Riwaya ya Kijasusi; Mtoto wa Rais

Riwaya ya Kijasusi; Mtoto wa Rais

Naamini komenti hii ni ya memba ambaye shule hakwenda ila alijifunza kusoma na kuandika akiwa mtaani.

Nakushauri utafute nukuu za fasihi andishi halafu chambua kipengele cha Riwaya, naamini ukifanya hivyo utakuwa umejinasua kwenye kundi la wasema ovyo.
Acha upumbavu mbwa wewe, sifa kubwa ya fasihi ni kuakisi mazingira husika. Watu kama nyie ndo mnashindwa kutofautisha hekaya na riwaya. By the way mi sikwenda shule kusomea ujinga kama wewe.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Acha upumbavu mbwa wewe, sifa kubwa ya fasihi ni kuakisi mazingira husika. Watu kama nyie ndo mnashindwa kutofautisha hekaya na riwaya. By the way mi sikwenda shule kusomea ujinga kama wewe.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
Siwezi kuendeleza ligi na mtu asiye na akili wala elimu. Na jinsi ulivyo na debe tupu lazima utarudi kuandika upupu.

Ila hujachelewa nipo tayari nikulipie ada angalau upate elimu, make kukosa vyote ni janga.
 
Siwezi kuendeleza ligi na mtu asiye na akili wala elimu. Na jinsi ulivyo na debe tupu lazima utarudi kuandika upupu.

Ila hujachelewa nipo tayari nikulipie ada angalau upate elimu, make kukosa vyote ni janga.
Hollywood kuna watu wanaitwa critical kazi yao ni kukosoa sana . Kabla ya movie yoyote kutoka huwa wanaitwa kuangalia, maoni yao ndio yanafanya movie inunuliwe au idode.
Mtu anapokosoa sio lazima awe ana chuki au wivu wakati mwingine anasaidia kuboresha ili kitu kiwe bora.
 
RIWAYA; MTOTO WA RAIS
HALFANI SUDY
0652 212391

Sehemu ya Ishirini na Tatu

Wakati Martin, Daniel, Amini, Amani na Karimu walitoka nje. Safari ya kuelekea Masaki nyumbani kwa Joash Mtoto ilianza. Walitoka na gari mbili, ya mbele ilikuwa imepandwa na Daniel Mwaseba, Martin na Karim. Wakati nyuma walifuatiwa na wakina Amini.

Kutokana na foleni waliyokutana nayo barabarani iliwachukua wakina Daniel saa zima kufika Masaki, nyumbani kwa Joash Mtoto. Wakiwa njiani mara kwa mara waliwasiliana na Hannan, na mara zote Hannan aliwaambia kuwa simu ya Aneth bado ilikuwa ndani ya nyumba namba hamsini na tisa, Masaki.

Walifika Masaki, walipaki gari mita chache nje ya nyumba ya Joash Mtoto. Na kama kawaida wakina Amini wao walipaki kwa mbali kidogo wakifatilia kila kitu.

"Timu ya wadunguaji wametuambia kila kitu kipo sawa. Sasa tunaenda kuingia katika hii nyumba, ambayo tunaamini Aneth yupo ndani yake. Umakini unahitajika kama ilivyo ada ya Mpelelezi yeyote yule duniani" Daniel aliwapa tahadhari.

"Tunaingiaje? Kwa kuvamia au kistaarabu?" Karim aliuliza.

"Tutaingia kistaarabu kwa kwenda kugonga geti. Mbinu itabadilika kutokana na tutakavyopokelewa huko ndani. Lengo la kwanza la misheni hii ni kumpata Aneth akiwa hai. Lengo la pili la misheni hii ni kumpata Aneth akiwa hai. Na lengo la tatu la misheni hii?" Daniel aliuliza.

"Ni kumpata Aneth akiwa hai" Martin na Karim walijibu kwa pamoja.

Walishikana mikono huku Daniel akigawa majukumu. Na misheni ilianza. Karim alibana upande wa kushoto wa geti. Daniel alibaki upande wa kulia, wakati Martin alienda kugonga geti. Kila mmoja alikuwa karibu sana na bastola yake. Hawakujua nini kitatokea katika sekunde inayofuata.

"Ngo ngo ngo" Martin aligonga geti kwa mkono wake wa kushoto.

"Ngo ngo ngo ngo" Aligonga tena kwa mara ya pili baada ya ile ya kwanza kupokelewa na ukimya. Lakini bado iliendelea kupokelewa na ukimya.

"Jaribu kusukuma geti" Daniel alisema kwa sauti ndogo iliyofikiwa na masikio ya Martin Hisia.

Martin akasukuma geti dogo. Geti likafunguka. Martin aliutumia upenyo huo kuchungulia ndani. Hakuona kitu chochote zaidi ya maua yaliyopangiliwa kwa mpangilio mzuri.

"Ingia ndani, kuwa makini sana Martin" Daniel alisema kwa kunong'oneza.

Martin alinyata taratibu, bastola ikiwa mbele. Aliingia mle ndani na kwa kasi alielekea katika kibanda cha mlinzi. Ilianza kufika bastola yake kibandani kabla ya yeye. Akiwa kibandani aliangalia mazingira yote ya mle ndani. Kulikuwa kimya kabisa, kimya, kimya, kimya.

"Mnaweza kuja kuko salama" Martin aliongea kwa kutumia vifaa walivyovaa masikioni. Wakina Daniel nao wakaingia ndani na bastola zao mikononi. Wote wakichukua tahadhari kubwa sana. Walielekea pale katika kibanda cha Mlinzi.

"Haujakuta mtu hapa?" Daniel aliuliza naye alipofika.

"Hapana, hakuna mtu" Martin alijibu.

"Yatupasa kwenda ndani. Bila shaka Aneth yupo ndani ya nyumba hii. Hannan kanitumia meseji kusisitiza bado simu yake ipo humuhumu ndani" Daniel alisema kwa uhakika.

"Sawa, tunaenda ndani kwa kulindana. Tuhakikishe hakuna anayefanya kosa lolote lile, kosa moja tu litaamua hatma ya mwengine" Martin alisema akitoa tahadhari.

Alianza Daniel Mwaseba, alijibiringisha kwa namna ya ajabu hadi mlangoni. Ilikuwa ni mithili ya tairi la gari likisukumwa na mtoto mdogo. Martin naye akafata kwa mtindo uleule, mwisho Karim alienda, lakini hakuweza kuwaiga wale wanaume wawili. Wakipekee. Yeye alitambaa kama nyoka wa kijani.

"Tunaingia ndani, umakini zaidi unahitajika. Nitapiga hodi, isipojibiwa tutaingia kwa namna yetu" Daniel alisema.

Alijaribu kupiga hodi. Lakini kulikuwa kimya. Akabisha tena hodi, bado kulikuwa kimya. Akajaribu kuufungua ule mlango. Ulikuwa umefungwa. Akatoa rundo la funguo mfukoni. Akajaribu funguo ya kwanza, ikakataa. Akajaribu ya pili, ikakataa, akajaribu funguo ya tatu, mlango uliitika. Mlango uliwachekea.

Daniel alitangulia kuingia ndani akifatiwa na Karim, kisha Martin. Wote bastola zilikuwa zimetangulia mbele ya vifua vyao. Walikuwa makini sana.

Pale sebuleni napo, hawakukuta mtu. Ila zaidi ilionesha sebule ilikuwa imetawanya vibaya sana. Wakajua kuwa kuna mtu asiyehusika alikuwepo pale kusaka kitu kisicho chake, ni nani huyo? Na alikuwa akisaka kitu gani?.

Wanaume walijigawa. Wakasonga mbele kila mmoja akipita upande wake. Walipekua kila chumba ndani ya nyumba ile, cha kushangaza mle ndani hakukuwa na mtu katika vyumba vyote vitano. Baada ya dakika nane wote walirejea tena sebuleni. Zaidi ya bastola zao mikononi, hawakuwa na Aneth wala Joash Mtoto...

"Lakini bado inaonesha simu ya Aneth ipo humu ndani" Daniel alisema akisisitiza.

"Tuitafuteni, pengine ipo sehemu fulani" Karim alishauri. Wakaingia kazini tena, wote wakaanza kuisaka simu ya Aneth katika kila chumba. Kila mmoja akitanguliza tahadhari na umakini kabla ya bastola yake.
Ni Karim ndiye aliyeikuta simu ya Aneth uvunguni mwa kitanda katika chumba cha tatu, upande wa kushoto. Ilikuwa rahisi kwake maana alipoingia tu chumbani, simu iliita. Na jina la mpigaji lilisomeka juu ya kioo cha simu.

'Kaka'

Kama walikuwa sahihi, basi Aneth alikuwa anapigiwa na kaka yake. Rais Mark alijaaliwa kupata watoto wawili katika uzao wake, wa kwanza alikuwa ni Moses na wa uzao wa pili ni Aneth. Kwa maana hiyo kaka wa Aneth ni Moses, je ndiye aliyekuwa anapiga simu?

Karim aliichukua ile simu hadi kwa wenzake.

"Simu ni hii hapa, lakini inaita" Karim alisema.

"Nani anapiga?" Daniel aliuliza.

"Jina limeandikwa Kaka" Karim alisema. Na simu iliacha kuita. Hapo ndipo Karim alipoangalia kwenye kioo. Kulikuwa na simu zilizopigwa bila kupokelewa thelathini na saba, na zote zilitoka kwa mtu mmoja tu 'Kaka'.

"Kuna kitu hakipo sawa" Daniel alisema.

"Unahisi Aneth ametekwa?" Martin aliuliza.

"Hilo ni jibu Martin. Sasa ni wakati wa kutafuta ni kina nani waliomteka? Na kwanini wamteke? Pia lazima tujiulize kwanini simu yake ije kutelekezwa nyumbani kwa Joash Mtoto?"

Wakiwa pale sebuleni, simu ya Daniel iliita.
Alikuwa ni Hannan.

"Daniel vipi mmempata Aneth?" Hannan aliuliza kwa pupa.

"Bado, vipi kuna taarifa zozote umezipata?" Daniel naye alitupa swali, huku hofu ikianza kumwandama moyoni mwake.

"Nimeona habari sasahivi mtandaoni. Kuna taarifa kuwa mwili wa Aneth umeokotwa katika ufukwe wa bahari ya Coco, inaonesha ameuwawa na kutupwa huko!"

"Aneth ameuwawa?" Daniel alistaajabu.

"Ndio, Daniel tokeni humo ndani kwa Joash Mtoto haraka sana, inawezekana ikawa ni mtego" Hannan alisema kwa sauti ya uwoga.

"Sawa Hannan, tunatoka na tunakuja nyumbani sasahivi kuongea vizuri" Daniel alisema.

Harakaharaka walitoka nje. Wakaingia kwenye gari. Wakawasiliana na kina Amini, kila kitu kilikuwa sawa. Mkuumkuu walirejea Tabata, kwenye makazi mapya ya Daniel Mwaseba.

***

Ilichukua dakika zipatazo sita tangu wakina Daniel waondoke nyumbani kwa Joash Mtoto. Gari tatu za Polisi na askari zaidi ya thelathini na tatu walifika pale nyumbani kwa Joash Mtoto. Mbele ya askari hao alikuwepo Moses, mtoto wa kiume wa Rais Mark. Moses akiambatana na askari walianza kuipekua ile nyumba ya Joash Mtoto.

Dakika kumi na mbili ziliwarejesha Polisi katika sebule ya Joash Mtoto. Hawakukiona walichokuwa wanakitafuta. Moses alitoa simu yake mfukoni na kupiga.

"Denis" Alianza kuongea mara tu simu ilipopokelewa. "Angalia tena mahali ilipo simu ya Aneth, tumefika katika nyumba namba hamsini na tisa lakini simu haipo"

Kilifata kimya. Moses akimsikiliza Denis,

"Unasema?" Moses alipayuka baada ya kusikiliza kwa muda.

Akasiliza tena.

Baada ya dakika mbili alijikuta akikaa chini bila kupenda. Kisha akasema kwa sauti ndogo.

"Simu imezimwa"

Itaendelea...
 
RIWAYA; MTOTO WA RAIS
HALFANI SUDY
0652 212391

Sehemu ya Ishirini na Nne

Baada ya dakika mbili alijikuta akikaa chini bila kupenda. Kisha akasema kwa sauti ndogo.

"Simu imezimwa"

Askari polisi wote walimwangalia Moses. Askari mmoja alipata nguvu ya kuuliza.

"Kwani hii nyumba inamilikiwa na nani?"

"Joash, Joash Mtoto" Moses alijibu akiwa amechoka.

"Usijari Moses, kama kweli simu ilikuwa hapa basi mmiliki wa nyumba hii ndiye Mtuhumiwa wetu wa kwanza. Tutamsaka Joash Mtoto popote pale alipo. Tutamsaka kusini na kaskazini, mashariki na magharibi, na lazima atuambie kwanini simu ya Aneth ionekane ikilia nyumbani kwake? Kisha izimwe?"

"Inspekta Adrian, nimempoteza dada yangu wa pekee. Najua unajua kwa namna gani inaumiza kupoteza mtu unayempenda. Zaidi ya kuwa dada yangu, Aneth ni Mtoto wa Rais, raia namba moja hapa nchini. Ahadi ya kuahidi tu kuwa mtamkamata Joash Mtoto haitoshi, niahidi pia mtamnyonga mtu aliyemuua dada yangu"

"Moses, jukumu letu kama jeshi la Polisi ni kumkamata muuaji. Tutahakikisha tunapata ushahidi wote na kumtia hatiani. Mahakama ndio itakayoamua, muuaji anyongwe ama la"

Moses alimwangalia Inspekta Adrian. Kichwani mwake mambo mengi sana yalikuwa yanapita.

Baada ya utaratibu wa jeshi la Polisi kukamilika waliondoka. Huku msako wa kumsaka Joash Mtoto ukianza. Na jalada la kuifatilia kesi hiyo akipewa askari kijana, Inspekta Adrian Kaanan.

***

Wakina Daniel walifika Tabata, maskani yao.

"Vipi hapa, kila kitu kipo sawa?" Daniel aliuliza.

"Ndio, kila kitu kipo sawa. Tumemaliza kazi uliyotuachia sio muda mrefu" Hannan alisema akiwa ameshika chupa kubwa ya maji.

"Eeh nambieni mmepata nini kwa Zayiid?" Daniel aliuliza kwa hamu.

"Taarifa hazitofautiani sana na zile za awali. Katika mitandao yote tuliyoingia tumepata taarifa zilezile. Zayiid ni mfuasi wa kikundi cha kigaidi cha Alqaeda. Na mengi tuliyoyapata kuhusu yeye ni misheni alizoshiriki. Kwa ujumla, Zayiid ameshiriki katika misheni tisini na tisa ndani ya miaka kumi na nne, hii ni misheni yake ya mia moja. Na rekodi inaonesha kuwa katika misheni zote tisini na tisa Zayiid hajawahi kushindwa. Zayiid ni mtu makini sana. Anayafanya mambo yake kwa akili na weledi wa hali ya juu" Hannan alisema.

Daniel alimwangalia Hannan kwa muda, kisha akasema "Kingine mlichokipata?"

"Tulijaribu kudukua mawasiliano ya Zayiid, lakini imekuwa ngumu kupata chochote. Vitu vyake vyote vimewekwa katika mfumo mgumu ambao si rahisi kwa mtu asiyehusika kuifungua." Leonard alisema.

Daniel alitafakari, aliuona ugumu wa kumfaham Zayid katika sura za kina Hannan.

"Sawa, tutaangalia tunamfaham vipi zaidi. Eeh niambie habari ya kifo cha Aneth, na huko mtandaoni wanasemaje?" Daniel aliuliza.

"Mtandaoni habari iliyopo ni juu ya kifo cha Aneth. Watu wengi inaoneshwa wameumizwa sana na kifo chake. Aneth anaelezwa ni mtu mwenye huruma na upendo kwa watu. Kupitia kampuni yake ya sheria amesaidia watu wengi sana, hasa kina mama wajane na mayatima. Huko mtandaoni kuna shuhuda nyingi za kina mama aliowasaidia kupata haki zao" Hannan alisema.

"Lakini kwanini mtu mwema namna hiyo auwawe kinyama?" Martin aliuliza.

"Hilo ndilo swali linaloumiza watu kichwa. Wengi wanasema Aneth hakustahili aina hiyo ya kifo. Kutokana na wema wake alikuwa anahitaji aina ya kifo cha starehe. Lakini haikuwa hivyo. Mara nyingi maisha hayatupi tunachokitaka" Hannan alisema kwa majonzi.

"Tutatafuta nafasi ya kwenda kuuona mwili wa Aneth, pengine tutapata kitu cha kutusaidia katika uchunguzi wetu" Daniel alisema.

"Tungeipata hiyo nafasi ingekuwa ni jambo jema sana. Mimi ninaamini muuaji hawezi kufanya mauaji bila kuacha ushahidi nyuma yake. Lazima tuende katika eneo ulipookotwa mwili wa marehemu, na zaidi lazima tukauone mwili wenyewe. Tatizo lililopo ni kwa namna gani tunaweza kulifanikisha hilo? Aneth ni Mtoto wa Rais, haitokuwa rahisi kuuona mwili wake" Martin alisema.

"Ngoja nijaribu kumpigia Dokta Viran nione kama anaweza kutusaidia katika hilo" Daniel alisema huku akitoa simu yake mfukoni. Akabonyaza namba za Dokta Viran, akaiweka simu sikioni.

"Daniel Mwaseba..." Sauti ya Dokta Viran ilisikika simuni.

"Dokta Viran, umesikia taarifa ya msiba wa Mtoto wa Rais?" Daniel alienda moja kwa moja kwenye hoja.

"Nimesikia Daniel. Ni taarifa ya kustusha sana. Hapa Muhimbili tumechanganyikiwa sana. Aneth alikuwa ni mjumbe wa bodi yetu hapa hospitali. Kwahiyo msiba wake umetugusa sana"

"Poleni sana Dokta. Sikuwa najua kama Aneth alikuwa mjumbe wa bodi yenu hapo hospitali. Vipi kuna tetesi zozote za sababu ya kifo chake?" Daniel aliuliza.

"Kwangu binafsi sijasikia tetesi yoyote. Ila ninasikitika sana kwa kifo kilichomkuta Aneth. Ni kifo cha kikatili sana. Hakustahili kufa kifo cha namna ile yule mtoto. Alikuwa ni mtu mwenye maono makubwa sana juu ya nchi hii. Ni miongoni mwa mabinti wachache wenye akili za kipekee. Tulipokuwa katika vikao vyetu, kila kauli yake kichwani nilikuwa namuona kiongozi ajaye wa Taifa hili, tumepoteza hazina kubwa sana kama nchi" Dokta Viran alisema kwa masikitiko.

"Nakupa pole tena Dokta Viran. Katika maneno yako naona kiasi gani umeumizwa na kifo cha Aneth. Sasa, kuna jambo moja naomba unisaidie Dokta.."

"Jambo gani?" Dokta Viran aliuliza.

"Ni jambo gumu kidogo hasa kwakuwa Aneth ni Mtoto wa Rais. Lakini ni gumu pia kwakuwa mimi si Mpelelezi rasmi wa kesi hii. Lakini ninaomba unisaidie kupata nafasi ya kuiona maiti ya Aneth!"

Daniel alisikia jinsi Dokta Viran alivyopumua kwa nguvu. Alijua kwa namna gani amemtwisha mzigo mzito. Lakini hakukuwa na namna nyingine yoyote ya kufanya.

"Daniel, nikwambie tu ukweli, hilo ni jambo gumu sana" Daniel aliisikia sauti ya Dokta Viran wakati akitafakari.

"Naujua ugumu wa jambo hilo Dokta Viran. Lakini ninaomba fanya uwezavyo unitafutie hiyo nafasi" Daniel alisisitiza.

"Daniel, labda uniambie kitu gani unakitaka katika mwili wa Aneth, ninaweza kukifanya kwa niaba yako"

"Dokta, ninachohitaji ni macho yangu mawili kuuona mwili wa Aneth"

"Umenipa mtihani mzito sana Daniel. Lakini nitaona kwa namna gani ninaweza kukusaidia. Naomba nipe muda nitakupigia kama baada ya dakika kumi na tano" Dokta Viran alisema, kisha akakata simu.

"Hannan, tulivyoenda nyumbani kwa Aneth hatukumkuta. Lakini wakati tukiendelea na upekuzi wetu tuliipata simu ya Aneth ikiwa chini ya kitanda. Hii hapa. Unaweza kuiangalia kama tutapata kitu chochote cha kutusaidia katika uchunguzi wetu" Daniel alisema huku akimkabidhi Hannan ile simu.

"Safi sana Daniel, hii inaweza kutusaidia katika uchunguzi wetu"

Hannan aliipokea ile simu. Akaiwasha. Kisha akaanza kuibonyazabonyaza. Akachukua waya mdogo na kuiunganisha na tarakilishi yake. Baada ya kama dakika tatu, akasema "Hakuna taarifa yoyote ndani ya simu hii. Bila shaka taarifa zake zimefutwa!"

"Daah hawa jamaa wapo makini sana na mambo yao. Lakini kiyama chao kinakaribia!" Daniel alisema kwa hasira. Mara simu yake ikaita.

"Dokta Viran" Daniel akasema kwa sauti ndogo.

"Daniel," Dokta Viran aliita baada ya simu yake kupokelewa. "Nimejaribu kuangalia namna ya wewe kuiona maiti ya Aneth lakini imekuwa ngumu sana. Aneth ni Mtoto wa Rais hivyo kila kitu kinachofanywa juu yake kimepangwa na Serikali katika utaratibu maalum. Hapa hospitali kuna sura ngeni nyingi sana, najua unajua namaanisha nini?"

"Dokta Viran usiniangushe. Tukifeli katika hili tutakuwa tumefeli sisi na Taifa kwa ujumla. Mimi binafsi nimejipa kazi ya kuchunguza sababu ya kifo cha Aneth, na kuwafikisha katika vyombo vya sheria wote walihusika. Naomba tusaidiane kuitafuta haki ya huyo binti. Kama ulivyonambia awali, Aneth hakuwa wa kuuwawa namna hiyo, sasa kauwawa. Usiruhusu wauaji watambe mtaani wakati tuna namna ya kufanya ili kuwatia katika mikono ya sheria" Daniel alilalama.

"Daah maneno yako yamenisikitisha sana. Ninaiona dhamira yako ya dhati katika kutafuta haki ya Aneth. Sasa kuna namna moja tu ya wewe kuiona maiti ya Aneth!"

"Njia gani hiyo?" Daniel aliuliza kwa hamu kubwa.

"Ni njia ngumu sana, lakini nd'o njia pekee kama unataka macho yako kuiona maiti ya Aneth. Maiti ya Aneth ipo katika chumba cha kuhifadhia maiti za watu maarufu. Nje kuna ulinzi wa askari wengi sana bila kusahau usalama wa Taifa. Kila daktari anayeenda kule anakaguliwa ipasavyo, na wanahakikisha ni daktari kweli. Njia pekee ya wewe kuingia katika chumba kile ni kufa!

"Unasemaje Dokta Viran?" Daniel alihamaki kwa nguvu.

"Nisikilize Daniel, kama kweli una nia ya kuiona maiti ya Aneth ni lazime ufe, ndipo upelekwe katika chumba ulipohifadhiwa mwili wa Aneth. Tunaweza kufanya hivi, tengeneza kifo chako kisha uletwe hapa. Mimi nitafanya juu chini maiti yako ipelekwe katika chumba ulipo mwili wa Aneth"

Itaendelea...
 
Hollywood kuna watu wanaitwa critical kazi yao ni kukosoa sana . Kabla ya movie yoyote kutoka huwa wanaitwa kuangalia, maoni yao ndio yanafanya movie inunuliwe au idode.
Mtu anapokosoa sio lazima awe ana chuki au wivu wakati mwingine anasaidia kuboresha ili kitu kiwe bora.
Umejibu vizuri sana mkuu, napenda watu wanaojibu kwa hoja kama wewe.

Binafsi nimeona mwandishi ameamua kwa makusudi kuwapa uwezo wa kiteknolojia Watanzania ambao tutaufikia baada ya miaka 1000. Bila shaka mwandishi ameamua kutupa dira kwamba kila kitu kinawezekana chini ya jua.

Vijana wengi tuna mawazo mazuri sana ila shida ni namna ya uwasilishaji, tunaamini matusi ndio kusonga mbele kumbe ni kinyume chake.
 
Umejibu vizuri sana mkuu, napenda watu wanaojibu kwa hoja kama wewe.

Binafsi nimeona mwandishi ameamua kwa makusudi kuwapa uwezo wa kiteknolojia Watanzania ambao tutaufikia baada ya miaka 1000. Bila shaka mwandishi ameamua kutupa dira kwamba kila kitu kinawezekana chini ya jua.

Vijana wengi tuna mawazo mazuri sana ila shida ni namna ya uwasilishaji, tunaamini matusi ndio kusonga mbele kumbe ni kinyume chake.
Wakati Musiba anaandika vitabu vyake ilikuwa miaka ya mwanzoni ya themanini , kitabu kama njama walizungumzia jinsi mpenzi wake toka Sieraleone alivyofika London akaingia kwenye computer na kuulizia kuhusu Willy Gamba. Wakati huo tuliona kama uongo fulani yaani haiwezekani mtu akaulizia taarifa za mtu kwenye computer lakini matumizi ya computer yalipoanza kushika kasi miaka ya tisini katikati ndipo tukaja kuelewa kumbe unaweza kuingia kwenye computer halafu internet ukatafuta habari za mtu au kitu chochote kupitia mitandao kama google na mingineyo.
Hivyo utaona vitabu vya Musiba vilikuwa vinazungumzia teknolojia ya mbele ambayo wakati huo hata hatukuiwazia
 
Hawa jamaa wanafanya operation kubwa km hiyo bila kushirikisha ofisi yao ya usalama! Kila siku hawaonekani kazini na bosi hana pressure.
 
Back
Top Bottom