Ni kawaida mbona,,, kila mtu ana maximum yake ya kuhimiliWasanii kwenye sanaa nimeona picha moja barnaba amezimia alafu mfiwa mkuu mbaki mutahaba mdogo wa marehemu ndio ananguvu za kumbeba ruge.
Yap, nimewaona wote hapo nyumbani. Ila uwanjani sikuwaonaMke wa rommy yupo amekaa karibu na ally kiba
Kbs ndio maana sikuwaona mapemaWote wapo angalia vizuri ila leo hakuna kale kaupendeleo ka nafasi
hivi ni kweli hako kabinti kameachiwa kitumbo cha miezi kadhaa?
Hivi mbona kila kona tangu dar hadi bukoba hadi kabale anapozikwa Ruge sasa naona nandy amekaa karibu na watoto wa marehemu Ruge. Vp nandy nae alikua bi mdogo au????
Kumbe Nandy alikuwa anaosha rungu la marehemu. Ooh pole kwake.
Mkwe kuna mijitu ilivyo minafiki yaani wameguswa na huu msiba kuliko hata walivyoguswa ni misiba ya wazazi wao.Mkwe ulishawahi kushangaa kitu mpaka ukaona aibu!
Natoka home nimevaa zangu tight na blouse , mdada wangu ananiambia mama si uvae kama dera flan hivi msibani utaendaje na tight, namuuliza msiba upi dada? anajibu si huu wanatangaza kwenye TV!
Niko zangu saluni nakata panki langu, naambiwa naona unajipiga sop sop uende msibani,
Nakuta foleni barabarani naambiwa oh wametoka kumpokea mwili unafika leo
Nafika kazini mtu ana nguo nyeusi oh msibani!
Naenda canteen nakuta watu wanaonyeshana video za mwili ulipowasili!
HAPO NIKASHTUKA
nikajiuliza hivi mimi niko sawa kweli, mbona kama NIKO DUNIA AMBAYO WENZANGU HAWAPO!
nikajitafakari kwanini nimepokea tu kuwa ni msiba na nikamuombea na kuendelea na ratiba zingine?
nikajikuta pengine sina tatizo!
PENGINE IT WAS MEANT TO BE THAT WAY!
basi nikajikubalia tu kuwa sijaelewa na sio lazima nielewe kila kitu.
watoto wote wapo sehemu ya wanafamilia na wote wamevaa nguo nyeupe, wapo na mama zao na Nandy pembeni.Ila jmn mbona wale watoto wadogo ni km familia imewatenga, naona mtoto mkubwa ndio yuko nao karibu.
Wale wengine mpk muda huu bado sijawaona
Sent using Jamii Forums mobile app
Kuzikwa na kanisa hakumuondelei dhambi mkuu, yaani hapa kanisa langu katoliki limeonesha UDHAIFU mkubwa sana, alikuwepo maaskofu wawili pale uwanjani Gymkhana na walitoa salamu za kumsifu Marehemu na kuomba aliyotenda yaendelezwe, kuacha kuongoza mwili wake kaburini ni unafiki mkubwa sana bora wasingehudhuria toka mwanzo..Afu kanisa katoliki ni kanisa la principles na linazifuata. Kuna waliosema eti kisa Ruge alikua maarufu basi atazikwa kwa misa na padre, lkn sheria za kanisa haziangalii umaarufu wala nini. Kwa mnaofatilia nadhan mnaona kinachotokea sasa, Ruge anaagwa tu na ibada ya Katekista na wala sio misa ya padri. Na hii ni kutokana na kutofunga ndoa.
Mtajiuliza mbona komba alisaliwa misa na padre??? Hii ni kwa sababu yy aliwahi kufunga ndoa na kuwa na mke wa pili kanisa linaona ni kama mchepuko na kama kanisa halina uwezo wa kuhukumu dhambi ya mtu.
Please kwa wale mlokua mnadhan kanisa katoliki linaangalia umaarufu mjue mnakosea sana. Kwa wanahistoria wazuri nadhan mnaweza kuelezea asili ya kanisa la Anglikana ambalo lilitengenezwa na mfalme wa Uingereza baada ya kujitoa katika kanisa katoliki kisa papa kumkatalia kuvunja ndoa yake angali mke wake akiwa hai. Huyu mfalme alidhan umaarufu wake ungemtetemesha papa lkn haikua hivyo coz hata yeye papa hayuko juu ya sheria.