Roma na wenzake wapatikana, wapelekwa Kituo cha Polisi Oysterbay kisha Mwananyamala Hosp na kuachiwa

Roma na wenzake wapatikana, wapelekwa Kituo cha Polisi Oysterbay kisha Mwananyamala Hosp na kuachiwa

Nimethibitisha kuwa ROMA na wenzake wamepatikana na wako kituo cha polisi Oysterbay.

Habari ya akina Roma kupatikana imethibitishwa na Mkurugenzi wa Tongwe Records - J. Mada. Tutaendelea kuwaletea habari zaidi
 
wametamka jeshi la polisi hawatambui wala.hawa kuhusika.sasa huko ostabey kafata nini
 
Mmmmmmh hii movie sijui director nani??
 
Kama kweli kamanda sirro anatakiwa kuwajibishwa kwa kutoa Taarifa za uongo maana alikanusha kuwa hakuna kituo kinacho mshikiria, lakin kwa upande mwingine tumsamehe tu mzee wawatu kwa sababu mzee wawatu alikuwa msafi ila anatiwa najisi bila ridhaa hana namna mzee wawatu anapitia kipind kigumu sana sasa nadhana atakuwa anataman mda wa kustaafu ufike haraka ili kikombe hiki akihepuke.
amepatikana huko alikopatikana halafu kapelekwa kituoni
 
hivi mmelishwa karanga za moto!
mbona kila tukio in dar ni bashite bashite! akha! asingesema chochote napo sijui mngesemaje kuna watu humu mnahukumu mtu hata uthibitisho hakuna! haya mambo naanza kuyaangalia upande wapili sasa...
Dah.... Alosto hizo.... wakipona wataacha[emoji13] [emoji13]
 
*Wanadamu wenzetu wanapotea tupo kimya* kama waliopotea sio binadamu ni *viazi mviringo*
Faru alipopotea hata DNA ilifanyika na *waziri mkuu alikuwa mkali kama mbogo* hii ni hatari na hii ni ishara tosha ya kuchokwa na wanaotutawala
*Kaa kimya kama Diamond alivyokaa kimya na kuimba kawimbo kake kakiboya kakujinyenyekeza as if aliyepotea sio mwanamziki mwenzake*, ipo siku utapotea ww na wengine watakaa kimya kama ulivyokaa kimya ww
Mfyuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu
*#BringBack Roma na wenzake*
*#BringBack Ben Ben-Rabiu Wa Saanane*
[HASHTAG]#TeamNyalila2020[/HASHTAG] [emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Ikiwezekana atafutwe Daktari binafsi ampime kama ana vimelea vyovyote vya sumu kali ya cyanide tafadhali. Hili lifanyike upesi kama siyo haraka tafadhalini.

Sio tu Vimelea Bali hata Malinda!
 
Kama kweli ameonekana je na wengine walipotea watuoneshe basi bensaa8
 
Nasubilia kwa hamu kuipata full story, maana mpaka Mond kafungukia hili swala, na pengine wamehofu kuwa ishu itakuwa kubwa sana wakimpoteza, ndio maana wamecheza bongo movie.
 
Back
Top Bottom