Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Rostam azua mapya



Kwa upande wake, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), aliuelezea mjadala unaozingira suala hili zima kuwa usio na msingi, na ambao unapaswa kukomeshwa.

Hata hivyo, Zitto alisema Rostam alipaswa kutambua kuwa, mbegu za ubaguzi ambazo zinajionyesha leo hii katika taifa, chimbuko lake ni kundi la mtandao ndani ya CCM, ambalo mbunge huyo wa Igunga alikuwa mmoja wao.

Alisema harakati za kibaguzi zilizoendeshwa na kundi hilo la mtandao dhidi ya mwanasiasa na mwanadiplomasia Dk. Salim Ahmed Salim, wakati wa mchakato wa kumpata mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho tawala, ndiyo msingi wa vitendo vya kibaguzi leo hii.

‘‘Baadhi yetu tulipata kuonya mapema kuhusu utamaduni wa kibaguzi, uliokuwa ukiratibiwa na kundi la mtandao, ambalo Rostam ni mmoja wao, wakati wa mchakato wa kutafuta mgombea urais kwa tiketi ya CCM mwaka 2005. Tuliwaeleza mapema kabisa kwamba ipo siku mambo haya yatawarudia,” alisema Zitto mmoja wa wanasiasa wanaoheshimika nchini.

Hata hivyo, Zitto alisema alikuwa akiamini kwa dhati kuwa, kama Mtanzania, Rostam Aziz alikuwa na haki ya kualikwa na kwenda katika hafla ya Kanisa la Kiinjili ya Kilutheri.

Alisema angepata nafasi ya kumshauri Rostam kabla ya kwenda pale, angemtaka aende akashiriki katika shughuli ile na kutoa mchango wake na kuondoka pasipo kusema neno.

‘‘Kilichowastua watu wengi ni yale maneno aliyoyasema alipokuwa kanisani, na si kwenda kwake pale kwani mimi naamini kama Mtanzania alikuwa na haki ya kuitikia wito na hata ikibidi kuchangia,” alisema Zitto.

Alipoulizwa kuhusu matamshi ya Rostam kuwa kuna kundi la watu maarufu na wazito ambao wana ajenda ya kuchafua baadhi ya watu, Zitto alikuwa na haya ya kusema: ‘‘Mbona unaniuliza kitu ambacho hata wewe unakijua? Ni jambo la kweli kwamba kuna makundi, na wewe unalijua hilo. Ninachosema mimi mjadala mzima huu hauongezi tija yoyote



Yes, I couldn't have said it better. Lazima tuliangalie hili jambo katika picha kubwa. Hawa jamaa wamekuwa wakituchezea mchezo wa chesi; wanaunda kamati wakijifanya kushughulikia ufisadi kumbe wana lengo la kuchafuana na kusafishana. Damu hii ya ubaguzi inaanza kuwatafuna ndani kwa ndani na wenyewe kwa wenyewe na itawamaliza wote. Walimtafuna kiongozi wetu shupavu Salim Ahmed Salim wakijua ndio mwisho. Walisahau kwamba mchawi hawezi kuishi bila kuloga. Uzuri ni kwamba mchawi huwa halogi nje ya ukoo wake, sasa watatafuna hadi wa mwisho. Watazunguka wee mwisho wa yote watamfikia boss wao JK na uponyaji wa taifa letu ndipo utakapoanza.

Zitto hapa amekomelea msumari wa mwisho.
 
Kwa wale wanaoijua kwa undani biashara ya utumwa wanaweza kl irahisi kueleza waarabu waliokuwa katika mikoa ya Ziwa walifuata nini wakati huo.

Natamani Rostam asije kuwafanya watanzania wakakumbuka kuwa babu zake walifanya hiyo biashara. yawezekana hawakufanya. Ila maelezo yake yanaturudisha katika enzi tujnazozichukia sana.

Waarabu waliwasweka babu zetu kama ng'ombe.Wakawauza kama mifugo ya kawaida kabisa. Walitesa sana njiani. Wengi wa babu zetu walikufa njiani wakipelekwa sokoni kuuzwa. Ninashangaa hawa waarabu walikuwa na roho za aina gani?

Rostam angalia watanzania wa leo wasijeunganisha matendo yako ya sasa na yale mambo machafu waarabu waliwafanyia babu zao.

Sisemi zaidi
 
Nafikiri ni kweli sasa imefika wakati hizi kashfa za ufisadi zitolewe maamuzi yawe ya kutufurahisha au yawe yakutufadhaisha ili tuanze kuangalia mustakabali wa taifa hili katika maendeleo ya uchumi na kuondoa kero za wananchi ambazo kadri siku inapobadilika ndiyo kwanza mateso na karaha zinaongezeka kwa wananchi.

JK uko wapi uyamalize haya yanayosemwa ili wakufurahi afurahi na wakuchukia achukie kwasababu sioni kama kuna lolote kubwa litakalofanyika hapa. Ni baada ya hapo habari zitageukia kwenye mambo ya maendeleo ya nchi badala ya kusoma jina baada ya jina la fisadi yule mara huyu.Huku kila anayeandamwa kuwa fisadi akiwa anatafuta ama wa kuwaanguka naye ama mahali pa kujisafishia.

Chonde mkuu wa kaya hebu maliza haya yote ya Richmond,EPA,Deepgreen,Meremeta na mengineyo yabaki kuwa historia ili nchi ianze kusonga mbele kama nchi.2010 inakaribia tunataka tuwapime kutokana na yale mliyoahidi katika ilani ya chama chenu.
 
Huyu mchungaji nilishawaambia ni muhuni na kuna wahuni wengi sana katika hizi harakati. Uzuri ni kwamba ni swala la muda; wataambuka moja baada ya mwingine. Sasa nani atamsikiliza tena Mtikila, kwisha habari yake na hao mawakala wa ufisadi hawatamhitaji tena!


Ndugu yangu kitila kwa jinsi navyoijua mimi Tanzania huyu bwana atakuja kusikika tu na watu watakuja kumsikiliza sana tu uko mbele kama ilivyokua mwanzoni..tunasubiri mda tu upite watu wasahau ( maana ndio ugonjwa wetu mkubwa watanzania )
 
Mtikila siasa zake alishazihamishia siku nyingi mahakamani si mwanasiasa tena.Ila hili tukio la karibuni naamini litamfuta zaidi kwenye ramani.Naamini waandishi makini hawatakubali kwenda kwenye press conference zake labda kama tu watakuwa na hamu ya kucheka kwasababu Mtikila anabaki kuwa muigizaji tu kama walivyo Ze Comedy.
 
Sasa naamini kuwa Mtikila ni FISADI na aliweza kupewa fedha na Rostam kiasi cha shilingi milioni 3 ili kulipeleka gazeti la mwanahalisi mahakamani.

Siku ambayo Mtikila alilipwa ,kwa mujibu wa tarehe zilizoko kwenye vocha aliyoonyesha Rostam ndio siku hiyo hiyo alifungua kesi ya madai dhidi ya gazeti la mwanahalisi kuwa limemchafua.

Pili siku hiyo hiyo ndio siku ambayo Rostam alifungua kesi dhidi ya gazeti la mwanahalisi ya madai kuwa gazeti lilimchafua.

Kila mmoja anadai mabilioni kwenye kesi hizo.

Swali ni kwanini siku hiyo hiyo wafungue kesi wote kwa pamoja?
Kwa nini hiyo siku ndio iwe siku ya Mtikila kuchukua pesa kwa Rostam?

Namalizia kwa kusema kuwa huyu Mtikila ni fisadi.

Kwa hiyo Mtikila na Rostam wakamatwe na TAKUKURU kwa kupeana RUSHA heeeeeeeeh

Asha
 
kuna connection ya ajabu sana kati ya Mtikila, Rostam na Kagoda...! ingawa sijaweza kuipinpoint conclusively lakini kwa yeyote atakayesoma Raia Mwema kesho hatashindwa kuiona. Nilitheorize jambo fulani kuhusu Kagoda na nikaenda kuangalia ushahidi ambao nilikuwa nao at the time.. na look and behold.... Mtikila na Rostam wana connection ya ajabu sana na Kagoda!

Mwanzoni tuliposikia habari hizi hatukujua ni Kagoda...
 
kuna connection ya ajabu sana kati ya Mtikila, Rostam na Kagoda...! ingawa sijaweza kuipinpoint conclusively lakini kwa yeyote atakayesoma Raia Mwema kesho hatashindwa kuiona. Nilitheorize jambo fulani kuhusu Kagoda na nikaenda kuangalia ushahidi ambao nilikuwa nao at the time.. na look and behold.... Mtikila na Rostam wana connection ya ajabu sana na Kagoda!

Mwanzoni tuliposikia habari hizi hatukujua ni Kagoda...

I like when Mwanakijiji is trying to connceting to the dot..
 
Mtikila ni mtu wa ovyo sana! RA alikuwa sahihi kusema kuwa Mtikila hastahili kujibia na yeye, maana mtikila ni njaa inayomsumbua!

Kuhusu madai ya kutaka kumshitaki Bw. Aziz kwa madai kuwa si raia wa Tanzania, Mchungaji Mtikila alisema wapo watu ambao wameanza kuandaa mashitaka na yatafunguliwa mkoani Tabora hivi karibuni.

Ina maana katika hili yeye hayupo tena! Mtu gani anashindwa kusimamia hoja yake mpaka mwisho! Mtikila amekuwa ni mtu wa kutoa "hint" na kukimbia, na kwa stahili hii huyu hatufahi!
 
RA keshasema hagombei ubunge 2010.

Hii inaelezea nini?

Kweli anamtayarisha jamaa fulani pale wizara ya madini achukue kiti chake cha Igunga, kama vile anaitwa Kafumu
Ubaya watu wengi hawamjui na wanaodai kumjua wanasema ni kibaraka wake
 
J
ushi huu ndani hueleweki wewe ni mchezaji timu ipi wala nafasi uichezeayo, contradicting arguments na misimamo tele ambayo unaonyesha dhahiri huwezi kuisimamia.
 
Kuna haja ya kumfuatilia kwa kina na kummulika kwa kina sana ili kuweza kujua huyu jamaa.

Ila mimi namuona naye ni fisadi tuu,tufuatilie lile Benzi lake kalipata kutoka fedha gani?

Huenda kalipata kupitia fedha za EPA kwani kalinunua baada ya issue za EPA kufanyika.
 
Gembe.. hivi umewahi kujiuliza Mtikila anapata wapi habari kumhusu Rostam?
Si rafiki yake wa karibu,kama inafikia mpaka unaenda kumuomba pesa kwa jili ya kumalizia nyumba yako,umeruka watu wangapi.

Huyu ndiye alitumiwa kumaliza Sumaye,asijidai kuchimba sana,sababu hivi karibuni Sumaye atapata pa kuzungumzia...
 
Kuna haja ya kumfuatilia kwa kina na kummulika kwa kina sana ili kuweza kujua huyu jamaa.

Ila mimi namuona naye ni fisadi tuu,tufuatilie lile Benzi lake kalipata kutoka fedha gani?

Huenda kalipata kupitia fedha za EPA kwani kalinunua baada ya issue za EPA kufanyika.
Benzi navyoona yalikuwa malipo ya kumsulubu Sumaye
 
Back
Top Bottom