Rostam ni Mfalme na mwamba hapa Tanzania

Ili uwe tajiri unahitaji ufanye biashara na state au serikali kama sio ya nchi yako basi ya nchi yoyote, hapo ndio utavuna utajiri na mifano iko wazi dunia nzima biashara za udaga, vitunguu, mahindi, mpunga tumia kukuzia mtaji ukishakua sajili kampuni anza kutafuta deal za mashirika makubwa au serikali huko utapata pesa chapchap yaani mfano una malori wewe tafuta tenda ya kubeba mahindi ya serikali au ya wfp kutoka wanapokusanyia hadi kwenye maghala yao hapo kutoboa chap hivo anachofanya RA sio kigeni wenye akili wote hufanya hivo
 
Umegeneralize, vijijini asilimia kubwa hajafika. Unafika sehemu ikiwa mahitaji napo ni makubwa
Huwezi kuuza mitungi ya gesi kule mliyabibi nguruka.

Ni sawa na ukafungue duka la spare za magari kule pangamawe rukwa
 
Ninachojua mimi serikali sio wajinga hawawezi kuifanya Taifa Gas kuwa sole distributor wa gas nchi nzima.
Huijui hii serikali ndugu yangu. Je kwa makampuni ya asimu imekuwaje? Je kuna ushindani? Anayetaka kupunguza bei anaitwa TCRA aeleze kwa nini anataka bei ndogo!
Tunahitaji competition kwenye utoaji wa huduma ili kuongeza ubora wa huduma na price stability
Competition Tanzania ni ndoto. CCM iko macho kuvuna kwa kampuni yoyote ile na itahakikisha hakuna ushindani. Ni kama vile anayeamua bei iwe ipi yuko Lumumba ambako tayari anapiga hesabu ya mavuno.
 
Umegeneralize, vijijini asilimia kubwa hajafika. Unafika sehemu ikiwa mahitaji napo ni makubwa
Huwezi kuuza mitungi ya gesi kule mliyabibi nguruka.

Ni sawa na ukafungue duka la spare za magari kule pangamawe rukwa

Gesi ikitumika uvinza, nguruka , kaliua, usinge, tayari inapunguza athari za kimazingira kwani rate ya matumizi ya mkaa na kuni nayo hupungua hivo ahueni ya kimazingira itakuepo nadhani umemsikia Rais alivyoshauri
 
Wewe ni mfanyakazi wa moja ya miradi yake?
 
Safari ya USA alikuwepo, Ya Kenya alikuwepo
, Oman pia.

He is almost every where .ana nguvu sana awamu hii.

Kila anachotaka kinafanyika with no compromise.
Imagine ameishinikiza Serikali iandae kongamano la kitaifa ya nishati ya kupikia huku kukiwa na mgao mkali wa maji na umeme nchi nzima lakini hakuna anayeongelea.
 
Gas ni kwa kundi flani la wa tz. Walio wengi Mkaa wa 1500 inatosha kwa siku.
 
Wife umeanza kujiangusha kwenye 18 za matajiri nini?!
Hubby no way. Inabidi tu sasa tujifunze kwa Rostam. Kwani baby wewe hautaki kumiliki vitalu vya gas ?Na kuwa king maker kwa kila utawala ?Inabidi tufanye biashara sasa hadi vitukuu wa vilembwe wetu waikute. Positive vibes tu leo honey ❤
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…