Roma Mkatoliki amwibua Mwakyembe, adai hana elimu ya kumshauri yeye mwenye digrii 4. Kama anapenda siasa aanzishe chama cha siasa

Roma Mkatoliki amwibua Mwakyembe, adai hana elimu ya kumshauri yeye mwenye digrii 4. Kama anapenda siasa aanzishe chama cha siasa

Roma arudi shule jamani

Mtu anaefundisha au aliwahi kufundisha chuo sio wa kumfananisha na alieishia darasa la saba jamani huo ni ukweli usiopingika

Mwakyembe alipasua GPA kubwa Bachelor akabakizwa kuwa mwanataaluma UDSM huwezi fananisha na Msanii yeyote hapa nchini

He is trying to instill common sense that mr Phd does not have
 
Binafsi mpaka sasa siamini kama Mwakyembe ndio kuongea huo upumbavu vinginevyo nitaendelea kuamini tuna watawala wapumbavu kuliko tunavyodhani
Kama kweli kayasema hayo, basi hayo ndo tunaita matumizi mabaya ya akili.

Hua najiuliza Kama hii ndo aina ya viongozi tunaowaamini kufanya maamuzi ya nchi, je nchi yetu iko salama kweli?
Natamani huu uzi uwe ni propaganda na isiwe kayasema hayo kweli .
 
"Kama msanii unang'ang'ana kuimba siasa na kukosoa serikali basi amua kuachana na muziki uanzishe chama cha siasa. Lakini kama unataka kupata maslahi kwenye muziki, basi nyimbo hizo hazilipi. Haiingii akilini nina shahada nne halafu msanii ambaye hajaenda hata shule anatunga nyimbo za kunikosoa. Wewe na darasa la nne lako sijui la 7 utanionya mimi mwenye degree nne na nimefundisha vyuo vikuu mbalimbali?" Dr.Harisson Mwakyembe (PhD), Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo.!
Hapa waziri amechemka. Akili sio una phd ngapi akili niuwezo kujibu changamoto nakutatua matatizo.
 
Hilo ni ingizo jipya kwenye mradi wa kulipwa elf 7
We jamaa, kwani usipochangia kila uzi unaoletwa humu jukwaani utapungukiwa nini? Au ndiyo siku haitaingia! Hivi huoni unakidhalilisha chama na pia unamdhalilisha mwenyekiti wako!!
 
"Kama msanii unang'ang'ana kuimba siasa na kukosoa serikali basi amua kuachana na muziki uanzishe chama cha siasa. Lakini kama unataka kupata maslahi kwenye muziki, basi nyimbo hizo hazilipi. Haiingii akilini nina shahada nne halafu msanii ambaye hajaenda hata shule anatunga nyimbo za kunikosoa. Wewe na darasa la nne lako sijui la 7 utanionya mimi mwenye degree nne na nimefundisha vyuo vikuu mbalimbali?" Dr.Harisson Mwakyembe (PhD), Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo.!
Alafu nilazima mkumbuke kijana anamlenga mtu mwingine kabisa wala sio hao tunawafhani. Sio waziri wala sio rais ila kuna mtu anamlenga. End
 
Mkuu embu turekebishie kichwa ha habari.
Nimejaribu kukigeuzageuza kinakataa kila uelekeo.
Aliyebeba kichwa cha habari ni Roma au ni Mwakyembe?
 
Kama kweli kayasema hayo, basi hayo ndo tunaita matumizi mabaya ya akili.

Hua najiuliza Kama hii ndo aina ya viongozi tunaowaamini kufanya maamuzi ya nchi, je nchi yetu iko salama kweli?
Natamani huu uzi uwe ni propaganda na isiwe kayasema hayo kweli .
Mtanisamehe watani zangu Wanyakysa hivi huyu ndo roll model wenu vile
 
Tatizo la wasomi wa taifa letu ni wao kuwa wabinafsi kutokana na umahiri wao ktk madesa, na kujiona fahari zaidi ya watu wengine kutokana na vyeti walivyovipata ktk taaluma zao. Huku wakiwaona watu waliokosa fursa kama wao kuwa ni vilaza na hawana akili ya kuweza kuchangia jambo la maana ktk jamii, isipokuwa ni wao "elites" tu.

Ktk hili la msanii Roma Mkatoliki, Dr. Mwakyembe kajipambanua kuhusiana na hulka hiyo potofu hakuwa juu wa watu wengine, hakuwa makini na hata amedhihirisha kukurupuka na kuropoka juu ya kazi ya kisanii iliyotolewa na msanii huyu. Hayo maganda yake manne ya shahada mbalimbali hayampi uhalali wa kudharau haki ya kikatiba ya mtu mwingine.

Hata kama Roma kaishia darasa la saba, kwa wakati wake si ndiyo ili kuwa elimu ya msingi. Elimu ambayo waheshimiwa wenzake na Mwakyembe umewafanya wastahili kuwa wabunge! Msukuma, Kibajaji n.k tunawaona walivyoamiwa na kuwa sehemu ya "think tank" ndani ya chama tawala, ktk hili sijui yeye analisemaje kwa kigezo hicho hicho cha maganda yake ya elimu ya juu.

Ukienda ktk makundi ya wafanyabiashara maarufu, wasanii wa filamu na muziki maarufu, viongozi wa dini na hata wazee wengi wastaafu, kwao kukosa elimu kama yake hakumfanyi kustahili kuwapa heshima, wala kuweza kujadiliana nae! Eti kwa kigezo hicho hicho cha kukosa elimu ya juu kama yeye. Nafikiri alipata mhemuko tu ili kumridhisha bosi wake, na wala si vinginenevyo.
 
"Kama msanii unang'ang'ana kuimba siasa na kukosoa serikali basi amua kuachana na muziki uanzishe chama cha siasa. Lakini kama unataka kupata maslahi kwenye muziki, basi nyimbo hizo hazilipi. Haiingii akilini nina shahada nne halafu msanii ambaye hajaenda hata shule anatunga nyimbo za kunikosoa. Wewe na darasa la nne lako sijui la 7 utanionya mimi mwenye degree nne na nimefundisha vyuo vikuu mbalimbali?" Dr.Harisson Mwakyembe (PhD), Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo.!
Mitume na manabii wa vitabu vya dini tunazoamini na kufuata hawakwenda shule yoyote. Ajishushae huinuliwa BUT ajiinuae hushushwa!
 
Roma arudi shule jamani

Mtu anaefundisha au aliwahi kufundisha chuo sio wa kumfananisha na alieishia darasa la saba jamani huo ni ukweli usiopingika

Mwakyembe alipasua GPA kubwa Bachelor akabakizwa kuwa mwanataaluma UDSM huwezi fananisha na Msanii yeyote hapa nchini
GPA za kumeza(Kukariri usiku mzima) kisha unatema kesho kwenye paper ndo kuwa na akili? Si huyu huyu aliyekana thesis yake showing kwamba hata alichokiandika mle either hakijui au aliandikiwa
 
Hatakama ulikuwa kipanga darasani kwa kiasi gani lakini ukishindwa kutafsiri elimu uliyonayo katika mazingira yako ni kazi bure,impact ya taaluma yako kwenye jamii ni nini?
Ulishawahi kujiuliza ni kwanini sikuhizi degree zinadharaulika?Unafahamu kwamba NGOs nyingi sikuhizi hawaangalii degree zaidi ya kuangalia capacity ya delivarence?
Roma arudi shule jamani

Mtu anaefundisha au aliwahi kufundisha chuo sio wa kumfananisha na alieishia darasa la saba jamani huo ni ukweli usiopingika

Mwakyembe alipasua GPA kubwa Bachelor akabakizwa kuwa mwanataaluma UDSM huwezi fananisha na Msanii yeyote hapa nchini
 
Back
Top Bottom