Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
TINA you are so beatiful, NAKUPENDA maana ni bora kuwa muwazi. Naomba contact zako niwasiliane na wewe
Boma kweli unasema haya kwenye mada nzito kama hii ? Ulishindw akutumia akili kidogo uka MP yakaishia huko badala ya kujaza nafasi na ku divert mjadala ?
Habari hii kutoka kwenye vyanzo vingine inathibitisha kuwa ni kweli.... ngoja tuifuatilie...
Habari za uhakikia kabisa ni kwamba Rostam Aziz ameanza kuhamishia mali zake nje ya nchi, sababu anahofia mambo yanavyokwenda serikalini kwa sasa. Kwa ushahidi tayari ameweka rehani hisa zake zote 35pc za Vodacom Afrika Kusini. Kabla ya kuhamishia hisa zake, alikua amenunua hisa za Planetel za mwenzake Peter Noni na mkewe, naye alifanya hivyo kuhofia mambo yanavyokwenda ofisini kwake BoT. Rostam alichukua hisa zote 35pc za Watanzania kupitia kampuni zake za Caspian na Mirambo. Nimethibitisha kwa macho yangu mwenyewe nikiwa bongo kwamba Chenge akiwa Waziri wa miundombinu alimsaidia kwa nguvu zake zote Rostam kufanikisha mkakati wake huo wa kuhamisha hisa zake nje kwa kisingizio cha kuweka rehani. Kuna watu serikalini walipinga (na wanaendelea kupinga) lakini jamaa aliwazidi kete kwa kusadiwa na Chenge na sasa inaelekea amefanikiwa kwa kiasi. Zaidi nitawaletea maana naharakisha kurejea majuu. Nitamwachia Invisible mambo yote ili siku mwafaka amwage hadharani
Jamani Sheria ya TCRA inasemaje kuhusu hisa za wazalendo? Naaambiwa inakataza wageni kumiliki hisa zaidi ya 65% lakini RA anataka kuzipeleka nje zote. Inadaiwa kwamba wanatoa kisingizio cha UFISADI alioufanya Mkapa kwa kuuza kinyemela hisa za serikali katika Mobitel (sasa TIGO) na hivyo Tigo sasa inamilikiwa kwa asilimia 100 na wageni lakini sheria inakataza. Wanajaribu kutoa tafsiri ya kisheria kupotosha kwamba eti sheria ilikua na maana na kuanzishwa tu then baadaye mzalendo anaweza kuuza popote wakitoa mfano wa TIGO walkati TIGO ni UFISADI wa Mkapa na genge lake. Sasa Chenge (akiwa Miundombinu) aliandika waraka kwa AG Mwanyika akitoa maeleekezo ya kutaka RA aachiwe auze hisa zake. AG inasemekana alikataa kabla ya kubanwa na kulegeza kamba, na baaaye Bodi ya TCRA ikagawanyika kabla ya kupitisha lakini Management hadi sasa ina maoni tofauti kuhusu uamuzi wa bodi, Inasema sawa, bodi ina uamuzi lakini si kukiuka sheria, sasa kazi ipo maana wanaandaa mabadiliko ya Sheria Ndogo (regulation) ambayo zamani ilikua Waziri anaweza kubadili tu kwa kutangaza katika gazeti la serikali (GN) lakini sasa Samuel Sitta, anaelezwa kuwa kizingiti kwa kuunda kamati ya bunge ya Sheria Ndogo ambayo sasa italazmika kupitia kwanza sheria ndogo kabla haijatangazwa katika GN. Ndio maana kulikua na mkakati maalumu wa kumng'oa Sitta ili kuruhusu hiyo regulation tena inabadilishwa kwa sababu ya mtu mmoja tu, RA. Hizo ni HABARI ZA UHAKIKA MNO!!!!!!
Habari zaidi kuhusu ufisadi wa Chenge, RA na EL tutawaleteeni soon,na kwa wale waliosikiliza Bunge leo, wafuatilie Mchango wa Mbunge mmoja mwanamke wa Chadema, anayetoka mkoani Kilimanjar, aliyeuliza fedha za Barabara ya MSata-Bagamoyo na fedha za uwanja wa Ndege wa Mwanza
Habari za uhakikia kabisa ni kwamba Rostam Aziz ameanza kuhamishia mali zake nje ya nchi, sababu anahofia mambo yanavyokwenda serikalini kwa sasa. Kwa ushahidi tayari ameweka rehani hisa zake zote 35pc za Vodacom Afrika Kusini. Kabla ya kuhamishia hisa zake, alikua amenunua hisa za Planetel za mwenzake Peter Noni na mkewe, naye alifanya hivyo kuhofia mambo yanavyokwenda ofisini kwake BoT. Rostam alichukua hisa zote 35pc za Watanzania kupitia kampuni zake za Caspian na Mirambo. Nimethibitisha kwa macho yangu mwenyewe nikiwa bongo kwamba Chenge akiwa Waziri wa miundombinu alimsaidia kwa nguvu zake zote Rostam kufanikisha mkakati wake huo wa kuhamisha hisa zake nje kwa kisingizio cha kuweka rehani. Kuna watu serikalini walipinga (na wanaendelea kupinga) lakini jamaa aliwazidi kete kwa kusadiwa na Chenge na sasa inaelekea amefanikiwa kwa kiasi. Zaidi nitawaletea maana naharakisha kurejea majuu. Nitamwachia Invisible mambo yote ili siku mwafaka amwage hadharani
dada tina mbona story yako inachanganya?hapa unatuleza kuwa rostam anahamisha mali zake,halafu unasema kuwa 'eti'Peter Noni na mkewe waliuza hisa zao kwa RA kwa kuofia mambo yanavyokwenda ofisini kwake.
unajua VODACOM ililetwa na nani hapa nchini?unajua kuwa noni aliuza hisa zake mwaka gani?kwa taharifa yako PLANETEL ndio iliyoileta VODA hapa nchini na noni aliuza hisa zake kabla jakaya hajaingia madarakani,hivyo nakushauri nenda kamuulize vizuri huyo aliyekupa hizi story