RIWAYA: Wivu-Beka Mfaume

RIWAYA: Wivu-Beka Mfaume

Habari wanajukwaa, kuna softcopy kadhaa nnazo za hadithi tofauti nkaona si vibaya ku-share ikizingatia watunzi wake wameziweka public hivyo kutohesabika kama wizi wa kazi za watu au kuharibu mapato.. Kila siku nitaweka sehemu moja, watakuwepo ambao wameshazisoma lakini pia kutakua na wengi ambao hawajahi kuzisoma,



mkuu naomba unipm hizi soft copy.
 
duu ngoja nimbembeleze Judy kwanza kwa alichofanyiwa na Richard then niendelee na Dina & John

Jamaa ni zaidi ya fundi - Beka Mfaume ni 1 of the best authors wa kizazi chake!
 

MTUNZI: BEKA MFAUME​


SEHEMU YA KUMI NA TATU

Ingawa hakuwa na uhakika na sababu hasa zilizomfanya mtu aliyejitambulisha kwake kwa jina la Mohsein kumletea habari hizo, lakini alikuwa mwepesi wa kuziamini kutokana na ukweli kuwa, hata yeye mwenyewe kwasiku za hivi karibuni alijengwa na mashaka makubwa yaliyomtishia kuwa, huenda Dina na Richard wakaurejesha uhusiano wa mapenzi katiyao baada ya Dina kuajiriwa kwenye kampuni ya baba yake Richarda mbako Richard anafanya kazi. Lakini, laiti asingekuwa na hofu hiyo tokea awali, kitendo cha Mohsein kumjia na kumpa habari hizo kingemuweka kwenye mashaka ya kutomuamini. Na pengine angemuwekea dhana kuwa, huenda Mohsein alimtaka Dina kimapenzi na baada yakukataliwa ndipo akaamua kumfanyia fitina.

Lakini ni ile hofu aliyokuwa nayo awali dhidi ya ajira aliyopewa Dina kwenye kampuni yababa yake Richard ndio iliyomfanya avutike na madai yaliyotolewa na Mohsein, ujio huo wa Mohsein akauona kama vile Mungu alimwelekeza aje amthibitishie mashaka aliyokuwa nayo dhidi ya ajira hiyo kuwa,yalikuwa ni ya kweli! Pamoja na kuziamini habari alizoambiwa naMohsein, lakini mara kwa mara John alijikuta akiwa kama haamini kamani kweli Dina angeweza kumfanyia usaliti wa aina hiyo.

Niusaliti ambao awali walipeana viapo vya kutosalitiana. Mara kadhaa walikwisha kumjadili Richard, wakaapa kupambana naye kuhakikisha hafanikiwi kuwatenganisha huku Dina akichukua jukumu la kula kiapo kuwa, hata iweje, katu asingeweza kurudiana na Richard! Leo kusikia Dina amekiasi kiapo hicho na kukubali kumsaliti, John alijihisi akiteketea kwa maumivu aliyoshindwa kuyafananisha na mengine yoyote yaliyowahi kumtokea tangu ajitambue kuwa anaishi duniani!

* ** * *

Jioni baada ya kutoka kazini, John hakwenda moja kwamoja nyumbani kama ilivyo kawaida yake, badala yake alikwenda baa nakukaa kaunta. Aliamua kukaa kaunta kwa sababu ya kuepuka kupata ushirika wa mtu anayejuana naye. Alihitaji awe peke yake, asizungumze na mtu yeyote. Mzongo wa mawazo ulishakuwa mshirika tosha kwake! Akanywa vya kutosha na muda wote wa kunywa alikuwa amekipakata kichwa kilichojiinamia kwenye mkono wake.

Hatimaye aliamua aondoke hapo baa. Aliuhisi ulevi ukiwa tayari kichwani, lakini hakuwa na uhakika kama alilewa vya kutosha, pengine aliridhika na kiwango alichokunywa na kukubali kinatosha. Alitoka baa na kuiwasha pikipiki,akarudi nyumbani. Alifika nyumbani usiku uliozidi saa nne, alikuwa hajala chakula cha usiku na hakukihitaji kukila. Alichohitaji ilikuwani pombe aliyokwishainywa kwa ajili ya kukabiliana na maumivu yaliyoletwa na Dina.

Wakati alipokuwa akiufungua mlango alijihisi alikuwa akiyumba, lakini aliamini alikuwa akiyumba kistaarabu. Akaenda moja kwa moja chumbani kwake na kusimama kwenye kabati la kuvalia nguo. Akaichukua picha iliyosimamishwa ambayo ilijengewa fremu yenye nakshi ya kupendeza. Ilikuwa ni picha aliyoipiga akiwa pamoja na Dina, waliipigia ufukoni ikizionyesha nyuso na vifua vyao. John alikuwa kifua wazi kama alivyokuwa Dina,wote walikuwa na mikufu ya dhahabu shingoni mwao, lakini Dina aliongezeka kwa kuwa na sidiria ya kuogelea huku miili yao na nywele ndefu za Dina zikionyesha kulowa maji kuonyesha walitoka kuogelea.Dina alikuwa nyuma ya John akiwa amemuegemea kwa kumuinamia hukua meizungusha mikono yake shingoni mwa John, wote walikuwa wakichekakwa furaha. Ilikuwa picha nzuri!

Akiwa ameishika picha hiyo kwa tahadhari kama vile alikuwa akiogopa isianguke, John alirudi taratibu kinyumenyume huku akiiangalia picha hiyo hadi alipofika kitandani na kukaa. Akaendelea kuiangalia. Mawazo yake yakaanza kuhama, ikawa kama vile picha hiyo ilikuwa ikimkumbusha vipindi vyote vya raha wakati akiwa na Dina. Aliyakumbuka maeneo mbalimbali yaliyowaletea furaha walipokuwa pamoja, lakini kwa wakati huoyalikuwa yakimletea mashambulizi yaliyokuwa yakimwumiza moyoni.Kumbukumbu za furaha na vicheko vilivyotawala vikamkumbusha jinsi walivyokuwa wakizienzi enzi zao za upendo huku kila mmoja akijionaamefika kwa mwenzake.

Hali hiyo ya kuyakumbuka matukio hayoilimfanya John azubae hapo kitandani kama taahira aliyeudhiwa. Ghafla akayahisi machozi yakimtoka. Akaiweka picha kandoni mwake, kisha akajilaza chali kitandani huku kichwa akiwa amekipakata kwenye viganja vya mikono yake na kuiangalia dari ya chumbani kwake. Machozi yakiwa yanatiririkia kupitia kwenye ncha za macho yake, John akaijenga taswira ya kumwona Dina alipokuwa akijinadi kwa kula viapo tofauti huku akimhakikishia kuwa, mwili wake ni kwa ajili ya John nasio Richard au mwanamume mwingine yeyote!

"Ni wewe ndiye uliyechaguliwa John!" John aliisikia sauti ya Dina ikisema nakufanya mwangi uliojirudia. Ilikuwa ni kauli aliyokuwa akiambiwa naDina mara kwa mara. Lakini kwa hapo alipo, John aliiona kauli hiyokama iliyozungumzwa miongo kadhaa iliyopita!

Hasira zikaanzakushindwa kudhibiti uwezo wa akili yake kuweza kujizuia. Akajiinua ghafla, kikafuatia kitendo cha haraka cha kuichukua ile picha nakuitupa kwa kuibamiza ukutani. Fremu ikajiachia na vipande vya vioo vilivyovunjika kuangukia chini na vingine kubingiria hadi kwenyepicha ilipoangukia! Kwa sekunde kadhaa akaiangalia ile picha ambayoilikuwa imejifunika, akalitafsiri tukio la kujifunika kwa picha hiyoni kama dalili za kumalizika kwa penzi lao! Akajikuta akilikataa wazohilo na kujaribu kuliondoa mawazoni mwake. Akili yake haikuamini kamatukio la aina hiyo linaweza likawatokea wao! Ndipo alipotambua kuwa,ni yeye ndiye anayetakiwa kuliokoa penzi hilo lisipotee. Ni yeyendiye aliyetakiwa kumrudisha Dina kwenye himaya yake!

Kumbukumbuza kuwepo kijijini kwao zikamrudia, akamkumbuka mganga aliyekuwaamemwendea! Akayakumbuka maagizo ya mganga na dawa alizopewa ambazoalihakikishiwa zingemfanya Dina awe kama Kondoo wake endapo atajipakadawa hizo usoni muda mfupi kabla hajakutana naye ana kwaana.

Namwendea huko huko Arusha! aliapa.

****

JOHNaliamka mapema asubuhi kabla hakujapambazuka vizuri akiwa amenyongeana kukosa amani ya moyoni. Mawazo yake yalielea kwenye bahari ya wivukila alipoijenga taswira ya uwepo wa Dina na Richard peke yao jijiniArusha. Furaha ilikuwa mbali na yeye na kuhisi maumivu ya moyo hukuakihofia huenda moyo wake umeathirika kiafya. Alikiri kuzidiwa ketena Richard, mpinzani wake wa muda mrefu ambaye leo anamshuhudiaakitumia utawala wa fedha kumyang'anya Dina kwenye mikonoyake.

John aliiwazia karata yake ya mwisho ambayo ingekuwa nisilaha pekee ya kupambana na Richard; karata ya ushirikina aliyopewana mganga! Ilikuwa ndio tumaini pekee la kumrudisha Dina mikononimwake. Aliamini ndio itakayommaliza Richard, ni karata itakayozifanyapesa na utajiri wa Richard visionekane vina umuhimu mbele ya Dina. Nikarata itakayomfanya Dina atekwe na penzi lake na kumwona yeye ndiyekila kitu kwake!

Akaanza kuijenga taswira ya jinsiatakavyomkabili Dina huko Arusha na nguvu ya dawa atakayokuwaamejipaka muda mfupi kabla ya kumkabili itakavyoweza kuifanya akiliya Dina itii kumsikiliza kila atakalomwambia. Aliipanga safari hiyoiwe na lengo moja la kufika na kumchukua Dina na kurudi naye Dar,huku akimuacha Richard akiwa haamini kile kilichotokea mbeleyake!

Lakini kabla ya kuianza safari hiyo ya kwenda Arusha,John alijikuta akipanga kwenda kumwona mama yake Dina na kumshitakiakuhusu usaliti unaofanywa na Dina, lakini pia, akaamua kuifanyasafari hiyo iwe ya siri, hata mama yake Dina asiijue.

Alimkutamama Dina akiwa amekwisha kujiandaa kimavazi kwa ajili ya kwendakazini. Alikuwa peke yake mezani akinywa chai tupu kama kichangamshamwili kabla ya kupata kifungua kinywa kamili atakapokuwa yuko kazini.Ujio wa John asubuhi ya mapema hivyo ulimshitua mama huyo.Akamkaribisha John, John akakaa kwenye meza. Naye akaungana na mamamkwe wake kujimiminia kikombe cha chai tupu.

Nafasi hiyo yakunywa chai pamoja, John akaitumia kuzijenga tuhuma zake dhidi yaDina huku mama huyo akiwa makini kuzisikiliza.

"Ni nanialiyekwambia hizi habari?" mama Dina aliuliza baada ya Johnkumaliza tuhuma zake.

"Aliyeniambia ni mtu wa karibu sana naDina, lakini sitokutajia jina kwa sababu nilimuahidi kuwa,sitomtaja."

"Sawa," mama Dina alisema kwa utulivu."Siwezi kukulazimisha unitajie, lakini kwa mimi ninavyofahamu, huyomtu amekudanganya mwanangu. Richard namchukulia kama mtoto wa hapanyumbani kutokana na jinsi tunavyoishi na wazazi wake na yeyemwenyewe analielewa hilo. Na hata Dina naye analielewa hilo! Uwepo wapamoja kwa Richard na Dina haukuanza juzi kwa sababu ya Dina kuanzakazi kwenye kampuni ya baba yake Richard, walijuana zamani na ukaribuwao ni wa muda mrefu na wako hivyo kama mtu na dada yake, na sivyohivyo unavyofikiri mkwe. Aliyekwambia amekudanganya!"

Johnakatambua alikuwa akitwanga maji kwenye kinu! Hakumlaumu mama huyo,lakini alishindwa kumuelewa ni vipi alikuwa akiliangalia tukio lakukutana kwa Richard na Dina wakati huo anaouzungumzia, kuwa walikuwana ukaribu wa dada na kaka kama majirani. Akaona asipoteze mudakuanza kumwelezea kwa kumthibitishia kuwa, Richard na Dina walikuwakwenye urafiki wa mapenzi wakati huo na angeweza kuiwekea msisitizohoja hiyo kwa kumthibitishia kuwa, ni Dina mwenyewe ndiyealiyeizungumza.

"Basi huyu mtu atakuwa hakunidanganya mimi,bali amejidanganya mwenyewe," John alisema kwa kuhitimisha kauli ya‘kubali yaishe!'

"Uwe mwangalifu na binaadamu mwanangu,ni watu wabaya!" "Kweli mama!" John alisema.

"Halafumkwe, mwenzio aliniambia ulikuwa na mpango wa kuleta mahari hivikaribuni, unatarajia lini?"

John akazikumbuka pesa hizo zamahari alivyompa mganga aliyemfuata kijijini. "Ni kweli nina mpangohuo mama, nitamtuma mshenga hivi karibuni," John alisema nakuyakwepesha kumwangalia usoni mama mkwe wake kwa sababu alikuwaakidanganya.

"Mahari ni muhimu mwanangu ukitoa mapema,itatupa sisi wazazi nguvu ya kumsihi mwenzako awe mwangalifu navitendo vinavyoweza kuashiria mashaka kama haya uliyokuja nayoasubuhi hii. Toa mahari haraka ili na sisi tuanze vikao vya harusi nahili la vikao litasaidia kuiweka akili ya mwenzako kumfanya ajionetayari ni mke wa mtu ili awe na nguvu ya kukabiliana kuepukavishawishi vingine. Usidhani kama kila mtu anapenda nyie mfunge ndoa,wapo watakaojitokeza kuizuia ndoa yenu isifanyike kwa kutumia hilatofauti kama huyo mtu uliyemtaja. Jitahidi mwanangu ulete maharimapema ili muwazibe midomo wabaya wenu!"
"Mama nimekusikia,naahidi nitalitekeleza hilo hivi karibuni," John alisema hukuhatia ikiwa imemtawala. Akaaga.

Kauli ya mama yake Dina kuhusu mahari ilimuweka John kwenye angalizo la awali kuwa, kama angekuwa ameilipa mahari hiyo angekuwa na nafasi ya kumkabili moja kwa moja Richard huko Arusha anakokwenda na angeweza kumpa onyo la kutojihusisha kimapenzi na Dina! Lakini kwa kuwa bado hajailipa mahari hiyo, hakuwa na haki ya kumkabili Richard. Uamuzi wowote wakumfanyia rabsha Richard, Richard angeweza kuuchukulia hatua yakumpeleka polisi!

* * * * *

John alianzia kwenda kaziniambako alitoa udhuru na kupewa ruhusa ya siku tatu bila ya malipo.Huko kukamchelewesha kuwahi kwenda kituo cha mabasi. Alipofikaaliyakuta mabasi yote yakiwa yamejaa kukawa hakuna nafasi ya kuongezaabiria. Akalazimika kupanda basi linaloishia mji mdogo wa Chalinzeambako aliteremka na kwenda kusimama njia panda ambako hupita mabasiyanayokwenda Tanga, Arusha, Mombasa na Nairobi. Huko akafanikiwakupata nafasi kwenye basi litokalo Morogoro ambalo lilikuwa likiendaArusha.

Baada ya safari ndefu ya kilomita kadhaa, basi lao likalazimika kusimama kwa muda wa dakika kumi mjini Mombo kwa ajiliya chakula cha mchana. John aliteremka kutoka kwenye basi lakini hakwenda kula chakula, ilikuwa ni kawaida yake akisafiri huamua kutokula hadi ahitimishe safari yake. Akaagiza soda. Wakati akiinywa soda, simu yake iliita.
Alikuwa Dina!

Simu hiyo ikamchanganya, akasita kuipokea moja kwa moja. Alikuwa hajajianda akiakili kuzungumza naye. Akahisi kama vile Dina amemwona hapo mjini Mombo akiteremka kutoka kwenye basi. Akagundua alikuwa akipoteza muda kwa kujituhumu kipumbavu. Akaipokea simu. "Hai," alisema.

"Mh,vipi mambo?" Dina alisema kwa kuchangamka.

"Huku poa nikama ulivyokuacha," John alisema kwa sauti tulivu, lakini akilini hakukuwa na utulivu.
"Vipi huko?"
"Huku mzigotu."

"Kuna jipya lolote?"
"Ah, litokewapi?"

John akapata akili ya kuuliza. "Huwa mnapiga kazi kuanzia asubuhi mpaka saa ngapi?"

"Huwa tunapiga hadi saakumi na moja, baada ya hapo tunarudi hotelini."

Johnakawaza, kama atawahi kufika Arusha angalau kwenye saa kumi na mbiliza jioni, basi kwenye muda wa saa mbili usiku angeweza kumfuata Dina hotelini. Na huko angemchukua na kwenda naye kwenye hoteli ambayo angefikia, labda vinginevyo, Dina amwombe walale pamoja kwenye hoteli ya Masai Shield alikofikia. Lakini wazo hili la pili kidogo alijikuta akilitia wasiwasi kutokana na kutojua kama Dina na Richard wanalala chumba kimoja au kila mmoja na chake.

"Lakini sio kazi zakukuchokesha sana?" John alisema baada ya kuridhika na hesabuzake.

"Kiasi," Dina alijibu kwa sauti ya maringo.

"Jamaavipi, kishatia timu?" John kwa mara ya kwanza aliuliza swali lililomlenga Richard kwa aina ya utani.

"NaniRichard?"

John akagundua swali la Dina lilikuwa la kuvutia pumzi kulijibu swali hilo. Aliamini hakukuwa na sababu yoyote yakuuliza hivyo wakati alikuwa akijua ni nani anayeuliziwa. "Ndiyo,"alijibu.

"Nasikia ameingia leo," Dina alisema.

Hasiraikachana kwenye moyo wa John! Ananidanganya! aliwaza na kulaani kwakumalizia na tusi. Ilibaki alimanusura ashindwe kuidhibiti akiliyake, na alikwishaanza kuinua ulimi wake kutaka kusema mbovu kupitiakwenye simu, lakini ghafla busara ilimjia, akajizuia. "Kwa hiyohamjaonana?" alisema huku akiilazimisha akili yake itulie.

"Badosijaonana naye, labda nitakaporudi hotelini huenda nikamwona kama nayeye atakuwa amefikia huko."

Likawa eneo jingine la John kujizuia baada ya kuongopewa tena! "Aisii," alisema kwa unyongena kutamani kuaga ili akate mawasiliano, lakini akashindwa kufanya hivyo kwa kuogopa Dina asije akaingiwa na hisia za mashaka za kujiona ameshitukiwa. Isitoshe, ni Dina ndiye aliyekuwa amepiga simu, kwa hiyo atalazimika asubiri hadi Dina mwenyewe atakapoaga kwenyesimu.

"Okay John, nilitaka kusikia sauti yako tu. Huenda baadaye usiku nikakupigia tena," Dina alisema.

Johnakashukuru Dina alivyotamka hivyo. "Poa Dina, hata mimi nimefurahikuisikia sauti yako," alisema.

"Kwa hiyo baadaye.""Poa."

Wakakata mawasiliano. John akasikitika peke yakehuku akiirudisha simu mfukoni.

* * * * *

Waliwasili mjini Arusha mwanga wa jioni ukiwa umeshapotea na John alipoiangalia saa yake ikaonyesha zilikuwa zimebaki dakika chache kufika saa kumina mbili na nusu. Alipoteremka kwenye basi akakumbana na baridi kali,akakodi teksi haraka kabla baridi haijatawala mwilini mwake.Akapelekwa kwenye hoteli moja ndogo iliyokuwa mitaa kadhaa kutokastendi.

Aliingia hotelini na kukaribishwa.

"Utakaasiku ngapi?" Mhudumu wa mapokezi alimwuliza John. "Usiku mmoja,"John alijibu. "Kesho asubuhi naondoka!" Akapewa chumba kilichopoghorofa ya kwanza.

Huko chumbani, John alioga haraka haraka,yalikuwa maji ya moto na yaliweza kuurudisha uchangamfu uliokuwaumepotezwa kutokana na uchovu wa safari. Akabadili shati, akavaafulana nzito ya baridi. Kingine alichokibadilisha ilikuwa chupi,lakini suruali aliirudia ile ile aliyokuwa amesafiri nayo ambayoilikuwa ni jeans. Baada ya kubadili hizo nguo, John alifikiria kwendakula, lakini akalipuuza wazo hilo baada ya kuwaza huendaatakapokutana na Dina, Dina anaweza akamkaribisha chakula cha usikukwenye hoteli ya Masai Shield. Hakuwa na uhakika na hali ambayoangeikuta huko, lakini alikuwa na matumaini Dina asingeweza kumleteaubishi wowote wakati wa mazungumzo yao.

John alizitoa kutokakwenye begi dawa alizopewa na mganga, akaziandaa juu ya meza. Akiwa amekaa kwenye kochi dogo la humo chumbani, alizitia pamoja dawa hizokwenye mkebe mdogo wa plastiki na kuzichanganya, baadaye akachukua kichupa kidogo chenye mafuta na kuyachanganya mafuta hayo pamoja nazile dawa. Akaanza kuzichanganya tena na wakati huo huo akitia niailiyokusudia kumfanya Dina pindi atakapokutana naye, akili ya Dina ipumbazike. Baada ya kuimaliza shughuli hiyo, akaingia hatua yakujipaka dawa hizo usoni na mikononi hadi aliporidhika. Akaenda kujiangalia kwenye kioo kama kulikuwa na mwonekano wowote wakuonekana zile dawa alizojipaka, baada ya kuridhika hakuna dalili zilizoonyesha kuwa amejipaka dawa, John akajiandaa kutoka.

Alitokahotelini na kukodi teksi iliyokuwa imeegeshwa kwenye baa iliyokuwajirani na hoteli aliyofikia. Hakuwa mgeni na mji wa Arusha, hivyomara tu baada ya kuingia kwenye teksi akamwagiza dereva ampelekekwenye hoteli ya Masai Shield.

* * * * *

Richardndiye aliyekuwa wa mwisho kumaliza kuvaa. Alikuwa amesimama mbele yakioo akijiangalia alipokuwa akijifunga tai huku Dina akiwa amekaakitandani naye akimalizia kujivika hereni kwenye sikio lake. Ni mudamfupi uliopita watu hawa wawili walikuwa wametoka kufanya mapenzi nakisha kuoga na kujiandaa kwa ajili ya kwenda kula chakula cha usikuna baada ya kumaliza kula, walikubaliana waende kucheza kamari kwenyeCasino iliyomo humo humo hotelini. Richard ndiye aliyemshawishi Dinaili akaijue kamari inavyochezwa. Dina alikuwa hajawahi kwenye maishayake kuingia kwenye Casino yoyote.

Wote walionekana nadhifu namwonekano wao ulidhihirisha walikuwa ni watu wenye kuogelea kwenyemaisha ya kifahari. Dina alikuwa amevaa gauni la jioni lenye kitambaachepesi, refu na lilifuata sambamba na mwonekano wa umbile lakekuanzia kifuani hadi chini. Kwa yeyote ambaye angemwona asingekuwa nahoja yoyote ya kupinga ughali wa gauni hilo dukani na ulimbwendeuliopo kwa msichana huyo. Licha ya mwonekano aliokuwa akionekana Dinandani ya gauni hilo, lakini Dina alizidi kurembeshwa na vito vyathamani vya dhahabu yenye kiwango bora inayomeremeta. Shingonialikuwa na mkufu mwembamba na mrefu, wenye kito cha almasi iliyokuwaikifanya miali inayong'aa kila kilipogeuka, masikioni mwakekulikuwa na hereni za mviringo mfano wa bangili huku vidole vyakeviwili vya mkono wa kushoto vikivikwa pete, moja yenye kito chaalmasi na nyingine iliyotengenezwa kwa mfano wa ua lichanualo. Kwenyemaungio ya kiganja na mkono wa kushoto kulionekana bangili nnezilizolaliana huku mkono wake wa kulia ukarembeshwa na saa ndogonyembamba ya kike yenye thamani kubwa. Vitu vyote hivyo vilivyokuwamwilini mwake zilikuwa ni zawadi alizonunuliwa na Richard.

"Upo tayari?" Richard alimwuliza Dina na kukitingisha kidogo kitanzi chatai kwa ajili ya kuiweka sawa.

Dina aliinuka moja kwa mojakutoka kitandani na kusema, "Twenzetu!"
Wakatoka.

Walikaribishwana mkuu wa mgahawa ambaye alikwishaanza kumzoea Dina na akawaanamuita kwa jina la ‘Mrs. Richard!' Walikaa kwenye meza ambayoilikuwa imewekwa kibao chenye neno ‘Reserved' na mara baada yakukaa, mhudumu alikiondoa kibao hicho.

Wote waliagiza chakulakilichofanana, viazi vilivyokaangwa na kutiwa vitunguu vilivyokaangwajuu yake na kuku wa kukaanga wa kuchovywa na unga wa ngano uliochanganywa na mayai. Pamoja na kila mmoja kujaziwa maji baridi kwenye glasi ndefu mfano wa puto zilizokuwa zimejenga ukungu wabaridi, lakini pia Richard aliagiza mvinyo mweupe kwa ajili yakusukumizia chakula chao.

Baada ya kumaliza kula, Richard naDina hawakuwa na haraka ya kuondoka mezani, hawakutaka kuwa watu wamwanzoni kuingia Casino. Waliamua kuagiza mvinyo mwingine nakuendelea kuzungumza kwa taratibu, yeyote ambaye angewaona asingesitakuwatabiri kuwa ni wapenzi wapendanao.

* * * * *

Johnaliteremka kutoka kwenye teksi iliyokuwa imesimama sawia kwenyemlango unaoingia moja kwa moja ndani ya jengo la hoteli ya Masai Shield. Teksi ikaondoka na yeye akageuka kuangalia mlangoni. Wahudumu wawili wenye sare za kazi wanaopokea wateja waingiao, walikuwa wamesimama ndani ya mlango wa kioo unaojifungua wenyewe pindi unapokaribiwa na mtu anayetaka kuingia au kutoka. Wote walimwona John alivyoteremka kwenye teksi na wakawa wanamwangalia.

Mara tu mlango ulipojifungua, John akaisikia harufu nzuri kutoka humo ndani; ni harufu ya aina moja ambayo duniani kote utakumbana nayo mara tuukiingia kwenye hoteli za kifahari kama hizo. Alipokuwa akiingia aliwasalimia watu wale na wote waliitika kwa nidhamu nakumkaribisha.

Mteja ni Mfalme! John aliwaza baada ya wahudumu wale kumuinamishia vichwa wakati walipokuwa wakisalimiana. Ilikuwa nimara yake ya kwanza kuingia kwenye hoteli hiyo ingawa alikuwa akiionana kuipita kwa mbali wakati wa siku za nyuma alipokuwa akija Arusha.Aliingia ukumbini kulikokuwa na mandhari ya kupendeza iliyokuwa ikimulikwa kwa taa zenye nuru hafifu ambayo miali yake ilichomoza kutoka kwenye matundu madogo na membamba yaliyopo kwenye dari iliyonakshiwa kwa ujenzi wa kisanii.


***JOHN ameamuakumuibukia DINA huko huko Arusha.....kimya kimya....NIIkitatokea?

**** MAMA DINA amekumbushia suala la mahari.....pagumu hapo!!!


culbbymlynAnalyseprincetxslim5MUSSOLIN ram Mphamvu ICHANA
 
Mtaipata baada ya siku tatu wakuu.. Itakua kwenye PDF

Siku zote hizo mkuu unakuwa unafanya nini? nchi zetu bado sana, huu urasimu tu, wacha niwe mpole maana kitu chenyewe ni msaada.
 
Beka Mfaume hajawahi kunifelisha hata mara moja, eti mtu akiwa zaidi ya "fundi mtaalamu" tunamwitaje!
 
MTUNZI: BEKA MFAUME

SEHEMU YA KUMI NA NNE​

John aliteremka kutoka kwenye teksi iliyokuwa imesimama sawia kwenye mlango unaoingia moja kwa moja ndani ya jengo la hoteli ya Masai Shield. Teksi ikaondoka na yeye akageuka kuangalia mlangoni. Wahudumu wawili wenye sare za kazi wanaopokea wateja waingiao, walikuwa wamesimama ndani ya mlango wa kioo unaojifungua wenyewe pindi unapokaribiwa na mtu anayetaka kuingia au kutoka. Wote walimwona John alivyoteremka kwenye teksi na wakawa wanamwangalia.

Mara tu mlango ulipojifungua, John akaisikia harufu nzuri kutoka humo ndani; ni harufu ya aina moja ambayo duniani kote utakumbana nayo mara tu ukiingia kwenye hoteli za kifahari kama hizo. Alipokuwa akiingia aliwasalimia watu wale na wote waliitika kwa nidhamu na kumkaribisha.

Mteja ni Mfalme! John aliwaza baada ya wahudumu wale kumuinamishia vichwa wakati walipokuwa wakisalimiana. Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuingia kwenye hoteli hiyo ingawa alikuwa akiiona na kuipita kwa mbali wakati wa siku za nyuma alipokuwa akija Arusha. Aliingia ukumbini kulikokuwa na mandhari ya kupendeza iliyokuwa ikimulikwa kwa taa zenye nuru hafifu ambayo miali yake ilichomoza kutoka kwenye matundu madogo na membamba yaliyopo kwenye dari iliyonakshiwa kwa ujenzi wa kisanii.

Kwenye ukumbi huo ambako kulikuwa na ukimya uliovunjwa na mziki mororo wa ala tupu uliosikika kwa sauti ndogo, eneo hilo lilikuwa na sofa za kupendeza ambazo baadhi zilikuwa zimekaliwa na wateja; wengi wao wakiwa ni Wazungu. Pia kulikuwa na matangazo ya huduma mbali mbali yaliyokuwa yakiwaka kwa kunakshiwa na taa za rangi kwenye baadhi ya kuta zilizomo humo ndani. John akaliona eneo alilokuwa akilihitaji; eneo la mapokezi ambalo lilikuwa lipo mbele yake. Kwenye meza ndefu iliyojengwa kwa muundo wa upinde kulionekana baadhi ya wateja waliokuwa wakihudumiwa na wafanyakazi watatu wa idara hiyo mapokezi. Wafanyakazi wote watatu walikuwa ni wasichana warembo wenye sare za kazi zilizofanana.

John alikwenda kusimama kwenye meza hiyo na kusubiri mmoja wa wafanyakazi hao amaliziane na baadhi ya wateja waliokuwepo hapo. Akapatikana mmoja aliyemwendea John.

"Karibu; nikusaidie nini?" msichana huyo wa mapokezi alimwambia John kwa lugha ya Kiingereza.

"Nataka kuonana na mgeni wangu, kati ya Richard Ken au Dina," John alisema kwa kujiamini kwa kutumia lugha ya Kiingereza ambayo hakuwa na umahiri nayo sana.

Msichana akainua simu na kupiga, akaonekana kusikilizia kwa makini. Akairudisha.
"Hawapo chumbani, nadhani watakuwa restaurant wakila chakula cha jioni," msichana alisema.

Hawapo chumbani! John alishangaa.
"Naweza kwenda kuwaona? Mimi ni mfanyakazi mwenzao," alisema na kujaribu kuificha taharuki aliyoipata.

"Unaweza kwenda kuwaona," msichana alisema na kuonyesha kumalizana na John, akataka kuondoka kwenda kuhudumia mteja mwingine aliyefika hapo ambaye alikuwa ni Mzungu.

"Unaweza ukanielekeza? Siijui restaurant yenu ilipo," John aliwahi kusema kabla msichana yule hajaondoka.

Msichana akamwelekeza. "Ahsante," John alisema.

"Unakaribishwa!" msichana alisema na kuonyesha tabasamu bandia la kikazi kisha akamfuata yule mgeni akiyekuwa amewasili.

Pamoja na kuwa alitarajia kitu kama hicho kingeweza kutokea, lakini ule ukweli uliojitokeza kutokana na kauli ya yule msichana wa mapokezi kutoa kauli iliyoonyesha kuwa, Richard na Dina hawakuwepo chumbani, ilimdhihirishia John kwamba, Richard na Dina walikuwa wakikaa kwenye chumba kimoja, ikawa kama vile jambo hilo hakuwahi kulifikiria kabla!

Udhihirisho huo uliomdhihirishia kuwa Richard na Dina walikuwa wakitumia chumba kimoja ulimchanganya. Hasira na wivu vilimjia kwa wakati mmoja na alijishangaa jinsi alivyoweza kujizuia mbele ya yule msichana kutoonyesha kuchanganyikiwa alikokupata. Mapigo ya moyo wake yalikuwa yakimwenda mbio wakati alipokuwa akielekea katika lifti itakayompeleka kwenye ghorofa ulipo mgahawa ambako ndiko alikoelekezwa waliko Richard na Dina. Mkanganyiko uliokuwa kichwani mwake ulimfanya alijihisi kutamani kumuua yeyote kati ya Dina au Richard! Akili yake ilimtuma kutoukubali uzoba aliokuwa akifanyiwa na watu hao.

Akiwa amesimama nje ya mlango kuisubiri lifti iwasili, John alirudia kama mara mbili au zaidi kushusha pumzi za hasira kama vile afanyavyo mtoto mwenye hasira aliyetoka kulia kwa ghadhabu. Alijaribu kuituliza akili yake na kujihisi kama anayeshindwa kuidhibiti. Subira yake ya kuisubiri lifti ilimfanya asitulie sehemu moja, alizunguka huku na kule na kuiona lifti hiyo ikichukua masaa kadhaa kuwasili. Lifti ikawasili, akaingia.

Lifti ilimchukua na kwenda kusimama kwenye ghorofa yenye mgahawa. John alitoka akiwa na baadhi ya wateja wengine waliokuwa wakienda kula kwenye mgahawa aliokuwa akielekea. Yeye na wale wateja kwa pamoja walikaribishwa na msimamizi wa huduma za mgahawani.

"Nataka kuonana na Richard Ken, nimeambiwa yuko huku anakula," John alimwambia mkuu wa mgahawa aliyekuwa ameanza kumwonyesha meza ya kwenda kukaa.

* * * * *

"Yesu wangu!" Dina alisema na papohapo kuonyesha kushituka wakati uso wake akiwa ameuelekeza mlangoni ambako wateja walikuwa wakiingia.

"Kitu gani?" Richard aliuliza na kuangalia alikokuwa akiangalia Dina. Akaonekana kutokigundua kilichokuwa kimemshitua Dina. "Vipi?" aliuliza tena huku akiurudisha uso wake kumwangalia Dina.

Dina alikuwa bado akiangalia mlangoni, kisha kwa sauti ndogo kama vile alikuwa anaongea peke yake akasema kwa kifupi, "John!"

Ndipo Richard akapata mshituko ulioungana na kitendo cha kuangalia tena mlangoni. Kauli yake ikapotea baada ya kumwona mkuu wa mgahawa akimwonyesha John mahali walipo!
John akawa kama aliyezubaa huku akiangalia upande walipo Richard na Dina.

"Wacha nimfuate kule kule!" Dina alisema ghafla na kuinuka. "Mwache aje hapa hapa!" Richard alisema na kumzuia Dina kwa
kumshika mkono. Richard alishaingiwa na wasiwasi kunaweza kukatokea patashika kati ya Dina na John endapo wangebaki peke yao na ndio sababu ya kumzuia Dina. Lakini pia alikifanya kitendo hicho kwa sababu alikuwa akijiamini kupigana, aliwahi kuchukua mafunzo ya karate wakati alipokuwa akisoma Uingereza. Hata hivyo alishakuwa na zaidi ya miaka miwili tokea aliposimama kuendelea na mafunzo hayo na hakuwa na mazoezi ya aina nyingine yoyote tokea alivyorudi nchini, hata hivyo aliamini angeweza kumdhibiti John asimfanyie fujo yoyote Dina kama angewafuata hapo.
"Niache nikazungumze naye," Dina alisisitiza kwa kujiamini. Richard akamuachia! Dina akaondoka na kuharakisha kwenda
kumkabili John kabla hajaingia eneo la ndani zaidi la mgahawa lenye wateja waliokuwa wakila chakula.

Akiwa amesimama huku akimwangalia Dina aliyekuwa akimjia, John alishindwa kuamini kama anayemwona hapo alikuwa ni Dina yule yule aliyekuwa akimlia viapo vya uaminifu. Alijiona kama aliyekuwa akimwangalia Dina mpya mwenye uzuri ulioongezeka ghafla kiasi kwamba hata baadhi ya wateja waliokuwemo humo mgahawani walikuwa wamegeuka kumwangalia.

Dina alipokuwa akielekea kule alikosimama John, hatua zake ziliufanya ule mkufu wa dhahabu wenye kito cha thamani aliouvaa shingoni, kidani chake kichezecheze na kutoa miali ya kung'ara kila kilipokuwa kikitikisika kifuani kwake, na wakati huo huo hereni za dhahabu zilizokuwa mfano wa bangili kubwa nazo zilikuwa zikiyumba masikioni mwake wakati akitembea. Mwonekano wa Dina ulimfanya John apigwe na ganzi huku akishindwa kuamini kama yeye ndiye mmiliki wa mapenzi wa msichana huyo anayekuja mbele yake. Akili yake ilikuwa imepumbazwa na uzuri wa binti huyo aliyeonekana kuwa kwenye daraja la juu la kimaisha. Hasira iliyokuwa imemvaa wakati akiwasili hapo ikaanza kunywea taratibu!

Ghafla akaiona fahari ya kummiliki msichana mzuri wa aina hiyo, tukio hilo likamfanya akumbuke kuwa ni msichana huyo ndiye anayemfanya aingie kwenye ushindani wa kumgombania kati yake na Richard! Na ndiye aliyekuwa akimhangaisha kwenda kwa waganga kwa ajili yake ili afanikiwe kumrudisha kwenye himaya yake!

Siwezi kumuachia Richard! aliapa ghafla. Akayakumbuka madawa aliyojipaka usoni kuwa yalikuwa na uwezo wa kuipumbaza akili ya Dina pindi atakapoangaliana naye machoni! Na hicho ndicho kilichomleta hapo Arusha; aje amchukue na kurudi naye Dar es Salaam!

"Vipi?" Dina aliuliza alipomkaribia John huku sura yake ikiwa kwenye mshangao na nusu kwenye kuchanganyikiwa.

Kitendo cha Dina kumwangalia sawia John kwenye macho yake wakati alipomwuliza swali hilo, ndicho John alichokuwa akikihitaji. Alihitaji Dina ayaangalie macho yake kwa kuamini madawa aliyojipaka ndipo yatakapofanya vyema kazi yake. Na yeye akayatuliza macho yake machoni mwa Dina na kupoteza sekunde kadhaa kama sehemu ya kukoleza ufanyaji kazi wa dawa hizo kabla ya kulijibu swali la aliloulizwa.

"Nimekufuata turudi Dar es Salaam!" John alisema baada ya kujitosheleza na muda alioutumia kuangaliana na Dina, na hata aliposema hivyo, alisema kwa kujiamini. Akatarajia Dina angegwaya.

Lakini badala ya kugwaya, Dina akashangaa!
"Hebu njoo huku!" alimwambia John kwa sauti ya upole lakini yenye amri. Alikuwa akijielewa jinsi anavyoweza kumdhibiti John na alikuwa na uhakika John angefuata alichosema.

John akamfuata! Wakaenda ulipo ukumbi wa baa, wakakaa kwenye sofa. Mhudumu akafika muda huo huo na kuwauliza wanachohitaji kunywa.
"Utakunywa nini?" Dina alimwuliza John.

John akazitambua fikra za Dina kuwa zipo kwenye kumwongoza kama alivyokuwa amezoea siku zote. Kwa kuwa na yeye alikuja hapo kwa imani ya kuleta mapinduzi ya kuyageuza mazoea hayo kwa kuamini dawa alizojipaka, akaona sasa ilikuwa zamu yake kuchukua utawala wa kumtawala Dina kimapenzi.

"Sihitaji kinywaji chochote Dina!" John alisema kwa sauti aliyotaka Dina aione ni amri.
"Nimekuja kukuchukua turudi zetu Dar! Kwa hiyo tuondoke!"

Dina akatengeneza tena mshangao usoni na kumwangalia John. "John umelewa?" aliuliza kwa kujiamini na kuonyesha kiburi kidogo kwenye sauti yake ili kuonyesha ni yeye ndiye mwenye turufu ya utawala wa kumtawala John.

"Ni mzima na akili yangu!" John alijibu kifedhuli huku mikono akiwa ameituliza juu ya magoti yake. Ghafla akajiona ana nguvu za kupambana na Dina kimazungumzo, akaamini dawa alizopewa na mganga zilikuwa zikimpa nguvu hizo!

Jibu la John likamfanya Dina amwangalie mhudumu aliyekuwa bado amesimama akisubiri maagizo.
"Nikikuhitaji nitakuita," alimwambia mhudumu kwa lengo la kumwondoa.
Mhudumu akaondoka.

"Umekuja kunichukua wakati unajua nimekuja huku kikazi?" Dina alimwuliza John kwa utulivu baada ya mhudumu kuondoka.

"Nimeamua! Kwa hiyo tunaondoka pamoja hadi hotelini nilikofikia!" John alisema kwa sauti yenye ushari.
"Na kesho asubuhi tunarudi Dar es Salaam!"

Dina hakujibu haraka. Alitulia kwa sekunde chache huku akimwangalia John kwa dalili zile zile za mtu aliyemzoea huku akionekana kama anayetaka kuisoma akili ya John.
"Unajua John sikuelewi!" alisema na safari hii sauti yake ilikuwa na ukali fulani.

"Hunielewi kwa sababu lugha niliyoizungumza huijui? Au hunielewi kwa lipi?" John aliuliza.

Hata hivyo, John alikuwa ameanza kushangazwa kumwona Dina akiwa bado anaonyesha aina fulani ya ubishi. Alitarajia Dina hadi muda huo angekuwa tayari amekwishapumbazwa na dawa alizojipaka na angekuwa anatii kila analoelezwa. Alitarajia endapo Dina kama angetokea kuhoji, basi angehoji maswali madogo madogo yasiyoashiria aina yoyote ya kuleta ubishi; lakini mwonekano uliokuwepo hapo ulianza kuwa tofauti na matarajio hayo. Dina alikuwa bado akionyesha kuwa na akili zile zile za utawala dhidi yake! John akaanza kuuhoji uwezo wa dawa alizojipaka kama zilikuwa na uwezo wa kumbadilisha Dina.

"Utakujaje ghafla bila ya kuniarifu?" Dina aliuliza kwa sauti iliyoonyesha kukerwa na kuonekana joho la utawala wa kumtawala John likiwa bado maungoni mwake.
"Halafu kufika tu unaniambia umekuja kunichukua unipeleke hotelini kwako! Hakuna kunisalimia, hakuna kuulizana! John umechanganyikiwa?"

"Nadhani nina haki ya kukwambia hivyo! Dina, mimi ni mchumba wako!" John naye alisema kwa ukali wa kujibu mapigo.

Dina akatoa kicheko kidogo cha dharau.
"Haki ya kunikokota unavyotaka? Bado hujawa na haki hiyo John!' alisema kwa utulivu huku akitingisha kichwa chake kuonyesha kusikitika. "Hata mahari yenyewe hujanilipia unaanza kusema hivyo! Je, ukinioa itakuwaje?"

John akamkumbuka mama yake Dina na kauli hiyo ya mahari. Akanywea kiaina, lakini akajipa matumaini ya kuyatawala mazungumzo hayo. Bado alikuwa akiamini dawa zake zingefanya kazi.
"Lakini mimi bado ni mchumba wako Dina!" alisema kwa ajili ya kuendeleza ligi ya ubishi. "Kuna makosa gani kukwambia hivyo?"

"Najua kuwa ni mchumba wako, lakini ndio uamue kunifuata huku Arusha bila ya kunifahamisha kama unakuja?" Dina alisema, kisha ghafla akaonyesha kukerwa na kitendo hicho.
"Kwa nini hukuniambia kama unakuja wakati mchana wa leo tulizungumza kwenye simu? Ulikuwa na mawazo gani kichwani mwako? Huniamini? Lengo lilikuwa ni kunifumania?"

John akapigwa na butwaa! Lakini halikuwa butwaa lililoletwa na kauli hiyo kali ya Dina; bali lilitokana na kule kutomwona Dina kutokuwa na dalili za kulainika! Alijiona bado akizungumza na Dina yule yule ambaye siku zote yuko juu yake.

"Kwa hiyo hatutakwenda hotelini nilikofikia?" John aliuliza swali ambalo alikuwa na uhakika sio jibu la swali aliloulizwa.

"Nakuomba kitu kimoja John!" Dina alisema kiukomavu na kumwangalia John machoni. "Naomba urudi Dar! Kama unalo lolote la kuniambia hata kama nimekuudhi, basi unisubiri hadi nitakapokuja Dar. Samahani kwa kukwambia hivyo, lakini sikudanganyi John; kweli umeniudhi!"

John akapoteza mhimili wa kujizuia, akaonyesha kuanza kuchanganyikiwa. Alizirudisha nyuma nywele zake kwa kuzisukuma na vidole vyake vya mkono. "Dina, bado unanipenda?" aliuliza huku akiwa amekiegesha upande kichwa chake. Swali lake halikuulizwa kimahaba, lilikuwa na aina ya ushari.

"John bwana! Maswali gani hayo unayoniuliza?"

John akagundua alikuwa akipoteza muda kusubiri nguvu za dawa alizojipaka zifanye kazi. Yule mshenzi amenitapeli! aliwaza. Akaachana na mawazo hayo ya kishirikina ambayo yalikuwa yamemjengea subira kwa wakati wote. Akairudisha akili yake kwenye uhalisia wa jambo analokabiliana nalo kuwa, Dina na Richard walikuwa wanalala chumba kimoja humo hotelini! Na isitoshe pia, amewafumania wakiwa kwenye meza moja wakila chakula wakionekana dhahiri ni wapenzi!
Wivu ukarudi upya na subira ikamtoka!

"Mimi najua kila kitu Dina! Usifikiri miye zoba!" John alibwata huku akionekana kuchachamaa ghafla. "Nina habari zenu zote kuhusu wewe na yule mshenzi wako uliyekuwa naye pale mezani!" alisema na kunyoosha mkono kuelekeza upande uliko mgahawa ambako yuko Richard.
"Kwa taarifa yako, najua kama ulisafiri naye kwenye ndege moja! Isitoshe vilevile, najua kama unalala naye chumba kimoja!" alinyamaza na kutweta huku macho yake yakitambaa mwilini mwa Dina.
"Ni nini kilichokubabaisha Dina? Au ni hiki kijiguo pamoja na hizi dhahabu alizoanza kukununulia? Hukuwanavyo hivi wakati ulipoondoka Dar! Uwongo? Kwa muda huu mfupi wa kuja hapa Arusha tayari umeamua kunisaliti? Umeisahau ahadi uliyoniahidi kuhusu huyu jamaa? Umesahau kama uliapa Miungu yote kunihakikishia kuwa hutotembea naye? Umesahau yote niliyokutendea? Umesahau tulikotoka? Unanifanyia haya ukiwa na pete yangu ya uchumba kidoleni mwako Dina?"

Dina aliganda. Akaonekana kama mlemavu asiyeweza kuzungumza. Alikuwa amenywea kama aliyenyeshewa. Akaonekana kama sanamu lenye kupepesa macho. Kiburi na kule kujiamini kukatoweka. Aligwaya!

John alikuwa tayari ameghadhibika!
"Tunaondoka pamoja kwenda hoteli nilikofikia!" alisema na kuukamata mkono wa Dina.

Dina akaufyetua mkono wake kutoka mkononi mwa John.
"Bwana tutakuja kuongea Dar!" Dina alisema na kuonekana kurejewa na fahamu. Akasimama kutaka kuondoka.

John akawahi kumzuia Dina kwa kumshika tena mkono.
"Huwezi ukazungumza na mimi halafu ukataka kuondoka kienyeji, rudi kwenye kiti!" alisema kwa sauti ndogo kujaribu kuwafanya watu wasifuatilie kinachoendelea hapo.

Dina akanywea tena, safari hii macho yake yakawa yameingia woga! Na yeye naye akazungukwa na kiwingu cha hofu kama ya mwenzake ya kuogopa watu wasilifuatilie tukio lao. Akarudi kwenye sofa.
"Mimi nazungumza na wewe halafu unaondoka!" John alisema,
munkari ulikwishaanza kumpanda. "Sasa mimi nakwambia, kwa yule mshenzi wako hurudi! Na utaondoka na mimi!"

"John mimi nipo kazini! Sasa mambo gani haya unayonifanyia? Utaniharibia kazi…" Dina alilalamika kwa sauti ya kujitetea, alikuwa hajawahi kumwona John akiwa katika hali ya hasira kama anayomwona nayo hapo na hali hiyo ilianza kumwogopesha.

"Kazi ya kuja..!" John alitaka kutukana, lakini na yeye akashindwa kumalizia alilotaka kulitamka. "Nitakutukana Dina!" alisema kwa hasira. "Sijawahi kukutukana hata mara moja! Tafadhali Dina!"

Dina hakujibu!
John akasimama.
"Twende!" alisema kwa jazba. Dina hakujibu wala hakuinuka!

Hasira na wivu vikampagawisha John! Akamuinamia Dina na kuukamata mkono wake karibu na kwapa, akaanza kumuinua kwa nguvu. "Nadhani ulikuwa hunijui!" alisema na kuanza purukushani ya kumvuta Dina ambaye alikuwa akigoma kuinuka.

Tukio hilo likaanza kuwavutia wateja na wafanyakazi waliokuwepo eneo hilo. Wahudumu wawili wa kiume wakaenda eneo walilokuwepo Dina na John, wote kwa pamoja wakamvaa John ili amwachie Dina huku wakimsihi aache vurugu. Kitendo hicho kikamfanya Dina apate upenyo wa kuchomoka. Akafyetuka kama mtego ulioteguka, akakimbia kurudi mgahawani alikomuacha Richard!

John alikuwa mtu wa kufanya mazoezi mara kwa mara hasa ya kuogelea na kukimbia, akatumia nguvu za kushitukiza kuwasukuma wahudumu wale wawili waliokuwa wamemzuia na kuwabwaga chini. Akaitumia nafasi hiyo kumkimbiza Dina aliyekuwa nusu anakimbia nusu anatembea!

* * * * *

Richard alikuwa amekosa amani muda wote tokea Dina alivyokuwa ameondoka. Aliwaona Dina na John wakiongozana kuelekea ulipo ukumbi wa baa na kupotea machoni kwake, tokea wakati huo kukawa na ukimya! Alikuwa na uhakika, John alikuja hapo Arusha ghafla kwa kushitukiza na alikusudia kumshitukiza Dina. Hakujua ni nini kilichomleta ghafla, lakini alihisi huenda kuna kidudu mtu aliyemvujishia mahusiano yake na Dina yalivyo hapo Arusha.
Hakutaka Dina akakabiliane na John kama Dina alivyokuwa amesisitiza wakati John alipokuwa ameingia hapo mgahawani. Alikuwa na wasiwasi Dina asingekuwa salama kuwa peke yake na John. Kitendo hicho cha kuondoka pamoja na kwenda kuzungumzia baa na ukimya uliokuwa unazidi kuendelea kukamfanya akose amani. Kuna kipindi alijikuta alishawishika kutaka kumtuma mhudumu wa humo hotelini ili afuatilie nyendo za watu hao wawili, kisha aje kumripotia. Lakini alijikuta akikwama kuutekeleza uamuzi huo kwa hofu ya kuruhusu watu wengine waingilie mambo yasiyowahusu.

Wasiwasi aliokuwa nao kuhusu Dina aliyekuwa mikononi mwa John akiwa peke yake, ulimfanya ajikute akiinywa pombe ya mvinyo kwa kasi iliyomshitua hata yeye mwenyewe. Aliliona jukumu la kumtetea na kumlinda Dina lilikuwa ni lake endapo John ataamua kufanya lolote la kumdhuru. Kwa hiyo, kitendo cha kuendelea kuwepo hapo akiendelea kumsubiri Dina arudi kikawa kinamtia kwenye hali hiyo ya kupoteza umakini wa unywaji wake. Ghafla akawaona wateja waliokuwa wakiendelea kula chakula humo mgahawani walioko upande ambao wanaliona eneo la ukumbi wa baa, wakigeuza sura zao kwa mpigo na kuliangalia eneo hilo.

Richard akatambua kuna walakini unaotokea kati ya John na Dina!

* * * * *

Hakusubiri! Richard aliinuka na kuanza kujitoa katikati ya meza na kiti alichokuwa amekalia. Akawaona wahudumu wakitaharuki, kisha wote kwa pamoja akawaona wakielekea eneo la baa. Tukio hilo likamfanya Richard afanye papara ya kutoka, na alipokuwa akitoka miguu yake ikakisukuma kiti kilichokuwa nyuma yake, kikapiga mwereka na kutoa sauti ya kuanguka. Akiwa hajali tukio la kuangusha kiti kutokana na akili yake kutekwa na kule watu wanakoangalia ambako ndiko waliko Dina na John, ghafla akamwona Dina akitokeza huku akikimbia kumfuata kule aliko! Baadaye akafuatia John aliyekuwa akimkimbiza Dina! Richard hakufikiri mara mbili, alijua Dina yuko hatarini na lilikuwa jukumu lake kumtetea. Akachomoka, lakini hakumfuata Dina!

Alimkabili John!

Wakavaana katikati kama fahali wawili wenye hasira. Wakashikana na kuzoana kimzobemzobe, wakaangushana kwa kishindo kwenye meza iliyokuwa jirani yao ambayo ilikuwa haina wateja. Nyenzo za kulia chakula zilizokuwa zimepangwa kwenye meza hiyo zikaanguka kwa kishindo cha kelele na kutawanyika chini. Hali ya vurugu ikawa imetawala kwa watu hao wawili. Wote walikuwa wameangukia sakafuni na kila mmoja akitaka kuwahi kuinuka kabla ya mwenzake. Wakakikirishana huku kila mmoja akionyesha misuli yake, lakini akawa ni Richard ndiye aliyewahi kutupa ngumi iliyompata John kwenye paji la uso. John alisukumwa chini na nguvu ya ngumi hiyo, Richard akawahi kupanda juu ya mwili wa John ambaye alianza kutoka damu sehemu aliyopigwa ngumi na kuanza kuikaba shingo ya John kwa mikono yake huku akitumia nguvu zote, kama vile alipania kumuua!

Wahudumu ambao walikuwa wakipiga kelele ya kutaka walinzi wa hoteli waitwe, walikwenda kwa pamoja kwenye ugomvi uliokuwa ukiendelea huku Richard akionekana amemdhibiti vyema John katika ile hali ya kumkaba koo. John akaonekana anapoteza nguvu!

"Mtoeni anamuua mwenzake!" kelele za wahudumu na wateja hasa wanawake zilisikika zikihimizana. Baadhi ya wahudumu wa kiume wakamvamia Richard na kuanza kumvuta kumwondoa kutoka mwilini mwa John na kufanikiwa kuwaachanisha. Kitendo hicho cha kuwaachanisha kikampa nafasi John ya kuokota kisu kabla ya Richard hajapata mhimili mzuri wa kujiinua. Kilikuwa kisu cha kulia chakula kati ya nyenzo zilizokuwa zimeeanguka chini, John akazitumia nguvu zake zote kumchoma kisu hicho Richard sehemu ya ubavuni!

Richard alipiga ukelele na kuangukia ubavu uliochomwa kisu na kukishikilia kisu hicho kilichojikita ubavuni mwake. Wakati huohuo damu ikachukua nafasi yake kutoka! Tukio hilo liliwachanganya watu wote waliokuwepo eneo hilo, sura zilizohamanika kwa hofu na taharuki iliyowatawala mioyoni mwao wakaonekana kuanza kuhaha kutafuta eneo la kukimbilia. Baadhi yao wakakimbilia kwenda kusubiri lifti.

Wakati vurugu za kila mmoja aliyekuwepo hapo akisema lake, John aliinuka na kuokota kisu kingine. Uso wake uliopigwa ngumi ukiendelea kuchirizika damu kwenye sehemu iliyopigwa, alianza kutamba kwa kuzunguka kama Sokwe na kuonekana kupagawa. Sura yake iliogofya, macho yake yaliyotapakaa damu aliyokuwa akijaribu kuifuta mara kwa mara kwa kutumia eneo la mkono karibu na bega lake yalionekana kuingiwa na woga. Akaanza mkwara wa kuwatisha kuwachoma kisu wateja wa hoteli waliokuwa wamesimama mbele yake. Wateja hao wakaanza kurudi nyuma huku wakitoa nafasi ya kumpisha John apite.

Kelele za kushakiziana zikaanza, "Jamani mkamateni anakimbia huyo!"

John alikuwa bado akitamba na kisu chake mkononi, aliupindisha mgongo wake kama anayepigana miereka. Alikuwa na mwonekano wa kutisha, alikuwa kama mwendawazimu aliyepandwa na kichaa, aliyazungusha macho yake yaliyoonekana kuwa makubwa ghafla, akawa kama aliyekuwa akitafuta kimbilio. Akawaona baadhi ya wateja waliokuwa wakiwahi kuingia kwenye lifti kulikimbia eneo hilo. Naye akatimua mbio kuelekea huko huko kwenye lifti!

Kelele za taharuki zikasikika! "Huyo anakuja!"

Watu waliokuwa wamekwishaingia ndani ya lifti ambayo ilikuwa haijafunga mlango wakapagawa walipomwona John akikimbilia kwenye lifti walipo wao!

"Jamani huyo anakuja!" kelele za kutaharuki zilisikika kutoka ndani ya lifti.


****WIVU umezua vita!!! vita ya kumuwania DINA....DINA asiyekuwa na msimamo!!!

***NANI ATAIBUKA MBABE????


culbbymlynAnalyseprincetxslim5MUSSOLIN ram Mphamvu ICHANA
 
[FONT=Helvetica, Arial, lucida grande, tahoma, verdana, arial, sans-serif]
[/FONT]

MTUNZI: BEKA MFAUME

SEHEMU YA KUMI NA TANO​
[FONT=Helvetica, Arial, lucida grande, tahoma, verdana, arial, sans-serif]
Keleleza taharuki zikasikika! "Huyo anakuja!"

Watu waliokuwawamekwishaingia ndani ya lifti ambayo ilikuwa haijafunga mlangowakapagawa walipomwona John akikimbilia kwenye lifti walipowao!

"Jamani huyo anakuja!" kelele za kutaharukizilisikika kutoka ndani ya lifti.

Lifti ikaonekana sio tenasehemu ya kujiokoa! Vurugu mechi za kila mmoja kutaka kuwahi kutokakwenye lifti zikaanza kuleta tafrani. Wengine waliowahi kutokawakajikuta wakiangukia mlangoni kutokana na kihere cha kumkwepa mtuwaliyekwishamhesabia kuwa ni mwendawazimu. Baadhi yao walioshindwakujiinua kwa haraka waliamua kutambaa kwa magoti kumkwepa Johnaliyekuwa akielekea kwenye lifti. Ndani ya sekunde zisizozidi tatu,lifti ikawa haina mtu hata mmoja!

Mlango wa lifti ukaanzakujifunga, John akawahi kuuzuia kwa kutanguliza mguu na mkono wake.Akaingia! Lifti ikajifunga mlango, watu waliokuwepo kwenye ukumbi huowote kwa pamoja wakajikuta wakiuangalia mshale uliopo juu ya mlangowa lifti ukionyesha lifti ilikuwa ikishuka chini!

Eneo lamapokezi lililopo chini nako kukawa na sintofahamu ya habari zakutatanisha zilizowafikia kuhusu rabsha inayoendelea mgahawani,habari zikapokewa kwa mitazamo tofauti na kuwaletea mkanganyiko watuwaliokuwepo huko. Kila mmoja alisema lake baada ya mwito wa haraka wakutakiwa walinzi wa hoteli wawahi kwenda eneo hilo. Taarifa hizozikawakurupua baadhi ya walinzi waliokuwepo kuwahi kwenda mgahawanikwa kutumia ngazi badala ya lifti ambayo ilionekana kuchelewa kufikachini.

Lifti aliyokuwemo John ilifika chini na kupishana nawale walinzi walioamua kutumia ngazi. Mlango ulifunguka na watuwaliopo pale wakamwona John akitoka akiwa ameshika kisu mkononi hukuakiwa na damu usoni na mkononi. Taharuki ikawafika, kila mmoja akatoanjia kumpisha John aliyekuwa akikimbia kuelekea mlangoni hukuakitishia kumchoma kisu yeyote aliyekuwa mbele yake!

Mlango wakioo ukajifungua wenyewe baada ya John kuukaribia, akatoka nje hukuwafanyakazi na baadhi ya wateja wakishangaa kumwangaliaakitokomea!



***

DINA alikuwa amechanganyikiwa!Hali hiyo ikawa inamzidia kila alivyokuwa akimwangalia Richardaliyekuwa amelala sakafuni huku akiwa amezungukwa na watu. Wakati huohuo mtu mmoja aliyekuwa amepiga magoti kando ya mwili wa Richardalionekana akitoa huduma ya kwanza kujaribu kuizuia damu kwakumuwekea nguo sehemu yenye jeraha la kisu.
Meneja wa hoteliambaye aliwasili muda mfupi baada ya John kufanikiwa kutoroka bila yakukamatwa, aliwahakikishia baadhi ya wateja na wafanyakaziwaliokuwepo eneo hilo kuwa, gari la wagonjwa lilikuwa lipo njianibaada ya kulipigia simu kulihitaji. Walinzi wachache wa hoteliwaliowahi kufika kabla ya John hajawahi kutoroka na lifti, naowalikuwa wakishutumiwa kwa kushindwa kumzuia John alipokuwa akitorokakwa kutumia lifti. Lakini wao walikuwa wakijitetea kuwa, mazingirayaliyokuwepo hayakuwawezesha kuweza kumkabili John, dai lao kubwalikiwa; hali aliyokuwa nayo John ilikuwa sio hali ya kumvamia bila yakuwa na silaha, vinginevyo angeweza kumjeruhi mtu mwingine au penginehata kuua!

Gari la wagonjwa liliwasili pamoja na gari laPolisi. Wahudumu wa gari hilo waliingia na machela, moja kwa mojawalimchukua Richard na kumwingiza kwenye gari la wagonjwa ambakowalichukua kifaa cha hewa ya oksijen na kukipachika eneo la usoni mwaRichard na kuondoka naye kumwahisha hospitali. Polisi waliowasiliwalipewa maelezo ya haraka kutoka kwa mashuhuda, hususan wafanyakaziwa hoteli waliokuwepo eneo hilo wakati wa mtafaruku huoulipotokea.

Dina akawa mlengwa namba moja wa kuisadia polisi,wakaondoka naye kumpeleka kituoni!

* * * * *

Mara tubaada ya kufanikiwa kutoroka kutoka hoteli ya Masai Shield, Johnaliitumia nafasi hiyo kujipa huduma ya kwanza ya kuizuia damuiliyokuwa ikimtoka usoni kwa kuikandamiza kwa nguvu sehemu yenyejeraha kwa kuitumia leso yake hadi damu hiyo ilipoacha kutoka.Akajifuta baadhi ya sehemu zilizoingia damu na kufanikiwa kwa kiasikidogo kuiondoa damu yote, kisha aliivua saa yake ya mkononi na viatualivyokuwa navyo, vyote akavitupa kwenye kichaka cha eneo lakichochoro alichokuwepo. Baada ya kujiridhisha na hali aliyokuwanayo, akajitokeza barabarani na kukodi teksi iliyomrudisha hotelinikwake.

Alipoingia hotelini, mwonekano aliokuwa naoulimwogopesha mfanyakazi wa mapokezi aliyekuwa zamu.

"Vipi?"mfanyakazi huyo aliuliza huku akionyesha dhahiri alikuwaameshituka.

"Nimevamiwa na wahuni!" John alimlalamikiamhudumu huyo. "Wapi?"

"Maeneo ya huko mitaani," Johnalisema na kuzuga kuelekeza mkono wake upande hewa anakokuzungumzia."Walinivamia kwa nyuma, wamenipiga na kuninyang'anya pesa na vituvingine!"

Mfanyakazi wa mapokezi akaiangalia miguu ya mtejawake na kumwona hana viatu.
"Wamekupora na viatu?" aliulizakama vile viatu ndio vilikuwa muhimu kwake.

"Na saa piawamechukua!"
"Walikuwa wangapi?"

"Siikumbukiidadi yao, nadhani hawakupungua watano. Walinivamia kama mbwamwitu!"

"Simu yako nayo?"

"Hawakufanikiwakuichukua, nilipata upenyo nikawachomoka na kukimbia!"

"Itabidituliripoti tukio hili polisi!"

"Halafu iweje?" Johnaliuliza kwa mshangao.
"Sidhani kama polisi watanisaidiakunirudishia pesa na vitu nilivyoibiwa! Isitoshe wanaweza kunipotezeamuda wangu kwa ajili ya kwenda mahakamani wakati sikumbuki hata suraya mmoja wa vibaka hao. Ninachoshukuru wameniachia uhai wangu.Sihitaji kufanya kesi na mtu yeyote! Nipe funguo yangu ya chumbaninikapumzike!"

"Pole sana!" mtumishi wa mapokezi alisemakisha alitoa funguo na kumpa John.

Huko chumbani, John akiwaamechanganyikiwa alivichukua vitu vyake alivyokuwa amevitoa kwenyebegi saa chache zilizopita wakati alipokuwa amewasili kwenye hotelihiyo akitokea Dar es Salaam na kuanza kuvirudisha tena ndani ya begi.Alikuwa ameamua kutoroka usiku huo kurudi Dar es Salaam harakaiwezekanavyo! Alikuwa na uhakika polisi watakuwa wanamtafuta kwa udina uvumba kutokana na tukio la kumchoma kisu Richard!

Akafanikiwakuvirejesha vitu vyote kwenye begi na kuamua kuondoka, lakinialijikuta akisimama ghafla na begi lake mkononi kabla ya kuufunguamlango wa chumbani. Kilichomfanya asimame hapo mlangoni ni baada yakujiuliza angeelekea wapi akishatoka hapo hotelini? Alikuwa nauhakika muda huo kusingekuwa na uwezakano wa kupata usafiri wa harakautakaomtoa nje ya Arusha! Usafiri pekee ambao ungeweza kumwondoaharaka na kumfikisha angalau mji wa Moshi ungekuwa ni wa teksi,lakini hakuwa na fedha ya kukodi teksi ya kuweza kulipia kwa umbalimrefu kama huo. Isitoshe, bado angehitajika kuwa na pesa nyingine zakulipa gharama za usafiri za kumfikisha Dar es Salaam.

Akaukumbukausafiri wa malori ambayo mengi huanza safari nyakati za jioni hadiusiku. Akaamini usafiri huo ungemsaidia kumwondoa hapo Arusha, lakinikikwazo kikawa, alikuwa hajui wapi angeyapata malori hayo usiku huo.Kwanza alikuwa halijui eneo linaloegeshwa malori hayo, pili, woga wakukamatwa na polisi ulikwisha kumwingia. Hofu hiyo ikamjengea hadhariendapo atahangaika kwenye mitaa kuyatafuta malori ya kumuwezeshakusafiri usiku huo kungeweza kuchangia kumkamatisha kirahisi kwapolisi. Hali ya kuchanganyikiwa ikaanza kumtesa!

Aliondokataratibu pale mlangoni alipokuwa amesimama na begi lake, akarudikitandani na kukaa huku akionekana kuchoka ghafla. Majuto ya tukioalilolifanya la kumchoma kisu Richard yalikuwa yakimtafuna wakatiwote na wakati huo huo akinung'unikia moyoni kuwa yote hayoyasingetokea kama sio Dina kumsaliti! Lakini pia kwa upande mwinginealijilaumu mwenyewe kwa hatua aliyoifanya ya kumchoma kisu Richard.Alijua ulikuwa ni wivu na hasira vilivyomfanya atende hayo. Nafsinialijirai mara kwa mara kuwa, alichotakiwa kufanya baada ya kugunduaukweli kuwa Dina alikuwa amemsaliti, ilikuwa ni kuondoka palehotelini, kisha angefanya maamuzi mengine dhidi ya Dina mbele yasafari.

Maji yalishamwagika!

Hata hivyo kuna wakatialikuwa akijiridhisha kwa kujipa moyo kuwa kitendo alichokifanyakilistahili kwa Richard kwa sababu alitaka kumfanya -----! AlimwonaRichard ndiye aliyepaswa kulaumiwa kwa sababu alikuwa akiyajuamahusiano yake na Dina, na pia, alikuwa akifahamu kuwa, walikuwawakikaribia kufunga ndoa! Kwa nini Richard anifanyie ushenzi kamahuu? alijiuliza. Alitaka kunifanya zoba? Alinidharau kuwa nisingewezakumfanya lolote? John akapiga kite cha hasira humo chumbani,akajiinamia na kukipakata mikononi kichwa chake. Alikiri alikuwaamejiingiza kwenye matatizo mazito ambayo hakuyatarajia, na kwa maraya kwanza alijikuta akiilani siku ambayo yeye na Dina walionana kwamara ya kwanza! Yasingenifika yote haya! aliwaza.

Akiwa badoamejiinamia, mawazo yake yalirudi hotelini Masai Shield nakulifikiria tena tukio lililotokea. Alijikuta akitaka kufahamu haliya kiafya aliyonayo Richard baada ya kumchoma kisu. Hofu ilikuwaimemtawala kwa kitendo hicho, lakini alijipa matumaini kuwa, kisualichokitumia kumchoma nacho Richard kilikuwa ni kisu cha mezani chakulia chakula na aliamini hakikuwa na urefu mkubwa wa kuweza kuingiakwenye mwili wa binadamu na kuleta madhara ya kutishia uhai wa mtu.Hakitakuwa kimemsababishia madhara makubwa! alijipa imani. Sidhanikama anaweza akafa! Wazo hilo likamfanya auinue juu uso wake nakufumba macho. Akasali kimya kimya yasitokee maafa kamahayo.

Kuingiwa na wazo la kuwa anaweza akawa ameua, alijikutaakiingiwa na hofu nyingine ya aina yake! Wazo la kutoroka usikuhuohuo likarudi kwa kasi mpya, lakini pia akapata mashaka na uamuzihuo. Alikiri kuwa, hata kama angeweza kuutekeleza uamuzi wa kutorokausiku huo, bado lingekuwa sio suluhisho, angeendelea kutafutwa napolisi bila kujali kama ameua au hakuua, kwani kosa alilokuwaamelifanya bado ni la jinai na lazima angetafutwa kwa ajilikushitakiwa.

Kwa mzunguko huo, John alikiri kukimbia sio dawaya tatizo hilo, labda angekimbilia nje ya nchi kama vile Kenya.Ingekuwa ni rahisi kwa kutokea hapo Arusha kuweza kukimbilia Nairobi,lakini angekimbilia kwa nani huko Nairobi? Kwanza katika maisha yakealikuwa hajawahi hata kulikanyaga jiji hilo! Pili, alikuwa hamjui mtuwake yeyote anayeishi huko!

Lakini pia, tatizo jinginealiloliona mbele yake ni familia aliyoingia nayo kwenye ugomvi.Familia ya mzee Ken Korogwe! Familia tajiri yenye uwezo wa kuapakupania kumtafuta na wakampata! Ni familia yenye nyenzo zote zauwezeshaji wa kurahisisha kutafutwa kwake popote atakapokimbilia naangepatikana! Ni familia ambayo kwao dunia ni kama kijiji pindiwakianza msako wa kumtafuta. Kwa hiyo hata kama angekimbilia maeneoya Alaska au Australia ambako ni mbali kwa kutokea ukanda wa Afrikaya Mashariki, bado angekamatwa! Hapo pakamvunja nguvu! Akakiri hanapa kukimbilia!

Kukiri huko kuwa hana pa kukimbilia, Johnakaanza kufikiria kujipeleka mwenyewe polisi! Aliuona uamuzi huo ndiowa busara, angejipeleka na angelielezea tukio zima linalohusishamahusiano ya mapenzi kati yake na Dina na wale wote waliojihusisha naDina kwa njia moja au nyingine na angemtaja Mohsein kuwa ndio chachuya kuyajua yote hayo.
Akauafiki uamuzi huo wa kujipeleka mwenyewekituo cha polisi!

* * * * *

Mtumishi wa Idara yaMapokezi wa hoteli aliyofikia John hakuridhika na maamuziyaliyofanywa na John kwa kuliacha tukio la kuvamiwa na wahuni kishakuporwa liishie kimya kimya. Matukio ya aina hiyo yaliwahi kutokeasiku za nyuma kwa wateja wao ambao walidai kama alivyodai John kuwamatukio yaliyowakuta yasiripotiwe polisi kwa ajili ya kukataausumbufu. Awali walikuwa wakizikubali hoja za namna hiyo zilizotolewana wageni wao wa hoteli, matokeo yake hoteli hiyo ikaingia lawamanikuwa ni hoteli inayoshirikiana na vijana wa kihuni kuwaibia wateja wahotelini hapo.

Lakini baada ya kuathirika kibiashara kutokanana sifa mbaya iliyowakuta, utawala wa hoteli hiyo ulichukua hatua zamakusudi kurudisha heshima ya hoteli hiyo kwa kujiweka karibu napolisi kwa matukio yote ya kihalifu ambayo yangewatokea wateja wao.Lakini licha ya kujiweka karibu na polisi, pia wakaamua kuandikawaraka kwa wafanyakazi wote kuwa watoe taarifa kwa uongozi wa hotelipindi linapotokea tukio la kihalifu kwa mteja wao. Waraka huoukasisitiza, yeyote atakayeshindwa kufanya hivyo, hatua kali zakisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Sheria hiyo mpya ndioiliyomlazimisha mtumishi huyo wa mapokezi kutolipuuzia tukio lavibaka kumvamia John lisiishie kimya kimya. Akaenda kuliripoti kwameneja wake wa zamu usiku huohuo.

"Anaitwaje huyo mteja?"meneja wa zamu alimwuliza mtumishi wake baada ya kupokea taarifahizo.

"John Sailas, anatokea Dar es Salaam na aliwasilijioni ya leo. Amepanga chumba namba 112, kwenye fomu ya maelezoamejaza kukaa kwa usiku mmoja. Maelezo yake yanaeleza ni mwajiriwa wacheo cha karani wa stoo na anatarajia kurudi Dar es Salaam baada yakuondoka Arusha."

"Alikuaga anakwenda wapi wakatialipotoka kabla ya kuvamiwa na vibaka?"

"Alikuja na kuachafunguo kwangu na kusema anatoka. Hakuniambia wapi anapoelekea nasikumwuliza. Aliporudi ndio akanieleza kuwa alivamiwa navibaka."

"Ulimwuliza ni wapi alikovamiwa navibaka?"

"Aliniambia alivamiwa maeneo ya katikati ya mji,hakunitajia sehemu rasmi. Tatizo ni kuwa, hakuonyesha kutakakulizungumzia sana tukio hilo na sijui ni kwa nini. Hatanilipomshauri tuliripoti tukio hili polisi, alikataa."

"Itabidituwaarifu polisi, wao ndio watakaoamua kama waje kumhoji au waliachekama mhusika anavyotaka. Huwezi kujua matokeo ya aina hii yana athariza aina gani. Je, kama ni jambazi ametoka kufanya uhalifu na kupatamisukosuko kisha akasingizia kuwa ni vibaka ndio waliomvamia? Hilisuala ni la kuliripoti polisi na wao watajua cha kufanya!"

Mudamfupi uliofuata, madai yaliyotolewa na John ya kuvamiwa na vibaka,meneja wa zamu wa hoteli hiyo akayaripoti polisi!


***


DINANzasa akiwa Kituo cha Polisi cha Mkoa wa Arusha alifanyiwa mahojianona kachero Mussa kuhusu tukio lililotokea hoteli ya Masai Shield.Kabla ya kuruhusiwa kuondoka, alikiri kumfahamu John na akaelezeakuwa ni mchumba wake, lakini pia, alikiri kitendo kilichofanywa naJohn kilitokana na wivu wa kumtuhumu kuwa anatembea na Richard.

"Nikweli unatembea naye?" kachero Mussa aliyekuwa akimhojialimwuliza.

"Siwezi kukujibu swali hilo!" Dinaalijibu.

Mussa akajikuna kichwani kwa kutumia kalamualiyoishika. "John alikuja kufanya niniArusha?"

"Sijui."

"Uliujua ujiowake?"

"Sikuujua. Nilimwona akiingia ghaflahotelini!"
"Alikuwa akijua kama upo Arusha?"

"Ndiyo,isitoshe nilimuaga."

"Alikuwa akijua kama ulifikia hoteliya Masai Shield?"

"Awali hakujua ningefikia hoteli ipi kwasababu hata mwenyewe nilikuwa sijui ningefikia wapi. Lakini baada yakuwasili hapa Arusha ndipo nikawasiliana naye kwa simu nikamwambiakuwa nimefikia hoteli ya Masai Shield."

"Unasema Johnanakutuhumu kuwa unatembea na Richard, ni mahusiano gani yaliyopokati yako na Richard mpaka John afikirie kitu kama hicho?"

"Kamanilivyokwambia awali, Richard ni bosi wangu. Hakuna zaidi yahilo."

"John aliwahi kuziweka wazi hisia za tuhuma hizokwako?"

"Kwa kipindi chote cha uhusiano wetu amekuwa nahisia hizo na alikuwa akizizungumza kwangu."

"Unayo sababuyoyote unayoijua ya kumfanya awe na hisia hizo?" "Kwa sababunilianza mahusiano naye baada ya uhusiano wangu na Richard kuvunjika.Hilo ndilo linalomfanya John asiwe na imani kuwa uhusiano wangu naRichard umekufa."

"Lakini si anajua kama mko pamojakikazi?"
"Anajua."

"Kabla ya tukio hili,kuliwahi kutokea tukio la wao kukutana na kutupiana maneno kwa ajiliyako?"

"Sidhani, kwa sababu hakuna yeyote kati yaoaliyewahi kunilalamikia."

"Ulisema John alipofika palehotelini alikukuta ukiwa umekaa meza moja naRichard?"

"Ndiyo."

"Alisema nini baada yakuwakuteni?"

"Kabla ya kutukaribia pale mezani, niliwahikuinuka nikamfuata na tukazungumza pembeni."

"Alikwambianini baada ya kuwa naye?"

"Tatizo alikuja kiushari,aliponiona tu, akadai kutaka kuondoka na mimi ili twende kwenyehoteli aliyofikia yeye. Nikamkatalia!"

"Alikupa sababu yauamuzi wake huo?"
"Sababu ni kuwa mimi ni mchumbawake."

"Sio kwa sababu amegundua kuwa una mahusiano yamapenzi na Richard?"

Dina hakujibu.

"Alikutajiahiyo hoteli aliyofikia?"

"Tulikosa kuelewana kabla hata yakunitajia hoteli yenyewe. Akataka kunichukua kwa nguvu, ndiponilipoamua kukimbia, akanifukuza. Richard akamzuia na matokeo ndiohayo yaliyotokea."

"Unaweza ukatabiri endapo kama hatorudihotelini ni wapi muda huu anaweza akawepo? Nakuuliza hivyo kwa sababuhatutarajii kumkuta hotelini akiwa amejificha baada ya kufanya tukiokama lile ingawa bado hatujajua ni hoteli ipi aliyofikia."

"Mimini mara yangu ya kwanza kuja Arusha na hajawahi kuniambia kama anajamaa yake yoyote hapa Arusha."

"Unayo pichayake?"

"Unamaanisha kwa kule hotelini nilipo?"

"Kamani hotelini au kwenye simu yako, nikiwa na maana kama nitaihitaji leoninaweza nikaipata?"

"Sina kawaida ya kutembea na pichayake."

Baada ya hapo, Mussa akaonekana kutokuwa na maswalizaidi ya kuhoji. Akalazimisha kuhoji maswali mengine ya hapa na palelakini yakakosa msaada wa kumsaidia kuweza kujua John angepatikanavipi.

"Richard amepelekwa hospitali gani? Nataka kwendakumwona!" Dina alisema baada ya kuhisi askari huyo hana maswalimengine zaidi.

"Bado sijajua. Itanibidi nifanye mawasilianona wenzangu walioondoka naye. Huenda tukaenda pamojahospitali."

Kachero Mussa alimsindikiza Dina hadi nje yaKituo cha Polisi na kumpeleka kwenye gari la polisi, akamwombaamsubiri humo kwenye gari. Kisha Mussa alirudi ndani kituoni nakufanya mawasiliano ya simu na polisi waliokuwa wameongozana naRichard alipokuwa akipelekwa hospitali.

Dina akiwa peke yakekwenye gari la polisi kwa takribani dakika zisizopungua kumi, alikuwakwenye shinikizo lililokuwa likimchanganya. Tukio la kupigana kati yaRichard na John lilimkosesha amani wakati wote na kujikuta akipatawakati mgumu wa kupata jibu baada ya kujiuliza, ilikuwaje John akajuakuwa yeye na Richard walisafiri pamoja kwenye ndege? Na alijuaje yeyena Richard walikuwa wakiishi chumba kimoja?

Dina akakumbukajinsi alivyokuwa amemdanganya John kwa kumwambia alikuwa hakusafirina Richard kwenye safari hiyo ya kuja Arusha. Au ni mama ndiyealiyemwambia John kuwa, yeye na Richard walisafiri pamoja kwenyendege? alijiuliza. Swali hilo likayafanya mapigo yake ya moyo yafanyemshituko baada ya kutambua upo uwezekano wa mama yake kumwambia Johnukweli huo! Dina alijikuta akitamani kujitafuna vidole vyake baada yakugundua alifanya kosa kutomhadharisha mama yake kuhusu sirihiyo!

Ujio wa kurudi kachero Mussa hapo garini ukamwondoa Dinakwenye jinamizi lililokuwa likimwandama baada ya kushituliwa namlango wa gari uliofunguliwa na kumwona Mussa akiingia na kukaa nyumaya usukani.

"Wenzangu walioshiriki kumpeleka Richardhospitali, wanasema Richard yuko chumba cha upasuaji akifanyiwaupasuaji. Nadhani suala la kwenda kumwona ni mpaka kesho atakapokuwaamepelekwa wodini," kachero Mussa alisema na papohapo akaliwashagari.
"Ni vyema nikurudishe hotelini na kesho asubuhinitakufuata kukupa taarifa za hospitali."

"Wanasemajekuhusu hali yake?" Dina aliuliza huku akijaribu kuituliza akiliyake.

"Wanasema, aliingizwa chumba cha upasuaji akiwaanaongea. Inaonyesha hayuko kwenye hali mbaya inayohatarisha maishayake."
"Mungu atamsaidia!" Dina alisema.

"Amen,"Mussa alijibu na kuliondoa gari.

* * * * *

Kwa mara yakwanza tokea awasili hapo Arusha na kuyafurahia maisha ya kifaharikwa kunywa mivinyo mitamu, vyakula vya bei ghali vyenye ladhainayokufanya ujisikie kula, kulala kwenye chumba cha kifahari chahoteli yenye hadhi ya nyota tano, Dina kwa mara ya kwanza alijikutaakiiangalia hoteli hiyo kwa mtazamo tofauti. Sasa hoteli hiyoalivyokuwa akiteremka kutoka kwenye gari la polisi alikuwa akiionakama ngome fulani ya Kishetani! Wakati akiingia hotelini humo eneo lamapokezi aliyahisi macho ya wafanyakazi yakimwangalia tokea mlangonina baadhi yao walidiriki kumpa pole na yeye alizipokea kwa kujibu kwasauti hafifu.

Chumbani ambako mara baada ya kufika alijitupakitandani kama mzigo akiwa na nguo zake. Macho yake yaliangalia juukwenye dari iliyonakshiwa na kujikuta akiirudisha kumbukumbu yakuwaona Richard na John walivyokuwa wakipigana. Tukio hilo lilikuwalimenasa kwenye ubongo wake na kuwa kama gurudumu la sinemalililokuwa likijizungusha kichwani mwake kwa wakati wote. Ni tukiolililomfedhehesha kila alipolifikiria.

Ghafla akaanza kulia!Majuto yalikuwa yamemwinamia na kila kitu kikaanza kujitokezakinyume. Alijiona ni mgeni hotelini hapo, hakuwa na mtu yeyote ambayeangeweza kumshirikisha kwa kumweleza matatizo yaliyomfika! Lakinipia, hata hapo Arusha alikuwa ni mgeni napo, hakuwa na mtu ambayepengine angesema amfuate nyumbani kwake au amuite hapo hoteliniangalau amshirikishe kulijua jinamizi linalomwandama usikuhuo!

Alikuwa peke yake!

Baada ya kulia kwa dakikakadhaa akiwa peke yake humo chumbani, hatimaye akili ikamjia kuwakulikuwepo na mtu hapo Arusha ambaye angeweza kuzungumza naye!Aliamini huyo angeweza kushirikiana naye kulizungumza tatizo hilopengine kwa mapana zaidi ingawa aliamini kusingekuwa na maelewanokati yao.

Alikuwa amemkumbuka John!

Alitaka kuzungumzanaye angalau amfahamishe kuwa polisi walikuwa wakimtafuta na alikuwatayari hata kumpa msaada wa kifedha usiku huo ili atoroke. Alikirinafsini mwake kuwa ni yeye ndiye aliyehusika kumwingiza John kwenyewakati huo mgumu. Fikra hizo za kumwona John ameingia ndani yamatatizo kwa ajili yake zilimwumiza moyo, akamwonea huruma kijanahuyo na kutambua ni jinsi gani anavyompenda!

Nafsi yake ikawaikimsuta jinsi alivyomsaliti mchumba wake huyo, akaulaani moyo wakejinsi ulivyoshindwa kukabiliana na vishawishi vilivyomkabili. Lakinibado alijiona anayo nafasi ya kumwomba msamaha John na angewezakuitumia nafasi ya kumpigia simu kuzungumza naye, pia angeitumianafasi hiyo kumshawishi aondoke haraka hapo Arusha kwakumtahadharisha kuwa polisi wanamtafuta na angemwahidi kumsaidia kwakumpa pesa za kutosha alizopewa na Richard! Angeweza kumtumia pesahizo kwa njia ya simu kwa kuzituma kupitia moja ya ofisi ya kampuniya simu ambayo ina tawi lake hapo hotelini ambalo linafanya kazi kwasaa ishirini na nne.

Dina alijifuta machozi kwa kutumiakiganja chake, kisha akajifuta kamasi nyembamba kwa kutumia nguoaliyoivaa. Uamuzi wa kumpigia simu John ndio ungefuata, lakinialijikuta akipata kigugumizi cha kuufanya uamuzi huo. Alikuwaakiogopa kuzikabili lawama atakazopewa na John, hakuwa na uhakikaangezijibu vipi shutuma hizo. Akapiga moyo konde, akaichukua simuyake na kumpigia John.

John hakupatikana!

Nguvuzikamwishia, kilio kikawa faraja yake!


***DINA katikamajuto, RICHARD hoi hospitali, JOHN katika harakati zakutoroka......NINI HATMA YA SAKATA HILI.[/FONT]
 
Back
Top Bottom