Tetesi: Robert Mugabe aanza rudisha mashamba kwa wazungu

Tetesi: Robert Mugabe aanza rudisha mashamba kwa wazungu

Tukirudi kwenye mada nchi kama LIBYA wazungu walikuwa hawanufaiki nayo kwasababu walikuwa wanajitosheleza kwa kilakitu na zaidi GADDAFI akataka kuiunganisha AFRIKA jambo ambalo lilishashindwa huko nyuma kwasababu waafrika ni wabinafsi.
...Kamuulize Mwingereza, Mfaransa na Mwitaliano kama walikuwa hawafaidiki na Libya. Hamna nchi duniani inayojitosheleza kwa kila kitu!

GADDAFI alijaribu kuwafanya waarabu wanaozalisha mafuta waungane ili wawe na sauti akasahau kuwa kuna vibaraka wa wazungu hata uarabuni ndio akaja na wazo hilo AFRIKA akiwa na maana nchi moja moja bila kujiunga tukaunganisha rasilimali tulizonazo haziwezi kujikomboa.
...Hakuna nchi ya Afrika itakaa kuunganisha raslimali. Single visa imetushinda hapa EAC. Nations have competing agendas!

Tulitakiwa tuunganishe nguvu tuwe kitu kimoja,uchumi wa nchi zilizoendelea unahitaji sana rasilimali zilizopo afrika ambapo wanaichukua kwa bei ya kutupa kupitia sera zao wanazotulazimishia kama ubinafsishaji,uwekezaji n,k lakini tungejiunga tungejikuta kwanza tunajitosheleza wenyewe kwamba kuna nchi zina njaa wakati zingine mazao yanaozea shambani,tungeanzisha viwanda kwa kutegemea malighafi zinazopatikana hapahapa AFRIKA,vitu ambavyo hatuna kwa umoja wetu tungevipata hata kwa kuagiza toka nje ya afrika au kuleta wataalamu wakatengeneza hapahapa.
...Hapa nchini kuna maeneo yana njaa, wakati mengine chakula kinaharibika. Ni issue ya demand and supply, miundombinu, pamoja na sera.

...Huwezi ukaamini, lakini, sera tu pekee, zinawezafanya sehemu moja chakula kikaoza wakati kwengine wanashinda njaa. Unakumbuka, vipindi ambavyo huwa ni marufuku kuuza chakula nje?

lakini haya yote yanashindikana kwasababu kwa kutumia demokrasia wazungu wanaamua nani wamuweke madarakani atakayewahakikishia maslahi yao hayatatetereka na anayeenda kinyume nao kwa vyovyote vile watamtoa.yapo mambo mengi sana ya kuyatafakari ambayo lazima tufikirishe akili zetu ili kuelewa kwanini wazungu hawakumtaka GADDAFI wala hawamtaki MUGABE.
...Demokrasia haitumiki kumuweka kibaraka. Uzoefu unaonyesha waliowahi kuitwa vibaraka, hawakutawala kwa kufuata mfumo wa demokrasia. Mobutu, Banda, Omar Bongo na wengine waliitwa vibaraka.

...Mengi ya matatizo yanayoihusu Afrika hayasababishwi na wazungu, bali sisi wenyewe!
 
Utaelewa tu taratibu,wazungu ukiwa na maslahi nao wao hakuna tatizo SADDAM alikuwa na urafiki na USA lakini unapopishana nao unakuwa adui yao.kumbuka hata OSAMA kuna kipindi alifundishwa mafunzo ya kijeshi na USA.
...Ulitegemea aingie Kuwait, halafu atishie interest zao kule, wao wamwachie?

...Hawakuhangaika na Osama hadi pale alipoanza kuwafanyia mzaha.

kuchukiwa na wananchi kunatengenezwa,kwa mfano MUGABE alikuwa na wazo zuri tu kuchukua mashamba na kuyagawa kwa wananchi maana wananchi walikuwa wanaishi kwa kufanya vibarua tu kwenye mashamba ya wazungu yani yale mambo ya ukitaka nikupe eneo la kulima kwanza itabidi uwe unanilimia mimi halafu nitakupa eneo na wewe ulime maana cheap labour ni wazawa,wazawa walikuwa hawana nafasi ya kulima ardhi yote iliyokuwa inafaa kwa kilimo ilihodhiwa na wazungu waliorithishana tangu ukoloni.
...Wazimbabwe walikuwa na wanahaki ya kumiliki ardhi, hasa ikizingatiwa kwamba, ilikuwa ya mababu zao. Mipango ya kugawa ardhi ilianza miaka mingi kwa ufadhili wa Mwingereza. Something went wrong, mpango ukasimama au kufa. Actually, watu wa kwanza kufaidi, walikuwa elites wa Zimbabwe. Mimi na wewe tukasahaulika.

...Ule ujinga uliofanyika baadae, ulikuwa ni wa kuokoa mambo. hali ilikuwa ngumu kisiasa.

MUGABE alipowaondoa wazungu akawekewa vikwazo,hata kama alitaka kuwaunganisha wakulima wawe katika vikundi halafu wasaidiwe na serikali ruzuku kuweza kuyaendesha mashamba imeshindikana kwasababu amewekewa vikwazo na hata kama alifanikiwa kuyaendesha lakini kumbuka wanunuzi wakubwa wa bidhaa hizo walikuwa ni wazungu kwahiyo soko likawa hakuna na vikwazo vikaongeza ugumu wa maisha kwahiyo lazima wananchi wakuchukie,ujiulize tu kidogo kwanini MUGABE aligeuka mbaya alipowanyang'anya wazungu mashamba tuu?kwani tangu ameanza kungangania madaraka ni leo?
...Waliofadika na unyan'ganyi ule ni vibaraka wake na wananchi wa kawaida wachache.

...Watu wasiokuwa na uwezo au ujuzi wa kulima mashamba kibiashara, ndio wamepata mashamba. Matokeo yake, wameshindwa kuyaendeleza.

...It was not a well thought after process, but a ad hoc one.
 
Wazungu wanaendelea kututawala kwa kigezo cha demokrasia,demokrasia siku zote inawagawa watu,siku zote kwenye demokrasia watu hawawi wamoja.Gadafi alikuwa na ubaya wake lakini kungangania madaraka haikuwa tatizo,tatizo alikuwa anatishia maslahi ya wazungu kwa kutaka AFRIKA iungane kuwe na kitu kama UNITED STATE OF AFRICA hiyo ajenda ndio iliomuua sio kitu kingine.
Mkuu tunashindwa kujitambua, matatizo ya nchi zetu za ki Africa ni sisi wenyewe. Tume shindwa kusimamia demokrasia na utawala bora tume baki kulalamikia wazungu. Ufisadi na ubifsi wetu hatuuoni tumebaki lawama ni wazungu. Hao wazungu tuiba pesa na kujiibia wanaturejeshea, kumbuka scandal za radar, standibic bank etc. Alie tuloga kesha kufa tutabaki mtafuta mchawi hadi kifo kitukute kila mtu kwa wakati wake, kalaga baho wazungu, wamarekani, waingereza etc fyuuu.
 
Wazungu wanaendelea kututawala kwa kigezo cha demokrasia,demokrasia siku zote inawagawa watu,siku zote kwenye demokrasia watu hawawi wamoja.Gadafi alikuwa na ubaya wake lakini kungangania madaraka haikuwa tatizo,tatizo alikuwa anatishia maslahi ya wazungu kwa kutaka AFRIKA iungane kuwe na kitu kama UNITED STATE OF AFRICA hiyo ajenda ndio iliomuua sio kitu kingine.

Gradation alikuwa Na lengo la kufanya Sarafu ya Afrika iwe moja, iwe Sarafu ya Dhahabu Na sio makaratasi wazungu walijua siku ikifikia hayo Ndio mwisho wao.
 
Libya ni ushenzi wa Gadafi kung'ang'ania madaraka na wala hakuna uchawi. Hivi kama angelikuwa anatawala Libya kwa ajili ya wananchi, ni kwa nini hakukubali kufanya demokrasia? Kama angelikubali kuongoza nchi kwa utashi wa wananchi wake, kwa maana ya kufanya uchaguzi wananchi wachague raisi wanayemtaka kwa wakati walipotaka, nayeye akabaki na heshima ya uraisi mstaafu akishuhudia na kushauri mwendelezo wa Libya, yangemkuta yaliyomfika? Walibya Wangeuana? Alidhani ataishi milele? Lazima kufa angelikufa kwa namna yoyote. Je baada ya kufa kwake, Waliby awasingegombana kama ilivyoleo? Kiongozi mzuri ni yule anayetawala na kuliangalia taifa kwa vizazi vijavyo na hivyo kuandaa mfumo sahihi wa maendeleo ya uma na si yale ya faimilia au kundi dogo analotaka yeye kinyume na wenye nchi.

Ni ujinga wa viongozi kudhani uraisi ni utemi.

Mugabe alipashwa kuzijua hizo hesabu kabla hajatwanga maji. . Mugabe siyo Zimbabwe. Kama maamuzi yake yalikuw ani kwa ajili ya Wazimbabwe, kwa nini kung'anng'ani madaraka na kuua watu kwa sana eti wanampiga?

Leo hii Zanzibar watu wakianza kufa na njaa mtalaumu Wazungu? Kila maamuzi yanagharama. Zingatia uwezo wa kufika bei kabla hujatoa order. Makeke bila nguvu ni upumbavu na fedheha!. Sasa yako wapi?

Zilikuwapo njia nyingi sana za kufanya uchumi shirikishi Zimbabwe ambazo kila upande ungenufaika na hatimaye kujenga uwezo mkubwa kwa wazawa zaidi ya ubabe wa kijinga ambao haujalipeleka taifa mahala popote. Na ndiyo sababu haka kazee hakataki kuachia nchi kwa hofu ya hasira za Wazimbabwe kalikowaua kwa kisingizio cha kuwalinda.
Naona information uliyonayo kuhusu Libya ni ile unayoisikia kwenye vyombo vya habari
 
Gradation alikuwa Na lengo la kufanya Sarafu ya Afrika iwe moja, iwe Sarafu ya Dhahabu Na sio makaratasi wazungu walijua siku ikifikia hayo Ndio mwisho wao.
...Kuifanya Afrika iwe na sarafu moja, ni sawa na lile wazo la kuifanya iwe moja. It takes a lot, kuwa na sarafu moja.

...Na ingekuwa sarafu ya dhahabu, mimi na wewe tusingeweza kuishika, achilia mbali kuwa nayo. Ni aghali kuwa na sarafu ya dhahabu. Halafu, unafanyaje biashara kwa kubadilisha kiasi fulani cha dhahabu, kiurahisi? Unazibebaje?

...Fedha ya karatasi ilizaliwa kutokana na urahisi wa kubadilishana na kuibeba, ikithaminishwa kwa vitu vya thamani kama dhahabu. Wazungu hawakuwa wa kwanza kutumia fedha ya karatasi bali wachina, kwasababu ukiwa na fedha nyingi -ambazo ni madini au vito- huwezi kuzibeba kiurahisi toka sehemu moja hadi nyingine.

...Tusiamini propaganda hizi, hazitusaidii.
 
...Kuifanya Afrika iwe na sarafu moja, ni sawa na lile wazo la kuifanya iwe moja. It takes a lot, kuwa na sarafu moja.

...Na ingekuwa sarafu ya dhahabu, mimi na wewe tusingeweza kuishika, achilia mbali kuwa nayo. Ni aghali kuwa na sarafu ya dhahabu. Halafu, unafanyaje biashara kwa kubadilisha kiasi fulani cha dhahabu, kiurahisi? Unazibebaje?

...Fedha ya karatasi ilizaliwa kutokana na urahisi wa kubadilishana na kuibeba, ikithaminishwa kwa vitu vya thamani kama dhahabu. Wazungu hawakuwa wa kwanza kutumia fedha ya karatasi bali wachina, kwasababu ukiwa na fedha nyingi -ambazo ni madini au vito- huwezi kuzibeba kiurahisi toka sehemu moja hadi nyingine.

...Tusiamini propaganda hizi, hazitusaidii.
Nadhani mtoa hoja hakulielewa/kulielezea hili kwa udadisi. Hela ya dhahabu ilikua itumike kwenye biashara ya mafuta na sio kwenye normal transactions. Alipropose hivyo na hio sio propaganda bali ni fact. Si hilo tu, na mengine mengi including owning our own satellites, kuanzisha AMF(African Monetary Fund), AIB, ACB na other institutions
 
Mugabe is the next level: neither Satan nor God would like to invite him. Kama duniani mmemchoka mjinyonge bora kumpenda tu. Mmemtafuta kumuua mmeshindwa....mkamuombea afe, lakini hafi. Msianze kutudanganya eti karudisha Shamba ooohhh mara kajiuzuru! Wazungu walikuwa zamani: Mugabe komaa ili Magufuli asione woga akawaachia tena waibe mali zetu Tanzania
 
Nadhani mtoa hoja hakulielewa/kulielezea hili kwa udadisi. Hela ya dhahabu ilikua itumike kwenye biashara ya mafuta na sio kwenye normal transactions. Alipropose hivyo na hio sio propaganda bali ni fact. Si hilo tu, na mengine mengi including owning our own satellites, kuanzisha AMF(African Monetary Fund), AIB, ACB na other institutions
...Attache, ninachokiita mimi propaganda, ni hii dhana ya kwamba ".....wazungu walijua siku ikifikia hayo Ndio mwisho wao" tukifanya hivi au vile.

...Nimeona hapa, kwamba dhahabu na fedha -to the tune of USD 7 bn- ilikuwa itumike kufanikisha kuwapo kwa sarafu ya Afrika, kitu ambacho ni utopian. Hata hivyo, hamna uhakika wa mpango huu kuwapo wakati huo.

...Na kwingine ni conspiracy theories kwa kwenda mbele.

...Nakubaliana nawe kwamba Gaddafi ali propose mambo lukuki, ila katika hayo, mengi hayatekelezeki, ni utopian ideas.
 
...Unaamini kuwa Afrika inaweza kuungana? Kama jibu ni ndio, nakubaliana nawe kwamba ndicho kilicho muua. Kama jibu ni hapana, basi tuangalie mambo mengine ambayo ndio yanaweza kuwa chanzo.
Gaddafi alikuwa na unafiki kuhusu Afrika kuungana maana ndo huyo alishauri Nigeria kugawanywa na kuwa nchi mbili ili kuepusha mgawanyiko kati ya kaskazini (Waislam) na kusini (Wakiristo) alitolea mfano wa Pakistan na India
 
...Kuifanya Afrika iwe na sarafu moja, ni sawa na lile wazo la kuifanya iwe moja. It takes a lot, kuwa na sarafu moja.

...Na ingekuwa sarafu ya dhahabu, mimi na wewe tusingeweza kuishika, achilia mbali kuwa nayo. Ni aghali kuwa na sarafu ya dhahabu. Halafu, unafanyaje biashara kwa kubadilisha kiasi fulani cha dhahabu, kiurahisi? Unazibebaje?

...Fedha ya karatasi ilizaliwa kutokana na urahisi wa kubadilishana na kuibeba, ikithaminishwa kwa vitu vya thamani kama dhahabu. Wazungu hawakuwa wa kwanza kutumia fedha ya karatasi bali wachina, kwasababu ukiwa na fedha nyingi -ambazo ni madini au vito- huwezi kuzibeba kiurahisi toka sehemu moja hadi nyingine.

...Tusiamini propaganda hizi, hazitusaidii.
Sifa moja ya pesa ni kwamba material iliyotengeneza hiyo pesa inabidi iwe cheap kuliko thaman ya hiyo pesa.
Kama sarafu ya tsh 50 ikiwa imetengenezwa na dhahabu yenye thamani ya 1000 basi watu watachukua hizo sarafu waziuze kama dhahabu.
Nina mashaka na hiyo stori yako
 
...Attache, ninachokiita mimi propaganda, ni hii dhana ya kwamba ".....wazungu walijua siku ikifikia hayo Ndio mwisho wao" tukifanya hivi au vile.

...Nimeona hapa, kwamba dhahabu na fedha -to the tune of USD 7 bn- ilikuwa itumike kufanikisha kuwapo kwa sarafu ya Afrika, kitu ambacho ni utopian. Hata hivyo, hamna uhakika wa mpango huu kuwapo wakati huo.

...Na kwingine ni conspiracy theories kwa kwenda mbele.

...Nakubaliana nawe kwamba Gaddafi ali propose mambo lukuki, ila katika hayo, mengi hayatekelezeki, ni utopian ideas.
Ukiona mtu yoyote anakwambia jambo fulani halitekelezeki ni wa kukaa nae mbali.
 
maamuzi ya Mugabe yalikuwa na nia njema tu lakini kwakuwa aligusa maslahi ya wazungu basi wamemkomoa kwa kumuwekea vikwazo lukuki,hata kama wazawa wangeweza kuendeleza hayo mashamba wangeuza wapi?wakati wamewekewa vikwazo?nikitafakari jinsi LIBYA ilivyosambaratika naona hakuna nchi ya AFRIKA hata moja itakuja kuwa nchi tajiri na kuwa moja kati ya nchi zilizoendelea hata kuwe na rasilimali za kila aina.
c kweli mkuu kuwa hakuna nchi y africa itayokuja kuendelea na kuwa nchi tajiri sema inategemeana na akili tu za watawala wa nchi yenyew kwa vitu alivyokuwa anafanya mugabe ulitegemea wazungu ba wao wafanyeje sasa?dawa ya fitna ni fitna mkuu hata nchi kama misri au angola huwa wanatofautiana sana na wazungu na marekan lakin linapokuja swala la biashara na uchumi wanashirikiana sana tu hata putin ni jeuri sana lakin huwa anajua kubalance mambo yake sasa mzee mugabe yeye allikua anapitiliza
 
Sifa moja ya pesa ni kwamba material iliyotengeneza hiyo pesa inabidi iwe cheap kuliko thaman ya hiyo pesa.
Kama sarafu ya tsh 50 ikiwa imetengenezwa na dhahabu yenye thamani ya 1000 basi watu watachukua hizo sarafu waziuze kama dhahabu.
Nina mashaka na hiyo stori yako
...Hizo sentensi zako mbili, zinaonyesha hukuelewa nilichozungumzia!
 
Ukiona mtu yoyote anakwambia jambo fulani halitekelezeki ni wa kukaa nae mbali.
...Ngoja niongee kiswahili unachokielewa. Je, unaamini kuwa EAC inaweza kuwa shirikisho la kisiasa? Kama ambavyo M7 amekuwa akipigia ndogondogo, ili aje awe Rais wa kwanza wa East Africa?

...Jibu lolote utakalotoa hapa, nakubaliana nawe!
 
Kama sarafu ya tsh 50 ikiwa imetengenezwa na dhahabu yenye thamani ya 1000 basi watu watachukua hizo sarafu waziuze kama dhahabu.
...Wakishaziuza watalipwa kwa sarafu gani? ya dhahabu?

...Au ulifikiri mie ndiye niliyesema sarafu ya dhahabu?

Nina mashaka na hiyo stori yako
...Bado una mashaka?
 
F
...Kuifanya Afrika iwe na sarafu moja, ni sawa na lile wazo la kuifanya iwe moja. It takes a lot, kuwa na sarafu moja.

...Na ingekuwa sarafu ya dhahabu, mimi na wewe tusingeweza kuishika, achilia mbali kuwa nayo. Ni aghali kuwa na sarafu ya dhahabu. Halafu, unafanyaje biashara kwa kubadilisha kiasi fulani cha dhahabu, kiurahisi? Unazibebaje?

...Fedha ya karatasi ilizaliwa kutokana na urahisi wa kubadilishana na kuibeba, ikithaminishwa kwa vitu vya thamani kama dhahabu. Wazungu hawakuwa wa kwanza kutumia fedha ya karatasi bali wachina, kwasababu ukiwa na fedha nyingi -ambazo ni madini au vito- huwezi kuzibeba kiurahisi toka sehemu moja hadi nyingine.

...Tusiamini propaganda hizi, hazitusaidii.
Fedha inabakia ya karatasi au madini dhaifu kuliko dhahabu,tofauti ni kwamba unaweza ukaibadilisha hiyo hela benki wakati wowote na ukapewa dhahabu inayolingana na Fedha unayoibadilisha.mfano unaenda benki na shillingi elfu kumi,utapewa dhahabu yenye thamani ya elfu kumi.hivohivo elfu ishirini na kuendelea.wataalam Wa uchumi wanaweza tufafanulia zaidi.
 
Back
Top Bottom