ROHO ni nini?

mizy gajo

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2016
Posts
801
Reaction score
887
salam wan jf
kwa wenye uwezo wa kureason naomba kupewa maana halisi ya neno roho na inamuingiliano gani na akili?
na je viumbe vyote vina roho??
 
Roho kama roho inakaaaga tumboni karibu na sifongo mkuu.
 
Ngoja nivute KITI niketi nisubiri wajuvyi wa Mambo watiririke ili nipate kujifunza jambo/kitu
 
Ni amri ya kuishi kiumbe chochote chenye uhai,amri hiyo inatoka kwa mwenyezi mungu mwingi wa rehma mwenye kurehemu.Muingiliano wa roho na akili upo kipindi roho yako inapokuwa hai ndipo na akili inakuwa na uwezo wa kufanya kazi.Hii elimu ya roho anayo Mwenyezi Mungu peeke hakuna anae ifahamu kwa usahihi ni hayo tu Bob.
 
unataka kutueleza kwamba roho ni pumzi kiongozi au ulikua una maana gani?
na je kama roho inaruhusu ubongo kufanya kazi ikiwa hai ina maana roho inakufaa pia??
 
nini mtazamo wako kuhusu hilo swalaa?
Mpka leo akuna jibu sahihi juu ya soul bado tunapambana kutafuta maana halisi,isipokuwa ipo mitazamo mingi yenye ambayo imetumiwa na dini,falsafa n.k..ambayo ndio hutumiwa lakini bado hakuna mwenye kutoa jibu sahihi..
 
Mungu hayupo thibitisha uwepo wake.
 
ROHO NI NINI

Hii ni miongoni mwa elimu ngumu sana katika kutolea maelezo. Lakini nitajotahidi kadiri nijuavyo lakini ajuaye zaidi ni Mungu.

Roho ya mtu huumbika (nurtured) sambamba na kuumbika kwa mwili wa mtu anapokuwa tumboni mwa mama yake yaani kama inavyojulikana mtu hadi awe kiumbe kamili huanza kutoka kwa baba kama tone la shahawa (sperms) ambapo katika shahawa moja ndipo hutokea mtu mmoja (naomba tusahau juu ya mapacha ili tuelewe kwa urahisi), hivyo roho huwemo ndani ya shahawa katika hali ya udhaifu (delicate and elusive) na wakati shahawa inapoingia kwenye ovary ya mwanamke ili irutubishwe kuwa kiumbe kamili hapo hapo pia roho iliyomo ndani ya shahawa nayo inarutubika sambamba na shahawa yenyewe pindi shahawa inapokuwa kiumbe kamili nayo roho inakuwa kamili na uhai unakuwa umekamilika, hivyo roho inaanzia kuwemo ndani ya shahawa na hukuzwa ndani ya tumbo la mama sambamba na kukuzwa kwa mwili mzima wa mtoto ndani ya tumbo la mama.

Basi ili tuweze kuifahamu roho inatupasa tutoe mifano ya vitu tunavyoishi navyo, Roho siyo sehemu ya mwili kama vile jicho au mkono au sikio nk, yalivyokuwa ni sehemu ya mwili lakini roho inayo mahusiano ya kiathari (cause and effect) na mwili mfano kama mtu atukanwe vibaya hapo moja kwa moja atapata maumivu katika roho na anaweza kutoka machozi kwa uchungu na utaona hayo machozi ni dalili kuwa mwili umepata athari halikadhalika kama mtu apewe mateso makali ya mwili athari itaenda kwenye roho kiasi kwamba mwili unakuwa si mahali pazuri kwa roho kukaa na hivyo roho huondoka na hatua hiyo tunaiita kifo, pia mtu anapofanya Ibada kwa vitendo (kimwili) anaipa athari za kiibada hiyo roho yake.

Kifupi ni kwamba roho imejificha ndani ya mwili kama vile moto ulivyojificha ndani ya njiti ya kiberiti, njiti ni njiti na moto ni moto wala havifanani lakini vinahusiana.
 
unataka kutueleza kwamba roho ni pumzi kiongozi au ulikua una maana gani?
na je kama roho inaruhusu ubongo kufanya kazi ikiwa hai ina maana roho inakufaa pia??
Sijazungumzia pumzi hapo,roho haifi inahama tu.
 
Ngoja nivute KITI niketi nisubiri wajuvyi wa Mambo watiririke ili nipate kujifunza jambo/kitu
WAtu kama nyie siku zote mpo. Hamfikirishi akili Bali mnavuta Kiti kusubiria wengine waje kuchangia. Hata kutoa definition ya roho kule Google kutuletea hapa UMESHINDWA. Ila kuvuta Kiti na kusoma michango ya wengine umeweza. Shubamitiiii!!
 
Roho ipo ndani ya moyoo[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…