Rostam Aziz: Historia ya Dkt. Slaa haimpi uhalali wa kujifanya anajali maslahi ya Mtanzania. Kampuni zangu hazihusiki na uwekezaji wa DP World

Rostam Aziz: Historia ya Dkt. Slaa haimpi uhalali wa kujifanya anajali maslahi ya Mtanzania. Kampuni zangu hazihusiki na uwekezaji wa DP World

Binafsi siwezi msikiliza Dr Mihogo na Njaa zake badala yake nitamsikoliza na kumpa attention Rostam Kwa sababu kwanza ni mlipa Kodi na Mwajiri ila huyo mwingine ni njaa zinamsumbua ni WA kupuuzwa ,ameshazeeka hana jipya Kwa umri wake..
Rostam kaongelea kuhusu ufanisi wa bandari,na amesema kama kuna maboresho kwenye mkataba yafanyike

Ova
 
Ana taka kusema walio muonga ubalozi (kama anavyo sema) hawana uadilifu pia?

Je huyo mwenye kutoa huo ubalozi ni nani?

Kama ni namba moja basi ina maana ata yeye viwanda vyake anavyo dai vilifunguliwa kwa kuwa alifanya kwa uadilifu, tuanze kujiuliza maswali kuanzia hapo?

Hizi sinema za wafanya biashara kuita press zimerejea tena!

Miqka ile ndio kulikuwa na hizi mambo, huku manji kule marehemu Mengi, huku sijui nani!
 
Na wa Dr Mihogo je? Hana moral authority kunyooshea wenzake vidole. Ameasi Kanisa,ameasi familia yake na ameasi chama chake.
Kwa hiyo mtu aliyeshindwa kuhimili genye zake akaasi kanisa na kupiga mzigo akikuambia kaona nyoka ndani ya shuka kitandani kwako utampinga na kutoamini kwa vile kaasi kanisa?
Hulka binafsi hazina nafasi katika kusema ukweli wa raslimali za taifa.
Rostam ni mwizi na mjanja mjanja tuu wa raslimali za taifa.
 

Attachments

  • jesus-christ-painting-come-follow-me-by-brent-borup-pano.jpg
    jesus-christ-painting-come-follow-me-by-brent-borup-pano.jpg
    29.2 KB · Views: 3
  • 7e4102ad0c92c5950194791ec05771da.jpg
    7e4102ad0c92c5950194791ec05771da.jpg
    52.1 KB · Views: 2
  • 3b0386280d5ffee5bd15771c651cb9bb64f15577.jpg
    3b0386280d5ffee5bd15771c651cb9bb64f15577.jpg
    62.7 KB · Views: 2
Nyerere, Omari Ally Juma na wengine wengi mikono ya hawa fisi inahusika sana.
Ni kweli hakuna jambo baya lolote ambalo limetokea nchi hii zama hizi na huyu jamaa hajahusika au kufahamu mpango huo.
Nashangaa watu wa aina hii huyu Mama anajihusisha nao kwa karibu.
Ni sawa na kumtunza nyoka kwenye mfuko wa koti
 
Binafsi toka apigwe na kutupiwa nje nguo zake na Josephine Mushumbusi baada ya mama kuanza kukopa kwa kutumia Jina na Cheo cha ufirst lady na jamaa kukimbia chadema. Hana uzalendo wala hawezi sema kitu nikamsikiliza. Hata ahutubie kwa kimachame huku anajichana chana au kichina ngozi za mwili wake.
Yeye sasa ni liability na sio asset tena.
 
Haya maneno yanauma sana
Na ndio ukweli wenyewe, sisi watu weusi tunaongea sana, na wengi tunatumia mdomo kama sehemu ya kupata ajira/uteuzi.
Bora tuwasikilize hawa wenye uwezo mkubwa waliofanya vitu 'tangible' vyenye uthibitisho, na wasiotaka teuzi wala ajira, kwa kuwa walishajitosheleza na wako 'level' nyingine.​
 


Mfanyabiashara mkubwa nchini Rostam Aziz amezungumza na waandishi wa habari Juni 26, 2023 ambapo ameeleza mambo mbalimbali ikiwemo sakata la bandari ya Dar na kuhusika kwake kwenye uwekezaji huo mkubwa.

---
Juzi katika mdahalo pale hoteli ya Serena nilisema kuwa sihusiki na hili jambo (mkataba wa bandari) kibiashara. Ningekuwa nahusika nisingekuwa jasiri wa kuyasema yale niliyoyasema katika mdahalo ule.

Unapohusika na jambo huwezi kulijadili, na pia huwezi kuwa na uwezo au neutrality (hali ya kutofungamana na upande wowote) ya kuzungumzia jambo lenyewe, hivyo ningekaa pembeni na kuacha wengine wajadili.

Mimi kama Rostam na kampuni zangu hatuhusiki na uwekezaji au utakaokuwa uwekezaji wa kampuni ya DP WORLD.

Mimi ni mfanyabiashara na nimewekeza ndani na nje ya nchi, na nimetangaza jina la Tanzania kote duniani kwa kuwavutia wawekezaji waje kuwekeza katika nchi yetu ili tuweze kupata ajira na tuimarisha uchumi wetu.


Watu wanapiga porojo na ninawapa changamoto waende mahakamani. Mimi ninaaminiwa na benki za ndani na za nje ndiyo maana wananikopesha,” amesema na kuongeza “Rais (John) Magufuli asigefungua viwanda vyangu kama mimi sio mfanyabiashara halali.

Mimi sifanyi kazi na serikali, huwezi kusikia Rostam anaomba tenda serikalini au anauza hata sindano serikalini. Mimi ni mfanyabiashara ninayefanya biashara na sekta binafsi ndio maana huwezi kunituhumu kuwa nimetoa rushwa au nimekula rushwa. Hayo maneno (ya Dkt. Slaa) ni ya uropokaji tu na yasiyifanyiwa utafiti.

Historia ya Dkt. Slaa haimpi heshima wala uhalali wa kujifanya eti yeye ni mtu wa kujali maslahi ya Watanzania. Siku zote amejijali yeye binafsi na maslahi yake binafsi.

Dkt. Slaa aliacha kazi ya utumishi wa Mungu kanisani baada ya utovu wa maadili kwa kuona maisha yake ni bora zaidi kuliko utumishi wa Mungu. Historia yake ni historia ya kukosa uaminifu an uadilifu.


Dkt. Slaa hakujiunga upinzani kutokana na imani yake kwa sababu jina lake lilikatwa alipogombea kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) na sababu iliyotolewa wakati wa kukatwa jina lake ni sababu ya kukosa uadilifu alipokuwa mtumishi wa Mungu kanisani.


Huyu Bwana Dkt. Slaa anaangalia maslahi yake binafsi, hakuwa mwanachama wa CHADEMA bali alipoona jina lake limekatwa (alipogombea kupitia CCM) ndio akahamia CHADEMA

Watanzania wakumbuke kuwa, huyu mtu (Dkt. Slaa) alipokuwa CHADEMA mwaka 2015 alikisaliti chama chake wakati kukiwa kinaelekea kwenye uchaguzi, alikisaliti chama chake kwa kuhongwa, alihongwa ndipo akaasi na kukisaliti chama chake (CHADEMA). Alikaa zake pale Serena baada ya pale akapanda ndege kwenda Canada na kisha akapewa ubalozi

Kwa kifupi Dkt. Slaa hana uadilifu wala uaminifu wa kunisema, mtu ambaye hana msimamo, mbinafsi , anayeangalia maslahi yake na hajawahi kuchangia chochote katika uchumi wa nchi yetu kazi yake ni kupiga tu mdomo. Mtu wa namna hii kumjibu ni shida lakini ni lazima wakati mwingine umjibu



---

My Take
CCM na Team ya Magufuli mje na nyinyi mtujibu mlimnunua Dr. Slaa kwa bei gani



Tujiulize kwanini Chadema hawamsemi Rostam. Ukweli hakuna ushahidi wowote wa Rushwa na nawapongeza wapinzani kwa hili. Ndiyo uzui wa kuwa na wapinzani ambao nao wanajua biashara. Ukaribu wa Rostam na Raisi Samia hauna maana moja kwa moja kwamba ni Rushwa . Rostam anaweza kuwa mshauri wa Raisi bila kuwa mla rushwa! inawezekana kabisa. Tumekuwa na utamaduni wa kuropoka na kusingizia watu vitu bila kuwa na ushahidi. Dr Slaa kila mtu anajua ni mbinafsi na ni mimi mimi mimi kila wakati.
 
Fisadi papa limeguswa kunako lime kurupuka, kama hausiki si akae kimya tuu, kuanza kusema mwenzie sio muadilifu yeye ana audilifu gani au uzalendo gani 🤔🤔 nimechukua kahawa yangu nasubiria mafuriko ya majibu kutoka upande wa pili, uzuri wanajuana ngoja wavuane nguo
Nb: hadi sasa rosti tamu amesha pigwa 3:1
 
Back
Top Bottom