Riwaya ya Kijasusi; Mtoto wa Rais

Riwaya ya Kijasusi; Mtoto wa Rais

RIWAYA; MTITO WA RAIS
MWANDISGI; HALFANI SUDY
SIMU 0652 212391

Sehemu ya Kumi na Nne


Daniel na Martin wakachukua gari kuelekea nyumbani kwa Daniel Mwaseba.

***

Ulinzi katika nyumba ya Donald Tengo ulikuwa mkubwa sana. Kuibiwa kwa Kasiki yenye mipango yao iliyotekelezwa iligonga taa ya tahadhari kubwa sana kwao. Yeye mwenyewe alihama katika nyumba ile na kuhamia katika nyumba yake mpya huko Goba. Pale, aliacha vijana wa Bahari nyekundu ambao walikuwa tayari kumuua yeyote yule atakayejipendekeza.

Huko Goba, Donald Tengo na Balozi Rwekaza walikuwa sebuleni, nje ya nyumba hiyo kulikuwa na ulinzi mkubwa sana. Vijana wa Bahari nyekundu wasiopungua ishirini walikuwa wanazunguka nje ya nyumba huku na kule. Jukumu lao kuu lilikuwa ni kuhakikisha Donald Tengo na yeyote yule aliyopo mle ndani wanakuwa salama salmin.

Wakati huo, Donald Tengo alikuwa ameshika albamu ya picha waliyoipata nyumbani kwa Daniel. Alianza kuifunua na kuangalia picha mbalimbali zilizomo katika albam hiyo.
Picha ya tatu katika albamu hiyo ilimwacha mdomo wazi. Ilikuwa ni picha ikiyomuonesha Daniel Mwaseba akiwa na mtu aliyemtambua kama Salma Lungu!

"Kumbe huyu malaya anajuana na Daniel Mwaseba?" Donald Tengo alisema akishangaa.

"Nani?" Balozi Rwekaza aliuliza huku akimsogelea katika sofa alilokaa.

"Salma Lungu! Angalia hii picha" Donald alisema akimkabidhi ile albam Mzee Rwekaza.

"Khaa, huyu mwanamke kumbe ni nyoka!" Balozi Rwekaza alisema kwa wah'ka mkubwa.

Donald Tengo alijaribu tena kumpigia simu Salma Lungu. Bado simu yake ilikuwa haipatikani.

"Sasa nimeelewa, muda mrefu nilikuwa najiuliza Daniel alijuaje kuhusu mahali ilipokuwa Kasiki yangu ya siri. Sasa nimepata jibu, ni Salma ndiye aliyemwambia. Bila shaka Salma hakuja kwangu kwa bahati mbaya. Ulikuwa ni mpango wa Daniel Mwaseba. Kumbe Joan alikuwa sahihi. Salma, Salma omba nisikukamate Mwanaharamu wewe, nitakuvunja kila kiungo chako cha mwili!" Donald Tengo alisema kwa hasira.

Mara Joan alifika pale sebuleni akiwa na tarakilishi mpakato mkononi. Alikuwa anatembea kaishika mkono mmoja huku mkono mwengine akiendelea kubonyazabonyaza.

"Simu zenu zote zimedukuliwa!" Joan alisema huku akiwasogelea.

"Zimedukuliwa?" Mzee Rwekaza aliuliza kwa pupa.

"Ndio. Nilikuwa naangalia usalama wa simu zenu. Zote zimedukuliwa, najaribu kuzitoa hapa" Joan alisema huku akibonyaza tarakilishi yake.

Donald na mzee Rwekaza walibaki na mshangao.

"Nimefanikiwa. Sasa mko salama" Joan alisema.

"Unaweza kumjua mtu aliyezidukua simu zetu?" Donald Tengo aliuliza.

"Ni ngumu kujua. Mfumo alioutumia unamficha kabisa, huu ni mfumo wa kisasa sana ambao unamficha mtu aliyewadukua. Lakini la muhimu sasa mko salama" Joan alisema.

"Mdukuaji hajaweza kujua zile simu zetu tulizopiga kwa wajumbe?" Mzee Rwekaza aliuliza.

"Hapana, simu kwa wajumbe ninatumia simu maalum sio simu hii" Donald Tengo alisema.

"Joan angalia hii picha" Mzee Rwekaza alisema.

Joan aliiweka tarakilishi yake juu ya sofa na kuichukua ile picha. Mstuko mkubwa ulionekana alipoiangalia ile picha.

"Daniel yupo na Salma!" Alisema.

"Joan ninataka kujua ni nani huyu Salma Lungu!" Donald Tengo alisema.

"Katika mtandao hakuna taarifa zozote kuhusu Salma Lungu. Nilianza kumchunguza ile siku aliyofika hapa nyumbani. Na ndio maana nilimtilia shaka na kukuomba uachane nae" Joan alisema.

"Yuko wapi huyu Binti?" Balozi Rwekaza aliuliza.

"Aliniaga anaenda kwa wazazi wake kijijiji lakini hadi sasa hajarudi. Nimegundua kwamba alikuwa anaondoka baada ya kumaliza kazi iliyomleta."

Joan aliichukua ile picha. Akaanza kuisachi katika mfumo maalum wa utambuzi wa picha. Majibu waliyoyapata kila mmoja alibaki mdomo wazi.

"Huyu mwanamke anajulikana kwa jina la Elizabeth Neville. Sio Salma Lungu kama alivyojitambulisha. Alikudanganya jina." Joan alisema huku akiitazama tarakilishi yake.

"Elizabeth Neville, ni nani?" Donald Tengo aliuliza.
Joan alianza kutafuta taarifa kuhusu Elizabeth. Baada ya dakika kumi ya kuzama katika mtandao wa majasusi alipata majibu.

"Elizabeth Neville ni Afisa wa Usalama wa Taifa!" Amanda alisema huku akimwangalia Donald Tengo.

"Afisa Usalama wa Taifa! Nilifanya kosa kubwa sana kumruhusu mwanamke yule aingie katika maisha yangu. Ona sasa, amepeleka taarifa muhimu sana kwa maadui zangu. Lazima tumsake huyo mwanamke alipe kwa alichotufanyia. Lazima tumsake huyo Malaya!" Donald Tengo alisema kwa hasira.

***

Wakina Daniel walifika nyumbani kwa Daniel. Hofu ilimpanda Daniel alipokaribia getini.

Geti lilikuwa wazi.

"Hapako sawa hapa" Daniel alisema.

"Bobby Bobby" Daniel alimwita mbwa wake lakini bado kulikuwa kimya. Akaichomoa bastola yake kiunoni. Akiwa na bastola mkononi alikuwa anasogea taratibu huku Martin akimfata kwa nyuma akiangaza huku na kule.

"Bobby" Daniel aliita tena huku akielekea katika banda la mbwa wake. Alipofika alimkuta Bobby akiwa amelala chini akichuruzika damu ya moto. Tundu la risasi bichi likionekana katika tumbo lake.

"Ameuwawa.." Daniel alisema kwa majonzi.

Sasa alielekea ndani kwake. Alizidisha tahadhari maradufu, bastola ikitangulia mbele. Huku Martin naye akiwa na bastola mkononi akiitembeza huku na kule. Walifika sebuleni, mlango nao ulikuwa wazi.
Walipofika sebuleni, walikuta kumetawanywa vibaya sana. Kila kitu hakipo sehemu yake. Kama hiki kilikuwa hapa, basi walikikuta pale.

"Martin, kwa walichokifanya hawa watu hawastahili msamaha hata kidogo" Daniel alisema akiificha hasira yake.

"Daniel tutoke nje!" Martin alisema kwa nguvu.

"Kuna nini?" Daniel aliuliza.

"Kuna hatari tutoke...." Martin alisema huku akikimbia na Daniel naye bila kufikiria alifata nyuma. Walivyofika nje tu mara ulisikika mripuko mkubwa sana. Nyumba ya Daniel ilianza kuwaka moto!
Wakati huo, wakina Daniel walikuwa wamerushwa mbali kwa kishindo cha bomu!

Baada ya kama dakika mbili kila mmoja aliinuka kutoka sehemu yake. Akiwa kachafuka vumbi.

"Tuondoke hapa" Daniel alisema baada ya watu kuanza kujaa. Walienda kimyakimya kwenye gari. Martin safari hii ndiye aliyeendesha.

"Wameteketeza nyumba yangu. Kuna vitu vyangu vingi sana vya thamani mle, wamenitia hasara sana" Daniel alisema kwa majonzi makubwa akijilaza kitini.

"Pole sana Daniel, la msingi tupo salama" Martin alisema huku akiwa makini na usukani.

"Martin, ulijuaje kama kumetegwa bomu mle ndani?" Daniel aliuliza akiwa katikati ya mawazo.

"Ni Hisia tu. Hisia za Martin. Ndio maana nikaitwa Martin Hisia"

"Ahsante sana Martin Hisia. Kwa mara nyingine tena hisia zako zimetuokoa katika hatari. Ila Martin naapa kuwasaka watu wote waliohusika kuichoma nyumba yangu. Hakuna atakayebaki salama, wameuchokoza moto mkali sana, katu hawataweza kuuzima. Naapa, hakuna jiwe litakalobaki juu ya jiwe. Nitayatawanya mawe yote!" Daniel alisema kwa uchungu.

Itaendelea...
 
Ahsante mkuu leta Mambo tunasubiri uhondo
 
RIWAYA; MTOTO WA RAIS
HALFANI SUDY
SIMU 0652 212391

SEHEMU YA KUMI NA TANO

Sasa alielekea ndani kwake. Alizidisha tahadhari maradufu, bastola ikitangulia mbele. Huku Martin naye akiwa na bastola mkononi akiitembeza huku na kule. Walifika sebuleni, mlango nao ulikuwa wazi.
Walipofika sebuleni, walikuta kumetawanywa vibaya sana. Kila kitu hakipo sehemu yake. Kama hiki kilikuwa hapa, basi walikikuta pale.

"Martin, kwa walichokifanya hawa watu hawastahili msamaha hata kidogo" Daniel alisema akiificha hasira yake.

"Daniel tutoke nje!" Martin alisema kwa nguvu.

"Kuna nini?" Daniel aliuliza.

"Kuna hatari tutoke...." Martin alisema huku akikimbia na Daniel naye bila kufikiria alifata nyuma. Walivyofika nje tu mara ulisikika mripuko mkubwa sana. Nyumba ya Daniel ilianza kuwaka moto!
Wakati huo, wakina Daniel walikuwa wamerushwa mbali kwa kishindo cha bomu!

Baada ya kama dakika mbili kila mmoja aliinuka kutoka sehemu yake. Akiwa kachafuka vumbi.

"Tuondoke hapa" Daniel alisema baada ya watu kuanza kujaa. Walienda kimyakimya kwenye gari. Martin safari hii ndiye aliyeendesha.

"Wameteketeza nyumba yangu. Kuna vitu vyangu vingi sana vya thamani mle, wamenitia hasara sana" Daniel alisema kwa majonzi makubwa akijilaza kitini.

"Pole sana Daniel, la msingi tupo salama" Martin alisema huku akiwa makini na usukani.

"Martin, ulijuaje kama kumetegwa bomu mle ndani?" Daniel aliuliza akiwa katikati ya mawazo.

"Ni Hisia tu. Hisia za Martin. Ndio maana nikaitwa Martin Hisia"

"Ahsante sana Martin Hisia. Kwa mara nyingine tena hisia zako zimetuokoa katika hatari. Ila Martin naapa kuwasaka watu wote waliohusika kuichoma nyumba yangu. Hakuna atakayebaki salama, wameuchokoza moto mkali sana, katu hawataweza kuuzima. Naapa, hakuna jiwe litakalobaki juu ya jiwe. Nitayatawanya mawe yote!" Daniel alisema kwa uchungu.

"Uelekeo wapi?" Martin aliuliza.

"Kinondoni Biafra, nyumba namba kumi na tatu, karibu na chuo Kikuu Huria" Daniel alisema.

"Kinondoni Biafra kufanyaje?" Martin aliuliza tena.

"Martin, kwa'sasa mapambano ndio yanaanza. Tunahitaji silaha kwa mapambano. Tunahitaji watu wa kutusaidia katika kazi hii. Kuna rafiki yangu yupo kinondoni tutapata vyote hivyo tunavyohitaji. Tutapata silaha pamoja na nguvukazi" Daniel alimfafanulia Martin.

"Lakini Daniel kwanini usiongee na Chifu. Ukimwambia Chifu kuhusu tunachokichunguza lazima atatupa silaha na nguvukazi kutoka ofisini" Martin alishauri.

"Huu sio wakati sahihi wa kumueleza Chifu mambo haya. Tuendelee na uchunguzi wetu endapo tukikwama kabisa basi ndipo tutamjulisha yeye" Daniel alisema.

Baada ya nusu saa walifika Kinondoni Biafra, nyumbani kwa rafiki yake Daniel. Walipiga hodi getini, mlango ulifunguliwa na kijana mmoja mwenye mwili mkubwa.

"Habari yako David. Tumemkuta Samson?" Daniel alisalimu, kuelezea lengo la kuwa pale.

"Nzuri kaka Daniel, naona umekuwa adimu sana siku hizi. Samson yupo ndani huko" David alisema kwa kuchangamka.

"Tupo kaka, mihangaiko tu ya mjini inayotufanya tusionane" Daniel alisema huku naye akichangamka.

Mara mlango wa nje ulifunguliwa.

"Bishoo kumbe upo hapo getini?" Kipande cha mtu alisema akiwa kasimama katika mlango wa kuingilia ndani.

"Nilikuwa napiga soga kidogo na David hapa" Daniel alisema huku akielekea alipokuwa Samson, Martin naye alifuata.

"Habari yako Daniel, umeadimika sana sikuhizi. Huonekani hata katika maeneo yetu. Umenisahau hata mimi Swahiba wako?" Samson alimuuliza Daniel huku akitabasamu.

"Habari ni safi kabisa, tupo wote Samson, ni mihangaiko tu ya kimaisha si unakua tena.." Daniel alisema huku naye akitabasamu.

"Mambo vipi kaka" Samson alimsalimia na Martin Hisia.

"Safi kaka, za hapa?"

"Hapa mambo yote yako poa. Eeh nambie Daniel una jipya gani? Maana najua ujio wako huu sio wa bure" Samson alisema akimwangalia Daniel.

"Samson nipo katika misheni moja ngumu sana, na pengine ndio sababu hatuonani mara kwa mara, na pia ndio sababu iliyonileta hapa kwako. Kwa nilipofikia katika misheni yangu nahitaji vitu viwili kutoka wako. Ninaomba unisaidie.." Daniel alisema kwa kirefu.

"Hesabu umepata chochote unachohitaji kutoka kwangu, wewe ni rafiki yangu wa siku nyingi sana. Wewe ndiye uliyenibadilisha kutoka katika ujambazi hadi kunisaidia kufungua kampuni halali ya ulinzi. Siwezi kukutupa Daniel. Niambie ni vitu gani unataka kutoka kwangu nami nipo tayari kukusaidia" Samson alikubali bila hata kujua vitu vyenyewe ambavyo Daniel alihitaji.

Daniel alivuta pumzi baada ya kuyatafakari maneno ya Samson. Yalimgusa sana. Alikumbuka siku ya kwanza alipokutana Samsoni katika misheni moja huko Mbeya. Baada ya sekunde chache akasema "Nimekuja kwako Samson, ninahitaji silaha kadhaa na watu wanne. Katika hao watu wanne, wawili wawe wadunguaji wenye shabaha kali, mmoja awe mtu wa teknolojia na mwengine awe mtu wa mapambano ya ana kwa ana"

"Kama nilivyosema awali, umepata, hata ukihitaji zaidi ya watu hao nitakupatia. Nifuateni.." Samson alisema,

Daniel na Martin walimfuata Samson, alielekea nyuma ya nyumba yake. Wakawakuta vijana wengi wakifanya mazoezi wakiwa wamevaa sare nyeusi. Walipomuona Samson waliacha kufanya mazoezi.

"Amani, Amini, Leonard na Karim nifuateni" Samson alisema. Kisha wakaelekea katika nyumba ndogo iliyopo pembeni ya nyumba ya Samson. Alipofungua, Daniel na Martin walibaki midomo wazi. Walikuwa wanatazamana na kila aina ya silaha.

"Chagueni silaha mzitakazo" Samson alisema.

Daniel na Martin walichagua silaha walizozitaka. Bunduki, bastola, visu, mabomu madogo ya mikono na ndegenyuki. Waliporidhika wakarejea ndani.

"Ahsante sana Samson, umenisaidia sana leo" Daniel alisema wakati wakiagana. Wakapanda gari wakaondoka wakiwa na wale vijana wanne. Moja kwa moja walielekea katika nyumba mpya ya Daniel Mwaseba, Tabata.
Ndani ya gari ilikuwa kimya.
Walipofika Tabata walishusha zile silaha na kuingia nazo ndani ya nyumba..

"Naona mmekuja na wageni" Hannan alisema huku akinyanyuka sofani.

"Ndio. Tumeamua kuongeza nguvu katika timu yetu. Wahenga waliwahi kusema kuwa umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Hannan nawe pia tumekuongezea nguvu. Huyu hapa ni Leonard ni mchawi mwenzio wa Kompyuta. Hawa hapa Amini na Amani ni wadunguaji, na huyu hapa mnene ni Karim, mtaalam katika mapigano ya aina zote" Daniel alitoa utambulisho.

"Karibuni sana katika familia hii. Hasa Leonard karibu sana" Hannan alisema huku akicheka.

"Ahsante sana sana" Wakina Amini walijibu.

"Amani, Amini, Karim na Leonard karibuni sana katika timu yetu. Hii ni timu mpya kwenu lakini nina imani mtafanya kazi kwa umahiri mkubwa sana. Mimi hapa ninaitwa Daniel Mwaseba, huyu mwenzangu anaitwa Martin Hisia na huyu dada anaitwa Hannan Halfani. Sisi tunafanya kazi ya uchunguzi kwa niaba ya Serikali. Kwasasa tunamchunguza waziri mmoja anaitwa Donald Tengo." Daniel alinyamaza na kuangalia umakini wa watu aliokuwa anaongea nao. Aliridhika na umakini wao.

"Leo hii tunaenda kuvamia nyumba ambayo tunaamini Donald Tengo atakuwepo. Bila shaka nyumba hiyo itakuwa na ulinzi mkali sana. Kuwa na ulinzi mkali hilo sio tatizo kwetu, tutaenda kuingia kwa namna yoyote ile, lengo kuu ni kumpata mtu anayeitwa Donald Tengo na tumlete hapa. Huyu mtu anatakiwa akiwa hai kwa maana kuna taarifa nyeti sana tunazihitaji kutoka kwake" Daniel alisema, wakati wengine wote wakimsikiliza.

Itaendelea...
 
RIWAYA; MTOTO WA RAIS
HALFANI SUDY
SUMU; 0652212391

SEHEMU YA KUMI NA SITA

"Leo hii tunaenda kuvamia nyumba ambayo tunaamini Donald Tengo atakuwepo. Bila shaka nyumba hiyo itakuwa na ulinzi mkali sana. Kuwa na ulinzi mkali hilo sio tatizo kwetu, tutaenda kuingia kwa namna yoyote ile, lengo kuu ni kumpata mtu anayeitwa Donald Tengo na tumlete hapa. Huyu mtu anatakiwa akiwa hai kwa maana kuna taarifa nyeti sana tunazihitaji kutoka kwake" Daniel alisema, wakati wengine wote wakimsikiliza.

"Amini na Amani mtakuwa katika gari yenu, mkitulinda na kuhakikisha hatufatiliwi na mtu yoyote yule. Mimi, Leonard na Martin tutakuwa katika gari yetu pia. Leonard utatusaidia kufanya utundu wako ili kujua namna ulinzi utakavyokuwa. Hapo ndipo mimi na Martin tutajua namna ya kuingia ndani ya nyumba. Karim na Hannan mtabaki hapa nyumbani mkihakikisha kila kitu kinaenda sawa" Daniel alisema.

"Daniel, ni sahihi kweli kwenda tena nyumbani kwa Donald Tengo? Sasahivi atakuwa ameimarisha ulinzi, itakuwa ni ngumu sana kuingia tena ndani kwake na kumpata" Hannan alisema kwa uwoga.

"Usihofu Hannan, kila kitu kitakuwa sawa. Wewe na Karim bakini hapa kuhakikisha ulinzi unaimarishwa hapa nyumbani. Hakikisheni Candy na Cindy wanakuwa salama. Hii ni nyumba yangu pekee iliyobaki baada ile ya awali kuungua" Daniel alisema.

"Imeungua nyumba yako Daniel?" Hannan alishangaa.

"Ndio, tumenusurika kuuwawa leo kwa bomu. Nyumba ya Daniel ilikuwa imetegwa bomu" Martin alisema kwa sauti ya kuchoka.

"Daah pole sana Daniel" Hannan alisema kiupole.

"Na kazi ikaanze kama ilivyopangwa. Hannan endelea kuchimba zaidi taarifa za Donald Tengo na Balozi Rwekaza tuone utapata kitu gani? Tukirudi utuambie, pia usisahau kuangalia na simu ya Robin kuna jipya gani?" Daniel alisema.

Wakaondoka.

Gari mbili ziliongozana na kutoka Tabata, nyumbani kwa Daniel Mwaseba zikielekea Masaki, nyumbani kwa Donald Tengo. Gari ya mbele, katika usukani alikuwepo Daniel mwenyewe, pembeni yake alikuwepo Martin na katika viti vya kati alikuwa amekaa Leonard, mtaalam wa teknolojia. Katika gari iliyokuwa inawafuata kwa nyuma walikuwepo Amini na Amani wakiwa makini na kila kinachoendelea.

Saa moja baadae walifika mita chache kutoka katika nyumba ya Donald Tengo. Daniel alipaki gari mita chache kutoka katika nyumba hiyo.

"Leonard, angalia namna ulinzi wao wa ndani ulivyo" Daniel alisema akimgeukia Leonard.

Katika siti za nyuma Leonard alimtoa Kipepeo wa plastiki, lakini kwa kumwangalia alifanana kila kitu na Kipepeo halisi. Alikuwa na rangi nyekundu na vibaka vidogovidogo vyeupe na vyeusi.

"Nakupenda sana kipepeo wangu. Naomba kanifanyie kazi yangu mpenzi wangu. Umesikia?" Leonard alisema mithili anaongea na mwanamke mrembo. Akamfungua yule Kipepeo kwa nyuma na kumweka betri ndogo ya saa. Akafungua dirisha la gari. Kisha akabonyaza kitufe kidogo kilichokuwa tumboni kwa yule ndege. Kipepeo alianza kuruka. Akachukua rimoti na kuanza kumuongoza. Kipepeo akaruka kuelekea nyumbani kwa Donald Tengo huku Leonard akifatilia katika simu yake.

"Tuambie chochote mchawi wetu" Daniel alisema baada ya kipepeo kuruka.

"Nimemrusha Kipepeo wa bandia, kipepeo yule macho yake ni kamera ambayo moja kwa moja inaleta picha zote katika simu yangu. Kipepeo wangu mpendwa anaenda kuchunguza mazingira yote ya ile nyumba. Tutaona ndani kuna walinzi wangapi na jinsi walinzi walivyojipanga.

"Safi sana Leonard, kazi nzuri" Daniel alisema kwa hamasa. Alivutiwa na mbinu ya Leonard.

"Getini kuna walinzi watano wenye silaha. Wote wamevaa nguo za walinzi nyekundu." Leonard alisema baada ya Kipepeo wake kufika maeneo ya getini.

"Angalia kwa ukaribu, ni walinzi kutoka kampuni gani?" Martin alisema.

Leonard akamsogeza yule Kipepeo karibu zaidi.

"Juu ya mfuko wa shati wa kulia wa sare zao kumeandikwa Bahari nyekundu..Itakuwa ni wa kampuni ya Bahari nyekundu" Leonard alielezea.

"Angalia hiyo kampuni kama ipo? Na Makao yao makuu yapo wapi?" Daniel alisema.

Leonard akaanza kupekua katika tarakilishi yake aliyoilaza katika kiti, kama dakika sita hivi, kisha akasema "Hakuna kampuni ya ulinzi iliyosajiliwa kwa jina hilo hapa Tanzania"

"Wamewatoa wapi sasa hawa walinzi?" Martin alishangaa.

"Ngoja nimzungushe Kipepeo nyumba yote tuone kuna walinzi wangapi?" Leonard alisema.

Baada ya kumzungusha, Leonard akasema "Jumla ya walinzi ishirini wenye silaha, na hapo bado hatujajua ndani kuna walinzi wangapi? Hapa mahali panalindwa kweli. Donald ni waziri wa fedha tu, au kuna lengine analolifanya? Kuwa na walinzi ishirini wa kampuni binafsi sio jambo la mzaha" Leonard alijiuliza.

"Hadi sasa tunajua ni waziri wa fedha" Martin alisema.

"Hiyo haitoshi. Kujua taarifa ambayo kila mtu anaijua huko si kumjua mtu. Kujua kama Donald ni waziri wa fedha hata mtoto wa darasa la nne anajua. Kumjua mtu ni kuyajua yale ambayo watu wa kawaida hawayajui" Leonard alisema huku akibonyaza tarakilishi yake kwa kasi ya ajabu. Wakati huo Kipepeo wake akiwa karibu na mlango wa kuingia katika nyumba ya Donald Tengo.

"Donald Tengo ni mmoja wa kiongozi wa kundi la Bahari nyekundu" Leonard alisema baada ya kubofyabofya.

"Ndio nini hiyo Bahari nyekundu?" Daniel aliuliza.

"Daniel! Hujawahi kusikia kuhusu Bahari nyekundu. Hiki ni kikundi cha kihalifu kinachoogopwa sana hapa jijini. Makundi mengi ya kihalifu yanawahofia sana Bahari nyekundu. Nasikia wanadhaminiwa na wauza madawa ya kulevya wakubwa hapa nchini" Leonard alisema.

Daniel na Martin walibaki kuwa wasikilizaji. Mara mlango wa kuingia ndani ya nyumba ya Donald Tengo ulifunguliwa. Leonard alimuongoza yule kipepeo kuingia ndani. Sasa zikaanza kuonekana picha kutokea ukumbini.

Ndani ya ukumbi kulikuwa na watu watatu. Daniel alimtambua mtu mmoja kati ya wale, yule jamaa aliyemfungia katika chumba kidogo chenye bomba la maji ya baridi.

Alikuwa Mzee Kizito.

"Hebu peleka kamera kwa hao wengine wawili" Daniel alisema.

"Ngoja tuwapige kabisa na picha ili tujue ni kina nani hawa?" Leonard alimjibu.

Kipepeo alipiga picha zisizo na mwanga.

Leonard akachukua waya akaunganisha kutoka katika simu yake kwenda katika tarakilishi. Zile picha za wale watu zikawa zinaonekana katika kioo cha tarakilishi yake. Akaanza kubonyaza harakaharaka kama ana vidole saba katika kila mkono wake. Mfumo maalum wa picha ukaanza kutafuta. Baada ya kama dakika mbili akasema.

"Huyu aliyevaa shati jeusi anaitwa Salum Taiwan" Ngoja nimpekue zaidi ni nani hasa huyu Salum Taiwan?

Leornad akasema tena baada ya kupekua "Salum Taiwan ni meneja wa tawi la benki la LDB huko wilayani Muheza, jijini Tanga"

"Na huyo mwengine?" Daniel aliuliza.

"Anaitwa John Gunda , yeye ni mfanyakazi wa benki ya LDB tawi la Mlimani city" Leornad alisema.

"Wote ni wafanyakazi wa benki ya LDB, hii inatupa picha gani?" Daniel aliuliza akimwangalia Martin.

"Tuna cha kukichunguza ndani ya benki ya LDB, matokeo haya yanatupa shaka" Martin alisema.

Wakati kina Daniel wakijadiliana, Salum na John waliagana na yule mtu mwengine. Wakapeana mikono na kuanza kutoka nje.

"Wanaondoka hawa" Leonard alisema.

"Tutawafuata kwa siri tuone wanaelekea wapi? Na lazima tujue walikuwa wanaongea nini na yule jamaa?" Daniel alisema.

"Vipi kuhusu Donald Tengo?" Martin aliuliza.

"Inavyoonesha Donald hayupo mle ndani, ila tutapata majibu sahihi kupitia kwa hawa wafanyakazi wa benki ya LDB" Daniel alisema.

Mara wale jamaa wakafungua mlango wa sebuleni. Leonard akaitumia nafasi hiyo kumtoa kipepeo wake. Akamuongoza hadi katika gari. Na wakati huo ndio geti kubwa lilifunguliwa. Wale majamaa walitumia gari moja kutoka nje. Na Salum Taiwan ndiye aliyekuwa anaendesha. Wakina Daniel wakaanza kuifuata ile gari kwa nyuma.

Itaendelea...
 
RIWAYA; MTOTO WA RAIS
HALFANI SUDY
SIMU; 0652 212391

SEHEMU YA KUMI NA SABA

Wakati kina Daniel wakijadiliana, Salum na John waliagana na yule mtu mwengine. Wakapeana mikono na kuanza kutoka nje.

"Wanaondoka hawa" Leonard alisema.

"Tutawafuata kwa siri tuone wanaelekea wapi? Na lazima tujue walikuwa wanaongea nini na yule jamaa?" Daniel alisema.

"Vipi kuhusu Donald Tengo?" Martin aliuliza.

"Inavyoonesha Donald hayupo mle ndani, ila tutapata majibu sahihi kupitia kwa hawa wafanyakazi wa benki ya LDB" Daniel alisema.

Mara wale jamaa wakafungua mlango wa sebuleni. Leonard akaitumia nafasi hiyo kumtoa kipepeo wake. Akamuongoza hadi katika gari. Na wakati huo ndio geti kubwa lilifunguliwa. Wale majamaa walitumia gari moja kutoka nje. Na Salum Taiwan ndiye aliyekuwa anaendesha. Wakina Daniel wakaanza kuifuata ile gari kwa nyuma.

Safari haikuwa ya mwendokasi sana. Jamaa walikuwa wanaendesha taratibu. Uelekeo wao ulikuwa ni maeneo ya Mwenge. Nyuma, wakina Daniel waliifatilia gari bila kuruhusu wakina Salum wajue kama wanafatiliwa. Nyuma yao, kama magari matano katikati, gari la kina Amani lilikuwa linawafata kwa umakini mkubwa sana. Amani na Amini walikuwa wanahakikisha wakina Daniel hawapatwi na matatizo.

Walipofika Mwenge gari la kina Salum likakata kushoto, likiifuata barabara ya Sam Nujoma. Baada ya mwendo kama wa dakika tano hivi wakakata kulia, wakaingia katika jengo la Mlimani city. Gari lao lilisimama katika sehemu ya kupaki magari ya Mlimani city bila yeyote kushuka, si Salum wala John. Ilichukua dakika zipatazo kumi ndipo John alishuka, na Salum naye akafata. Wote walielekea katika jengo la Mlimani city.

Nyuma yao, wakina Daniel walipaki gari yao karibu na uzio wa Mlimani city. Walishuhudia kila hatua waliokuwa wanaipiga wakina Salum. Waliposhuka na kuingia katika jengo la Mlimani city, Daniel akamwambia Martin, "Tuwafate, tuone wanaelekea wapi? Leonard utabaki ndani ya gari ukitusubiri"

Kisha Daniel akawapigia simu wakina Amini.

"Niambie mkuu" Amini alisema baada ya kupokea simu.

"Vipi hali ya usalama?"

"Usalama uko poa. Tumewafata tangu nyumbani kwa Donald Tengo, hakuna hatari yoyote ile na wala hakuna mkia wowote unaotufatilia" Amini alisema.

"Safi Amini, sasa sisi tunawafata hawa jamaa ndani ya jengo. Nataka ninyi mhakikishe usalama wetu. Mkiona kitu chochote kile cha ajabu msisite kutuambia" Daniel alisema.

"Hakuna shida mkuu, tutawalinda" Amini alisema, simu ikakatwa.

Daniel na Martin nao walishuka ndani ya gari. Wakaufuata uelekeo wa jengo la Mlimani city.

"Humu ndani kuna tawi la benki la LDB, bila shaka watakuwa wameingia humo" Daniel alisema.

"Inawezekana. Hawa watu wana mpango gani na benki ya LDB?" Martin aliuliza.

"Tutajua sio muda" Daniel alisema.

Waliingia ndani ya jengo la Mlimani city, na moja kwa moja walielekea katika eneo ambalo kulikuwa na ofisi ya benki ya LDB, wakaingia. Wakaangaza angaza, lakini hawakuwaona wakina Salum.

"Twende kwenye dirisha la mapokezi tukaulize" Martin alisema.

"Tusiende wote, nenda wewe" Daniel alimwambia Martin.

Martin akasogea hadi katika dirisha la mapokezi. Kulikuwa na wadada wawili waliovaa fulana za kijani za benki ya LDB, huku chini wakiwa wamevaa sketi fupi za kijivu. Martin alimfata Mhudumu aliyekuwa hana mteja. Alikuwa dada mmoja mweupe huku nywele zake akiwa amezisuka kwa mtindo wa rasta.

"Habari yako dada?" Martin alisalimia.

"Karibu LDB kaka yangu, sijui nikusaidie nini?" Yule dada alisema huku akitabasamu.

"Samahani, nilikuwa namuulizia rafiki yangu, anaitwa Salum Taiwan" Martin alisema.

Yule Dada alifikiria kidogo, kisha akasema "Hakuna mfanyakazi mwenye jina hilo hapa"

Martin akajua yule dada alikuwa sahihi. Kwa mujibu wa taarifa za Leonard, Salum Taiwan alikuwa ni mfanyakazi wa LDB lakini katika tawi la Muheza huko mkoani Tanga.

"Basi sawa dada yang..." Lakini kabla Martin hajamalizia kusema yule mhudumu mwengine alidakia.

"Fina, Salum Taiwan si nd'o yule mfanyakazi mpya tuliyetambulishwa leo asubuhi" kauli hii ilimstua sana yule dada mwingine. Mstuko ambao ulionwa na macho ya Martin.

"Atakuwa yupo wapi?" Martin aliuliza.

"Nilimwona akielekea katika ofisi ya meneja, nenda kamwangalie kule" Yule Mhudumu alisema huku akionesha kwa kidole ilipo ofisi ya meneja. Martin alielekea mahali alipoelekezwa baada ya kumshukuru yule dada. Njiani aliandika ujumbe mfupi kuelekea kwa Daniel, kisha, akapapasa bastola yake, ilikuwa sawa. Katu hakumhofia yule mlinzi mmoja aliyekuwa akirandaranda ndani ya benki na bunduki yake mkononi.

Daniel alitoka pale alipokuwa amesimama na kwenda katika dirisha la mapokezi. Alimfuata yule dada ambaye aliulizwa mwanzoni na Martin kuhusu Salum Taiwan.

"Habari yako dada" Daniel alisalimu.

"Samahani kaka naomba akuhudumie huyo, kuna kazi kidogo naifanya" Yule dada alisema huku akichezea simu yake.

"Nd'o hata salamu hutaki kuitikia, au kwasababu unamtumia meseji Salum Taiwan!!" Daniel Mwaseba alisema bila wasiwasi wowote ule.

Itaendelea..
 
Bado watu wawili itimie section ya kimapigano poti asante sana wanyumbani
 
RIWAYA; MTOTO WA RAIS
IMEANDIKWA NA HALFANI SUDY
0652 212391

SEHEMU YA KUMI NA NANE

Mstuko mkubwa sana ulionekana katika sura ya yule dada. Hakuweza kustahamili kuishika simu yake, ilimdondoka chini bila ya kupenda.

"Vipi Fina?" Irene alimuuliza mwenzake.

Fina hakujibu kitu, alibaki katika mshangao tu huku akimwangalia Daniel Mwaseba kwa macho yaliyojaa uwoga, wakati Daniel alikuwa anatabasamu.

"Wewe ni nani?" Irene aliipata sauti yake.

"Sidhani kama kuna umuhimu wa kulijua jina langu, kwasasa nitakwambia kazi yangu tu, mimi ni afisa wa jeshi la Polisi, na kuanzia sasahivi upo chini ya ulinzi" Daniel alisema huku akikidondosha kitambulisho chake juu ya meza, tabasamu lake likiwa palepale.

"Kwani kuna nini? Mbona sielewi jamani?" Irene aliuliza kwa wasiwasi.

"Fina atakuelewesha, haya Fina mwambie mwenzio, kuna nini?"

Fina alibaki kimya, alichoweza kufanya ni kutetemeka tu mwili mzima.

Daniel alichomoa simu yake, akabonyaza namba fulani na kuipiga. Akaiweka simu sikioni.

"Hallo Leonard" Akasema.

"Nambie kaka, vipi kila kitu kipo sawa?" Leonard akauliza.

"Kila kitu kipo sawa. Naomba mchukue askari mmoja hapo getini uje naye ndani ya benki ya LDB"

"Sawa kaka, nimekuelewa"

"Samahani kaka usinipeleke Polisi" Fina alianza kulia kama mtoto mdogo.

"Ninaweza nisikupeleke Polisi, lakini endapo utaniambia Salum Taiwan ni nani?" Daniel alisema huku akimwangalia Fina.

"Mimi simfahamu Salum Taiwan kwa kina, ila alinifata leo asubuhi na kunipa shilingi laki mbili, nilimuuliza za nini? Akaniambia za kumfanyia kazi yake ndogo tu. Nilimuuliza kazi gani? Aliniambia ya kumpa taarifa endapo mtu yeyote atakuja kumuulizia hapa mapokezi" Fina alisema.

"Na ndio ulikuwa unaitekeleza hapo hiyo kazi yako" Daniel alisema bila wasiwasi wowote.

Fina alibaki kimya.

"Sasa twende katika ofisi ya Meneja" Daniel alisema akimwangalia Fina.

Fina akasimama huku akitetemeka. Yeye na Daniel walielekea katika ofisi ya Meneja. Wakati wakiwa njiani simu ya Daniel iliita.
Alikuwa ni Leonard.

"Upo wapi Daniel, tupo ndani ya benki ya LDB"

"Njooni moja kwa moja katika ofisi ya Meneja"

Daniel na Fina waliingia katika ofisi ya Meneja.

"Kazi nzuri sana Martin" Daniel alisema baada ya kuona alichokifanya Martin.
Mle ndani kulikuwa na watu watatu, Martin alikuwa kawadhibiti wote kwa kuwafunga kamba na kuwaweka konani. Yeye, alikuwa ametulia tuli kwenye kiti mithili ya Meneja.

"Wamesema lolote?" Daniel aliuliza.

"Sijawahoji kitu, nilikuwa ninakusubiri wewe" Martin alisema.

Mara mlango ulifunguliwa, aliingia Leonard akiwa na askari mwenye silaha.

"Kuna nini humu?" Askari aliuliza kwa ukali.

"Tulia afande, sisi ndio tumekuita humu ndani" Daniel alimtuliza.

"Yaani mnataka kumteka Meneja wa benki?" Askari alihoji tena huku mishipa ya kichwa ikiwa imemsimama.

"Tungetaka kumteka Meneja wa benki ungelialikwa humu ndani?" Daniel naye alitupa swali.

"Daniel hatuna haja ya kupoteza muda. Tuwahoji hawa watu askari ataambiwa kaitiwa nini hapa?" Martin alisema.

Daniel alimeza funda la mate, kisha akasema " Mimi ninaitwa Daniel, Daniel Mwaseba "Watu wote walishangaa baada ya Daniel kutaja jina lake. Mle ndani hakuna ambaye hajawahi kulisikia jina la Daniel Mwaseba, mpelelezi namba moja aliyekuwa haishwi kuandikwa kila leo katika magazeti na vitabu mbalimbali vya kijasusi.
"Kwa kifupi tupo tunapeleleza matukio fulani ya kihalifu. Katika uchunguzi wetu ukatufikisha hadi katika nyumba ya waziri wa fedha, Mh Donald. Na wakati tukiwa katika harakati za kuingia ndani tuliona hawa watu wawili wakitoka. Tuliamua kuachana na mpango wa kuingia katika nyumba ya Donald na kuwafata watu hao. Lengo letu ni moja tu, kujua mlifata nini katika ile nyumba? Au mna uhusiano gani na Mh. Donald Tengo?" Daniel aliuliza swali.

Wale watu wote walibaki kimya.

"Nadhani nyote mna masikio yanayosikia vyema. Tusilazimishane mpaka tuumizane ndipo mseme. Mna hiyari ya kuamua kusema hapa kabla sijawafanya kitu kibaya!" Daniel alisema kwa ukali.

Kwa macho yake, Daniel alimwona Salum akimwangalia Meneja kwa uwoga. Daniel akajua kwamba Salum ndiye mtu sahihi wa kumchukua kwa pale. Alionekana anataka kusema kitu ila alihofia uwepo wa wenzake.

"Salum Taiwan" Daniel akaliita jina sahihi la Salum. Mstuko dhahiri ulionekana kwa watu wote watatu. Daniel hakuwa na wasiwasi, alikuwa anamsogelea huku akichomoa kisu kidogo kiunoni kwake. "Utanieleza juu ya maswali yangu, kabla ya kunieleza sababu ya kutoka Muheza hadi hapa. Ukileta ubishi, nakukata vidole vyako vyote!" Daniel alisema akimaanisha.

"Daniel, sio mimi, ni Hashim!" Salum alisema akimwangalia meneja.

"Hashim ndio nani?" Daniel aliuliza.

Salum akayapeleka tena macho kwa Meneja. Daniel akajua kwamba yule meneja ndio Hashim.

"Afande, unaitwa nani?" Daniel akamgeukia yule askari.

"Afande Peter" Askari alijibu kwa heshima.

"Unatoka kituo gani?" Daniel akamuuliza tena.

"Kituo cha Polisi cha Oysterbay" Peter alijibu.

"Sasa, waambie wenzako waje humu ndani. Mtawachukua Meneja wa benki, John na Fina na kuwapeleka kituoni. Nitakuja kuwahoji huko. Kwasasa tunaondoka na Salum kwa mahojiano maalum. Tukimaliza naye tutamleta aungane na wenzie" Daniel alisema.

"Sawa Afande" Peter alisema huku akipiga saluti.

Kwa kutumia simu ya upepo ya Polisi, afande Peter aliwaita wenzake. Wakaja na kuwabeba wakina John, huku wakina Daniel wakiondoka na Salum Taiwan.

"Kwanini hukumhoji palepale?" Martin alimuuliza kwa siri Daniel.

"Salum ana mambo mengi sana ya kutueleza. Lakini pale hapakuwa sehemu sahihi. Asingekuwa huru kutueleza mambo mbele ya Meneja Hashim" Daniel alisema.

"Nimekuelewa Daniel" Martin alikubali. Walienda kuingia kwenye gari wakiwa na Salum, na kuelekea nyumbani kwa Daniel Mwaseba.

"Martin, mpeleke Salum katika chumba cha mahojiano" Daniel alimwambia Martin walipofika nyumbani kwake.

"Naona mmerudi na mgeni, vipi kuna mafanikio yoyote huko?" Hannan aliuliza.

"Ni kweli tumerudi na mgeni. Anaitwa Salum Taiwan, ni meneja wa benki ya LDB huko Muheza. Hayo ni machache tunayoyajua kwasasa, nataka umchimbe zaidi kabla sijaenda kuongea nae" Daniel alisema.

"Ok ngoja nizitafute taarifa zake" Hannan alisema huku akianza kuchezea tarakilishi yake.

"Jamani hii kazi bado haijatufikisha katika matumaini. Angalau tumejua lengo la watu hawa ni kumuua Rais, lakini bado hatujajua watamuua kwa namna gani? Na nini sababu ya kumuua Rais? Tukipata majibu ya maswali hayo pia tutakuwa tumejua wakina nani ni wahusika. Niwaombe kitu kimoja ndugu, tutaifanya kazi mfululizo, usiku na mchana hadi tupate majibu. Na hivyo ndivyo nifanyavyo kazi siku zote. Kuna muda ninaweza kufanya kitendo kibaya sana, msinichukulie mimi ni katili sana, ni namna tu ya kupata taarifa muhimu. Naomba tuvumiliane" Daniel alisema huku akiwaangalia wakina Amini kwa zamu.

"Tumekuelewa mkuu. Na pia tuna furaha sana kufanya kazi na mtu kama wewe" Amini alijibu kwa niaba ya wenzake.

"Eeh Hannan umepata nini juu ya Salum Taiwan?" Daniel alimgeukia Hannan.

"Salum Taiwan ni baba wa mtoto mmoja. Mtoto wake anaitwa Aisha. Salum hana mke, mkewe alifariki mwezi mmoja uliopita baada ya gari lake dogo kutumbukia katika daraja la mto Wami, wakati akitoka Dar es salaam kuelekea Muheza.

Siku chache zilizopita Salum amehamishwa kutoka katika tawi la benki la Muheza alipokuwa anafanya kazi na kupelekwa tawi la Mlimani city" Hannan alisema huku akiangalia kioo cha tarakilishi yake.

"Nimejaribu pia kudukua simu ya mkononi ya Salum, lakini cha kushangaza hakuna kitu chochote kile. Taarifa zote zimefutwa" Hannan alisema.

"Kuna cha kutilia shaka, kwanini taarifa za simu ya Salum zifutwe?" Amini aliuliza.

"Hatuna haja ya kujiuliza maswali wakati Salum mwenyewe yupo humu ndani. Ngoja nikapate majibu" Daniel alisema huku akielekea katika chumba cha mahojiano alipokuwa Salum.

"Martin, unaweza kutoka nje, nataka humu ndani tuwe mimi na Salum tu" Daniel alisema. Salum aliyekuwa amekaa katika kiti alikuwa anamwangalia Daniel kwa uwoga mkubwa sana.

Daniel alisogea ukutani na kubonyaza swichi, alizima kamera zote mle ndani.

"Salum, sasa tupo mimi na wewe. Nataka uniambie kila kitu unachopaswa kuniambia. Usinifiche kitu chochote kile" Daniel alisema.

Salum alikuwa anamwangalia.

"Sipendi kukutesa Salum. Sitaki Aisha akakosa baba pia. Aisha hastahili kuwa yati.." Daniel hakumaliza alichotaka kusema.

"Nooo! Usiseme chochote kuhusu Aishaaa.." Salum aliongea huku akidondosha machozi.

"Salum, niambie ulifata nini nyumbani kwa Donald Tengo?" Daniel hakujari kama Salum alikuwa analia".

Itaendelea..
 
Duh kama ndo mm Naingia kumuhoji salum dah poti mbona atakoma
 
Back
Top Bottom