Rombo: Miaka 30 jela kwa kumlawiti mwanaume mwenzie

Rombo: Miaka 30 jela kwa kumlawiti mwanaume mwenzie

Muuza Kangala

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2021
Posts
1,242
Reaction score
4,813
MAHAKAMA ya Wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro imemuhukumu Valency Panclas Mtales (43) mkazi wa kijiji cha Mamsera chini, Kwenda jela miaka 30, kwa kosa la kumlawiti mwanaume mwenzie mwenye umri wa miaka 24.

Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Regina Futakamba Machi 22 mwaka huu baada ya Mahakama kujiridhisha pasipo na shaka ushahidi uliotolewa na mashahidi wanane wa upande wa mashitaka.

Mahakama hiyo chini ya kifungu namba 154 kifungu cha kwanza A cha sheria ya kanuni ya adhabu namba 16 ambayo imefanyiwa marejeo mwaka 2022 ilimtia hatiani mshitakiwa huyo na kutumikia kifungo cha miaka 30 gerezani.

Chanzo: Nipashe
 
Kama aliyelawitiwa ni Mwanaume maana yake sio mtoto, ni Mwanaume Shoga na kama hakunyweshwa pombe akazima au kupewa madawa yakamlevya basi aliridhia kulawitiwa, je yeye amehukumiwa miaka mingapi?

Au amehukumiwa kunyongwa?

Mnamhukumu Basha mnamwacha shoga lake?
 
Kama aliyelawitiwa ni Mwanaume maana yake sio mtoto, ni Mwanaume Shoga na kama hakunyweshwa pombe akazima au kupewa madawa yakamlevya basi aliridhia kulawitiwa, je yeye amehukumiwa miaka mingapi?

Au amehukumiwa kunyongwa?

Mnamhukumu Basha mnamwacha shoga lake?
Inaonekana ni wale wanaofumania na kuamua kulawiti mgoni
 
Habari ya kuokoteza .

Habari haijakamilika hii, tuambie sababu ya kumlawiti mwenzake ni nini , na mlawitiwa aliridhia au lah alibakwa, kama aliridhia basi wote wafungwe
 
Habari za kupapulisha hizi,aliyelawitiwa ameachwa ili awakamatishe wengine au?
 
Huyu wa miaka 24 kinachofanya awe huru mpaka sasa ni nini?
Habari ya kuokoteza .

Habari haijakamilika hii, tuambie sababu ya kumlawiti mwenzake ni nini , na mlawitiwa aliridhia au lah alibakwa, kama aliridhia basi wote wafungwe
Au Mwenye miaka 24 kala mke wa mtu nae kaliwa?? Hii stori haijashiba nyama
 
Back
Top Bottom