RIWAYA: Wivu-Beka Mfaume

MTUNZI: BEKA MFAUME



SEHEMU YA KUMI


* * * **

***MOHSEIN amechomolewa na DINA kuhusu kuagana....RICHARDanamchanganya DINA kwa kumweleza kuwa atasafiri na ndege...jeatamnasa???
*** JOHN ameenda kwa mganga ....vipi atafanikiwa shidazake??
 

sijui nilikuwa wapi, ndiyo naiona leo, naomba uskose kuniita Casuist!
 
Last edited by a moderator:
Reactions: ram
MTUNZI: BEKA MFAUME

SEHEMU YA KUMI NA MOJA







***DINA mtegoni AMEFUNDISHWA KUTUMIA UMA na sasa anataka kulishwa…..je atanasa????
**Nini hatma ya wivu wa JOHN SAILAS na MOHSEIN
 
Ni kweli Mphamvu, ndiye yeye huyu huyu! Namkubali sana huyu jamaa!

Wa ukweli, pamoja na kuwa mwandishi wa riwaya pendwa lakini anaiandika katika namna ambayo inavutia hata wapenzi wa riwaya dhati.
 
Last edited by a moderator:
Haya njoo uendelee basi
 
MTUNZI: BEKA MFAUME


SEHEMU YA KUMI NA MBILI


Walpokuwa wakiendelea kula, ghafla Richard alichukua kipande cha samaki alichokikata na kukiinua kwa uma.

"Nataka kukulisha," Richard alisema huku akimwangalia Dina usoni. Dina akawa kama aliyeshangaa, akamwangalia Richard usoni bila ya kutoa jibu la haraka. Wakaangaliana kwa makini kama waliokuwa wakisomana akili zao. Hatimaye Dina akaufungua mdomo bila ya kutamka
lolote, akamruhusu Richard amlishe!

* * * * *
Jioni ya saa kumi na moja, Dina akiwa ameamka sekunde chache zilizopita na kabla hajakiweka vyema kichwa chake kutafakari, akausikia mlango wa chumbani kwake ukigongwa. Moja kwa moja akahisi ni Richard ndiye angekuwa anaugonga mlango huo. Akakumbuka wakati alipoachana naye mara tu baada ya kumaliza kula chakula cha mchana walichokula pamoja, Richard alimuaga na kumtaka apumzike, akisema wataonana baadaye. Ndipo naye alipoamua kulala na kupata usingizi mzuri hadi alipoamka na kusikia mlango ukigongwa.

Alipoufungua, akashangaa kumwona mhudumu wa vyakula akiwa amesimama na tray iliyobeba birika mbili, zote zilikuwa ndogo zenye ukubwa uliotofautiana, na kijaluba cha sukari, pembeni kukiwa na sahani iliyofunikwa na kitambaa.

"Sijaagiza!" Dina alisema, usoni akiwa na mshangao.
"Mzee Richard ameniagiza nikuletee," mhudumu alisema.

Mzee Richard! Dina alishangaa na kutaka kujiuliza mtu huyo ni nani. Ghafla akapata jibu kuwa ni heshima aliyokuwa akipewa Richard. Akatabasamu na moyoni kukasuuzika baada ya kukiri, Richard alikuwa akimjali.
"Karibu," alimwambia mhudumu na kumpa nafasi ya kuingia.

Mhudumu aliingia chumbani na kuangaliwa na Dina aliyekuwa amesimama mlangoni kwa ajili ya kumsubiri atoke.
"Nakwenda," mhudumu aliaga baada ya kuviweka kwenye meza vitu alivyoingia nao.
"Yeye yuko wapi?" Dina aliuliza wakati mhudumu akiwa mlangoni anatoka.
"Yupo duka la kahawa akinywa chai," mhudumu alijibu.
"Ahsante na karibu tena," Dina alisema kisha akaufunga mlango nyuma ya mgongo wa mhudumu aliyetoka.
Dina aliiendea tray iliyoletwa na mhudumu na kuvipekua vitu vilivyoletwa. Birika kubwa ilikuwa na chai, birika ndogo ilikuwa na maziwa na alipokifunua kitambaa kilichofunika sahani, akaiona keki iliyomtamanisha, akatengeneza tabasamu dogo. Huduma ya V.I.P! aliwaza.

Akiwa anakaribia kumaliza kunywa chai aliyoletewa, simu ya chumbani kwake iliita. Alishituka na kuiangalia. Ilikuwa ni mara ya kwanza kuisikia ikiita tokea alivyoingia asubuhi. Hakuwa na uhakika kama alikuwa akipigiwa yeye au simu hiyo iliingia kwa makosa. Aliamini kama angekuwa ni Richard ndiye anayempigia basi angempigia kwa simu yake ya mkononi kama alivyofanya asubuhi.

Akaifuata simu hiyo na kusimama kando yake, badala ya kuiinua, akasita. Akaiangalia kama vile kilikuwa kitu cha ajabu kilichojenga uhai na kutoa mlio. Kisha kama vile anategua bomu, aliinua simu hiyo kwa uangalifu na polepole, akaiweka sikioni.
"Haloh," alisema kivivu baada ya kuipokea huku akiamini sio yeye anayepigiwa.

"Umekwisha kunywa chai?" sauti ya kiume kutoka upande wa pili wa simu ilisema.

Dina akatabasamu kwenye simu baada ya kuigundua sauti ya Richard.
"Nimeshakunywa," alisema.
"Nasikia uko duka la kahawa ukinywa chai?"

"Ni kweli. Utakuja?"
"Labda nikishaoga."

"Basi nakuomba ufanye kitu kimoja," Richard alisema kwa utulivu. "Ukishaoga uvae lile gauni jeusi katika zile nguo tulizozinunua leo."

"Umelipenda?"

"Ni kati ya nguo zilizokupendeza mno wakati ulipokuwa ukizijaribu dukani, pia ni nguo ya jioni inayostahili kuingia nayo restaurant kwa chakula cha usiku."

"Sawa mkubwa," Dina alisema kiutani.
"Utanifuata nikishamaliza kuoga?"

"Utakapokuwa tayari njoo duka la kahawa."

Akiwa bado hajamaliza kuzungumza na Richard kwenye simu, simu yake ya mkononi ikaita. Akaiangalia pale kitandani ilipokuwepo, lakini hakwenda kuipokea, alisubiri hadi alipomaliza kuzungumza na Richard ndipo alipoifuata. Ilikuwa imekwishaita zaidi ya mara mbili, na alipokuwa anaichukua ikaita tena. Alikuwa John!

"Mbona umechelewa kuipokea simu?" John alianza na lawama. "Bado nipo kazini!" Dina alidanganya.
"Vipi mzima?"

"Mimi mzima, nilitaka kukufahamisha kuwa nimekwisharudi Dar, vipi huko Arusha?"

"Ni kipindi cha baridi na ni kali."
"Umefikia hoteli ipi?"

"Masai Shield."

"Masai Shield?" John aliuliza kwa sauti iliyojaa mshangao kuonyesha alikuwa haamini Dina kufikia kwenye hoteli kubwa na ya kifahari kama hiyo.
"Aisey, hiyo hoteli ni ya kifahari sana! Richard uko naye?"

Wivu! Dina aliwaza.
"Tumemuacha huko huko Dar. Nasikia anaweza akaja baada ya siku mbili au tatu," Dina alidanganya tena.
"John, nitakupigia baadaye nikipata mwanya, sasa hivi bado tuko bize sana."
"Poa, Dina. Baadaye."

"Baadaye John."

"I miss you!"
"I miss you too!"
Zikawa ni simu zilizofuatana! Mara baada ya kumaliza kuongea na John, simu yake ikaita tena. Safari hii alikuwa Mohsein!

"Dina, vipi mambo?" Mohsein alisema kwenye simu.
"Poa. Vipi, za huko Dar?"

"Huku poa. Wangu hata kunipigia simu kunifahamisha kama umefika salama?"

"Tumefika na kuingia kazini moja kwa moja na jamaa bado nipo naye karibu."

"Mmefikia hoteli gani?"

Dina akahisi na huyo naye atapigwa na mshangao kama aliopigwa nao John. "Masai Shield!" alisema.

"Eti wapi Dina?" Mohsein alipayuka kwenye simu kwa sauti iliyojaa mshangao.

"Masai Shield!"


"Unaona Dina? Huyo jamaa yupo kwenye kukupumbaza…" "Nitakupigia baadaye!" Dina alisema kwa mkato na kukata simu. Dina akakunja uso kwa hasira. Alitamani aizime simu yake ili asiwe na mawasiliano na watu hao wawili ambao wote alijua hoja zao zilianza kujikita kumjadili Richard, na yeye kwa wakati huo hakuwa tayari kulijadili hilo. Alihitaji amani, na kwa mara ya kwanza akakiri kuwa, Richard ndiye aliyekuwa akimpa amani aliyokuwa akiihitaji tokea alivyowasili hapo Arusha. Akatamani awe karibu naye kwa wakati huo, kuliko kuwa na mazungumzo na watu hao wawili yanayomjadili Richard!

Dina alikwenda kuoga huku akihisi watu hao wawili wakiwa kama mzigo kwake. Alipomaliza kuoga, aliiva nguo aliyoambiwa na Richard aivae.

Alipendezwa na nguo hiyo! Akaenda duka la kahawa kumfuata Richard. Alipokuwa akitoka kwenye lifti kuingia duka la kahawa, kila aliyekuwepo eneo hilo kuanzia wafanyakazi na wateja ambao wengi wao walikuwa ni Wazungu walimwangalia. Alionekana kama mlimbwende aliyekuwa akitembea juu ya jukwaa la mashindano ya urembo. Akamwona Richard, akatengeneza tabasamu dogo lililopokewa na Richard aliyekuwa amekaa peke yake mezani.

"Umependeza!" Richard alisema wakati akiwa amesimama na kumvutia kiti Dina.

"Ahsante," Dina alisema wakati akikaa. "Utaongeza chai?"

"Hapana." Mhudumu akafika.

"Hapana, sihitaji chochote," Dina aliyekuwa akitabasamu alimwambia mhudumu kabla ya kuulizwa.

"Ningependa tuzunguke zunguke nje ya hoteli uiangalia mandhari iliyoizunguka hoteli, lakini baridi iliopo huko nje ni balaa!" Richard alisema baada ya mhudumu kuondoka.

"Mchana kulikuwa na baridi vile, sasa hivi kutakuwaje huko nje! Lakini hii hoteli ni nzuri nje hadi ndani Richard, utadhani upo kwenye pepo! Na yale mandhari ya nje yanatamanisha uzunguke zunguke kama ulivyosema."

"Mwezi wa Novemba tutarudi tena, hali ya hewa itakuwa imebadilika na tutaweza kutembea tembea kwa miguu. Au unasemaje?"

Kikazi au kibinafsi? Dina alijiuliza. Mazingira halisi ya siku moja hiyo yalikwisha kuonyesha kuwa, wameurudisha uhusiano wao, kwa hiyo ujio mwingine wa kuja tena Arusha hakuujua ungekuwaje. "Sawa," alijibu kwa sauti ya chini huku akiiangalia meza. Alikiri kwa hatua ambayo wameifikisha kwa siku hiyo, kamwe asingeweza kukataa chochote atakachoambiwa na Richard!

"Unaonaje tukienda baa kupata kinywaji cha kuvuta muda ili baadaye tukale chakula cha usiku?" Richard alisema.

"Sawa," Dina alikubali.

Wakaenda! Wakati wakisubiri mhudumu aje awaulize na kuwahudumia vinywaji watakavyoagiza, Richard akakumbuka kinywaji alichomwona nacho John wakati akimpelekea Dina alipowakuta kwenye hoteli ya BBH eneo la bwawa la kuogelea. Richard akajiuliza kama Dina angekiagizia tena kinywaji kile alichopewa na John?

Crème de Menthe! alikikumbuka kinywaji hicho.

* * * * *

Usiku walikula chakula ghali na Richard aliagiza kinywaji cha Champagne. Mhudumu alipowahudumia kwa mara ya kwanza kuwatilia kinywaji hicho kwenye glasi zao na kisha kuondoka, Richard akawa wa kwanza kuinua glasi yake juu na kumwambia Dina, "Tunywe kwa furaha ya kuurudisha uhusiano wetu. Cheers!"

Kauli hiyo ya Richard ikawa imemwingiza Dina ili akiri kwa kauli yake mwenyewe kuwa, hatua ya kukubali kuigonganisha glasi yake na ya Richard na kutamka neno ‘cheers' atakuwa tayari amekubali kuurudisha uhusiano huo!

Kwanza Dina alionekana kusita na kujikuta akimfikiria John, kisha akamfikiria Mohsein! Tuhuma ya kuongeza mwanamume wa tatu ilimtuhumu, akauona ni uhuni usiokubalika kwake. Akakiri moyoni lazima amteme mmoja wao. Mohsein akawa kafara, akalengwa kuachwa yeye!

"Cheers!" alisema na kuigonganisha glasi yake na ya Richard, akanywa funda moja kabla ya kuirudisha glasi mezani.

Richard naye akafanya hivyo hivyo.

Baada ya kumaliza kula, hawakuondoka mapema mezani. Waliendelea kuagiza Champagne na kuzungumza, walionekana kutulia na mazungumzo yao yalitawaliwa na sauti za chini huku wakiwa wanaangaliana ana kwa ana. Mwanga hafifu wa mshumaa uliokuwa ukiwaka kwenye meza yao, ulionyesha sura zao zikiwa kwenye masikilizano na kuzingirwa na mandhari ya mahaba kwa kila mmoja wao.

Usiku huo, Dina hakulala chumbani kwake, alikwenda kulala chumbani kwa Richard!

* * * * *

Dina alihamia rasmi chumbani kwa Richard ilipofika siku ya pili baada ya kukubaliana chumba alichokuwa akilala kirudishwe. Wakaanza kuishi kama bibi na bwana. Walilala, waliamka na kwenda kazini pamoja huku uchipuaji wa penzi jipya ukishamiri kwa kasi. Kila jioni baada ya kumaliza kazi, walichagua pa kwenda kama hawakuhitaji kurudi mapema hotelini. Ikawa kama vile huko Arusha walikokwenda, walikwenda zaidi kama fungate kuliko kikazi.

***

MOHSEIN alibaki na kinyongo tokea siku aliyokatiwa simu na Dina! Kitendo hicho alikichukulia ni dharau aliyofanyiwa! Hakuamini kama kulikuwa na dharura iliyomfanya Dina aikate simu hiyo ghafla, tena bila hata kuomba samahani au kutoa neno lolote la kumtafadhalisha kabla ya kuikata simu hiyo. Moja kwa moja Mohsein akakichukulia kitendo hicho alichofanyiwa na Dina kilikuwa ni kiburi kilichoonyesha kumthamini Richard na kumdharau yeye!

Tukio hilo likawa limemdhihirishia kuwa, tayari Dina ameanza kuwa karibu na Richard! Ni mazingira ambayo alikuwa ameyatabiri awali kuwa, uendaji wa pamoja wa safari hiyo, lengo lake lilikuwa ni hilo, lakini Mohsein hakutarajia kama lingefanyika kwa haraka hivyo. Hofu iliyoingia wivu ikaanza kumtafuna, wasiwasi wa kuwa huenda Richard na Dina wamekwishafanya mapenzi ikampandisha jazba. Dhana hiyo ikamgubika kwenye wingu kubwa la wivu. Donge likamkaa kooni, akatambua kuwa, Dina ndio basi tena kwake! Kitendo cha kuhisi Richard amekwishaingiliana kimwili na Dina huko Arusha waliko kilikoleza moto wa wivu uliokuwa ukiuteketeza moyo wake. Akatamani kupiga kelele, akajizuia. Akaanza kumlaumu Dina moyoni kwa kujirahisisha kwake kwa Richard!

Kwa mara ya kwanza aliilaumu nafsi yake kwa kukubali kujiingiza kwenye penzi la kumpenda Dina, alikiri alikuwa akimpenda na alikuwa akimhitaji awe karibu naye wakati wote. Lakini pia, akamwona Dina kuwa ndiye aliyemwingiza kwenye penzi na baada ya muda mfupi ameamua kumwumiza moyo! Aliiona ilikuwa ni aina ya dhihaka aliyofanyiwa. Mohsein akaapa na yeye lazima amwumize Dina kama vile alivyoumizwa yeye!

Akaanza kufikiria njia za kulipiza kisasi za kumkomoa Dina. Akamkumbuka John!

Alikuwa hajawahi kumwona, lakini alikuwa na habari zake zote! Ni Dina ndiye aliyemwambia wakati alivyomjulisha kuwa ana mchumba! Dina alizungumzia mengi yanayomhusu John na kumjulisha hadi anakofanyia kazi. Akapanga amfuate John kazini kwake! Akaenda! Akamwulizia kwa mlinzi, mlinzi akamwambia yupo, Mohsein akaomba aitiwe.

John alipotoka akashangaa kumwona mtu asiyemjua!

"Naitwa Mohsein, najua hunijui, lakini mimi nakujua," Mohsein alisema huku akiangaliwa na John kwa makini. "Nadhani wewe ni mume mtarajiwa wa Dina? Au sivyo?"

Kwanza John alisita kujibu, akaonyesha wasiwasi wa kutojua kule anakopelekwa kimazungumzo. "Ni nani aliyekueleza kama mimi ni mume mtarajiwa wa Dina?" aliuliza.

"Dina!" Mohsein alijibu kiuhakika.

John akaganda na kuonekana kushitushwa na jibu alilopewa. "Ilikuwaje akakwambia wewe?"

"Tunafanya kazi pamoja. Alishanipa kadi ya mchango ya Send off ili nimchangie. Katika maongezi yetu ya kawaida alinitajia unapofanya kazi na ndio sababu nipo hapa kwa ajili yako. Swali langu liko palepale, wewe ndiye mume wake mtarajiwa?"

"Ndiyo ni mimi," John alijibu akionekana bado yuko kwenye wasiwasi.

"Sasa sikiliza, mimi ni mwanamume mwenzio!" Mohsein alizungumza kwa sauti ya kishari iliyokaza. "Hawa wanawake unatakiwa uwajue kabla ya kuamua kuwaoa. Uzijue tabia zao na ujue uadilifu wao. Je, una kifua cha kuzijua habari zake?"

John alianza kuonekana kuchanganyikiwa baada ya kuambiwa hayo. "Nipo tayari," alisema akijaribu kuifanya sauti yake imjengee taswira kuwa ni kweli alikuwa tayari. Hata hivyo uso wake ulijenga hofu ya kile alichokuwa akisubiri kuambiwa.

"Tatizo sio kuwa tayari," Mohsein alisema kama vile Mwalimu anayemwelekeza kitu mwanafunzi wake. "Kifua chako kipo tayari kuhifadhi siri ninayotaka kukwambia? Sio tena uende ukapayuke kwake, Ooh, Mohsein ndiye aliyeniambia!"

"Niamini, sitomwambia!" John alijaribu kusema kwa utulivu. Mohsein akawa na uhakika kwa wakati huo mapigo ya moyo ya John yalikuwa yakipiga kwa nguvu kifuani pake, na hapo ndipo alipokuwa akipataka! "Nadhani unajua kama Dina yuko Arusha?" alisema.

"Ndio nafahamu," John alijibu huku sura yake ikionekana kama aliyepigwa na msukule.

"Najua amekuaga kuwa anakwenda kikazi, lakini kwa taarifa yako hakwenda kikazi, bali amekwenda kustarehe na mtoto wa tajiri mwenye kampuni, anaitwa Richard!"

Kutajiwa jina la Richard, John akahisi aina ya kizunguzungu kikiwa kimemwandama. Mapigo ya moyo wake yakaanza kumwenda mbio, damu ikamchemka na uso wake ukawa mzito. Akajizuia ili asiyumbe au kuanguka.

"Najua amekwenda Arusha, lakini kikazi!" hatimaye John alipata nguvu ya kusema. "Unataka kuniambia hakwenda kikazi?"

"Kiofisi imetafsiriwa kikazi, lakini ni zaidi ya hivyo!"

John alijishika kiuno akauinamisha chini uso wake na kuviangalia viatu vyake, akaonekana kufikiri haraka haraka. "Namfahamu Richard, lakini sikujua kama wana mahusiano ya aina hiyo," alisema. "Kwa hiyo waliondoka pamoja?"

"Walipanda ndege moja kwenda Arusha!"

Ilikuwa ni habari mpya kwake! Dina alikuwa hakumwambia kama angesafiri kwa ndege. "Safari hiyo Dina alikuwa akiijua kabla?" aliuliza.

"Mbona aliambiwa mapema tu, siku tano kabla!" "Na alijua kama angesafiri na Richard?"

"Richard ndiye aliyemuita kumfahamisha safari hiyo na kumuahidi kuwa wangeondoka pamoja kwa ndege. Haikuwa safari ya ghafla!"

Dina alinidanganya! John aliwaza baada ya kukumbuka kuambiwa na Dina kwenye simu kuwa, Richard alibaki Dar es Salaam. "Naomba kukuuliza swali moja la msingi…" alisema na kumwangalia Mohsein machoni.

"Niulize," Mohsein alisema kwa kujiamini.

"Kwa nini umekuja kuniambia habari hizi?" John aliuliza na sura yake ikawa makini kumwangalia Mohsein usoni.

Swali hilo lilionekana dhahiri kumyumbisha Mohsein na akaonekana kukosa jibu sahihi. "Ina maana nimekosea kuja kukwambia?" alijikuta akiuliza badala ya kujibu.

"Sina maana hiyo! Nataka kukuuliza swali jingine…" Mohsein hakujibu!.

"Ulikuwa ukinijua?"

"Tatizo nilikuwa sijakuona, lakini nilikuwa nikijua kuna mtu kama wewe ambaye anataka kumuoa Dina! Kwani vipi?"

John alishusha pumzi kwa nguvu kama aliyechoka, kisha akasema, "Basi nimekusikia na nitazifanyia kazi habari ulizonipa."

"Wewe ni mwanamume mwenzangu na mimi hili jambo limeniumiza. Kwa nini akufanyie upuuzi wa namna hii? Dina atakuwa na maana gani ya kukubali kuolewa na wewe halafu papohapo atembee na mwanamume mwingine? Wewe chunguza hizi habari na mwenyewe utajionea. Lakini utakuja kunipa mkono kama nilichokwambia ni kweli!"

"Sawa nimekusikia," John alisema na kuonyesha hakuwa tayari tena kuendelea kuwepo hapo. "Nashukuru kwa taarifa yako!" akamuaga Mohsein na kabla ya Mohsein hajajibu, John akaondoka.

Mohsein akabaki ameduwaa huku akimwangalia John alivyokuwa akiondoka.

John alirudi kufanya kazi akiwa na mtafaruku wa mawazo, muda mwingi alijikuta akizubaa kuzifikiria tuhuma alizotuhumiwa nazo Dina. Moyo wake ulikuwa ukifukuta na mapigo ya moyo wake yalikuwa yakienda kasi. Wivu ulikuwa umetawala kila sehemu ya kiungo chake na hatimaye kujigundua kuwa, hata mikono yake ilikuwa ikitetemeka! Kila wakati alikuwa akisonya peke yake na kuna kipindi alitamani aipige ngumi meza yake ya ofisini!

Ingawa hakuwa na uhakika na sababu hasa zilizomfanya mtu aliyejitambulisha kwake kwa jina la Mohsein kumletea habari hizo, lakini alikuwa mwepesi wa kuziamini kutokana na ukweli kuwa, hata yeye mwenyewe kwa siku za hivi karibuni alijengwa na mashaka makubwa yaliyomtishia kuwa, huenda Dina na Richard wakaurejesha uhusiano wa mapenzi kati yao baada ya Dina kuajiriwa kwenye kampuni ya baba yake Richard ambako Richard anafanya kazi. Lakini, laiti asingekuwa na hofu hiyo tokea awali, kitendo cha Mohsein kumjia na kumpa habari hizo kingemuweka kwenye mashaka ya kutomuamini. Na pengine angemuwekea dhana kuwa, huenda Mohsein alimtaka Dina kimapenzi na baada ya kukataliwa ndipo akaamua kumfanyia fitina.

Lakini ni ile hofu aliyokuwa nayo awali dhidi ya ajira aliyopewa Dina kwenye kampuni ya baba yake Richard ndio iliyomfanya avutike na madai yaliyotolewa na Mohsein, ujio huo wa Mohsein akauona kama vile Mungu alimwelekeza aje amthibitishie mashaka aliyokuwa nayo dhidi ya ajira hiyo kuwa, yalikuwa ni ya kweli! Pamoja na kuziamini habari alizoambiwa na Mohsein, lakini mara kwa mara John alijikuta akiwa kama haamini kama ni kweli Dina angeweza kumfanyia usaliti wa aina hiyo.

Ni usaliti ambao awali walipeana viapo vya kutosalitiana. Mara kadhaa walikwisha kumjadili Richard, wakaapa kupambana naye kuhakikisha hafanikiwi kuwatenganisha huku Dina akichukua jukumu la kula kiapo kuwa, hata iweje, katu asingeweza kurudiana na Richard! Leo kusikia Dina amekiasi kiapo hicho na kukubali kumsaliti, John alijihisi akiteketea kwa maumivu aliyoshindwa kuyafananisha na mengine yoyote yaliyowahi kumtokea tangu ajitambue kuwa anaishi duniani!

* * * * *

WIVU wa MOHSEIN unampelekea kumuuza DINA kwa JOHN....Je nini kitatokea???
***RICHARD amemuweka DINA kimapenzi....je? Atamuoa???

culbby mlyn Analyse princetx slim5 MUSSOLIN ram
 
Last edited by a moderator:
Haya njoo uendelee basi

samahani, msaada wako pse, mimi huku napata vipande vipande vya hii stori, tena vingine vimerukwa, ram naomba msaada wa link yenye mtiririko full!
 
Last edited by a moderator:
duu ngoja nimbembeleze Judy kwanza kwa alichofanyiwa na Richard then niendelee na Dina & John
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…