Ruangwa kama Chato

Ruangwa kama Chato

Wokovu unaanzia samaria mpaka mwisho wa nchi
Tochi humulika kuanzia miguuni kwako baada ndio unamulika kwingine
Kuwa mwelewa
Mwitongo na Lupaso walikuwa bahati mbaya kwa kufuata mtazamo wako wewe.
 
Wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu 2015 , sisi Watu wa Kyela tuliokuwa tunampinga Mwakyembe (Aliyetajwa kama PM ajaye) Tulishambuliwa vibaya mno.

Binafsi nimefuatwa inbox na zaidi ya watu10 ili nisimpinge Mwakyembe maana akiwa Waziri Mkuu Kyela yetu ingekuwa Paradiso , Hata hivyo Mwakyembe alipewa ushindi wa mabavu na alipokosa U PM Kyela yote iliripuka kwa furaha (sijui kwanini) .

Nadhani haya ya Ruangwa ndio niliyokuwa naambiwa inbox na wadau .
Waziri Mkuu Mwakyembe?

Mungu atuhurumie.

Hivi bado yupo na ni mbunge? Mbona hasiskiki kabisa.

Kweli dunia ina mambo. Enzi zile Mwakembe alikuwa hakosekani kwenye habari za nchi. Hebu ona sasa!
 
Waziri Mkuu Majaliwa hana tofauti kubwa na marehemu Magufuli kila mara yuko nyumbani kwao Ruangwa na ni kupeleka miradi kila baada ya miezi kadhaa.

Hajui yeye ni Waziri Mkuu wa nchi nzima? Leo ametoa mikopo Milioni 256, hii hela ni nyingi sana kwa wilaya moja.

Bado nradi wa maji sijui nafikiri Bilioni 500. Kwanini haya mambo ya upendeleo na ubaguzi yameanza wakati wa Magufuli?

Nchi hii haikuwa na mawaziri wakuu kabla? Haya ni matumizi mabaya ya nafasi.

Lini atatembelea wilaya zingine na kupelekea neema ya miradi inayofanana na ambayo amekuwa akiipeleka Ruangwa kila mara?

Amesahau yeye ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?

Atumikie watanzania wote kwa usawa.
Mara nyingi mno anakuwa yupo Ruangwa, nilifikiri ofisi ya PM imehamishiwa huko!
 
Mkuu acha tu wajenge kwao,nipo Butiama jioni hii,nimetoka kumuagiza boda maziwa mtindi boda kaniambia huwezi kupata,nimeenda mwenyewe kutafuta,Hakuna duka linalouza mtindi butiama.Naongelea maziwa mtindi guys,Butiama inasikitisha sana.Acha viongozi wajenge kwao.
Nenda Kiabakari mkuu
 
Mara nyingi mno anakuwa yupo Ruangwa, nilifikiri ofisi ya PM imehamishiwa huko!
Anenda kama Mbunge wa Ruangwa kwa kuwa ili uwe PM lazima uwe mbunge, asipokwenda wengine watahoji tena zile gharama za mafuta na huduma zingine anazolipiwa na serikali achilia mbali za Uwaziri Mkuu anazipeleka wapi na jimboni haendi.....nimewaza tu kwa sauti ila kwa angle ngingine
 
Waziri Mkuu Majaliwa hana tofauti kubwa na marehemu Magufuli kila mara yuko nyumbani kwao Ruangwa na ni kupeleka miradi kila baada ya miezi kadhaa.

Hajui yeye ni Waziri Mkuu wa nchi nzima? Leo ametoa mikopo Milioni 256, hii hela ni nyingi sana kwa wilaya moja.

Bado nradi wa maji sijui nafikiri Bilioni 500. Kwanini haya mambo ya upendeleo na ubaguzi yameanza wakati wa Magufuli?

Nchi hii haikuwa na mawaziri wakuu kabla? Haya ni matumizi mabaya ya nafasi.

Lini atatembelea wilaya zingine na kupelekea neema ya miradi inayofanana na ambayo amekuwa akiipeleka Ruangwa kila mara?

Amesahau yeye ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?

Atumikie watanzania wote kwa usawa.
Milioni 256 ni nyingi ukilinganisha na wapi, je kama hizo 256 million ni asilimia 10 ya makusanyo ya ndani kwa ajiri ya wajasiamali? Maana kila halmashauri ina kiwango chache kulingana na makusanyo
 
Acha wivu kaka! Lindi ipo nyuma sana,huwezi linganisha Lindi na Chato kwa vyovyote vile!

Nije kwenye point yako sasa,hivi unaweza vipi sema Ruangwa inaweza kua kama Chato, Ruangwa ni Wilaya ndogo sana tena sana,haina hata lami! Tokea hapo Nanganga hadi Liwale hakuna lami,sasa hivi ndiyo wanaweka lami tokea Nanganga hadi Ruangwa,huo mradi wa maji wa 500B hivi unajua 500B ni mradi wa maji Mkubwa sana,ambao unaweza vuta maji toka Mwanza hadi Shinyanga?? Sasa 500B ziwekwe wilayani Ruangwa kweli??

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Milioni 256 ni mikopo ya Halmashauri ya Ruangwa kwa vikundi vya vijana 4%, wanawake 4% na walemavu ni 2%.Mikopo hiyo ni asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri au Manispaa au majiji husika kwa wananchi wao na huwa inawekwa kwenye bajeti za Halmashauri zote hapa nchini.
 
Kwa lindi mtwara mi nasema hiyo hela ni kidogo sana iongezwe. Mi nitaman mikoa kama hiyo atlist kila familia serikali iangalie uwezekano wa kuchukua mtoto mmoja kwa lazima asomeshwe mpaka master kwa gharama za serikali. Bado sana
 
Kwa miaka ile aliyotawala Nyerere alikuwa na uwezo wa kuifanya Butiama kuwa kama Dubai na hakuna mtu angehoji!! ila ndio hivyo uadilifu ulimzidi mzee wetu! Pumzika kwa amani Mwl. Nyerere baba wa Taifa letu! Sijui mchakato wa kumfanya mtakatifu umeishia wapi?
 
Back
Top Bottom