Roman Abramovich: Utajiri wa Damu, Risasi na Umafia

Roman Abramovich: Utajiri wa Damu, Risasi na Umafia

Habari ndugu zangu, binafsi napenda sana kumpongeza ndugu Habib Hanga kwa kazi nzuri nmekuwa nikifatilia makala zake miaka mingi sana humu JF wakati mwengne nasoma kwa shauku ya kutaka kujua kitachoendelea nasahau hata kulike, ila kiukwel ni mtu mwenye kipaji chake hongera sana na pia nawaomba wana Jf tuwe na shukrani acheni roho mbaya kazi ya kuandika ni ngumu sana, hivyo msiwe na maneno maneno mabaya
 
ROMAN ABRAMOVICH: UTAJIRI WA DAMU, RISASI NA UMAFIA



SEHEMU YA SABA



Yule mwalimu wake wa chuo kikuu Profesa Anatoly Sobchak ambaye Putin aliporejea kutoka Ujerumani na kupangiwa jukumu la kishushushu chuo kikuu cha Leningrad alifufua upya urafiki naye, mwaka 1990 Profesa Sobchak aligombea kiti cha Umeya wa mji wa Leningrad na kushinda. Baada ya kushinda kiti cha Umeya alimteua Putin kuwa mshauri wake wa masuala ya Kimataifa.



Mwaka uliofuata Putin alijiuzulu nyadhifa zake zote ndani ya KGB kutokana na kutoridhishwa na msimamo mpya wa idara hiyo na utendaji wake. Nikiwa mahususi zaidi, kujiuzulu huku kwa Putin kulikuwa ni siku ya tarehe 20 August mwaka 1991. Kama unafahamu vyema historia ya Urusi unaweza kuona kwamba hiyo ilikuwa ni siku mbili tu baada ya jaribio la kumpindua rais Michail Gorbachev. Hii ilikuwa ni namna yake Putin kuonyesha kwamba hakukubaliana na kile ambacho kilikuwa kimetokea. Uamuzi huu wa kujiuzulu kutoka shirika la kijasusi la KGB ulikuwa ni mgumu sana kwa Putin kwani maisha yake yote ya ukubwa aliyaishi kama jasusi ndani ya shirika hili.



Nchini Urusi katika ofisi ya Meya shughuli zinaendeshwa kupitia kamati mbalimbali ambazo zinakuwa chini ya ofisi ya Meya. Mwaka huo huo 1991, Putin ‘akaula’ tena… akateuliwa kuongoza kamati ambayo inashughulika na Mahusiano ya kimtaifa, uwekezaji kutoka nje na usajili wa makampuni (tusichanganye na kile cheo chake cha awali, “Mshauri wa Meya juu ya Masuala ya Kimatifa”). Hapa ndipo ambapo nataka hasa kupawekea mkazo zaidi.



Eneo la Leningrad lina utajiri mkubwa sana wa migodi ya chuma na uzalishaji aluminium. Kwa hiyo cheo hiki kipya cha kuongoza kamati ya kushughulikia uwekezaji, usajili wa makampuni na mahusiano ya nchi za nje kilikuwa ulaji mkubwa. Siku nikiandika kuhusu Putin nitaeleza kisanga ambacho kilitokea mwaka wake wa kwanza tu baada ya kuteuliwa kuongoza kitengo hiki mpaka kupelekea kuchunguzwa na Baraza la Bunge la Mji wa Leningrad.

Niwape kwa muhtasari tu… ni kwamba katika kipindi hiki Urusi ndio ilikuwa ina-recover kutoka kwenye mdororo wa kiuchumi. Jamii nyingi zilikuwa zinaishi kwenye umasikini wa kupitiliza. Kwenye baadhi ya miji walikuwa wanaweza masharti nafuu ya uwekezaji kama vile misamaha au unafuu wa kodi.

Sasa kuna makampuni kutoka nje ya Russia ambayo kwa maelekezo ya Putin kama mwenyekiti wa kamati ya uwekezaji ya Leningrad yaliuziwa kiasi cha ‘metals’ zenye thamani ya dola milioni 93 kwa makubaliano kwamba walete chakula cha msaada. Chakula hiki cha msaada hakikuonekana Leningrad. Ikazuka minong’ono kwamba kuna watu Putin alikula nao dili kwenye mchezo huu. Ndipo hapa ikaundwa tume ikiongozwa na mwanamama machachali Marina Salye……. Kuchunguza kisanga hiki. Kuna vimbwanga vingi sana ndani ya skandali hii ambavyo sitaviongelea leo hii, lakini mwisho wa uchunguzi wa kamati wakatoa pendekezo kwamba Putin afutwe kazi na pia afunguliwe mashtaka.



Lakini hakuna lolote kati ya hayo mapendekezo ambayo kilitekelezwa ambalo lilitekelezwa. Kwa nini?

Ukiwa porini, ukila nyama hakikisha unakula na simba… hakuna ambaye atathubutu kukusogolea kupoka mnofu wako.

Habari za ndani zinasema kwamba kuna uwezekano mkubwa Putin alifanya dili hii kwa kushirikiana na Oligarch Berezovsky ambaye kwa kipindi kile alikuwa na ushawishi mkubwa sana ndani ya Moscow. Tunakumbuka kwamba Borozovksy pia ndiye kwa kipindi hicho alikuwa ‘mentor’ wa Roman Abramovich.

Skandali hii ndio kwa mara ya kwanza ilimfanya Abramovich kumfahamu Putin na kuvutiwa naye kutokana na historia yake ya kutumikia kwenye shirika la ujasusi,uimara wa misimamo yake na pia haiba yake ya kutaka mabadiliko ya kimfumo ndani ya Russia. Putin alikuwa anajulikana mjini Leningrad kutokuung mkono sera za kijamaa ambazo zilikuwa zinatumika huko nyuma kuendesha nchi.





Wanasema ukiona vyaelea ujue vimeundwa. Ni nandra mno mno kwa mtu yeyote yule kwenye ulimwengu wa sasa kupanda mpaka nafasi ya juu kabisa ya utumishi wa nchi kama vile Urais kwa bahati mbaya. Kuna watu watasema “vipi kuhusu Trump.” No, it wasn’t an accident. Kuna wengine wanahisi hata rais fulani hapa Afrika Mashariki mwaka 2015 aliukwaa Urais kwa bahati mbaya bila kujua historia yake ndani ya Idara ya Ujasusi wa nchi hiyo na bila kujua kikao cha kimkakati cha April 23, 2015 kilichofanyika nje kidogo ya mji wa Morogoro kati ya maafisa waandamizi wa idara ya ujasusi wa nchi hiyo na viongozi watatu wakubwa wastaafu. Too bad siwezi kuandikia hayo mambo…

Ninachotaka kusema ni kwamba ukiona vyaelea ujue vimeundwa… ni nadra mno katika ulimwengu wa leo mtu kuinuka mpaka kufikia uongozi wa juu wa nchi kwa bahati mbaya. Kila kiongozi anaundwa na kufinyangwa na mtu fulani.



Nimeeleza kwamba skandali ya uuzaji wa ‘metals’ zenye thamani ya dola milioni 93 ndizo ambazo zilimfanya Abramovich kumfahamu Putin na hatimaye kuvutiwa naye… sasa taratibu Abramovich akaanza kumfinyanga Putin. Huko nyuma nilishaeleza ni namna gani ambavyo Abramovich aliweza kujijenga kiushawishi na mpaka hatimaye kuwa kati ya wale wajulikanao kama “The Family” ndani ya Moscow na hata baadae ushawishi wake kupitiliza kuwa pengine mtu mwenye kusikilizwa zaidi na Rais Boris Yeltsin.

Ni katika kipindi hiki ambacho Roman Abramovich akaanza kumjenga Putin. Nitaeleza namna ambavyo Putin alikuwa anapanda ngazi kwa kasi ya ajabu mara baada ya kwenda Moscow.





Sasa,



Katika uchaguzi ambao ulifuata yaani uchaguzi wa mwaka 1995 yule Profesa rafiki wa Putin alipoteza kiti chake cha Umeya. Hii ilimlazimu Putin kuhamia Moscow kuangalia fursa nyingine. Baada ya kuwasili tu Moscow kwa ushawishi wa Abramovich Putin aliteuliwa kuwa deputy Chief wa Idara ya Presidential Property Management. Idara hii ilikuwa inahusika na menejiment ya mali za Urusi nje ya mipaka yao (kama vile uwekezaji) lakini pia Idara hii ilihusika na kuhamisha mali za nchi ambazo awali zilikuwa chini ya Shirikisho la Urusi kabla ya kuvunjika na kuzihamishia kwenye umiliki wa Urusi ya sasa. Unaweza kuona ni kwa kiasi gani jukumu huli lilikuwa ni nyeti.



Mwaka mmoja baaadae, kwa mara nyingine tena kwa ushawishi wa Abramovich Putin aliteuliwa kuwa Naibu katibu mkuu Kiongozi. Wakati anateuliwa katika nfasi hii, ile ya ile nafasi ya kwanza pia bado alikuwa anaendelea nayo (nafasi ya Deputy Chief of Presidential Property Management Department). Miezi michache baadae ile nafasi ya kwanza ambayo aliteuiwa kama Deputy chief, akapandishwa cheo kuwa Chief. Kwa hiyo kwa wakati mmoja Putin alikuwa ni Naibu katibu Mkuu kiongozi na pia alikuwa Chief of Presidential Property Management Department.



Kila baada ya miezi kadhaa Putin alikuwa anapanda cheo kwa kasi ya ajabu na kuna mahala maalumu ambako Abramovich alikuwa anataka Putin afike.



Siku ya tarehe 25, July mwaka 1998 kwa nguvu na ushawishi wa muda mrefu wa Oligarch Roman Abramovich… Putin aliteuliwa kuwa Mkurugenzi mkuu wa Federal Security Services (FSB). Hii FSB ndio idara ambayo iliundwa kurithi kazi za kijasusi za KGB ambayo ilivunjwa. Kwa hiyo kwa muda wa miaka miwili tu tangu aingie Moscow Putin alikiwa amepanda vyeo kwa kasi na sasa alikiwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa wa Russia.



Usione vyaelea, vimeundwa.





Tunarejea pale ambapo ma-oligarch walimfuata Abramovich kumuomba mawazo… ni nani anafaa kumrithi rais Boris Yeltsin??

Wao walikiwa wanauliza leo… lakini mwenzao alijiandaa kuwajibu swali hili miaka minne nyuma. Tayari alikuwa na mtu kichwani kabla hata hawajauliza au kwa usahihi zaidi, alikuwa na jibu la swalo lao kabla hata hawajaanza kuwaza kuhusu swali hilo.



Maana halisi kabisa ya mtu anayeishi kimkakati na Kuwaza kimkakati. A natural born tactician.







Maoligarch, tukutane hapa siku ya jumanne mchana kwa ajili ya sehemu ya nane…











The Bold – 0718 096 811

To Infinity and Beyond
 
SEHEMU YA SABA


Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi @Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM @Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu The Certified DON SINYORI mij addenbwii ONTARIO Kobe The Vein Mondray jaxonjaxon successor mzee wa liver sawariya Sitaki ukuda Domhome Mpatanishi MKANDAHARI mtugani wa wapi huyo wealthier cluecell Toyota escudo mgumu2 troublemaker Linamo shedede kamtu33 SteveMollel ngushi Donald stewart Mshuza2 Glycel mnonje Ochuanilove SingleFather Santi DEOD 360 ngushi anatory antony ukhuty chris van chicha auxillius Goma Son Hubeb pes KING DUBU VILLAIN mwayena donbeny Aleppo JipuKubwa shoo61 BOMBAY John mungo Nyakageni bato Dogo 1 sufra chamlungu painscott wegman Bravo Engliash MOSELBAY wa stendi FaizaFoxy bigmind cadabraa Internal Kelvin mwalukas mnonje Kelvin X Somoche Wgr30 Miiku Poise Jabman kalamuyamwalimu BOMBAY the say juxhb witnessj Gide MK Mmanyema mgogoone Mnongane Mandingo koncho77 afsa ngaboru Paradoxer Heavy Metal KIMBURU 06 Raaj kichekoh ngumba njeche kikale DullahTza Goodluck Mshana julius Darcy Denis Kasekenya mashonga kitalembwa Khaleed Shaban middle east SirChief jiwe jeusi Mkambarani mansakankanmusa gambada ynwa ney kush mossad 03 white wizard xtaper Mzigua90 Ollachuga Oc Gidbang Mateja M.G Yango jipu abaa4all DIBAJI Agenda1 Grahnman The MaskmaN Slim5 Xubzero agprogrammer JoJiPoJi Architectus blance86 Mamtolo monde arabe Ngao Ya Imani stardust JK naiman64 Dharra seledunga ABB SHAMMA Richard Waziri wa Kaskazini Mwinjuma1 Kanungila Karim baracuda Mwamba028 besaro Pyepyepye Bilionea Asigwa ibn Kiti Chema Tugas Royal Warrior mederii mmangO manzi james LIKUD adrenaline Royal Son Mhadzabe salaniatz Natasha Ismail jiwe jeusi chibalangunamchezo
John Mloy conjuget Van Pauser great G Mtoto wa nzi Zeus1 hindustan Sci-Fi MAN OF PEACE kashata emnly danny baraka bb MTOTELA kbosho TEMLO DA VINCA
 
ROMAN ABRAMOVICH: UTAJIRI WA DAMU, RISASI NA UMAFIA



SEHEMU YA SABA



Yule mwalimu wake wa chuo kikuu Profesa Anatoly Sobchak ambaye Putin aliporejea kutoka Ujerumani na kupangiwa jukumu la kishushushu chuo kikuu cha Leningrad alifufua upya urafiki naye, mwaka 1990 Profesa Sobchak aligombea kiti cha Umeya wa mji wa Leningrad na kushinda. Baada ya kushinda kiti cha Umeya alimteua Putin kuwa mshauri wake wa masuala ya Kimataifa.



Mwaka uliofuata Putin alijiuzulu nyadhifa zake zote ndani ya KGB kutokana na kutoridhishwa na msimamo mpya wa idara hiyo na utendaji wake. Nikiwa mahususi zaidi, kujiuzulu huku kwa Putin kulikuwa ni siku ya tarehe 20 August mwaka 1991. Kama unafahamu vyema historia ya Urusi unaweza kuona kwamba hiyo ilikuwa ni siku mbili tu baada ya jaribio la kumpindua rais Michail Gorbachev. Hii ilikuwa ni namna yake Putin kuonyesha kwamba hakukubaliana na kile ambacho kilikuwa kimetokea. Uamuzi huu wa kujiuzulu kutoka shirika la kijasusi la KGB ulikuwa ni mgumu sana kwa Putin kwani maisha yake yote ya ukubwa aliyaishi kama jasusi ndani ya shirika hili.



Nchini Urusi katika ofisi ya Meya shughuli zinaendeshwa kupitia kamati mbalimbali ambazo zinakuwa chini ya ofisi ya Meya. Mwaka huo huo 1991, Putin ‘akaula’ tena… akateuliwa kuongoza kamati ambayo inashughulika na Mahusiano ya kimtaifa, uwekezaji kutoka nje na usajili wa makampuni (tusichanganye na kile cheo chake cha awali, “Mshauri wa Meya juu ya Masuala ya Kimatifa”). Hapa ndipo ambapo nataka hasa kupawekea mkazo zaidi.



Eneo la Leningrad lina utajiri mkubwa sana wa migodi ya chuma na uzalishaji aluminium. Kwa hiyo cheo hiki kipya cha kuongoza kamati ya kushughulikia uwekezaji, usajili wa makampuni na mahusiano ya nchi za nje kilikuwa ulaji mkubwa. Siku nikiandika kuhusu Putin nitaeleza kisanga ambacho kilitokea mwaka wake wa kwanza tu baada ya kuteuliwa kuongoza kitengo hiki mpaka kupelekea kuchunguzwa na Baraza la Bunge la Mji wa Leningrad.

Niwape kwa muhtasari tu… ni kwamba katika kipindi hiki Urusi ndio ilikuwa ina-recover kutoka kwenye mdororo wa kiuchumi. Jamii nyingi zilikuwa zinaishi kwenye umasikini wa kupitiliza. Kwenye baadhi ya miji walikuwa wanaweza masharti nafuu ya uwekezaji kama vile misamaha au unafuu wa kodi.

Sasa kuna makampuni kutoka nje ya Russia ambayo kwa maelekezo ya Putin kama mwenyekiti wa kamati ya uwekezaji ya Leningrad yaliuziwa kiasi cha ‘metals’ zenye thamani ya dola milioni 93 kwa makubaliano kwamba walete chakula cha msaada. Chakula hiki cha msaada hakikuonekana Leningrad. Ikazuka minong’ono kwamba kuna watu Putin alikula nao dili kwenye mchezo huu. Ndipo hapa ikaundwa tume ikiongozwa na mwanamama machachali Marina Salye……. Kuchunguza kisanga hiki. Kuna vimbwanga vingi sana ndani ya skandali hii ambavyo sitaviongelea leo hii, lakini mwisho wa uchunguzi wa kamati wakatoa pendekezo kwamba Putin afutwe kazi na pia afunguliwe mashtaka.



Lakini hakuna lolote kati ya hayo mapendekezo ambayo kilitekelezwa ambalo lilitekelezwa. Kwa nini?

Ukiwa porini, ukila nyama hakikisha unakula na simba… hakuna ambaye atathubutu kukusogolea kupoka mnofu wako.

Habari za ndani zinasema kwamba kuna uwezekano mkubwa Putin alifanya dili hii kwa kushirikiana na Oligarch Berezovsky ambaye kwa kipindi kile alikuwa na ushawishi mkubwa sana ndani ya Moscow. Tunakumbuka kwamba Borozovksy pia ndiye kwa kipindi hicho alikuwa ‘mentor’ wa Roman Abramovich.

Skandali hii ndio kwa mara ya kwanza ilimfanya Abramovich kumfahamu Putin na kuvutiwa naye kutokana na historia yake ya kutumikia kwenye shirika la ujasusi,uimara wa misimamo yake na pia haiba yake ya kutaka mabadiliko ya kimfumo ndani ya Russia. Putin alikuwa anajulikana mjini Leningrad kutokuung mkono sera za kijamaa ambazo zilikuwa zinatumika huko nyuma kuendesha nchi.





Wanasema ukiona vyaelea ujue vimeundwa. Ni nandra mno mno kwa mtu yeyote yule kwenye ulimwengu wa sasa kupanda mpaka nafasi ya juu kabisa ya utumishi wa nchi kama vile Urais kwa bahati mbaya. Kuna watu watasema “vipi kuhusu Trump.” No, it wasn’t an accident. Kuna wengine wanahisi hata rais fulani hapa Afrika Mashariki mwaka 2015 aliukwaa Urais kwa bahati mbaya bila kujua historia yake ndani ya Idara ya Ujasusi wa nchi hiyo na bila kujua kikao cha kimkakati cha April 23, 2015 kilichofanyika nje kidogo ya mji wa Morogoro kati ya maafisa waandamizi wa idara ya ujasusi wa nchi hiyo na viongozi watatu wakubwa wastaafu. Too bad siwezi kuandikia hayo mambo…

Ninachotaka kusema ni kwamba ukiona vyaelea ujue vimeundwa… ni nadra mno katika ulimwengu wa leo mtu kuinuka mpaka kufikia uongozi wa juu wa nchi kwa bahati mbaya. Kila kiongozi anaundwa na kufinyangwa na mtu fulani.



Nimeeleza kwamba skandali ya uuzaji wa ‘metals’ zenye thamani ya dola milioni 93 ndizo ambazo zilimfanya Abramovich kumfahamu Putin na hatimaye kuvutiwa naye… sasa taratibu Abramovich akaanza kumfinyanga Putin. Huko nyuma nilishaeleza ni namna gani ambavyo Abramovich aliweza kujijenga kiushawishi na mpaka hatimaye kuwa kati ya wale wajulikanao kama “The Family” ndani ya Moscow na hata baadae ushawishi wake kupitiliza kuwa pengine mtu mwenye kusikilizwa zaidi na Rais Boris Yeltsin.

Ni katika kipindi hiki ambacho Roman Abramovich akaanza kumjenga Putin. Nitaeleza namna ambavyo Putin alikuwa anapanda ngazi kwa kasi ya ajabu mara baada ya kwenda Moscow.





Sasa,



Katika uchaguzi ambao ulifuata yaani uchaguzi wa mwaka 1995 yule Profesa rafiki wa Putin alipoteza kiti chake cha Umeya. Hii ilimlazimu Putin kuhamia Moscow kuangalia fursa nyingine. Baada ya kuwasili tu Moscow kwa ushawishi wa Abramovich Putin aliteuliwa kuwa deputy Chief wa Idara ya Presidential Property Management. Idara hii ilikuwa inahusika na menejiment ya mali za Urusi nje ya mipaka yao (kama vile uwekezaji) lakini pia Idara hii ilihusika na kuhamisha mali za nchi ambazo awali zilikuwa chini ya Shirikisho la Urusi kabla ya kuvunjika na kuzihamishia kwenye umiliki wa Urusi ya sasa. Unaweza kuona ni kwa kiasi gani jukumu huli lilikuwa ni nyeti.



Mwaka mmoja baaadae, kwa mara nyingine tena kwa ushawishi wa Abramovich Putin aliteuliwa kuwa Naibu katibu mkuu Kiongozi. Wakati anateuliwa katika nfasi hii, ile ya ile nafasi ya kwanza pia bado alikuwa anaendelea nayo (nafasi ya Deputy Chief of Presidential Property Management Department). Miezi michache baadae ile nafasi ya kwanza ambayo aliteuiwa kama Deputy chief, akapandishwa cheo kuwa Chief. Kwa hiyo kwa wakati mmoja Putin alikuwa ni Naibu katibu Mkuu kiongozi na pia alikuwa Chief of Presidential Property Management Department.



Kila baada ya miezi kadhaa Putin alikuwa anapanda cheo kwa kasi ya ajabu na kuna mahala maalumu ambako Abramovich alikuwa anataka Putin afike.



Siku ya tarehe 25, July mwaka 1998 kwa nguvu na ushawishi wa muda mrefu wa Oligarch Roman Abramovich… Putin aliteuliwa kuwa Mkurugenzi mkuu wa Federal Security Services (FSB). Hii FSB ndio idara ambayo iliundwa kurithi kazi za kijasusi za KGB ambayo ilivunjwa. Kwa hiyo kwa muda wa miaka miwili tu tangu aingie Moscow Putin alikiwa amepanda vyeo kwa kasi na sasa alikiwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa wa Russia.



Usione vyaelea, vimeundwa.





Tunarejea pale ambapo ma-oligarch walimfuata Abramovich kumuomba mawazo… ni nani anafaa kumrithi rais Boris Yeltsin??

Wao walikiwa wanauliza leo… lakini mwenzao alijiandaa kuwajibu swali hili miaka minne nyuma. Tayari alikuwa na mtu kichwani kabla hata hawajauliza au kwa usahihi zaidi, alikuwa na jibu la swalo lao kabla hata hawajaanza kuwaza kuhusu swali hilo.



Maana halisi kabisa ya mtu anayeishi kimkakati na Kuwaza kimkakati. A natural born tactician.







Maoligarch, tukutane hapa siku ya jumanne mchana kwa ajili ya sehemu ya nane…











The Bold – 0718 096 811

To Infinity and Beyond
Safi Sana Oligarch The Bold
 
Asante The bold kwa kazi nzuri.wengine hatuishii kuburudika tu bali tunajifunza pia.hasa wale ambao tunafikiria kuwa kuna mambo huwa yanatokea kwa bahati mbaya.naomba ni add tena kwenye tag list yako mkuu.
 
........ Kuna wengine wanahisi hata rais fulani hapa Afrika Mashariki mwaka 2015 aliukwaa Urais kwa bahati mbaya bila kujua historia yake ndani ya Idara ya Ujasusi wa nchi hiyo na bila kujua kikao cha kimkakati cha April 23, 2015 kilichofanyika nje kidogo ya mji wa Morogoro kati ya maafisa waandamizi wa idara ya ujasusi wa nchi hiyo na viongozi watatu wakubwa wastaafu. Too bad siwezi kuandikia hayo..,......

[emoji115][emoji115][emoji115][emoji115][emoji115][emoji2534][emoji115][emoji2534][emoji115][emoji2534][emoji115][emoji2534]Ungeongeza nyama na hapa kidogo mkuu.[emoji848][emoji848][emoji848]
 
Umenifundisha mambo mawili. Mosi fursa za namna hii tunakutana nazo sana wengine lakini tunambwelambwela kuzichangamkia na pili imani zetu wenine kidini zinatufanya tusite sana kudaka baadhi ya fursa
 
........ Kuna wengine wanahisi hata rais fulani hapa Afrika Mashariki mwaka 2015 aliukwaa Urais kwa bahati mbaya bila kujua historia yake ndani ya Idara ya Ujasusi wa nchi hiyo na bila kujua kikao cha kimkakati cha April 23, 2015 kilichofanyika nje kidogo ya mji wa Morogoro kati ya maafisa waandamizi wa idara ya ujasusi wa nchi hiyo na viongozi watatu wakubwa wastaafu. Too bad siwezi kuandikia hayo..,......

[emoji115][emoji115][emoji115][emoji115][emoji115][emoji2534][emoji115][emoji2534][emoji115][emoji2534][emoji115][emoji2534]Ungeongeza nyama na hapa kidogo mkuu.[emoji848][emoji848][emoji848]
Nimesoma nakurudia mara 3 maelezo hayo natamani aongeze nyama nyingi
 
Balance shobo
Mi na ww mwenye shobo nani? Memquote The bold na kindly tumeshayamaliza ww kiherere cha nn kuingilia yasiyokuhusu? Kadange mbele ki front front punguza ama ukiweza acha😉😉
 
Back
Top Bottom