Royal Tour ni sumaku ya kisiasa Mkakati wa Kenya una changamoto chanya kwa Tanzania

Royal Tour ni sumaku ya kisiasa Mkakati wa Kenya una changamoto chanya kwa Tanzania

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2015
Posts
18,487
Reaction score
13,611
Video ya Rais William Ruto akiongea na wakenya waishio ughaibuni (diaspora) siku za karibuni, imejaa kila aina ya somo jema kwa uhai wa miaka mingi wa Tanzania yetu.

Ruto kawa muwazi kwa wakenya kwamba anabariki jitihada zao za kutafuta maisha huko ughaibuni, kwamba wanachokipata huko kinapokelewa kwa mikono miwili kinaporudishwa Kenya. Huu ni mtazamo chanya wa Kenya kimataifa na Ruto sio kiongozi wa kwanza kuwa na maono ya aina hii.

Kenya ni nchi imejengwa kibepari, inaruhusu raia wa nchi yake kwenda huko nje kupambania mkate wa kila siku na kurudisha nchini mwao faida (remittance) inayopatikana. Wanatumia kila sekunde ya kujenga nchi katika kujenga raia wenye uwezo wa kushindana katika soko la ajira.

Anachowaambia raia wa Kenya ughaibuni ni ule msingi wanaoujenga miaka na miaka wa kuandaa nguvu kazi zenye kutakiwa na soko la wakati husika ndani ya muda wowote.

Naona kama TZ tunazidi kukwama linapokuja suala la utayari wa nguvu kazi yetu kupambana kimataifa, bado mpaka leo tuna mijadala ya kiswahili na kingereza eti ni ipi lugha yenye soko na itakayowapa raia wetu ile faida ya asili katika kupigania soko la kimataifa la ajira!.

Royal Tour ulikuwa ni mkakati wa kitaifa wa kukaribisha wageni waje wafanye utalii, lakini siuoni uwiano wa Royal Tour na ile jeuri kama aliyoifanya Ruto ya kuwaambia wakenya waende huko nje wakapambanie ajira kwa nia ya kuja na mrejesho chanya kiuchumi. Je kwa mikakati kama Royal Tour tunajiandaa kuwa wapokeaji wa kudumu wa wageni tusiozifahamu faida za sisi kuwa sehemu ya soko pana la ajira huko duniani?.

Watalii kuja kwao ni kuitikia ile nguvu ya matangazo ya kiserikali na binafsi kuhusu kuitangaza TZ. Lakini wanapokuwa hapa tunakuza vipi uhusiano wa kibiashara na wao ili matokeo yake yawe ni kukua kwa uchumi kusikoyumba kirahisi?.

Jina TZ na thamani yake linapanda zaidi iwapo tunakuwa na nguvu kazi isiyo na uoga kujieleza, isiyo na uoga kuaminisha watu kuwa sisi ni taifa makini. Jina TZ linapanda hadhi na viwango iwapo tunabadilika haswa hizi tabia zetu za kila siku zenye kutukwaza kimataifa.

Yapo mengi yanayoshusha thamani jitihada zIlizokula pesa nyingi za Royal Tour. Na ule muonekano mzima chanya wa wanadiplomasia waliosomeshwa kwa nguvu na fedha ili siku moja waje kufanya mengi mema kwa ajili ya TZ.
 
.

Mimi nina mtazamo tofauti na huu wa William Ruto. Kwanza kabisa I’m not against diaspora remittances, in fact I like diversity, lakini sio inayoletwa na hardship and lack of home opportunities, kama Ethiopia , Eritrea, Somalia and the likes. Huko kwenye nchi hizo watu wamekimbia mateso, unyanyasaji na sera mbovu za uchumi/Siasa ndiyo wakakimbia nchi.

I believe in a leader who is focusing in creating HOME opportunities kwanza. Maana amechaguliwa kwa platform ya kuondoa hali ngumu ya maisha hii unaiondoa kwa kuongeza ajira nyumbani watu wafanye kazi

Ikitokea mtu anataka kwenda nje aende tu kwa mapenzi yake for new experience or exposure, lakini sio hili la kukosa opportunities and Hope ya kufanikiwa akiwa nyumbani

Ukimuuliza Ruto ni ajira ngapi atatengeneza ndani ya Kenya mwaka ujao nina uhakika hana jibu la maana, lakini anakupa projection za kupeleka Wakenya manamba ughaibuni, hii haijakaa vizuri.

HAPANA.
 
Tanzania ni taifa ambalo ata kupata pasipoti ni dili.Sasa tutaendaje ughaibuni?maana ata Watanzania walioenda asilimia kubwa walizamia.Ingia YouTube account ya Big light Worldwide wasikilize Watanzania wanavyoeleza jinsi walivyoondoka nchini kwenda ughaibuni!
 
Video ya Rais William Ruto akiongea na wakenya waishio ughaibuni (diaspora) siku za karibuni, imejaa kila aina ya somo jema kwa uhai wa miaka mingi wa Tanzania yetu.

Tanzania hatuna diaspora wa maana kuleta uchumi hapa nchini. Diaspora wetu ni uchwara tu. Kina lemutuz 30 ulaya karudi na dola 500. Mtu kama Mange ana mchango gani wa kumpa uraia pacha?
 
Tanzania hatuna diaspora wa maana kuleta uchumi hapa nchini. Diaspora wetu ni uchwara tu. Kina lemutuz 30 ulaya karudi na dola 500. Mtu kama Mange ana mchango gani wa kumpa uraia pacha?
Umenena lililo kweli. Wengi walioko nje kwanza wanatudhalilisha tu kwa mambo yao wanayofanya. Hoja inafikirisha.
 
.

Mimi nina mtazamo tofauti na huu wa William Ruto. Kwanza kabisa I’m not against diaspora remittances, in fact I like diversity, lakini sio inayoletwa na hardship and lack of home opportunities, kama Ethiopia , Eritrea, Somalia and the likes. Huko kwenye nchi hizo watu wamekimbia mateso, unyanyasaji na sera mbovu za uchumi/Siasa ndiyo wakakimbia nchi.

I believe in a leader who is focusing in creating HOME opportunities kwanza. Maana amechaguliwa kwa platform ya kuondoa hali ngumu ya maisha hii unaiondoa kwa kuongeza ajira nyumbani watu wafanye kazi

Ikitokea mtu anataka kwenda nje aende tu kwa mapenzi yake for new experience or exposure, lakini sio hili la kukosa opportunities and Hope ya kufanikiwa akiwa nyumbani

Ukimuuliza Ruto ni ajira ngapi atatengeneza ndani ya Kenya mwaka ujao nina uhakika hana jibu la maana, lakini anakupa projection za kupeleka Wakenya manamba ughaibuni, hii haijakaa vizuri.

HAPANA.

Ninadhani umeshika kitu kidogo katika vingi vikubwa. Mkuu, ajira unazotaka watu wawe nazo Tz ni zile za mtu kulipwa mshahara wa milioni moja akaiona kubwa?? Ajira hiyo hiyo US atalipwa milioni 10??

Poor economies cannot create job opportunities as fast as learning institutions release the learned!! Poor economies cannot pay as high as developed economies can!! Ndio maana ukaja msemo wa kubeba box, ambazo ukibeba nyumbani kwa mfano unaweza kulipwa pesa ya kula tu!! Dakari wa Tz anapata mshahara mdogo kuliko taxi driver US (sina maana ya kusema taxi driver ni mtu mdogo). Jua kuwa hakuna nchi inayoweza kutengeneza ajira kwa raia wake wote. Raia wako kupata kazi nje kunapunguza tatizo la ajira nchini mwako. Ruto anachowahimiza ni kuleta wanachopata nyumbani kitu ambacho kitaongeza shughuli za uchumi na kutoa ajira kwa walio nyumbani. Sisi kwa kuwakana diaspora tunazuia pesa zisiwekezwe hapa!!

By the way, wanaokwenda diaspora ni wale wanataka kupata pesa ya kutosha ndoto zao katika wakati mfupi. Wengine wanafanikiwa na wengine hawafanikiwi. Eti exposure!

Ni watu wenye mawazo kama yako ndio kikwazo cha maendeleo. Hakuna kiu ya maendeleo, mnabakiza chuki na husuda kwa diaspora!!
 
.

Mimi nina mtazamo tofauti na huu wa William Ruto. Kwanza kabisa I’m not against diaspora remittances, in fact I like diversity, lakini sio inayoletwa na hardship and lack of home opportunities, kama Ethiopia , Eritrea, Somalia and the likes. Huko kwenye nchi hizo watu wamekimbia mateso, unyanyasaji na sera mbovu za uchumi/Siasa ndiyo wakakimbia nchi.

I believe in a leader who is focusing in creating HOME opportunities kwanza. Maana amechaguliwa kwa platform ya kuondoa hali ngumu ya maisha hii unaiondoa kwa kuongeza ajira nyumbani watu wafanye kazi

Ikitokea mtu anataka kwenda nje aende tu kwa mapenzi yake for new experience or exposure, lakini sio hili la kukosa opportunities and Hope ya kufanikiwa akiwa nyumbani

Ukimuuliza Ruto ni ajira ngapi atatengeneza ndani ya Kenya mwaka ujao nina uhakika hana jibu la maana, lakini anakupa projection za kupeleka Wakenya manamba ughaibuni, hii haijakaa vizuri.

HAPANA.
Bahati mbaya haujui kuwa hao wahabeshi na wasomali wanapeleka pesa nyingi makwao kuliko unavyodhani, na baadhi ya pesa hizo ndizo zinszochochea vita kwao.
 
Hatuwezi kuwa na diaspora wa kukuza uchumi kama hatuweki English as teaching language kuanzia chekechekea.
Lengo la kiswahili mashuleni ni kutufanya raia tubaki maskini tusioweza kwenda nje kupiga kazi. Na wanaotufanya tubaki maskini ni wazee wanaofikiri watabaki madarakani milele!

Halafu kitu kizuri wazee watunga sera siku wakifa huwa wanapelekwa kuzikwa kijijini walikokimbia maisha yao yote.

Wanaochimba makaburi yao ni vijana wasio na ajira kutokana na sera zao mbovu za kufanya watu wawe maskini milele!

Wanaobeba masanduku yenye miili yao ni watu maskini waliowatesa kwa ufisadi wao na sera mbovu wakiwa madarakani
 
Husomeshi watu ili wakafanye kazi kimataifa. Lakini hata hivyo, serikali ikitaka watu waende nje iondoe urasimu wa kuzuia watu kwenda nje.
 
Tanzania hatuna diaspora wa maana kuleta uchumi hapa nchini. Diaspora wetu ni uchwara tu. Kina lemutuz 30 ulaya karudi na dola 500. Mtu kama Mange ana mchango gani wa kumpa uraia pacha?
Lemutuz karudi na jeans 👖 zilizopauka na perfume za sampuli duty free 😂😂😂
 
I believe in a leader who is focusing in creating HOME opportunities kwanza. Maana amechaguliwa kwa platform ya kuondoa hali ngumu ya maisha hii unaiondoa kwa kuongeza ajira nyumbani watu wafanye kazi
Umepiga penyewe hasa!

Hata Kenya usiiondoe kwenye hizo nchi ulizotaja, kama Ethiopia na kwingine, ni hardship' na kukosekana kwa fursa ndiko kunakowasukuma hata kwenda kuwa watumwa huko Arabuni na kupata shida chungu nzima.

Lakini kati ya yote uliyoandika, ni mstari huo mmoja na robo tatu ndio ulionifanya nsisimukwe mwili.

Sikutaka kuandika kirefu, lakini mawazo yanapanuka zaidi kwenye kuchangia huku.

Ngoja nigusie sehemu ninayowasifu Kenya, hasa viongozi wao ikihusiana na hiyo uliyoandika "..leader who is focusing in creating HOME opportunities..."
Pengine kwa kutojua kwetu, lakini Kenya 'are doing the very thing we are discussing here', hata kama matokeo hayajaonekana, na hata utekelezaji wa mipango hiyo huko nyuma haikufanyika kwa ufanisi.
Toka enzi za Kibaki, hadi kwa Uhuru Kenyatta na sasa kwa Ruto, hwa wote wamejitahidi kuanzisha juhudi za kuwaunga raia wao kutafuta maendeleo kwa kuanzisha mifuko mbalimbali za kifedha; kwa mfano 'UWEZO Fund', 'Youth Fund' ingawa matapeli walivuruga; na sasa Ruto kaleta 'Hustler Fund'.na nyingi nyingine.

Hizi zote ni juhudi za kuwawezesha wananchi wajikwamue kimaisha.

Sasa pamoja na ujenzi wa nyumba nafuu kwa watu wenye kipato cha chini, ambapo pia ni fursa ya kuongeza pato kwa hawa wajasiriamali wadogo, hizi zote ni juhudi za "creation of HOME opportunities', ambapo kwa hapa kwetu hakuna kabisa mipango ya aina hiyo. Hapa hasa ndipo wanapotuacha kwenye mataa tukishangaashangaa na CCM yetu!

Kuna mengi nisiyokubaliana na Kenya, lakini nidhahiri sasa kwamba, pamoja na matatizo mengi yanayowakabili, kuliko yanayotukabili sisi, lakini kwa hakika wanapiga hatua mbele.
 
TANZANIA NI LAZIMA ILIANGALIE SUALA HILI, ISAIDIE INAPOBIDI WATU KWENDA NGAMBO LAKINI KWA SHUGHULI HALALI ZINAZOFAHAMIKA, MREJESHO WA REMITANCE NYUMBANI UTASAIDIA KUSTAWISHA FAMILIA DUNI AMBAZO KIJANA WAO ATAKUJA NGAMBO.
 
Mada ni nzuri, lakini imechanganywa na mambo mengi yasiyoijengea nguvu.

Kwa mfano, sioni maana ya kuchanganya Royal Tour na Diaspora, kama mfano mmoja tu wa mkanganyiko.

Lakini ngoja niache tarakimu kidogo hapa kuunga mkono mada.

Diaspora Kenya mwaka uliopita wameingiza zaidi ya dollar za Marekani Billion 3. Hii ni hela nzuri sana ya nje, na ndiyo inayosaidia katika kushikiza thamani ya shilingi ya Kenya. Sisi diaspora yetu, hata Benki kuu huwa hawajisumbui sana kuitaja. Nadhani ni kama dollar million tano hivi kwa mwaka uliopita

Utalii, kwetu ni nafuu zaidi ya Kenya kwa kiasi cha pesa kinachoingia, nadhani itakuwa kwenye bilion moja na zaidi kwa mwaka uliopita. Tunawazidi Kenya, lakini siyo sana. Lakini kutokana na vivutio tulivyonavyo, tungekuwa mbali zaidi ya majirani zetu wote.

But all in all, Tanzania tunashindwa tu sisi wenyewe kutumia fursa nyingi tulizojaliwa hapahapa nyumbani hata bila ya kukimbilia huko nje. Badala yake, sasa tunatapanya tu bila ya mpangilio wowote.

Niondoke na swali: Hivi diaspora wa Kenya waliopo hapa Tanzania wanapeleka kiasi gani kwao? Nasikia tu kwamba kiasi hicho kilikuwa kinono kuliko walichopata toka Afrika Kusini, nchi ambayo huwa kinara kwao katika bara la Afrika.
 
Tanzania hatuna diaspora wa maana kuleta uchumi hapa nchini. Diaspora wetu ni uchwara tu. Kina lemutuz 30 ulaya karudi na dola 500. Mtu kama Mange ana mchango gani wa kumpa uraia pacha?
Nadhani wenzetu Kenya hawafanyi masihara katika suala zima la elimu. Wanahakikisha wanakuwa na wasomi competitive katika kila sekta, wanaoajirika inapotokea usaili wa kimataifa wa ajira.

Kina Lemutuz na Mange ni cases chache sana, tunaongelea upande mwingine wa zile akili makini zenye kuweza kushandania zile ajira nzito nzito, bado TZ tunalo deni la kuwa na wasomi washindani sio wasomi wanaosomea kufaulu mitihani tu.
 
Mada ni nzuri, lakini imechanganywa na mambo mengi yasiyoijengea nguvu.

Kwa mfano, sioni maana ya kuchanganya Royal Tour na Diaspora, kama mfano mmoja tu wa mkanganyiko.

Lakini ngoja niache tarakimu kidogo hapa kuunga mkono mada.

Diaspora Kenya mwaka uliopita wameingiza zaidi ya dollar za Marekani Billion 3. Hii ni hela nzuri sana ya nje, na ndiyo inayosaidia katika kushikiza thamani ya shilingi ya Kenya. Sisi diaspora yetu, hata Benki kuu huwa hawajisumbui sana kuitaja. Nadhani ni kama dollar million tano hivi kwa mwaka uliopita

Utalii, kwetu ni nafuu zaidi ya Kenya kwa kiasi cha pesa kinachoingia, nadhani itakuwa kwenye bilion moja na zaidi kwa mwaka uliopita. Tunawazidi Kenya, lakini siyo sana. Lakini kutokana na vivutio tulivyonavyo, tungekuwa mbali zaidi ya majirani zetu wote.

But all in all, Tanzania tunashindwa tu sisi wenyewe kutumia fursa nyingi tulizojaliwa hapahapa nyumbani hata bila ya kukimbilia huko nje. Badala yake, sasa tunatapanya tu bila ya mpangilio wowote.

Niondoke na swali: Hivi diaspora wa Kenya waliopo hapa Tanzania wanapeleka kiasi gani kwao? Nasikia tu kwamba kiasi hicho kilikuwa kinono kuliko walichopata toka Afrika Kusini, nchi ambayo huwa kinara kwao katika bara la Afrika.
Rais Ruto anavyoongea na wakenya na kuwaahidi ushirikiano watu wa diaspora, kuna aina fulani ya mkakati wa kiserikali wa kujitanua na kujitangaza kimataifa.

Kuna siku na sisi tutakuja kuwa na jeuri kama hii hii ya majirani ya kujitangaza kimataifa kwa maana ya nguvu kazi?.

Naona kila mara marais wetu wanapopata muda kuongea na diaspora wanakuwa wakituma ujumbe tofauti wa kitaifa kulingana na nani yupo ikulu, unadhani ni lini rais wetu ataongea kwa uwazi kwa diaspora akahimiza juu ya wanachokifanya huko nje chenye faida kwa TZ yetu ijayo?.
 
Ninadhani umeshika kitu kidogo katika vingi vikubwa. Mkuu, ajira unazotaka watu wawe nazo Tz ni zile za mtu kulipwa mshahara wa milioni moja akaiona kubwa?? Ajira hiyo hiyo US akalipwa milioni 10??

Poor economies cannot create job opportunities as fast as learning institutions release the learned!! Poor economies cannot pay as high as developed ecomonies can!! Ndio maana ukaja msemo wa kubeba box, ambazo ukibeba nyumbani kwa mfano unaweza kulipwa pesa ya kula tu!! Dakari wa Tz anapata mshahara mdogo kuliko taxi driver US (sina maana ya kusema taxi driver ni mtu mdogo). Jua kuwa hakuna nchi inayoweza kutengeneza ajira kwa raia wake wote. Raia wako kupata kazi nje kunapunguza tatizo la ajira nchini mwako. Ruto anachowahimiza ni kuleta wanachopata nyumbani kitu ambacho kitaongeza shughuliza uchumi n kutoa ajira kwa walio nyumbani. Sisi kwa kuwakana diaspora tunazuia pesa zisiwekezwe hapa!!

By the way, wanaokwenda diaspora ni wale wanataka kupata pesa ya kutosha ndoto zao katika wakati mfupi. Wengine wanafanikiwa na wengine hawafanikiwi. Eti exposure!

Ni watu wenye mawazo kama yako ndio kikwazo cha maendeleo. Hakuna kiu ya maendeleo, mnabakiza chuki na husuda kwa diaspora!!

Sasa kuna Diaspora alizuiwa kuja kuwekeza hapa Tanzania?

Kwani ukiwa Mtanzania Diaspora,huwezi kuja kufanya maendeleo yako na familia yako hapa?

Sema wazi!
kinachopiganiwa hapa ni kupata Uraia Pacha ili mkiisha beba maboksi kwa miaka mingi huko basi muambulie na Pensheni zinaoendana na Maisha yao.

Wengi wa wakenya walioko nje wanajitambua kilichowapeleka huko.
Tofauti na Watanzania ambao wameondoka wenyewe kwa hiari zao.na kufika huko mnabaki kulilia Uraia Pacha!

For your Own interests na msisingizie ooh Maendeleo ya nchi wala nini!

Tunaposema Uraia Pacha bado hatujajiandaa nao kwa sasa.
Ni kwa maslahi mapana ya kitaifa.

Ila ukiwasikiliza huko Spaces na Club houses wanalalama siasa tupu.

Ukimuuliza what have you done since ever umekaa huko!

Utaishia kuambiwa wewe na Watanzania wenzio ni waoga sana kuchukua maamuzi magumu!

Wengine ndio hao kina Lissu,ambao watoto na familia zao wana Uraia wa nje tayari.

Lakini kazi yao ku-Snitch na makampuni ya nje kisha kubaki wakituzodoa baada ya kufanikiwa kuzisaidia hizo kampuni.

Sasa hivi tu bado tuna Uraia wa nchi moja,lakini Wapinzani wa kisiasa Tanzania,wanapishana Uzunguni kuomba msaada wa kuiondoa Serikali Madarakani.

Je!
Uraia Pacha wakiupata? Itakuwaje??

Na kama mnaona Uraia wetu unazingua kwa nini msiombe wa huko mlipo na kuukana U-Bongo

Jibu ni kwamba nyingi wengi wenu sio material ambazo zinaweza pewa uraia wa huko kirahisi.

Sababu elimu pia ni ya kuungaunga!

Unless Otherwise Uolewe au Kuowa huko.
 
Ukimuuliza Ruto ni ajira ngapi atatengeneza ndani ya Kenya mwaka ujao nina uhakika hana jibu la maana, lakini anakupa projection za kupeleka Wakenya manamba ughaibuni, hii haijakaa vizuri.
Ndiyo akili zetu (za kiTanzania/kiccm) kwamba maprofesa na madaktari wa Kenya wanaofanyakazi America, Canada Australia etc ni manamba. Ni ujinga kufikiri kwamba wamekimbia kwao kwa kukosa ajira. Ni kwamba wana uwezo wa kukidhi viwango vya kuajiriwa huko duniani kwenya kipato kikubwa na hivyo wananufaika zaidi wao binafsi na taifa lao kwa jumla. Na rais Ruto si kwamba amesahau mikakati ya kuzalisha ajira ndani ya Kenya, bali anapambania ziada kwa manufaa ya nchi yake.
Au ulitaka adanganye tumejenga viwanda 3,000 kama 'shujaa' alivyowadanganya wanyonge?
 
Ndiyo akili zetu (za kiTanzania/kiccm) kwamba maprofesa na madaktari wa Kenya wanaofanyakazi America, Canada Australia etc ni manamba. Ni ujinga kufikiri kwamba wamekimbia kwao kwa kukosa ajira. Ni kwamba wana uwezo wa kukidhi viwango vya kuajiriwa huko duniani kwenya kipato kikubwa na hivyo wananufaika zaidi wao binafsi na taifa lao kwa jumla. Na rais Ruto si kwamba amesahau mikakati ya kuzalisha ajira ndani ya Kenya, bali anapambania ziada kwa manufaa ya nchi yake.
Au ulitaka adanganye tumejenga viwanda 3,000 kama 'shujaa' alivyowadanganya wanyonge?
Wanaposema kuwa madaktari wa kinigeria ndio wamejaa USA ni habari yenye kuwajenga wao na nchi yao kwa pamoja.

Hatuwezi kutengeneza mkakati wa kitaifa wa kuwaongelea kwa ushahidi halisi wataalam wetu huko nje?.

Kwanini wataalam wa diaspora wa nchi nyingine za afrika wawe na habari chanya zenye kuwahusu halafu sisi tukiongelea mafanikio ya diaspora ni kina Mange na Lemutuz?.

Tatizo letu haswa ni lipi, kutawatambua wataalam wa kitanzania wa diaspora au ni kule kusambaa kwa habari hasi zenye udaku ndani yake kama ilivyo kawaida ya hulka zetu?.
 
Rais Ruto anavyoongea na wakenya na kuwaahidi ushirikiano watu wa diaspora, kuna aina fulani ya mkakati wa kiserikali wa kujitanua na kujitangaza kimataifa.
Hapana, siyo "mkakati", wameamua iwe sera ya nchi yao. Lakini hilo halina maana kwamba na sisi inalazimu tufanye hivyo.

Jambo la maana zaidi ninaloliona katika mpango huo ni kwa wale wenye ujuzi maalum (special skills) wanaoweza kuleta uzoefu wao nyumbani, lakin hawa wengine wote wanaokwenda kuwa mayaya huko uarabuni, ni hivyo visenti tu wanavyopata ndiyo faida inayotokana na mpango huo. Na wengi wao ni wa aina hii.

Huu "mkakati wa kitaifa" unaouzungumzia wewe, nchi nyingi tu duniani hufanya hivyo, kwa kuwapeleka watu wao kusoma huko kunakopatikana elimu maalum, na siyo lazima iwe kwa watu kwenda kupata ajira. Katika miaka ya 80, China imefanya sana hili. Vyuo vingi huko Ulaya na Marekani ungedhani ni vyuo vya wachina kwa jinsi walivyokuwa wanajazana huko. Hii ni kwa elimu baada ya shahada ya kwanza (postbraduate).
Hata nchi nyingi za kiarabu , kama Iraq kabla ya Saddam kupata matatizo, walijitahidi sana kupeleka watu wao kwenye vyuo vya huko ulaya na Marekani.

Lakini naomba unielewe, sipingi kamwe habari ya diaspora, lakini sikubaliani na dhana ya kuwa nchi kama Tanzania haiwezi kumudu kufanya mambo yake mewngi kabisa bila ya kutegemea mpango huo.

Tatizo letu ni hili tu la kutokuwa na viongozi wanaojuwa mahitaji ya Taifa na kuwa na malengo maalum juu yake na kuwa na uwezo wa kusimamia utekelezaji kwa umakini mkubwa.

Ngoja nikwambie: Tanzania hii wataalam tunao wengi sana karibu katika kila nyanja, lakini tumewaacha wasitumie utaalam wao, na mbaya zaidi wengi wao inawalazimu wajiingize huko huko kwenye ubovu wa kisiasa.

Hatuna mikakati ya kutumia elimu na utaalam wao.
 
Back
Top Bottom