Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Hebu tuangalie upande mwingine kidogo:

i) Mtikila ni muhuni, ni bahati bahati mbaya kwamba uhuni wake haujulikani kwa watu wengi. Nakumbuka mwaka jana (naomba wenzangu tuliokuwa wote wanisamehe kwa kuleta hii habari hapa) tulikuwa tunataka kufungua kesi fulani kuhusu tume ya uchaguzi ikihusisha vyama vya upinzani na tukaamua kumshirikisha Mtikila. Tulipompa hili wazo alijichodai cha kwanza ni kwamba apewe sh. mi.10 (milioni kumi) ndipo atakubali kushiriki kwenye hiyo kesi. Tukaachana naye kwa sababu alitaka kugeuzi hii issue kama mtaji.

Kuna ushahidi wa kutosha pia kwamba amekuwa na tabia ya kwenda kuchukua pesa kwa watu fulani wenye matatizo ya kisiasa ili asiwaseme, na kuna habari kwamba Sumaye aliwahi kumtolea nje maombi yake ya pesa na ndiyo ikawa chanzo cha yeye kumchafua Sumaye kwa madai ambayo maskini wa Mungu yalikujua kujulikana kwamba hayakuwa na ukweli wowote, na guess what? Waliomtumia kumchafua Sumaye ni hawa akina Rostam na JK. Mimi binafsi nashukuru sana hii incidence ya Rostam kanisani imejitokeza na na inasaidia kumjua Mtikila vizuri zaidi. Ukweli ni kwamba kwa tukio hili, hata apayuke au watu wamtetee namna gani, Mtikila will never be the same; Shetani kaamua kuonyesha uchafuka wake na amechafuka hasa na sioni sabuni ya kumsafisha tena hata kama atatumia magadi!

ii) Rostam: Hajawahi kuwa mtumishi wa serikali kwa maana ya uwaziri, katibu mkuu, n.k. Kwa hiyo, technically, Rostam hajawahi kushiriki kufanya maamuzi yeyote yenye tija au athari kwa serikali. Basis ya madai ya ufisadi wa Rostam ni makampuni yake kupata tenda za serikali kwa njia ya kitapeli.

Ok, hebu tukubaliane kwa muda kwamba Rostam kajitajirisha kwa tenda za kitapeli alizozipata serikalini, swali langu linakuja, kwa nini tumlaumu yeye? Hiyo tenda alijipa au alipewa? Hizo kanuni za tenda ni yeye ndiye aliyetunga? Kwa hiyo ukichunguza kwa makini utagundua kwamba tunarusha silaha zetu kwa mtu mwingine na tunamwacha adui. Ningekuwa kwenye kamati ya Mwakyembe ningechambua kwa makini nyaraka zilizompatia tenda Rostam, kisha, kama ningegundua loop hole katika tenda, ninge-deal na hao waliotengeneza hizo tender documents na kujua kwa hakika kulikuwa na motive gani behind it. Lakini so far hatuskii hao watumishi wa serikali wakishughulishwa kwa kuingiza nchi hasara iliyotokana na uzembe, ulafi au ujinga wao katika maswala ya tenda ya Richmond na Dowans. Kwa maneno mengine kuna watu serikali wanapata easy ride na ndio maana hawawi makini na kazi zao.

In other words, kwa mara ya kwanza katika mapambano ya rushwa, mtoa rushwa (Rostam) ndiye anaonekana mbaya zaidi kuliko mpokeajii rushwa, which is, to me, a bit strange.

So, yes Rostam kashiriki kutuingiza hasara kwa tenda za kitapeli. Lakini tusisahau alichofanya Rostam ni kutumia ulafi, ujinga, uzembe na kutokujali kwa watu wetu serikalini. Mfanyabiashara yeyote atatumia loop holes za kumpa faida. Si kazi ya mfanyabiashara kuziba mianya ya rushwa na ufisadi katika serikali; hiyo ni kazi ya serikali! CCM walipoamua kukumbatia wafanyabiashara badala ya traditional followers-wakulima na wafanya kazi-walikuwa wanatengeneza the untouchables, akina Rostam. Kwa hiyo tunapomlaumu Rostam leo kwa kutajirika kifisadi utaona kwamba inasaidia nyoyo zetu kujifurahisha na kujiridhisha kwa kuwa tunapata mtu wa kutolea hasira zetu.

Kwa maana ingine, tunachokifanya hapa ni kukiri kwamba CCM hatuwawezi, wapo juu sana ya uwezo wetu wa kupambana nao; inabidi tutafute kibonde wa kumuonea, akina Rostam. Hii ni njia ya kawaida kisaikolojia inayotumiwa na wanyonge katika kujiridhisha (consolation), lakini ni njia ambayo kwa hakika haisaidi kutatua tatizo walilonalo. Kwa maana ingine, so long as tumeamua kuwalenga vibonde wetu, akina Rostam, kwa kuwa tumegundua kuwa haya majamaa ya CCM-JK na wenzake, hatuyawezi, tutaendelea kujifurahisha kwa kuwazomea akina Rostam na akina Mkapa (waliokwisha toka madarakani) lakini tutaendelea kubaki na ufisadi wetu. Of course it hurts, it really does!
 
Kitila,

Mie napenda mawazo yako sana , upo tofauti na baadhi ya wanachadema humu. Ukweli ni huo.

Ila naomba kutofautiana nawewe kidogo. Hatuna ushahidi kuwa Rostam anapatiwa Tenda isivyo halali. Kumbuka hata Richmond na Dowans hazimiliki yeye, tunajua kuwa Richmond ni ya akina GIRE, kwa hiyo yoote ya tenda ni hearsay.

Tukubaliane ndugu kuwa Rostum ni mjanja na intelligent sana. tumeshindwa kumnasa na tuhuma kibao zinazomkabili, hivyo basi tusimshutumu na kumuhukumu jamani.

La sivyo itakuwa hakuna tofauti kati ya JF na vikao vya kahawa mtaani.
 
Kitila,


Ila naomba kutofautiana nawewe kidogo. Hatuna ushahidi kuwa Rostam anapatiwa Tenda isivyo halali. Kumbuka hata Richmond na Dowans hazimiliki yeye, tunajua kuwa Richmond ni ya akina GIRE, kwa hiyo yoote ya tenda ni hearsay.

Ndiyo maana nikasema kwamba tufanye kama ni kweli (assumption). Bahati mbaya kamati ya Mwakyembe ilishindwa pia kuthibitisha mmiliki wa Richmond na Dowans. Terribe, isn't it?
 
Hebu tuangalie upande mwingine kidogo:

i) Mtikila ni muhuni, ni bahati bahati mbaya kwamba uhuni wake haujulikani kwa watu wengi. Nakumbuka mwaka jana (naomba wenzangu tuliokuwa wote wanisamehe kwa kuleta hii habari hapa) tulikuwa tunataka kufungua kesi fulani kuhusu tume ya uchaguzi ikihusisha vyama vya upinzani na tukaamua kumshirikisha Mtikila. Tulipompa hili wazo alijichodai cha kwanza ni kwamba apewe sh. mi.10 (milioni kumi) ndipo atakubali kushiriki kwenye hiyo kesi. Tukaachana naye kwa sababu alitaka kugeuzi hii issue kama mtaji.

Kuna ushahidi wa kutosha pia kwamba amekuwa na tabia ya kwenda kuchukua pesa kwa watu fulani wenye matatizo ya kisiasa ili asiwaseme, na kuna habari kwamba Sumaye aliwahi kumtolea nje maombi yake ya pesa na ndiyo ikawa chanzo cha yeye kumchafua Sumaye kwa madai ambayo maskini wa Mungu yalikujua kujulikana kwamba hayakuwa na ukweli wowote, na guess what? Waliomtumia kumchafua Sumaye ni hawa akina Rostam na JK. Mimi binafsi nashukuru sana hii incidence ya Rostam kanisani imejitokeza na na inasaidia kumjua Mtikila vizuri zaidi. Ukweli ni kwamba kwa tukio hili, hata apayuke au watu wamtetee namna gani, Mtikila will never be the same; Shetani kaamua kuonyesha uchafuka wake na amechafuka hasa na sioni sabuni ya kumsafisha tena hata kama atatumia magadi!

ii) Rostam: Hajawahi kuwa mtumishi wa serikali kwa maana ya uwaziri, katibu mkuu, n.k. Kwa hiyo, technically, Rostam hajawahi kushiriki kufanya maamuzi yeyote yenye tija au athari kwa serikali. Basis ya madai ya ufisadi wa Rostam ni makampuni yake kupata tenda za serikali kwa njia ya kitapeli.

Ok, hebu tukubaliane kwa muda kwamba Rostam kajitajirisha kwa tenda za kitapeli alizozipata serikalini, swali langu linakuja, kwa nini tumlaumu yeye? Hiyo tenda alijipa au alipewa? Hizo kanuni za tenda ni yeye ndiye aliyetunga? Kwa hiyo ukichunguza kwa makini utagundua kwamba tunarusha silaha zetu kwa mtu mwingine na tunamwacha adui. Ningekuwa kwenye kamati ya Mwakyembe ningechambua kwa makini nyaraka zilizompatia tenda Rostam, kisha, kama ningegundua loop hole katika tenda, ninge-deal na hao waliotengeneza hizo tender documents na kujua kwa hakika kulikuwa na motive gani behind it. Lakini so far hatuskii hao watumishi wa serikali wakishughulishwa kwa kuingiza nchi hasara iliyotokana na uzembe, ulafi au ujinga wao katika maswala ya tenda ya Richmond na Dowans. Kwa maneno mengine kuna watu serikali wanapata easy ride na ndio maana hawawi makini na kazi zao.

In other words, kwa mara ya kwanza katika mapambano ya rushwa, mtoa rushwa (Rostam) ndiye anaonekana mbaya zaidi kuliko mpokeajii rushwa, which is, to me, a bit strange.

So, yes Rostam kashiriki kutuingiza hasara kwa tenda za kitapeli. Lakini tusisahau alichofanya Rostam ni kutumia ulafi, ujinga, uzembe na kutokujali kwa watu wetu serikalini. Mfanyabiashara yeyote atatumia loop holes za kumpa faida. Si kazi ya mfanyabiashara kuziba mianya ya rushwa na ufisadi katika serikali; hiyo ni kazi ya serikali! CCM walipoamua kukumbatia wafanyabiashara badala ya traditional followers-wakulima na wafanya kazi-walikuwa wanatengeneza the untouchables, akina Rostam. Kwa hiyo tunapomlaumu Rostam leo kwa kutajirika kifisadi utaona kwamba inasaidia nyoyo zetu kujifurahisha na kujiridhisha kwa kuwa tunapata mtu wa kutolea hasira zetu.

Kwa maana ingine, tunachokifanya hapa ni kukiri kwamba CCM hatuwawezi, wapo juu sana ya uwezo wetu wa kupambana nao; inabidi tutafute kibonde wa kumuonea, akina Rostam. Hii ni njia ya kawaida kisaikolojia inayotumiwa na wanyonge katika kujiridhisha (consolation), lakini ni njia ambayo kwa hakika haisaidi kutatua tatizo walilonalo. Kwa maana ingine, so long as tumeamua kuwalenga vibonde wetu, akina Rostam, kwa kuwa tumegundua kuwa haya majamaa ya CCM-JK na wenzake, hatuyawezi, tutaendelea kujifurahisha kwa kuwazomea akina Rostam na akina Mkapa (waliokwisha toka madarakani) lakini tutaendelea kubaki na ufisadi wetu. Of course it hurts, it really does!

MWL Kitila
ume make point moja matata sana ya kwamba Mfanya biashara azibe loopholes zinazoweza kumwingizia kipato Hii kali sana.
 
ROSTAM -MALASUSA-MTIKILA

Wenzangu mimi nisingependa kuingilia sana swala la Kama ROSTAM anu umiliki wa DOWANS au RICHMOND, ila ninalotaka tulijadili hapa ni kuhusu kuuli za wachungaji wetu wa type ya akina Malasusa na Mtikila ambao wamekuwa sikuzote mstari a mbelee kuwaandikia kadi za mialiko watu wenye pesa zao kwa aijili ya kuchangisha Pesa Kwa aijili ya makanisa yao!Swali linakuja hivi!Je kabla ya mialiko huwa wanaachukua kigezo gani kumualika mtu kama sio pesa zke tu?arafu hili kanisa La KKKT wao kama kanisa je wana haki ya kumhukumu mtu hata kama amepatikana na kosa?,Je kila kwaya au jumuiya yoyote ya kidini kwenye vigango wakitaka kumualika mtu wamekuwa wakiujulisha uongozi wa juu?na Je Spika Yeye sio Fisadi kwa matumizi ya ofisi yake ya bunge ambayo yameonyesha kwamba amepeleka risiti feki mara kwa mara je Malasusa hilo Halioni.
Ndugu mtikila nilishasema tangu mwanzo kwamba tumuache kwani kila mmoja wetu anamuelewa kuhusu "Up stairs" yake kwamba imejengwa kwa cement feki kama ya Maghorofa ya Ilala
 
Kitila,

Nilishakutabiria mambo makubwa kwa muda mrefu!!! Post yako ina make sense sana... Ndio maana ni muhimu watu kama ninyi kuja hapa kuandika mapema... ili kutoacha kujaziwa kurasa za utumbo na ukanjanja.

Simply that is it!!!

Ahadi kwako mkuu; 2010 nitakuunga mkono ukigombea nafasi yoyote mkuu... na kwa chama chochote hata kama ni mgombea binafsi... tuombe Mungu CCM na Serikali yake waridhie ushauri wa Mahakama Kuu.
 
ROSTAM -MALASUSA-MTIKILA

Wenzangu mimi nisingependa kuingilia sana swala la Kama ROSTAM anu umiliki wa DOWANS au RICHMOND, ila ninalotaka tulijadili hapa ni kuhusu kuuli za wachungaji wetu wa type ya akina Malasusa na Mtikila ambao wamekuwa sikuzote mstari a mbelee kuwaandikia kadi za mialiko watu wenye pesa zao kwa aijili ya kuchangisha Pesa Kwa aijili ya makanisa yao!Swali linakuja hivi!Je kabla ya mialiko huwa wanaachukua kigezo gani kumualika mtu kama sio pesa zke tu?arafu hili kanisa La KKKT wao kama kanisa je wana haki ya kumhukumu mtu hata kama amepatikana na kosa?,Je kila kwaya au jumuiya yoyote ya kidini kwenye vigango wakitaka kumualika mtu wamekuwa wakiujulisha uongozi wa juu?na Je Spika Yeye sio Fisadi kwa matumizi ya ofisi yake ya bunge ambayo yameonyesha kwamba amepeleka risiti feki mara kwa mara je Malasusa hilo Halioni.
Ndugu mtikila nilishasema tangu mwanzo kwamba tumuache kwani kila mmoja wetu anamuelewa kuhusu "Up stairs" yake kwamba imejengwa kwa cement feki kama ya Maghorofa ya Ilala
Kwenye hili nilishasema kwamba kanisa lilikurupuka period!
 
RA ni mwanasiasa, ni mwakilishi wa wananchi bungeni, ashashika dhamana ya uweka hazina katika chama cha wakulima na wafanyakazi(ccm). pia ni mwananchi ambaye anajukumu la kulinda sheria za jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama ilivyo mimi na wewe. mtu akitumia njia za udanganyifu kwa kushirikiana na mafisadi kuwahujumu watanzania halafu useme kwa sababu mtu huyo hana dhamana ya uongozi serikalini hivyo basi asiguswe na makombora ya wananchi, mimi ninadhani hiyo ni argument ya ajabu, HOJA YAKO BWANA KITILA NADHANI INGEKUWA BALANCED ZAIDI KAMA USINGEM"EXCLUDE" R.A KATIKA WATU WANAOTAKIWA KUSHUKIWA NA GHADHABU YA MTANZANIA IWAPO KWELI AMESHIRIKAINA NA MAFISADI , MIMI KWA MAONI YANGU NINAONA KWAMBA MTU YEYOTE PASIPO KUJALI NAFASI YAKE KATIKA JAMII, IWAPO WANASHIRIKIANA KUIHUJUMU JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA WATU WAKE, BASI WOTE NI WA KULAUMIWA NA GHADHABU YA WANANCHI HAINA BUDI KUWASHUKIA WOTE PASI NA KUMUONEA ASIYEHUSIKA.

bw Kitila hapa tunazungumzia haki na wajibu wa raia katika Taifa, nini nafasi ya raia katika kuilinda kuijenga Tanzania, je Raia ambaye ni mfanya biashara anayeshirikiana na viongozi wa serikali kuihujumu nchi huyo raia kweli asilaumiwe na wananchi wenziwe eti kwa sababu siyo kiongozi?.

tunaona jinsi wananchi wanavyowashughulikia wezi mitaani, hii inamaanisha kwamba wananchi wana hasira za ajabu dhidi ya wezi. sasa vipi kuhusu wale wanaoshirikiana na wenye dhamana serikalini kukwapua Mali ya wananchi?, unadhani kweli wananchi watakaa kimya?.

namalizia kwa kusema kwamba, Wote, viongozi serikalini na raia hawatakiwi kulihujumu Taifa, wakifanya hivyo wananchi watawakemea wote,na bila shaka ni haki ya wananchi kufanya hivyo.
 
MWL Kitila
ume make point moja matata sana ya kwamba Mfanya biashara azibe loopholes zinazoweza kumwingizia kipato Hii kali sana.

Ndio nasema hilo haliwezekani Ni kazi ya serikali kutengeneza mazingira mwafaka kwa sekta binafsi na wafanyabiashara kufanya biashara zao na wakati huohuo kuhakikisha kwamba inaziba mianya yoyote, kwa njia ya sheria, kanuni, n.k., ya kuliingiza hasara taifa na kupoteza mapato halali kwa njia ya kodi. Inavyoonekana ni kama vile tulitaka Rostam asitumie mianya iliyokuwepo na ambayo ipo ya kumfanya apate faida haraka na kubwa, I bet hili haliwezekani kwa mfanyabiashara yeyote, simply because hiyo sio kazi yake!

CCM walipoamua kuwakumbatia wafanyabiashara waliamua pia kukumbatia utapeli na ujanjaujanja wa wafanyabiashara kama akina Rostam. Rostam anasema wazazi wake walianza biashara tangu 1852, sasa cha kujiuliza ni kwa nini yeye amejulikana kuanzia kipindi cha wakati wa Mwinyi na kushamirisha biashara zake kipindi cha kampeni za urais wa 2005? Ni kwamba huko nyuma hapakuwa na loop holes za kijinga kama zilivyo sasa.

Tuache kuwa simplistic because simplicity is the enemy of truth. Hatuwezi kuishinda vita ya ufisadi kwa kuwashambulia mawakala wa ufisadi; ifike mahala tuamue ama kuwashambulia wazalisha ufisadi CCM au kama, hatuwawezi, tukae kimya na tukubaliane kwamba hayo ndiyo maisha yetu!
 
Hawa takukuru mbona hawajakamata watu wa richmond na Dowans waliokuwa wakikinga pesa kwa kutumia makampuni ya mfukoni?

Au kuna takukuru ni kwa ajiri ya rushwa ndogo za traffic, waiba miwa, nk?

anyway kazi nzuri.



Mbona inaeleweka TAKUKURU ni kwa ajiri ya kada za chini tu. Wakubwa wa serikali - MAFISADI HALISI wanaokula mabilioni TAKUKURU inawaogopa kama moto wa mafuta
 
Gamba la Nyoka: Tupo pamoja kabisa. Ni kweli kabisa kila raia, akiwemo Rostam, anawajibika kuheshimu na kulinda sheria za nchi. Lakini ambacho unashindwa kukipata hapa ni kwamba tatizo letu, hasa hili la ufisadi, sio kwamba watu wanavunja sheria. Tatizo ni kwamba tuna sheria, kanuni na taratibu ambazo zinatoa mwanya kwa watu kufanya utapeli na wizi. Kwa maana ingine sheria zetu zinalinda utapeli na wizi.

Kwa mfano, hatuumii leo kwa sababu watu walivunja sheria katika kujipatia mkataba wa IPTL, isipokuwa ni kwamba watu walitengeneza huo mkataba ili uwe kama vile ulivyo. Vivyo hivyo, kinachogomba hapa kwenye swala la Richmond na Dowans sio kwamba kuna watu walivunja sheria au kanuni, isipokuwa kuna watu serikalini walitengeneza mkataba ili uwe vile ulivyokuwa. Hakuna mtu aliyevunja sheria kuhusu kuongeza mkataba wa TICTIS (sijui ndio hivyo inaandikwa) kule bandarani hadi kuwa miaka 25, isipokuwa kuna watu katika serikali yetu walitengeneza huo mkataba uwe vile. Sasa wewe ungekuwa mfanyabiashara ukaambiwa tunakupa mkataba wa miaka 25 ungekataa? Au wewe ungekuwa ndiyo kampuni ya IPTL ungekataa kukubali mkataba mnono kama ule? Wewe ingekuwa ndiyo wewe unapewa kuendesha KIA kwa dola 1000 kwa mwaka ungekataa? Ingekuwa wewe ndiyo mfanyabiashara unaambiwa tuletee umeme tutakulipa sh. mil 152 kwa mwezi hata baada ya kazi kwisha ungekataa?

Nadhani unaipata hoja yangu. Ninachokataa mimi ni kuwalaumu watu wanaotumia udhaifu, ujinga na ulafi wa watu serikalini katika kujinufaisha kibiashara kwa sababu hatuwi wa kweli. Ninakataa pia tabia ambayo inaibuka ya kushambulia mawakala wa ufisadi bila kuwashambulia wafisadi wenyewe. Kwa mfano katika swala la Richmond, tunajua jinsi ambavyo JK alilishikia bango na kulitetea kwa nguvu zake zote na kutuhakikishia kwamba hiyo ni kampuni imara sana. Sasa ilikuwaje kamati ya Mwakyembe haikukiona hili? Na inakuwaje sisi tunambebea bango Rostam na kumwacha JK? Kwa nini JK amekuwa aki-take an easy ride kwenye sakata la ufisadi wakati yupo katikati?
 
Ndio nasema hilo haliwezekani Ni kazi ya serikali kutengeneza mazingira mwafaka kwa sekta binafsi na wafanyabiashara kufanya biashara zao na wakati huohuo kuhakikisha kwamba inaziba mianya yoyote, kwa njia ya sheria, kanuni, n.k., ya kuliingiza hasara taifa na kupoteza mapato halali kwa njia ya kodi. Inavyoonekana ni kama vile tulitaka Rostam asitumie mianya iliyokuwepo na ambayo ipo ya kumfanya apate faida haraka na kubwa, I bet hili haliwezekani kwa mfanyabiashara yeyote, simply because hiyo sio kazi yake!

CCM walipoamua kuwakumbatia wafanyabiashara waliamua pia kukumbatia utapeli na ujanjaujanja wa wafanyabiashara kama akina Rostam. Rostam anasema wazazi wake walianza biashara tangu 1852, sasa cha kujiuliza ni kwa nini yeye amejulikana kuanzia kipindi cha wakati wa Mwinyi na kushamirisha biashara zake kipindi cha kampeni za urais wa 2005? Ni kwamba huko nyuma hapakuwa na loop holes za kijinga kama zilivyo sasa.

Tuache kuwa simplistic because simplicity is the enemy of truth. Hatuwezi kuishinda vita ya ufisadi kwa kuwashambulia mawakala wa ufisadi; ifike mahala tuamue ama kuwashambulia wazalisha ufisadi CCM au kama, hatuwawezi, tukae kimya na tukubaliane kwamba hayo ndiyo maisha yetu!

Kitila nakubaliana nawewe 100%
Hakuna mfanya biashara yoyote duniani ambaye anaweza kukuambia rekebisha ktk sera zako hizo maana zinaonekana kunipendelea mimi mfanya biashara na zitanipatia faida kubwa.

Ukweli tunao takiwa kuupigia mayowe ,makele ya hali ya juu ni Sheria zetu pamoja na katiba ni legelege .

Nabahati ya Kahama mining, Geita mining ,Buzwag,Tarime mining,Nzega mining,mwadui ni kwamba wao hawakuzaliwa Igunga-Tanzania.

Sheria zetu nyingi ni Butu ambazo wajanja zinawapa haki ya kisheria kuingia Tenda na Mikataba butu ,Na matokeo yake wanakua na haki kisheria kumliki na ndio maana mwisho hatuwezi kuwafanya chochote zaidi ya kuwabembeleza.

Pengine ni sheria zetu ndizo zinawatia kishawishini viongozi nao kujiingiza ktk biashara hizo.
Na nafikiri sheria zinatungwa na wananchi kwa kupitia wabunge wao.
 
ROSTAM -MALASUSA-MTIKILA

Wenzangu mimi nisingependa kuingilia sana swala la Kama ROSTAM anu umiliki wa DOWANS au RICHMOND, ila ninalotaka tulijadili hapa ni kuhusu kuuli za wachungaji wetu wa type ya akina Malasusa na Mtikila ambao wamekuwa sikuzote mstari a mbelee kuwaandikia kadi za mialiko watu wenye pesa zao kwa aijili ya kuchangisha Pesa Kwa aijili ya makanisa yao!Swali linakuja hivi!Je kabla ya mialiko huwa wanaachukua kigezo gani kumualika mtu kama sio pesa zke tu?arafu hili kanisa La KKKT wao kama kanisa je wana haki ya kumhukumu mtu hata kama amepatikana na kosa?,Je kila kwaya au jumuiya yoyote ya kidini kwenye vigango wakitaka kumualika mtu wamekuwa wakiujulisha uongozi wa juu?na Je Spika Yeye sio Fisadi kwa matumizi ya ofisi yake ya bunge ambayo yameonyesha kwamba amepeleka risiti feki mara kwa mara je Malasusa hilo Halioni.
Ndugu mtikila nilishasema tangu mwanzo kwamba tumuache kwani kila mmoja wetu anamuelewa kuhusu "Up stairs" yake kwamba imejengwa kwa cement feki kama ya Maghorofa ya Ilala


I agree man, I posted article Rostam vs Kikwete katika-Jukwaa la kisiasa. many questions on this issue.
 
Yani we Mkumbo unataka watu wafuate Mkumbo kwa kauli zako hizo za kimkumbo mkumbo zinazoleta na kupelekea KASHESHE juu ya Kasheshe...Kwani naona hata ccm mafiasadi wanakukubali.

Kuna watu wamewatuma kuwa sasa kina RA hawana makosa simply kwasababu ni ya system,na sheria mbovu eti walizozitumia?

Mmejidanganya...Mnasahau kanuni moja kubwa ya UTAWALA...ACCOUNTABILITY!

Sasa kama wewe Kitila ndio mwalimu na wewe ni lecturer..Basi sishangai kwa kukuta kizazi nilichokikuta bongo na pia sishangai kuwa UFISADI NI SIFA HATA KWA VIJANA!

Kitila UMECHEMMSHA NA SASA NAONA UNAPULIZA PULIZA TU na kina YEBO YEBO WALIOFUNGUWA MATAWI HUKO UINGEREZA NA SASA WAKO HUKO NA WATOTO WA VIGOGO WANAKULA RAHA!

KICHEFU CHEFU!
 
jmushi, kama unashindwa kujibu hoja ni vizuri usijibu hoja, hizo ad hominem zao zimeanza kuchosha hapa.
 
Inaudhi kuona mtu anayejulikana kuwa ni kiongozi wa CHADEMA ANAMTETEA ROSTAM!

Hapo nani HANA HOJA?

Huu mjadala tushachangia na sasa tunaendelea na mijadala mingine..

Lakini unapo pop up ni lazima turudi kutetea hoja.

Na mimi kusema kufuata "MKUMBO" NI "KASHESHE" ZA "KIYEBO YEBO" NI KUKOSA HOJA?

Mimi kusema UWAJIBIKAJI NI MUHIMU NI KUKOSA HOJA???

Ama ni yule aliyesema kuwa RA na wafanyabiashara wengine wasilaumiwe kwa sababu eti walizitumia sheria MBOVU...?!

Gimme A BREAK GUYS!!!!1
 
Kimya kingi kina mshindo mkuu! Baada ya kimya cha muda mrefu nahisi Mkuu atarudi tena kwenye jukwaa la kila mwisho wa mwezi kuteta na Taifa kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya. Najiaminisha kuwa safari hii Muungwana atakuwa na ripoti zote nyeti kibindoni hivyo ataunguruma kuliko hao kina Raiasi,Siridiklea na Mtukula!Na aungurumapo simba mcheza nani?
 
Huyu fisadi RA kudai anafanya biashara safi na pesa zake ni safi huku akijua kuwa ni FISADI. Kama hapo ndio kufanya biashara safi, siku akianza kufanya ufisadi Tanzania itakuwa wapi!!! DO MATHS.
 
Kimya kingi kina mshindo mkuu! Baada ya kimya cha muda mrefu nahisi Mkuu atarudi tena kwenye jukwaa la kila mwisho wa mwezi kuteta na Taifa kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya. Najiaminisha kuwa safari hii Muungwana atakuwa na ripoti zote nyeti kibindoni hivyo ataunguruma kuliko hao kina Raiasi,Siridiklea na Mtukula!Na aungurumapo simba mcheza nani?

He better do that!

Na ni better awe SIMBA MNGURUMAJI MWENYE KULINDA BINADAMU NA SI KUWATAFUNA!

Kama anataka kuunguruma..Basi afanye FASTER kwani RA NDIYE ANAYENGURUMA KWASASA NA MKAPA NDIYE RAIS WA TANZANIA HUKU ROLE YA JK IKIWA NI UWAZIRI WA MAMBO YA NJE ULIOVIKWA KOFIA YA UENYEKITI WA AU!

Sasa si mambo ya ZIMBABWE TENA!

Hiyo vita RABBITS SISI TUMESHASHINDA NA HIVYO HIYO KAULI YAKO YA SIGNATURE KUHUSU MFANO WA MWALIMU HAIKUZIGATIA KUWA USHINDI UNATOKANA NA NIA NA RESOLVE YA WAZALENDO!

Tunamsubiri hapa WASHINGTON MWEZI UJAO!

ILA KABLA HAJAJA HAPA NI LAZIMA AONYESHE KUWA USIMBA WAKE NI WA ARFRIKA NA SI SIMBA KANYABOYA, MZEE AMA KIBOGOYO!

KUWA YEYE SI SIMBA WA KITSIVANGIRAI TSIVANGIRAI!
 
Back
Top Bottom