The Sunk Cost Fallacy 2
JF-Expert Member
- Nov 8, 2022
- 9,436
- 10,944
Nakubalina na Rostam Aziz, Wawekezaji wa Nje waje ku compliment pale ambapo Wawekezaji wa Ndani wamekwama tena Kwa Ubia.
Sasa taasisi zetu zikisia uwekezaji wao wanaweza Wazungu na hata Sasa wako busy kutafuna posho Kwa visingizio vya kuandaa majukwaa ya uwekezaji na mataifa ya Nje.
Wanapishana angani Nchi na Nchi eti kutafuta wawekezaji. Mbona hatujawahi waona Mikoani wakihamasisha huo uwekezaji Kwa wazawa? Au nyie mtuambie ni lini Investment promotion agencies za Nchi zingine Huwa zinakuja Tanzania eti kutafuta wawekezaji?
Hii mentality ya kijinga ikomeshwe mara Moja,ni lazima Serikali ijielekeze kuwezesha wazawa Kwa namna yeyote Ile.Mfani nimeona Tarura wameanzisha Samia infrastructure Bond kusaidia Wakandarasi.Taasisi zingine wanafanya nini?
Hongera bwana Rostam Kwa kuwapa shule Hawa watu wetu wasiojielewa.👇👇
View: https://youtu.be/fzFNcqqzYrw?si=WTtRcYkKL2o8DU6p
----
Mfanyabiashara na mwekezaji, Rostam Aziz amesema kuna umuhimu wa kuwakumbatia wawekezaji wa ndani katika utekelezaji wa miradi ya ndani ili kujenga uchumi wa nchi.
Rostam ameyasema hayo leo Alhamisi, Desemba 5, 2024 kwenye mjadala ulioandaliwa na Clouds Media Group unaoongelea namna Serikali imefanya uwezeshaji kwa wawekezaji wazawa. Amesema mwekezaji kutoka nje anachoangalia ni biashara na faida ya haraka kisha aangalie fursa iliyoko nchi nyingine.
“Mfanyabiashara kutoka nje akija anafanya shughuli iliyomleta kwa kutazama faida, anakuja na watu wake anaowaamini kuwapa ajira na faida atakayoipata atawekeza huko alikotoka au sehemu anayotaka kwenda kuwekeza,” amesema Rostam.
Ameshauri kwamba miradi mikubwa ya nchi kama ujenzi wa barabara, madaraja na miundombinu mbalimbali wapewe wazawa waitekeleze ili kuzungusha pesa ndani ya nchi ambapo biashara zitazaana.
Amesisitiza hakuna nchi dunani iliyojenga uchumi wake kwa kutegemea wawekezaji kutoka nje kwakuwa wawekezaji kutoka nje wanachoangalia ni masilahi yake hadi anakuja nchini lazima ahakikishe faida yake inakua kubwa na siku akimaliza anaondoka.
“Serikali ijiwekeze katika kupendelea wawekezaji wa ndani ndio wawe na matumizi makubwa wa pesa za Serikali za miradi kwasababu ikibaki nchini watanzania wengi watanufaika. Kodi zitalipwa biashara zitazunguka,” amesema Rostam.
View: https://www.instagram.com/reel/DDMK6Asqp20/?igsh=MnFmdDYzZmN0ZWp3
Chanzo: Mwananchi
Sasa taasisi zetu zikisia uwekezaji wao wanaweza Wazungu na hata Sasa wako busy kutafuna posho Kwa visingizio vya kuandaa majukwaa ya uwekezaji na mataifa ya Nje.
Wanapishana angani Nchi na Nchi eti kutafuta wawekezaji. Mbona hatujawahi waona Mikoani wakihamasisha huo uwekezaji Kwa wazawa? Au nyie mtuambie ni lini Investment promotion agencies za Nchi zingine Huwa zinakuja Tanzania eti kutafuta wawekezaji?
Hii mentality ya kijinga ikomeshwe mara Moja,ni lazima Serikali ijielekeze kuwezesha wazawa Kwa namna yeyote Ile.Mfani nimeona Tarura wameanzisha Samia infrastructure Bond kusaidia Wakandarasi.Taasisi zingine wanafanya nini?
Hongera bwana Rostam Kwa kuwapa shule Hawa watu wetu wasiojielewa.👇👇
View: https://youtu.be/fzFNcqqzYrw?si=WTtRcYkKL2o8DU6p
----
Mfanyabiashara na mwekezaji, Rostam Aziz amesema kuna umuhimu wa kuwakumbatia wawekezaji wa ndani katika utekelezaji wa miradi ya ndani ili kujenga uchumi wa nchi.
Rostam ameyasema hayo leo Alhamisi, Desemba 5, 2024 kwenye mjadala ulioandaliwa na Clouds Media Group unaoongelea namna Serikali imefanya uwezeshaji kwa wawekezaji wazawa. Amesema mwekezaji kutoka nje anachoangalia ni biashara na faida ya haraka kisha aangalie fursa iliyoko nchi nyingine.
“Mfanyabiashara kutoka nje akija anafanya shughuli iliyomleta kwa kutazama faida, anakuja na watu wake anaowaamini kuwapa ajira na faida atakayoipata atawekeza huko alikotoka au sehemu anayotaka kwenda kuwekeza,” amesema Rostam.
Ameshauri kwamba miradi mikubwa ya nchi kama ujenzi wa barabara, madaraja na miundombinu mbalimbali wapewe wazawa waitekeleze ili kuzungusha pesa ndani ya nchi ambapo biashara zitazaana.
Amesisitiza hakuna nchi dunani iliyojenga uchumi wake kwa kutegemea wawekezaji kutoka nje kwakuwa wawekezaji kutoka nje wanachoangalia ni masilahi yake hadi anakuja nchini lazima ahakikishe faida yake inakua kubwa na siku akimaliza anaondoka.
“Serikali ijiwekeze katika kupendelea wawekezaji wa ndani ndio wawe na matumizi makubwa wa pesa za Serikali za miradi kwasababu ikibaki nchini watanzania wengi watanufaika. Kodi zitalipwa biashara zitazunguka,” amesema Rostam.
View: https://www.instagram.com/reel/DDMK6Asqp20/?igsh=MnFmdDYzZmN0ZWp3
Chanzo: Mwananchi