", ghafla kiza kilichokuwa kimemzunguka baston kikatoweka na kujikuta amesimama katika eneo kubwa. Moja kwa moja alitambua kuwa eneo hilo liliitwa Emerald. Mbeke yake alikuwa mwanamke aliekuwa katika kombat ya jeshi "Spectre" aliita Baston.
Hakujibiwa ila mwanamkw huyo akapotea na baada ya hapo Baston akaona eneo kubwa. Ulikuwa ni uwanja ambao Spectre alikuwa amesimama. Tayari Baston na Spectre walishaungana na kuwa kitu kimoja.
"Kila kitu kimekamilika" alisikia tena sauti.
Baston akaanza kunyoosha viungo, na wakati huwo Spectre akaanza kunyoosha viungo.
Kah! Kah!
Sauti za vyuma zikasikika, sehemu ya mabega chuma kikafunguka. Bomba mbili zenye urefu wa mita moja zikatokea kila upande. Visu virefu vikachomoza chini ya viganja, pande zote mbili za kiuno kukafunguka zikaonekana bastola mbili.
Sehemu ya nyuma chini ya mgongo, kukikuwa na chuma kikichochongwa kama pochi. Kikafunguka, ikaonekana mipini mili meusi. Sehemu ya magoti nayo ikafunguka, vikaonekana vitu vyenye ncha kali. Wakati Baston alikuwa akiangalia silaha zote za Spectre. Akastaajabu sana, ni kweli katika kumbukumbu alizozirithi kwa Gilbot, Spectre alitajwa lakini hakukuwa na maelezo mengi sana.
Wakati huu ndio Baston akafahnu kuwa Spectre alitengezwa kwa kazi moja tu. Nayo ilikuwa ni kufanya mauaji, pia ikamfunukia kichwani kuwa Spectre alitengenezwa makhususi kwa ajili ya kamanda Dalia. Maana kila kiungo cha roboti huyo kilikuwa ni silaha ya mauaji.
Fwoooosh!!!
Sehemu ya pembeni ya kichwa karibu na masikio, pakafunguka na maji mengi yakatoka na kusababisha roboti zima kurowa. Baada ya sekunde chache mapovu yakaonekana yakijitemgeza katika mwili wa Spectre na baada dakika tatu mwili mzima ukawa umefunikwa na mapovu.
Maji yakatoka tena na povu lote likasafishwa kisha mvuke ukafuate na sekunde chache tu maji yakakauka. Sehemu ya kifua upande wa kushoto chini ya sehemu ilipoingua almasi ya damu kukafunguka, na chuma kidogo kikasogea mbeke. "Spectre" ndio lilisomeka katika chuma hicho.
Spectre alikuwa mweusi tii, weusi ambao haukung'ara ulipopigwa na jua bali ulinyonya mwanga wote uliotua katika chuma hicho na kukifanya kizidi kuwa cheusi.
Mashine ikazidi kunguruma na baada ya dakika mbili mngurumo wote ukapotea. Akaanza kutembea na kadri sekunde zilivyochanika ndivyo kasi ilivyoongezeka na mwisho akaanza kukimbia. Mara kadhaa alitikisika na kufannya miondoka ambayo ambayo haikuwa rahisi kwa roboti kufanya.
"Mungu wangu, lile roboti au binadamu" aliongea mtu mmoja akishika kichwa chake. Ila hakuna aliemsikia hata mmoja kila mtu alikuwa amepigwa na bumbuwazi la aina yake.
Ghafla Spectre akabiringitia na kutoa bastola, akafanya shambulizia na papo hapo akariudisha kupeleka mikono yake. Ile sehemu ya vusu ikafunguka, akatoa visu viwili na kushika kila kimoja katika mkono mmoja.
Akafanya mashambulizi ya kasi kama matano hivi akavizungusha na kuvirudisha katika pochi yake. Akarusha ngumi kadhaa kwa kasi mno, wengi hawakuona ila kwa wale wenye macho makali walishuhudia vitu vye ncha kali vikitoka pale ngumi zilipofika mwisho na kurudi mkono uliporudi nyuma.
Akazunguka mara kadhaa na kuachia mateke ambayo haya kuwa rahisi kwa roboti kufanya. Ila mateke hayo hayakuwa yakawaida tu. Kulikuwa visu vikali vilivyokuwepo kwenye visigino na vidole vya miguu.
Baada majaribio yote kukamilika, Spectre akasimama na moshi laini ukaonekana ukitoka katika mwili wa chuma hicho. Kwa wataalamu na magwiji wa vita waliokuwepo eneo hilo katika vichwa vyao kulikuwa na sentensi moja tu. "Kila pigo lilitoka kwa Spectre lilitoka na maana moja tu, kuuwa"
Walikuwa sahihi kwa asilimia thamanini lakini kiti ambacho hawakukifahamu. Spectre hakuwa tu roboti wa kufanya mauwaji bali mauaji ya halaiki. Spectre ilikuwa ni mashine iliyotengenezwa kuwa muwindaji. Hata baadhi ya Zestra wa ngazi za juu waliifahamu kazi ya Spectre. Kwao alikuwa ni shetani shuwaini asiye na huruma hata kidogo.
Baada ya nusu saa mashine ya kubebea roboti ikafika na kulibeba Spectre. Likarudishwa ndani, sehemu ya kifua ikafunguka. Baston akatoka akiwa karowa jasho mwili mzima, mwili wake wote ulikuwa umetutumka. Misuli ilikuwa imevimba na kufanya nguo aliyovaa kugandana na mwili kisawasawa.
Alipokanyaga tu ardhi akayumbayumba almanusura aanguke. Mishipa ya kichwa ilikuwa imevimba na kutweta kama mapigo ya moyo.
"Mbona umechoka sana" aliuliza profesa Bagani.
"Ngoja nipumzike kwanza nitaeleza kila kitu" aliongea
Baston kwa tabu vifuniko vya macho vikawa visito na hatimae akapoteza fahamu. Mzee Rozaliv akaita watu na kuwaagiza wampeleke chumba cha mapumziko.
Karibia wote walikuwa na maswali kedekede lakini hakukuwa na kuwapa majibu. Ni kweli kuna wakati marubani hupoteza fahamu baada ya kuendesha roboti. Ila hali hiyo huwa inakuja baada ya matumizi muda mrefu zaidi ya saa tatu. Lakini kwa Baston ilikuwa ni ajabu. Kwasababu yeye alikuwa katika roboti hilo kwa saa moja tu.
Hata hivyo hawakuwa na namna zaidi ya kumsubiri Baston aamke ndio wapate majibu. Kila mwenye swali alilieka swali lake pembeni na kuangalia mkanda (video) ya majaribio ya Spectre. Jopo la wataalamu lilikuwa limekusanyika katika ukumbi mdogo wakidadavua kila sekunde ya video hiyo.
To the end (mpaka mwisho) 11
Tariq Haji
0624065911
Baada ya roboti hilo kushushwa uwanjani, milango ikafungwa pamoja na ngao maalum zilizotengenezwa kwa nguvu ya sumaku (electromagnetic force field "EMFF"). Lengo la EMFF kuzuia mawimbi makali yenye madhara yatakayosababishwa na shughuli za mashine hiyo.
Mzee Rozalive na wengine wakapanda sehemu iliyokuwa juu na kukaa eneo ambalo lilitumika kuangalia majaribio hayo. Siyo wao tu, hata baadhi ya wafanyakazi wengine nao walikaa maeneo kama hayo wakitaka kushuhudia labda miujiza ingetokea. Maana wao walijaribu mbinu zote lakini Spectre hakuinua hata kidole.
"Kuna mtu anataka kujiaibisha leo"
"Hahaha, halafu nimesikia ni bwana mdogo hata bado unyevunyevu nyuma ya masikio yake haujakauka" "Fufu watu wengine hawajui kipi bora kwao"
Baadhi ya waangaliaji walikuwa wakinong'ona, hakuna alietaka kuamini kama roboti lililolala katika eneo hilo kwa miaka karibia mia na hamsini bila kuinua hata kidole kama lingetikisika.
Dakika tano, kumi, kumi na tano, bado kimya.
"Ah, hili pande la chuma labda lishakufa" aliongea profesa Bagani. Watu wote walikuwa kimya wakiliangalia roboti lililosimama uwanja bila hata kutikisika. Na kuna baadhi wakawa tayari wameanza kuonesha dharau.
Fwoooosh!!
Vitu kama maji vikatoka kwenye maungio ya Spectre, ukafuata mvuke mwingi mweupe. Watu wote wakatoa macho, hata wale ambao tayari walishaanza kuondoka wakasimama na kugeuka.
Vruuum!!!
Mashine ikanguruma na kusababisha mtetemeko ulisikika mpaka kwa waangaliaji, taratibu vyuma vya nje vya Spectre vikaanza kutikisika na kujipanga sehemu zake. Watu wakazidi kushangaa, roboti iliyolala miaka mia na hamsini imeamka mbele yao.
"Karibu, tafadhali ingiza jina lako" sautu ikasikika masikioni mwa Baston.
"Baston" alijibu.
"Karibu Baston", ghafla kiza kilichokuwa kimemzunguka baston kikatoweka na kujikuta amesimama katika eneo kubwa. Moja kwa moja alitambua kuwa eneo hilo liliitwa Emerald. Mbeke yake alikuwa mwanamke aliekuwa katika kombat ya jeshi "Spectre" aliita Baston.
Hakujibiwa ila mwanamkw huyo akapotea na baada ya hapo Baston akaona eneo kubwa. Ulikuwa ni uwanja ambao Spectre alikuwa amesimama. Tayari Baston na Spectre walishaungana na kuwa kitu kimoja.
"Kila kitu kimekamilika" alisikia tena sauti.
Baston akaanza kunyoosha viungo, na wakati huwo Spectre akaanza kunyoosha viungo.
Kah! Kah!
Sauti za vyuma zikasikika, sehemu ya mabega chuma kikafunguka. Bomba mbili zenye urefu wa mita moja zikatokea kila upande. Visu virefu vikachomoza chini ya viganja, pande zote mbili za kiuno kukafunguka zikaonekana bastola mbili.
Sehemu ya nyuma chini ya mgongo, kukikuwa na chuma kikichochongwa kama pochi. Kikafunguka, ikaonekana mipini mili meusi. Sehemu ya magoti nayo ikafunguka, vikaonekana vitu vyenye ncha kali. Wakati Baston alikuwa akiangalia silaha zote za Spectre. Akastaajabu sana, ni kweli katika kumbukumbu alizozirithi kwa Gilbot, Spectre alitajwa lakini hakukuwa na maelezo mengi sana.
Wakati huu ndio Baston akafahnu kuwa Spectre alitengezwa kwa kazi moja tu. Nayo ilikuwa ni kufanya mauaji, pia ikamfunukia kichwani kuwa Spectre alitengenezwa makhususi kwa ajili ya kamanda Dalia. Maana kila kiungo cha roboti huyo kilikuwa ni silaha ya mauaji.
Fwoooosh!!!
Sehemu ya pembeni ya kichwa karibu na masikio, pakafunguka na maji mengi yakatoka na kusababisha roboti zima kurowa. Baada ya sekunde chache mapovu yakaonekana yakijitemgeza katika mwili wa Spectre na baada dakika tatu mwili mzima ukawa umefunikwa na mapovu.
Maji yakatoka tena na povu lote likasafishwa kisha mvuke ukafuate na sekunde chache tu maji yakakauka. Sehemu ya kifua upande wa kushoto chini ya sehemu ilipoingua almasi ya damu kukafunguka, na chuma kidogo kikasogea mbeke. "Spectre" ndio lilisomeka katika chuma hicho.
Spectre alikuwa mweusi tii, weusi ambao haukung'ara ulipopigwa na jua bali ulinyonya mwanga wote uliotua katika chuma hicho na kukifanya kizidi kuwa cheusi.
Mashine ikazidi kunguruma na baada ya dakika mbili mngurumo wote ukapotea. Akaanza kutembea na kadri sekunde zilivyochanika ndivyo kasi ilivyoongezeka na mwisho akaanza kukimbia. Mara kadhaa alitikisika na kufannya miondoka ambayo ambayo haikuwa rahisi kwa roboti kufanya.
"Mungu wangu, lile roboti au binadamu" aliongea mtu mmoja akishika kichwa chake. Ila hakuna aliemsikia hata mmoja kila mtu alikuwa amepigwa na bumbuwazi la aina yake.
Ghafla Spectre akabiringitia na kutoa bastola, akafanya shambulizia na papo hapo akariudisha kupeleka mikono yake. Ile sehemu ya vusu ikafunguka, akatoa visu viwili na kushika kila kimoja katika mkono mmoja.
Akafanya mashambulizi ya kasi kama matano hivi akavizungusha na kuvirudisha katika pochi yake. Akarusha ngumi kadhaa kwa kasi mno, wengi hawakuona ila kwa wale wenye macho makali walishuhudia vitu vye ncha kali vikitoka pale ngumi zilipofika mwisho na kurudi mkono uliporudi nyuma.
Akazunguka mara kadhaa na kuachia mateke ambayo haya kuwa rahisi kwa roboti kufanya. Ila mateke hayo hayakuwa yakawaida tu. Kulikuwa visu vikali vilivyokuwepo kwenye visigino na vidole vya miguu.
Baada majaribio yote kukamilika, Spectre akasimama na moshi laini ukaonekana ukitoka katika mwili wa chuma hicho. Kwa wataalamu na magwiji wa vita waliokuwepo eneo hilo katika vichwa vyao kulikuwa na sentensi moja tu. "Kila pigo lilitoka kwa Spectre lilitoka na maana moja tu, kuuwa"
Walikuwa sahihi kwa asilimia thamanini lakini kiti ambacho hawakukifahamu. Spectre hakuwa tu roboti wa kufanya mauwaji bali mauaji ya halaiki. Spectre ilikuwa ni mashine iliyotengenezwa kuwa muwindaji. Hata baadhi ya Zestra wa ngazi za juu waliifahamu kazi ya Spectre. Kwao alikuwa ni shetani shuwaini asiye na huruma hata kidogo.
Baada ya nusu saa mashine ya kubebea roboti ikafika na kulibeba Spectre. Likarudishwa ndani, sehemu ya kifua ikafunguka. Baston akatoka akiwa karowa jasho mwili mzima, mwili wake wote ulikuwa umetutumka. Misuli ilikuwa imevimba na kufanya nguo aliyovaa kugandana na mwili kisawasawa.
Alipokanyaga tu ardhi akayumbayumba almanusura aanguke. Mishipa ya kichwa ilikuwa imevimba na kutweta kama mapigo ya moyo.
"Mbona umechoka sana" aliuliza profesa Bagani.
"Ngoja nipumzike kwanza nitaeleza kila kitu" aliongea
Baston kwa tabu vifuniko vya macho vikawa visito na hatimae akapoteza fahamu. Mzee Rozaliv akaita watu na kuwaagiza wampeleke chumba cha mapumziko.
Karibia wote walikuwa na maswali kedekede lakini hakukuwa na kuwapa majibu. Ni kweli kuna wakati marubani hupoteza fahamu baada ya kuendesha roboti. Ila hali hiyo huwa inakuja baada ya matumizi muda mrefu zaidi ya saa tatu. Lakini kwa Baston ilikuwa ni ajabu. Kwasababu yeye alikuwa katika roboti hilo kwa saa moja tu.
Hata hivyo hawakuwa na namna zaidi ya kumsubiri Baston aamke ndio wapate majibu. Kila mwenye swali alilieka swali lake pembeni na kuangalia mkanda (video) ya majaribio ya Spectre. Jopo la wataalamu lilikuwa limekusanyika katika ukumbi mdogo wakidadavua kila sekunde ya video hiyo.