Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Naona hapa kuna one big question ambayo wengi tunai-overlook, na ni Rais wa hii Jamhuri, hivi yuko wapi na all this nonesense?

I mean huyu Rostam na wenziwe, wanachofanya sasa hivi ni kuonyesha wazi kuwa wao wana serikali yao ndani ya serikali ya Jamhuri yetu, sasa Rais wa Jamhuri anafanya nini na haya madudu? Huwezi kusema kuwa hii ni part ya demokrasia kwa sababu it is not! this is a mafia style of living.

Hawa kina Rostam wanachofanya ni kui-undermine serikali halali iliyochaguliwa kwa mujibu wa sheria zetu, Mheshimiwa Rais Kikwete, hivi kweli Tanzania tumeshuka busara za kisasa kiasi hiki? What is this? Viongozi wanaoshutumiwa kuwa ni mafisadi badala ya kufikishwa kwenye mkono wa sheria zetu za Jamhuri wanaachiwa na kutucheka wananchi kiasi hiki?

Mbunge mzima wa taifa, na mjumbe wa kamati kuu ya CCM, hawa zamani tulizoea kuwaona kwenye ishu muhimu za taifa, walikuwa wakizungumzia chakula, Kilimo, kuwahamasisha wananchi, sasa leo huyu anaita waandishi wa habari mkutano mzima kuzungumzia mipasho ya taarabu?

Mheshimiwa Rais, how low can we go kabla huja-claim tena kuwa wewe ndiye Rais wa Jamhuri yetu, maana wananchi tulikuchagua wewe sio hawa mafisadi?
 
Siku zote kama mie nikikuchagua na ukashinda inabidi ufuate matakwa yangu na ukinigeuka nina uwezo wa kukutoa kwa njia halali baada ya kipindi kuisha au kabla.

Baada ya kusema hayo nadhani utajua ni nani alimchagua MKuu wa nchi
 

FMES, nchi iliyo na Rais mambo huwa hayaendi shakalabaghala kiasi hichi! Hatuna Rais huo ndiyo ukweli wa mambo tuna mtu tu anaishi pale Ikulu lakini hana uwezo wowote wa kuchukua control ya nchi kwa kutumia mamlaka aliyopewa na katiba, badala ya walio chini yake kumuogopa na kumheshimu yeye sasa yeye ndiye anawaogopa walio chini yake. Inasikitisha sana lakini ndiyo ukweli wa mambo
 

Wakuu,

Pamoja na kwamba Rais wetu ni "mnyonge" lakini katika hili mnataka aingilie nini? Mbona haya mambo ni ya kawaida tu na wala hayaingiliani na utawala au serikali yake?

Mambo ya RA kusema bila ya kutaja wahusika, eti
.. wanatembea na watoto wadogo,
.. nimeshawahi kumpa Mtikila milioni 3,
.. mbona wakristo hutangazwa wakisaidia taasisi za kiislamu,
.. na kadhalika

haya hayaingiliani na utawala wa nchi, mpaka tumuhusishe Rais, kwa sisi haya ni malumbano ya wafanyabiashara, na kwa upande mwingine ni mpambano wa wanasiasa!

Katika hili Rais hatakiwi kufungua mdomo, anatakiwa kufungua mdomo iwapo serikali yake imeguswa, ama mmoja wa wasaidizi wake anaguswa moja kwa moja na maneno hayo ya RA! Na uzuri wa RA anazungumza bila kuweka wahusika, hata hao wahusika ni sisi (JF) ndio tunaowataja! Sasa katika hili Rais aanzie wapi?
 


FMES,

Matukio: Imagine Rostam alishangiliwa pale Kanisani, Lowassa na Chenge walipokelewa kwa kishindo majimboni mwao. CCM Mbeya walijitoa kwenye mapokezi ya Dr Mwakyembe, Anna Kilango aliandikiwa barua ya kumuonya asizungumzie Richmond bungeni etc.

Mpe nafasi JK, haya maji ni mazito kwa rais yoyote yule africa. Hawa ndio waliomuweka madarakani inambidi JK awe makini sana...akikurupuka kama wanavyokurupuka wakina RA nchi itayumba zaidi ya hivi inavyoyumba sasa.

Wananchi wetu ni maskini sana iwapo watu wameweza kuchukua over 200 USD kutoka BoT na kuweza kuchukua another Millions of $'s kutoa Richmond, Dowans, Meremeta, IPTL, Radar etc inahitaji umakini kuwashughulikia, sababu sio rahisi kujua mizizi yao imejichia chini umbali gani..!!! This is not to say JK should do nothing, rather is to say Wananchi need to do out part. Kwa maneno mengine wananchi walio wengi hawajaukataa ufisadi kwa kiwango cha kutosha..!! Ushahidi ni matukio hayo machache hapo juu.

 

I thought you/re thinking big, but you don't leave up to your name.
 

Wako ni mtizamo mmoja wa hii ishu, lakini ni kwa mtizamo mwingine hasa kwa nchi zilizoendela hii kitu ni distraction kwa watawala, kwa sababu ina-undermine the positive political message kwa wananchi, ukizingatia kuwa Rostam ni rafiki wa karibu wa Rais wa Jamhuri yetu!
 

Mkuu

Kilichosababisha haswa akina RA wakatoa tamko na kuingia na mgogoro na KKKT ni tatizo zima la UFISADI.

Nini chanzo cha Ufisadi, Je unaweza kutenganisha makampuni ya Richmond, Dowans na EPA na mengine?

Je Rais JK ameshughulika vipi na haya mambo?

Je watu wanapoanza kushutumiana na yeye akiwa ndiye kiongozi aliyekalia haya mambo yote anajisikiaje?

Je anataka nani amutaje nani wakati kiini cha matatizo yote anakifahamu?

Anyway nafikiri atakuwa either amezidiwa nguvu au nayeye ni mmoja wapo.

Lakini kadiri mambo yanavyoendelea kama mkuu wa kaya hawezi kukaa kimya.
 

Aaanzie na yule aliyetoa kauli kuwa IKULU ilisema pesa za EPA zitolewe kwani ni za USALAMA WA TAIFA.

Kama ni IKULU YAKE si kweli kwasababu ikulu yake haikuwa madarakani kwani pesa za EPA..Zilitumika kwenye uchaguzi wa kumweka yeye madarakani.

Hivyo IKULU ILIYOPITA YA AWAMU YA TATU WAULIZWE.

JK ana haki ya kufanya mapinduzi na kuwashughulikia wale waliomtega la sivyo NA YEYE ATAKWENDA NA MAJI.

Kwani ni wazi kuwa hizi kashfa hakuna namna ya kuzitetea zaidi ya ukweli kuwekwa wazi kuwa wanamtandao walimvunja meno kiongozi mkuu wa nchi na amekuwa Kibogoyo...Akitusikiliza sisi wananchi atapata meno mapya kwani tunaujuwa ukweli.

Lakini tatizo ni kama utando wa buibui na kumwondoa hapo unahitaji kuuvurugia mbali..Nasema hivyo kwani hata SINCLAIR MWENYEWE kambana JK zaidi na hivyo kazi ya Mkapa na wenzake inakuwa rahisi kama kumsukuma mlevi wa TOGWA VILE.
 
alichokifanya RA hakina tofauti na UDAKU wa magazeti!

.. wanatembea na watoto wadogo
.. wanatoa misaada misikitini wanatangazwa

sasa kweli hii issue ni political? Mnataka kila wagombanapo wafanyabiashara/ wanasiasa basi Rais aingilie!
 
alichokifanya RA hakina tofauti na UDAKU wa magazeti!

.. wanatembea na watoto wadogo
.. wanatoa misaada misikitini wanatangazwa

sasa kweli hii issue ni political? Mnataka kila wagombanapo wafanyabiashara/ wanasiasa basi Rais aingilie!

EPA,RICHMOND NA DOWANS NI ISSUE YA WAFANYABIASHARA AMBAYO RAIS HATAKIWI KUI INGILIA KWASABABU NI YA USALAMA WA TAIFA?

Hapa ni MASALHI YA TAIFA ACHA MANENO YAKO MACHAFU YA KUSEMA NI YA WAFANYA BIASHARA...AMA UMITUMWA?

Sasa issue ya usalama wa taifa asipoiamulia Rais nani mwingine mwenye uwezo huo?

Na kama hawezi...Basi ajiuzulu na ngoma ianze UPYA!
 


Kwa hiyo JK aingilie suala hili kama nani, Rais ama rafiki?

Nina uhakika RA ana marafiki wengi, tena anaowaheshimu zaidi ya Rais wetu! Sasa kwanini tuanze kufikiri kuwa ni JK pekee anayeweza kusuluhisha hili.
 

I am sick! Mkuu natanguliza heshma, mimi sielewi msingi wa uoga unaotaka Rais awe nao (tayari anao). Ingawa Mhe. Pinda alionyesha mtizamo kama huo wa kwako, lakini mimi bado hauniingii akilini vinginevyo Rais na vyombo vya dola vimekuwa dhaifu sana. Ni jambo la ajabu mafisadi kuogopwa eti wanamizizi..., wanapesa nyingi..., ni maalwatani nk. No! president should act vigorously against mafisadi soon not later, vinginevyo nchi itangawika.
 

Yametoka Wapi Hayo????????
 

Mi nakubali..TAIFA LIGAWANYWE KWASABABU KUNA WENGINE HAWATAKUBALI UPUUZI NA UNYANYASAJI HUU UINGIE KWENYE HISTORIA YETU BILA KUPINGWA!
 
Ni jambo la ajabu mafisadi kuogopwa eti wanamizizi..., wanapesa nyingi..., ni maalwatani nk. No! president should act vigorously against mafisadi soon not later, vinginevyo nchi itangawika.

May be watawala wanataka msaada wa wananchi waliowachagua.

Je huo utakuwa masaada gani wakati tayari wananchi waliwapa kura hili waweze kusimamia maswala mbali mbali kwa mujibu wa sheria tulizo nazo?

Je si waseme tu kuwa wameshindwa badala ya kukaa kimya wakati wananchi wanaona mambo si shwari?
 
Mkuu

Kilichosababisha haswa akina RA wakatoa tamko na kuingia na mgogoro na KKKT ni tatizo zima la UFISADI.

KakindoMaster,

Nakubaliana na wewe moja kwa moja!

Lakini si tunafahamu kuna kamati kwenye kila uchunguzi?
RA anahusishwa na Richmond mpaka sasa (kwa mujibu wa ripoti ya Mwakyembe) na tunasikia PM anasubiri kibali cha Spika ili kutangaza utekelezaji wake.

Sasa katika hili Rais afanye nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…