Kafanya "jambo la kiungwana sana", huku akishaufikisha ujumbe alionuia kuufikisha kwa wahusika.Rostam Aziz ameomba radhi kwa majaji akisema ulimi uliteleza na hakumaanisha ambacho alikisema kuhusu majaji kuhongwa. Nadhani amefanya jambo la kiungwana sana.
Tusimuingize Mungu kwenye mambo ya TAKUKURU.Mtu,Basi huyo Jaji hata uwona ufalme wa Mungu!!
Duh....nimejikuta nacheka mwenyewe!!!!!Nilijua tu, lazima angelegea na kuomba radhi, kutoa shutuma bila kuwa na ushahidi wa kutosha wa shutuma dhidi ya wale unaowalalamikia ni udhaifu, lakini pia, tena zaidi, kama wale unaowalalamikia ni wenzako - CCM.
Sasa matokeo yake Rostam kwa sababu ya kutokuchagua cha kuzungumza, na wapi akizungumze, amejikuta ameenda kutengeneza maadui zaidi ya yule Dr. Slaa aliyemdhamiria, hapo sasa kwa msamaha wake, amejikuta amejichafua yeye mwenyewe, na kuwasafisha wachafu - CCM na mahakama zake.
"Kama nilisema..." bado haamini kuwa alisema.Kama nilisema hivyo ilikuwa ni kuteleza kwa ulimi maana kusudio langu lilikuwa likilenga kuhusu uwekezaji nchini na maana yangu ilikuwa ni kwamba ili tuweze kupata uwekezaji nchini mwetu hatuna budi kuendana na taratibu zinazoongoza uwekezaji Duniani.
KabisaJapo ni fisadi, katika hili, kasema ukweli.
Kwa hiyo na upuuzi wote aliozungumza ni kuteleza ulimi??Mfanyabiashara, Rostam Aziz amekiangukia Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania (JMAT), akiomba radhi kutokana na kauli aliyoitoa dhidi ya Mahakama nchini.
Rostam ameomba radhi saa chache baada ya JMAT kutoa taarifa kwa umma kupitia vyombo vya habari, kikimtaka mfanyabiashara huyo athibitishe tuhuma alizotoa dhidi ya Mahakama au aombe radhi hadharani.
Rostam, Juni 26, mwaka huu mbele ya waandishi wa habari alisema, "Hakuna mwekezaji atawekeza kwenye nchi ambayo kesi ikipelekwa hapo Kisutu kiongozi yoyote anaweza kupiga simu akaielekeza mahakama nini cha kufanya.”
Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Rostam alizungumzia faida za uwekezaji wa sekta binafsi katika uendeshaji wa bandari, akirejea mkataba wa ushirikiano uliosainiwa na Serikali ya Tanzania na Dubai kuhusu uwekezaji na uendelezaji wa bandari nchini.
Hata hivyo, sakata hilo limeibua hisia tofauti za wananchi, wengine wakikosoa kutokana na kile wanachoeleza kuwa, baadhi ya vifungu vya mkataba huo vina kasoro na hatari kwa masilahi ya nchi.
JMAT ilitangaza kusikitishwa na kauli hiyo ikisema, "Anapaswa athibitishe kauli yake akibainisha jina la Jaji na lini alipewa maagizo na Serikali kutoa maamuzi kinyume na taratibu zilizopo. Akishindwa kutoa uthibitisho, tunamtaka atumie jukwaa lile lile kuomba radhi kwa uzito ule ule.”
Baada ya taarifa hiyo, Rostam leo Jumanne, Julai 4, 2023 amezungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake jijini Dar es Salaam, akieleza alichokizungumza siyo kusudio lake ni kuteleza kwa ulimi.
"Kwa sababu ya kutambua na kuheshimu dhima, hadhi na wajibu wa kikatiba wa Mahakama, ningependa kusema yafuatayo.
"Ningependa kuuhakikishia umma, kwamba wakati nikizungumzia uwekezaji halikuwa kusudio langu kuidharau Mahakama," amesema.
Alichokizungumza, amesema ameteleza ulimi na si kusudiolake.
"Niliteleza ulimi, maana kusudio langu lilikuwa ni kueleza kuhusu uwekezaji nchini na maana yangu ilikuwa ni kwamba, ili tupate uwekezaji nchini hatuna budi kuendana na taratibu," amesema.
MWANANCHI
Rushwa nchi wameikamata vizuri snHawa Caucasians wanatamba sana. Wanafanya watakalo nchi hii.
Ndiyo imefanya waarabu waombe sheria za uingereza, walijua wa Tanzania ni manguli wa sheria, rostam wangemfilisi
Ujumbe umefika,hata kama kaomba radhiMbona kila kitu kinajulikana
Kauli ya mwanzo huwa ni sahihi sana. Hata Polisi wanaheshimu sana maelezo ya tahadhari ya mwanzo
Heh heh ujumbe keshawafikishia hao waheshimiwa majaji na mahakimu, huwezi ukalinganisha majaji , mahakimu na wanasheria wetu na wale wa nchi jirani ya Kenya, hawa wasomi wetu ni wa hovyo kupitiliza, eti tuna wanasheria kama Fatuma Karuma, Tundu Lissu, Kibatalla,Mwakyembe na wengineo. Hawa huwezi kuwalinganisha na wa enzi za akina Lamwai, Mabero Marando, Ringo Tenga, Jaji Nyirabu, Warioba...Rostam Aziz ameomba radhi kwa majaji akisema ulimi uliteleza na hakumaanisha ambacho alikisema kuhusu majaji kuhongwa. Nadhani amefanya jambo la kiungwana sana.
========
Leo Jumanne July 4, 2023 mfanyabiashara mashuhuri nchini, Rostam Aziz ameongea na vyombo vya habari, pamoja na mambo mengine ameomba radhi na kusema hakukusudia kudharau mahakama.
Rostam Aziz: Baada ya kuona tamko la chama cha majaji na mahakimu kuhusiana na kauli niliyoitoa Jumatatu iliyopita wakati nikiongea kuhusiana na uwekezaji wa kampuni yetu kule Zambia.
Nimesoma taarifa ya chama, kwasababu ya kutambua na kuheshimu dhima, hadhi na wajibu wa kikatiba wa mahakama, ningependa kusema yafuatayo
Ningependa kuuhakikishia umma kwamba wakati nikizungumzia kuhusu uwekezaji, halikuwa kusudio langu kudharau mahakama zetu. Kama nilisema hivyo ilikuwa ni kuteleza kwa ulimi maana kusudio langu lilikuwa likilenga kuhusu uwekezaji nchini na maana yangu ilikuwa ni kwamba ili tuweze kupata uwekezaji nchini mwetu hatuna budi kuendana na taratibu zinazoongoza uwekezaji Duniani.
Pia, soma=>Rostam Aziz: Hakuna mwekezaji atakubali kuwekeza halafu umwambie aende Mahakama ya Kisutu ambapo Majaji wanaweza kupigiwa simu na watu wa Serikali
Ana wachora tu hah hah, nani kama Rost TamuUjumbe umefika,hata kama kaomba radhi
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] hatariii tupuuhapo ulipo unatumia bundle yeye anamgao wake kupitia kampuni za Mitandao ya simu anayomiliki hisa nyingi sana
uki charge simu hapo anakula mgao kupitia umeme anaouza kupitia symbion ambayo zamani iliitwa Dowans kabla ya hapo iliitwa Richmond
sasa hivi anasambaza Gesi za kupikia
huyu Mdosi anasambaza zile necessity goods mwanzo mwisho
hapo staki kukupa breaking news ya matokeo ta zabuni ya kusambaza pembejeo za kilimo
ukiskia Serikali inaruhusu exports ya mazao ujue anacheka
ukiskia vibali vya kuruhusu mzigo fulani uingie bila ya kodi kupambana na Inflation mwenzio anaitikia Kidumu Chama Cha Mapinduzi
Haukumpa fidia dhidi ya udhalilishaji huo??hapo alokusudia na ndio ukweli
kuna watu walifungiwa Akaunti zao za kibiashara na hata walipokwenda kufungua kesi ma Register walikataa kusajili hizo kesi
kuna Mfanyabishara zama za mawe alichukua mkopo mkubwa Bank na wakati anaendelea na marejesho akaunti yake ikafungwa kwa maelekezo …Bank wakaendelea kumpa riba na penalt za kushindwa kulipa , jamaa akakimbilia kwny sheria kuweka zuio hata kufunguliwa tu kesi akazuiawa na hatimae akapoteza Nyumba ya dhamana
kuna Choko mmoja alikuwa ananizingua nikamchana sana akashtaki kimtaa Mtaa kuwa nithibitishe kuwa Yeye ni choko …nikawaambia tu njia za kuthibitisha hilo zinaweza pia zikaonekana kama namdhalilisha zaid …na kwa kufupisha mjadala naomba radhi kwa kuwa sipo tayari kuthibitisha sio kuwa ziwezi kuthibitisha