moneytalk
JF-Expert Member
- Jan 23, 2017
- 7,976
- 16,769
wewe ndo ulipotea seeker mimi siwezi kukosekana kwenye raha zangu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
wewe ndo ulipotea seeker mimi siwezi kukosekana kwenye raha zangu
Nimekukubali uko makini bibie[emoji1666]Naapia,Leonard ni msaliti kwel an i wish wamngundue mapema maana atawakwamisha sana
Unanikumbuka lakiniwewe ndo ulipotea seeker mimi siwezi kukosekana kwenye raha zangu
bado navuta kumbukumbuku,uniwie radhi lakini c unajua na uzee nao unachangia
mkuu tuongezee japo kimoja basiRIWAYA; MTOTO WA RAIS
IMEANDIKWA "NA HALFANI SUDY
Whatsapp 0652 212391
Sehemu ya Ishirini na Tano
Dokta Viran usiniangushe. Tukifeli katika hili tutakuwa tumefeli sisi na Taifa kwa ujumla. Mimi binafsi nimejipa kazi ya kuchunguza sababu ya kifo cha Aneth, na kuwafikisha katika vyombo vya sheria wote walihusika. Naomba tusaidiane kuitafuta haki ya huyo binti. Kama ulivyonambia awali, Aneth hakuwa wa kuuwawa namna hiyo, sasa kauwawa. Usiruhusu wauaji watambe mtaani wakati tuna namna ya kufanya ili kuwatia katika mikono ya sheria." Daniel alilalama.
"Daah maneno yako yamenisikitisha sana. Ninaiona dhamira yako ya dhati katika kutafuta haki ya Aneth. Sasa kuna namna moja tu ya wewe kuiona maiti ya Aneth!"
"Njia gani hiyo?" Daniel aliuliza kwa hamu kubwa.
"Ni njia ngumu sana, lakini nd'o njia pekee kama unataka macho yako kuiona maiti ya Aneth. Maiti ya Aneth ipo katika chumba cha kuhifadhia maiti za watu maarufu. Nje kuna ulinzi wa askari wengi sana bila kusahau usalama wa Taifa. Kila daktari anayeenda kule anakaguliwa ipasavyo, na wanahakikisha ni daktari kweli. Njia pekee ya wewe kuingia katika chumba kile ni kufa!
"Unasemaje Dokta Viran?" Daniel alihamaki kwa nguvu.
"Nisikilize Daniel, kama kweli una nia ya kuiona maiti ya Aneth ni lazime ufe, ndipo upelekwe katika chumba ulipohifadhiwa mwili wa Aneth. Tunaweza kufanya hivi, tengeneza kifo chako kisha uletwe hapa. Mimi nitafanya juu chini maiti yako ipelekwe katika chumba ulipo mwili wa Aneth."
"Mfyuuuuuuuuu..." Daniel alipumua kwa nguvu. "Ni njia ngumu sana hiyo. Hakuna njia nyingine Dokta Viran?"
"Daniel ngoja nikwambie kitu kimoja, kifo cha Aneth kimegubikwa na utata mwingi sana. Wakati nimekwambia unipe dakika kumi na tano nitafakari kimetokea kitu cha ajabu sana hapa hospitali."
"Kitu gani kimetokea?" Daniel aliuliza.
"Alikuja askari aliyekabidhiwa kupeleleza kifo cha Aneth akitaka kwenda kuiona maiti ya Aneth. Lakini cha ajabu hata yeye amezuiliwa kuiona. Sasa fikiria, Polisi mwenye dhima na kesi hii amezuiliwa kuiona maiti ya Aneth, je wewe? Hivyo zaidi ya wewe kufa kifo bandia sidhani kama kuna njia nyingine ya kuiona maiti ya Aneth." Dokta Viran alisema kwa kirefu.
"Dokta hapo hospitali kuna monchwari nyingi. Na umesema mwili wa Aneth umewekwa katika chumba maalum. Sasa mimi nikifa nitawekwa katika chumba hicho?" Daniel aliuliza.
"Daniel hayo mengine niachie mimi. Ukiletwa mwili wako hapa nitajua ninafanyaje ukaingizwe katika chumba ulipo mwili wa Aneth."
"Sawa Dokta. Ngoja nione tunafanyaje. Nitakupigia kukutaarifu nitakapofikia." Daniel alikata simu.
Daniel alichukua nafasi ya kuwaeleza wakina Martin yote aliyoongea na Dokta Viran.
"Haiwezekani! Haiwezekani!" Hannan alikataa kwa nguvu." Hatuwezi kufanya mchezo wa hatari kama huo."
"Hannan, hata mimi najua tunataka kufanya kitu cha hatari sana. Lakini lazima tufanye. Lazima nife ili nikaingie mahali ilipo maiti ya Aneth. Hakuna njia nyingine yoyote ya kuiona maiti ya Aneth zaidi ya hiyo."
"Daniel, tunaweza kutumia njia nyingine kuwasaka wauaji wa Aneth na kuwapata. Sio lazima tutumie njia ya hatari kiasi hicho. Tunataka kufanya uchuro Daniel! Je ukifa kweli?"
"Nakubaliana na wewe Hannan." Daniel alisema "Tunaweza kutumia njia nyingine ili kuweza kuwanasa wauaji wa Aneth. Lakini, mimi kuna kitu ninataka kujua. Kwanini wazuie watu kuuona mwili wa Aneth. Kwanini wamzuie hata afisa wa jeshi la Polisi mwenye dhamana ya kupeleleza mauaji haya asiuone mwili wa marehemu. Kuna kitu! Na hiko kitu ndicho ninachotaka kwenda kukiona huko monchwari"
"Daniel..." Hannan aliita, machozi yalikuwa yamemlenga "Kwanini hauheshimu hisia za wengine? Kwanini hauheshimu hisia za watu wanaokupenda? Kwanini mara zote unajari hisia zako tu? Haujui kama maisha yako yana umuhimu na kwa watu wengine pia. Haujuii, haujuii. Usijari hisia zako tu." Hannan alianza kulia.
Daniel alikuwa anashangaa. Hannan aliongea maneno kwa hisia na uchungu mkubwa sana. Alikuwa katika mtihani, lipi afanye?
"Usilie Hannan." Daniel alimsogelea Hannan na kumshika bega. "Usiingize hisia binafsi katika kazi. Tupo hapa kwa ajili ya Taifa letu. Sisi ni vijana wazalendo kwa nchi yetu. Tumeapa kufa ili kuhakikisha nchi hii inakuwa salama. Tumeamua kuyaweka rehani maisha yetu kwa sababu ya mama yetu Tanzania. Najua tunaenda kufanya kitendo cha hatari sana, lakini lazima tukifanye kwa mustkabali wa nchi yetu. Mimi ninaenda kufa kifo cha bandia. Sifi kweli. Hivyo lazima hapa wote tukibariki kitendo hiki. Ili kifanikiwe, na kwa pamoja tufanikiwe. Tuwajue madhalimu hawa wa taifa letu, umenielewa Hannan?"
Hannan alipangusa mafua huku akitingisha kichwa. Alikubali. Aliubariki mpango huu wa Daniel Mwaseba.
"Ndugu zangu, kuna mwingine yeyote ana wasiwasi juu ya tunachoenda kukifanya?"
Watu wote walikuwa kimya. Walikuwa wamekubaliana na mpango wa kifo cha bandia cha Daniel Mwaseba.
***
Saa mbili baadae, mtandao wa kijamii ulichafuka tena. Ikiwa bado kifo cha Aneth kikitawala mtandaoni, ikafata taarifa nyingine ya kusikitisha sana.
'Mpelelezi mahiri nchini Tanzania, Daniel Mwaseba alikuwa ameuwawa na watu waliosadikiwa kuwa ni majambazi'
Habari hii ilisambaa mithili ya upepo wa Kimbunga. Kutokana na umaarufu wa Daniel, taarifa ya kifo chake ilifunika ile ya kifo cha Aneth.
Vyombo vya habari vya ndani na vya kimataifa vilitawaliwa na habari hii. Kenya iliandika. Uganda iliandika. Rwanda iliandika. Nigeria iliandika. Sudan iliandika. Burundi iliandika. Afrika yote ilizizima. Kifo cha Daniel Mwaseba kilikuwa ni alama ya umoja wa Bara la Afrika.
Nyumbani kwa Daniel, Hannan alikuwa analia isivyo kawaida. Ingawa alijua ni kifo bandia lakini kwake alihisi kama Daniel amefariki kweli. Hakuweza kuyadhibiti maumivu makubwa yaliyopo moyoni mwake. Lilikuwa ni pigo lililo juu ya uwezo wake.
Taarifa za kifo cha Daniel Mwaseba zilipokelewa kwa furaha sana na maadui zake. Watu wasio penda amani ya dunia, wahalifu, wauzaji wa madawa ya kulevya. Wao kwao kifo cha Daniel kilikuwa ni jambo jema sana. Walishukuru kwakuwa mtu aliyekuwa anakwamisha mambo yao alikuwa amefariki.
Nyumbani kwa Donald Tengo ilikuwa ni furaha. Walipanga jioni wafanye sherehe kufurahia kifo cha Daniel Mwaseba. Furaha yao ilikuwa haina mfano. Maana kwasasa walikuwa wamepiga hatua nyingi sana mbele kukamilisha mipango yao.
Mwili wa Daniel Mwaseba ulipelekwa hospitali ya taifa ya Muhimbili. Hospitali ambayo ilikuwa inalindwa vibaya sana kwa kipindi hiko. Ingawa ilikuwa ngumu sana, lakini Dokta Viran alipambana mpaka mwili wa Daniel ulipelekwa katika chumba ulipohifadhiwa mwili wa Aneth.
Mpango uliopangwa, sasa ulikuwa katika utekelezaji. Daniel alikuwa amekubali kufanya jambo la hatari sana kwa maslahi ya nchi yake.
Nje ya chumba cha maiti, walikuwepo watu wengi sana. Wengi wakiwa ni watu kutoka katika vyombo mbalimbali vya ulinzi na usalama. Miongoni mwa watu hao alikuwepo Martin Hisia, ndugu wa pekee wa Daniel kwa wakati ule. Macho ya Martin yalikuwa hayatulii sehemu moja. Kila sekunde yakipepesa huku na kule. Yakimchunguza kila mtu yamwonaye. Akiwa pale nje, aliona mambo mengi yasiyokuwa ya kawaida. Hii ilimwaminisha kwamba kuna kitu cha ziada katika msiba huu.
Ni kitu gani hiko?.
Hapo ndipo kwa moyo wote, bila wasiwasi hata chembe alikubaliana na mpango wa Daniel Mwaseba. Ingawa kwake pia ilikuwa ngumu sana kukubaliana na mpango huu wa kifo bandia cha Daniel Mwaseba. Lakini ushawishi wa Daniel ulimfanya akubaliane nao. Kwake, ugumu ulikuwa ni vipi wazazi wa Daniel watachukulia taarifa za kifo cha mtoto wao? Vipi Chifu ataichukulia taarifa ya kifo cha Daniel? Raia je?. Lilikuwa ni jambo gumu kulikubali, lakini lilipaswa lifanywe. Alipokuwa pale alikiri kweli hii ndio ilikuwa namna pekee kuingia mle ndani kama alivyoshauri Dokta Viran. Hakukuwa na njia nyingine yoyote ile.
Martin akaanza kufanyia kazi mpango wa kifo cha Daniel. Alienda kwa Samson na kupanga namna ya kufanya ili Daniel aonekane ameuwawa na watu kutoka katika kikundi chao, lakini watambulike kama majambazi. Mpango ulienda sawa, risasi tatu zilipenya katika kifua cha Daniel Mwaseba, lakini zilikutana na kizuia risasi. Daniel alirushwa juu na kubwaga chini katika makutano ya barabara ya Keko! Wote walioona kitendo hiko waliamini kwamba Daniel alikuwa ameuwawa kweli!. Hapo ndipo taarifa za kuuwawa kwa askari zilisambaa kwa kasi, kabla ya baadae kusemekana askari huyo aliyepigwa risasi ni Daniel Mwaseba. Kutokea hapo, maiti ya Daniel ilipelekwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili, ambapo Dokta Viran alisimamia kila kitu kuhakikisha mwili wa Daniel unapelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti alichomo Aneth.
Na kwasasa Daniel alikuwa ndani...
Itaendelea...
Shukrani mkuuNaweka kwa kadri ninavyozipata mkuu
Umesomeka mkuuNaweka kwa kadri ninavyozipata mkuu