Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Huyu RA mbona hajatoa risiti zingine? Naamini pesa yake chafu ilitumika katika sana 2005. Atoe risiti zote.
 
tatizo lako JMushi1 huamini katika mawazo ya kujitegemea; unafikiri kila mtu anayetofautiana na msimamo wa "wengi" atakuwa ametumwa! Mawazo kama ya kwako hayo yanafukuza watu wengi kwenye forum hii kwa kuogopwa kuwa labelled. Jirekibishe!
 
Mwanakijiji,

1. Kuhusu Richmond na Dowans, Bunge lenu lilichunguza likasema hakuna sehemu walipoona kwamba Mh. Rostam Aziz anahusika... sasa nini kifanyike tena...

2. Mamlaka za kuchunguza zinachunguza kukiwa na hoja,,, sio kila anachosema mwanakijiji kichunguzwe... wanapoona unaongea utumbo wanakuacha na utumbo wako.

3. Mpaka sasa ni Mambo ya Umbea tu... hakuna kitu Tangible hata kimoja... umaskini wenu tu... kila mkimuona mtu tajiri mnadhani ameiba...

4. Narudia... tunaomba kuona -ushare-holding wa Rostam Aziz, kwenye hizo kampuni mnazozungumzia kama hamna... acheni mambo ya kitoto hapa!
Mjenga nchi ni mwananchi.
 
tatizo lako JMushi1 huamini katika mawazo ya kujitegemea; unafikiri kila mtu anayetofautiana na msimamo wa "wengi" atakuwa ametumwa! Mawazo kama ya kwako hayo yanafukuza watu wengi kwenye forum hii kwa kuogopwa kuwa labelled. Jirekibishe!

WEWE UNA CHAMA..NA MIMI NI HURU!

MAWAZO YA KUMTETEA ROSAMA HAYANA HOJA NA SIONI SHAKA NI LAZIMA WALE WENYE KUUTETEA UFISADI BILA HOJA WATAOGOPA!

JF INA MEMBER WA KILA AINA!

ILA INA WATU HURU PIA!

INDEPENDENT MINDED PEOPLE..WATU WASIOKUWA NA VYAMA!

WATU WASIOJALI KAMA MICHANGO YAO ITAWAUDHI CHADEMA, ccm AMA CHAMA CHOCHOTE KILE...AMA HATA ROSAMA MWENYEWE NA KIKWETE!

SI NILIFUNGIWA HAPA KWA KUMWITA JK MAFIA?

NANI ALITAKIWA KUMWOMBA MWENZAKE MSAMAHA?

Na baada ya hapo si watu walitwist na kudai nimesema damu imwagike?

Sasa nani wa kuombwa msamaha?

Wewe unaweza ukaniita jina lolote base na msimamo wangu...LAKINI NI WAZI KUWA JINA HILO LAZIMA NI "MZALENDO"

KWANI HAPA NI MASLAHI YA TAIFA...PERIOD!
 
Dada Asha,

Rule of law. Tukitaka kuwa kama usemavyo basi itakuwa ni UDIKTETA!
Tunahitaji Dikteta wakati huu kuliko kipindi chochote katika historia yetu kama taifa.
UONGOZI NI KOMBINESHENI YA MBINU NYINGI,MBAYA NA NZURI KWA MTAZAMO WA WANANCHI NA JUMUIYA YA KIMATAIFA.
 
Thanks Kitila! Asante Kasheshe!

Kitila, nashukuru kwa kumvua nguo Mtikila, huyu ni mtu mbaya sana! Na hivi majuzi alipokuja na madai kuwa RA ni raia wa Iran, nadhani alikuwa anataka kuvuta mshiko mwingine kutoka kwa RA, na wala sio kumshtaki na kusaidia taifa! Mtikila hana tofauti na Akwilombe, Tambwe Hiza! Wote hawa hupiga domo si kwa masilahi ya taifa bali tumbo zao!

Narudia tena waTanzania tunapenda sana kuongea (na udaku ndani yake) .. bila ya kuwa na vitendo! Hivi waTanzania milioni 40 hakuna hata mmoja mwenye ushahidi wa kumshtaki RA? Je wenye ushahidi wako wapi?

Mtikila anadai anamjua RA ni raia wa Iran, sasa anangoja nini kumburuza RA mahakamani? Humu JF mbona hamkujitokeza kwenye Kamati ya Mwakyembe kuelezea kuwa Richmond ni RA! Ile kamati mpaka imemaliza kazi yake, imeshindwa kujibu swali la "Richmond ni nani". Mwakyembe alilalamika sana kwenye vyombo vya habari waTanzania mnapenda sana kuongea njooni kwenye kamati kutoa ushahidi! HAKUNA MTU!!

Ndio sikatai RA anaharufu ya Ufisadi lakini huu wapi ushahidi wa moja kwa moja? Naye anajigamba mwenye ushahidi amburuze mahakamani, lakini matokeo yake waTanzania tunaendelea kulia lia "FISADI WEWE" "FISADI WEWE"! Yuko wapi "HERO" wa kumburuza RA mahakamani, ili kizazi chetu kimwekee alama ya NDIYO!

Yuko wapi "HERO" wa kuwaburuza MAFISADI mahakamani, ili kizazi chetu kimwekee alama ya NDIYO!

Wimbo wa "FISADI WEWE" "FISADI WEWE" ni mzuri lakini for the long run ulemaza na kupumbaza akili!
 
thanks Kitila! Asante Kasheshe!

Kitila, Nashukuru Kwa Kumvua Nguo Mtikila, Huyu Ni Mtu Mbaya Sana! Na Hivi Majuzi Alipokuja Na Madai Kuwa Ra Ni Raia Wa Iran, Nadhani Alikuwa Anataka Kuvuta Mshiko Mwingine Kutoka Kwa Ra, Na Wala Sio Kumshtaki Na Kusaidia Taifa! Mtikila Hana Tofauti Na Akwilombe, Tambwe Hiza! Wote Hawa Hupiga Domo Si Kwa Masilahi Ya Taifa Bali Tumbo Zao!

Narudia Tena Watanzania Tunapenda Sana Kuongea (na Udaku Ndani Yake) .. Bila Ya Kuwa Na Vitendo! Hivi Watanzania Milioni 40 Hakuna Hata Mmoja Mwenye Ushahidi Wa Kumshtaki Ra? Je Wenye Ushahidi Wako Wapi?

Mtikila Anadai Anamjua Ra Ni Raia Wa Iran, Sasa Anangoja Nini Kumburuza Ra Mahakamani? Humu Jf Mbona Hamkujitokeza Kwenye Kamati Ya Mwakyembe Kuelezea Kuwa Richmond Ni Ra! Ile Kamati Mpaka Imemaliza Kazi Yake, Imeshindwa Kujibu Swali La "richmond Ni Nani". Mwakyembe Alilalamika Sana Kwenye Vyombo Vya Habari Watanzania Mnapenda Sana Kuongea Njooni Kwenye Kamati Kutoa Ushahidi! Hakuna Mtu!!

Ndio Sikatai Ra Anaharufu Ya Ufisadi Lakini Huu Wapi Ushahidi Wa Moja Kwa Moja? Naye Anajigamba Mwenye Ushahidi Amburuze Mahakamani, Lakini Matokeo Yake Watanzania Tunaendelea Kulia Lia "fisadi Wewe" "fisadi Wewe"! Yuko Wapi "hero" Wa Kumburuza Ra Mahakamani, Ili Kizazi Chetu Kimwekee Alama Ya Ndiyo!

Yuko Wapi "hero" Wa Kuwaburuza Mafisadi Mahakamani, Ili Kizazi Chetu Kimwekee Alama Ya Ndiyo!

Wimbo Wa "fisadi Wewe" "fisadi Wewe" Ni Mzuri Lakini For The Long Run Ulemaza Na Kupumbaza Akili!

Warudi Bungeni Na Tutajuwa Nani Ni Nani Na Baada Ya Hapo Ni Mahakani!

Hatutaki Mtu Yeyote Atuambie Nani Ni Msafi...iwe Ni Kitila, kasheshe Ama Mtu Yeyote Yule.

Iwe Ni Kauli Za Kanisani Ama Hata Kempiski!
 
ROSTAM -MALASUSA-MTIKILA

Wenzangu mimi nisingependa kuingilia sana swala la Kama ROSTAM anu umiliki wa DOWANS au RICHMOND, ila ninalotaka tulijadili hapa ni kuhusu kuuli za wachungaji wetu wa type ya akina Malasusa na Mtikila ambao wamekuwa sikuzote mstari a mbelee kuwaandikia kadi za mialiko watu wenye pesa zao kwa aijili ya kuchangisha Pesa Kwa aijili ya makanisa yao!Swali linakuja hivi!Je kabla ya mialiko huwa wanaachukua kigezo gani kumualika mtu kama sio pesa zke tu?arafu hili kanisa La KKKT wao kama kanisa je wana haki ya kumhukumu mtu hata kama amepatikana na kosa?,Je kila kwaya au jumuiya yoyote ya kidini kwenye vigango wakitaka kumualika mtu wamekuwa wakiujulisha uongozi wa juu?na Je Spika Yeye sio Fisadi kwa matumizi ya ofisi yake ya bunge ambayo yameonyesha kwamba amepeleka risiti feki mara kwa mara je Malasusa hilo Halioni.
Ndugu mtikila nilishasema tangu mwanzo kwamba tumuache kwani kila mmoja wetu anamuelewa kuhusu "Up stairs" yake kwamba imejengwa kwa cement feki kama ya Maghorofa ya Ilala
Hongera ASKOFU MOKIWA.
 
kitila,

Nilishakutabiria Mambo Makubwa Kwa Muda Mrefu!!! Post Yako Ina Make Sense Sana... Ndio Maana Ni Muhimu Watu Kama Ninyi Kuja Hapa Kuandika Mapema... Ili Kutoacha Kujaziwa Kurasa Za Utumbo Na Ukanjanja.

Simply That Is It!!!

Ahadi Kwako Mkuu; 2010 Nitakuunga Mkono Ukigombea Nafasi Yoyote Mkuu... Na Kwa Chama Chochote Hata Kama Ni Mgombea Binafsi... Tuombe Mungu Ccm Na Serikali Yake Waridhie Ushauri Wa Mahakama Kuu.
Pride Goes Before Fall And Fools Rush Where Angels Fear To Tread.
 
Nduguzanguni,
Mnajadili nini wakati Bwana Mkubwa kasema mfunge midomo?! Quelle arrogance!

Mwaka 1852 Waarabu waliokuwepo nchini Tanganyika ni wale waliokuja kufanya biashara za kununua watumwa na kwenda kuwauza kwa Waarabu wengine huko kwao. Mheshimiwa Rostam asitake watu wakaanza kumkashifu bure kwa statement zake ambazo zinadhihirisha dharau kubwa aliyonayo kwa Watanzania wenziwe. Utawaambiaje watu wanaojadili jambo muhimu wafunge midomo yao eti kwa vile tu hawana ushahidi wa kupeleka jambo hilo Mahakamani? Kama aliamua kuingia kwenye siasa na kuanza kusuguana mabega na viongozi basi asichukie kujadiliwa. Anajadiliwa Mkapa aliyekuwa mkuu wa nchi, itakuwa yeye mfanyabiashara?

Jamani Mtikila pamoja na shortcomings zake ana nia njema na Taifa la Tanzania kama si Tanganyika! Kama nimeelewa nilichosoma maana ni magazeti mengi yametoa nukuu tofauti tofauti za hotuba ya Rostam, kuna mahali wanasema Rostam alimpa Mtikila masaada kama anavyofanya kwenye makanisa mengine na akaweka signature kwamba amepokea hizo pesa. Kama ilikuwa ni msaada signature ni ya nini? Ukimsaidia mtu humuombi aweke sahihi kwamba umemsaidia. Kwa hiyo, kama Mtikila aliweka sahihi basi anachosema ni kweli kwamba alikopeshwa fedha hizo na hakusaidia kama walivyosaidiwa wana Kwaya wa KKKT na wengine ambao sasa hivi wanaadhiriwa kwa kutajwa kwamba walikuwa 'ombaomba'!
 
Rostam ajikanganya

2008-07-14 09:36:06
Na Simon Mhina


Mbunge wa Igunga (CCM), Bw. Rostam Aziz, ameibuka jijini Dar es Salaam na kutoa shutuma za kujikanganya baada ya kuwageukia na kuwatuhumu baadhi ya wanasiasa na wafanyabiashara kuwa wanamuonea wivu.

Aidha, Mbunge huyo, alisema hana ugomvi na Kanisa la Kilutheri la Kiinjili Tanzania (KKKT) ila viongozi wa kanisa hilo wanatumiwa na kushinikizwa na watu hao kumkana

Bw. Rostam alikuwa akijibu taarifa ya KKKT iliyokana kumsafisha na tuhuma za ufisadi na kutaka mtu mwenye ushahidi kuwa yeye ni fisadi autoe hadharani.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Bw. Rostam, alisema taarifa ya KKKT haikutokana na matakwa ya viongozi wa kanisa hilo, bali shinikizo la watu wanaomuonea wivu kibiashara na kisiasa.

``Ili kutenda haki na kujua ukweli wa mambo, natoa changamoto kwa yeyote mwenye ushahidi wa madai ya ufisadi dhidi yangu awasilishe ushahidi huo katika vyombo vya sheria vinginevyo wafunge midomo,`` alisema.

Aidha, alisema kundi hilo limeungana na kundi lingine la wanasiasa ambao wanadhani kwamba yeye aliwakwamisha kupata nafasi fulani serikalini.

Akifafanua, Bw. Rostam alisema utajiri wake na fedha alizonazo ni \'safi\' na wala sio \'chafu\' kama ilivyoripotiwa.

Alisema fedha na biashara zake, ni matokeo ya biashara ya familia yake aliyoirithi toka vizazi kadhaa vya ukoo wao vilivyopita.

Alisema biashara anazomiliki zilianza mwaka 1852 huko Tabora na amezirithi toka kwa mababu zake.

Bw. Rostam alisema hakwenda katika kanisa hilo kujisafisha na wala hakuvamia, bali alikaribishwa.

``Nilikwenda katika sherehe hizo kwa mwaliko na wala sikujialika (kama KKKT walivyosema) siku ya sherehe, mzee wa Kanisa alikuja kunichukua nyumbani kwangu, nilipokelewa Ofisi za Kanisa nikajaza kitabu cha wageni. Nilifanya mazungumzo kadhaa na uongozi na baadaye nikapelekwa kwenye uwanja wa tukio,``alisema.

Aliwataka viongozi wa Kanisa la Kinondoni kupuuza kile alichokiita chuki, wivu na ubaguzi.

Alisema ni kweli siku za nyuma hakuwa na tabia ya kukutana na waandishi wa habari kwa vile mambo yake hataki yatangazwe na akasisitiza kuwa, mara baada ya mkutano huo wa jana, ataendelea na msimamo wake wa kutofanya mikutano kama hiyo.

Nimeona haja ya kuitisha mkutano huu kufuatia mwendelezo wa kampeni maalum ya kujaribu kunichafulia jina, hadhi na heshima yangu mbele ya jamii.

Alidai Mchungaji Christopher Mtikila pia alitumiwa na kikundi hicho kulishinikiza Kanisa kutoa taarifa ya kumkana.

Hata hivyo, alisema ameamua kujibu baadhi za hoja za Mtikila kwa vile aliligusa kanisa, vinginevyo angenyamaza kwa vile Mtikila hana hadhi ya kujibiwa na yeye (Rostam).

``Nataka niweke jambo moja wazi kwamba kama Mtikila angenituhumu mimi tu, nisingeitisha mkutano huu kwa vile hastahili heshima ya kujibiwa na mimi kilichofanya nichukue nafasi hii ni kwa vile amelitia msukosuko Kanisa ili lione kuwa limefanya dhambi kunikaribisha,`` alisema.

Bw. Rostam aliwaomba waumini wa KKKT Kinondoni wamwalike tena kwa vile hana kinyongo nao na atakwenda.

Alisema amekuwa akishirikiana na Makanisa mengine kama Moravian, Pentekoste na Katoliki.
Hata hivyo, akijibu tuhuma hizo Mchungaji Mtikila alisema ameshangazwa na madai hayo.

``Amesema alinipa milioni tatu? Kwa hiyo alinipa fedha hizo ili ninyamaze kusema kuwa yeye sio fisadi. Amenipa pointi nzuri sana, kwamba kumbe mimi siwezi kuhongwa wala kununuliwa, ninaweza kupewa milioni tatu, halafu nikabaki na msimamo wangu,`` alijigamba
 
Mtikila asituchezee akili na anachofanya anajua,hii ndio sample ya viongozi wengi serikalini..matapeli watupu!
 
JMushi1: Umekosea tena. Kuwa mwanachama wa chama cha siasa au la haina uhusiano kabisa na uhuru wa kifikra. Unaweza ukawa sio mwanachama wa chama chochote cha siasa na ukawa na utegemezi wa kutisha wa kimawazo and vice versa.

Kuna watu hapa ambao wametangaza kuwa hawana vyama vya siasa lakini ndio wategemezi wa kutisha wa mawazo. Kila waandikapo unaona jinsi wanavyojiegesha kwa mawazo ya mtu fulani, hawawezi kujitegemea. Wakisikia fulani ni fisadi na wao mbiombio kujiunga kwenye kampeni za kulaani. Wakisikia fulani ni hero kwa sababu alimshutumu mtu fulani bungeni hawachelewi kuunga behewe la kumwaga sifa. Huo ndio utegemezi wa mawazo.

Anyway, hatutachoka kukuelimisha maana wengine ndio kazi tuliosomea na inayotuweka mjini!
 
Mtikila asituchezee akili na anachofanya anajua,hii ndio sample ya viongozi wengi serikalini..matapeli watupu!

MAFISADI NA MAMLUKI WAO NDIO WASITULETEE ZA KULETA!

WARUDI BUNGENI WASILETE UPUUZI HAPA.

Hapa ni jf...Na hayumbishwi MTU!

Wengine hatutalala mpaka HAKI IPATIKANE.

Na pia narudia...JK ASIJE WASHIGTON KABLA YA MKAPA NA WENZAKE KUJIBU MASHTAKA!
 
JMushi1: Umekosea tena. Kuwa mwanachama wa chama cha siasa au la haina uhusiano kabisa na uhuru wa kifikra. Unaweza ukawa sio mwanachama wa chama chochote cha siasa na ukawa na utegemezi wa kutisha wa kimawazo and vice versa.

Kuna watu hapa ambao wametangaza kuwa hawana vyama vya siasa lakini ndio wategemezi wa kutisha wa mawazo. Kila waandikapo unaona jinsi wanavyojiegesha kwa mawazo ya mtu fulani, hawawezi kujitegemea. Wakisikia fulani ni fisadi na wao mbiombio kujiunga kwenye kampeni za kulaani. Wakisikia fulani ni hero kwa sababu alimshutumu mtu fulani bungeni hawachelewi kuunga behewe la kumwaga sifa. Huo ndio utegemezi wa mawazo.

Anyway, hatutachoka kukuelimisha maana wengine ndio kazi tuliosomea na inayotuweka mjini!

We ni mwanachama wa CHADEMA...NINA SWALI MOJA NA KAMA UKINIJIBU INAVYOTAKIWA...BASI NITAJIUNGA NA UPANDE WAKO HUO HURU WA KIFIKRA...

JE CHADEMA ILIKUMBWA NA KASHFA AMA IMEGUSWA NA KASHFA YA EPA?
Naomba jibu tafadhali...

Maana sasa tunajuwa hata ile pointi yetu ya wabunge kutangaza maslahi yao IME PREVAIL...JE NA WEWE UKO RADHI KUTANGAZA YAKO?

Je unamtetea nani?

Unajifanya kuchambuwa pointi lakini ni wazi unamtetea fisadi.

Na kama mimi napingana na wewe...Ni kwa hoja...Hivyo naomba tuanze na hilo hapo juu!
Ahsante.
 
Nduguzanguni,
Mnajadili nini wakati Bwana Mkubwa kasema mfunge midomo?! Quelle arrogance!

Mwaka 1852 Waarabu waliokuwepo nchini Tanganyika ni wale waliokuja kufanya biashara za kununua watumwa na kwenda kuwauza kwa Waarabu wengine huko kwao. Mheshimiwa Rostam asitake watu wakaanza kumkashifu bure kwa statement zake ambazo zinadhihirisha dharau kubwa aliyonayo kwa Watanzania wenziwe. Utawaambiaje watu wanaojadili jambo muhimu wafunge midomo yao eti kwa vile tu hawana ushahidi wa kupeleka jambo hilo Mahakamani? Kama aliamua kuingia kwenye siasa na kuanza kusuguana mabega na viongozi basi asichukie kujadiliwa. Anajadiliwa Mkapa aliyekuwa mkuu wa nchi, itakuwa yeye mfanyabiashara?

Jamani Mtikila pamoja na shortcomings zake ana nia njema na Taifa la Tanzania kama si Tanganyika! Kama nimeelewa nilichosoma maana ni magazeti mengi yametoa nukuu tofauti tofauti za hotuba ya Rostam, kuna mahali wanasema Rostam alimpa Mtikila masaada kama anavyofanya kwenye makanisa mengine na akaweka signature kwamba amepokea hizo pesa. Kama ilikuwa ni msaada signature ni ya nini? Ukimsaidia mtu humuombi aweke sahihi kwamba umemsaidia. Kwa hiyo, kama Mtikila aliweka sahihi basi anachosema ni kweli kwamba alikopeshwa fedha hizo na hakusaidia kama walivyosaidiwa wana Kwaya wa KKKT na wengine ambao sasa hivi wanaadhiriwa kwa kutajwa kwamba walikuwa 'ombaomba'!

Bibi Ntilie, hapa umesema kitu muhimu sana. Msaada usio na masharti hautiliwi saini. Swali moja ambalo hamtalisoma kwenye magazeti (unaweza kumsikiliza mwenyewe Rostam) ni kuhusu misaada yake kwa watu wengine, ambapo aliulizwa na mmoja wa waandishi kama anaorodha/majina ya watu wengine aliowapa misaada? Jibu lake lilikuwa ni kuwa watu hao wasiwe na wasiwasi, kwani alitoa misaada tu na hana sababu ya kuwataja.
 
Nduguzanguni,
Mnajadili nini wakati Bwana Mkubwa kasema mfunge midomo?! Quelle arrogance!

Mwaka 1852 Waarabu waliokuwepo nchini Tanganyika ni wale waliokuja kufanya biashara za kununua watumwa na kwenda kuwauza kwa Waarabu wengine huko kwao. Mheshimiwa Rostam asitake watu wakaanza kumkashifu bure kwa statement zake ambazo zinadhihirisha dharau kubwa aliyonayo kwa Watanzania wenziwe. Utawaambiaje watu wanaojadili jambo muhimu wafunge midomo yao eti kwa vile tu hawana ushahidi wa kupeleka jambo hilo Mahakamani? Kama aliamua kuingia kwenye siasa na kuanza kusuguana mabega na viongozi basi asichukie kujadiliwa. Anajadiliwa Mkapa aliyekuwa mkuu wa nchi, itakuwa yeye mfanyabiashara?

Jamani Mtikila pamoja na shortcomings zake ana nia njema na Taifa la Tanzania kama si Tanganyika! Kama nimeelewa nilichosoma maana ni magazeti mengi yametoa nukuu tofauti tofauti za hotuba ya Rostam, kuna mahali wanasema Rostam alimpa Mtikila masaada kama anavyofanya kwenye makanisa mengine na akaweka signature kwamba amepokea hizo pesa. Kama ilikuwa ni msaada signature ni ya nini? Ukimsaidia mtu humuombi aweke sahihi kwamba umemsaidia. Kwa hiyo, kama Mtikila aliweka sahihi basi anachosema ni kweli kwamba alikopeshwa fedha hizo na hakusaidia kama walivyosaidiwa wana Kwaya wa KKKT na wengine ambao sasa hivi wanaadhiriwa kwa kutajwa kwamba walikuwa 'ombaomba'!

Na Kitila...Si vizuri kufuata MIKUMBO kama ulivyosema!

Sasa mjibu Bibi Ntilie hapo juu...Maana wewe si unamtetea FISADI?

Si unadai yeye hana kosa bali ni sheria alizotunga?

Kwahiyo kinyesi kilaumiwe na aliyekunya aachwe?

HII KALI!

Na sasa Mtikila ndio toilet paper?

ama kanisa la kilutheri na misikiti?

WARUDI BUNGENI WAACHE UTANI!
 
Bibi Ntilie, hapa umesema kitu muhimu sana. Msaada usio na masharti hautiliwi saini. Swali moja ambalo hamtalisoma kwenye magazeti (unaweza kumsikiliza mwenyewe Rostam) ni kuhusu misaada yake kwa watu wengine, ambapo aliulizwa na mmoja wa waandishi kama anaorodha/majina ya watu wengine aliowapa misaada? Jibu lake lilikuwa ni kuwa watu hao wasiwe na wasiwasi, kwani alitoa misaada tu na hana sababu ya kuwataja.

Kwahiyo sasa hiyo pointi hapo juu imemaliza mchezo kwani hapo ni JK anapigwa kijembe kuwa akitaja na yeye atatajwa kama ilivyotokea kwa MTIKILA...

SASA KWANINI HATUMKAMATI SHATI AMIRI JESHI MKUU NA SASA TUNAPAMBANA NA WAZALENDO WENZETU KAMA WENGINE SI MAMLUKI WA MAFISADI!?

Nimeamini kuwa RA alizigawa na kweli kila mtu ana bei yake!
 
Hizi ni kauli za Mchungaji ambazo kwa kweli ni tata zinajichanganya alipo kuwa akiongea na waandishi wa habari walipo kuwa wanampigia cmu.

"Ni kweli niliomba fedha kwa Rostam kama mkopo, na nikaandika kwa mkono wangu maelezo kwamba nitazirejesha. Nilimueleza kibanda changu pale Mikocheni kilikuwa kimechakaa na kilihitaji marekebisho. Sikwenda kwake kuomba fedha za ujenzi wa kanisa," alisema Mtikila ambaye alidai alikuwa akijiandaa kumchukulia hatua za kisheria mwanasiasa huyo." (Gazeti la Tanzania Daima).

**********************************************
"Ni kweli, Rostam ni rafiki yangu sana, tena siku nyingi, lakini alinipa sh 3 milioni kama mkopo, si fedha za kuendeleza kanisa kama anavyosema. Muulizeni kanisa gani, mimi sijengi kanisa wala siendelezi, wapo wafadhili wa kanisa. Ni fedha za mradi wangu na ni mkopo," alisisitiza Mtikila.

Mtikila alipoulizwa tena katika mahojiano mafupi kwa njia ya simu, kwamba mkopo huo alipaswa kuurejesha kwa muda gani na ni mradi gani hasa aliufanya, alijibu tena: "Ni mradi wangu fulani hivi, muda wa kurejesha mkopo ulipaswa kuwa within two months (ndani ya mienzi miwili)",

Katika mahojiano hayo, Mtikila alipoulizwa zaidi, kwamba hadi jana miezi miwili ilipita vipi hakuweza kurejesha fedha hizo, alijibu:
"Ahaa ni kana kwamba mkopo ni mkopo tu, hata serikali bado inadaiwa na wafadhili na haijalipa hadi sasa, ila mimi nitamlipa ndani ya wiki moja hadi mbili kuanzia sasa,"

Mtikila alipoulizwa zaidi, kwamba hata kama ni mkopo, vipi alikopa fedha kwa mtu ambaye amekuwa akimuita fisadi na mwenye kumiliki fedha chafu kwa kuwa pia alipinga Rostam kutoa fedha kwa KKKT, alijibu:
"Ni kana kwamba zile fedha si chafu ni za nchi yetu, ni za serikali yetu sema tu matumizi yake na amezipataje" Gazeti la Mwananchi..



soucre;Globalpublisher
 
JE CHADEMA ILIKUMBWA NA KASHFA AMA IMEGUSWA NA KASHFA YA EPA?
Naomba jibu tafadhali...

Maana sasa tunajuwa hata ile pointi yetu ya wabunge kutangaza maslahi yao IME PREVAIL...JE NA WEWE UKO RADHI KUTANGAZA YAKO?

1) Yes, Chadema imeguswa lakini haikumbwa na kashfa za EPA

2) Swali lako la pili halieleweki, maslahi gani haya ambayo wabunge walitakiwa kutangaza? Fafanue ili ujibiwe.
 
Back
Top Bottom